Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
<strong>Wewe</strong><br />
<strong>Maisha</strong> <strong>Yako</strong><br />
<strong>Ndoto</strong> <strong>Zako</strong><br />
Kitabu cha Vijana balehe
<strong>Wewe</strong>, <strong>Maisha</strong> <strong>Yako</strong>, <strong>Ndoto</strong> <strong>Zako</strong>:<br />
Kitabu cha Vijana Balehe<br />
Catherine Watson na Ellen Brazier
i<br />
© Ubora wa Afya kwa Familia Duniani, 2009.<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO Shukurani<br />
Taasisi za kujitolea zinaruhusiwa kutumia kitabu hiki kwa kutoa nakala au nukuu lakini<br />
hawaruhusiwi kuuza nakala hizo. Ubora wa Afya kwa Familia Duniani wangependa kuona<br />
wanatajwa kwenye nukuu au nakala hizo kama wamiliki wa kitabu hiki.<br />
Kwa kupata nakala zaidi kitabu cha <strong>Wewe</strong>, <strong>Maisha</strong> <strong>Yako</strong>, <strong>Ndoto</strong> <strong>Zako</strong>: Kitabu cha Vijana Balehe,<br />
tafadhali wasiliana na wafuatao:<br />
<strong>Family</strong> <strong>Care</strong> <strong>International</strong>-Kenya<br />
Anwani: S.L.P 45763<br />
00200 Nairobi, Kenya<br />
Simu:. (254-20) 4443167<br />
Simu ya upepo: (254-20) 4443204<br />
Barua pepe: fcikenya@fcimail.org<br />
Tovuti: www.familycareintl.org<br />
<strong>Family</strong> <strong>Care</strong> <strong>International</strong><br />
588 Broadway,Suite 503<br />
New York,NY 10012<br />
Simu:. (1-212) 941-5300<br />
Simu ya upepo: (1-212) 941-5563<br />
Barua pepe: fcipubs@familycareintl.org<br />
Kitabu cha <strong>Wewe</strong>, <strong>Maisha</strong> <strong>Yako</strong>, ndoto <strong>Zako</strong> ni tafsiri ya “You, Your life, Your Dreams”<br />
kilichoandikwa kwa mara ya kwanza mwaka 2000 na shirika la “<strong>Family</strong> <strong>Care</strong> <strong>International</strong>”<br />
lenye Makao Makuu Mjini New York, nchini Marekani kwa kushirikiana na shirika la “Straight<br />
Talk Foundation” la Uganda. Toleo la awali kabisa liliandikwa na catharine Watson Mkurugenzi<br />
Mhariri wa “Straight Talk Foundation” kwa kushirikiana na ellen brazier ambaye wakati huo<br />
alikuwa Mkurugenzi wa Programu ya Afrika ya Mashariki katika Shirika la Ubora wa Afya kwa<br />
Familia Duniani.<br />
Tafsiri ya kitabu hiki iliwezeshwa kwa msaada wa shirika la “Tanzania German Programme to<br />
Support Health” (tGPSh) kupitia “Reproductive Health Component (Repro/GTZ)”. Kupiga chapa<br />
kitabu hiki kuliwezeshwa kwa msaada wa Richard and Rhoda Goldman Fund. Japo uratibu wa<br />
kutafsiri kitabu hiki ulifanywa na bi Rehema l. Mwateba, aliyekuwa mratibu wa Shirika la Ubora<br />
wa Afya Kwa Familia Duniani; watu wengi walishirikishwa. Shirika la “<strong>Family</strong> <strong>Care</strong> <strong>International</strong>”<br />
kwa kupitia ofisi yake ya Ubora wa Afya kwa Familia Duniani Tanzania linawashukuru wafuatao<br />
kwa mchango wao mkubwa katika kufanikisha tafsiri hii:-<br />
Kwanza kabisa Shirika la Ubora wa Afya kwa Familia Duniani linawashukuru wafuatao kwa<br />
kufanya tafsri na kupitia maandishi na michoro ya kitabu hiki:-<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Bi. Margreth Mtafya Kilembe kwa kufanya tafsiri kutoka lugha ya Kiingereza kuwa Kiswahili.<br />
Bi. Benadicta Maganga kwa kupitia muswada kwa mara ya kwanza.<br />
Bwana Michael Kadege kwa kupitia muswada kwa mara ya pili.<br />
Bwana Abdalla Athumani Mhagama kwa kuratibu shughuli za mapitio ya wasomaji<br />
mbalimbali na kutupatia maoni ya wasomaji.<br />
Bwana Sunnny Kiluvia na Bwana Elikunda Matteru kwa kupitia muswada baada ya wasomaji.<br />
Kwa kuwa si rahisi kumtaja kila mtu aliyeshiriki kwa namna moja au nyingine katika uandishi wa<br />
kitabu hiki, shirika linapenda kuwashukuru walioshiriki kuratibu shughuli za wasomaji sehemu<br />
mbalimbali nchini Tanzania:-<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Bi. Lucy Ikamba aliyewaratibu wasomaji wa mradi huko Mbeya Vijijini.<br />
Bi. Catherine Ndawi aliyewaratibu wasomaji, Mbeya Manispaa.<br />
Bwana Ole Sepere aliyewaratibu wasomaji, wilaya ya Pangani.<br />
Bi. Emiliana Malambugi aliyeratibu upatikanaji wa maoni ya wasomaji kutoka kwa viongozi<br />
wa madhehebu ya dini.<br />
Bwana Benard Msami aliyewaratibu wasomaji, walimu wa shule za msingi - Turiani, Morogoro<br />
Vijijini.<br />
Bwana Dickson Reginald Ituwe kwa utaalamu wake wa kupanga maandishi katika kompyuta.<br />
Bwana Juma Lugendwa kwa kuchora upya picha zilizoombwa kurudiwa na wasomaji.<br />
Bwana Stanley Matteru na Richard Ndago kwa mchango wao katika utawala.<br />
Bi. Margret Mbede na Bi. Dawa Mhagama kwa mchango wao katika uchapaji.<br />
ii
iii<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO Utanguzi<br />
Shukurani za pekee kwa Bi Cordula Schuemer kwa utetezi kwa vijana na kuhakikisha kuwa vijana<br />
wanapata taarifa sahihi kuhusu masuala ya jinsia na afya ya uzazi.<br />
Kwa kuwa Kitabu hiki ni tafsiri ya kitabu “You, Your life, Your Dreams”, shirika la Ubora wa Afya<br />
kwa Familia Duniani (FCI) lingependa kuwashukuru wale wote waliohusika katika uchapishaji<br />
wa kitabu hiki kwa lugha ya kingereza.Hii inatia ndani udhamini wa shirika la Ford Foundation,<br />
European Commission, William and Flora Hewlette Foundation, John D.and Catherine T.<br />
MacArthur Foundation na Blanchette Hooker Rockefeller Charitable Fund.<br />
FCI ingependa pia kuwashukuru Adolescent Reproductive Health Education Project; CEDPA;<br />
FAWE, Hesperian Foundation na United Nations haswa UNICEF kwa matumizi ya picha zao. FCI<br />
inawapa shukrani Regina C. Faul-Doyle, Timothy Kiwala, Mashet Ndhlovu, ODIA na Philip Odida<br />
kwa michoro yao.<br />
Sehemu mbalimbali za kitabu “You, Your life, Your Dreams”, zilipata mchango kutoka kwa Eva<br />
Agutti, Grace Canada, Claire Mcminn, Edith Mukisa, Dr. Sarah Naikoba na Joy Oguttu. Maandishi,<br />
mifano na michoro ilichambuliwa na Dr. A. Ananie Arkutu, FRCOG, Ghana; Regina Goergen, GTZ,<br />
Tanzania; Muriithi Kinyua, <strong>Family</strong> Planning Private Sector, Kenya; Dr. Margaret Makumi,Ministry<br />
of Health, Kenya; Dr. Elizabeth Odera, Malezi Preparatory School, Kenya; Rehema Mwateba,<br />
Independent Consultant, Tanzania na Mary Waithaka, Nairobi Primary School, Kenya.<br />
Msaada katika kufanya majaribio ulitolewa na wawakilishi kutoka Ministry of Health Ghana;<br />
<strong>Family</strong> Planning Association of Kenya;Planned Parenthood Association of Ghana; Young<br />
Christian Women’s Association, Ghana. Shukrani pia kwa wawakilishi kutoka Kenya Association<br />
of Professional Counsellors; Kuleana Centre for Child Rights, Tanzania; Mathare Youth Sports<br />
Association, Kenya; Media Trust for Development, Zimbabwe; Naguru Teenage Health Centre,<br />
Uganda; The New Vision, Uganda na Trendsetters Newspaper, Zambia kwa kuwanukuu vijana<br />
balehe.<br />
FCI inawapa shukrani wafanyakazi wake wote kwa mchango wao mbalimbali katika kufanikisha<br />
uchapishaji wa kitabu ‘<strong>Wewe</strong>, <strong>Maisha</strong> <strong>Yako</strong>, <strong>Ndoto</strong> <strong>Zako</strong>’ kwa lugha ya kiingereza na Kiswahili.<br />
Kubalehe ni kipindi katika maisha ya wanadamu ambapo kijana anabadilika na kuwa mtu mzima.<br />
Kipindi hiki kina msisimko mkubwa, lakini pia ni kipindi chenye kuchanganya sana. Wakati wa<br />
kubalehe utaona mabadiliko mengi ya kimwili na kihisia, pia unaweza kuwa na maswali mengi<br />
kuhusu mwili wako na uhusiano wako na wengine.<br />
Kitabu hiki kimeandikwa kwa ajili ya vijana balehe, ambao wana umri kati ya miaka 14 na 19 ili<br />
kiwasaidie kukabiliana na changamoto nyingi zinazotokea wakati wa mabadiliko kutoka utoto<br />
kwenda utu uzima.Kitabu hiki kinatoa taarifa sahihi kuhusu mabadiliko yanayotokea katika<br />
kipindi cha balehe, pamoja na mambo mengine, kwa mfano: jinsi ya kuwa na afya njema ya kimwili<br />
na kihisia, kuepuka magonjwa yanayosababishwa na ngono zisizotakiwa, jinsi ya kupambana<br />
na misukumo ya kufanya ngono, na jinsi ya kujiepusha na matumizi mabaya ya vileo na dawa za<br />
kulevya. Pia, kitabu kinatoa ushauri kuhusu uhusiano mwema na wazazi, marafiki, wapenzi, jinsi<br />
ya kuweka malengo ya maisha, mbinu za kufaulu shuleni na maishani na jinsi ya kukabili vikwazo.<br />
Kitabu hiki kina taarifa nyingi lakini si lazima usome kurasa zote. Unaweza kuangalia katika<br />
sehemu inayoonyesha “Yaliyomo” na kuona mada zinazokupendeza zaidi. Ukizimaliza,<br />
unaweza kurudi tena kwenye “Yaliyomo” na kuchagua tena mada inayokuvutia. Pia, unaweza<br />
kufunuafunua tu kitabu na kuangalia sehemu zenye michoro, katuni na nukuu mbalimbali toka<br />
kwa vijana. Unaweza pia kuangalia sehemu maalumu zilizo na kichwa “je, Wafahamu”. Hizi<br />
zinatoa taarifa sahihi kuhusu mambo mbalimbali.<br />
Ingawa kitabu hiki kilikusudiwa zaidi kwa vijana ambao hawajaoa/kuolewa wenye umri wa miaka<br />
14 hadi 19, zipo pia sehemu za kitabu hiki zinazowafaa vijana wenye umri uliozidi na hata walio<br />
kwenye ndoa. Kisome kitabu hiki pamoja na marafiki zako, kaka na dada zako na wazazi wako.<br />
Ongea nao na jaribu kuona wao wanazichukuliaje mada zilizomo kwenye kitabu hiki.<br />
Furahia kitabu hiki na uwe salama!<br />
Molly Anyango<br />
Mshauri rika wa Vijana<br />
<strong>Family</strong> Planning Association of Kenya<br />
iv
v<br />
Watu wazima wengi hudhani kuwa vijana hawana sababu ya kuwa na wasiwasi wala matatizo. Hata<br />
hivyo, balehe ni kipindi cha kuchanganya na kufadhaisha. Maswali na dukuduku nyingi hutokea<br />
wakati huu wa mabadiliko ya mwili na hisia. Pia, vijana hujiuliza maswali yanayohusu elimu, ajira<br />
na uhusiano kwa marafiki na wazazi. Kipindi cha kubalehe kinaambatana na misukumo toka kwa<br />
marafiki. Vijana huwa na wasiwasi kuhusu maisha yao ya baadaye.<br />
Lakini kubalehe ni hatua muhimu na inayosisimua. Ni kipindi ambacho kijana hukua kimwili, kihisia<br />
na kiakili. Pia, kijana huanza kupata majukumu na kuwa na ndoto kuhusu maisha ya baadaye. Vijana<br />
balehe hujifunza kufanya uamuzi binafsi ambao huweza kubadili maisha yao ya leo, kesho na miaka<br />
mingi ijayo.<br />
Wakati wa kubalehe, kijana anahitaji taarifa sahihi ili zimsaidie kufanya uamuzi wenye nguvu na<br />
usalama. Wazazi, walimu na watu wazima wengine hupata wasiwasi kuhusu uamuzi waufanyao vijana<br />
wao unaohusu uhusiano, ngono,dawa za kulevya na vileo au kupanga maisha ya baadaye.<br />
Hata hivyo, utafiti unaonyesha kuwa vijana wanaweza kupanga mambo yao kwa busara kama wakiwa<br />
na taarifa sahihi pamoja na mbinu mbalimbali za maisha kama vile uwezo wa kufanya uamuzi,<br />
mawasiliano, maelewano, wakisaidiwa na miongozo toka kwa watu wazima.<br />
Kitabu cha “<strong>Wewe</strong>, <strong>Maisha</strong> <strong>Yako</strong>, <strong>Ndoto</strong> <strong>Zako</strong>” kinachambua masuala mbalimbali yanayowakuta<br />
vijana balehe katika Bara la Afrika. Yaliyomo humu yameandaliwa kwa kuwashirikisha vijana<br />
wenyewe toka nchi mbalimbali. Kitabu kimebobea katika masuala ambayo vijana wenyewe waliyaona<br />
yana umuhimu: Kuingia utu uzima, kutunza afya, kukabili mifadhaiko, kuelewana na wazazi, kujenga<br />
uhusiano wa kirafiki na kimapenzi, kukabili mifadhaiko na kuvunjika moyo, afya njema ya ujinsia,<br />
kupata mimba, kutoa mimba, kukabili matumizi mabaya ya dawa za kulevya na vileo, masuala ya<br />
elimu na ajira.<br />
Zipo sababu mwafaka za kutaka kuhakikisha vijana wetu wanazo taarifa sahihi kuhusu masuala<br />
haya. Vijana wanakumbana na mambo mengi yanayoongeza changamoto na uwezekano wao wa<br />
kudhurika, ikiwa majumbani, mitaani, shuleni na hata kwenye vyombo vya habari. Leo hii, kijana ana<br />
uwezekano wa kupata matatizo mengi ya kiafya kama vile magonjwa ya zinaa, VVU/UKIMWI, mimba<br />
zisizotakiwa na utoaji mimba usio salama. Kiasi cha asilimia 60 ya maambukizi mapya ya VVU katika<br />
Bara la Afrika yanatokea kwa vijana wa miaka 10 hadi 24. Hii ina maana kuwa vijana wanaambukizwa<br />
VVU kwa kasi zaidi kuliko kundi lolote lingine.<br />
Kijana aliyeko kwenye hatari zaidi ya kuambukizwa VVU ni yule asiye na taarifa sahihi. Kijana wa aina<br />
hii anategemea zaidi kupata taarifa toka kwa marafiki, video au filamu na muziki wa kizazi kipya,<br />
taarifa ambazo kwa kiwango kikubwa huwa si sahihi. Kwa hiyo, kitabu hiki kimekusudia kuhakikisha<br />
vijana balehe wanapata taarifa sahihi na wanajijengea uwezo wa kukabili misukumo ya kutenda<br />
yasiyofaa, kujenga uhusiano wenye faida na la muhimu zaidi; kuwawezesha vijana wafanye uamuzi<br />
salama na wa busara.<br />
Napenda kuwasisitiza wazazi, walimu na watu wazima wengine wasome kitabu hiki na<br />
wawashirikishe vijana wao na wengineo. Aidha, nawasisitiza watu wazima waongee na vijana kuhusu<br />
taarifa zilizomo na wawashauri vijana inavyopasa. Watu wazima wawasaidie vijana kuwa salama<br />
katika kipindi cha mabadiliko kuingia utu uzima ili waweze kutimiza ndoto zao maishani.<br />
Dr. A. Ananie Arkutu<br />
Kwa Wazazi, Walimu, na Watu wazima wengine<br />
Yaliyomo<br />
ShuKuRani ................................................................................................................................................................... ii<br />
utanGuliZi ....................................................................................................................................................................iv<br />
Kwa Wazazi, Walimu, na Watu wazima wengine ..................................... ....................................................... ......... v<br />
SuRa Ya 1: ujana balehe: baDiliKO KubWa, chanGaMOtO KubWa ....................................................... 1<br />
Nini maana ya ujana balehe? ...................................................................................................................................................... 2<br />
Ukweli kuhusu maisha ..................................................................................................................................................................4<br />
Maadili.......................................................................................................................................... ................................................ ......5<br />
Stadi za maisha................................................................................................................... ............................................................6<br />
SuRa Ya 2: MabaDiliKO Ya MWili............................................................................. ............................................9<br />
Mfoko wa ukuaji: mwanzo wa balehe.............................................................................. ........................................................9<br />
Vichocheo (Homoni).............................................................................................................. .......................................................12<br />
Via vya uzazi - Sehemu za siri............................................................................................ .......................................................13<br />
Nywele za mwilini na mabadiliko ya ngozi....................................................................... .....................................................13<br />
Uwezo wa kufikiri..................................................................................................................... ........................................... .........14<br />
SuRa Ya 3: WaVulana........................................................................................................ .............................. .......17<br />
Umbo na ukubwa wa mwili...................................................................................................... ...................................................17<br />
Sauti yako................................................................................................................................... .............................................. ......18<br />
Via vyako vya uzazi (Sehemu zako za siri)........................................................................ .................................... ...............19<br />
Mazoezi ya usafi...................................................................................................................... ......................................................21<br />
Kudinda kwa uume................................................................................................................... ....................................................22<br />
Kumwaga manii “kukojoa”...................................................................................................... ....................................................23<br />
<strong>Ndoto</strong> nyevu (“Kutoa manii/ Shahawa ukiwa usingizini”)........................................... ............................ .......................24<br />
SuRa Ya 4: WaSichana.................................................................................................... ............................. ..........27<br />
Maumbile na ukubwa wa mwili............................................................................................ ...................................... ..............27<br />
Matiti yako................................................................................................................................ ............................................. .........27<br />
Sidiria......................................................................................................................................... .......................................................31<br />
Via vya uzazi ( Sehemu zako za siri )............................................................................ ...........................................................31<br />
Kufanya usafi wa mwili vizuri................................................................................. ..................................................................33<br />
Hedhi na mzunguko wa hedhi................................................................................ ...................................................................35<br />
Kutunza kalenda............................................................................................................ ........................................... ...................39<br />
Hedhi inavyokosesha raha........................................................................................ ....................................... ........................40<br />
Ngono na hedhi................................................................................................................. ............................................. ................41<br />
Kujisikia vizuri/ Afya na usafi ................................................................................... ..................................... ........................41<br />
Utatumia nini kujihifadhi na hedhi.............................................................................. .................................... .......................42<br />
SuRa Ya 5: MaMbO Ya MSinGi KatiKa KutunZa MWili........................... ....................... ...........................45<br />
Jiweke safi, nukia vizuri................................................................................................... ......................................... .................45<br />
Utunzaji wa meno yako..................................................................................................... ......................................... ................46<br />
Chunusi.............................................................................................................................................................................................47<br />
Utunzaji nywele................................................................................................................. ........................................... ................48<br />
Lishe nzuri.............................................................................................................................. .............................................. ..........49<br />
Mazoezi.................................................................................................................................. ...........................................................51<br />
Mapumziko mazuri............................................................................................................ ...........................................................53
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO SURA YA 1 | UJANA BALEHE: BADILIKO KUBWA CHANGAMOTO KUBWA<br />
SuRa Ya 6: utunZaj i aFYa Ya aKili na MOYO............................ ..................................................................55<br />
Kujiheshimu..................................................................................................................... ...............................................................55<br />
Kujiamini............................................................................................................................ ............................................. ................58<br />
Usiwe na wasiwasi, furahi........................................................................................ ...................................... ..........................60<br />
Kukabili huzuni.......................................................................................................... ........................................... ........................63<br />
Kuishi vizuri na watu................................................................................................ ........................................ ...........................64<br />
SuRa Ya 7: ueleWanO na WaZaZi WaKO................................................. .......................... ...............................71<br />
Kuthamini familia...................................................................................................... ......................................... ..........................72<br />
Fahamu yale wazazi wako wanayoyataka........................................................ ................................. ..................................72<br />
Kukidhi matarajio ya wazazi wako...................................................................... ..................................... ...............................74<br />
Mawasiliano na wazazi wako................................................................................ ...................................... .............................74<br />
Vyanzo vingine vya kupata msaada................................................................... ....................................................................78<br />
SuRa Ya 8: uRaFiKi na MaPenZi................................................................... ......................................................81<br />
Urafiki.......................................................................................................................... .............................................. .......................81<br />
Jinsi ya kumtambua mtu ambaye si rafiki wa kweli................................... ............................. .........................................83<br />
Kuelewana na jinsi nyingine................................................................................ ...................................... ...............................84<br />
Kuanza uhusiano na mtu unayempenda ........................................................ ................................... ...................................85<br />
Kujenga uhusiano wa kweli ............................................................................... ........................................................................87<br />
Mapenzi.................................................................................................................... ............................................ ..........................88<br />
Kupumbazika....................................................................................................................................................... ..........................90<br />
Kuachana kimapenzi............................................................................................. .......................................... .............................91<br />
SuRa Ya 9: ujinSia na nGOnO..................................................................... ........................... ..............................93<br />
Ujinsia wenye afya njema...................................................................................... ....................................... ...........................94<br />
Hisia za kijinsia........................................................................................................ ........................................... ..........................96<br />
Punyeto...................................................................................................................... ............................................. ........................96<br />
Ubikira........................................................................................................................... ............................................. .....................98<br />
Kujamiiana..................................................................................................................... ................................................................101<br />
Kuweka kiwango cha kujamiiana........................................................................... ................................................................102<br />
Uamuzi wa kutofanya ngono.................................................................................... ..................................... ........................104<br />
Kuzungumza na mwenzi wako kuhusu ngono......................................................................................... ..........................104<br />
SuRa Ya 10: KutunZa aFYa YaKO Ya KiujinSia ...................................... ....................... ...........................109<br />
Magonjwa ya zinaa....................................................................................................... ......................................... ....................109<br />
Utajuaje kama umepata maambukizi ya magonjwa ya zinaa?......................... .............................................................111<br />
Kwenda kuchunguzwa magonjwa ya zinaa............................................................... ...........................................................112<br />
VVU / UKIMWI....................................................................................................................... .......................................................114<br />
Utajuaje kama una VVU.............................................................................................................................................................116<br />
Kuishi kwa matumaini na VVU....................................................................................... .........................................................118<br />
Ngono salama / Mapenzi salama................................................................................... .......................................................120<br />
Kondomu................................................................................................................................. ........................................................121<br />
Matatizo mengine ya afya ya uzazi............................................................................... .......................................................124<br />
SuRa Ya 11: MiMba na uZuiaji Wa MiMba .................................................... ..................................................129<br />
Mimba inatokeaje?........................................................................................................... .........................................................129<br />
Dalili za mimba.................................................................................................................. ..........................................................130<br />
Hatari za mimba na uzazi kwa wasichana balehe.................................................. ..........................................................131<br />
Kustahimili mimba katika umri mdogo...................................................................... ................................. ........................132<br />
Kujitunza wakati wa ujauzito..................................................................................................................................................134<br />
Mimba na VVU..................................................................................................................... ........................................................134<br />
Maandalizi ya kujifungua................................................................................................ ....................................... ..................135<br />
Kujitunza na kumtunza mtoto baada ya kujifungua............................................. ..........................................................136<br />
Kuharibika mimba............................................................................................................ ..........................................................136<br />
Namna ya kuepuka kupata mimba.............................................................................. .........................................................138<br />
Je vidonge vya kuzuia mimba ni salama?................................................................... ........................................................139<br />
Kuzuia mimba kwa dharura.............................................................................................. .......................................................139<br />
Kinga mara mbili............................................................................................................... ..........................................................141<br />
SuRa Ya 12: nGOnO Ya KulaZiMiShWa na nGOnO bila Ya RiDhaa YaKO..... ....................................145<br />
Shinikizo kutoka kwa rafiki wa kiume au wa kike............................................................ ...............................................145<br />
Shinikizo kutoka kwa watu wazima............................................................................... .................................. ...................146<br />
Unyanyasaji kijinsia............................................................................................................ ........................................ ..............148<br />
Kudhalilisha kijinsia.......................................................................................................... .........................................................150<br />
Ubakaji.................................................................................................................................. .........................................................150<br />
Kitu cha kufanya ubakaji ukitokea.............................................................................. .........................................................154<br />
SuRa Ya 13: MatuMiZi MabaYa Ya DaWa.......................................................... .......................... ...................157<br />
Aina ya dawa na vitu ambavyo vinatumika vibaya................................................ ............................. ............................157<br />
Sigara na pombe.............................................................................................................. ...........................................................159<br />
Kutawaliwa na dawa.......................................................................................................... .........................................................161<br />
Kwa nini watu wanaanza kutumia dawa...................................................................... ........................................................163<br />
Namna ya kushughulikia shinikizo la kutumia dawa.............................................. ............................ ...........................166<br />
Kuacha dawa................................................................................................................................................................... ............168<br />
SuRa Ya 14: KutiMiZa nDOtO ZaKO...................................................................... ............................................171<br />
Kuzitambua ndoto zako............................................................................................................................................ ................172<br />
Mipango ya baadaye kuhusu kazi.................................................................................. ..................................... ..................173<br />
Kuweka malengo.................................................................................................................... ........................................... ..........174<br />
Kufanya uamuzi mzuri (wa busara)................................................................................ ..................................... ..................176<br />
Zingatia bila kuyumba katika malengo na ndoto zako........................................... ............................ ...........................178<br />
Kufanya vizuri katika masomo shuleni........................................................................ .................................. .....................179<br />
Kuacha shule........................................................................................................................ .........................................................181<br />
Kutatua vipingamizi............................................................................................................ ......................................................182<br />
FahaRaSa .................................................................................................................... ........................................ .......187<br />
MaRejeleO...................................................................................................................... ............................................193
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Ujana Balehe:<br />
Badiliko Kubwa,<br />
Changamoto Kubwa<br />
Patric, kutoka Kenya(umri,miaka 16)<br />
“Nilichokifurahia katika ujana balehe wangu ni kuwajibika katika majukumu<br />
ya nyumbani hasa wazazi wanapokuwa hawapo. Majukumau haya<br />
nayapenda kwasababu ninadhani nimeshakua na ninaweza kujidhibiti mimi<br />
mwenyewe na wadogo zangu”.<br />
naana, kutoka Ghana. (umri; miaka 17)<br />
“Yapo mambo mengi yanayomhusu kijana balehe ambayo siyapendi. Ninakumbuka<br />
nilipokiwa na umri mdogo nilikuwa na uhuru zaidi kuliko sasa.<br />
Lakini kwa sasa zipo sheria na miongozo mingi.”<br />
Watu wengi duniani wanatafsiri “ujana balehe”<br />
kama kipindi cha maisha kati ya miaka 10 na 19.<br />
Kama una umri wa miaka kati ya 10 na 19, basi<br />
wewe ni kijana balehe. Hongera! <strong>Wewe</strong> ni mtu<br />
muhimu sasa.<br />
Ni kweli kuwa kwa muda wote uliopita umekuwa<br />
mtu muhimu, lakini kwa sasa hivi umekuwa<br />
mtu muhimu zaidi. Unapitia mabadiliko mengi<br />
sana na unajaribu mambo mengine mapya,<br />
kutoka mwonekano mpya,kujitambua kupya<br />
kama vile kuandamana na marafiki wa jinsi<br />
tofauti,kushikana mikono na kubusiana.<br />
Wazazi wako wanaweza kukuta ujana balehe wako<br />
unautumia vibaya.<br />
1<br />
SURA YA 1
2<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Mwonekano wako mpya na kujitambua kwako kunawafanya wazazi, shangazi zako na wajomba<br />
kuwa na wasiwasi kwa sababu wasingependa upate matatizo na wala wasingependa ufanye<br />
makosa makubwa kama vile kupata mimba (au kwa kumpa mimba rafiki wa kike) wakati ungali<br />
unasoma. Zaidi ya yote wanakuwa na wasiwasi kwa sababu wanafahamu kwamba umri kati ya 10-<br />
19 unaweza kuwa na athari kubwa katika ukuaji wako na aina ya maisha utakayokuwa nayo.<br />
nini Maana Ya ujana balehe?<br />
• Ujana balehe ni kipindi ambacho unabadilika na kukua kimwili na kiakili kutoka utoto na<br />
kuingia utu uzima. Wakati wa ujana balehe mambo yafuatayo hutokea:<br />
• Mwili wako utabadilika kwa jinsi unavyopenda uwe au wakati mwingine hata usivyopenda<br />
uwe.<br />
• Utaanza kupata hisia za kutaka kujamiiana, na unaweza usijue ufanye nini baada ya kupata<br />
hisia hizo.<br />
• Utaanza kufikiri bila ya kumtegemea mtu mwingine na kutaka kufanya maamuzi peke yako.<br />
• Hisia zako kuhusu familia na mahusiano yako na wazazi, yanaweza kubadilika kwa uzuri<br />
au kwa ubaya. Wazazi wanaweza kukupa majukumu zaidi ambayo ni dalili nzuri kwamba<br />
wanakuamini na kukutegemea. Lakini wanaweza vilevile wakaanza kuwa wakali hata<br />
kutokuruhusu ukutane na marafiki zako. Wakati mwingine watajaribu kufanya maamuzi<br />
kuhusu masomo na mustakabali wa maisha yako ya baadaye. Wanaweza wakaonyesha<br />
kuwa na upendo mdogo kwako kuliko walivyokuwa huko nyuma na unaweza vilevile usipate<br />
mahusiano yenye upendo kama ulivyokuwa ukiwa mtoto.<br />
• Marafiki zako, na hata yale wanayofikiria, vinaweza kuwa vya muhimu zaidi kuliko ilivyokuwa<br />
awali.<br />
• Hisia zako zinaweza kuwa na utata zaidi kuliko ulivyozoea na wakati mwingine wewe<br />
mwenyewe unaweza usifahamu hasa kile unachohisi au ni kwa nini unahisi hivyo.<br />
• Kwa hakika unaweza kuhisi kutaka kupendwa au kuwa karibu na mtu mwingine.<br />
• Unaweza kukumbana na maamuzi mazito na zinaweza kuwepo nyakati ambapo hujui umtake<br />
nani ushauri.<br />
Ujana balehe ni kipindi maalum kwa kila mtu, kote duniani – mashariki au magharibi,kaskazini<br />
au kusini.Lakini pia ni kipindi chenye changamoto. Hiki ni kipindi cha mabadiliko makubwa, na<br />
mabadiliko makubwa huchukua muda. Utakutana na mambo mengi ya kuyafanyia maamuzi<br />
unapopitia ujana balehe na maamuzi mengine utakayofanya yatadumu nawe katika maisha yako<br />
yote.<br />
Yapo mambo mengi sana ambayo unaweza kuyafanya ili kupitia salama ujana balehe. Hivyo<br />
ni vema uelewe mwili wako na mabadiliko yanayotokea .Ni vema ujielewe na pia uelewe kile<br />
unachokitaka katika maisha. Tumia muda kufikiria maisha yako ya baadaye na kupanga<br />
yatakuwaje. Utu uzima una majukumu makubwa hivyo basi ni lazima kujiandaa vema wakati wa<br />
ujana balehe.<br />
Wakati wa ujana usiwe mpweke na kufanya mambo peke yako. Umezungukwa na watu<br />
wanaoshughulikia matatizo muhimu kila siku. Unao ndugu wengi, kama akina shangazi, wajomba,<br />
binamu na wengi wengineo, amabao unaweza kuwaomba ushauri. Pia kwa vile wewe ni sehemu ya<br />
jamii, zipo mila na desturi nyingi ambazo mafunzo yake yanaweza kukusaidia.<br />
SURA YA 1 | UJANA BALEHE: BADILIKO KUBWA CHANGAMOTO KUBWA<br />
Mahali pengi ujana umekuwa mgumu kueleweka, na hasa siku hizi vijana wanapata matatizo<br />
ambayo wazazi wao, mabibi hata babu zao hawakuwahi kuyapitia; matatizo hayo ni:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Msukumo wa kutaka kujamiiana.<br />
Madawa ya kulevya shuleni na kwenye jamii.<br />
Wazazi ambao kwa sababu ya shughuli nyingi hawana muda au wanaona aibu kuzungumza<br />
kuhusu mabadiliko yanayowatokea watoto wao.<br />
Magonjwa yaambukizwayo kwa kujamiiana ikiwa ni pamoja na VVU/UKIMWI.<br />
Kuwa yatima kwa sababu ya UKIMWI au ajali.<br />
Vita au kuyumba kisiasa kwa nchi.<br />
Ili kuyamudu yote haya na kupitia kipindi cha ujana balehe salama unahitaji kuwa jasiri , mbunifu,<br />
mtafutaji na mwenye kujipa matumaini. Jaribu kujifunza kutoka kwa watu wanaokuzunguka<br />
ambao ni jasiri na watulivu wakati unapokutana na matatizo. Kila wakati jione kuwa utashinda<br />
matatizo yako kama walivyoweza wengine.<br />
Vijana huFiKiRia KWaMba haKuna janGa linalOWeZa KuWaPata<br />
Ni tabia ya vijana duniani kote, katika nchi tajiri na maskini – kufikiria kwamba mambo mabaya<br />
hayawezi kuwatokea. Hujiambia,<br />
“ Haitatokea kwangu”. Wakati mwingine hujiamini sana<br />
na kuhisi wako salama mno.<br />
Je wewe uko hivi? Unadhani unaweza kujaribu kitu cha hatari<br />
na lisikupate jambo? Kwa mfano, wewe na rafiki yako wa kike<br />
(msichana) mnafahamu kuhusu dawa za kuzuia mimba. Lakini<br />
mnadhani kwamba ili mradi hamjamiiani mara kwa mara,<br />
msichana hawezi akapata mimba.<br />
Au unaweza ukawa na ufahamu mkubwa kuhusu<br />
VVU, virusi vinavyo sababisha UKIMWI. Unaweza<br />
ukafahamu kwamba maambukizi yanaweza<br />
kutokea kwa njia ya kujamiiana bila kinga,<br />
lakini unafikiri kwamba rafiki yako wa kiume<br />
hawezi kuwa na maambukizo. Unakataa kufikiri<br />
kuwa unaweza kupata maambukizo ya VVU na<br />
haiwezekani pia kwa wale watu unaowafahamu<br />
kupata ugonjwa huo.<br />
je haya yanakuhusu? Kama ndivyo, hapa kuna<br />
mambo ambayo unahitaji kuyazingatia:<br />
Vijana wengi hujiingiza kwenye vitendo vya<br />
hatari wakidhani kuwa hawatadhurika....<br />
3
4<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Mimba inaweza ikatungwa utakapojamiiana kwa mara ya kwanza bila kinga.<br />
Kusema kweli, kila watu wawili wanapojamiiana bila kinga kuna uwezekano wa 1:12 mimba<br />
kutungwa. Maana yake ni kwamba iwapo mtajamiiana bila kinga mara moja kwa mwezi, mnaweza<br />
kukumbwa na mimba isiyotarajiwa.<br />
...mimba huweza tungwa hata kamaumejamiiana<br />
mara moja.inaweza kutungwa utakapojamiiana<br />
kwa mara ya kwanza.<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Ili kupita kipindi cha ujana salama unahitaji angalau mambo matatu:<br />
Ukweli Kuhusu <strong>Maisha</strong><br />
Kumbuka pia kwamba maambukizi ya VVU<br />
hutokea kwa vijana pia, na hutokea kwa vijana<br />
zaidi kuliko hata kwa wengine. Vijana wanapata<br />
maambukizo ya VVU haraka zaidi kuliko kundi<br />
lingine lolote Afrika. Maambukizi mapya kwa<br />
watu kumi,watu sita huwa ni vijana.<br />
Usiruhusu ukawa mmojawapo kati ya<br />
vijana wenye mimba zisizotakiwa au wenye<br />
maambukizi mapya ya VVU. Soma kitabu hiki<br />
kwa uangalifu ili ujue jinsi unavyoweza kufanya<br />
maamuzi mazuri, ili uwe salama na mwenye afya.<br />
Tafadhali washirikishe marafiki zako kusoma<br />
kitabu hiki ili nao pia wajifunze jinsi ya kuchagua<br />
yale yaliyo mema.<br />
Maadili – Unahitaji kujua yale unayoamini ni ya kweli ili uweze kufanya maamuzi unayoweza<br />
kuishi nayo.<br />
Stadi za maisha, ili utumie ukweli unaoujua na kubakia mkweli ndani ya maadili yako.<br />
uKWeli KuhuSu MaiSha<br />
Nini maana ya “hali halisi/mambo ya ukweli”? Ukweli kuhusu maisha ni upi?<br />
Ukweli ni taarifa zote muhimu za mambo unayotakiwa kuyafahamu ili kuyamudu maisha ya kila<br />
siku na kufanya maamuzi mazuri.<br />
Kufahamu ukweli maana yake ni kufahamu jinsi ya kujitunza mwenyewe – kimwili na kifikra – kwa<br />
kula vizuri; kutunza mwili vizuri; na kutunza vizuri afya ya akili na maono yako. Kufahamu ukweli<br />
vile vile maana yake ni kufahamu jinsi mimba inavyotokea, jinsi VVU/UKIMWI na magonjwa<br />
mengine yatokanayo na kujamiiana yanavyosambaa na jinsi unavyoweza kuzuia usiambukizwe.<br />
Ukweli ni kufahamu ni kwa namna gani madawa ya kulevya na pombe vinaweza kuudhuru mwili na<br />
ubongo na jinsi maisha yako yanavyoweza kuharibika. Ukweli ni kufahamu njia nzuri za kumudu<br />
hali ngumu na matatizo yako, ili uweze kufanikisha ndoto zako.<br />
La muhimu zaidi, kufahamu ukweli ni kubainisha kati ya yaliyo ya ukweli na yaliyo ya uongo. Ni<br />
muhimu sana kujua mambo ya ukweli wakati unapojaribu kuchagua. Chagua lililo la muhimu na<br />
amua la kufanya.<br />
SURA YA 1 | UJANA BALEHE: BADILIKO KUBWA CHANGAMOTO KUBWA<br />
Unahitaji mambo ya ukweli ili uwe salama. Kitabu hiki kimejaa ukweli, hivyo kitakupa ukweli<br />
kuhusu:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Mabadiliko yanayotokea mwilini mwako (Sura ya 2,3, na 4).<br />
Kutunza afya yako ya kimwili na kimaono (Sura ya 5 na 6).<br />
Mahusiano na watu wengine (wazazi, marafiki wa kike na marafiki wa kiume)<br />
(Sura ya 7 na 8 ).<br />
Ujinsia, ngono, na kutunza afya ya ujinsia.(Sura ya 9 na 10).<br />
Mimba na madawa ya kuzuia mimba (Sura ya 11).<br />
Kulazimishwa na kujamiiana (Sura ya 12).<br />
Madawa ya kulevya na pombe.(Sura ya 13).<br />
Kupanga maisha yako ya baadaye na kufikia malengo yako.(Sura ya 14).<br />
MaaDili<br />
Neno maadili lina maana ya mambo unayoyaamini, unayoyathamini na tabia unazodhani ni<br />
muhimu<br />
katika maisha yako. Maadili mema ni kama yafuatayo:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Kuwa mkweli.<br />
Uwazi.<br />
Uvumilivu.<br />
Ukarimu.<br />
Hisani/Wema.<br />
Kusamehe.<br />
Yaliyotajwa hapa juu ni machache tu kati ya maadili mema, waweza kuwa na mengine; kwa mfano<br />
kusoma kwa bidii, kusaidia wazazi, uaminifu kwa rafiki zako, kujitolea kwenye shughuli za jamii<br />
yako au za kidini.<br />
Maadili yanasaidia kuongoza matendo na maamuzi yako. Yanakusaidia katika kuchagua yaliyo<br />
mema kwako na kwa wengine. Kwa mfano, kijana mkarimu na mvumilivu atamsadia mwanafunzi<br />
mwenzie mlemavu au jirani yake aliyefanyiwa mabaya na watu wengine. Mtu mwaminifu<br />
atachagua kurudisha pesa za muuza duka alizomzidishia wakati akimpa chenji.<br />
Je, una maadili gani? Kipi ni kitu muhimu na chenye thamani kwako? Unaamini katika misingi gani<br />
ya maisha? Unaposoma kitabu hiki, jaribu kujiuliza kuhusu maadili yako.<br />
Kufahamu maadili yako kutakusaidia kufanya maamuzi makini ili uwe salama wakati wote wa<br />
mabadiliko ya ujana balehe.<br />
5
6<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Ukijua unachokithamini itakusaidia kuwa mkweli kwako binafsi, hata wakati mtu mwingine<br />
anapokulazimisha kufanya kitendo unachodhani ni makosa. Maadili yako yatakusaidia kuchagua<br />
lililojema kwako; ambalo wakati mwingine, baada ya kuchagua, itabidi uishi nalo daima.<br />
StaDi Za MaiSha<br />
Unahitaji stadi za maisha pia ili uwe salama. Kusema kweli<br />
“Stadi za maisha” zinaweza kuwa stadi za kuokoa maisha,<br />
kama vile uwezo wa :-<br />
Kuelezea hisia zako. Hisia zako ni muhimu, lakini watu<br />
wengine hawawezi kujua unavyojisikia mpaka uwaeleze.<br />
Jifunze jinsi ya kuwafanya watu wengine wajue kile<br />
unachofikiri na unachokitaka kwa kusema moja kwa<br />
moja na kutumia sentensi zinazoanzia na “mimi” – “mimi<br />
ninataka” “mimi ningelipenda” “mimi ninahitaji”“mimi<br />
Sipendi” ………… .” Fanya mazoezi ya kutumia sentensi<br />
zinazoanza na<br />
“mimi” mpaka utakapozoea na kujisikia huru kuzitumia.<br />
tetea hoja yako. Una uhuru wa kufikiri na kujihisi<br />
unavyopenda. Ni vema kujifunza jinsi ya kuwasilisha<br />
mawazo yako kwa wengine bila ya kuwaudhi au kuwafanya<br />
wajisikie vibaya, usionyeshe uadui, ugomvi wala kukosoa<br />
sana.<br />
tetea unachoamini bila kujali wanayosema watu wengine.<br />
Kila mtu ana imani na yaliyo sahihi na yasiyo sahihi, mazuri<br />
na mabaya. Imani hizi zinaitwa kanuni. Wakati mwingine<br />
unaweza ukawa unajua kanuni zako lakini mambo yanaweza<br />
yasiwe wazi sana kiasi cha kukufanya utumie muda<br />
kufikiria lipi ni sahihi kwako na ni kwa nini.<br />
Iwapo unao uhakika wa usahihi wa kile unachofikiria na kwa<br />
nini unakifanya, na kwa nini hupendelei kukifanya utaweza<br />
kusimama imara na lile unaloamini. Hivyo basi msimamo<br />
wa namna hii utakupa heshima mbele za watu.<br />
jihadhari na yanayotokana na shinikizo.<br />
Kuwa na msimamo wa pekee ndiyo<br />
stadi za <strong>Maisha</strong>.<br />
Jinsi unavyoelekea kwenye utu uzima unatakiwa kufanya maamuzi mengi peke yako. Wakati<br />
mwingine watu wengine wanaweza kukuhimiza na kukusukuma kufanya maamuzi fulani na<br />
ukushawishika kufanya hivyo.<br />
Lakini ufahamu kuwa kufanya maamuzi mazuri maana yake ni kupima chaguo zote zilizopo na<br />
kufikiria matokeo kwa kila chaguo.Inaweza ikawa kazi ngumu iwapo kuna mtu anakuharakisha au<br />
anakushinikiza uamue haraka. Kitu muhimu katika kufanya maamuzi bora ni kuwa na uhakika wa<br />
kanuni zako na malengo yako ya maisha kwa ujumla.<br />
SURA YA 1 | UJANA BALEHE: BADILIKO KUBWA CHANGAMOTO KUBWA<br />
Jambo lingine la muhimu katika kufanya<br />
maamuzi ni kujipa muda wa kutosha.<br />
Kumbuka,unaweza kumueleza mtu kwamba<br />
“ninahitaji kufikiria zaidi kuhusu jambo hili na<br />
nisubiri nitakujibu”<br />
Stadi hizi za maisha zina majina yake, kama<br />
vile “kuongea bila woga wala jazba”<br />
“Mawazo yenye ubunifu” “Kutatua matatizo”,<br />
“Kufanya maamuzi” na“Kujitambua”.<br />
Stadi za maisha ni muhimu sana. Ukweli ni<br />
kwamba stadi za maisha ni muhimu kama<br />
ilivyo kuufahamu “ukweli.” Kuufahamu “ukweli<br />
wa mambo” peke yake hakuwezi kukulinda<br />
hadi uwe pia na stadi za maisha. Kwa mfano<br />
unaweza ukafahamu kwamba kujamiiana bila<br />
kinga kunaweza kukusababisha mimba na<br />
magonjwa ya zinaa ikiwa ni pamoja na VVU/<br />
UKIMWI. Vilevile unaweza ukawa umeamua<br />
kwamba hutaki kujamiiana, lakini bado ukawa<br />
huna uwezo wa kujieleza na kutetea hoja zako<br />
kwa rafiki yako wa kiume.<br />
Unahitaji Stadi za maisha ili uutumie<br />
ukweli unaoufahamu kusimama imara<br />
katika yale unayoyataka na kuyaamini,<br />
hasa pale inapotokea watu unaowajali na<br />
kuwaheshimuwanatofautiana na wewe.<br />
je, unazo Stadi za maisha? Unaweza<br />
ukasimama imara na kuwa na msimamo kwa<br />
yale unayoyaamini kuwa ni sahihi hata kama<br />
marafiki zako wanawaza tofauti? Unao ujasiri<br />
wa kutosha kutetea afya yako au maisha<br />
yako? Anza kuzitumia stadi zako kadri<br />
unavyoendelea kusoma kitabu hiki.<br />
Kufanya maamuzi mazuri na kusimama imara kwa<br />
unachokiamini ni stadi bora za maisha<br />
7
8<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Mabadiliko ya mwili<br />
Wasichana na wavulana wengi wanabalehe kati ya umri wa miaka 10 na 16. Balehe ni kipindi<br />
ambacho unabadilika kimwili, kihisia/kifikra na kiakili kutoka utoto na kuingia utu uzima.<br />
MFOKO Wa uKuaji: MWanZO Wa balehe.<br />
Ipo tofauti ndogo sana kimaumbile kati ya wasichana na wavulana kati ya miaka 9 na 10.<br />
Japokuwa via vyao vya uzazi ni tofauti lakini vifua vyao na misuli vinafanana.<br />
Tofauti kubwa ya kimwili kati ya wasichana na wavulana huanza kujitokeza kipindi cha balehe.<br />
Kwa wastani wasichana wanaanza kuonyesha mabadiliko makubwa ya ukuaji kimwili kati ya umri<br />
wa miaka 10 au 11. Kipindi hiki cha kukua haraka kinaitwa mfoko wa ukuaji. Kwa wasichana kipindi<br />
hiki cha mfoko wa ukuaji hudumu miaka mitatu. Wakati huu wasichana wanakuwa warefu na<br />
wakubwa zaidi ukilinganisha na wavulana wa umri huo huo.<br />
Wavulana wanachelewa kidogo kufikia mfoko wa ukuaji kuliko wasichana, kwa wastani katika<br />
umri wa miaka 12 au 13. Kwa wavulana; mfoko wa ukuaji hudumu muda mrefu kuliko wasichana,<br />
ukweli ni kwamba wavulana wengine huendelea kukua mpaka wanapofikia miaka 19 au 20.<br />
Lakini kumbuka kwamba miaka hii ya ukuaji ni ya wastani tu.<br />
Vijana wengine huanza mfoko wa ukuaji mapema zaidi na wengine<br />
huchelewa. Kuanza mapema au kuchelewa hakuna athari yoyote<br />
katika namna utavyorefuka au namna utakavyokua haraka.Wale<br />
wanaoanza mapema, wengine wanakua haraka wakati wengine<br />
wanakuwa taratibu. Vile vile kwa wale wanaochelewa kuanza<br />
wengine wanakua haraka na wengine taratibu.<br />
Katika kipindi hiki cha makuzi ya haraka, mara nyingi wavulana<br />
na wasichana wanajisikia hovyo. Hii ni kwa sababu sehemu mbali<br />
mbali za mwili hukua kwa wakati tofauti na kwa kiwango tofauti.<br />
Mara nyingi, viganja vya mikono na nyayo huongezeka kwanza<br />
ikifuatiwa na mikono, miguu, kiuno/nyonga na kifua. Vijana<br />
wengi wanaokua haraka hujikuta mara nyingine wakiteguka na<br />
kuanguka. Inashangaza kujiona umeongezeka sentimeta kadhaa<br />
ghafla!<br />
Mfoko wa ukuaji<br />
Mfoko wa ukuaji<br />
9<br />
SURA YA 2
10<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Wavulana na wasichana wengine hukua haraka sana wakati wa balehe kiasi cha kwamba ngozi<br />
yao inashindwa kustahimili ukuaji haraka wa mifupa. Wakati mwingine inapotokea hivyo alama<br />
za misitari hutokea kwenye ngozi. Alama hizi zinaweza kupotea au zisionekane kiurahisi mtu<br />
anavyoendelea kukua, lakini zinaweza zisipotee moja kwa moja.<br />
Hata kama unajiona kukua haraka,bado balehe ni kitendo<br />
cha taratibu mno. Itachukua muda mrefu kabla hujawa<br />
mtu mzima kimwili na kifikra. Kwa wakati huu yafuatayo ni<br />
mambo ya kuzingatia.<br />
Kila Mtu YuKO tOFauti<br />
Kila mtu hufikia balehe kwa wakati tofauti na kwa kiwango<br />
tofauti. Matiti yako yanaweza kuchelewa kukua kuliko ya<br />
rafiki zako lakini wewe unaweza ukavunja ungo mapema<br />
au unaweza kuyapata yote haya baadaye sana. Matiti<br />
yanaweza yakakua na ukavunja ungo akiwa na umri wa<br />
miaka 12 na wewe matiti yanaweza kukua na ukavunja ungo<br />
ukiwa na umri wa miaka 15.<br />
Au kama wewe ni mvulana unaweza ukawa na rafiki yako<br />
ambaye sauti yake ili badilika kuwa nzito akiwa na umri wa<br />
miaka 13. Anaweza akawa ameota mavuzi na misuli wakati<br />
wewe hujakua hata sentimeta moja!<br />
Wavulana hawa wote wana umri wa miaka<br />
13,lakini wanakua kitofauti<br />
Wasichana hawa wote wana umri wa<br />
miaka 13,lakini wanakua kitofauti<br />
Kumbuka kila mtu yuko tofauti na kila yanapokutokea mabadiliko huu ndio wakati muafaka<br />
kwako.<br />
Kila Mtu ana MabaDiliKO YaKe<br />
Kwa kutumia kigezo cha afya, haitegemei kama mwili<br />
wako unakua haraka au taratibu kuliko rika lako.<br />
Mwili wako utabadilika muda utakapofikia. Hakuna<br />
unachoweza kufanya kuhusu muda wa mabadiliko.<br />
Wasichana na wavulana wengine wenye afya nzuri<br />
huchelewa kukua kuliko wenzao wa rika moja.<br />
Wasichana na wavulana wengine wanakua mapema<br />
kuliko wenzao wa rika moja na wala hawana kasoro<br />
yoyote na wana afya nzuri pia.<br />
Lakini hata hivyo unaweza kupata matatizo kama<br />
utakuwa tofauti na wengine.Kwa mfano: inaweza kuwa<br />
vigumu kwa msichana kuwa wa kwanza kuwa na matiti<br />
darasani, au mvulana kuwa wa mwisho kubadilika sauti.<br />
Hii inaweza kusababisha kutaniwa na unaweza kujisikia<br />
upo tofauti sana na kundi rika lako.<br />
SURA YA 2 | MABADILIKO YA MWILI<br />
Sherifan, kutoka Ghana (umri wa miaka 15)<br />
“Nilianza kuona mabadiliko katika mwili wangu nikiwa na miaka 11. Matiti<br />
yalianza kuota, nywele zikaota kwapani na kwenye via vya uzazi. Nilijisikia<br />
vibaya sana kwa sababu nilipata mabadiliko haya mapema sana na<br />
nilijiona niko tofauti sana na wenzangu wa rika moja”<br />
Sherry, kutoka Ghana (umri wa miaka 19)<br />
“Nilikuwa darasa la sita(6), sifahamu kama marafiki zangu walikuwa<br />
wanachelewa kukua au mimi nilikuwa nimewahi kukua, lakini nilijisikia<br />
vibaya matiti yalipoanza kukua. Niliwahi kumsikia mama akisema jinsi<br />
walivyokuwa wakitumia tapoli, “kifaa kidogo cha ubao kilichotumika kusaga<br />
pilipili”, kujaribu kuondoa uvimbe kwenye matiti wakati wa enzi zao.<br />
Kwa hiyo nilijaribu, kama mara tatu hivi. Lilikuwa ni jambo la kuchekesha,<br />
lakini hata hivyo haikusaidia kitu. Lakini sasa hivi waliokuwa wananitania<br />
wana matiti makubwa kuliko ya kwangu.”<br />
Kumbuka kuwa mambo haya yanaisha kadri muda unavyopita. Utakapofikisha miaka 20<br />
hakutakuwa na tofauti yoyote kwako au kwa mtu mwingine, iwapo sauti yako ilibadilika ukiwa na<br />
miaka 13 au miaka 17. Hakutakuwa na tofauti iwapo ulivunja ungo ukiwa na miaka 11 au miaka 16.<br />
Sherry, kutoka Ghana (umri; miaka 19)<br />
“Ebu tuyaache mambo yaende kama yalivyopangwa kwani hata kama<br />
hupendi huwezi kubadili kitu isipokuwa kujikubali tu.”<br />
Ingawa huwezi kuubadili mwili wako yapo mambo yanayokuhusu ambayo unaweza<br />
kuyabadili:<br />
1. Unaweza kuhakikisha kuwa wewe ni mtu mzuri. Hakikisha kuwa unafanya kazi kwa<br />
bidiii katika lolote utakalokuwa unafanya (shuleni, kazini na nyumbani). Unaweza<br />
ukakuza haiba yako, ucheshi wako,pia na tabia yako. Angalia kuwa wewe ni nani na<br />
unataka uweje baadaye na wala sio vile unavyoonekana.<br />
2. Jitahidi sana kutotilia maanani utani jaribu kupuuza na usiwaruhusu wanaokutania<br />
waone umefadhaika. Mwishowe watachoka kukutania.<br />
3. Heshima na kukubalika na rafiki zako visije vikakushawishi kufanya mambo ambayo<br />
sio mazuri kwako. Usiruhusu marafiki zako kukulazimisha kufanya mambo ambayo<br />
unajua sio sahihi, kama vile kutania watu wengine, kutumia madawa ya kulevya au<br />
kujiingiza kwenye mambo yanayoweza kukudhuru.<br />
4. Jielimishe mwenyewe kwa kutafuta taarifa sahihi. Hakihisha unafahamu wapi utapata<br />
taarifa unazozihitaji na majibu ya maswali yako yote wakati unapoupitia ujana<br />
11
12<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Pia, weka akilini haya: Watu wa umri wako mara nyingi wanajua taarifa nyingi za uongo kuliko za<br />
ukweli hasa inapokuwa ni za kuelezea balehe na kujamiiana. Marafiki zako wanaweza kukueleza<br />
mambo ambayo si ya kweli, hivyo unahitaji kufahamu wapi uende ili kupata ukweli. Kwa mfano,<br />
unaweza kuambiwa kwamba, matiti au uume utakua iwapo utajamiiana. Au unaweza kutaniwa<br />
kwamba matiti yako ni makubwa kwa sababu umekwishajamiiana. Hali kadhalika unaweza<br />
kusikia kwamba chunusi ni dalili za kwamba unatakiwa ujamiiane. Lakini hakuna lolote katika<br />
haya lenye ukweli. Yote ni uzushi/uwongo.<br />
Uzushi kama huu unaweza kuleta hatari zaidi kwa sababu unaongeza hofu. Uzushi kama huu<br />
unakufanya ufikirie kwamba unaweza kufanya mambo ili kubadilisha yale ambayo huwezi<br />
kuyadhibiti.<br />
VichOcheO (hOMOni)<br />
Ni kitu gani hudhibiti mabadiliko ndani ya mwili wako? Ni kitu gani hufanya ukue haraka au<br />
taratibu? Ni kitu gani hukufanya uongezeke?<br />
Mwili wako wakati wote unatengeneza homoni, ambazo ni kemikali tarishi maalumu ambayo<br />
huuambia mwili namna gani na lini ubadilike na kukua. Mfoko wa ukuaji wako husababishwa na<br />
homoni za ukuaji ambazo zinatoka kwenye ubongo kwa wingi.<br />
Pamoja na homoni za ukuaji, homoni za jinsi nazo huanza kutolewa wakati wa balehe. Kwa<br />
wasichana homoni za jinsia zinatengenezwa ndani ya ovari na kwa wavulana zainatengenezwa<br />
ndani ya korodani. Homoni za jinsi ndizo zinazosababisha tofauti katika maumbile ya mwanaume<br />
na mwanamke. Wasichana wanapoingia kipindi cha balehe nyonga zao huongezeka. Kawaida<br />
nyonga hukua haraka kuliko kifua . Nyonga ya msichana hupanuka na kujiviringa, na kiuno<br />
huonekana kidogo na chembamba. Matiti vilevile huanza kukua.<br />
Kwa wavulana, homoni za jinsia husababisha kifua kupanuka, mikono na miguu inakuwa minene<br />
yenye misuli. Matiti ya wavulana hayabadiliki sana kama ya wasichana yanavyobadilika wakati<br />
wa balehe, lakini hubadilika kidogo. Kwa wavulana wengine, matiti yao hukua kipindi cha balehe<br />
lakini kawaida hupotea kadri muda unavyokwenda.<br />
Homoni huathiri pia hisia zako. Vijana wengi hujisikia kuwa na hisia kali. Dakika moja tu anaweza<br />
kuwa na furaha na msisimko, lakini dakika inayofuata akawa na huzuni karibia kulia. Anaweza<br />
kujisikia vizuri siku moja na vibaya siku inayofuata. Mabadiliko haya katika hisia yanaitwa “hisia<br />
za kuyumba”.<br />
Kipindi cha balehe huwa kina ambatana na hisia kali<br />
SURA YA 2 | MABADILIKO YA MWILI<br />
Jambo hili huwatokea vijana wengi mara kwa mara. Wakati wa ujana balehe, utengenezaji wa<br />
homoni huongezeka ghafla, kitendo ambacho huwafanya vijana wengi wawe na hisia kali za aina<br />
mbalimbali.<br />
Baadaye katika maisha utengenezaji wa homoni utapungua na utajisikia unao uwezo wa kudhibiti<br />
hisia.<br />
Weka akilini kwamba mabadiliko yote ya kimwili, kihisia na kiakili yanayotokea wakati wa balehe<br />
yanasababishwa na homoni zinazotengenezwa na mwili wako. Hakuna unaloweza kufanya<br />
kuharakisha au kuchelewesha utengenezaji wa homoni. Jaribu kukumbuka tu kwamba wewe ni wa<br />
pekee na huna kasoro yoyote.<br />
Via VYa uZaZi “SeheMu Za SiRi”<br />
Pamoja na kuleta mabadiliko katika umbo la mvulana na msichana, homoni hufanya via vya<br />
uzazi kukua. Via vya uzazi maana yake ni zile sehemu za siri za mwili wako ambazo mara nyingi<br />
zinafunikwa na chupi/nguo za ndani.<br />
Kabla hujawa kijana balehe, sehemu za siri zilikuwa kwa ajili ya kujisaidia tu (kukojoa). Wakati wa<br />
ujana balehe hata hivyo, sehemu za siri zinakuwa kubwa. Kwa wasichana ngozi na tishu huwa laini<br />
na yenye mafuta mafuta, kwa wavulana uume huanza kurefuka na kunenepa. Korodani vilevile<br />
hukua na kuanza kutengeneza mbegu za kiume.<br />
Kipindi cha balehe via vya uzazi huanza kutengeneza majimaji pia.<br />
Wavulana huanza kutengeneza shahawa, majimaji yaliyo kama kamasi ambayo mbegu za kiume<br />
huogelea. Shahawa hutoka nje ya uume wakati mvulana anapofikia mshindo. Wasichana vilevile<br />
hutoa majimaji ya ukeni na damu ya hedhi. (soma sura ya 3 na ya 4 kwa maelezo zaidi kuhusu<br />
wavulana na wasichana)<br />
nYWele Za MWilini na MabaDiliKO Ya nGOZi<br />
Ngozi yako na nywele za mwilini hubadilika vilevile katika kipindi cha balehe. Kwa vijana wengi<br />
ngozi inakuwa na mafuta. Ngozi ya utotoni hupotea. Hii hupelekea chunusi kutoka, jambo ambalo<br />
ni tatizo la kawaida kwa vijana wengi (soma sura ya 5 kwa maelezo zaidi kuhusu utunzaji mzuri<br />
wa ngozi).<br />
Dalili nyingine ya balehe ni nywele kuota sehemu mpya za mwili. Wavulana na wasichana wote<br />
wanaweza kuota nywele kidogo miguuni na mikononi. Kwa kuongezea wavulana huota nywele<br />
sehemu za siri, usoni kifuani na kwapani. Wasichana vilevile huota nywele sehemu za siri na<br />
kwapani.<br />
Nywele zinazoota sehemu za siri zinaitwa mavuzi, watu wengine wana mavuzi mengi na wengine<br />
wanayo kidogo. Mavuzi husaidia kufanya eneo la via vya uzazi liwe safi, jambo ambalo ni zuri<br />
sana kwani ngozi inayozunguka via vya uzazi ni laini/nyororo sana na ni rahisi kuumia.Mavuzi<br />
husaidia kuzuia jasho na vitu vingine kutoka kwenye ngozi laini ya via vya uzazi.<br />
13
14<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Vijana wengine hawafurahii nywele mpya zinazoota mwilini hasa mavuzi yanapotokea kwa mara<br />
ya kwanza.<br />
Kumbuka ya kwamba mavuzi ni kitu cha asili na yana kazi yake, kwa hiyo iwapo unayo mengi au<br />
kidogo usihofu sana.<br />
Vilevile, nywele huota kwapani kipindi cha balehe, ingawa mara nyingi ni wakati wa mwisho<br />
wa kipindi cha balehe. Wasichana wengi hawaoti nywele kwapani mpaka baada ya matiti<br />
kuanza kuota na baada ya kuvunja ungo. Kwa wavulana nywele za kwapani kwa kawaida huanza<br />
kujitokeza mwaka mmoja au zaidi baada ya mavuzi kuota. Kama mavuzi, nywele za kwapani<br />
zina kazi maalum.Wakati wa balehe jasho linatoka sana na nywele husaidia kuzuia jasho lisitoke<br />
kwenye ngozi.<br />
Kwa kawaida,kwa wavulana, nywele za usoni huwa za mwisho kuota. Huanza kuota pembeni mwa<br />
midomo ya juu. Nywele zinazoota juu ya midomo ya juu (masharubu) huendelea kuota, na zingine<br />
huota sehemu ya juu ya kidevu na chini kidogo katikati ya midomo ya chini na mwisho zingine<br />
huota kwenye kidevu. Nywele hazioti kidevuni mpaka via vya uzazi vya mvulana viwe vimekomaa<br />
kabisa. Kwa wavulana wengi, nywele za usoni huanza kuota hasa wakiwa na umri kati ya miaka 14<br />
na 18.Lakini zinaweza kuanza kuota mapema zaidi au zikachelewa.<br />
uWeZO Wa KuFiKiRi<br />
balay, kutoka Kenya (umri, miaka 16)<br />
“Nilistushwa! Sikujua kama mtu anaweza kuota nywele<br />
sehemu zake za siri. Nilidhani ninaumwa, na nikamwuliza<br />
mama ambaye alinihakikishia kwamba ilikuwa ni jambo la<br />
kawaida.”<br />
Diana, kutoka Zambia (umri, miaka 17)<br />
“Zilipoota, nilijisemesha mwenyewe kwamba itabidi<br />
nikubaliane na hali halisi”<br />
Doglas, kutoka Zimbabwe (umri miaka 12)<br />
“Yalipoota mavuzi haikunifurahisha yalinifanya nionekane<br />
mbaya”<br />
bernard, kutoka Kenya (umri, miaka 17)<br />
“Marafiki zangu walinicheka ati kwa sababu mavuzi yalikuwa<br />
hayajaota.”<br />
Wakati mabadiliko dhahiri yanayotokea katika mwili kipindi cha balehe, akili nayo pia hubadilika<br />
bila ya kutambulika kiurahisi.Katika kipindi cha ujana balehe, uwezo wa akili unaongezeka sana<br />
hasa katika kufikiri kwa makini na kutoa maoni ya kina. Matokeo ya mabadiliko haya husababisha<br />
utambulisho binafsi kuanza kujengeka.Unaanza kujiona kama mtu wa kipekee. Unapenda kufikiri<br />
mwenyewe na kufanya maamuzi yako binafsi.<br />
SURA YA 2 | MABADILIKO YA MWILI<br />
Mara nyingi, kwa mara ya kwanza utayaona mambo tofauti na wazazi wako wanavyoyaona.<br />
Unaweza kujisikia kutaka kujua imani za wazazi wako na sababu zake. Unaweza kutaka kujaribu<br />
kuishi maisha yako mwenyewe kuliko kutegemea ya kuambiwa na wengine. Unaweza kujaribu<br />
mambo mapya mwenyewe na wakati mwingine kujaribu mambo ya hatari.<br />
Mabadiliko yote haya ya akili ni dalili nzuri za kuonyesha kwamba unaingia utu uzima.<br />
Hata hivyo haina maana ya kwamba tayari umeishakuwa mtu mzima. Ingawa uwezo wako<br />
wa kiakili unaongezeka sana, bado kuna mambo mengi unakuwa hujayajua. Ukweli hutaweza<br />
kuyajua yote, kwa hiyo ni muhimu kujua wapi uende na umwone nani kwa ajili ya taarifa<br />
unayoihitaji. Kutakuwepo wakati ambapo itakuwa muhimu kutumia uzoefu na maarifa kutoka<br />
kwa waliokuzidi umri. Hivyo basi unatakiwa kuuliza maswali, usidhani unayo majibu yote. Jitahidi<br />
kujifunza mengi iwezekanavyo.<br />
Vijana wengine hutaniwa wanapokuwa wameota mavuzi au wanapokosa kuota.<br />
15
16<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Sura ya 2<br />
MabaDiliKO KatiKa MWili WaKO<br />
Ujana, ambao kawaida huanzia umri kati ya miaka 10 na 16 ni mabadiliko ya hatua kutoka<br />
utoto kuingia utu uzima. Kila mtu anaanza kubadilika wakati wake. Wakati watu wengine<br />
hukua haraka zaidi, wengine hukua taratibu. Tunatofautiana, na hakuna unaloweza kufanya<br />
kuthibiti muda wa mabadiliko hayo.<br />
Ni yapi uyategemee unapobadilika kutoka msichana na kuwa mwanamke au kutoka<br />
mvulana na kuwa mwanaume?<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Mfoko wa ukuaji; viganja, nyayo, miguu, mikono, nyonga kifua vyote vitaongezeka<br />
ukubwa mwili utatengeneza homoni, kemikali maalumu ambazo hutoa ujumbe namna<br />
mwili utakavyokua na kubadilika.<br />
Via vya uzazi (au sehemu za siri) vitakuwa vikubwa na vitaanza kutengeneza majimaji<br />
(giligili).<br />
Ngozi inaweza kuwa na mafuta zaidi.<br />
Utaanza kuota mavuzi na nywele kidogo kwapani, miguuni, mikononi na kama ni<br />
mvulana, usoni pia.<br />
Utaanza kupata hisia nzito mbali mbali.<br />
Uwezo wa kufikiri utaongezeka.<br />
Bila ya kujali mabadiliko yanatokea haraka au taratibu, wakati gani yanaanza, jaribu<br />
kukumbuka kwamba mabadiliko haya ni ya kawaida na hayana kasoro yoyote.<br />
Inaweza kuchukua muda mrefu kuyazoea mabadiliko haya kwa hiyo kuwa mvumilivu na<br />
usihofu.<br />
Wavulana<br />
Katika sura ya pili umesoma baadhi ya mabadiliko kadhaa ambayo wavulana wanayapata katika<br />
kipindi cha balehe. Sura hii itakupa maelezo zaidi kuhusu mabadiliko haya.<br />
uMbO na uKubWa Wa MWili<br />
Mfoko wa ukuaji kwa wavulana wengi unaanza kati ya miaka 12 na 13. Hata hivyo wavulana<br />
wengine wanaanza ukuaji mapema zaidi na wengine wanachelewa. Wakati wa mfoko wa ukuaji,<br />
mwili wako utaanza kuwa mrefu zaidi na mkubwa.<br />
Sehemu mojawapo ya mwili wako itakayoanza kukua ni miguu. Ukweli ni kwamba, mifupa ya<br />
miguu inakua haraka zaidi kuliko sehemu zingine za mwili. Hivyo basi miguu inaweza kukua hadi<br />
mwisho kabla ya sehemu zingine kukua sana. Iwapo utajisikia kama vile unakuwa mzito ghafla,<br />
inawezekana ni kwa sababu ya miguu yako imekuwa mikubwa kuliko ilivyokuwa muda mfupi<br />
uliopita. Unatakiwa kuwa mvumilivu kwani hali hii inaweza kukuchukua muda kabla hujaizoea<br />
Mifupa mingine ya mwili nayo itakuwa zaidi kuliko mingine na kusababisha umbo la mwili<br />
kubadilika. Kwa mfano, mabega yatakua zaidi wakati nyonga inaweza kukua kidogo tu. Nyonga<br />
yako inaweza kuonekana nyembamba ukilinganisha na upana wa mabega. Inawezekana miguu na<br />
mikono ikakua zaidi kuliko uti wa mgongo, hivyo basi miguu inaweza kuwa mirefu ukilinganisha<br />
na kifua au kiwiliwili. Matokeo yake umbo lako litakuwa tofauti sana na lile la mvulana mdogo.<br />
Misuli vile vile inakuwa, hasa ile ya miguuni na mikononi. Kadri misuli inavyokua, ndivyo<br />
unavyokuwa na nguvu zaidi. Mlundikano wa misuli na mafuta utasababisha kifua kuwa kikubwa.<br />
Vile vile wavulana wengi hugundua kwamba kuna mabadiliko ya chuchu na matiti katika kipindi<br />
cha balehe. Chuchu huongezeka na kuwa kubwa kidogo. Miduara inayozinguka chuchu nayo huwa<br />
mikubwa na rangi yake kuwa nyeusi kidogo.<br />
Wavulana wengine wanajikuta matiti yao yamevimba na yanauma. Kwa wachache, uvimbe<br />
huzidi, hivyo kuwasababishia wasiwasi kuwa wataota matiti makubwa kama wanawake. Usiwe<br />
na wasiwasi, haya ni mambo ya kawaida uvimbe na ulaini unasababishwa na homoni ndani ya<br />
mwili. Uvimbe unaweza ukadumu mwaka mmoja au mwaka mmoja na nusu, lakini baada ya hapo<br />
hupungua kwa vile mwili unaacha kutengeneza homoni nyingi.<br />
Wakati wa mabadiliko yote haya unatakiwa kuwa mvumilivu kwani mwili wako hauna matatizo<br />
yoyote, na wewe ni wa kawaida kabisa. Hata kama hukui haraka ukilinganisha na rafiki zako<br />
wanavyokua, usiwe na wasiwasi utakua tu, muda bado. Ni wakati gani unaanza kukua na kiasi<br />
gani utakua,inategemea sifa bainifu unazorithi kutoka kwa wazazi wako. Hata ukichelewa<br />
17<br />
SURA YA 3
18<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
kuanza kukua, unaweza kujikuta wewe ni mrefu kuliko wavulana wengine waliopata msukumo wa<br />
ukuaji mapema.<br />
Sauti YaKO<br />
Sauti yako ni dalili nyingine ya uhakika kwamba unaingia kipindi cha balehe. Sauti huanza<br />
kubadilika baada ya mfoko wa ukuaji kuanza, kwa kawaida ni katika umri wa miaka 14 au 15.<br />
Sauti ya wavulana hubadilika kuwa ya chini na nzito katika kipindi cha balehe, kwa sababu ya<br />
homoni inayoitwa “testosterone”.Aina hii ya homoni husababisha zoloto (sehemu ya mwanzo wa<br />
koromeo inayohusika na utoaji wa sauti) kuwa kubwa. Kwa jinsi nyuzi za sauti zinavyokuwa nene<br />
na ndefu ndivyo sauti inavyokuwa ya chini na nzito.<br />
Precious, mvulana kutoka Ghana (umri, miaka 15 )<br />
“Kitu cha kwanza nilichogundua ni kukatika kwa sauti, kupanuka kifua<br />
na mabega. Nilifurahi kwa sababu niliona kwamba sasa ninakuwa<br />
kijana balehe.”<br />
Panaito, kutoka Kenya.<br />
“Nilipata mabadiliko ya sauti mara baada ya kupata ndoto nyevu.”<br />
aloysious kutoka uganda (umri, miaka 19)<br />
“Sauti yangu ilipobadilika nikiwa na umri wa miaka 15. Nilitambua kuwa<br />
nilikuwa ninakua. Nilikua haraka sana na nilifurahi.”<br />
Dalili ya kwanza kuonyesha kwamba sauti yako inabadilika ni kuanza kukwaruza kwa sauti<br />
ghafla. Wavulana wengine hujisikia vibaya sauti zao zinapoanza kukwaruza, kwa vile mara nyingi<br />
haitabiliki itaanza lini.<br />
Sauti huwa ya kawaida na kubadilika katika muda mfupi. Mara inakuwa ya kawaida, dakika<br />
chache baadaye inakuwa ya juu na nyembamba.<br />
SURA YA 3 | WAvULANA<br />
Via VYaKO VYa uZaZi (SeheMu ZaKO Za SiRi)<br />
Uume umetengenezwa na misuli inayozunguka mrija mwembamba. Mrija huu hupitisha mkojo na<br />
shahawa. Uume una kichwa na mwili.Mwili au mpini ni ile sehemu ya uume kama bomba. Kichwa<br />
ni ile sehemu ya juu ya uume. Ni sehemu ambayo ina hisia kali na inahitaji uangalifu mkubwa.<br />
Unapozaliwa kichwa cha uume kinakuwa kimefunikwa<br />
na ngozi nyembamba iliyojikunja. Ngozi hii inaitwa<br />
“govi” Jamii nyingi za Afrika huondoa govi kwa njia<br />
ya upasuaji. Kitendo hiki kinaitwa “kutahiri”. (Angalia<br />
ukurasa wa 20 kwa maelezo zaidi kuhusu kutahiri.)<br />
Ukubwa wa uume unatofautiana kati ya mwanaume na<br />
mwanaume na hauna uhusiano kabisa na ukubwa wa<br />
mwili. Mara nyingi, jinsi uume unavyokuwa mkubwa<br />
ukiwa laini ndivyo unavyoongezeka kidogo unapokuwa<br />
umedinda. Vivyo hivyo, kama ni mdogo unapokuwa<br />
laini unaweza kuongezeka zaidi unapokuwa umedinda.<br />
Vijana wengi wa kiume, “hata wanaume wakubwa”<br />
wanatumia muda mwingi kufikiri na kuwa na wasiwasi<br />
kuhusu uume wao. Je ni mdogo sana? Kwa nini<br />
umepinda kuelekea huku? Je, kuna tatizo lolote?<br />
Sehemu za siri za mwanaume kwa ndani<br />
aloysius kutoka uganda (umri, miaka 19)<br />
“Wakati mwingine tulikuwa tunavuta uume na kulinganisha nani<br />
anao mkubwa zaidi?!”<br />
Iwapo umewahi kujishangaa kama uume wako una ukubwa wa kutosha, kumbuka tu kwamba<br />
tendo la ngono halitegemei ukubwa wa uume. Kwa uhakika ni kwamba ukubwa wa uume hauna<br />
athari zozote kwa mwanamke katika kufurahia tendo la kujamiiana (ngono).<br />
Ukweli ni kwamba kufurahia ngono kwa wanawake na wanaume wengi kunategemea zaidi jinsi<br />
gani kila mmoja wapo anavyompenda mwenzie. Kilicho cha muhimu ni mahusiano na wala sio<br />
ukubwa wa uume.<br />
Kinachoning’inia chini ya uume ni mapumbu. Pumbu ni kama mfuko au kifuko cha ngozi<br />
kinachoshikilia korodani au makende, ambako mbegu za kiume hutengenezwa tangu kipindi<br />
cha balehe hadi uzeeni. Ngozi ya mapumbu ina nywele kidogo na mafuta. Hudaka uchafu ambao<br />
kama haukusafishwa husababisha harufu mbaya.<br />
Katika kipindi cha utoto, mapumbu hujikunja na kuwa karibu na mwili. Lakini, kadri unapopitia<br />
balehe, mapumbu huanza kulegea na kuning’inia chini, ingawa ukijisikia baridi au kuogopa au<br />
kuwa na hamu ya kujamiiana, mapumbu yako yanaweza kujikunja na kurudi karibu na mwili.<br />
Mapumbu yananing’inia chini kwa sababu korodani zinahitaji kuwa katika hali yenye joto chini ya<br />
joto la mwili ili kutengeneza mbegu za kiume.<br />
19
20<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Tohara ni kitendo cha kuondoa ngozi iliyojikunja inayozunguka kichwa cha uume. Ngozi hii huitwa<br />
govi, hufunika kabisa kichwa cha uume lakini inaweza kuvutwa chini ya “mpini” (shafti).<br />
Kufuatana na mila na desturi za waafrika, pamoja na dini fulani fulani kama vile Waislamu na<br />
Wayahudi, watoto wanatahiriwa wakiwa na umri wa siku chache. Katika desturi nyingine za Afrika,<br />
wavulana wanatahiriwa wanapofikia balehe, utaratibu huu unachukuliwa kama utaratibu wa mpito<br />
kutoka utoto kwenda utu uzima.Zipo tamaduni nyingine Afrika ambazo mila haziruhusu kutahiri<br />
kabisa.<br />
Hakuna ubaya wowote wa kutahiri au kutokutahiriwa. Kutahiriwa ni utaratibu wa kidini au<br />
kiutamaduni/kimila. Iwapo katika jamii yenu hawatahiri ni sawa sawa tu.<br />
Je, kutahiri kunaleta tofauti zozote katika hisia ya kujamiiana? Ni vigumu sana kujua jambo<br />
hili kwani kila mwanaume anayo namna yake ya kujisikia. Lililo la uhakika ni kwamba wote,<br />
aliyetahiriwa na asiyetahiriwa wanaweza kufurahia ngono na wanaweza kuwafurahisha wapenzi<br />
wao.<br />
Wakati kutahiri ni utaratibu wa kidini au kimila/ kiutamaduni, watu wengine wanaamini kwamba<br />
kuna faida za kiafya iwapo mwanaume ametahiriwa kwa sababu ni rahisi kusafisha uume wake.<br />
Lakini zipo sababu zingine za kiafya zinazoweza kusababisha watu kutahiriwa. Wapo wavulana na<br />
wanaume wengine ambao govi linakuwa limeshikana sana na kichwa cha uume kiasi cha kwamba<br />
inawia vigumu kuivuta kwa chini. Hii inaweza kusababisha kuvimba kwa uume na maumivu<br />
makali. Namna pekee ya kutatua tatizo hili ni kutahiri.Watu wengine wanafikiri kwamba kutahiri<br />
kunasaidia kuzuia maambukizi ya VVU/UKIMWI na magonjwa mengine ya ngono. Ukweli ni<br />
kwamba, hata kama umetahiriwa unaweza kupata maambukizi ya VVU/UKIMWI na magonjwa ya<br />
ngono. Unashauriwa kufanya mapenzi salama wakati wote.<br />
Mambo yote haya yana maana gani kwako? Kama utamaduni wako hauruhusu wavulana kutahiriwa,<br />
Je, ungependa utahiriwe ili iwe rahisi kuuweka uume wako msafi? Jibu ni hapana unachotakiwa ni<br />
kuwa msafi, kumbuka kusafisha kwa ungalifu chini ya govi. Kwa kawaida haya ndiyo unayotakiwa<br />
kuyafanya. Hata hivyo wavulana ambao hawawezi kuviringisha govi na wale ambao husikia<br />
maumivu uume unapodinda, wanashauriwa kumweleza mfanyakazi wa afya kwa ushauri zaidi.<br />
Sasa hivi watu wengi wanatahiriwa katika vituo vya afya. Lakini sehemu nyingine wanatahiri<br />
wataalamu wa kienyeji (mangariba) kama sehemu ya sherehe. Wakati wowote inapotokea hivyo,<br />
inatakiwa vitumike vyombo visafi, vilivyochemshwa, ili kuua vijidudu kila baada ya kumtahiri<br />
mtu mmoja. Ni hatari sana kutumia kisu kimoja kutahiria wavulana wengi kwa sababu kama<br />
mmojawapo atakuwa na maambuziki ya VVU, kisu kinaweza kueneza maambukizi kwa wavulana<br />
wengine.<br />
Iwapo utatahiriwa kimila, hakikisha utaratibu wa kisasa unatumika ili kuzuia maambukizi ya VVU<br />
na magonjwa mengine yanayotokana na damu. Usikubaliane kabisa na mila/desturi na utamaduni<br />
utakaosababisha maambukizi ya VVU. Taratibu hizo zinaweza kubadilishwa ukawa salama.<br />
Kwa mfano, watu wa Mbale, Uganda walichukua hatua zifuatazo ili kuhakikisha wanatahiri<br />
kiusalama:<br />
• Kila aliyetaka kutahiriwa alilazimishwa kuja na kisu chake.<br />
• Lazima kisu kichemshwa kabla ya kutumika.<br />
• Lazima Mangariba waoshe mikono yao kwa uangalifu kabla na baada ya kumtahiri kila mtu.<br />
MaZOeZi Ya uSaFi<br />
SURA YA 3 | WAvULANA<br />
JE UNAFAHAMU KUHUSU TOHARA? Je, ulikuwa unajua kwamba kuna uzushi mwingi kuhusu uume?<br />
Yafuatayo ni maelezo mbalimbali ya uzushi kuhusu uume:<br />
1. Iwapo huufanyii mazoezi uume kwa kujamiiana, uume wako hautafanya kazi na utakuwa<br />
mdogo. huu ni uongo! Kujamiana sio “mazoezi” ya uume. Uume hauhitaji mazoezi yoyote.<br />
Utafanya kazi vizuri bila hata ya kujamiiana.Kutojamiiana au subira kamwe haviwezi<br />
kuudhuru uume wako.<br />
2. Uume unaongezeka ukubwa kila unapofanya ngono mara nyingi. Sio kweli! Ukubwa wa<br />
uume wako utategemea sifa urizorithi kutoka kwa wazazi wako, na wala sio unachofanya<br />
na uume wako.<br />
3. Uume mdogo hauwezi kumridhisha mwanamke. Sio kweli! Ukubwa wa uume unaathari<br />
ndogo sana kwa mwanamke kufurahia ngono. Hii ni kwa sababu hisia za kutaka kujamiiana<br />
kwa mwanamke zipo kwenye kinembe na eneo linalozunguka uke.Uke wenyewe hauna<br />
mishipa mingi ya fahamu kwa hiyo haujisikii sana<br />
4. Wavulana wenye uume mdogo hawawezi kutumia kondomu. Sio kweli! kondomu<br />
zimetengenezwa kwa jinsi ya kubana, hivyo kila mtu anaweza kuzitumia vema.<br />
5. Lazima ujamiiane kila uume unapodinda. Si kweli! Kwa vyovyote vile hii sio kweli kabisa.<br />
Kwa mfano utafanya nini kama uume wako ungedinda darasani? Uume utalegea wenyewe.<br />
Kamwe huwezi kudhurika kwa kutokufanya ngono uume unapokuwa umedinda.<br />
6. Wavulana wenye dole gumba kubwa wana uume mkubwa. Sio kweli! Watu wengi husema<br />
mambo kama haya ikiwa ni pamoja na wavulana wenye pua kubwa, miguu mikubwa,<br />
masikio n.k, lakini sio kweli. Hakuna mahusiano yoyote kati ya ukubwa wa uume na viungo<br />
vingine vyovyote vya mwili wako. Hakuna jinsi unavyoweza kufahamu ukubwa wa uume<br />
kwa kumwangalia tu.<br />
7. Mbegu za kiume zikizidi zinasababisha mgongo kuuma, kichaa, kichwa kuuma, kuwa<br />
hanithi na kuota chunusi. Sio kweli! Hata kama korodani zinatengeneza mamilioni ya<br />
mbegu za kiume, haiwezekani mbegu hizo kujazana na kusababisha matatizo. Zaidi ya<br />
hapo mbegu za kiume haziwezi kwenda sehemu nyingine ya mwili.<br />
8. <strong>Ndoto</strong> nyevu ni dalili ya kwamba unahitaji kujamiiana. Sio kweli! <strong>Ndoto</strong> nyevu ni njia<br />
mojawapo ya mwili kupunguza mbegu za kiume na shahawa. Sio dalili ya kwamba unahitaji<br />
kujamiiana. Mwili wako unaweza kujirekebisha wenyewe bila ya wewe kujihatarisha kwa<br />
vyovyote vile.<br />
Ni muhimu kuosha na kusafisha uume wako kila siku, uwe umetahiri au la. Hii ni lazima iwe<br />
desturi kama unavyofanya kwa sehemu nyingine za mwili wako. Unatakiwa vile vile kuosha<br />
mapumbu, katikati ya mapumbu na mapaja na katikati ya matako.<br />
Kama hujatahiriwa, unatakiwa kurudisha nyuma govi na kusafisha eneo hilo kwa utaratibu.<br />
Unaweza kuhisi viuvimbe vidogo mwanzoni mwa kichwa cha uume viuvimbe hivyo ni matezi<br />
yanayotoa majimaji meupe yanayoitwa smegma. Smegma inasaidia govi kuteleza nyuma<br />
kiulaini. Hata hivyo, iwapo Smegma itajaa chini ya govi inaweza kusababisha harufu mbaya au<br />
maambukizi. Ni muhimu wakati wote eneo la chini ya govi liwe ni safi .<br />
21
22<br />
KuDinDa KWa uuMe<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
iwapo hujatahiriwa rudisha nyuma govi na safisha taratibu chini yake.<br />
Kwa kawaida uume ni laini na huninginia chini. Wakati unadinda, damu nyingi huelekea kwenye<br />
uume isivyo kawaida na damu kidogo hurudi. Hii husababisha uume kuwa mkubwa na mgumu,<br />
na kusimama. Uume uliodinda kwa kawaida hujikunja kidogo kuelekea juu, na unaweza kujikunjia<br />
upande mmoja.<br />
Uume unapokuwa umedinda unaweza ukashindwa kukojoa kiurahisi kwa sababu msuli hufunga<br />
kibofu cha mkojo. Itakubidi usubiri uume ulegee ndipo ukojoe.<br />
Uume unaweza kudinda iwapo utaguswa au kushikwa shikwa, au wakati umepata mhemuko wa<br />
kutaka kujamiiana au kwa kumuona mtu anayekuvutia. Uume unaweza kudinda kwa sababu ya<br />
kuwa na wasiwasi na mfadhaiko. Ni kawaida kwa wavulana kuamka asubuhi na uume uliodinda.<br />
Ukiwa usingizini uume unaweza kudinda mara 5 mpaka 7. Hii ni kawaida kabisa na haina madhara<br />
yoyote.<br />
Kudinda kwa Uume kunawatokea wanaume wote wa umri mbalimbali ikiwa ni pamoja na watoto<br />
wadogo na wazee. Wakati mwingine wavulana huhofu wanapodindisha mara kwa mara. Hali hii<br />
inawasumbua wakiwa darasani, ndani ya basi au hata wakati wa matembezi. Wakati mwingine<br />
zipo sababu za msingi za uume kudinda, kwa mfano, unaweza ukawa umekaa karibu na mtu<br />
anayekuvutia. Hata hivyo, kuna wakati uume unadinda bila sababu yoyote ya msingi.<br />
nfune kutoka Zambia (umri wa miaka 13)<br />
“Kudindisha kwa uume hakuzuiliki na hutokea mara kwa mara.<br />
Wakati mwingine ni dalili ya kuonyesha una msisimko wa<br />
kutaka kujamiiana. Hali hii naichukia sana hasa ninapokuwa<br />
shuleni au hadharani.”<br />
Tafadhali usiwe na wasiwasi, wewe ni wa kawaida, mwenye afya na homoni nyingi. Unaweza<br />
kufedheheka ikitokea darasani au hadharani, lakini wakati wote ni wewe peke yako unayefahamu<br />
kwamba umedindisha.<br />
Wakati mwingine wavulana wanadhani njia pekee ya kuthibiti uume kudinda ni kufanya ngono<br />
Hii sio kweli ni uzushi ikiwa ni sababu ya wavulana kufanya ngono. Uume kudinda sio dalili ya<br />
kwamba unahitaji kufanya ngono, la hasha.<br />
KuMWaGa Manii “KuKOjOa”<br />
SURA YA 3 | WAvULANA<br />
Unapofikia balehe unaweza kuanza kuona majimaji yenye rangi ya maziwa ambayo yananata na ni<br />
mazito, sio mepesi kama mkojo.<br />
Majimaji kama ute hutoka kupitia kwenye uume wakati mwanaume anapofikia mshindo. Kukojoa<br />
manii ni kilele cha msisimko wa kijinsia, wakati mwanaume anapokuwa amedindisha uume.<br />
Kumbuka ya kwamba sio lazima kukojoa manii kila uume unapokuwa umedinda. Kama utasubiri,<br />
uume utalegea wenyewe bila hata ya kukusababishia madhara yoyote.<br />
Majimaji kama ute yametengenezwa na vitu viwili. Karibia 10% ya majimaji ni mamilioni ya<br />
mbegu za kiume. Mbegu za kiume ni ndogo sana kiasi ambacho hatuwezi kuziona kwa macho<br />
labda kwa darubini. Ukiziona zinaonekana kuwa na kichwa cha mviringo na mkia mrefu na<br />
mwembamba.<br />
Asilimia 90 ya ute huo ni majimaji yenye rangi ya maziwa yanayoitwa shahawa. Shahawa<br />
huwezesha mbegu za kiume kuogelea na pia huzipa chakula na kuziwezesha kuwa hai. Shahawa<br />
sio chakula kwa wasichana, kama watu wengine wanavyozusha.<br />
Mbegu za kiume zinatengenezwa katika Korodani/Makende (angalia kielelezo uk 19). Shahawa,<br />
ambazo ni majimaji yenye rangi nyeupe/maziwa zinatengenezwa kwenye vifuko vya shahawa.<br />
Hizi ni tezi zilizopo nyuma ya kibofu cha mkojo. Mwanaume anapofikia mshindo mbegu za kiume<br />
zinachanganyika na shahawa kutoka kifuko cha shahawa. Mchanganyiko huu huitwa manii. Manii<br />
hupitia kwenye mirija ya kupitishia mbegu na kutoka nje ya uume kupitia kwenye tundu dogo<br />
lililopo kwenye kichwa cha uume.<br />
Inaweza kuonekana kana kwamba manii nyingi hutoka wakati mwanaume “anapokojoa” Ukweli<br />
ni kwamba kiasi kinachotoka ni kama kijiko kidogo cha chai kilichojaa. Usije ukadharau uwezo<br />
wa hiki kijiko kidogo cha chai kilichojaa manii;<br />
kinaweza kuwa na mbegu za kiume karibia<br />
milioni mia tano!. Kila mojawapo ya mbegu<br />
hizo inaweza kumfanya msichana apate mimba.<br />
Unapofikiria mbegu za kiume zipatazo milioni<br />
mia tano, utaelewa ni kwa namna gani msichana<br />
anavyoweza kupata mimba kirahisi.<br />
Iwapo mvulana au mwanaume ana maambukizi<br />
ya VVU, kijiko cha chai kimoja kilichojaa<br />
shahawa kinaweza kuwa na mamia kwa maelfu<br />
ya virusi vinavyosababisha UKIMWI.<br />
Mbegu ya kiume<br />
Kijiko kidogo cha chai kilichoja shahawa kina<br />
mamilioni ya mbegu za kiume na kinaweza kuwa na<br />
VVu iwapo mvulana atakuwa ana maambujizi.<br />
23
24<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Wavulana wengi wanakuwa na wasiwasi kwamba kondomu haiwezi kuhifadhi mbegu za kiume<br />
zipatazo milioni 500. Lakini mbegu za kiume ni ndogo sana na kwa hiyo kondomu inaweza<br />
kuzizuia zote ili mradi inavaliwa kwa usahihi (angalia sura ya 10 kwa maelezo zaidi kuhusu<br />
kondomu).<br />
Wavulana wengine wanakuwa na wasiwasi kwamba wakikojoa manii mara kwa mara<br />
watapunguza kiasi cha shahawa mwilini mwao. Wasiwasi wa kwamba wanaweza kuishiwa<br />
shahawa na hivyo kutokuwanazo za kutosha watakapozihitaji. Hili haliwezi kutokea hata mara<br />
moja kwani mwanaume anatengeneza mbegu za kiume na shahawa tangia kipindi cha balehe<br />
mpaka siku anayokufa.<br />
Vilevile kumbuka ya kwamba haiwezekani mbegu za kiume na shahawa zikalundikana au<br />
zikajenga shinikizo mwilini. Mwili wako ni kama mashine iliyokamilika, unazo njia za kuondoa<br />
mbegu za kiume na shahawa inayozidi, mojawapo ni ndoto nyevu.<br />
nDOtO nYeVu (“KuKOjOlea” KitanDani)<br />
Wakati mwingine wavulana wanakojoa manii<br />
kitandani wakiwa usingizini.Kitendo hiki kinaitwa<br />
“ndoto nyevu” wavulana wengi wanapopata ndoto<br />
nyevu huwa inakuwa ni mara yao ya kwanza shahawa<br />
kutoka mwilini mwao. Wanaweza kuamka na kukuta<br />
doa bichi kitandani au kwenye nguo.<br />
Kama hufahamu lolote kuhusu ndoto nyevu unaweza<br />
kuchanganyikiwa na kuwa na wasiwasi. Unaweza<br />
kufikiri umekojoa kitandani au damu inakutoka au<br />
unaumwa, lakini utaona kwamba majimaji yana rangi<br />
ya maziwa/meupe, na sio kama damu au mkojo.<br />
ndoto nyevu kwa mara ya Kwanza<br />
<strong>Ndoto</strong> nyevu hutokea usingizini tu. Ukisinzia kidogo mchana unaweza kupata ndoto nyevu, lakini<br />
wavulana wengi hupata ndoto nyevu usiku wakiwa usingizini. Wavulana wengi wanapojikuta<br />
wamekojoa manii huwa wanakumbuka kwamba walikuwa wanaota ndoto zinazohusiana na<br />
mapenzi. Lakini unaweza kupata ndoto nyevu hata kama hujaota ndoto za mapenzi.<br />
Karibu wavulana wengi wanafedheheka wakipata ndoto nyevu. Ni sahihi kufedheheka, lakini<br />
kumbuka ya kwamba ndoto nyevu ni za kawaida wakati wa ujana balehe. Vijana balehe wengi<br />
wanapata ndoto nyevu ingawa sio wote.<br />
Mvulana hawezi kujizuia kupata ndoto nyevu; ni za asili na ni za kawaida. Ni njia ambayo mwili<br />
unatoa nafasi kwa ajili ya mbegu za kiume mpya kutoka kwenye korodani. Kupata ndoto nyevu<br />
haimaanishi uanze kujamiiana.<br />
SURA YA 3 | WAvULANA<br />
adamu, kutoka uganda (umri, miaka 13)<br />
“Sidhani kupata ndoto nyevu kunamaanisha ninatakiwa kujamiiana. Ni<br />
kukua tu. Ninaona aibu tu kwa vile inabidi nibadilishe mashuka kila baada<br />
ya siku moja.”<br />
Wavulana wengine wanapoanza kupata ndoto nyevu wanaona ni tukio kubwa sana ambalo<br />
wanalifurahia.<br />
Panaito kutoka Kenya<br />
“Nilipopata ndoto nyevu kwa mara ya kwanza nilijisikia kama nimekomaa<br />
kijinsi. Nilifurahi kuwa mmojawapo wa wale ambao tayari walishapata.<br />
Lakini ningelikuwa sijapata taarifa, ningeweza hata kwenda kumuona<br />
daktari,ninamshukuru Mungu kwamba nilijua kilichokuwa kinatokea”.<br />
adamu kutoka uganda (umri, miaka 13)<br />
“Nilipopata ndoto nyevu kwa mara ya kwanza nilimwambia kaka yangu mkubwa<br />
ambaye alinihakikishia kwamba ilikuwa ni sehemu ya ukuaji.”<br />
Wavulana wengine hawawi na furaha sana wanapoanza kupata ndoto nyevu. Hili ni jambo la<br />
kawaida vilevile.<br />
nfune kutoka Zambia (umri wa miaka 13.”<br />
“Ninaona kama zinanichukiza”<br />
Wavulana wengine wanao marafiki wasio na huruma, ambao huwatania kuhusu kupata ndoto<br />
nyevu. Ni makosa kumtania au kumcheka mtu kwa vile amepata ndoto nyevu. <strong>Ndoto</strong> nyevu ni<br />
jambo la kawaida.<br />
bernard kutoka Kenya (umri wa miaka 17)<br />
“Nilipokuwa darasa la 8, sikutegemea kama ningeanza kukojoa manii<br />
mapema kiasi hicho. Nilimwambia rafiki yangu siri, badala ya kunieleza kwa<br />
nini yametokea, alinicheka. Nilijisikia kufedheheka. Sikutaka mtu yoyote<br />
afahamu, lakini aliwaeleza watu wengine, na wengine wakasema nilikuwa ninapiga<br />
punyeto. Nilimfuata rafiki yangu mwingine ambaye alikuwa mkubwa<br />
kwangu ambaye alinieleza kwamba ndoto nyevu ni kawaida.”<br />
Unatakiwa usiwe na wasiwasi kuhusu ndoto nyevu kwa vile ni jambo la kawaida halina kasoro.<br />
Unavyoendelea kuujua mwili wako ndivyo utakavyokuwa na raha na mabadiliko unavyokuwa<br />
unayapitia. Kwa kuongezea, ukiwa na taarifa iliyokamilika utaweza kuwasaidia wavulana wadogo<br />
kuelewa kitu gani kinawatokea wanapopitia ujana balehe.<br />
Yapo maelezo na mafunzo mengi mazuri ndani ya kitabu hiki,kwa hiyo usiachie kukisoma kitabu<br />
hiki kwa undani.<br />
25
26<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Sura ya 3<br />
WaVulana<br />
Katika kipindi cha balehe mvulana anategemea mabadiliko mengi kutokea. Mabadiliko<br />
haya ni ya taratibu na hutokea katika umri tofauti kwa wavulana tofauti. Yafuatayo ni<br />
mabadiliko ambayo unaweza kuyategemea:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Mwili wako utakua , hasa mifupa ya mabegani, mikono, miguu na nyayo. Vilevile misuli<br />
itajengeka na utakuwa na nguvu.<br />
Sauti itabadilika halafu itakuwa nzito kadri vinyuzi sauti vinavyokuwa vinene na<br />
kurefuka.<br />
Uume wako utaongezeka na mapumbu yataanza kuninginia chini.<br />
Uume wako utadinda mara kwa mara.<br />
Unaweza kupata ndoto nyevu (kukojoa manii usingizini) usiku.<br />
Unapopitia mabadiliko haya elewa kwamba:<br />
Kila ukubwa wa uume ni sahihi.<br />
Hakuna ubaya wowote kutahiriwa na wala hakuna ubaya wowote kutokutahiriwa kwa<br />
mwanaume.<br />
Oga na kusafisha uume wako kila siku. Kila mara rudisha nyuma govi na kusafisha chini<br />
yake iwapo hujatahiriwa.<br />
Sio lazima kujamiiana eti kwa vile uume umedinda.<br />
<strong>Ndoto</strong> nyevu ni tukio la kawaida, huwapata wengi, hakuna haja ya kuwa na wasiwasi, sio<br />
dalili ya kwamba unatakiwa kuanza kujamiiana.<br />
Wakati wowote mabadiliko haya yanapotokea mwilini mwako ndio wakati mwafaka. <strong>Wewe</strong><br />
ni wa kipekee na uko kawaida kabisa.<br />
Wasichana<br />
Sura ya pili ilielezea kidogo kuhusu mabadiliko ya msichana wakati wa balehe. Sura hii inatoa<br />
maelezo ya kina na naamini utayafurahia kuyasoma.<br />
MauMbile na uKubWa Wa MWili<br />
Wasichana wengi huanza kukua haraka haraka wanapokaribia umri wa miaka 10 hadi 11. Lakini<br />
wapo wasichana wanaoanza kukua wakiwa chini ya umri huu au umri mkubwa zaidi ya huu. Miguu<br />
mara nyingi huwa ndiyo sehemu ya mwili inayokua haraka. Unaweza kuwa mfupi, lakini ukajikuta<br />
miguu yako ghafla imekuwa mikubwa sana! Usijali sehemu nyingine ya mwili itakua na kulingana<br />
na hiyo miguu mikubwa. Mwili wako unakua kwa wakati wake.<br />
Mifupa mingine itaanza kukua pia kila mmoja kwa wakati wake. Mikono na miguu yako inaweza<br />
kutangulia kukua haraka wakati sehemu ya uti wa mgongo ikiwa inakua taratibu zaidi.<br />
Mabadiliko mengine unayoweza kuyahisi ni kuanza kukua nyonga. Mifupa ya nyonga inakuwa<br />
mikubwa, na laini, tishu zenye mafuta hukua kwenye nyonga, mapaja na matako. Kadri nyonga<br />
inavyozidi kupanuka, kiuno kitaonekana chembamba ukilinganisha na sehemu zingine. Mwili<br />
utakuwa wa mviringo, ukionyesha umbo la kike.<br />
Matiti YaKO<br />
catheryn, kutoka Ghana (umri, miaka 15)<br />
“Nilikuwa na miaka 10 nilipoanza kuhisi mabadiliko ya mwili wangu.<br />
Watu waliniambia bila mabadiliko hayo nisingeliweza kuwa<br />
mwanamke kwa hiyo nilifurahi. Nilikuwa naingia katika kundi la<br />
wanawake hivyo sikuwa na budi kujihadhari.”<br />
Wasichana wengine wanaanza kuota matiti wakiwa na umri kati ya miaka 8 au 9, lakini wengine<br />
yanachelewa kuota. Kuota kwa matiti kunasababishwa na homoni inayoitwa estrojeni.<br />
Estrojeni inasababisha tishu ndani ya matiti kukua ili siku moja utakapokuwa na mtoto, uweze<br />
kutengeneza na kuhifadhi maziwa.<br />
Kabla matiti yako hayajaanza kukua, pengine chuchu zako zitakuwa kubwa na kusimama kuliko<br />
zilivyokuwa awali. Mabadiliko mengine unayoweza kuyaona ni duara jeusi na kubwa la ngozi<br />
litakalozunguka chuchu zao.<br />
27<br />
SURA YA 4
28<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Unaweza vilevile kuona vinundu vidogo vidogo kuzunguka duara hilo. Hivi vinundu ni tezi ambazo<br />
ni za kawaida. Mwanamke anapokuwa na mtoto, tezi hizi zinatoa kiini kinachosaidia kulinda<br />
chuchu wakati mtoto ananyonya.<br />
Margaret kutoka tanzania (umri, miaka 18)<br />
“Matiti yangu yalipoanza kukua, nilijisikia vizuri japo kuwa<br />
wakati mwingine kulikuwa na maumivu kidogo”<br />
Kadri chuchu na duara vinavyozidi kuwa vikubwa, matiti nayo yanakuwa makubwa na kujaa.<br />
Mabadiliko haya yanavyoanza kutokea, matiti yanaanza kuuma. Unaweza kujisikia maumivu<br />
ukiyabinya au ukiyagonga. Hii ni kawaida, na hakuna haja ya kuhofu. Matiti ni sehemu ya mwili<br />
ambayo ni nyepesi kuhisi kitu. Iwapo kutatokea kiamshi cha namna tofauti, kama kuguswa au<br />
hata ubaridi, chuchu zinakuwa ngumu na husimama.<br />
Kwa wasichana wengine, matiti yao hukua taratibu na kwa wengine hukua haraka. Kwa wastani,<br />
inachukua muda wa miaka 4 matiti kukua kabisa, lakini wasichana wengine matiti yao yanakua<br />
kabisa kabla ya miaka 4, wakati wasichana wengine matiti yanaweza kuchukua hadi miaka 6<br />
kukua kiukamilifu. Hivyo iwapo matiti yako yanachukua muda mrefu kukua tulia tu, yatakua.<br />
Debora kutoka uganda, (umri, miaka 15)<br />
“Matiti yangu yamekua hivi karibuni, lakini ninaogopa jinsi<br />
yanavyoongezeka haraka. Sijali kuwa na matiti, ila ninatumaini<br />
hayatakuwa makubwa sana. Mara ya kwanza nilikuwa<br />
ninashangaa kwa nini yamechelewa kuota, lakini sasa ukubwa<br />
wake unanitisha.”<br />
Kuna matiti ya maumbo na ukubwa mbalimbali. Ukubwa na maumbile ya matiti yanatokana na<br />
tabia vinasaba ulivyorithi toka kwa wazazi wako. Ukubwa pia unategemea tishu zenye mafuta<br />
katika matiti. Hakuna unachoweza kufanya ili matiti yako yawe unavyotaka. Hakuna kiasi<br />
chochote cha mazoezi kinachoweza<br />
kuongeza ukubwa wa matiti yako.<br />
Mazoezi yanajenga misuli lakini matiti<br />
hayana misuli. Kumbuka tu kwamba<br />
matiti yote, makubwa au madogo –<br />
yana kazi kubwa moja - kunyonyesha<br />
watoto.<br />
Pia unatakiwa ujue kwamba, matiti<br />
hayakui yote pamoja sawasawa. Titi<br />
moja linaweza likawa kubwa kidogo<br />
kuliko jingine. Ukweli ni kwamba<br />
hakuna hata mmoja ambaye ana matiti<br />
yanayolingana ukubwa na si rahisi<br />
kuona tofauti hizi.Maumbile ya chuchu<br />
vilevile yanatofautiana sana. Wanawake<br />
wengine chuchu zao zimegeukia<br />
ndani badala ya nje, wengine chuchu<br />
zimezama ndani ya mduara n.k.<br />
Kama matiti yako ni makubwa au madogo,<br />
ni sahihi yalivyo kwako.<br />
SURA YA 4 | WASICHANA<br />
Matiti yana maana tofauti kutoka jamii moja hadi nyingine. Katika utamaduni mwingine<br />
wanawake wanaweza kuacha matiti wazi, wakati katika tamaduni zingine wanashangaa na sio<br />
heshima hata kidogo. Katika sehemu nyingi hata hivyo kuota matiti ni tukio kubwa katika maisha<br />
ya msichana. Ni ishara ya msichana kukua. Wasichana wengi huyapenda matiti yao.<br />
Prossy,kutoka uganda (umri,miaka 13)<br />
“Ninayapenda matiti yangu. Nilikuwa nawahusudu dada zangu<br />
walivyokuwa na matiti. Nilikuwa nachukua soksi na kuzikunja<br />
halafu naweka ndani ya gauni nionekane kama nina matiti.”<br />
barlay kutoka Kenya (umri, miaka 16)<br />
“Nilikuwa ninawahusudu wasichana wanovaa nguo zinazobana<br />
mwili. Nilifurahi nilipopata matiti, hivyo na mimi niliweza kuvaa<br />
nguo zinazobana mwili.”<br />
cathy kutoka uganda (umri, miaka 17)<br />
“Matiti yangu yalikua nikiwa darasa la kwanza .Nilijiona kama<br />
msichana mkubwa kuliko wote darasani. Ilichukuwa muda kukubaliana<br />
na mabadiliko ya mwili wangu. Lakini nilikuwa napenda<br />
nyonga yangu illivyo ya mduara. Marafiki zangu walisema nyonga<br />
yangu inashawishi na hii ilinifanya nijivunie.”<br />
Sherifan kutoka Ghana (umri, miaka 15)<br />
“Nilifurahi sana kwa sababu nilianza kuonekana kama mama<br />
yangu. Nilipokuwa sina matiti nilikuwa ninavaa sidiria ya mama<br />
yangu na kuweka soksi ndani yake nionekane nina matiti kama<br />
mama yangu.”<br />
Baadhi ya wasichana wanajisikia vibaya matiti yao yanapoanza kukua.Pia hii ni kawaida.Hii ni<br />
kwa sababu marafiki zao wa rika moja hawajaota matiti bado.<br />
irene kutoka uganda (umri, miaka 16)<br />
“Wakati matiti yangu yalipoanza kukua, nilikuwa ninavaa flana<br />
zinazobana sana, flana za wadogo zangu. Nilitaka kujisawazisha<br />
mwili nionekane kama sina matiti.”<br />
angela kutoka Kenya (umri, miaka 17)<br />
“Nilikuwa nina wasiwasi mno na nilikuwa ninavaa sweta wakati<br />
wote matiti yangu yalipoanza kuonekana. Nilikuwa sijisikii vizuri<br />
kwani nilikuwa ninasoma shule ya mchanganyiko na sikujua wavulana<br />
wangesema nini.”<br />
Wasichana wengine wanajipinda vibaya kwa kuinamisha vifua vyao kwa sababu ya<br />
kufedheheshwa na kukua kwa matiti yao. Jambo hili linasikitisha kwa sababu kila mtu anatakiwa<br />
kuupenda mwili wake, na kutojali watu wengine wanasema nini. Vyovyote vile matiti yako<br />
yalivyo,kama ni makubwa au madogo yaliyochongoka au ya mviringo ni mazuri jinsi yalivyo.<br />
29
30<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Rita kutoka uganda (umri, miaka 16)<br />
“Ninayapenda matiti yangu kwa sababu yananifanya nijisikie mwanamke<br />
haswa. Wasichana wakubwa ambao hawana matiti hutaniwa na<br />
kufananishwa na wanaume”<br />
Si vema watu kuwatania wasichana kuhusu matiti yao. Huu si ustaarabu. Msichana ajaribu kadri<br />
awezavyo kuwadharau na kutojali matusi yao.<br />
UNAJUA KUWA KUNA IMANI POTOFU NYINGI KUHUSU MATITI?<br />
Watu husema mambo mengi potofu kuhusu matiti, yafuatayo ni baadhi yake:<br />
1. Wasichana wenye matiti yaliyochongoka huvutia kingono. hii Si Kweli. Kuvutia kingono<br />
ipo kwenye akili ya anayejiona hivyo na si kwenye mwili wake.<br />
2. Kuweka jibini kwenye chuchu au kumfanya mdudu ang’ate chuchu hufanya matiti yakue<br />
haraka. hii si Kweli pia. Homoni ndizo zinazofanya matiti yakue. Hamna kitu chochote<br />
zaidi ya hicho kitakachobadilisha matiti.<br />
3. Wasichana wenye ngozi iliyo nyeusi kuzunguka chuchu zao wamewahi kufanya ngono.<br />
huu ni uongo! Kama ilivyo rangi ya ngozi yako, rangi ya mduara wa chuchu inatokana na<br />
tabia vinasaba ulivyorithi kutoka kwa wazazi wako.<br />
4. Matiti yanaweza kuwa makubwa kama wavulana watayashikashika. Si kweli! Ukubwa wa<br />
matiti unategemea tabia vinasaba ulizorithi kutoka kwa wazazi wako.<br />
5. Wasichana wenye matiti yaliyolala wameshawahi kufanya ngono au wameshawahi kutoa<br />
mimba. huu pia ni uongo! Matiti hulala/huanguka kutokana na uzito na maumbile. Kama<br />
una matiti makubwa uwezekano wa kulala au kuanguka kwa sababu ya uzito ni mkubwa<br />
zaidi.<br />
6. Kuvaa sidiria hufanya matiti kuanguka. uongo! Sidiria hushikilia matiti na huzuia ngozi na<br />
tishu za matiti kutanuka na kupunguza kunyumbuka.<br />
7. Wasichana wenye matiti makubwa watakuwa na maziwa mengi kwa ajili ya watoto wao.<br />
uongo! Uzalishwaji wa maziwa hautokani na ukubwa wa matiti; hata matiti madogo huzalisha<br />
maziwa yanayomtosheleza mtoto.<br />
naMna Ya KutunZa Matiti YaKO<br />
Matiti ni sehemu nyeti, kwa hiyo kuna vitu fulani ambavyo unatakiwa uvijue kuhusu utunzaji<br />
wake. Hata siku moja using’oe nywele zinazozunguka chuchu, zinaweza kusababisha madhara.<br />
Ni kawaida kuwa na vinyweleo hivyo. Kuna baadhi ya wasichana wanatokwa majimaji kwenye<br />
chuchu zao: hiki ni kitu cha kawaida. Lakini kama majimaji hayo yana damu au rangi ya kahawia<br />
unatakiwa kumwona daktari maana inaweza kuwa ni uambukizo.<br />
Kutunza matiti ni pamoja na kuhakikisha kuwa hakuna anayeyashika bila ridhaa yako. Mara nyingi<br />
wavulana na wanaume hugundua kwamba matiti ya wanawake yanavutia sana, lakini hata hivyo<br />
mtu hana ruhusa kuyashika labda upende mwenyewe.<br />
Matiti ya wanawake wengi ni rahisi sana kuhisi yanapoguswa.Kuguswa kunaweza kuleta ashiki ya<br />
kusisimua, na hii inaweza kusababisha utende usilotegemea au uponzeke.<br />
SiDiRia<br />
SURA YA 4 | WASICHANA<br />
Si lazima kuvaa sidiria kama una matiti madogo au yaliyosimama imara. Lakini kama matiti yako<br />
ni makubwa, unaweza ukajisikia vizuri kama ukivaa sidiria ambayo inasaidia matiti yasitikisike<br />
au kurukaruka unapotembea, kukimbia, kucheza dansi au kucheza michezo. Wasichana wengine<br />
waliobalehe wanafedheheka na matiti yao, hivyo kuvaa sidiria kunawafanya kutokuwa na<br />
wasiwasi na pia hupunguza kufedheheka/kujishuku.<br />
Ili kupata kipimo sahihi, wanawake wengi wanajaribisha namba mbalimbali za sidiria kuona ni ipi<br />
itamtosha vizuri. Unashauriwa kufanya hivyo.<br />
Wanawake wengine huwa wanachukuwa vipimo ili waweze kupata saizi ya sidiria. Ili uweze<br />
kupata vipimo vyako, unahitaji kujua saizi ya kifua chako pamoja na saizi ya titi.Pima kifua chako,<br />
chini kidogo ya matiti, ili upate saizi ya kifua. Kisha pima sehemu iliyojaa zaidi ya matiti ili kupata<br />
ukubwa wa titi, kama viko sawa unahitaji kikombe A. Kama kipimo cha matiti ni 2.5 Sm zaidi ya<br />
kifua unahitaji saizi ya titi B. Iwapo kipimo cha matiti ni 5 Sm zaidi ya kifua basi unahitaji saizi ya<br />
titi C.<br />
Via VYa uZaZi/SeheMu ZaKO Za SiRi<br />
Uke ndilo tundu pekee lililo kubwa kuliko matundu yote matatu katika eneo la via vya uzazi.<br />
Mashimo mengine ni tundu la mkojo (mbele ya uke) na mkundu (nyuma ya uke). Uke una kina cha<br />
sm 7 na upana wa sm 3 – 4. Ngozi yake ni laini iliyokunjamana.<br />
Uke wa mwanamke mtu mzima ni imara sana; hutanuka sana na una misuli imara. Wakati wa<br />
kuzaa mtoto uke unatanuka sana kuliko ukubwa wake wa kawaida ili kuruhusu mtoto kutoka<br />
tumboni mwa mama yake. Lakini uke wa msichana ni mwembamba na hauwezi kutanuka<br />
sana. Hii ni mojawapo ya sababu ya madhara<br />
yanayompata msichana aliyezaa angali mdogo.<br />
Uke wa msichana mdogo unaweza kuchanika<br />
au kupasuka wakati wa kuzaa. Hii husababisha<br />
matatizo makubwa sana. (Soma Sura ya 11).<br />
Katika kipindi cha balehe, kuta za uke zinaanza<br />
kutoa majimaji ukeni. Maji maji hayo ni mazito na<br />
yananata kuliko mate na yana kazi yake ambayo<br />
ni kuuweka uke safi, na kutengeneza mazingira<br />
mwafaka ambapo bakteria wazuri wanaozuia<br />
maambukizo ya magonjwa wanaweza kuishi.<br />
Wanawake wengi wanaanza kuona maji maji<br />
ukeni katika nyakati tofauti katika mzunguko<br />
wa mwezi na wakati wanapopata ashiki. Hii ni<br />
kawaida.<br />
Sehemu za siri za mwanamke kwa nje<br />
31
32<br />
Upo uzushi mwingi kuhusu uke:<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Je ? Unajua ukweli kuhusu uke?<br />
1. Uke ni sehemu chafu kuliko sehemu zote mwilini. Si kweli! Mdomo ndio sehemu chafu<br />
kuliko zote mwilini. Ukweli ni kuwa majimaji ya ukeni na damu ya hedhi ni safi. Lakini<br />
mara baada ya kutoka mwilini, bakteria wanaweza kuzaliana kwenye majimaji na damu<br />
na kufanya yatoe harufu mbaya.<br />
2. Uke haujazibwa mwisho, ni tundu lisilo na mwisho. Si kweli pia! Uke umezibwa na mlango<br />
wa tumbo la uzazi. Kondomu au sodo (tampon) haziwezi kusafiri hadi ndani ya kizazi.<br />
3. Ni tabia mbaya kushika uke. Si kweli! Uke ni kama sehemu nyingine yoyote ya mwili<br />
kuishika ni kama kushika sikio. Hata hivyo uke ni sehemu nyeti ya mwili, hivyo unatakiwa<br />
kujishika wakati uko peke yako.<br />
4. Uke ni kwa ajili ya kumfurahisha mwanaume. Si kweli! Uke ni sehemu ya mwili wa<br />
mwanamke. Ni yake pekee yake! Usimruhusu mtu yeyote kuushika bila ridhaa yako.<br />
Eneo linalozunguka mlango wa uke linaitwa vulva. Kwa kawaida mlango wa uke umefungwa, na<br />
unalindwa na mashavu ya nje na ya ndani. Mashavu haya yana mikunjo miwili ya ngozi. Kuna tezi<br />
ndogo ndogo katika mashavu, hivyo unaweza kujihisi unatoa jasho na unatoa majimaji meupe<br />
sehemu hizo.<br />
Mbele ya tundu la mkojo, ambapo midomo ya ndani inakutana, kuna kinembe au kisimi. Kinembe<br />
ni kinundu kidogo mfano wa kunde. Kinembe hiki kimejaa neva na ni sehemu ambayo ni nyepesi<br />
kupata hisia/ashiki katika sehemu za via vya uzazi. Kinahisia kali kikiguswa.<br />
Ndani kabisa, mwisho wa uke wako kuna mlango wa mfuko wa uzazi. Mlango wa kizazi unafunga<br />
mwisho wa uke. Upo uwazi mdogo tu kwenye mlango wa kizazi, na uwazi huu unaelekea kwenye<br />
mfuko wa uzazi. Uwazi ni mdogo kiasi kwamba damu za hedhi tu zinaweza kutoka na mbegu za<br />
kiume tu zinaweza kuogelea kwenda juu. Watu wengine huhofia kwamba wakati wa kujamiiana<br />
kondomu inaweza kutoka kwenye uume na kuingia kwenye tumbo la uzazi. Hii haiwezekani kwa<br />
sababu uwazi uliopo kwenye mlango wa mfuko wa uzazi ni mdogo sana. Mlango wa mfuko wa<br />
uzazi unafunguka tu wakati wa kuzaa mtoto ili mtoto aweze kutoka kupitia ukeni na kisha nje ya<br />
mwili.<br />
Ngozi ya mlango wa mfuko wa uzazi ni laini sana, hususani kwa wasichana wadogo na wanawake<br />
wadogo. Mlango wa mfuko wa uzazi unaweza kuharibika au kuambukizwa bakteria na virusi<br />
ambavyo vinaweza kuingia mwilini wakati wa kujamiiana. Hii inaweza ikasababisha saratani<br />
ya mlango wa mfuko wa uzazi. Wasichana wanaoanza kujamiiana mapema au walio na wapenzi<br />
wengi wa kufanya nao ngono, au walio na VVU, wako kwenye hatari ya kupata saratani ya mlango<br />
wa mfuko wa uzazi kuliko wale ambao ni waangalifu katika kufanya ngono. Kutoanza kujamiiana<br />
mapema na kutumia kondomu kunaweza kukulinda usipate saratani ya mlango wa mfuko wa<br />
uzazi, (soma sura ya 10 zaidi kuhusu afya ya uzazi).<br />
KuFanYa uSaFi Wa MWili ViZuRi<br />
SURA YA 4 | WASICHANA<br />
Uke na mkundu vinapaswa kuoshwa mara kwa mara na kubakia vikavu. Ni jambo zuri kuepuka<br />
kuchangia mataulo na ndugu wengine katika familia au marafiki kwani yanaweza kusababisha<br />
kuenea kwa maambukizi ya magonjwa kutoka mtu mmoja hadi mwingine. Baada ya kuoga vaa<br />
chupi za pamba zilizo safi. Katika kipindi cha joto, epuka kuvaa chupi za nailoni kwa sababu huwa<br />
zinahifadhi unyevunyevu na joto, hali ambayo husababisha kuota bakteria. Kama huwezi kupata<br />
chupi za pamba, vaa zilizozungushiwa kitambaa cha pamba.<br />
Baada ya kukojoa au kwenda haja kubwa, unapaswa kujisafisha mwenyewe kwa kusafisha<br />
kuanzia mbele ya sehemu zako za siri mpaka kwenye mkundu. Kama ukitumia karatasi la chooni,<br />
karatasi, maji, majani au matawi ya miti kujisafisha, epuka kujisafisha kutoka nyuma kwenda<br />
mbele. Ukijisafisha kutoka nyuma kwenda mbele, kuna hatari ya kuvuta vijidudu vya maradhi<br />
kutoka kwenye mkundu kwenda kwenye uke na kwenye njia ya mkojo. Hii inaweza kukupa<br />
maambukizi ya magonjwa.<br />
Kamwe usijaribu kuosha ndani ya uke labda tu kama umeshauriwa na daktari.<br />
Kwa bahati mbaya wasichana na wanawake wengine wanaosha ndani ya uke kwa kutumia sabuni<br />
kali. Wanawake wengine wanapenda kupaka odorono au kupuliza manukato. Haya yote hayana<br />
umuhimu, na yanaweza kukuletea madhara kwa sababu sabuni, na manukato vikitumiwa ukeni<br />
vinaweza kubadilisha mfumo wa kawaida wa majimaji ndani ya uke na kusababisha ngozi ndani<br />
ya uke kuwasha.<br />
Katika nchi nyingine, kama vile, Zimbambwe na Zambia, wanawake huweka mitishamba, vipande<br />
vya nguo, na vitu vingine ndani ya uke ili kusafisha au kuufanya ubane. Kiafya, hii sio njia nzuri<br />
kwa sababu ngozi ndani ya uke ni laini mno. Unapoingiza vitu vigeni, vinaweza kusababisha<br />
majeraha madogo madogo au michumbuko na uvimbe mambo ambayo yanaweza kukufanya kuwa<br />
na maambukizi na uwezekano wa kukuweka kwenye hatari ya kupata VVU.<br />
Kwa ujumla, ni vizuri kutokuweka kitu chochote ndani ya uke wako, isipokuwa pamba za damu na<br />
dawa kama umeandikiwa na dakitari. Hakikisha tu unafuata maelekezo kwa makini.<br />
Ni vizuri kuchunguza kwa makini majimaji yanayotoka ukeni wakati wa mzunguko wa kila mwezi<br />
ili kuweza kuona dalili na mabadiliko yasiyo ya kawaida. Ukiwa makini , utagundua kwamba<br />
majimaji yanayotoka ukeni sio sawa wakati wote. Wakati mwingine yanaweza kuwa meupe<br />
wakati mwingine yanaweza kuwa meupe kidogo kama ute mweupe wa yai. Wakati wa uovishaji,<br />
majimaji ya ukeni yanaweza kuwa na utelezi zaidi na angavu. Vilevile majimaji ya ukeni yanaweza<br />
kubadilika iwapo mwanamke atashikwa ashiki.<br />
Iwapo majimaji ya ukeni yatakuwa mazito na kubadilika rangi kuwa njano, kijani au kahawia au<br />
yanasababisha muwasho sehemu za siri, unaweza kuwa umeambukizwa maradhi. Harufu mbaya<br />
ya majimaji toka ukeni, maumivu ndani ya uke na damu kutoka wakati hauko katika siku zako<br />
za hedhi ni dalili pia za maambukizi ya ugonjwa. Iwapo utapata mabadiliko yoyote kati ya haya,<br />
itabidi umwone daktari.<br />
Iwapo hushiriki ngono isiyo salama, na kama unazingatia usafi, huwezi kupata matatizo haya.<br />
Ukiutunza vizuri uke wako utajikamilisha kulingana na mazingira. Unachotakiwa kufanya ni<br />
kuosha kwa uangalifu eneo la via vya uzazi kila siku na maji safi au osha kwa sabuni ya kuogea.<br />
Tenganisha mashavu ya nje ili kusafisha uchafu unaojikusanya sehemu hizo.<br />
33
34<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
UNAJUA KUHUSU UKEKETAJI WA WANAWAKE?<br />
Katika mila nyingine, kisimi/kinembe na/au sehemu zingine za via vya uzazi vya<br />
mwanamke zinakatwa au kuondolewa kabisa. Utaratibu huu unaitwa kutahiri<br />
wanawake au ukeketaji wa wanawake. Ukeketaji huu unatofautiana katika nchi<br />
mbalimbali. Wengine hukata kuzunguka kisimi, na wengine hukata kisimi na mashavu<br />
(ya ndani na nje). Kukata kisimi na mashavu na kushona/kupunguza ukubwa wa uke<br />
kunaitwa mfyato, na huu ndiyo ukatili wa kiwango cha juu kabisa.<br />
ni wakati gani unafanyika? Umri ambao wanawake wanakeketwa unatofautiana nchi<br />
moja hadi nyingine. Unafanyika wakati wa uchanga, utoto, ujana balehe, wakati wa<br />
kuolewa au wakati mwanamke ana mimba ya kwanza.<br />
Kwa nini unafanyika? Baadhi ya tamaduni, mila,desturi na imani zinaunga mkono<br />
wanawake kukeketwa, lakini Biblia na Korani haviungi mkono jambo hili. Katika jamii<br />
zingine wanaamini kwamba kukeketa kutalinda ubikira wa wasichana na kuwafanya<br />
wanawake wasiwe wahuni (Malaya). Pia watu wengine wanaamini kwamba kukeketa<br />
kunaongeza raha ya kujamiiana kwa waume zao, na kitendo hiki kinaaminika kuongeza<br />
uwezekano wa wanawake kuolewa na kuimarisha uwezo wa kuzaa.<br />
unafanyikaje? Kwa kawaida wanaofanya kazi hii ni watu wazima/wazee au wakunga<br />
wa jadi wanaotumia visu maalumu, mikasi, vipande vya kioo, nyembe na vifaa vingine<br />
ambavyo si visafi kukeketea. Mara kwa mara ukeketaji unafanyikia katika mazingira<br />
machafu na mwanga hafifu. Kwa kawaida,hazitolewi dawa za kutuliza maumivu, wala<br />
za usingizi,wala dawa za kuzuia maambukizi!<br />
Madhara yake ni nini? Kukeketa wanawake kunaweza kusababisha matatizo makubwa<br />
ya kiafya na kisaikolojia (kihisia):<br />
• Kutoka damu nyingi. Kukata sehemu za via vya uzazi kunaweza kusababisha<br />
kutoka damu nyingi. Hii inaweza kusababisha kifo au upungufu mkubwa wa damu.<br />
• Maambukizi ya magonjwa. Mambukizi ya magonjwa yanaweza kutokea kwa<br />
sababu ya kutumia vifaa vichafu na pia yanaweza kutokea kwa kutumia dawa<br />
za kienyeji za kuponyesha vidonda. Maambukizi yanaweza yakaenea hadi<br />
kwenye tumbo la uzazi, mirija ya kupitishia mayai, na kwenye mayai ya uzazi na<br />
kusababisha maumivu ya mara kwa mara hata ugumba. Mambukizi ya magonjwa<br />
yanaweza kusababisha kifo.<br />
• Mshituko: Mshituko kupita kiasi au kupoteza fahamu kunaweza kutokea kwa<br />
sababu ya kutoka damu nyingi na maumivu makali.<br />
• Kubana mkojo: Baada ya kukeketwa wanawake wanaweza kubana mkojo kwa<br />
masaa au siku kwa sababu ya maumivu au kwa kuogopa kupitisha mkojo kwenye<br />
vidonda. Hata baada ya vidonda kupona mwanamke aliyeshonwa uke, tundu<br />
linaweza likawa dogo mno kuweza kutoa mkojo.<br />
• Matatizo wakati wa siku za hedhi: Kama mlango wa uke ni mdogo sana kiasi cha<br />
kutoruhusu damu ya hedhi kutoka vizuri, damu inaweza kukusanyika ndani ya uke<br />
na tumbo la uzazi. Hii inaweza kusababisha maambukizi ya magonjwa, na tumbo la<br />
uzazi kuvimba kwa sababu ya damu ya hedhi.<br />
heDhi na MZunGuKO Wa heDhi<br />
SURA YA 4 | WASICHANA<br />
UNAJUA KUHUSU UKEKETAJI WA WANAWAKE? (Endelea)<br />
• Maumivu wakati wa kujamiiana na matatizo wakati wa kujifungua.Wasichana<br />
waliokeketwa wanaweza kupata maumivu wakati wa kujamiiana pia wanaweza kupata<br />
matatizo wakati wa kuzaa iwapo njia ya uke ni ndogo kupitisha mtoto (angalia sura II).<br />
• athari za kisaikologia na kijamii: Ukeketaji kwa mwanamke unaweza kuwa na athari<br />
za muda mrefu kimaisha na kiakili. Anaweza kupoteza imani kwa jamii,wazazi au hata<br />
walezi. Anaweza pia kuathiriwa na hisia za kutokamilika, hofu, mfadhahiko na kupoteza<br />
hamu ya kujamiiana.<br />
Kwasababu ya athari kubwa za kiafya zinazotokea na kwasababu ukeketaji sio hitaji la<br />
kiafya, ndio maana watu wengi sasa huita Ukataji wa via vya uzazi vya mwanamke. (FGM =<br />
Female Genital Mutilation). Tendo hili linachukuliwa kama ni uvunjaji wa haki za wanawake<br />
na wasichana juu ya afya zao kimwili na kiakili na haki za uhuru, usalama na ukamilifu wa<br />
mwili (ujumla na ukamilifu wa miili yao). Kama wewe mwenyewe au unamfahamu msichana<br />
anayelazimishwa kukeketwa, peleka suala hili kwa utawala wa serikali wa mahali ulipo<br />
au mhudumu wa afya ili waweze kuongea na wazazi na ndugu zake juu ya athari mbaya<br />
zinazotokana na kitendo hicho.<br />
Wasichana wengi wanaanza kupata damu ya hedhi au kuingia mwezini kati ya umri wa miaka<br />
10 na 16. Kuvunja ungo (mwanzo wa hedhi) ni dalili ya kwamba mabadiliko makubwa yanatokea<br />
ndani ya mwili wa mwanamke. Vilevile ni dalili ya<br />
kwamba anaweza akapata mimba akifanya ngono na<br />
mwanaume.<br />
Katika kipindi cha balehe, homoni husababisha<br />
ovari ambavyo ni viungo viwili vyenye umbile la<br />
yai kukomaa na kuanza kutoa yai kila mwezi. Kila<br />
mwanamke anazaliwa na mayai ambayo ni madogo<br />
mno kiasi kwamba hawezi kuyaona bila darubini.<br />
Mrija wa falopio<br />
Tumbo la uzazi<br />
Kadri ovari zinavyozidi kukomaa, mfuko wa uzazi<br />
pia unakua, ngozi laini inaanza kutengenezwa<br />
Uke<br />
kuzungukamfuko wa uzazi. Hivi ndivyo mfuko wa<br />
uzazi unavyofanya matayarisho ya kupokea yai<br />
lililorutubishwa.Kama hakuna yai lililorutubishwa,<br />
ngozi laini inayozungukamfuko wa uzazi inakatika<br />
na kutoka kupitia mlango wa mfuko wa uzazi, kupitia<br />
kwenye uke na kutoka nje. Hii ndio damu ya hedhi au Sehemu za siri za mwanamke kwa ndani<br />
“kuingia mwezini”. Kwa vile ngozi laini ya mfuko wa<br />
uzazi imetengenezwakwa mishipa ya damu, inaitwa damu ya hedhi.<br />
Wasichana ambao wameanza kupata hedhi (kwenda mwezini) wanao “mzunguko wa mwezi”.<br />
Katika miaka michache ya mwanzo wasichana wengi mzunguko wao hauna mpangilio<br />
unaoeleweka.<br />
Ovari<br />
Seviksi<br />
35
36<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Hawajui ni lini wataingia mwezini tena. Inakuwa hakuna mfumo maalum, na mara nyingine<br />
wanaweza kukaa miezi kadhaa bila kupata damu ya hedhi kabisa. Hii ni kawaida, baada ya miaka<br />
michache mzunguko wa hedhi unakuwa wa kawaida. Wanawake wengine pia hawapati hedhi zao<br />
kulingana na mzunguko wa kawaida wa kila mwezi, jambo hili ni la kawaida pia.<br />
Hata kama mzunguko ni wa kawaida, muda wa mzunguko wa hedhi unatofautiana kwa<br />
wanawake/wasichana. Kwa wengine mzunguko ni mfupi, siku 21 (hata chini ya hapo). Wengine<br />
mzunguko ni mrefu, siku 35. Wastani wa mzunguko ni siku 28. Tuangalie mzunguko wa hedhi wa<br />
mwanamke wa wastani ambao ni siku 28.<br />
Siku inapoanza kutoka damu, hesabu kuwa ndiyo siku ya kwanza. Katika siku 5 hadi 7 zinazofuata<br />
ukuta wa mfuko wa uzazi unajiachia na damu inatoka kupitia ukeni. Wakati huo huo mwili<br />
unakuwa umeshahisi kwamba hakutakuwa na mimba mwezi huo, na mwili utajua kwamba<br />
unahitaji tena kutayarisha yai jingine.Yai jingine litaanza kuchomoka kutoka kwenye Ovari. Mara,<br />
baada ya hapo tumbo litaanza tena kutengeneza ngozi laini nyingine kuzunguka mfuko wa uzazi.<br />
Katikati ya mzunguko kama siku 14 au wiki 2 hivi tangu damu ianze kutoka ovari inaachia yai<br />
ambalo huanza kubingirika kuelekea kwenye mirija ya falopia. Hiki ni kipindi cha urutubisho.Hiki<br />
kipindi ambacho uwezekano wa mwanamke kupata mimba ni mkubwa. Yai linakaa siku chache<br />
kwenye mirija ya falopia, na kama litakutana<br />
na mbegu za kiume linaweza kurutubishwa na<br />
mwanamke atapata mimba. (Angalia sura ya 11<br />
taarifa zaidi kuhusu mimba).<br />
Kama yai halijarutubishwa linaingia ndani ya<br />
mfuko wa uzazi, kupitia mlango wa mfuko<br />
wa uzazi na uke, na kutoka nje ya mwili. Hii<br />
itakuwa inakaribia siku ya 20.<br />
Karibu wiki mbili hivi baadaye, mwili<br />
unapotambua kwamba yai halikurutubishwa,<br />
ngozi laini ya ukuta wa mfuko wa uzazi<br />
inabomoka tena kama damu ya hedhi na<br />
mzungo unajirudia tena.<br />
ukuta wa tumbo la uzazi uliotayari<br />
kupokea yai<br />
Hivi ndivyo mzunguko wa hedhi unavyokuwa.<br />
Wanawake walio wengi wanadhani kwamba<br />
kipindi cha uzazi nikatikati kabisa ya<br />
mzunguko, lakini hii ni kweli kwa wanawake<br />
wenye mzunguko wa siku 28 tu. Kwa upande wa<br />
wanawake wenye mzunguko mfupiau mrefu,<br />
haiwezekani kuwa katikati ya mzunguko.<br />
Hii ni kwa sababu uovishaji (kutoka kwa<br />
yai) kunatokea karibu siku 14 kabla ya hedhi<br />
nyingine kuanza. Hivyo basi inamaanisha<br />
kwamba mwanamke mwenye mzunguko wa<br />
siku 21 pengine anaovusha siku ya 7, ambapo<br />
mwanamke mwenye mzunguko wa siku 35<br />
pengine anaovusha siku ya 21. hedhi:Kubomoka kwa ukuta wa tumbo la<br />
uzazi<br />
Mzunguko wa hedhi hautulii katika kipindi cha balehe.Unaweza kuathiriwa na mfadhaiko wa<br />
mawazo, huzuni, kusafiri na mabadiliko mengine katika maisha ya msichana. Kwa hiyo ni vigumu<br />
sana kujua kipindi cha uzazi kitakuwa lini. Wasichana wengi wanapata mimba kwa makosa kwa<br />
sababu wanajamiiana siku ambazo wanafikiri ni salama, siku ambazo wanafikiri uwezekano wa<br />
kupata mimba ni mdogo.<br />
Wasichana na wavulana wengi wamewahi<br />
kusikia kuhusu “siku salama” lakini hakuna<br />
“siku salama” kwa wasichana balehe. Hii ni kwa<br />
sababu mzunguko wa hedhi hubadilika sana<br />
wakati wa ujana balehe. Kama mzunguko wako<br />
ni wa kawaida, unaweza ukabadilika ghafla na<br />
ukawa sio wa kawaida.<br />
Zaidi ya hapo, hakuna siku salama dhidi ya<br />
VVU na magonjwa mengine ya ngono.Unaweza<br />
kuambukizwa magonjwa ya ngono siku yeyote<br />
ya mwezi.<br />
Kusubiri siku salama sio njia nzuri ya kuzuia<br />
mimba au kuzuia magonjwa ya ngono. Kama ni<br />
kijana balehe uliyeanza kujamiiana usitegemee<br />
sana siku salama kama kinga. Kuna njia nzuri<br />
za kujikinga (soma sura ya 10 na 11 kwa taarifa<br />
zaidi kuhusu ngono salama na uzuiaji mimba).<br />
KuVunja unGO<br />
SURA YA 4 | WASICHANA<br />
Hakuna “SIKU SALAMA” kwa vijana balehe<br />
Kupata damu ya hedhi kwa mara ya kwanza ni tukio kubwa sana katika maisha ya msichana.<br />
Wasichana wengi wanakumbuka siku waliyovunja ungo.<br />
Ruvimbo, kutoka Zimbambwe (umri, miaka 13)<br />
“Nakumbuka ilikuwa mwezi Juni tarehe 10 nilipoamka na kukuta<br />
nguo zangu zina damu. Nilimwambia mama. Mama alinipa pamba<br />
na akanielekeza namna ya kuitumia. Aliniambia pia kwamba kama<br />
sina pamba ninaweza kutumia nguo za zamani.”<br />
Kupata hedhi maana yake ni kwamba mwili unakua na unafanya kazi katika njia mpya. Vilevile<br />
kupata hedhi inamaana ya kwamba unaweza kupata mimba endapo utajamiiana. Lakini kupata<br />
hedhi haimaanishi mwili wako upo tayari kujamiiana au kupata mtoto, kwani uke bado ni mdogo<br />
na haujakomaa.Uke hukomaa msichana anapofikia umri wa miaka 18 hadi 20. Isitoshe, nyonga na<br />
mifupa ya nyonga inaweza kuwa midogo sana kumuwezesha kuzaa kwa njia ya kawaida.<br />
Kupata hedhi ni dalili ya afya, lakini wasichana wengi wanashituka na kusikitika wanapovunja<br />
ungo – mara nyingi ni kwa sababu hawakujua kilikuwa ni kitu gani na walidhani kuna kosa<br />
limefanyika.<br />
37
38<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Diana kutoka Zambia (umri; miaka 17)<br />
“Nilishituka nilipopata hedhi kwa sababu sikujua. Lakini mama<br />
yangu akanieleza kwa nini ilinipasa kupitia hatua kama hiyo”<br />
Sherifan kutoka Ghana (umri; miaka 15)<br />
“Sikujua kilikuwa ni kitu gani. Nilifadhaika na kuona aibu kwa<br />
wazazi wangu na marafiki zangu. Nilisali na kumuomba Mungu<br />
aniepushe na mambo hayo. Baadaye nilitambua kwamba ni<br />
sehemu ya maisha.”<br />
Stabisile kutoka Zimbambwe (umri; miaka 19)<br />
“Sikuwa na uhakika kilichokuwa kinaendelea. Sikuwa na ufahamu<br />
wa namna ya kulikabili suala hili. Kupata hedhi kulinifanya<br />
nikose raha.”<br />
Wasichana wanaojua hedhi ni kitu gani na wale ambao mama zao na dada zao wakubwa<br />
wanazungumza nao kuhusu kupata hedhi, inakuwa rahisi kwao kuikubali hali hii.<br />
Sandra, kutoka uganda (umri; miaka 13)<br />
“Bado sijaingia mwezini, lakini hata kama nitaingia, tayari<br />
ninajua hedhi ni kitu gani na kwa vipi unaweza kukabilana na<br />
hali hiyo”<br />
Demitrida, kutoka tanzania (umri; miaka 13)<br />
“Bado sijapata hedhi, nikipata nitamwambia mwalimu mlezi<br />
wangu. Pia nitamwambia mama ili anipatie pamba au kipande<br />
cha nguo.”<br />
Utajua kama umeanza kuingia mwezini utakapoona damu kidogo inatoka kwenye uke. Damu<br />
haimwagiki kama maji yanavyotoka kwenye bomba. Inadondoka taratibu. Kawaida muda<br />
utakaogundua ubichi usio wa kawaida, chupi yako itakuwa imenyonya damu yote, na nguo zako<br />
nyinginezo zitakuwa salama.<br />
Lakini wakati mwingine kunakuwa na damu nyingi au inakuja ghafla. Au inaweza kukuchukuwa<br />
muda mrefu kujionyesha, kinatokea nini. Cathy mwenye umri wa miaka 17 kutoka Uganda<br />
alichafua chupi yake hadi kwenye nguo.<br />
cathy, kutoka uganda (umri; miaka 17)<br />
“Ilinitokea darasani nikiwa na wanafunzi wenzangu. Nilisimama<br />
na kwenda chooni. Nikagundua kuwa nimechafua nguo.<br />
Aah, lilikuwa tukio baya sana. Nilifedheheka sana. Marafiki<br />
zangu walinisaidia lakini ilibidi nikae nyumbani wiki nzima.”<br />
Kama hii itatokea, tulia. Sio kosa lako hukujua kwamba jambo hili litakutokea! Kila mtu<br />
inamchukuwa muda kuelewa namna ya kushughulikia hedhi.<br />
Unaujua Ukweli kuhusu hedhi?<br />
Kila mtu anayo maswali mengi kuhusu hedhi. Yafuatayo ni baadhi ya maswali na majibu yake:<br />
1. Nitapoteza damu kiasi gani kila mwezi? Katika kipindi chote cha kutoka damu ya hedhi<br />
cha mwezi, kiasi cha damu itakayotoka ni kama ml za ujazo 60 hadi 70. Ukipima ml 70. za<br />
ujazo wakati wa kipindi cha Sayansi. utaona kuwa siyo damu nyingi sana. Hata hivyo huo<br />
ni wastani tu, wanawake wengine hupoteza kidogo zaidi- kiasi cha vijiko vichache tu vya<br />
chai. Wengine wanapoteza kikombe kizima kilichojaa.<br />
2.<br />
3.<br />
Kama nikiweka kumbukumbu kwenye kalenda yangu naweza nikajua siku gani ni salama<br />
kwangu, Siku ambazo siwezi kapata mimba?<br />
Hapana, huwezi. Wasichana balehe huwa hedhi yao sio ya kawaida hivyo hawawezi kujua<br />
siku salama ni zipi. Isitoshe, hakuna siku salama dhidi ya maambukizi ya VVU na magonjwa<br />
ya ngono. Unaweza kuambukizwa magonjwa ya zinaa siku yoyote na usije ukafikiri<br />
siku salama ni njia salama ya kujikinga na maambukizi.<br />
4. Ninaweza kuingia mwezini mara mbili katika mwezi mmoja? Angalia ukurasa wa “40”<br />
Susan alipata damu ya hedhi mara mbili mwezi Aprili.<br />
5. Naweza nikajamiiana wakati niko mwezini? Hili sio jambo zuri, hasa kama ni ngono isiyosalama<br />
(bila Kondom). Kama una VVU vitakuwa kwenye damu yako hivyo mwenzi wako<br />
anaweza kuambukizwa kwa urahisi. Vilevile wewe uko hatarini iwapo utajamiiana wakati<br />
huu na mwanaume aliye na VVU au magonjwa ya ngono. Uko hatarini kuambukizwa kuliko<br />
wakati wowote ule katika mwezi.<br />
6. Je, ngono inatibu maumivu ya mkakamao wa tumbo wakati wa hedhi? Hapana! Ngono<br />
haiwezi kutibu maumivu ya mkakamao wa tumbo wakati wa hedhi. Huu ni uzushi tu ambao<br />
vijana wengi wanaueneza.<br />
KutunZa KalenDa<br />
SURA YA 4 | WASICHANA<br />
Kwa wasichana wengi, inawachukuwa muda kuzoea hedhi. Kujisikia vibaya kuhusu hedhi ni<br />
kawaida kabisa. Jaribu kukumbuka kwamba hedhi ni dalili<br />
ya utu uzima na afya nzuri. Pia unapaswa kujua kwamba<br />
hedhi haita dumu milele. Wanawake wengi wanaacha<br />
kupata hedhi wanapokuwa mwishoni mwa miaka 40 na<br />
miaka ya 50. Umri huu unaitwa “wakati wa kukoma hedhi”<br />
Wasichana wengi wanaona kuna umuhimu wa<br />
kutunzakumbukumbu za tarehe aliyoingia mwezini.<br />
Hata kama hedhi haina mpangilio uliotulia kuweka<br />
kumbukumbu husaidia kutoa mwanga ni lini msichana<br />
balehe ataingia mwezini ili aweze kujiandaa.Unaweza<br />
kununua kalenda ndogo na kutia alama X siku unayoanza<br />
kutoka damu. Kwa kuhesabu siku kati ya X na X utagundua<br />
mzungukowako ni wa siku ngapi na pia kama hedhi yako<br />
ina mpangilio uliotulia au la.<br />
Weka mtiririko wa siku zako za hedhi kwa<br />
kutumia kalenda<br />
39
40<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Susan, mwenye umri wa miaka 19, ana mzunguko wa kawaida wa siku 28. Mwezi Aprili, alianza<br />
kutoka damu tarehe 1, hivyo hedhi nyingine ilikuwa tarehe 29 ya Aprili. Mwezi Mei alipata hedhi<br />
tarehe 27. Mwezi wa sita alipata hedhi tarehe 23. Mwezi wa saba aliingia mwezini tarehe 20<br />
Mwezi wa nane aliingia mwezini tarehe 16 . Umegundua kuwa hedhi inaanza siku tofauti kila<br />
mwezi japo mzunguko wake una mpangilio uliotulia.<br />
Kumbuka, utaratibu wa kuwa na kalenda ni mzuri. Hukusaidia kufanya mandalizi ya kuingia<br />
mwezini lakini sio njia nzuri ya kujua siku salama zitakuwa lini. Kama unapenda sana kufanya<br />
ngono tafuta njia bora ya kujikinga dhidi ya mimba na magonjwa ya ngono, pamoja na VVU/<br />
UKIMWI.<br />
heDhi inaVYOKOSeSha Raha<br />
Wasichana wengi matiti huvimba na kuongezeka na yanakuwa laini sana kabla ya kuingia<br />
mwezini au wakati yai limerutubishwa.Hali hii haifurahishi, ila ni ya kawaida.Hali hii<br />
inasababishwa na homoni zinazosababisha tishu za matiti kuwa na majimaji zaidi kuliko ilivyo<br />
kawaida. Ukivaa sidiria inayokutosha vizuri itakufanya ujisikie vizuri, na vyakula vyenye chumvi<br />
kidogo vitakusaidia kupunguza kiasi cha maji kinachohifadhiwa na mwili.<br />
Hedhi inaweza kumwathiri mwanamke katika hali yake kitabia. Kabla ya hedhi kuanza kila mwezi,<br />
wasichana wengine hujisikia kulia au kuwa na huzuni. Mara nyingine wasichana wanakuwa na<br />
hasira kwa sababu ya kuvimba matiti yao au mwili kuvimba kidogo au kuvimba sana. Hali hii<br />
mara nyingine inajulikana kama “mahangaiko kabla ya hedhi” na ni matatizo ya kawaida. Jaribu<br />
kuyapuuza yasikusumbue sana.<br />
Wasichana wengine hujisikia maumivu kidogo ya tumbo au mkakamao wa tumbo wakati wa siku<br />
zao za hedhi. Huu mkakamao unatokea kwa sababu misuli ya tumbo la uzazi inabana wakati<br />
ngozi laini inayozunguka tumbo la uzazi inapojiachia na ukuta. Mkakamao huo ni wa kawaida<br />
na unaweza ukavumilika. Iwapo maumivu ni makali lala chini na jaribu kuupumzisha mwili kwa<br />
kuvuta hewa nyingi na taratibu. Vilevile unaweza kuliminyaminya tumbo lako. Njia nyingine ni<br />
kuweka chupa ya maji ya moto tumboni na itakusaidia kupata nafuu. Kama njia hii haikusaidii,<br />
tafuta dawa za tumbo za kutuliza maumivu kwenye maduka ya dawa au dukani.<br />
Mazoezi pia yanaweza kusaidia japo hili halitakuwa jambo la kwanza kulifikiria. Unaweza<br />
kujisikia kama kulala chini, lakini kufanya matembezi au kukimbia huwa kunawasaidia baadhi ya<br />
wasichana kushughulikia tatizo la mkakamao wa tumbo. Ukiweza kupata kisodo aina ya tampoon<br />
unaweza hata kwenda kuogelea. Kuwa katika hedhi kisiwe kikwazo cha kufanya shughuli zako za<br />
kila siku ikiwa ni pamoja na kufanya mambo unayoyafurahia.<br />
Mkakamao wakati wa hedhi na maumivu mara nyingi ndio dalili za awali za balehe na<br />
unapofikisha umri wa miaka 18 au zaidi pengine mambo haya hayatakusumbua sana. Lakini<br />
wasichana wengine hupata maumivu yasiyo ya kawaida wakati wa siku zao. Hawa mara nyingi ni<br />
wasichana wenye hedhi nzito.<br />
Wasichana wenye hedhi nzito mara nyingi wanatumia pedi nyingi usiku na mchana na bado<br />
wanaacha alama ya damu kwenye mashuka au nguo. Mara nyingine wanakosa kwenda shule kwa<br />
sababu wanatoka damu nyingi au wana maumivu makali. Hebu fikiria kukosa kwenda shule kila<br />
mwezi na madhara utakayoyapata katika masomo yako!<br />
Kuna ufumbuzi wa kushughulikia hedhi kali, hivyo usiumie bure. Iwapo kweli una maumivu makali<br />
wakati wa siku zako au unatoka sana damu – kama unakosa kwenda shule kwa sababu ya siku<br />
zako muone muhudumu wa afya. Wahudumu wengine wa afya wanaweza kupendekeza vidonge<br />
vya kuzuia mimba ili kupunguza hedhi nzito yenye maumivu makali. Vidonge vinafanya hedhi<br />
isibadilike badilike ovyo ovyo na vinasaidia kupunguza kiasi cha damu inayopotea kila mwezi.<br />
Iwapo unahitaji kuonana na mganga wako mwulize kuhusu vidonge vya kuzuia mimba. Unaweza<br />
kumeza vidonge hivi hata kama bado ungali hujaanza kufanya ngono. Vidonge vina dozi ndogo ya<br />
homoni ambayo kwa asili inapatikana mwilini. Ni salama kwa vijana wanao balehe.<br />
Kama Mganga hataki kukuandikia cheti cha dawa hizo jieleze,ukipenda mwuulize ufanye nini<br />
kupunguza udhia unaoupata kila mwezi. Usikose kwenda shule kwa sababu ya tatizo linaloweza<br />
kutatuliwa.<br />
Unaweza pia kumwona mhudumu wa afya unapoanza kutoka damu katikati ya mzunguko wa<br />
hedhi au kama siku zako za hedhi zinachukua zaidi ya siku 8.<br />
nGOnO na heDhi<br />
Hakuna ukweli kabisa kuhusu uvumi kwamba ngono inatibu maumivu ya hedhi. Ukweli ni kwamba<br />
kufanya ngono wakati wa hedhi kunaweza kukuongezea uwezekano wa kuambukizwa magonjwa<br />
ya ngono ukiwemo UKIMWI. Damu ya hedhi ni mazingira mazuri kwa bakteria na virusi kukua<br />
haraka.<br />
Iwapo mwanamke aliye katika hedhi amefanya ngono na mwanaume mwenye magonjwa ya<br />
ngono, kuna uwezekano mkubwa kuambukizwa kuliko wakati mwingine wowote wa mzunguko<br />
wake; vilevile kuna uwezekano wa kupata maradhi mengine hatari wakati wa hedhi. Hii ni kwa<br />
sababu mlango wa tumbo la uzazi hufunguka kuliko kawaida ili damu ya hedhi iweze kupita.<br />
Vijidudu vya magonjwa ya ngono vinaweza kusafiri hadi kwenye tumbo la uzazi na kupitia mirija<br />
ya kupitishia mayai, hivyo kusababisha maambukizi kwenye via vya uzazi vya mwanamke,na<br />
hatimaye kusababisha ugumba.<br />
Kwa mwanaume, kufanya ngono na mwanamke aliye katika hedhi ni hatari vilevile.<br />
Kama ameambukizwa VVU, damu yake itakuwa na virusi vingi vya VVU.<br />
KujiSiKia ViZuRi, aFYa na uSaFi<br />
Katika tamaduni zingine, wanawake walio katika hedhi wanachukuliwa kama wachafu. Lakini<br />
ukweli damu ya hedhi ni safi. Baada ya damu ya hedhi kutoka mwilini bakteria wanaweza<br />
wakakua ndani yake, na kusababisha inuke, ndio maana usafi ni muhimu unapokuwa katika hali<br />
hii. Wakati wa hedhi, oga angalau mara moja ili uwe msafi. Usitumie manukato kwenye via vya<br />
uzazi yanaweza kukusababishia muwasho.<br />
Vidokezi vitakavyosaidia kuzifanya siku zako ziwe nyepesi na starehe:<br />
•<br />
•<br />
SURA YA 4 | WASICHANA<br />
Wakati wote kuwa tayari, zijue siku zako za hedhi ili usije ukashitukizwa.<br />
Acha kutumia chumvi nyingi, chumvi inafanya mwili wako uwe na maji mengi, hasa wakati wa<br />
siku zako.Hii inaweza kukufanya kujisikia mwili mzito kuvimba tumbo kutokuwa na raha na<br />
kuwa na mfadhaiko.<br />
41
42<br />
•<br />
•<br />
Kunywa maji mengi au juisi ya mtunda.<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Kula kwa wingi vyakula vyenye chuma nyingi kama samaki, maini, maharagwe, nyama na<br />
mboga za majani. Vyakula hivi vitasaidia kurudishia madini ya chuma yaliyopotea kwa<br />
sababu ya damu iliyotoka.<br />
utatuMia nini KujihiFaDhi na heDhi?<br />
Kihistoria, wanawake na wasichana wakati wote wamepata hedhi na wameweza kuimudu hata<br />
kama kulikuwa hakuna vifaa vya kisasa kuweza kuvinunua madukani kama sasa. Hivyo hata<br />
kama huna fedha ya kununulia pedi na tampons, unaweza kushughulikia siku zako kama kawaida.<br />
Moja ya vitu vya kawaida na rahisi sana kutumia ni vipande vya nguo chakavu. Unaweza<br />
kuvichana kwa ukubwa wa kuenea kwenye eneo la chupi yako na kuvipanga vipande vya nguo<br />
chakavu kimoja juu ya kingine. Hakikisha ni visafi vioshe vizuri na vianike ili viweze kukauka.<br />
Vianike mahali pa siri lakini penye jua ili viweze kukauka. Jua ni dawa nzuri sana ya kuua vijidudu<br />
vya maradhi.<br />
Karatasi za chooni pia siyo aghali, unaweza kununua mabunda matano kwa bei ya bunda moja<br />
la pedi. Itakubidi utengeneze karatasi<br />
nene na refu la kutosha. Mara nyingine<br />
karatasi za chooni zinakwaruza na<br />
zinawezakukusababishia muwasho na uvimbe<br />
kwenye ngozi yako.<br />
Pedi nazo ni nzuri, zimetengenezwa kuweza<br />
kutosha vizurikatikati ya mwili na chupi. Zina<br />
vitu vya kuifanya ijishikizevizuri kwenye chupi<br />
na kukinga tundu la uke.Pedi zinakaratasi<br />
la nailoni kuzuia damu kupenya.Ukitumia<br />
pedi, unatakiwa kuzitupa ndani ya choo cha<br />
shimo au kuchoma moto baada ya matumizi.<br />
Usizitupe ndani ya choo chakuvuta maji kwani<br />
zitakwama na kuziba choo.<br />
Wanawake wengine wanatumia tampon/sodo<br />
ndogo ambayo ni pamba ngumu inayoingizwa<br />
ndani ya uke wakati wa hedhi.Pamba hiyo<br />
hulainika huku ikiendeleakunyonya damu<br />
inayotoka kwenye tumbo la uzazi na kuingia<br />
ndani ya uke. Kuna uzi ambao umefungwa<br />
kwenyesodo ambao unaninginia nje ya uke.<br />
Vuta uzi huu kutoa tampon.<br />
Kitu kizuri kuhusu tampon ni kwamba<br />
haisumbui, hivyo unaweza ukasahau kabisa<br />
kuwa ipo. Lakini tampon zinahitaji uangalifu<br />
zaidi. Wakati wote osha mikono yako kabla ya<br />
kuiingiza. Kama utajiandaa mwenyewe,siku zako za<br />
hedhi hazitakuwa za kutatanisha kwako.<br />
SURA YA 4 | WASICHANA<br />
Unahitaji pia kuzibadili mara kwa mara kwa sababu inaweza kukuletea maambukizi ya magonjwa<br />
ikiachwa muda mrefu kwenye uke. Usiache sodo ndani ya uke zaidi ya masaa 8. Usiitumie usiku<br />
kwa sababu unaweza kulala zaidi ya masaa manane.<br />
Chochote utakachotumia, vitambaa vikuukuu, karatasi za chooni, pedi au sodo vibadili mara kwa<br />
mara kuepuka kuacha damu kwenye nguo au harufu mbaya. Damu ya hedhi inapokutana na hewa,<br />
inaacha harufu mbaya iliyochacha.Chupi zako au nguo zikipata madoa ziloweke kwenye maji<br />
baridi, yenye chumvi kidogo, maji ya moto yanaifanya damu igande na kubakiza doa la kudumu.<br />
Hedhi ni sehemu yako. Ukijiandaa ujio wake, utaona kwamba siyo jambo kubwa la usumbufu,<br />
unaweza kujishughulisha, ukacheza na kufurahi wakati wa siku zako, na hedhi isikukoseshe<br />
kwenda shule au kazini.<br />
43
44<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Sura ya Nne<br />
Wasichana<br />
Wakati wa kubalehe, msichana ategemee mabadiliko mengi ya mwili. Yafuatayo ni baadhi<br />
tu ya mabadiliko yanayoweza kutokea:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Mwili utaongezeka urefu; nyonga itapanuka, mifupa ya mikono, miguu itarefuka.<br />
Msichana atapata umbo la mviringo la kike.<br />
Matiti yatakua na chuchu itaongezeka ukubwa na kuwa na rangi nyeusi.<br />
Sehemu za siri zitakomaa na kuta za uke zitaanza kutoa majimaji.<br />
Damu ya hedhi itaanza kuonekana kila mwezi.<br />
Dalili hizi hutokea kwa muda muafaka ambao ni tofauti kwa kila msichana. Wakati<br />
mabadiliko haya yanatokea, kuna vitu vichache vya kuzingatia:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Kwamba matiti yana ukubwa unaotofautiana kwa kila mwanamke. Matiti yote<br />
yanavutia hivyo yalivyo na ni muhimu kwa kunyonyesha watoto.<br />
Safisha sehemu za siri- ila sio ndani ya uke- kila siku. Vaa chupi zilizotengenezwa kwa<br />
kitambaa cha pamba.<br />
Ni muhimu kuifahamu harufu na hali ya kawaida ya majimaji ya uke ili inapotokea<br />
mabadiliko ujue kuwa ni dalili za maambukizi.<br />
Siku za hedhi kwa msichana anayebalehe hubadilika badilika hivyo hakuna “siku<br />
salama’ za kutopata mimba wala hakuna siku salama ambazo hutaambukizwa VVU au<br />
magonjwa mengine ya ngono.<br />
Ingawa wakati wa hedhi ni kawaida kuumwa tumbo, kuvimba au kujisikia vibaya,<br />
hali hii isifanye msichana akakosa raha. Mazoezi na vyakula vyenye chumvi kidogo<br />
husaidia kupunguza maumivu. Kama maumivu yanakuwa makali na damu nyingi sana<br />
inatoka, kamuone mhudumu wa afya.<br />
Mabadiliko Ya Msingi<br />
Katika Kutunza Mwili<br />
Sura hii inazungumzia jinsi ya kutunza afya ya mwili wako kwa ujumla. Hili linaweza kuonekana<br />
kama sio muhimu ukilinganisha na mambo mengine yaliyomo katika kitabu hiki, lakini ni muhimu<br />
kujua jinsi ya kuishi na afya njema. Kwa kweli matatizo mengi ya afya yanaweza kuepukwa kama<br />
ukila vizuri, ukifanya mazoezi, ukiwa msafi na ukijisikia vizuri.<br />
Ni wajibu wako kuangalia mambo haya kila siku, na kuonekana na kujisikia vizuri iwezekanavyo.<br />
Mwili wako ndio utakaokuwa nao katika kipindi chote cha uhai wako. Kwa hiyo unatakiwa<br />
kuutunza kweli kweli!<br />
jiWeKe MSaFi, nuKia ViZuRi.<br />
Kila mtu anataka kuonekana msafi,<br />
lakini kujihisi kuwa na mvuto<br />
inaonekana ni muhimu hususani katika<br />
kipindi cha ujana balehe kwa sababu<br />
ya mabadiliko makubwa yanayotokea<br />
katika mwili. Sio tu mwili unabadilika<br />
umbo wakati wa balehe, lakini vilevile<br />
unaanza kutoa harufu mpya, majimaji<br />
mapya na hofu mpya hasa kwa vijana.<br />
Hivyo kujizoesha kuwa msafi inaweza<br />
kuwa ni njia nzuri ya kujisikia raha ili<br />
kukabiliana na mabadiliko haya yote<br />
yanayotokea.<br />
Oga angalau mara moja kwa siku ili kujisikia<br />
vizuri na safi.<br />
Sandra, kutoka uganda (umri ; miaka 13)<br />
“Siku zote oga, fua na piga pasi nguo ili uonekane nadhifu.”<br />
Usafi mzuri wa mwili hususani wakati wa balehe ni muhimu kwa sababu ngozi yako inaanza<br />
kutoa majimaji zaidi kuliko ilivyokuwa wakati ukiwa mtoto, na baadhi ya haya majimaji yanaweza<br />
kusababisha harufu mbaya kama huogi.<br />
Majimaji utakayoyaona zaidi ni ya jasho. Jasho linatokana na tezi zilizopo kwenye ngozi. Tezi za<br />
jasho zinakuwa hai zaidi wakati unapofikia balehe.<br />
45<br />
SURA YA 5
46<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Kwa hiyo, vijana balehe hugundua kwamba wanatoka jasho jingi sana. Pia wanagundua kuwa<br />
jasho lao hutoa harufu na ladha yake ni tofauti kuliko jasho la maji ya kawaida analotoka mtoto<br />
ambaye amekimbia wakati wa jua.<br />
Kwapa zako zina tezi nyingi za jasho, lakini pia una tezi nyingi za jasho katika mikono yako, miguu,<br />
na hata katika via vya uzazi, hivyo utagundua kuwa unatoka jasho sana katika sehemu hizi.<br />
Harufu ya jasho lako itabadilika katika kipindi cha balehe, lakini mabadiliko haya ya harufu ya<br />
mwili ni ya kiasili na kiafya. Ni dalili ya kukua.<br />
Ingawa watu wengi wanahofia harufu ya jasho lao, hasa jasho linalotoka kwapani, kuoga mara<br />
moja au mbili kwa siku, na kuvaa nguo safi inatosha kukuweka nadhifu na safi. Kama unatoka<br />
jasho kwa wingi na linakusumbua, vaa chupi iliyotengenezwa kwa pamba na nguo zisizobana<br />
zilizotengenezwa kwa pamba.Nguo za pamba zinauwezo wa kufyonza jasho kuliko nguo za mpira.<br />
Pia pamba huruhusu hewa kupita hivyo husaidia kuleta ubaridi.Baadhi ya watu hununua odorono<br />
za kupaka au kupulizia marashi ili kuzuia harufu inayotoka kwapani.Hivi vyote vinaweza kuwa<br />
aghali.Kuoga na kuvaa nguo safi kunasaidia vema tu.<br />
Kama lilivyo jasho, majimaji mengine ni damu ya hedhi, majimaji ya ukeni, manii na utoko<br />
(vilainisho vyeupe chini govi) - kimsingi vitu hivi ni safi. Lakini punde tu majimaji haya<br />
yanapokuwa yametoka mwilini, bakteria wanaweza kuota ndani yake, na kusababisha harufu<br />
mbaya au wakati mwingine maambukizi.Kwa hiyo, ni muhimu kusafisha maeneo ya via vya uzazi -<br />
eneo la uke na uume kila siku.Wavulana ambao hawajatahiriwa wanahitaji kuvuta nyuma govi na<br />
kusafisha utoko (Angalia sura ya Tatu).<br />
Wasichana inawalazimu kusafisha katikati ya mashavu ya ndani na nje ya uke, lakini hawahitaji<br />
kusafisha ndani ya uke kwa sabuni kwa sababu uke hujisafisha na kujilinda wenyewe kwa kutoa<br />
uchafu. Usafi ni muhimu hususani wakati wa kipindi cha hedhi (angalia sura ya Nne).<br />
Kwa kusafishia via vya uzazi, sabuni ya kawaida ya kuogea ni nzuri kutumia. Hutakiwi kutumia<br />
sabuni zenye kemikali au zenye kuondoa harufu kwapani, kwenye via vya uzazi kwasababu<br />
zinaweza kusababishia mwasho. Kwa kuongezea, sabuni zenye nguvu za kemikali zinaweza<br />
kuuwa bakteria wazuri wanaoishi sehemu kama za uke ambao wanasaidia kulinda baadhi ya<br />
maambukizi. Baada ya kujisafisha unatakiwa kujikausha na kuvaa nguo safi.<br />
Kama una ngozi inayokauka paka mafuta ya mgando (vaselini) mafuta yeyote mengine au losheni<br />
katika viganja vyako, mikono na miguu itasaidia kulainisha ngozi.Losheni inayopakwa mara<br />
baada ya kuoga inasaidia kuhifadhi unyevu unyevu katika ngozi yako.<br />
Osha mikono yako mara kwa mara. Kila mara nawa mikono yako baada ya kutoka chooni na kabla<br />
ya kula au wakati wa kuandaa chakula. Weka kucha zako safi kwa kuzikata na kuwa fupi.<br />
utunZaji Wa MenO YaKO<br />
Mdomoni mwako ni sehemu ambayo bacteria wanaishi pia. Kwa hiyo utunzaji wa meno ni muhimu<br />
ili kulinda afya. Bakteria wa mdomoni wanaweza kutoboa meno yako.<br />
Kutoboka kwa meno kunaweza kusababisha maumivu makali. Meno yaliyooza yanaweza<br />
kusababisha maambukizi ambayo yanaweza kudhuru sehemu nyingine za mwili wako.<br />
SURA YA 5 | MABADILIKO YA MSINGI KATIKA KUTUNZA MWILI<br />
Piga mswaki meno yako angalau mara mbili kwa siku,au baada ya mlo na kabla ya kulala. Hii<br />
inaweza kusaidia kuua bakteria ambao wanakula chakula kinachobaki mdomoni kati ya meno<br />
yako na kusababisha kuoza kwa meno au kupata ugonjwa wa fizi. Kuweka meno yako safi<br />
kunasaidia kuwa na uhakika wa kupumua hewa nzuri.<br />
Unatakiwa kusafisha kila jino - kote mbele na nyuma ya mdomo wako. Pia unatakiwa kusafisha<br />
katikati ya meno yako. Miswaki na dawa za meno ni nzuri, lakini kama huna dawa ya meno<br />
unaweza kusafisha kwa maji tu. Unaweza pia kusafisha meno yako kwa kutumia chumvi kidogo<br />
na maji, ili kulinda ufizi na maambukizi ya mdomoni.<br />
Unatakiwa kuepuka kula vyakula vyenye sukari na soda. Licha ya kwamba vinalishe kidogo,<br />
vina sababisha kuoza kwa meno. Ni muhimu kuepuka kuchangia miswaki kwa sababu inaweza<br />
kueneza maradhi.<br />
chunuSi<br />
Wakati wa balehe, tezi za mafuta katika mwili wako zinakuwa hai zaidi, na zinaanza kutoa vitu<br />
vyenye mafuta vinavyoitwa sebum. Unazo hizi tezi za mafuta katika mwili wako wote; zipo zaidi<br />
kwenye uso wako, shingoni, mabegani, kifuani na mgongoni.<br />
Sebum ni vitu vizuri kwa sababu vinasaidia kuufanya mwili wako uwe laini, nyororo na uonekane<br />
kijana. Japokuwa, wakati wa balehe, tezi zako za mafuta zinaweza kutoa sebum nyingi, na<br />
kuwepo sebum kwa wingi kunaweza kusababisha kuziba kwa vitundu vidogo vidogo vilivyopo<br />
katika ngozi yako. Hii inaweza kusababisha matatizo, kama chunusi.<br />
Kuwepo kwa mafuta katika ngozi yako, na kuwa na sebum za ziada zinazotolewa kipindi cha<br />
balehe, inaonyesha ni jinsi gani ambavyo unaweza kupata matatizo ya ngozi. Kuwa na chunusi ni<br />
kitu cha kawaida kwa hakika, angalau vijana 8 kati ya 10 wana chunusi wakati wa ujana balehe.<br />
Chunusi kwa kawaida zinatokea katika umri wa kati ya miaka 14 na 17, lakini hutokea vilevile kwa<br />
watu wazima, wavulana na wasichana.<br />
Baadhi ya vijana wana chunusi nyingi - tatizo linaloitwa “acne”. Chunusi zina kawaida ya kutokea<br />
kutegemeana na familia. Kama wazazi wako au kaka na dada zako walikuwa na chunusi, utakuwa<br />
katika nafasi ya kubwa ya kuzipata. Zinaweza kuendelea kuwa tatizo kwa baadhi ya watu hata<br />
baada ya ujana kupita.<br />
Presha za maisha zinaweza kusababisha chunusi. Vijana wengi wanajikuta wana chunusi<br />
nyingi hususani wakati wa matukio muhimu kama, mitihani, miadi au kitu chochote ambacho<br />
kitamsisimua.<br />
Baadhi ya wasichana wanakuwa na chunusi nyingi wanapokaribia kipindi cha kupata hedhi.<br />
Kuna porojo nyingi kuhusu chunusi, na watu wengine wanasema maneno ya uongo kama: “chunusi<br />
ni dalili ya msichana au mvulana aliye ana hamu ya kufanya ngono.” Sio kweli, ngono haitibu<br />
chunusi.<br />
47
48<br />
utaFanYa nini na chunuSi<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Chunusi ni jambo la kawaida kwa vijana balehe. Kwa bahati mbaya , hakuna jinsi tunavyoweza<br />
kuzikwepa kabisa; wala hakuna matibabu ya ajabu ya kutibu chunusi. Hata hivyo, yapo mambo<br />
kadhaa ambayo unaweza kuyafanya ili kushughulikia chunusi.<br />
Ni jambo muhimu sana kutunza ngozi yako, hususani kama unaishi sehemu zenye joto, vumbi<br />
na unyevu unyevu. Unaweza kutumia sabuni ya kuogea na maji ya uvuguvugu kuosha taratibu<br />
sehemu za mwili wako zenye mafuta – usoni, shingoni, mabegani, mgongoni na juu ya kifua.<br />
Ukiosha sehemu hizi angalau mara moja kwa siku itasaidia kuondoa mafuta kwenye ngozi na<br />
kusababisha vinyweleo kuwa safi na wazi.<br />
Lakini usisugue sana ngozi yako au kutumia sabuni zenye nguvu na kali kwa sababu zinaweza<br />
kusumbua ngozi yako na kusababisha chunusi zaidi. Kamwe usitumie sabuni za kufulia, sabuni<br />
ya unga na dawa ya madoa, kwani zitaharibu ngozi yako. Jaribu kutoruhusu mafuta unayopaka<br />
kichwani yasifike usoni kwa sababu mafuta haya yanaweza kuzuia vinyweleo vya ngozi yako.<br />
Mwisho, kuwa mwangalifu na matumizi ya krimu za usoni na zile za kung’arisha ngozi. Ingawa<br />
zimeandikwa kwamba ukizitumia ngozi yako itakuwa nyororo na nzuri, krimu zingine zinaharibu<br />
ngozi kabisa. Kwa nyongeza, dawa nyingi za kulainisha ngozi zina vitu ambavyo si vizuri kwa afya<br />
yako.<br />
Ingawa wakati mwingine<br />
unashawishika kuminya<br />
chunusi,sio vizuri. Kama<br />
utafanya hivyo, usaha<br />
unaweza kutawanya<br />
maambukizi kwenye<br />
vinyweleo vingine, na<br />
vilevile unaweza kupata<br />
makovu ya kudumu.<br />
Chunusi zinasumbua,<br />
zinaweza kusababisha<br />
maumivu na uchungu, na<br />
zinaweza kuleta usumbufu<br />
wakati mwingine. Lakini ni<br />
sehemu ya ujana balehe.<br />
Vijana wengi wanajihisi<br />
Hata kama unafikiria kwamba chunusi zako ni mbaya, watu wengine<br />
hawajaziona bado.<br />
kuwa ni wao pekee wenye kusumbuliwa na matatizo ya ngozi, lakini hii ni kwa sababu hawajui<br />
kwamba hata wenzao wa rika moja wanazo chunusi. Za kwako zinaonekana zaidi kwako<br />
kuliko watu wengine wanavyoziona chunusi zako. Unaweza kudhani kilamtu anaziangalia, na<br />
anaangalia ngozi yako mbaya tu na wala hakuangalii wewe. Lakini hii sio kweli. Watu wengine<br />
wanayo mambo mengi ya kufikiria na kwa hakika wanachoangalia ni kujua wewe ni nani na wala<br />
sio ngozi yako inaonekanaje. Kwa hiyo, usivunjike moyo na usiache chunusi chache zikunyime<br />
raha! Hautakuwa nazo milele.<br />
utunZaji Wa nYWele<br />
Tunazo nywele mwili mzima, lakini zaidi kichwani, kwapani na maeneo yanayozunguka via vya<br />
uzazi. Kutunza nywele zako ni sehemu nyingine ya kutunza usafi na kutunza vizuri mwili wako.<br />
SURA YA 5 | MABADILIKO YA MSINGI KATIKA KUTUNZA MWILI<br />
Nywele zilizopo kichwani mwako ni rahisi kuzitunza hususani kama utakuwa unazipunguza kila<br />
mara. Hata kama unakata nywele kila mara na kuzisuka, unatakiwa kuziosha ili zisiwe na vumbi<br />
na ziwe safi. Kama uko shuleni, jaribu kutochangia chanio kwa sababu unaweza kupata chawa,<br />
maambukizi ya fangasi, na minyoo. Kama utachangia vitana, hakikisha unaviosha vizuri kwa maji<br />
ya moto yenye sabuni kabla na baada ya kutumia.<br />
Watu wengine wana matatizo ya mba, hali ambayo inasababishwa na ngozi ya nywele kuwa kavu<br />
mno.Mba unasababishwa na chembechembe ndogo za ngozi mfu, na watu wengine wenye mba<br />
nyingi wanatumia shampuu maalumu zenye dawa ili kuzuia mba.<br />
Ni vema kuoga mara kwa mara ili kuziweka safi nywele zilizopo kwenye mwili wako, nywele<br />
zilizopo kwenye kwapa, na nywele zilizopo kwenye maeneo ya via vya uzazi. Kama ulivyosoma<br />
sura ya 2 nywele hizi zinasaidia kuondoa jasho na uchafu kwenye mwili wako. Hata hivyo, sehemu<br />
nyingine za Afrika watu wananyoa nywele hizi kwa vile wanajisikia vizuri bila nywele hizo.<br />
Kama mila na tamaduni zako zinapinga kuwa na mavuzi yakate kwa kutumia mkasi. Usiziondoe<br />
zote kabisa kwa kutumia krimu ya kuondolea nywele au kwa kunyoa. Mafuta ya kunyolea nywele<br />
yanasumbua na kuumiza ngozi laini katika sehemu za siri. Pia kunyoa mavuzi kuna madhara<br />
yake. Kama unanyoa mavuzi, uwezekano wa kujikata ngozi ni mkubwa. Iwapo utajamiiana,<br />
mikato hii ni milango ya kupitishia VVU. Hii ni hatari. Tatizo lingine la kunyoa mavuzi ni wakati<br />
mavuzi yanaota tena. Nywele zinakuwa na incha kali kiasi cha kuweza kutoboa kondomu. Vilevile<br />
maeneo yanayozunguka via vya uzazi yaliyonyolewa yanaweza kupata maambukizi kidogo<br />
kwenye vinyweleo au sehemu ambazo mavuzi yanaota. Kunyoa mavuzi kiasi ni salama kidogo,<br />
lakini kuwa mwangalifu usiondoe nywele zote.<br />
liShe nZuRi<br />
Margareth, kutoka tanzania (umri; miaka 18,)<br />
“Nilipokuwa darasa la sita, nilianza kuota nywele sehemu za siri. Mama<br />
yangu aliniambia kuwa, zikikua na kuwa ndefu ninatakiwa nizipunguze na<br />
kuzisafisha vizuri, la sivyo nitanuka.”<br />
lois kutoka tanzania (umri; miaka 13)<br />
“Nimeona nywele kwenye kwapa, kwa vile sio muda mrefu nilipoziona<br />
sijazikata bado”<br />
Lishe nzuri ni muhimu kwa afya njema. Kula chakula chenye virutubisho ni muhimu katika maisha<br />
yote lakini ni muhimu zaidi wakati wa utoto na wakati wa balehe kipindi ambacho mwili wako<br />
unakua na unaongezeka kwa kasi sana.<br />
Mwili wako unahitaji chakula kizuri ili ukue na upate nguvu kwa ajili ya kufanya vizuri shuleni,<br />
kucheza michezo na kufanya kazi.<br />
Wakati mwingine vijana wadogo hawali mlo wenye lishe na wanasahau kula kwa wakati maalum<br />
uliopangwa. Wanaweza kuacha mlo kamili na badala yake wakakazania kula biskuti, chips,<br />
chokoleti, vitu vitamu na soda. Hivi vyakula havina lishe, na mwili wako unahitaji zaidi ya hivi ili<br />
uwe na afya.<br />
49
50<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Kila aina ya chakula ina kazi yake mwilini kwa hiyo unahitaji kula milo yenye kila aina ya chakula.<br />
Aina za msingi za vyakula ambayo mwili unahitaji ili uweze kufanya kazi vizuri ni:<br />
“Vyakula vyenye wanga” au vyakula vyenye kuleta nguvu”: Vyakula hivi vinajumuisha ugali,<br />
fufu, mihogo, viazi vitamu, viazi mviringo, mikate, mchele, ndizi, ulezi, na mtama.<br />
“Vyakula vya kulinda mwili”: Vyakula vya kulinda mwili ndani yake vina vitamini na madini<br />
muhimu ambayo mwili wako unahitaji ili uweze kufanya kazi vizuri na uwe na afya. Vitamini na<br />
madini vinapatikana katika mboga za majani, (kama vile spinachi, majani ya maboga, kisamvu),<br />
nyanya, maboga na karoti. Pia matunda ya aina zote kama, papai, embe, chungwa,na nanasi nayo<br />
yana vitamini muhimu.<br />
“Vyakula vya kujenga mwili”: Vyakula vya kujenga mwili vina protini. Protini husaidia mwili<br />
wako uweze kukua na kujengeka vizuri, hususani wakati wa ujana balehe.Pia husaidia mwili wako<br />
ujiponye na kujikarabati wenyewe ukiumia.<br />
“Vyakula vya kujenga mwili” vinajumuisha karanga, njegere, maharage, kunde, nyama, kuku,<br />
samaki wabichi, samaki wa kukaushwa na konokono. Mayai, maziwa, maziwa mgando na jibini<br />
yana protini vilevile. Vyanzo vingine vya protini – nyama, samaki, maharage na njegere, pamoja<br />
na mbogamboga za majani ya kijani kilichokoza – ni vyanzo vya madini ya chuma pia.Madini ya<br />
chuma ni muhimu hususani kwa wasichana na wanawake kwasababu wanahitaji madini ya chuma<br />
ya ziada wakati wakiwa katika hedhi na wakati wakiwa wajawazito.<br />
Mafuta na vitu vitamu: Mafuta ni chanzo cha nguvu mwilini. Baadhi ya mafuta, kama vile ya karanga,<br />
ya nazi, ya mawese yanatokana na mimea wakati mengine kama vile siagi au samli yanatokana<br />
na wanyama. Mafuta yanaleta nguvu nyingi, lakini mwili unahitaji nguvu kidogo tu. Hivyo<br />
basi, ukila mafuta mengi sana unaweza ukapata matatizo ya kiafya siku za usoni.Chanzo kingine<br />
cha nguvu mwilini ni sukari. Kwa ujumla vitu vitamu ni vibaya kwa meno yako.<br />
Fikiria kuhusu mlo wako na hakikisha unapata aina zote muhimu za chakula kama zilivyoonyeshwa<br />
katika ukurasa wa 51, “Vyakula vya kuleta nguvu” vinatakiwa kuwa ni vya msingi katika mlo wako<br />
na unatakiwa ule vyakula hivi. “Vyakula vya kulinda mwili ni muhimu sana pia, kwa hiyo kula kwa<br />
wingi matunda na mboga mboga. “Vyakula vya kujenga mwili” ni muhimu sana, lakini huna haja ya<br />
kula mara nyingi kwa siku. Mwisho ni vyema kula kidogo vyakula vya mafuta na vyakula vitamu.<br />
NI KIASI GANI CHA NGUVU MWILI UNAHITAJI?<br />
Nguvu unayohitaji inategemea na nguvu unayotumia. Ukuaji wakati wa balehe unatumia nguvu<br />
nyingi. Kwa hakika kijana balehe anahitaji nguvu nyingi ukilinganisha na mtu mzima.<br />
Nguvu inapimwa kwa kalori. Kama ukila vyakula vyenye nguvu zaidi kuliko mwili wako unvyohitaji<br />
kwa siku, kiwango cha ziada cha karoli kitabadilishwa na kuwa mafuta na mwili wako utahifadhi<br />
mafuta hayo kwa muda. Watu wengi hudhani kuwa na mafuta mengi ni afya njema na ni jambo la<br />
kawaida, lakini inaweza kuwa ni tatizo kama ukiwa na mafuta mengi. Baadhi ya watu hususani<br />
watu ambao wanakula sana vyakula vyenye kalori nyingi (vyakula vyenye mafuta na sukari) na<br />
ambao hawafanyi mazoezi – wanakuwa wanene sana.<br />
SURA YA 5 | MABADILIKO YA MSINGI KATIKA KUTUNZA MWILI<br />
Katika baadhi ya miji ya Afrika, wapo wavulana na wasichana wengi wenye uzito mkubwa kuliko<br />
wanavyotakiwa wawe. Hii ni kwa sababu kufanya mazoezi katika miji ni vigumu. Pia vyakula<br />
vingi vya kukaangwa huuzwa mijini. Vyakula vilivyokaangwa vinaweza kuandaliwa kwa haraka<br />
na urahisi - vinaweza kuandaliwa haraka zaidi kuliko vyakula vya asili, kama vile maharagwe<br />
na michuzi. Japokuwa chakula kilichokaangwa kinaweza kuwa na ladha nzuri na kinaweza<br />
kuandaliwa haraka, sio kizuri kwa afya njema. Mlo wa chakula kilichokaangwa kinaweza<br />
kuwafanya watu wawe wanene sana na baada ya muda mrefu, kinawadhuru moyo na mishipa ya<br />
damu.<br />
Jaribu kuepuka kula chakula chenye mafuta na kilichokaangwa. Vilevile epuka chakula na<br />
vinywaji vyenye sukari.<br />
MaZOeZi<br />
Lishe bora inajumuisha mchanganyiko wa vyakula vya aina tofauti, kwa viwango tofauti<br />
Kila mtu anahitaji mazoezi: Watoto, vijana, wazee – wasichana na pia wavulana. Mazoezi<br />
yanakufanya uwe mzuri ung’ae, mwenye umbo zuri na macho maangavu. Yanakufanya uwe<br />
mwenye nguvu kwa sababu yanaimarisha moyo wako na mapafu; hujenga misuli na unene wa<br />
mifupa yako. Yanakufanya uwe na uwezo zaidi wa kupambana na magonjwa kwa kuongeza nguvu<br />
ya mfumowa kulinda mwili.<br />
nfune kutoka Zambia (umri; miaka 13)<br />
“Nina afya nzuri kwa sababu nakula mlo kamili na ninafanya mazoezi<br />
kwa wingi.”<br />
51
52<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Mazoezi yana faida nyingine zaidi, yanaimarisha hisia<br />
zako, yanajenga kujiamini, yanakufanya ujisikie vizuri.<br />
Kama unajihisi kuwa na mfadhaiko, hali mbaya au<br />
huzuni, tembeatembea au cheza mchezo wa kurusha<br />
mpira.Fanya mchezo wa kukaa na kunyanyuka. Cheza<br />
mpirawa pete. Endesha baiskeli, ruka kamba, ogelea,<br />
Cheza mpira wa wavu au mpira wa meza. Fanya kitu<br />
chochote kitachofanya moyo wako uende kasi ili<br />
kuongeza morali.<br />
Mazoezi yanaweza pia yakawa njia nzuri ya kukufanya<br />
uwe hodari katika stadi muhimu za maisha, kama<br />
kujiamini, ushirikano na kufanya kazi kwa pamoja. Watu<br />
wengi kwanza hujifunza stadi hizi wakati wakicheza<br />
michezo au wakati wanapojiunga na timu.<br />
Kufanya mazoezi mengi haimaaanishi kuwa lazima<br />
ujiunge na klabu ya michezo. Kusaidia kazi za shambani,<br />
kwenye bustani au kuzunguka nyumba yanaweza kuwa mazoezi mazuri. Shughuli za nyumbani<br />
zinaweza kujenga mahusiano mazuri na wazazi wako.<br />
Baadhi ya watu ni wakimbiaji wazuri lakini wengine<br />
sio. Baadhi ya watu wana vipaji maalum vya mpira<br />
wa miguu, kukimbia kwa kasi au kuogelea vizuri,<br />
kama vile ambavyo watu wengine ni wazuri katika<br />
hisabati au katika kujifunza lugha. Hata kama wewe<br />
si mkimbiaji, unatakiwa kufanya mazoezi kwa wingi.<br />
Kila mtu ana mwili ambao unatakiwa autumie. Kwa<br />
mfano kwa kujinyoosha, kusukuma au kujaribu<br />
mambo kadhaa. Unaweza kujikuta unapofanya<br />
mazoezi unafurahi zaidi na zaidi. Unaweza ukawa<br />
mwana riadha bila ya wewe mwenyewe kujua!<br />
Iwapo hujazoea kufanya mazoezi, inaweza kuwa<br />
vigumu unapoanza. Unaweza kujikuta unashindwa<br />
kupumua wakati wa kukimbia. Mazoezi yanaweza<br />
Kuna njia nyingi nzuri za kufanya mazoezi kukufanya ujisikie vibaya na hivyo kutoendelea<br />
nayo. Kwa hiyo, anza taratibu. Tafuta mchezo<br />
unaoupenda na jenga nguvu zako, hivyo unaweza<br />
kufanya zaidi na zaidi. Nia ni kufanya moyo wako uende kasi, kujisikia kwamba unapumua<br />
haraka kuliko kawaida, na kuwa na joto mwilini. Jaribu kufanya hivi kwa angalau dakika 20, mara<br />
3 kwa wiki.<br />
Fanya mazoezi yako kila mara na utaona maendeleo mazuri.Ngozi yako itang’aa. Macho yako<br />
yatang’aa, utakuwa na furaha na raha. Utajiamini zaidi na kuwa na uwezo wa kuyakabili matatizo.<br />
Na kwa hakika utakuwa na nguvu na mwenye afya pia. Kwa hivyo endelea na mazoezi na usiache<br />
kufanya ati kwa sababu ni kipindi cha mitihani.Wakati wa mitihani ndio unahitaji kufanya mazoezi<br />
zaidi.<br />
SURA YA 5 | MABADILIKO YA MSINGI KATIKA KUTUNZA MWILI<br />
Ruvimbo kutoka Zimbabwe (umri;miaka 13)<br />
“Naendesha baiskeli ili kujishughulisha na<br />
kwa sababu za kiafya. Vijana wanatakiwa<br />
wajishughulishe, Dunia ina mambo mengi ya<br />
kufanya.”<br />
Godfrey, kutoka Zimbabwe (umri; miaka 19)<br />
“Napenda michezo, Nacheza mpira wa kikapu<br />
kuuweka mwili wangu imara na wenye afya<br />
nzuri.”<br />
Maumbile mazuri hupatikana kwa kufanya mazoezi;<br />
maumbile mabaya husababisha maumivu katika kifua na mgongo.<br />
MaPuMZiKO MaZuRi<br />
endelea na mpangilio wako wa mazoezi na<br />
utaona tofauti !<br />
Pamoja na chakula kizuri na mazoezi ya kutosha, unahitaji kupumzika vya kutosha. Kupumzika<br />
kunaruhusu mwili kuhifadhi zaidi nguvu. Kupumzika kunaweza kuwa katika hali ya kupumzika<br />
kimwili au kulala usingizi<br />
Tumia muda kupumzika kila siku kwa kusoma kitabu, kufanya kitu unachofurahia, kusikiliza redio,<br />
au kwa kutafakari maisha yako. Kwa kiwango kidogo, televisheni inaweza kukufanya upumzike,<br />
lakini usitumie muda mwingi kuangalia televisheni au video.<br />
Kulala ni njia muhimu ya kupumzika. Ni wakati wa kulala tu ndio moyo wako unapunguza mapigo<br />
na misuli yako inapumzika. Hii inaruhusu mwili wako kurudisha na kujiponya na hali ya mfadhiko<br />
au majeraha. Unahitaji kulala sana kipindi cha balehe kwa sababu mwili wako unatumia nguvu<br />
nyingi. Watu wengi wanahitaji kama kiasi cha masaa 8 ya kulala usiku mmoja. Baadhi ya watu<br />
wanahitaji pungufu, na baadhi ya watu wanahitaji zaidi. Kama, unajisikia kuchoka muda wote,<br />
hakikisha unakwenda kulala mapema. Mabadiliko yote yanayotokea mwilini mwako yanachosha,<br />
kwa hiyo hakikisha unaupa mwili wako nafasi ya kupumzika!<br />
53
54<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Sura ya 5<br />
MAMBO YA MSINGI KATIKA KUTUNZA MWILI<br />
Kuna vitu vichache, rahisi na vya msingi unatakiwa kuvijua kuhusu kutunza mwili wako.<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Utakapofikia kipindi cha balehe, utaanza kutoa jasho zaidi. Kuoga kutakufanya uwe<br />
msafi na kunukia vizuri<br />
Osha meno yako angalau mara mbili kwa siku ili kuepuka meno kuoza na pia ili utoe<br />
pumzi nzuri.<br />
Kama tezi zako za jasho, zinatoa mafuta, unaweza kuwa na chunusi. Chunusi ni sehemu<br />
ya ujana balehe na hakuna njia ya kuziekwepa. Kuuweka mwili wako safi kwa kuoga na<br />
maji na kutumia sabuni ni suluhisho lakini usisugue ngozi yako sana, na usitumie sabuni<br />
ya kufulia kwa sababu itaharibu ngozi yako<br />
Kula mlo wenye lishe ukiwa na vyakula vya “kulinda” na “kujenga mwili”. Epuka kula vitu<br />
vyenye sukari na vyakula vilivyo kaangwa<br />
Fanya mazoezi ya kutosha. Mazoezi yanaimarisha moyo wako, mapafu, na misuli,<br />
yanakuweka imara na yana amsha ari.<br />
Mabadiliko yote unayoyapitia ni muhimu sana, kwa hiyo upe mwili wako nafasi ya<br />
kupumzika kiasi cha masaa 8 kwa usiku.<br />
Kwa kujizoesha kuwa msafi, kula vizuri, kufanya mazoezi vizuri na kupumzika, utaruhusu<br />
mwili wako kufanya kazi vizuri, utajisikia vizuri, kimwili na utajisikia vizuri kiakili.<br />
Utunzaji Afya Ya Akili<br />
Na Moyo<br />
Sura hii inahusu afya ya hisia zako. Afya ya hisia inahusisha mambo mengi, kama kujipenda,<br />
kujiamini, kustahimili wasiwasi, mfadhaiko, na huzuni na kuelewana na watu wengine. Kuwa<br />
mwenye afya nzuri ya hisia maana yake ni kujisikia vizuri wewe mwenyewe. Vile vile maana yake<br />
ni kuwa na nguvu za ndani za kuweza kustahimili raha na shida katika maisha.<br />
Madaktari hawajajua ni kwa nini mtu awe na afya nzuri kihisia na mwingine asiwe nayo.<br />
Inawezekana ni mchanganyiko wa haiba ya kuzaliwa nayo na namna ambavyo ulilelewa ukiwa<br />
mtoto mdogo. Afya nzuri kihisia inategemea pia na mtazamo wako - je upo tayari kutengeneza<br />
afya yako iwe nzuri kihisia?<br />
Kila mtu anaweza kujitahidi awe na afya nzuri ya kihisia. Hii inamaanisha kujienzi na kujiamini.<br />
Vile vile ina maana ya kujenga stadi ili kumudu wasiwasi, mfadhaiko na huzuni. Vile vile<br />
inamaanisha kujenga mahusiano na watu wengine.<br />
KujiheShiMu<br />
Kamusi ya “Oxford inatafsiri “Kujiheshimu” kama “mawazo” mazuri kuhusu tabia ya mtu<br />
mwenyewe” Iwapo unajiheshimu sana, maana yake ni kwamba unajisikia vizuri.Unajua kwamba<br />
unayothamani - mtu unayestahili<br />
kupendwa. Unajiheshimu mwenyewe. Hisia<br />
za namna hii ni nzuri sana, unapojihisi<br />
kupendwa na kuheshimiwa unategemea<br />
hivyo hivyo kutoka kwa watu wengine<br />
vilevile.<br />
Unapojiheshimu sana haina maana ya<br />
kwamba wewe huwezi kujichukia au<br />
kujikasirikia mwenyewe. Kuna wakati kila<br />
mtu hukata tamaa, lakini yule mwenye<br />
kujiheshimu anakubali makosa na kusonga<br />
mbele.<br />
Kujiheshimu ni tofauti na kujidai au kuwa<br />
na majivuno mengi.Watu wanaojienzi<br />
wanajipenda, lakini haina maana ya kwamba<br />
wanajifikiria wao hawana dosari yoyote, au<br />
wao ni bora kuliko wengine.<br />
55<br />
SURA YA 6
56<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Kujienzi ni kitu ambacho kipo ndani yako. Lakini hiyo haimaanishi huwezi kuifanyia kazi au<br />
kuhitaji kuikuza na kuijenga. Unaweza kuzingatia yafutayo ili ujenge tabia ya kujienzi:<br />
•<br />
•<br />
JE UNAJUA Maana ya kuwa na Afya nzuri kihisia?<br />
Inaweza ikawa vigumu kuelezea afya nzuri ya kihisia. Lakini kawaida utaijua kwa kuona.<br />
Kwa mfano tumchukulie Rose, anaelekea kuwa na furaha wakati wote na anaonekana<br />
kuyamudu maisha ya raha na tabu.<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Anapopata maksi za chini anakubaliana nazo na anaongeza bidii.<br />
Akiachwa na mpenzi wake, analia lakini baadaye anaamua kwamba siyo mwisho wa<br />
dunia.<br />
Kipindi cha mitihani, huwa hafadhaiki sana. Hufanya mazoezi na kuzungumza na rafiki<br />
yake mpenzi kukabili mfadhaiko.<br />
Rose anajienzi sana. Hashindwi na hisia anapoachwa na mpenzi wake. Hujitambua kama ni<br />
mtu muhimu. Vile vile anajiamini sana. Ni kweli kwamba alifanya vibaya kwenye majaribio,<br />
lakini anajua anaweza kufanya vizuri zaidi. Hahitaji kumlaumu mwalimu. Njia anayotumia<br />
kupambana na mfadhaiko ni nzuri. Michezo na kumwambia rafiki anayemwamini matatizo<br />
yanayomsibu kunamsaidia kushughulikia wasiwasi na kisha kusonga mbele.<br />
Aidha, watu wengine wanapata shida sana kumudu raha na shida za maisha. Kwa mfano<br />
Emma, ambaye yuko katika mazingira yanayofanana na ya Rose, hufanya kila kitu tofauti.<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Hakubali kukosolewa badala yake humlaumu mwalimu kwa kupata alama mbaya.<br />
Akiachwa na mpenzi wake anafadhaika. Hutangaza mambo ya uongo kuhusu mvulana<br />
huyo na huanza kufanya mbwembwe na wavulana wengine.<br />
Anapokuwa na mfadhaiko anaanza kunywa pombe na kuvuta sigara.<br />
Inakuwaje Emma anapata shida sana kuyamudu matatizo haya? Jambo mojawapo ni<br />
kujienzi. Anaumia sana anapoachwa na mpenzi wake na anayamudu maumivu kwa<br />
kumsema rafiki yake vibaya. Anajaribu kujihakikishia kwamba bado anapendwa kwa<br />
kumpenda mvulana mwingine. Njia yake ya kupambana na mfadhaiko haifai kabisa, pombe<br />
na sigara vinaweza kukusahaulisha kwa muda lakini havitatui tatizo.<br />
Epuka kujilinganisha na wengine mara kwa mara. Weka malengo yako, na usijihukumu<br />
mwenyewe kwa kuangalia mafanikio ya mtu mwingine. <strong>Maisha</strong> ni safari ndefu. Kuna wakati<br />
utaenda mbele na wakati mwingine utarudi nyuma.<br />
Tambua vipaji vyako na kujikubali vile ulivyo.Tengeneza orodha ya mambo unayoyafanya<br />
vizuri. Je wewe ni msanii? Mwanariadha.Mwimbaji, msimuliaji wa hadithi au mnenguaji<br />
(mcheza dansi) Ni masomo gani unayofanya vizuri shuleni?<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Fikiria wewe ni mtu wa aina gani na kutengeneza orodha ya sifa ulizonazo. Unapenda nini<br />
kuhusu wewe mwenyewe? Wema wako? Ucheshi? Ubunifu? Umakini?<br />
Fahamu mambo yanayokuhusu ambayo ungependa kuyaboresha, lakini usijikosoe sana.<br />
Kuwa mhalisi na weka malengo ambayo yanatekelezeka na yatakayoonyesha mafanikio ili<br />
uridhike unapoyakamilisha.<br />
Jiamini, na jiambie “ninaweza!”.<br />
Tumia muda wako na watu wanaokujali wanaofanya ujisikie vizuri na kuongeza hadhi ya<br />
kujiheshimu. Kaa mbali na watu wanaojaribu kuharibu heshima yako, hasa kama wanafanya<br />
hivyo kwa sababu fulani.<br />
Kwa vyovyote vile kuifanyia kazi heshima yako haina maana kuwa hutaweza kupata matatizo.<br />
Kuifanyia kazi heshima yako itakusaidia matatizo kuwa mepesi. Kujiheshimu kunakulinda wewe<br />
binafsi. Wakati mtu anakutendea vibaya hisia za kujiheshimu zinapiga kelele “Hee! haya ni<br />
makosa, usiruhusu mtu huyu akakutendea hivi”.<br />
Hebu fikiria kana kwamba marafiki zako wamekuacha. Wamejiunga pamoja na kukuacha peke<br />
yako. Ghafla unajisikia kutetemeka na huna uhakika wa mambo yako. Ni kwa nini hawakutaki<br />
tena? Je kuna makosa umefanya? Heshima yako inaanza kufifia kama ua linavyonyauka.Unaanza<br />
kujisikia vibaya.<br />
Katika mazingira ya namna hii, watu wengine hupata hofu. Wanachukua njia rahisi ya kurudisha<br />
heshima inayoshuka ili apendwe tena, hata kama itamaanisha kufanya jambo ambalo wanafikiria<br />
ni kosa. Kwa mfano, vijana wengine ambao wamekataliwa na marafiki zao wa zamani huanza<br />
kujiunga na makundi ya vijana wanaokunywa pombe, wanaovuta bangi na kujiingiza kwenye<br />
matatizo makubwa. Hivyo wanaanza nao kula madawa ya kulevya, kunywa pombe ili waweze<br />
kukubalika.<br />
Ni vizuri kutafuta kukubalika na kweli inapandisha hadhi lakini haisaidii kutatua matatizo ya<br />
kujiheshimu na wala kukubalika hakudumu. Unaweza kujisikia vizuri kwa muda lakini baada<br />
ya muda mfupi sauti ndogo ndani yako huanza kukusumbua: “Watu hawa hawako makini”. Sauti<br />
hii ni kwamba haujawa mkweli kwako mwenyewe, unajizuia kufanya mambo unayoyataka na<br />
unayoyaweza. Hujisikii vizuri kutokana na yale unayoyafanya kwa mkumbo...” Hiyo sauti ndogo ni<br />
nafsi yako. Ni vema wakati wowote kuisikiliza.<br />
Kurekebisha kujienzi kwako ni kazi kubwa kuliko kujiunga na makundi mapya, au kupoteza<br />
mawazo kwa kutumia pombe, na madawa ya kulevya, (kwa taarifa zaidi kuhusu madawa ya<br />
kulevya na pombe soma sura ya 12). Itakusaidia zaidi kurekebisha kujienzi kwako. Unapopitia<br />
matatizo ya kujienzi, yafuatayo ni mambo machache unayoweza kuyafanya ili yakusaidie:-<br />
•<br />
•<br />
SURA YA 6 | UTUNZAJI AfYA YA AKILI NA MOYO<br />
Jaribu kuliweka tatizo lililopo katika mtazamo sahihi. Jaribu kukumbuka kwamba dunia<br />
imejaa mambo ya raha na shida, na kwamba huu sio mwisho wa dunia.<br />
Zungumza na mtu wa karibu yako na unayemwamini kuhusu matatizo yako na hisia<br />
zako. Mtafute kijana mtoa ushauri nasaha au mtu ambaye anakujali na ambaye anaweza<br />
kukusaidia.<br />
57
58<br />
•<br />
•<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Kumbuka kuwa watu wengine wanakuthamini kutokana na vile ulivyo. Mtafute mtu ambaye<br />
atakuthamini – rafiki mpya, mwalimu, dada, kaka, mzazi au ndugu mwingine.<br />
Kuwa mvumilivu. Kujiheshimu hakujengeki katika siku moja.Unaweza kujisikia vizuri baada<br />
ya siku kadhaa.<br />
KujiaMini<br />
Unapokuwa unajenga kujienzi, unajenga kujiamini pia. Kujiamini ni jambo la msingi katika afya<br />
ya kihisia. Kama kujienzi maana yake kujisikia vizuri na ukamilifu kuhusu tabia yako na namna<br />
ulivyo, kujiamini maana yake kujisikia vizuri kuhusu uwezo wako wa kufanya mambo.<br />
Kujiamini ni jambo kubwa. Watu wanaojiamini<br />
wanajisikia huru kujaribu kufanya mambo<br />
mapya bila ya kuwa na wasiwasi mkubwa<br />
kama watashindwa. Hawaogopi kujiingiza<br />
katika mazingira mapya na kati ya watu wasio<br />
wafahamu. Hawajali hata kidogo watu wengine<br />
watawafikiriaje.<br />
Kujiamini kunavutia sana. Watu wanaojiamini<br />
mara kwa mara wanapendwa sana kwa sababu<br />
wanaonekana kufurahia maisha kwa kiwango<br />
kikubwa wanapopata changamoto mpya na<br />
uzoefu wa mambo mapya.<br />
Kujiamini kunajitosheleza. Kwa maneno mengine,<br />
kujiamini kunasabisha kujiamini zaidi. Hii maana<br />
yake ni kwamba kwa jinsi unavyojaribu kufanya<br />
mambo mapya ndivyo unavyozidi kujiamini. Hii<br />
inasababishwa na sababu mbili zifuatazo:<br />
1. Unajifunza kwamba unaweza kufanikiwa katika mambo mengi ambayo hukuwahi kufikiria<br />
ungeweza.<br />
2. Unajifunza kwamba hata kama unashindwa kufanya jambo fulani hakuna neno.<br />
Unapojiamini, wakati mwingine unaweza kushindwa, lakini mara nyingi utafanikiwa. Hii ni<br />
kwasababu unaposhindwa kufanya kitu, mara kwa mara ni kwa sababu unakuwa na wasiwasi<br />
au kiwewe. Unapojiamini hata hivyo unaweza kufanya mambo mapya. Kwa ujumla, wasiwasi na<br />
kutojiamini hakuleti matatizo makubwa katika kuwa makini kwa lolote unalojaribu kufanya.<br />
Lifanyie kazi suala la kujiamini, itakusaida maisha yako yote. Unaweza:-<br />
Kujifikiria kama mtu unayeweza – yule ambaye unaweza kufanikisha.<br />
•<br />
•<br />
Kujiamini kunakuwezesha kujaribu mambo<br />
mapya bila kuhofu kushindwa<br />
Jipe changamoto. Jaribu mambo mapya na uwe muwazi katika mambo ambayo hukuyazoea.<br />
Jizoeshe kusema “sifahamu jinsi ya kufanya kile lakini ningependa kujaribu”<br />
JE? Unafahamu kwa nini wasichana wana matatizo zaidi ya kujiheshimu na<br />
kujiamini kuliko wavulana?<br />
Wakati mwingine wasichana wana matatizo ya kujiamini na kujienzi kidogo kuliko wavulana<br />
wa rika moja. Kwa nini iwe hivi? Je, kujienzi na kujiamini kunahusiana na jinsi ya mtu?<br />
Jibu ni “Hapana” kujienzi na kujiamini hakuhusiani na jinsi ya mtu. Hata hivyo heshima na<br />
imani ya mtu inaweza kuathirika sana kwa namna au jinsi anavyotendewa na watu wengine<br />
– wazazi, wadogo zake, ndugu, walimu, majirani viongozi wa dini na viongozi ndani ya jamii,<br />
n.k.<br />
Kwa bahati mbaya katika utamaduni mwingine wavulana na wasichana wanatendewa<br />
tofauti kabisa; na hii inaweza kuathiri sana namna wanavyojiona na uwezo wao. Kwa mfano;<br />
katika familia zingine wavulana wanaweza kupewa nafasi zaidi katika elimu na mafunzo<br />
ya kazi; na walimu wakati mwingine wanawajali zaidi wavulana. Kwa upande mwingine<br />
wasichana wanaweza wasipate nafasi kama hiyo. Wanaweza wasiruhusiwe kucheza na<br />
wenzao au kucheza michezo kama kaka zao wanavyofanya. Zaidi ya hapo kazi ngumu<br />
wanazofanya nyumbani na shambani zinaweza zisionekane na wala zisitambulike. Matokeo<br />
yake wasichana na wanawake hujiona hawana thamani na wanaweza kuanza kuamini<br />
kwamba thamani yao ni ndogo kuliko ya wavulana na wanaume. Lakini hii sio kweli! Watu<br />
wote ni sawa. Iwapo wote watapata nafasi sawa, wasichana wanaweza kufanya vizuri<br />
shuleni, katika kazi na kitu chochote wanachotaka kufanya.<br />
Inaweza kuwa vigumu sana kama wewe ni msichana na unaishi katika mazingira ambayo<br />
mara kwa mara unajisikia huthaminiwi kama ambavyo mvulana anavyothaminiwa. Haya<br />
hapa ni mambo machache ambayo unaweza kufanya ili kuimudu hali hiyo:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
SURA YA 6 | UTUNZAJI AfYA YA AKILI NA MOYO<br />
Wakati wote kumbuka kwamba una thamani kubwa bila kujali watu wengine wanasema<br />
nini. <strong>Wewe</strong> una akili na uwezo sawa na mvulana yeyote.<br />
Jitahidi mara dufu katika kujenga kujienzi na kujiamini kwako.<br />
Jisifu mwenyewe na ridhika unapofanya kazi vizuri. Usisubiri kusifiwa na watu<br />
wengine ambao wanaweza wasikusifu.<br />
Tumia kila nafasi uliyo nayo kujifunza stadi mpya na fanya mengi kati ya hayo.<br />
Kumbuka, kila unapofanikisha jambo utakuwa unajihakikishia mwenyewe na watu<br />
wengine kwamba unayo thamani kama ambavyo wengine walivyo nayo.<br />
Tambua changamoto unazokumbana nazo; lakini usikate tamaa. Kama unaishi katika<br />
jamii ambayo wanawake wanadharauliwa sana usitegemee hali hiyo kubadilika katika<br />
siku moja, lakini hata hivyo lisikufanye ukate tamaa.<br />
Zungumza na wazazi wako au mtu mzima yeyote anayejali. Kwa mfano; kama wazazi<br />
wanataka kukuachisha shule au wanataka uolewe jaribu kutafuta mtu wa kuzungumza<br />
naye. Eleza namna elimu ilivyo ya muhimu kwako na waombe kama wanaweza<br />
kukusaidia kumudu hali hiyo.<br />
59
60<br />
•<br />
•<br />
•<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Kuwa mcheshi. Usiruhusu aibu au wanachofikiria watu wengine iwe ni sababu ya kutofanya<br />
mambo mapya.<br />
Vione vikwazo kama ni nafasi ya kujaribisha na kujifunza mambo mapya, Fikiria mwenyewe<br />
“sawa, nitalishughulikia vipi tatizo hili?”<br />
Ukishindwa kitu, kuwa na mtazamo sahihi. Usiwe na wasi wasi au kuchukizwa nalo. Fikiria<br />
kosa limetokea wapi na ungefanya nini cha tofauti safari nyingine. Halafu achana nacho.<br />
uSiWe na WaSiWaSi, FuRahi<br />
Umewahi kusikia wimbo wenye maneno ya kichwa cha habari hapo juu? Sauti yake ni rahisi na<br />
inavutia. Unadhani ni rahisi kuwa na furaha? Hata hivyo kila mtu anao wasiwasi, na vijana balehe<br />
wana wasiwasi mwingi – wasiwasi kuhusu wao wenyewe namna wanavyoonekana, rafiki zao,<br />
mafanikio shuleni, maisha ya baadaye, n.k.<br />
Wasiwasi unaweza kukukosesha raha. Kwanza jiulize kama kuna haja ya kuwa na wasiwasi huo.<br />
Mara nyingi watu wanakuwa na wasiwasi usiokuwa wa lazima. Yapo mambo mengine ambayo<br />
hayahitaji kuwa na wasiwasi nayo, kama haya yafuatayo:<br />
Mambo ambayo huna uwezo wa kuyabadili, kama vile sura yako, rangi ya ngozi yako, umbile la<br />
nywele na ukubwa wa matiti au uume. Huwezi ukabadilisha vitu hivi, kwa hiyo ni vema kuvikubali<br />
kama vilivyo. <strong>Wewe</strong> ni mzuri kama ulivyo. Isitoshe<br />
ni haiba yako ndiyo inakufanya uwavutie watu<br />
wengine. Lenga katika wewe ni nani na wala sio<br />
unavyoonekana.<br />
Mambo ya dunia ambayo huna uwezo nayo.<br />
Unaona gauni zuri dukani. Usibabaike kwa sababu<br />
huna uwezo wa kulinunua. Utahitaji mshahara wote<br />
wa mwezi mmoja kutoka kwa baba yako ili uweze<br />
kulinunua. Kwa kuongezea, hata kama ungelipata<br />
gauni hilo ungejikuta baada ya miezi michache<br />
unahitaji gauni lingine, na hata zaidi. Mambo<br />
ya dunia hayaleti furaha wala kuwa mwisho wa<br />
matatizo; kwa hiyo lenga katika mambo ambayo<br />
yako ndani ya uwezo wako. Ridhika jinsi ulivyo na<br />
kile ulichonacho.<br />
Kama tu ningepata gauni lile zuri, ningekuwa<br />
na furaha zaidi…”<br />
Kutokuwa na rafiki wa kike au kiume. Watu wengine hupata rafiki wa kike au wa kiume kipindi<br />
cha ujana balehe. Lakini wengine hawampati mtu huyo maalumu mpaka baadaye sana katika<br />
maisha. Kwa kuongezea, mapenzi ya vijana hayadumu sana. Inaweza kuchukua muda kumpata<br />
mpenzi wa moyo.<br />
Hivyo kuwa mvumilivu usikimbilie katika mahusiano ati kwa sababu unafikiri unahitaji kuwa na<br />
rafiki wa kike au kiume wakati huo.<br />
Shinikizo kutoka kundi rika ili kufanya kitu ambacho hutaki kukifanya: Fanya mambo yale<br />
tu ambayo unafikiri ni mazuri kwako. Hata siku moja usiruhusu tamaa ya kuwafurahisha watu<br />
wengine ikufanye wewe utende yale ambayo huyataki na unafikiria ni makosa.<br />
• Kuwa mpweke: Upweke ni jambo ambalo<br />
linampata mtu yeyote kwa wakati fulani katika<br />
maisha. Kutatokea muda mfupi utakapojisikia<br />
kama huna mtu yeyote wa kuzungumza naye<br />
au hakuna mtu ambaye anakuelewa vizuri. Kwa<br />
kawaida nyakati kama hizi hudumu kwa muda<br />
mfupi na kila mtu anazipitia.<br />
Lakini bila shaka zipo hali ambazo unastahili kuwa na<br />
wasiwasi nazo. Kwa mfano:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
SURA YA 6 | UTUNZAJI AfYA YA AKILI NA MOYO<br />
Wazazi wako hawezi kukulipia karo ya shule na<br />
hujui uende wapi kuomba msaada.<br />
Hili ni tatizo kubwa ambalovijana wengi wanalipata. Zungumza na Mwalimu au mshauri<br />
katika kituo cha vijana kilichopo katika eneo lako kama wana maoni yoyote. Vilevile<br />
zungumza na viongozi wa dini au viongozi wa kijiji ili kuona kama wanamfahamu mtu yeyote<br />
ambaye anaweza kutoa msaada. Labda unaweza kubadilisha shule yenye karo nafuu au<br />
kutafuta kazi ya kufanya mwishoni mwa wiki ili kupata pesa.<br />
<strong>Wewe</strong> na rafiki yako wa kike mlifanya mapenzi yasiyo salama na sasa anafikiria huenda<br />
akawa amepata mimba.<br />
Huu ni wasiwasi mkubwa. Jambo zuri la kufanya ni kwenda kliniki kupima mimba na kupata<br />
ushauri. Nenda na rafiki yako wa kike kwa ajili ya kumpa moyo. Kama ni mja mzito, usikatae<br />
kwamba sio mimba yako. Wote mnawajibika (angalia sura ya 11 kwa taarifa zaidi kuhusu<br />
mimba).<br />
umesikia tetesi kwamba mmojawapo wa marafiki zako wa zamani ana uKiMWi. huna<br />
uhakika kama ni kweli, lakini je upime?<br />
Huu nao ni wasiwasi mkubwa. Ndio, nenda kwa washauri nasaha na upimaji ili uweze kutuliza<br />
akili yako au uchukue hatua zinazostahili. Nenda na mtu mmoja kwa ajili ya msaada (angalia<br />
sura ya 10 kwa ajili ya taarifa zaidi kuhusu VVU (UKIMWI).<br />
Mtu mzima au mwanafunzi mwenzako amekuwa anakupatia zawadi ndogo ndogo na<br />
starehe. lakini sasa anataka mfanye ngono. anasema anakudai pesa nyingi ambazo<br />
amekuwa anatumia kwa ajili yako.<br />
Usikubaliane na shinikizo hilo. Unaweza kuishia kupata mimba kwa makosa na kuachwa na<br />
mwanaume au mvulana. Kaa mbali naye. Kuwa jasiri na zungumza na wazazi wako, shangazi<br />
au mtu yeyote mzima kuhusu hali hii. Usijaribu kumudu jambo hili peke yako.<br />
Katika hali mbaya kama hizi wasiwasi unaweza kukusaidia. Unahitaji kufikiria sana chaguzi<br />
zote ulizonazo ili kumudu tatizo, halafu unahitaji kuzipima chaguzi na matokeo yake ili uweze<br />
kufanyia kazi yale yanayokufaa.<br />
Hata hivyo wasiwasi juu ya hali mbaya kama hizi unaweza kukuongezea mfadhaiko, yaani pale<br />
unapoanza kujisikia umeelemewa na matatizo yako na wasiwasi. Unapokuwa na mfadhaiko<br />
mwili wako utatoa ishara: Huwezi kuacha kufikiria tatizo. Moyo unadunda kwa nguvu. Unaweza<br />
ukajisikia unakosa hewa. Tumbo linaweza kukuuma. Unaweza kukosa usingizi au unaweza<br />
kuota ndoto mbaya (kupata jinamizi). Unaweza kuwa msahaulifu. Iwapo unazipata dalili hizi za<br />
mfadhaiko chukua hatua zifuatazo:<br />
61
62<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
• Vuta hewa kwa nguvu. Iwapo umefadhaika sana<br />
na unajisikia kukosa hewa na kichwa chepesi, acha<br />
kufanya kile ulichokuwa unafanya na polepole vuta<br />
hewa nyingi, ukiizuia hewa ndani ya mapafu yako<br />
kwa sekunde chache kabla hujaitoa.<br />
• tafuta chanzo cha mfadhaiko Je, unaweza<br />
kuupunguza mfadhaiko? Je, umefaidhaika na<br />
kitu ambacho hustahili kuwa na wasiwasi nacho?<br />
Tengeneza orodha ya vitu vyote vinavyosababisha<br />
uwe na mfadhaiko halafu iangalie kwa makini. Je,<br />
majukumu yamezidi? Je unaweza kufanya lolote ili<br />
kupunguza orodha yako?<br />
• Zungumza na watu. Hakuna haja ya kutatua<br />
matatizo peke yako. Watu wengine wamepitia<br />
wakati mgumu kama wewe na wanaweza kutambua Usijaribu kumudu wasiwasi wako<br />
peke yako. Zungumza na mtu.<br />
namna ya kushughulikia tatizo lako. Anaweza<br />
kuwa mzazi wako, shangazi au wajomba , kaka<br />
au dada, rafiki wa karibu, mwalimu, jirani, mfanyakazi wa afya, kijana mshauri nasaha,<br />
kiongozi wa dini na mzee wa kijiji. Hawa ni watu wachache ambao wanaweza kukupa ushauri.<br />
Wanaweza kupendekeza ufumbuzi ambao hujaufikiria.<br />
• Fanya mazoezi.<br />
Kimbia, cheza mpira wa miguu au tembea haraka haraka, ogelea. Mazoezi ni<br />
njia nzuri sana ya kushinda mfadhaiko.<br />
• Pata usingizi wa kutosha. Jaribu kwenda kulala ukiwa na hali nzuri ya akili. Epuka kuangalia<br />
televisheni (luninga) kabla ya kwenda kulala. Jaribu kupumzisha misuli yote mmoja baada ya<br />
mwingine kadri unavyolala kitandani.<br />
• Kula chakula bora, Zingatia kupata kifungua kinywa, na milo yote ya siku.<br />
• tumia kusali au kutaamali. Hii ni njia nzuri ya kujituliza mwenyewe na kumudu mfadhaiko.<br />
Sala zimejaa mategemeo na hekima kuhusu namna ya kuyaendesha maisha yako ya kila siku.<br />
• Fanya kile unachokifurahia – Hivi ni vitu ambavyo vitakufanya uondokane na mawazo ya<br />
kuwa na wasiwasi, kama kutumia muda wako na rafiki wa karibu, kuchora, kuimba, kulima<br />
bustani, kupika, kusikiliza muziki n.k.<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Zifuatazo ni njia chache za kupambana na mfadhaiko ambazo unatakiwa uepukane nazo:<br />
Kutumia pombe na madawa ya kulevya kama njia ya kutuliza mawazo. Hii sio dawa. Pombe<br />
na madawa ya kulevya vinatuliza zile sehemu za ubongo ambazo zinasaidia kufikiria na<br />
kudhibiti tabia yako. Pombe na madawa ya kulevya vinaweza kukufanya utende mambo<br />
ambayo baadaye utayajutia.<br />
Kuficha hisia zako na kuyaweka matatizo yote ndani ya roho yako hakuwezi kukusaidia<br />
kuyamudu na wala kumaliza mfadhaiko wako. Mwisho wake utajisikia kama unayetaka<br />
kupasuka.<br />
•<br />
Kuhamishia mfadhaiko wako kwa watu wengine. Jihadhari mfadhaiko wako usije ukakufanya<br />
kuwa na kiburi, mkali au mbaya kwa watu wengine. Hii itakufanya wewe mwenyewe ujisikie<br />
vibaya zaidi.<br />
Njia hizi za kukabiliana na mfadhaiko sio nzuri na wala hazifai. Zitazidisha ugumu wa maisha yako<br />
na zinaweza kukuongezea mambo mengine mabaya zaidi ya kukufadhaika. Mfadhaiko ni kitu<br />
unachoweza kukidhibiti, kwa hiyo usiruhusu ukutawale.<br />
KuMuDu huZuni<br />
Wakati mwingine matatizo yanaweza kukufanya ujisikie mnyonge na ukashindwa kupata njia<br />
ya kuyaweka maisha sawa. Hivyo kula matunda na mboga mboga, kucheza michezo na kulala<br />
usingizi wa kutosha kutakufanya ujisikie vizuri zaidi.<br />
Wakati mwingine unayo kila sababu ya kuwa na huzuni. Kwa mfano; ukifiwa na mtu wa karibu<br />
sana, utasikitika sana. Unaweza ukamkumbuka marehemu sana na kupata hisia kali ya<br />
kuhuzunika. Kama umefiwa na rafiki yako wa kiume au wa kike unaweza kujisikia mpweke sana,<br />
na unaamini kuwa hutaweza kumpata mtu mwingine kama yeye.<br />
Kupotelewa kwa namna hii ni kugumu, lakini unaweza kuyakabili matatizo. Baada ya kipindi<br />
cha huzuni, utajisikia uko tayari kuendelea na maisha. Ingawa masikitiko ya kumpoteza mtu<br />
unayempenda yatabakia palepale, mwishowe utakuwa na furaha tena.<br />
Lakini wakati mwingine watu wanakuwa na huzuni kubwa kiasi cha kutoyatamani maisha tena.<br />
Wanadhani maisha hayana maana tena na hakuna faida yoyote ya kuishi. Wanajisikia watupu na<br />
hawafai kabisa. Wanajisikia hawana raha. Wanajiona wamepoteza mwelekeo.<br />
Hisia hizi za kuwa na huzuni sana na kujiona hufai zinaitwa “unyong’onyevu”. Kunyong’onyea au<br />
kuvunjika kwa moyo kunaweza kukasababishwa na jambo linalohuzunisha kama kifo, lakini<br />
mara kwa mara watu wanaopatwa na tatizo hili wanapata shida kutambua sababu maalumu<br />
au kilichosababisha kuvunjika kwa moyo. Matokeo yake wanapata tabu kutambua kama<br />
wamevunjika moyo. Wanaweza kugundua mabadiliko mbalimbali yakiwatokea, kama vile:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Kuwa na huzuni wakati wote.<br />
Kukosa nguvu.<br />
Kushindwa kufikiri vizuri.<br />
Kuumwa kichwa mara kwa mara na matatizo ya tumbo.<br />
Kushindwa kufurahia mambo ambayo mwanzo yalikuwa yanafurahisha.<br />
Mabadiliko katika ulaji, (kama vile kula pelemende) au unywaji (kunywa pombe ili kujaribu<br />
kusahau matatizo).<br />
Je, umewahi kujisikia hivi au kuona mabadiliko kama haya yakimtokea rafiki yako? Kuvunjika<br />
moyo ni jambo la hatari, iwe ni wewe mwenyewe au rafiki yako, hivyo chukueni hatua zifuatazo:-<br />
•<br />
SURA YA 6 | UTUNZAJI AfYA YA AKILI NA MOYO<br />
Jaribu kutambua ni kitu gani kinachofanya uwe na huzuni.<br />
63
64<br />
•<br />
•<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Zungumza na watu wengine kuhusu hisia zako<br />
Fanya mazoezi, na fanya mambo ambayo yanakufanya uwe na furaha na ujisikie vizuri.<br />
Pamoja na haya, jaribu kutoka nje ya nyumba<br />
yenu na pitisha muda na watu wengine. Jihusishe<br />
na shughuli za kanisa/msikitini au kikundi cha<br />
vijana. Kupitisha muda na watu wengine kunaweza<br />
kukusaidia kuondoa fikra za mambo ambayo<br />
yanakufanya uhuzunike sana. Kusaidia kazi<br />
watu wengine kunaweza vilevile kuwa njia nzuri<br />
ya kukufanya ujisikie vizuri. Kwa mfano; jaribu<br />
kumsaidia mtoto anayejifunza kusoma, msaidie<br />
rafiki au jirani yako kazi wanazozifanya. Inaonekana<br />
kama upuuzi, lakini utashangaa namna ambavyo<br />
kumsaidia mtu mwingine kazi kunavyoweza<br />
kukufanya ujisikie vizuri zaidi pamoja na matatizo<br />
uliyonayo.<br />
unapojisikia hovyo, kusaidia watu wengine<br />
kazi kunaweza kukufanya ujisikie vizuri zaidi.<br />
Kama yote hayo hayakukusaidia kiasi cha kufikiria kujiua, tafadhali mtafute mtu wa kuzungumza<br />
naye mara moja. Huyu anaweza akawa ndugu yako, mwalimu au mtaalamu wa ushauri nasaha.<br />
Wachungaji, mashehe na viongozi wa dini wengi ni washauri nasaha wazuri, na wanatoa msaada<br />
na ushauri kwa watu wakati wote. Ufumbuzi wa matatizo yako unaweza kupatikana, kwa hiyo<br />
usijaribu kuyatatua peke yako unapojisikia umenyong’onyea sana.<br />
UNAJUA kwamba pombe inaongeza mfadhaiko?<br />
Watu wengi hunywa pombe nyingi wanapokuwa na matatizo wakiamini kuwa inawasaidia<br />
kusahau shida walizo nazo. Pombe hufanya ubongo uwe kama umepata ganzi na kufanya<br />
matatizo kupungua papo hapo.<br />
Kwa bahati mbaya, pombe haiwezi kutatua matatizo yako ya huzuni au kusononeka. Ukweli<br />
ni kwamba pombe inaangukia katika kundi la madawa ya kupunguza uwezo wa ubongo<br />
na sehemu zingine za mwili kufanya kazi vizuri. Pombe na dawa zingine za kupunguza<br />
wasiwasi kwa hakika zinaongezea hali ya kusononeka. Kwa kuongezea, zinamsaidia mtu<br />
akwepe kutatua matatizo yanayomfanya asononeke. Matokeo yake, pombe inaweza kuwa<br />
ngao ya kutegemewa hasa matatizo yanapotokea. Watu wengine wanatawaliwa sana na<br />
pombe kiasi cha kwamba hawawezi kuishi bila kunywa.<br />
KUISHI VIZURI NA WATU<br />
Kuishi na kuelewana na watu ni sehemu nyingine muhimu katika afya ya hisia. Mahusiano<br />
mazuri na wazazi na marafiki zako yatakufanya wewe mwenyewe ujisikie vizuri kwa ujumla na<br />
yatakusaidia kupambana na raha na shida za maisha. Kuelewana na watu wengine kunahitaji<br />
stadi muhimu kama vile:-<br />
SURA YA 6 | UTUNZAJI AfYA YA AKILI NA MOYO<br />
Kujitambua: Kujitambua maana yake ni kuwa na uwezo wa kuelewa hisia zako ni zipi na kwa<br />
nini ziko hivyo. Kujitambua maana yake ni kuwa unapojisikia ovyo ovyo unaachana na kufikiria<br />
kile unachohisi – iwe huzuni, hasira, kukata tamaa, wasi wasi, n.k. Na baada ya kuachana<br />
na unachohisi unaendelea na kufikiria ni kitu gani kinakufanya uwe hivyo. Kwa mfano je ni<br />
wasiwasi juu ya masomo yako? Je unashuku urafiki ambao unaonekana kufifia? Je kuna<br />
mtu amekufanya ujisikie vibaya?<br />
Kujitambua ni muhimu kwa sababu kunakusaidia<br />
uelewe tatizo na chanzo chake. Kwa<br />
kutumia taarifa hii unaweza kuanza kutatua<br />
tatizo. Kama una wasiwasi na kazi za shule,<br />
unaweza kuzungumza na wazazi au mwalimu<br />
wako na kuanza kupata msaada unaouhitaji<br />
ili ujiamini tena. Kama una wasiwasi na rafiki<br />
yako, unaweza kuchukua hatua ya kuzungumza<br />
naye na kumueleza namna urafiki wenu<br />
ulivyo wa muhimu, na kwa pamoja mnaweza<br />
kuangalia namna ya kuufanya uwe urafiki wa<br />
nguvu. Iwapo kuna mtu anakukosesha raha,<br />
unaweza kuamua kukabiliana naye ili afahamu<br />
kwamba unajisikia vibaya anapokutendea<br />
vile, au kama hiyo haisaidii, unaweza kuamua<br />
kukaa mbali na huyo mtu anayekufanya<br />
ujisikie vibaya.<br />
Kujitambua ni uwezo wa kugundua unachohisi na<br />
kinachokufanya uhisi hivyo<br />
Mwisho, kujitambua kunaweza kukusaidia kuujua udhaifu wako, - udhaifu unaotakiwa<br />
kuufanyia kazi mwenyewe. Je, unazo tabia au mwelekeo fulani ambao ungependa kuubadilisha?<br />
Kwa mfano: unaweza kugundua kwamba unapofanya vibaya mitihani yako ya shule<br />
unakuwa na tabia ya kumlaumu mtu mwingine. “Mwalimu hanipendi” unajisemesha mwenyewe.<br />
Au unafikiria “wanafunzi wengine walikuwa wanapiga kelele kwa hiyo nilishindwa<br />
kufikiri.”<br />
Ni rahisi sana kulaumu watu wengine, lakini ni tabia mbaya kwa sababu huwi mkweli na hujiwajibishi.<br />
Labda ulipokuwa mtoto ilikuwa sawa kulaumu watu wengine hasa kwa vile yapo<br />
mambo mengine ambayo watoto hawawezi kuyadhibiti. Lakini unapoingia utu uzima, unahitaji<br />
kuwajibika kwa matendo yako. Kama kuna jambo ambalo haliendi kama unavyotaka ni<br />
juu yako kujaribu kulibadilisha. Kujisikitikia na kujifanya kana kwamba wewe ni mwathirika<br />
wa matendo ya watu wengine haitatatua jambo lolote.<br />
Ushirikeli (uwezo wa kuelewa hisia za mtu mwingine): Uwezo wa kuelewa hisia za mtu<br />
mwingine ni sawa na kujitambua ijapokuwa huu ni uwezo wa kuelewa kile ambacho mtu<br />
mwingine anahisi na kwa nini anahisi hivyo. Kuwa na uwezo wa kuelewa hisia za mtu<br />
mwingine maana yake ni kuwa na uwezo wa kufikiri na kujua pale penye tatizo la mtu<br />
kama - rafiki, mzazi, ndugu, n.k. Unaweza kujua hofu zao,wasiwasi, woga na mahitaji yao, na<br />
unaweza kuelewa wanavyojihisi. Kama ambavyo kujitambua kunavyosaidia ujue mahitaji<br />
yako, ushirikeli unakuwezesha kujua hisia za mtu mwingine. Kwa mfano; kama rafiki yako<br />
ana huzuni, kufahamu tatizo lake kunaweza kukusaidia ujue namna ya kumsaidia kulitatua.<br />
65
66<br />
Kutatua tatizo na kufikiri kwa<br />
ubunifu: Ili kupata ufumbuzi wa<br />
matatizo kunahitaji kufikiri kwa<br />
ubunifu. Kufikiri kwa ubunifu ni uwezo<br />
wa kufikiri ufumbuzi wa tatizo usio<br />
wazi. Ni uwezo wa kusumbua akili<br />
yako ili kupata fumbuzi mbalimbali<br />
bila kujiwekea mipaka ya mazoea<br />
uliyoyasikia ya utatuzi wa jambo fulani.<br />
Kwa mfano: fikiria kuwa umepata<br />
mimba ukiwa unasoma shule. Wasichana<br />
wote unaowafahamu waliopata mimba<br />
waliacha shule na hawakuweza kumaliza<br />
masomo. Kufikiria kwa ubunifu maana<br />
yake ni kutokudhani kwamba lazima<br />
uache shule eti kwasababu wasichana<br />
wengine waliacha. Labda inawezekana<br />
ukakaa shuleni ukiwa na mimba. Au<br />
unaweza kurudi shuleni baada ya<br />
kujifungua mtoto. Labda kipo kituo kwa<br />
ajili ya vijana waliozaa ambako unaweza<br />
kuendelea na masomo au mafunzo.<br />
Kufikiri kwa ubunifu kunahusisha<br />
kuzungumza na watu wengine. (walimu,<br />
vijana washauri wazazi, shangazi,<br />
wajomba marafiki) na kuchunguza<br />
chaguzi zote zilizoko mbele yako.<br />
Stadi za makubaliano. Hizi ni stadi<br />
ambazo unahitaji ili kutatua tatizo au<br />
tofauti ulizonazo na watu wengine.<br />
Kwa mfano, unaweza ukataka kutoka<br />
na rafiki yako, lakini wazazi wako<br />
wanataka ukae nyumbani. Hali kama<br />
hii inahitaji stadi nzuri za makubaliano.<br />
Inaweza ikawa vigumu kukubaliana<br />
na wakati wingine kukatishwa tamaa.<br />
Unaweza kujisikia kama upasuke,<br />
kwamba umevunjika moyo kiasi cha<br />
kusema “potelea mbali” na kuondoka<br />
ukiwa umekasirika na kuchoshwa.<br />
Lakini unahitaji kuwa mvumilivu na<br />
mtulivu wakati unaeleza kwa nini<br />
unajisikia hivyo, na kile unachohitaji.<br />
Vilevile unahitaji kuwa mkweli, mtu<br />
unayeelewa na kuheshimu yale ambayo<br />
watu wengine wanayahisi na kuyahitaji.<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Je, unajua maana ya kutatua tatizo kwa<br />
ubunifu bila woga wala jazba?<br />
Anne ana umri wa miaka 16 na ni yatima.<br />
Anaishi na shangazi yake ambaye anamtaka<br />
afanye kazi dukani kwake kila siku baada ya<br />
kutoka shule. Hili ni tatizo kubwa kwa Anne.<br />
Hapati muda wa kutosha wa kujisomea.<br />
Ameanza kufadhaika kwa vile mitihani<br />
inakaribia. Hapati usingizi vizuri usiku kwa<br />
sababu ana wasiwasi sana kuhusu masomo.<br />
Ameanza kumchukia shangazi yake.<br />
Anashangaa iwapo shangazi yake anamwona<br />
kama kitendea kazi na kwamba hampendi<br />
wala kujali maisha yake ya baadaye.<br />
Anne anajitambua. Anajua kuwa anayo<br />
tabia ya kuficha hisia zake mpaka<br />
anapolipuka kwa hasira. Tabia hii haimsaidii<br />
sana. Shangazi yake naye anakasirika na<br />
kusema ameanza kukosa heshima.Safari hii<br />
anaamua kufanya mambo tofauti. Badala<br />
ya kumwambia shangazi yake kiugomvi<br />
“Hunipendi” anamweleza shangazi yake bila<br />
woga wala jazba “Ninawasiwasi sana kuhusu<br />
mitihani yangu lakini nataka pia kukusaidia<br />
kazi za dukani”. Hapa ameonyesha tabia ya<br />
kujiamini.<br />
Kwa kujieleza mwenyewe kwa njia hii,<br />
Anne amesimama imara na kuomba<br />
muda zaidi wa kujisomea. Lakini kwa<br />
wakati huo huo anaelewa shangazi yake<br />
anahitaji msaada wa dukani. Anaonyesha<br />
ushirikiano kwa shangazi yake ambaye ana<br />
majukumu mengine. Akifuata utaratibu huu,<br />
shangazi naye anaelewa pia. Kwa pamoja<br />
wanafikiri kwa ubunifu kutatua tatizo hili.<br />
Wanatengeneza ratiba inayompa Anne muda<br />
zaidi wa kujisomea jioni na pia kumsaidia<br />
shangazi yake jioni inapokuwa lazima.<br />
Inatia moyo kwa jinsi Anne alivyojisikia<br />
vizuri. Ghafla mfadhaiko unapungua na<br />
anaweza kuyafurahia maisha tena.<br />
Hata hivyo sio kila tatizo linaweza kujadiliwa na kufikia maelewano. Wakati mwingine<br />
utalenga katika matokeo ambayo yatakufanya uwe salama, hata kama mtu mwingine<br />
hatafurahia. Mathalani, rafiki yako wa kike au wa kiume amekataa kutumia kondomu<br />
pamoja na kumshawishi kwa nguvu zote. Katika hali kama hii zingatia usalama wako.<br />
Ondoka sehemu hiyo ikibidi.<br />
Msimamo: Msimamo ni stadi ya msingi katika kuelewana na watu wengine. Msimamo<br />
maana yake kutetea na kuyaenzi yale unayoyaamini wewe mwenyewe. Kuwa muwazi na<br />
mwaminifu kwako mwenyewe na watu wengine kuhusu kile unachokihitaji na kukitaka.<br />
Watu ambao hawana msimamo juu ya maisha yao huwa ni wanyenyekevu. Hata kama<br />
wanatendewa vibaya, hawajitetei. Watu ambao hawana msimamo mara kwa mara<br />
wanakosa imani ya kujienzi na kutetea mahitaji yao na kulinda hisia zao au hata miili yao ili<br />
wasiumizwe.<br />
Msimamo ni tofauti sana na kuwa mgomvi. Watu wagomvi ni watundu na hawana huruma,<br />
hawajali watu wengine wanahisi nini. Sio vizuri kuwa mgomvi kwa faida ya afya ya hisia<br />
kwa sababu, kwa undani kabisa, utajisikia vibaya kutokuwa na huruma kwa wengine.<br />
Misingi ya msimamo:<br />
SURA YA 6 | UTUNZAJI AfYA YA AKILI NA MOYO<br />
• amua unachohisi au unachotaka na kiseme. Usiogope kuwa mkweli kuhusu hisia<br />
zako. Watu wanatakiwa kuziheshimu hisia hizo. Kwa mfano, labda ulijisikia vibaya na<br />
unakosa raha baada ya rafiki yako wa kiume kukugusa sehemu zako za siri. Unatakiwa<br />
kumwambia, “Nilikosa raha uliponigusa sehemu zangu za siri sitaki uniguse hivyo tena”.<br />
Mtu anayekupenda kweli hatataka kufanya vitendo ambavyo vinakukosesha raha.<br />
• Mtazame mtu machoni: Kumwangalia mtu machoni ni kudhihirisha msimamo wako.<br />
Inamjulisha mtu mwingine kwamba hutanii kuhusu kile unachokisema na kwamba<br />
unaangalia kama wanakusikiliza au hawakusikilizi. Tamaduni nyingi haziungi mkono<br />
kumwangalia mtu machoni wakati wa mazungumzo. Wakati mwingine katika maeneo<br />
mengine huliona jambo hili ni ufedhuli (kutokuwa na ustaarabu/heshima) kijana<br />
mdogo anapomwangalia mtu mzima moja kwa moja usoni. Unaweza kufuata mila na<br />
desturi, kama kupiga magoti, kuonyesha heshima lakini kwa wakati huo huo endelea<br />
kumwangalia mtu huyo usoni kama unataka kuonyesha ujasiri/msimamo wako.<br />
• usitoe visingizio. Hisia zako ni sababu tosha. Kwa mfano, kama hujisikii kufanya<br />
mapenzi lakini rafiki yako wa kike au kiume anakulazimisha, epuka kutumia watu<br />
wengine kama kisingizio. Usiseme, “mama yangu karibu atarudi nyumbani au tumbo<br />
linaniuma au ninaogopa kupata mimba au nina kazi ya kusoma kwa hiyo sio muda mzuri<br />
kwangu”. Unaweza ukamchanganya rafiki yako na visingizio hivi. Anaweza kudhani<br />
unataka kwenda sehemu nyingine, au kwamba labda unataka kutumia kondomu.<br />
Anaweza asitambue kwamba unachotaka kumwambia ni “siko tayari kufanya tendo hilo<br />
kwa hiyo sitaki”. Kwa hiyo basi sema kile unachotaka.<br />
• usisemewe na mtu mwingine. Iwapo hutaki kufanya jambo fulani, sema mwenyewe<br />
na usiulize mtu mwingine kama ni sawa. Kwa mfano, kama mtu ana kushawishi unywe<br />
pombe au madawa ya kulevya usiseme; “nisingependa, lakini kama unaona sawa …?<br />
Badala yake sema “Hapana, ninashukuru.<br />
67
68<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Sihitaji kitu chochote”. Waonyeshe kwamba unajua unachotaka, hivyo hutafuti kibali chao.<br />
Usibabaishwe na hoja za watu wengine. Endelea kurudia msimamo wako juu ya yale<br />
unayoyataka na usiyoyataka. Labda rafiki yako wa kike anaendelea kukulazimisha mfanye<br />
mapenzi na ana tumia hoja hizi: “Hivi hunipendi?”, “Unajua nilifanya mapenzi na mvulana<br />
wangu wa zamani. Simama imara na usikubali. Mwambie “mimi sio mvulana wako wa<br />
zamani. Mimi ni mimi. Sitaki kufanya mapenzi na wewe.<br />
Kumbuka, unayohaki ya kubadilisha mawazo. Labda wewe na rafiki yako mlizungumza<br />
kuhusu kufanya mapenzi siku chache zilizopita, na ulimwambia mtafanya mapenzi. Lakini<br />
umefikiria kiundani na unaona ni makosa kufanya hivyo. Iwapo atasema; “Lakini ulikubali<br />
mwenyewe kwamba tungefanya mapenzi”. Mwambie: “Nimebadilisha mawazo. Siko<br />
tayari”. Kama kweli anakupenda, ataheshimu maamuzi yako mapya na atasubiri mpaka<br />
utakapokuwa tayari.<br />
Kuwa na msimamo ina maanisha kuwa na uhakika na kile unachotaka<br />
Kuwa na stadi za maisha zilizojadiliwa katika sura hii,kujitambua,ushirikeli,kutatua<br />
matatizo kwa kufikiri, kwa ubunifu,stadi za makubaliano,kuwa na msimamo ni baadhi ya<br />
nguzo za afya ya hisia nzuri.Ukizifahamu stadi hizi utakuwa salama na si ajabu utafanikiwa<br />
katika vitu vingi utakavyojaribisha maishani.<br />
SURA YA 6 | UTUNZAJI AfYA YA AKILI NA MOYO<br />
Sura ya Sita<br />
utunzaji afya ya akili na Moyo<br />
Kuwa na afya njema ya hisia ina maana zifuatazo:<br />
· Kujisikia vizuri wewe binafsi. Ni kujipenda na kujiheshimu. Pia ni kujithamini.<br />
· Kujikubali kuhusu uwezo wako. Unakuwa huna wasiwasi sana kuhusu<br />
udhaifu wako na huogopi kujaribu mambo mapya. Unakuwa unajiamini.<br />
· Kuweza kukabili wasiwasi na mfadhaiko. Unakuwa huna wasiwasi na<br />
mwonekano wako, huna wasiwasi kwa vile eti huwezi vitu fulani, huna<br />
wasiwasi na maneno ya marafiki zako wala huna wasiwasi kwa vile tu<br />
huna mpenzi.<br />
· Kukabili huzuni. Unajitahidi huzuni na hasira zisikutawale na kukukosesha<br />
matumaini.<br />
· Kutambua hisia zako na sababu za hisia hizo. Unapojisikia vibaya (iwe<br />
hasira, uchovu, kukata tamaa) acha kufikiria hisia hizo na sababu zinazosababisha<br />
ujisikie hivyo.<br />
· Kuelewa hisia na sababu wanazotoa watu wengine. Unajiuliza ingekuwa<br />
wewe ungefanyaje? Unakuwa mtu unayejaribu kuelewa wasiwasi, matatizo<br />
au mahitaji ya watu wengine. Huu ni uwezo wa kutambua hisia za watu<br />
wengine.<br />
· Kutatua matatizo na kufikiri kiubunifu. Unakuwa na njia nyingi za<br />
kutatua tatizo linapojitokeza. Pia unatumia njia bora zilizojificha ambazo<br />
hutatua tatizo kwa urahisi zaidi.<br />
· Kumweleza mtu mwingine kuhusu hisia zako, unachokitaka na sababu<br />
zako. Unapojaribu kusuluhisha tatizo au mgongano wa mawazo unakuwa<br />
ni mtu wa kujadili bila kumvunjia heshima mwenzio. Unatafuta suluhisho<br />
lenye manufaa kwa pande zote mbili. Unakuwa ni mtu wa mapatano.<br />
· unakuwa na msimamo wako. Unasisitiza unachokitaka na unachokihitaji.<br />
Unakuwa muwazi na mkweli kuhusu hisia zako. Unakataa kushurutishwa<br />
kwa kitu usichokitaka.<br />
Hisia njema ya mtu mmoja hujengwa na waliomzunguka. Kutakuwa na muda utahitaji<br />
ushauri na msaada toka kwa wengine- toka kwa wazazi, marafiki, walimu,<br />
wajomba, shangazi, kaka , dada, viongozi wa dini au mshauri nasaha. Kitu muhimu<br />
katika kujenga hisia njema ni kuweza kuomba ushauri unapouhitaji.<br />
69
70<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Maelewano Na<br />
Wazazi Wako<br />
Vijana wengine wamebahatika kuwa na wazazi ambao wanaweza wakaelewana na kuzungumza<br />
mambo muhimu. Lakini vijana wengi wanashindwa kuelewana na wazazi wao hasa kipindi cha<br />
balehe. Mahusiano na wazazi wao yanaanza kuwa magumu. Wanaanza kushindana na kubishana<br />
katika kila kitu na wazazi wao. Wanajisikia kama wazazi wao wamepitwa na wakati na wana<br />
mambo ya kizamani. Wanajisikia kama wazazi wao hawawaamini na hawana imani nao.<br />
Gifty, kutoka Ghana (umri, Miaka 14)<br />
“Wazazi wangu wako huru na tunashirikiana katika matatizo<br />
yangu hivyo huwa nakubaliana nao. Kila mara wananifanya<br />
nijisikie mwenye furaha na wananishauri mambo mengi. Ninataka<br />
wazazi wawe na muda mwingi kwa ajili ya watoto wao. Ni vema<br />
wazazi wazungumze na watoto wao na kuwashauri kwa sababu<br />
watoto wanawategemea sana wazazi ili ndoto zao ziwe kweli”.<br />
cathy kutoka uganda (umri, Miaka 17)<br />
“Ukali wa mama yangu na mabadiliko katika mwili wangu<br />
vilijitokeza pamoja. Alinikataza nisijumuike na makundi, wakati<br />
mimi ndio muda niliokuwa nahitaji sana makundi ili kuweza<br />
kubadilishana mawazo.”<br />
Panaito kutoka kenya (umri, miaka 14 )<br />
“Wazazi wangu mara nyingine walinizuia kuchanganyika na vijana<br />
wenzangu”.<br />
barlay kutoka Kenya (umri; miaka 16)<br />
“Wazazi wanajaribu kutufanya tuwe wazuri lakini mara nyingine<br />
huwa wakali. Wanatuchagulia marafiki, na kitendo hicho<br />
sikipendi.”<br />
71<br />
SURA YA 7
72<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
halima kutoka Kenya (umri; Miaka 14)<br />
“Mimi na wazazi wangu mara zote hatukubaliani kuhusu mimi<br />
kutoka nyumbani bila baibui (gauni nyeusi na mtandio wanazovaa<br />
wanawake wa Kiislamu), na baada ya kumaliza mtihani<br />
hawapendi mimi nitoke kila wakati”.<br />
Bila kujali upande uliofungamana nao bado kuna mambo mengi unaweza kufanya ili<br />
kudumisha na kuboresha uhusiano na wazazi wako. Wakati mwingine inaweza kuwa kazi<br />
ngumu lakini ukidhamiria na kujituma jitihada zako zinaweza kufanikiwa, maelewano<br />
yatakuwa mepesi zaidi.<br />
KUTHAMINI FAMILIA<br />
Orodhesha mambo unayoyaenzi na kuyafanya. Pengine unafikiri kuwa ucheshi ni moja<br />
ya sifa zako nzuri. Pengine unapenda unavyotabasamu. Pengine unajisikia vizuri kuhusu<br />
kipaji chako. Pengine unajisikia vizuri kuhusu kipaji chako cha useremala au wepesi katika<br />
hesabu.<br />
Baada ya hapo, jaribu kufikiria wapi hivyo vipaji vilipotoka.. Kwa mfano, Ulijifunza wapi na<br />
toka kwa nani? Unaweza kubainisha baadhi ya tabia hizi kwa wazazi wako, shangazi zako,<br />
na wajomba au ndugu zako wengine? Je, ucheshi ni wa mama yako? Tabasamu ni la baba<br />
yako? Nani alikufundisha mambo ya useremala?n.k<br />
Mara nyingine ni rahisi kuingia katika malumbano na wazazi wako na ndugu wengine<br />
katika ukoo kiasi kwamba sio rahisi kuona ni kiasi gani umerithi toka kwao. Unapata<br />
matatizo ya kuona mambo mnayofanana kwa sababu ya tofauti za mtizamo, tofauti kuhusu<br />
jambo fulani. Mara nyingine unaweza kujisikia unaaibishwa na ndugu zako. Labda wazazi<br />
wako hawana fedha za kutosha, hivyo familia yako wanaishi katika chumba kimoja hata<br />
kukufanya uone aibu kuwaleta marafiki nyumbani.<br />
Ni muhimu kuthamini familia yako na kuikubali kama ilivyo – tajiri au masikini. Lenga<br />
katika kile ambacho ndugu zako wameweza kukupatia, kuliko kile ambacho hawakuweza<br />
kukupatia. Kumbuka kuwa familia yako imefanya kazi kukufanya uwe ulivyo na<br />
utakavyokuwa. Familia yako pia imekupa maadili ya kukuwezesha kuishi kama unavyoishi.<br />
Hii haina maana ya kwamba uko sawa sawa na wazazi wako. Zinaweza kuwepo tofauti<br />
nyingi kati yenu kama kulivyo kufanana kwingi. Kwa kuongezea, kipindi cha balehe ndio<br />
muda ambao vijana wengi wanataka kugundua tofauti kati yao na wazazi wao. Wanataka<br />
kujitegemea, jambo ambalo ni la kawaida na zuri. Hata hivyo, kujitegemea siyo jambo rahisi.<br />
Ukweli linaweza kuwa vigumu sana kwako na hata kwa familia yako.<br />
FAHAMU YALE WAZAZI WAKO WANAYOYATAKA<br />
Unapojaribisha muonekano na tabia mpya na njia mpya za maisha, familia yako inaweza<br />
kuona shida sana. Watashangaa nini kimekupata, wapi umepata mawazo hayo ya ajabu?<br />
Wapi kijana wao wa kiume au kike amekwenda? Huyu kijana ni nani ambaye anapenda<br />
kutumia muda wake mwingi akiwa peke yake au kuzururazurura kwenye vijiwe?<br />
Inaweza kuwa vigumu kwa wazazi kutambua kuwa unakuwa mtu mzima unayeweza kufikiri<br />
mwenyewe na ambaye unayo maoni yako. Bado wanafikiria ungali mtoto. Kuwa mtulivu wakati<br />
wazazi wanajirekebisha kwa mabadiliko yako makubwa.<br />
Grace, kutoka Kenya (umri; Miaka 14)<br />
“Hatukubaliani mara nyingine kuhusu mavazi, kwa sababu wanasema<br />
suruali na jinzi ni kwa ajili ya wanaume. Lakini ninadhani<br />
kuzivaa ni salama kwangu kuliko kuvaa gauni na sketi. Hawataki<br />
pia nisuke rasta. Wanasema ni mtindo wa watu wabaya. Lakini<br />
mimi sifikirii hivyo nachukulia kama mtindo tu”.<br />
bernard, kutoka Kenya (umri; Miaka 17)<br />
“Mara nyingine mawazo yangu yanapingana na ya wazazi wangu.”<br />
Kumbuka kwamba wazazi wako walikua kipindi cha zamani tofauti na wewe. Hata hivyo, kama<br />
wazazi wako wanafuata mila, waonyeshe angalao jambo jipya zuri. Wazazi wako ni kiunganishi<br />
cha utamaduni wa zamani na wa kisasa. Huu ni utajiri kwako. Unaweza kujifunza mengi kuhusu<br />
utamaduni kutoka kwa wazazi wako na wakubwa zako. Litakuwa jambo la kuhuzunisha kama<br />
utapoteza mambo haya:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
SURA YA 7 | MAELEWANO NA WAZAZI WAKO<br />
Lugha ya asili au lugha ya mama.<br />
Historia ya watu wako.<br />
Vifaa vya asili vya muziki, nyimbo na hadithi<br />
Ngoma za asili na upishi.<br />
Ingekuwaje kama usingejua hata moja kuhusu<br />
utamaduni wako? Ungelikuwa nani? Ungelikuwa<br />
upande gani?<br />
Jifunze kuhusu historia yako, utamaduni,<br />
mila, muziki, ala, na kucheza ngoma<br />
Bila kuwa na fikra ya utamaduni wetu na historia yetu tutapotea. Wahenga wetu, lugha yao,<br />
utamaduni na imani ni mambo muhimu ya utambulisho wetu. Usiyadharau!<br />
Bila shaka, utamaduni wa kisasa una mambo mengi mazuri - yale yanayofanya maisha yetu<br />
yaonekane bora kama elimu, madawa ya kisasa na mawazo mapya juu ya wajibu wa wanaume na<br />
wanawake.<br />
Kwa mfano, wasichana sasa wanayo nafasi zaidi katika elimu na kazi nzuri ukilinganisha na bibi<br />
zao. Mitazamo ya zamani kama kuamini kwamba wanawake na wasichana wanalazimika kukaa<br />
nyumbani kupika na kuangalia nyumba zinabadilika. Mtazamo kuhusu kuendeleza mila za ndoa<br />
katika umri mdogo nazo zinabadilika.<br />
Kwa sasa unaishi kipindi cha kusisimua. Mambo mengi yamewekwa wazi. Unayo nafasi ya<br />
kutosha kuchagua namna unavyotaka kuishi. Unaweza ukachagua mazuri kutoka kila upande<br />
– mazuri ya utamaduni wa asili na mazuri ya utamaduni wa kisasa. Unaweza kuyakumbatia<br />
unayofikiri ni mazuri, na kuyakataa yale unayofikiri ni mabaya.<br />
73
74<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Kadri unavyojaribu kufanya maamuzi yako kuhusu yapi unayotaka kuishi nayo, kati ya kiasili na<br />
ya kisasa jaribu kuwa mwangalifu kuhusu hisia na imani za wazazi na wazee wako. Zungumza nao<br />
ili kujua misimamo yao. Waeleze hisia zako na kile unachowaza.<br />
KuMuDu MataRajiO Ya WaZaZi WaKO<br />
Wazazi wengi wanatarajia mengi kutoka kwa vijana wao. Wanataka uishi maisha mazuri kuliko<br />
walivyoishi, hivyo wanataka ufanye kazi kwa bidii zaidi, ufanye vizuri shuleni, na uwe makini zaidi!<br />
Mategemeo ya wazazi wakati mwingine<br />
yanaweza kuonekana kama mzigo mzito.<br />
Mara nyingine inakuwa kana kwamba<br />
wamelenga sana katika maisha yako ya<br />
baadaye wanayofikiria uwe nayo, kiasi cha<br />
kwambahawasikilizi mawazo na matakwa yako.<br />
Huenda baba yako anataka uwe daktari, lakini<br />
huna uwezo katika masomo ya sayansi. Au<br />
pengine mama yako anategemea wewe uoe na<br />
kuishi kijijini ulikozaliwa, lakini unataka uende<br />
Chuo Kikuu ukawe mwandishi wa habari.<br />
Hali ya namna hii inaweza kuwa ngumu. Wazazi unataka kuwa mwalimu, nasema hapana… atakuwa<br />
wako mara kwa mara wanadhani wakati wote daktari. hivyo ndivyo nataka kijana wangu<br />
wanajua kipi kizuri kwako, hata kama hawajui.<br />
Inaweza kuwa vigumu kwao kutambua kwamba wewe ni mtu unayejitegemea mwenye kipaji<br />
chako, mawazo na ndoto zako. Wanaweza kuwa wanapata shida kutambua kati ya ndoto zako na<br />
ndoto walizonazo wao.<br />
Jaribu kuwa mvumilivu na kumbuka kwamba wazazi wako wanataka maisha yako kuwa mazuri.<br />
Endelea kuzungumza na wazazi wako. Waeleze kuhusu malengo na ndoto zako, na kwa nini<br />
unataka kufuatilia ndoto hizo. Waonyesha jinsi ulivyodhamiria.<br />
MaWaSilianO na WaZaZi WaKO<br />
halima, kutoka Kenya (umri; Miaka 14)<br />
“Mara nyingine wazazi wangu wananipa presha kubwa. Wanategemea<br />
nifanye kila kitu vizuri na nisifanye makosa yoyote.<br />
Wananitegemea niwe sahihi, jambo ambalo halitawezekana,<br />
kwasababu sisi sote ni binadamu ambao tunaweza kufanya<br />
makosa wakati wowote!”.<br />
Kukosekana kwa mawasiliano ya wazi ndicho chanzo cha malumbano kati ya vijana na wazazi<br />
wao. Cha kushangaza ni kuwa inakuwa vigumu kukaa chini na kuwa na mazungumzo yenye<br />
manufaa kwa pande mbili.<br />
SURA YA 7 | MAELEWANO NA WAZAZI WAKO<br />
Wazazi wengi hupenda sana kuwasaidia<br />
watoto waoili wapite salama katika kipindi cha<br />
balehe lakini mara nyingi hushindwa namna<br />
ya kuwasaidia. Wanaogopa kuwaaibisha au<br />
kujiaibisha wao wenyewe. Huenda hata wazazi<br />
wao pia hawakuzungumza nao juu ya balehe na<br />
mabadiliko yote anayopitia kijana. Hivyo ni vigumu<br />
sana kwao kukusaidia wakati wao wenyewe<br />
hawakupata msaada wowote. Kama ilivyo kwako,<br />
wanaweza wasiwe na uzoefu mkubwa katika eneo<br />
hili au wasiyajue majukumu yao.<br />
Kwa vipi kijana anaweza kujifunza kuongea kwa<br />
uwazi na wazazi, shangazi, wajomba, babu na bibi<br />
au jamaa yeyote katika familia? Unajenga vipi<br />
julia, kutoka Ghana (umri: Miaka 22)<br />
“Nilipoanza kuona mabadiliko mwilini mwangu, niliona vigumu<br />
kuyazungumza kwa wazazi wangu. Lakini kadri muda ulivyoenda<br />
nilijisikia huru zaidi na niliweza kuongea nao. Niliwauliza swali<br />
lolote nililotaka kuwauliza.”<br />
Waonyeshe wazazi wako kuwa unajali<br />
kuwafurahisha<br />
uhusiano wakati wanapokuamini na hasa kama mlikuwa mnabishana muda mfupi uliopita?<br />
Utaanzaje kujenga uhusiano huo? Bila shaka hakuna jibu rahisi lakini hapa kuna vidokezo<br />
unavyoweza kujaribu:<br />
• Waonyeshe wazazi wako kuwa unaweza kuwafurahisha. Jitolee kuwasaidia wazazi<br />
wako katika shughuli yoyote wanayoifanya – jikoni, kuzunguka nyumba au bustanini.<br />
Wakati mnafanya kazi pamoja eleza suala lako unalotaka mlijadili.<br />
anthony, kutoka Kenya (umri: miaka 15)<br />
“Njia bora zaidi kukabiliana na wazazi ni baada ya kuwa umefanya<br />
kazi fulani ya kuwafurahisha ndipo unapoweza kwenda kuongea<br />
nao jambo unalotaka.”<br />
• chagua muda mzuri wa kuongea. Uchaguzi wa muda ndio kila kitu! Chagua muda<br />
ambao wazazi wako hawajachoka sana au wakati hawana shughuli nyingi. Yaweza kuwa<br />
vizuri kusubiri hadi mwisho wa wiki wakati wanapumzika na hawafikirii sana masuala<br />
ya kazi.<br />
• anza na mada rahisi. Anza na mada ambayo sio ya kutahayarisha kwako au kwao na<br />
ambayo hamtofautiani nao sana. Katika familia nyingi wazazi na watoto wao huanza<br />
kuongea pale tu kunapokuwa na jambo zito – mfano wakati watoto wanapotaka<br />
kufanya kitu wasichopenda wazazi. Hapa ni mahali pagumu kuanzia.<br />
Unaweza kuanza kujaribu kuzungumza na wazazi wako juu ya hali au tatizo la rafiki yako<br />
kwanza kabla ya kwako.<br />
75
76<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Hii inaweza kuwapa wote wewe na wazazi wako hisia za kumthamini kila mmoja wenu na<br />
inaweza kusaidia kujenga uaminifu na uelewa juu ya hali isiyokuwa ya binafsi sana. Lakini<br />
usisaliti uaminifu wa rafiki yako, pia linda siri zake. Kwa mfano unaweza kuongelea tatizo<br />
la rafiki yako kwa wazazi wako, lakini usimtaje kwa jina huyo rafiki yako aliye katika hali<br />
ngumu.<br />
•<br />
Waonyeshe wazazi wako kuwa unayajali<br />
mawazo yao. Waulize wazazi wako<br />
wanafikiria nini na kwa nini wanajihisi<br />
hivyo katika hali fulani. Jaribu kuelewa<br />
mtazamo na wajibu wao. Labda unadhani<br />
wazazi wako hawataki uende disko kwa<br />
sababu ni wakali. Lakini huenda kuna kitu<br />
wanakijua kuhusu disko ambacho wewe<br />
hukijui. Huenda wamesikia kuwa wasichana<br />
hubakwa huko au watu huuza madawa ya<br />
kulevya huko. Wanaweza kuwa na sababu<br />
nzuri sana ya kuhisi hivyo na wangependa<br />
uvutiwe na sababu zao na uyajali mawazo<br />
yao.<br />
Waulize wazazi wako nini wanafikiri na kwa<br />
nini. Wanaweza wakawa na sababu nzuri kuhusu<br />
mienendo yao.<br />
• uwe na heshima. Wazazi wako, ndugu zako na wakubwa zako wanajali sana suala la<br />
heshima. Hivyo hata kama unahisi kukatishwa tamaa, jaribu kutopiga kelele na kufanya<br />
wakuone huna heshima. Pia uwe na heshima kwa maadili yao. Wakati baadhi ya maadili<br />
yanaweza kuwa sawa na ya familia yako lakini mengine yaweza kuwa tofauti. Kama<br />
unataka kuishi katika maadili tofauti na ya wazazi wako ni sawa, lakini usiwakosee<br />
wazazi wako juu ya imani zao hata kama kwako zitaonekana kupitwa na wakati au kuwa<br />
za kijadi mno kwako.<br />
• jenga kuaminika. Waonyeshe wazazi wako kuwa unawajibika na kuwa wanaweza<br />
kukuamini. Wakikuambia kuwa uwe nyumbani wakati fulani, hakikisha kuwa unakuwa<br />
nyumbani wakati huo. Uwe muwazi kwao kwa kitu unachotaka kufanya na elezea<br />
sababu zake. Usijaribu kwenda disko kwa siri wakati umewaambia wazazi wako kuwa<br />
unaenda nyumbani kwa rafiki yako. Ukijaribu kuwadanganya huenda wakagundua na<br />
utakuwa umevunja imani yao kwako.<br />
Wazazi wako wanatakiwa kuheshimu mambo yako ya faragha. Lakini usitumie vibaya<br />
faragha hiyo kwa kuishi maisha ya siri na ya hatari. Wazazi wako pia wanatakiwa<br />
waheshimu uchanguzi wako wa marafiki lakini pia unahitaji kuwaonyesha kuwa unaweza<br />
kuchagua marafiki wazuri. Usijihangaishe na watu ambao hawakujali na ambao maadili yao<br />
kimsingi yanapingana na ya familia yako.<br />
aloysious, kutoka uganda (umri: Miaka 19)<br />
“Unatakiwa kufanya ulichoambiwa hata kama hupendi na<br />
usiwafadhaishe wazazi kwa kufanya vitu ambavyo unajua vita<br />
waumiza moyoni. Kwa kufanya yote haya utakapoongea nao<br />
hawatakukatalia lolote utakalowaambia.”<br />
SURA YA 7 | MAELEWANO NA WAZAZI WAKO<br />
• uwe muwazi kwa wazazi wako. Kumbuka<br />
kuwa unabadilika haraka sana kiasi<br />
kwamba wazazi wako wanaweza kuhisi<br />
kuwa hawakuelewi vizuri. Ni wajibu wako<br />
kuhakikisha kuwa wanakuelewa. Ongea<br />
nao kuhusu ndoto zako, matarajio yako,<br />
na mahitaji yako ili wahisi kujiamini kuwa<br />
wanakufahamu wewe na unachokitaka.<br />
Shirikiana nao katika masikitiko na<br />
mashaka yako. Waulize wangekuwa ndio<br />
wenyewe katika nafasi yako wangefanyaje.<br />
Waruhusu wazazi wako wakutane na rafiki<br />
zako ili wajue ni nani unayekwenda naye<br />
matembezini.<br />
Kwa wazazi wako, watambulishe marafiki zako<br />
ili wajue kuwa wanaweza kukuamini.<br />
Wakati wazazi wako wanapohisi kuwa wanakuelewa vizuri, watajisikia vizuri zaidi<br />
wakikuamini. Itawasaidia kuanza kukukubali kama mtu unayeelekea ukubwani na kuacha<br />
kukuchukulia kama mtoto. Itasaidia pia wakuruhusu ufanye maamuzi mengi mwenyewe.<br />
Prisca, kutoka Kenya (umri: Miaka 14)<br />
“Njia nzuri ya kukabiliana na wazazi wako ni kuwaeleza matatizo<br />
yako na kuwaomba kama wanaweza kukusaidia. Ukiwaomba<br />
hawawezi kukataa kwasababu wana mapenzi na uelewa. Unaweza<br />
kupanga siku ya kukaa nao pamoja na kubadilishana nao mawazo<br />
juu ya vitu unavyotaka kuzungumzia kwa sababu hawawezi<br />
kukataa.”<br />
• Waonyeshe wazazi wako kuwa unawajali. Kama unavyotaka wao wakuonyeshe kuwa<br />
wanakupenda, ni wajibu wako kuwaonyesha kuwa unawajali. Wafanyie vitu vizuri<br />
kuonyesha kuwa unawapenda na unataka kuwafurahisha.<br />
Sherifan, kutoka Ghana (umri: Miaka 15)<br />
“Unatakiwa wakati fulani uwanunulie wazazi wako zawadi. Huwa<br />
wanafurahi sana.”<br />
Ni vigumu sana kuelewana vizuri na wazazi wako, na kumudu ukali wao, kuyakidhi matarajio<br />
yao makubwa, na kuyakubali maadili yao ya kiutamaduni. Itachukua muda na subira kubwa.<br />
Lakini kila dakika itakuwa na thamani kwa juhudi kidogo utakayoifanya. Itakuwa ya<br />
thamani kwa sababu kuna wakati marafiki na wenzako hawawezi kukushauri kama wazazi<br />
wako”.<br />
Gifty, kutoka Ghana (umri: Miaka 14)<br />
“Unapaswa uwaheshimu wazazi wako na uweke aibu kando.<br />
Uwaeleze wazazi wako matatizo yako kwa sababu ndio watu<br />
pekee wa kuwa na majibu kwa matatizo yako. Ongea na wazazi<br />
wako mara kwa mara”.<br />
77
78<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
VYANZO VINGINE VYA KUPATA MSAADA.<br />
Wakati mwingine kunatokea tofauti kubwa kati<br />
ya wazazi wako na wewe mwenyewe kuhusu<br />
mitazamo mbalimbali. Umejaribu kuzungumza nao<br />
lakini hukufanikiwa. Wanakataa kukusikiliza na<br />
tatizo linazidi kuwa zito. Kwa mfano, inawezekana<br />
wazazi wakasema kuwa wanataka kukuachisha<br />
shule ili wakuoze kwa mwanaume mzee.<br />
Umejaribu kuwaelezea umuhimu wa shule kwako.<br />
Umewaeleza kuhusu ndoto yako ya kuwa mwalimu<br />
na hawajakusikiliza.<br />
Kuna hali nyingi ngumu kama hizi ambazo huwezi<br />
kuzimudu peke yako. Unahitaji kumtafuta mtu<br />
mzima anayeweza kukusaidia.<br />
jenifer, Kutoka Ghana (umri: Miaka 17)<br />
“Unapaswa kuwasaidia nyumbani katika chochote<br />
wanachokifanya. Katika kuwasaidia mambo yote haya<br />
mapenzi kati yako na wao yatadumu muda mrefu.”<br />
Kama unaona ni tatizo kuongea na<br />
wazazi, jaribu kumuuliza mtu mzima<br />
mwingine kwa ushauri na msaada.<br />
evans, kutoka Kenya (umri: Miaka 16).<br />
“Kama huwezi kuzungumza na wazazi wako kutatua tatizo au<br />
mabishano, unapaswa kuzungumza na ndugu wa karibu, mtu<br />
kama shangazi yako au mjomba ambaye atakusaidia wewe na<br />
kujua lipi zuri kwako.”<br />
Jaribu kuzungumza na mtu mzima mwingine ambaye ni mpole, anayejali na unayemwamini<br />
– mtu anayekufahamu, kama ndugu, kaka, mtu mzima au dada, mwalimu, rafiki wa familia,<br />
baba wa rafiki yako, kiongozi wa dini au afisa jamii. Mwombe akupe ushauri na akusaidie<br />
kuzungumza na wazazi wako kuhusu jambo hilo.<br />
Hata kama huna tatizo kubwa na wazazi wako, lakini unahitaji ushauri, unaweza kujikuta<br />
kuwa ni rahisi zaidi kuzungumza na shangazi, mjomba au ndugu. Wako watu wengi<br />
wanaokujali na wako tayari kukusaidia ukiwaomba.<br />
SURA YA 7 | MAELEWANO NA WAZAZI WAKO<br />
Sura ya 7<br />
MAELEWANO NA WAZAZI WAKO<br />
Ujana balehe ni kipindii ambacho vijana wengi inawawia vigumu kupatana na<br />
wazazi wao. Lakini sio lazima mara kwa mara iwe hivi. Yapo mambo mengi unaweza<br />
kuyafanya kuimarisha uhusiano na wazazi wako:<br />
thamini familia yako. Ikubali familia yako jinsi ilivyo - tajiri au masikini. Tumia muda<br />
wako kufikiria kile ambacho familia yako imekupatia, kama vile nguvu ulizonazo,<br />
kuthaminiwa na vitu vingine vinavyokuhusu wewe mwenyewe. Usiangalie tu nini<br />
hawajakupatia.<br />
elewa imani na vitu wanavyothamini wazazi wako. Wazazi wako walikua kipindi<br />
tofauti na wewe. Hata kama unafikiria wazazi wako wanafuata mila za kizamani,<br />
tafuta yaliyo mema. Jifunze kutoka kwao kuhusu historia yenu, mila na desturi,<br />
muziki na lugha.<br />
Kumbuka kwamba wazazi wanakutakia mema. Kumudu matarajio ya wazazi wako<br />
inaweza kuwa vigumu, hasa ikiwa matarajio ya ndoto zao na zako yanatofautiana.<br />
Zungumza na wazazi wako kuhusu malengo yako na kwa nini unataka<br />
kuyaendeleza. Waonyeshe kuwa unayo nia na unafanya kazi kwa bidii.<br />
Kuwa mwaminifu na muwazi kwa wazazi wako. Angalia wakati mwafaka wa<br />
kuzungumza na wazazi wako. Wape nafasi ya kujua utakuwa mtu mzima wa<br />
namna gani. Waonyeshe kwamba ni mwaminifu na muwajibikaji.<br />
Waonyeshe wazazi wako kwamba unajali hisia zao na unataka kuwafurahisha.<br />
Waulize wazazi wako kwa nini wanahisi wanavyo hisi. Jaribu kuelewa tatizo lao.<br />
Waonyeshe kwamba unapenda na kujali wanachofikiria.<br />
Kuwa na heshima. Hata kama hukubaliani na wazazi wako, jaribu kutokuongea kwa<br />
sauti kali au kuwaonyesha ufidhuli.<br />
Kuwa mvumilivu kwa wazazi wako. Wape muda wazoee ukweli kuwa umeanza kuwa<br />
mtu mzima mwenye maoni na ambaye anayeweza kufikiri mwenyewe.<br />
Kuwa mvumilivu kwako binafsi. Kujenga mahusiano ya karibu na ya wazi na wazazi<br />
wako inachukua muda na ni kazi ngumu. Usivunjike moyo na kukata tamaa, uhusiano<br />
mzuri hauwezi kujengwa kwa siku moja.<br />
Mara nyingine, tofauti ya maoni kati yako na wazazi wako inaweza kuwa kubwa sana.<br />
Tafuta mtu mzima anayejali na unayemwamini – shangazi au mjomba, mtu mzima,<br />
rafiki wa familia, mwalimu, kiongozi wa dini au afisa ustawi na omba ushauri. Pengine<br />
wanaweza wakasaidia kutatua tatizo ulilonalo dhidi ya wazazi wako.<br />
79
80<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Urafiki Na Mapenzi<br />
Sura hii ianahusu urafiki na mapenzi. Kila mtu anahitaji urafiki ulio mzuri na kila mtu<br />
anahitaji kujisikia anapendwa na watu wengine.<br />
uRaFiKi<br />
Marafiki wanachukua nafasi kubwa katika<br />
kutufanya sisi tuonekane kama tulivyo.<br />
Wanatufanya tucheke na wanatufanya tujisikie<br />
wenye furaha. Wanatufahamisha mambo<br />
mapya na mawazo mapya, wanakuza upeo wetu.<br />
Wanashiriki ndoto zetu na kujaribu kutusaidia<br />
kutengeneza mipango ya maisha ya baadaye.<br />
Marakifi zetu pia wanaweza kujibu maswali<br />
yetu mengi hasa katika kipindi cha ujana balehe<br />
na wanatusaidia tujisikie vizuri pamoja na<br />
mabadiliko kadhaa yanayotokea. Tukiwa na<br />
matatizo, wanatutia moyo na kutusadia kutatua.<br />
Wanatusaidia kututhibitishia tulivyo.<br />
urafiki ni muhimu wakati wa balehe na<br />
katika maisha yote<br />
naana, kutoka Ghana (umri wa miaka 17)<br />
“Marafiki zangu wengi walianza kuona mabadiliko katika miili yao<br />
karibia wakati huo huo nilipoyaona mimi. Kwa hiyo sikuwa na hofu<br />
nayo. Tulijadili mabadiliko na niligundua kwamba tuna matatizo<br />
yanayofanana.”<br />
Grace, kutoka Kenya (umri wa miaka 14)<br />
“Marafiki zangu ni watu wazuri. Tunaheshimiana na kupendana<br />
kama dada na kaka. Wananipenda jinsi nilivyo na kama nimekosea<br />
wananiambia wazi namna ninavyotakiwa kufanya. Wengine<br />
wanafikiri ni vibaya kuwa na marafiki wa jinsi nyingine. Mawazo<br />
yao ni mazuri na tunayajadili, tunaweza kuomba ushauri kutoka<br />
kwao.”<br />
81<br />
SURA YA 8
82<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Gift, kutoka Ghana (umri wa miaka 14)<br />
“Marafiki zangu wananipenda na kuniheshimu sana kwa sababu mimi ni<br />
mwaminifu na ninawashauri kuhusu nini msichana anatakiwa kufanya.”<br />
Unaweza kuwa na urafiki na watu wa jinsi moja au na watu wa jinsi tofauti.<br />
Seif, kutoka tanzania (umri wa miaka 13)<br />
“Ninao marafiki wa kike watatu. Tunakaa na kuongea au kusoma<br />
pamoja. Rafiki wa kike ni kama rafiki wa kawaida tu.”<br />
evans, kutoka Kenya (umri wa miaka 16)<br />
“Mimi na rafiki yangu wa kike tunasaidiana kazi za shule na<br />
kubadilishana mawazo kuhusu maisha na namna ya kujiheshimu mbele<br />
za watu wazima.”<br />
halima, kutoka Kenya (umri wa miaka 14)<br />
“Kuwa na rafiki mvulana au msichana maana yake ni kusaidiana na<br />
kufanya maamuzi pamoja. Vile vile kuzungumza kama kuna tatizo.”<br />
Wavulana na wasichana wanaweza kuwa marafiki na wanaweza kuwa na urafiki bila ya<br />
kujamiiana. Wavulana na wasichana wanaweza kuwa na mahusiano ya kimapenzi ambayo<br />
hayahusishi ngono. Kwa hiyo tunapotumia maneno “rafiki wa kiume” na “rafiki wa kike”<br />
haina maana ya kwamba mahusiano hayo ni ya kufanya ngono.<br />
anthony, kutoka Kenya (umri wa miaka 15)<br />
“Urafiki wetu sio wa kufanya ngono au kufanya kitu chochote<br />
kitakachotufanya tujute baadaye. Urafiki wetu ni wa kusaidiana kama<br />
marafiki na sio kitu kingine.”<br />
Kwame, kutoka Ghana (umri wa miaka 17)<br />
“Watu wanafikiri rafiki wa kike ni mtu ambaye unahusiana naye kingono<br />
tu. Rafiki wa kike ni mtu ambaye unaweza kumwomba ushauri, mtu<br />
ambaye unaweza kushirikiana naye kwenye matatizo.”<br />
Urafiki mzuri na wa nguvu unapendeza sana. Unakufanya ufurahi.Unachangia katika kukua<br />
kwa hisia kwa sababu unakufundisha jinsi ya kuwa karibu na mtu.<br />
Urafiki mzuri vile vile unachangia katika kujiheshimu. Ukiwa na rafiki mzuri, unajisikia<br />
vizuri. Inapendeza kuwa na mtu ambaye unaweza kumweleza siri zako. Vile vile inapendeza<br />
kuwa na mtu anayejisikia vizuri kukueleza siri zake. Unaweza kushirikiana naye mawazo<br />
bila wasiwasi wa kuchekwa. Unaweza kushirikiana naye siri na kujua kwamba hazitatoka<br />
nje. Inapendeza kufahamu kwamba rafiki yako atakupenda na kukuheshimu hata kama<br />
hukubaliani naye kuhusu jambo fulani.<br />
Kupitia urafiki wa karibu, unaweza kujifunza jinsi ya kukubali au kukataa mambo tofauti.<br />
Unajifunza pia jinsi ya kuwa na nguvu za kutosha kutetea maoni yako.<br />
Kujiamini ni muhimu kwa maisha ya baadaye na kwa mahusiano na watu wengine. Ukweli ni<br />
kwamba marafiki wanakusaidia kujenga stadi nyingi muhimu ambazo unazihitaji ili kufanikiwa<br />
maishani. Stadi hizo ni pamoja na kuwa na uwezo wa:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
SURA YA 8 | URAfIKI NA MApENZI<br />
Kuwasiliana vizuri na kuwa muwazi kuhusu hisia zako na mawazo yako.<br />
Kusikiliza na kujua hisia za mtu mwingine na maoni yake.<br />
Kusaidia pale mtu anapokuwa na matatizo au anajisikia hovyo.<br />
Kujadili (kwa mfano, wewe na rafiki yako hamjakubaliana kuhusu jambo fulani, utahitaji<br />
kujadiliana na kuafikiana au kufikia mwafaka).<br />
Kushirikiana, kufanya kazi pamoja na kuwajibika kwa pamoja<br />
Kukubali na kuheshimu tofauti za maoni, imani na mazoea. (Kwa mfano, wewe na rafiki<br />
yako mnaweza msiafiki kuhusu jambo fulani. Ni sawa tu.<br />
Hasa urafiki unajengeka katika kipindi cha ujana balehe kwa sababu vijana wengi wanaona<br />
aibu kuongea na wakubwa. Iwapo wazazi wako wanafikiri kutumia muda wako na marafiki<br />
ni kupoteza muda, jaribu kuwaeleza namna marafiki zako walivyo muhimu kwako na kwa<br />
nini. Unahitaji marafiki.<br />
Urafiki mzuri na wa nguvu unachukua muda na bidii kuujenga. Hautokei usiku mmoja na<br />
huwezi kupata marafiki wa kweli kila siku.<br />
JINSI YA KUMTAMBUA MTU AMBAYE SI RAFIKI WA KWELI.<br />
Inaweza ikatokea wakati mwingine mtu ambaye ulifikiri ni rafiki akageuka kuwa rafiki mbaya.<br />
Kwa mfano rafiki anapotoa siri kwa watu wengine, au anaeneza uvumi wa hovyo kuhusu<br />
wewe, huyu hafanyi vile ambavyo rafiki wa kweli anatakiwa kufanya. Rafiki wa namna hii<br />
anaweza kukuumiza, lakini hayo ndiyo maisha. Jaribu kuzungumza naye na muombe aache<br />
kufanya kitu chochote ambacho kina kukasirisha. Kama rafiki yako haachi kukufanyia<br />
vibaya, kaa mbali naye. Kupoteza rafiki inasikitisha/inahuzunisha, lakini utapata rafiki<br />
mwingine aliye bora zaidi.<br />
ayoo, kutoka uganda (umri wa miaka 15)<br />
“Niliwapoteza marafiki zangu wote kwa sababu<br />
hawakuheshimu<br />
maoni yangu. Sasa ninaye rafiki wa kweli mmoja tu, lakini<br />
tunaheshimiana.”<br />
Marafiki wanaweza kuwa chanzo cha shinikizo – Hasa shinikizo la kundi-rika ambalo ni<br />
chanzo kikubwa cha wasiwasi kwa wazazi. Shinikizo la kundi-rika mara nyingi huwafanya<br />
vijana wafanye makosa, kama kunywa pombe, au madawa ya kulevya. Shinikizo la kundi<br />
rika linaweza kuwafanya vijana wajamiiane wakati kwa kweli hawapendi kufanya hivyo.<br />
Florence, kutoka Ghana (umri wa miaka 16)<br />
“Ninapata shinikizo kutoka kwa wasichana wengine<br />
wanapojipamba na wanapotoka na kwenda kwa wavulana.<br />
Ninajishauri mwenyewe nisionyeshe tabia mbaya au kufanya<br />
mambo mabaya.”<br />
83
84<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Katika kipindi cha ujana balehe, ni jambo la kawaida kuona vijana wakiwa katika makundi ya<br />
kirafiki, wakilazimika kufanya mambo fulani fulani katika kundi hilo au kuwa na mtazamo fulani<br />
kama unataka kujiunga au kubaki katika kundi hilo. . Jihadhari na shinikizo la kundi rika kwani<br />
lina nguvu sana kwa sababu unataka kupendwa na unataka kuwa sehemu ya kikundi; na unataka<br />
kuwafurahisha marafiki zako ndani ya kikundi na unataka kuhakikisha hubaki nyuma.<br />
Wakati wote hakikisha akili yako iko sawasawa na<br />
unakuwa mkweli. Usijihatarishe ati kwa sababu unataka<br />
kuwa na kundi la marafiki.<br />
Jambo jingine la kukumbuka: Unaweza ukatokea<br />
wakati fulani kipindi cha ujana ukajisikia kama vile<br />
huna marafiki wa karibu. Hii inaweza kukufanya ujisikie<br />
mpweke, mwenye huzuni na wasi wasi. Usihofu kuwa<br />
una tatizo lolote. Inawezekana wewe umekomaa kidogo<br />
kuliko wenzako wa umri mmoja. Labda unataka mambo<br />
tofauti na rafiki zako wa rika moja. Jinsi utakavyo kuwa<br />
unakua na kukutana na watu wapya, utatengeneza<br />
marafiki wazuri na wa nguvu. Kuwa mvumilivu. Ipo siku.!<br />
KueleWana na jinSia nYinGine<br />
Vijana wengi wanapata shida kuelewana na mtu wa<br />
jinsi nyingine. Hawajui jinsi ya kutendeana kwa heshima na inavyofaa, na hawajui wafanye nini<br />
wanapokuwa wamezungukwa na watu wa jinsi nyingine. Vifuatavyo ni vidokezo kwa wavulana:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Usimwangalie au kumpigia mlunzi msichana kwa sababu ya jinsi anavyoonekana, gauni<br />
alilovaa au namna anayotembea.<br />
Msikilize rafiki yako wa kike anachosema na elewa anaposema “hapana” ana maanisha<br />
“Hapana” na sio vinginevyo. Usijaribu kujishawishi mwenyewe kwamba anamaanisha “labda”<br />
au “ndio” wakati anaposema hapana.<br />
Usipitepite karibu na msalani wa wasichana na/au kuziba njia yao.<br />
Usiwanyanyase au kuwatisha kwa makusudi wasichana usiku au sehemu zisizo na watu.<br />
Usivumishe mambo mabaya kuhusu wasichana.<br />
Wasichana vile vile wanaweza kuwa na mtazamo mbaya kwa wavulana. Vifuatavyo ni<br />
vidokezo vya jinsi ya kuelewana na wavulana:<br />
Usiwatafute wavulana ili upate pesa au zawadi kutoka kwao.<br />
Wakati mwingine vijana wa rika lako<br />
wanaweza kukutenga kwenye kundi lao. hii<br />
inaweza kuwa vigumu na unaweza kufikiri<br />
ufanye lolote ili ujiunge nao. Kuwa mkweli<br />
na usijihatarishe kwa ajili ya kupata<br />
heshima yao.<br />
Kubali kwamba wavulana nao wanashawishika na wanazo hisia kama zako. Usiwacheke,<br />
kuwatania au kuwafanyia mzaha.<br />
Kuwa muwazi kwa wavulana. Yaweke wazi yale unayotaka kuyafanya na yale ambayo hutaki<br />
kuyafanya. Sema yale ambayo kweli unayafikiria na usiogope kujieleza. Kuwa na uhakika,<br />
jiamini, kama hutaki kufanya jambo fulani sema “HAPANA” na ng’ang’ania hivyo hivyo.<br />
•<br />
SURA YA 8 | URAfIKI NA MApENZI<br />
Usianzishe uzushi kuhusu wavulana.<br />
Mara nyingi wasichana na wavulana wanaishia katika mahusiano mabaya kwa sababu hawana<br />
uelewa na uzoefu wa namna ya kuishi na jinsia nyingine. Wavulana hawajui wasichana<br />
wanataka nini kutoka kwa wavulana na wasichana vile vile hawajui wavulana wanataka nini<br />
kutoka wasichana. Hapa kuna vidokezo vichache vitakavyokusaidia:<br />
• Wasichana wanataka upendo, kujaliwa, uaminifu na heshima. Wasichana wanapata<br />
hofu kama wavulana hawawaheshimu. Wanapenda wavulana wanaotumia muda kuwasikiliza<br />
bila mzaha.<br />
• Kuwa pamoja: Wasichana wanaona kwamba kuwa pamoja na kujumuika na wavulana<br />
kunafurahisha na kusisimua. Pia wanawapenda wavulana ambao wanaweza kuwasaidia<br />
wanapopata matatizo na ambao wanaweza kustarehe, kutaniana na kucheka nao.<br />
• uhuru: Wasichana wanataka kupewa nafasi ya kufikiri wenyewe.Wanawapenda wavulana<br />
wanaotambua kwamba wasichana wana akili na wanapenda kuzitumia.<br />
• Wavulana wanaojiamini: Wasichana wanawahusudu wavulana ambao wanajiamini na<br />
ambao hawawaogopi wasichana.<br />
• Wavulana wasiojifanya: Wasichana wanawapenda wavulana ambao hawaigi wengine<br />
na kujifanya wana hali fulani kumbe sio. Wavulana wanataka nini? Wavulana wengi wanayataka<br />
yale yote ambayo wasichana wanayataka katika mahusiano.<br />
• Wavulana wanataka upendo, kujaliwa, uaminifu na heshima. Wavulana wengi wanapenda<br />
kuwa na msichana anayejali na kusaidia – mtu anayesikiliza, aliye na heshima na<br />
asiye na mzaha<br />
• Kuwa pamoja: Kila mtu anapenda kujumuika. Wasichana na wavulana pia wanataka mtu<br />
ambaye wanaweza kutumia muda naye kucheka, kusimuliana hadithi na kuzungumza<br />
kuhusu maoni yao, ndoto na hata malengo.<br />
• uhuru: Wavulana wengi wanasukumwa kutenda mambo kinguvu. Wanatenda kama vile<br />
hawana hisia na hawajisikii kitu. Wanataka mtu ambaye wanaweza kushirikiana naye<br />
kimawazo na kihisia.<br />
• Wasichana wanaojiamini: Tofauti na ambavyo wasichana wengi wanavyoamini, wavulana<br />
wanawapenda wasichana wanaojiamini– wasichana ambao hawaogopi kujieleza<br />
wenyewe kwa uhuru.<br />
• Wasichana wasiojifanya: Wavulana wanawapenda wasichana ambao ni halisi - wasichana<br />
ambao hawaigi mambo ya wengine kama kukomaa, kujisikia au kuringa.<br />
Msingi wa mahusiano mazuri ni urafiki wa nguvu – sio tu jinsi mtu anavyoonekana au mvuto<br />
wa kimapenzi. Katika uhusiano mzuri, hakuna mtu anayejaribu kumdhibiti mwenzake au<br />
kumlazimisha katika kufanya mambo. Pia hakuna mtu ambaye anamnyonya mwenzake au<br />
kumtumia mwenzie kwa namna yoyote ile.<br />
Kumbuka kuwa mahusiano mazuri na ya kudumu hayaji katika muda mfupi. Inachukua muda<br />
kufahamiana kikweli kweli na kujenga urafiki wa nguvu.<br />
KUANZA MAHUSIANO NA MTU UNAYEMPENDA.<br />
Ujana balehe ni wakati ambao unaweza kuanza kujisikia una hamu au unavutiwa na watu<br />
wengine. Unaweza kumuona mtu shuleni kwako ambaye anaonekana mzuri na unafikiria<br />
ungependa muwe marafiki.<br />
85
86<br />
Lakini huna uhakiki utamuanza namna<br />
gani. Hujui kama atapendelea kuwa rafiki<br />
yako. Unachokijua ni kuwa anaweza asiwe<br />
amegundua nia yako.<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Prisca, kutoka Kenya<br />
(umri: miaka 14)<br />
“Njia nzuri ya kumwendea<br />
msichana au mvulana<br />
ni kumwendea kwa<br />
upole. Njia nzuri ya<br />
kuanza urafiki ni kwa<br />
kumjali rafiki yako na<br />
kusaidiana naye nyakati<br />
za matatizo.”<br />
Mercy, kutoka Ghana<br />
(umri: miaka 16)<br />
“Kitu cha kwanza cha kufanya ili kuanza urafiki ni kuwa rafiki wa mtu huyo<br />
na mkishafahamiana vizuri unaweza kumuambia kilichoko kichwani au<br />
moyoni mwako kwa kuzungumza na kufungua hisia zako.”<br />
Ni vigumu kumwendea mtu mpya hususani kama unampenda kimapenzi. Unaweza kuogopa<br />
kumwendea msichana au mvulana kwa sababu hutaki kukataliwa na kuumiza roho yako.Kwa<br />
upande mwingine iwapo hutamfuata mtu huyo hutakuwa na mahusiano ya aina yoyote na<br />
mtu huyo kabisa.<br />
Kuna njia mbili za kujua kama mtu anakupenda na<br />
ana hamu na wewe. Unaweza kuzungumza naye<br />
wewe mwenyewe au unaweza kumwomba rafiki<br />
yako aongee naye.<br />
Iwapo utachagua kumpata rafiki wa kumwendea<br />
mtu unayempenda, kuwa mwangalifu kuchagua<br />
rafiki mzuri - mtu ambaye anaaminika sana.<br />
Usingependa kumchagua rafiki ambaye ataishia<br />
kuwaeleza watu wengine kwamba unampenda<br />
mtu fulani. Vile vile usingependa kumchagua rafiki<br />
ambaye ataongea maneno mengi na yule mtu. Kwa<br />
mfano unaweza kutaka rafiki yako ataje jina lako<br />
tu kuona kama yule mtu anakujua wewe ni nani na<br />
kama ana nia na wewe.<br />
ujana balehe ni wakati ambao utaanza kujisikia<br />
kuvutiwa na watu wengine<br />
Kama unavutiwa na mtu, onyesha urafiki na<br />
kuwa mkweli. tafuta nafasi ya kukutana nae.<br />
Ni sawa kabisa kumuomba rafiki yako kumuendea mtu unayempenda, lakini itafikia wakati<br />
ambao utalazimika kuongea naye wewe mwenyewe. Hii inaweza kukuwia vigumu.Unaweza<br />
kuona aibu. Mikono inaweza kulowa jasho. Unapoanza kuzungumza unaweza kusahau<br />
kabisa ulichotaka kusema. Haya yote ni hisia za kawaida kwa mtu anapokuwa na hali ya<br />
wasiwasi au ya kusisimka.<br />
SURA YA 8 | URAfIKI NA MApENZI<br />
Jaribu kutulia na kujikumbusha kwamba wewe ni mtu unayevutia unayefurahisha na mwenye<br />
akili. Huna cha kupoteza. Kuwa mwema kwa mtu unayempenda. Anza mazungumzo naye. Tafuta<br />
anapendelea nini na nenda ukamwone. Iwapo msichana au mvulana ni mwema, chukua hatua<br />
inayofuata. Mweleze ungependa mfahamiane zaidi. Muulize kama anaweza kwenda kufanya kitu<br />
na wewe.<br />
KujenGa MahuSianO YenYe nGuVu<br />
Zipo njia nyingi za kumuelewa mtu vizuri na kujenga urafiki wa karibu na mahusiano mazuri.<br />
Mnaweza kwenda kutembea naye, kwenye sherehe, kuangalia sinema au kunywa na kula pamoja.<br />
Mnaweza kucheza michezo na mnaweza kujihusisha katika shughuli za kijamii au za kidini<br />
pamoja. Mnaweza kusoma pamoja. Mnaweza kutumia muda pamoja mnapokuwa kwenye kikundi<br />
cha marafiki.<br />
Kama lengo lako ni kumuelewa mtu vizuri na kujenga mahusiano ya karibu na ya kudumu,<br />
mkifanya shughuli mbalimbali pamoja, ni vizuri zaidi kuliko kujamiiana tu. Ukweli ni kwamba<br />
kuanza kujamiiana kabla mahusiano hayajawa ya karibu na yenye nguvu kunaweza kuharibu<br />
mahusiano. Au mahusiano yenu yanaweza yakawa ya kujamiiana tu.<br />
Kumbuka ngono na upendo ni vitu viwili tofauti. Kujamiiana hakumaanishi watu wawili hawa<br />
wanapendana.<br />
Sherifan, kutoka Ghana (umri wa miaka 15)<br />
“Unapofanya ngono, haina maana mnapendana. Mtu anaweza<br />
akawa anakutumia, kwa sababu unapendeza na unamvutia, lakini<br />
sio kwa sababu anakupenda”.<br />
hamson, kutoka Ghana (umri wa miaka 15)<br />
“Ngono na kupenda havifanani. Ukilala na msichana haina maana<br />
kwamba msichana huyo anakupenda”.<br />
Watu wengi wanafikiri ngono inafanya mahusiano yawe na nguvu, lakini hii sio kweli.Ngono sio<br />
njia nzuri ya kuweka mahusiano, na wakati mwingine inaweza kuharibu mahusiano kabisa.<br />
Okakah, kutoka Kenya (umri wa miaka 17)<br />
“Mmoja wa marafiki zangu wa karibu aliniambia kwamba ningempoteza<br />
rafiki yangu wa kike kama nisingemridhisha kimapenzi.<br />
Kwa kweli hili lilinipa dukuduku sana kwa hiyo nilianza kujaribisha<br />
naye, hata kama hakuwa katika hali ya kutaka. Hili lilinifanya<br />
niwe na dukuduku zaidi. Nilimwuliza kwa nini alikuwa katika<br />
hali hiyo. Alinieleza kwamba kufanya mapenzi kungesababisha<br />
mimba isiyotakiwa na kama ikitokea tungepoteza hadhi yetu<br />
katika jamii. Mwishowe tuligundua kwamba wapenzi wanahitaji<br />
kuheshimiana na kuelewana, na wanahitaji kupuuza shinikizo<br />
kutoka kwa vijana wengine.”<br />
87
88<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Marafiki wa Okakah walimwambia kwamba angempoteza rafiki yake wa kike iwapo asingefanya<br />
naye ngono, lakini ukweli ni kwamba ilikaribia kumpoteza rafiki yake wa kike kwa kumwambia<br />
wafanye ngono! Alichokuwa anaambiwa na rafiki zake haikuwa kweli.<br />
Kumbuka, watu wawili wanaweza kuwa na mahusiano ya karibu sana bila ya hata kufanya ngono.<br />
Wanaweza kubadilishana uzoefu; wanaweza kujifunza mambo mengi ya muhimu kuhusu kila<br />
mmoja wao – jinsi kila mtu anavyoona maisha, jinsi watakavyofanya maamuzi pamoja, kila mmoja<br />
atakuwa mwenzi na mzazi wa namna gani na namna kila mmoja anavyoiona mipango ya maisha ya<br />
mwenzake.<br />
Yote haya ni muhimu kabla hujaanza mahusiano ya kimapenzi na mtu yeyote. Mnatakiwa kwanza<br />
muwe marafiki wa kweli. Ngono bila urafiki wa kweli wakati wote ni hatari kwa afya yako na kwa<br />
moyo wako. Unaweza kuumia. Kwa hiyo kwa ajili ya mahusiano yenye afya na afya ya ujinsia –<br />
kuweni marafiki wa kweli kwanza.<br />
MaPenZi<br />
Ni vigumu kutafsiri mapenzi kwa sababu yanahusu hasa hisia. Mapenzi ni kitu kikubwa na kuna<br />
aina mbalimbali za mapenzi. Mapenzi kwa wazazi na marafiki, mapenzi kwa rafiki wa kiume au wa<br />
kike na mapenzi kwa jamii.<br />
Vile vile mapenzi ni hisia ngumu, na watu wanaweza kueleza maana ya mapenzi kwa njia tofauti<br />
kutegemeana na uzoefu wao na mahusiano yao ya kupenda. Mapenzi ni hisia yenye utata na watu<br />
hutoa tafsiri ya mapenzi kutegemeana na uzoefu wa mahusiano ya kimapenzi.<br />
Godfrey, kutoka Zimbabwe (umri wa miaka 19)<br />
“Siwezi kuyaelezea mapenzi. Ni vizuri sana kuwa katika mapenzi.”<br />
Patrick, kutoka Ghana (umri wa miaka 16)<br />
“Mapenzi ni muungano wa watu wawili ukiwa na sanaa ya<br />
kuelewana na kuwa mwaminifu kwa kila mtu.”<br />
Sherifan, kutoka Ghana (umri wa miaka 15)<br />
“Mapenzi ni kitu ambacho kipo kati ya watu wawili. Aidha<br />
mvulana au msichana. Mapenzi ni kushirikiana katika matatizo<br />
na kujaliana”.<br />
Stabisile, kutoka Zimbabwe (umri wa miaka 19)<br />
“Kuwa na mpenzi ni mojawapo ya vitu vizuri duniani”.<br />
jennifer, kutoka Ghana (umri wa miaka 17)<br />
“Mapenzi ni wewe, familia yako na marafiki kushirikiana<br />
mawazo pamoja. Hivi ndivyo ninavyofahamu kuhusu mapenzi.”<br />
SURA YA 8 | URAfIKI NA MApENZI<br />
Kuwa na mpenzi kunaweza kuwa kama uchawi.<br />
Unakutana na mtu maalumu halafu kila kitu<br />
kinabadilika. Jua linaonekana kung’ara zaidi, nyasi<br />
zinakuwa za kijani zaidi na unajiona kama unatembea<br />
hewani.<br />
Kuwa na mpenzi ni tofauti na kumpata rafiki mpya.<br />
Unapokuwa na mpenzi, unaweza kujisikia joto, na<br />
hisia zilizojaa. Unaweza kujisikia kutabasamu kila<br />
wakati kwa sababu mawazo ya yule unayempenda<br />
yanakufanya uwe na furaha. Unataka kuwa na mtu<br />
huyu kila wakati. Unapata njozi za mchana za tamaa<br />
ya mambo yasiyowezekana kuhusu mtu huyo. Kuna<br />
wakati unaweza kupoteza hamu ya kula au kukosa<br />
usingizi usiku.<br />
Sherry, kutoka Ghana (umri wa miaka 19)<br />
“Ni jambo la ajabu. Huelewi kinachokupata. Huwezi kuelezea.<br />
Unajaribu kuacha kumfikiria lakini unagundua mawazo hayawezi<br />
kutoka. Unaweza ukawa unasoma kwa ajili ya mtihani lakini unaona<br />
akili yako haiendani na macho yanavyoangalia ukurasa wa kitabu.”<br />
Sara, kutoka uganda (umri wa miaka 18)<br />
“Nina miaka 18 na yupo mvulana ninayempenda sana. Anapokuwa<br />
mbali na mimi, ninashindwa kuwa makini na kitu chochote.<br />
Anapokuwepo karibu na mimi ninatetemeka na siwezi kufanya<br />
kitu chochote cha maana,hata kama akiniambia nijifanye kama<br />
hayupo. Hisia hizi zinanifanya nichanganikiwe kabisa.”<br />
angela, kutoka Kenya (umri wa miaka 18)<br />
“Inasisimumua kuwa katika mapenzi.Hutaki kumuumiza.Unajisikia<br />
mpya kama vile kitu kimeongezeka.Wakati mwingine kujisomea<br />
inakuwa matatizo.Akikuandikia barua ,itasomwa kwa masaa.<br />
“Penzi la kwanza” ni mojawapo ya uzoefu mzito wa maisha. Kuwa na mpenzi sio sawa na<br />
uzoefu wowote ulioupata ukiwa mtoto. Ni kitu ambacho unatakiwa kukichukulia taratibu.<br />
Usikimbilie. Tunza moyo wako na wa wale unaowapenda wachukulie kwa uangalifu.<br />
Diana, kutoka Zambia (umri wa miaka 17)<br />
“Ninafikiri kuwa mapenzi yaje kikawaida kuliko inavyotokea kwa<br />
vijana ambao wanaenda kutafuta mapenzi badala ya kuacha mapenzi<br />
yawatafute. Watu wanatakiwa kuangaliana kwa njia chanya.<br />
Mapenzi yanaweza kupatikana bila kulazimisha ili usije ukajuta<br />
baadaye.”<br />
89
90<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Kama una mapenzi ya kweli na mtu, mtaheshimiana. Hamtafanya kitu chochote kitakacho<br />
muumiza mmoja wenu. Hutamlazimisha mwenzako kufanya kitu chochote ambacho hakipendi.<br />
Utataka awe na furaha. Linganisha mapenzi yako na pointi hizi:-<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Mapenzi yanakufanya wewe na unayempenda kujisikia vizuri mwenyewe na kila mmoja wenu.<br />
Mapenzi ni uaminifu, kujaliana na ukweli.<br />
Mapenzi ni heshima na hadhi<br />
Mapenzi hayaruhusu mtu mmoja kumtumia mtu mwingine.<br />
Mapenzi hayaweki ngono mbele kabla ya urafiki na kamwe mapenzi yasiwe sababu ya<br />
kufanya ngono isiyo salama.<br />
Mapenzi ya kweli yanahusisha hisia ya kuwajibika na kujihusisha kwa watu wengine. Ni hisia<br />
inayotafuta mambo mazuri kwa ajili ya mtu mwingine. Mapenzi hayakasirishi, yana uvumilivu<br />
wala hayana maana ya kushikanashikana. Mapenzi hayana kinyongo. Watu wengine wanadhani<br />
wivu ni dalili ya mapenzi, Si kweli; wivu ni dalili ya kutojiamini na kutoamini kuwa unajali.<br />
Wivu si dalili ya mapenzi. ni dalili ya kutojiamini.<br />
Hata hivyo wakati mwingine wivu ni dalili ya matatizo makubwa zaidi. Kwa mfano, wivu ni dalili<br />
ya kuwa mtu anataka kumdhibiti mtu mwingine. Mahusiano mengi ya unyanyasaji (wanaume<br />
wanapiga wake zao au wanaume wanaobaka marafiki zao wa kike) wanaanza na tabia ya wivu,<br />
ambayo hujengeka kuwa mbaya.<br />
KuPuMbaZiKa<br />
cathy, kutoka uganda (umri wa miaka 17)<br />
“Hisia zangu haziji kwa haraka. Hii ni kwa sababu wakati wote<br />
ninataka kumjua mtu ambaye ananivutia vizuri zaidi. Ninazionyesha<br />
hisia zangu baada ya kuridhika kwamba hayupo<br />
kunitumia bali kwa mahusiano ya kweli.”<br />
Wakati mwingine inakuwa vigumu kufahamu kama mapenzi yenu ni ya kweli. Moyo unadunda na<br />
unajisikia kukosa pumzi na kizunguzungu unapomwona mvulana au msichana fulani.<br />
Unadhani lazima ni mapenzi yanakupa kiwewe! Lakini unapomfahamu mvulana au msichana<br />
huyo, hisia zinatoweka ghafla, na hujisikii kuvutiwa tena na mtu huyo. Hivyo ilikuwa<br />
kupumbazika.<br />
Kupumbazika hakuna ubaya na ni kitu cha kawaida tu. Ukweli ni kwamba vijana balehe<br />
wengi hupumbazika. Kupumbazika kunaweza kusisimua, kufurahisha na hatari isiwepo,<br />
kupumbazika hakugeuki kuwa mahusiano. Unaweza ukawa umepumbazika na mtu na<br />
usitake kuwa na mahusiano naye. Unaweza kufurahi kwa kumtamani kwa mbali. Hiyo ni<br />
sawa tu.<br />
Kuachana KiMaPenZi<br />
SURA YA 8 | URAfIKI NA MApENZI<br />
naana, kutoka Ghana (umri wa miaka 17)<br />
“Ninafahamu kwamba unapompenda mtu unafanya kile<br />
kilicho<br />
kizuri sana kwa ajili yake na kuwa na yale yote<br />
yanayompendeza moyo wake. Lakini sijawahi kumpenda mtu.<br />
Ninaweza kusema nimewahi kuwahusudu baadhi ya wavulana,<br />
lakini kamwe sijawahi kupenda.”<br />
Sio kila mapenzi hudumu daima. Hisia za kupenda zinaweza kutoweka haraka kama<br />
zinavyokuja, lakini vile vile zinaweza kuwa za kweli na zenye nguvu.<br />
Wakati mwingine, jinsi mnavyokua watu wazima wewe na rafiki yako mnaweza mkajikuta<br />
mmeachana. <strong>Ndoto</strong> zenu zinawachukua njia tofauti. Mtajikuta yale mnayopendelea<br />
yamebadilika na mnakosa cha kuzungumza. Hamcheki tena pamoja kama mlivyozoea.<br />
Sio vizuri kwa afya yako kihisia kuwa katika mahusiano wakati hakuna mapenzi.<br />
Inahuzunisha na inaweza kuwa vigumu hususani kama mmoja wapo bado ana hisia za<br />
kupenda wakati mwingine hajisikii kabisa.<br />
Iwapo unataka kuvunja mahusiano, kuwa mkweli kuhusu sababu zinazofanya kuvunja<br />
mahusiano. Vile vile kuwa na huruma na mfikirie rafiki yako. Jaribu kutomuumiza, lakini<br />
wakati huo huo maliza mahusiano hayo– usimwache aendelee kutegemea au kufikiria<br />
kwamba utabadilisha mawazo yako.<br />
Iwapo rafiki yako atakuacha, inaumiza sana. Ni vigumu kuacha kufikiria kwamba labda<br />
atabadilisha mawazo kukurudia. Inaweza kuwa vigumu kuamini kwamba hakupendi tena.<br />
Unaweza kujisikia mpweke sana na uliyekataliwa.<br />
Jipe muda wa kumudu maumivu.Usikimbilie kutafuta mahusiano mapya na mtu mwingine<br />
ili ujisikie nafuu. Hata kama utakasirika na kuumia usimlaumu mtu mwingine na kamwe<br />
usieneze uvumi au hadithi mbaya kuhusu mwenzi wako wa zamani. Hizi sio njia nzuri za<br />
kuchukua kwa mtu aliye komaa.<br />
Kupoteza marafiki na kupata marafiki wapya ni sehemu ya maisha. Hatimaye utapata<br />
mpenzi wa kweli ambaye mtaishi naye, hivyo vumilia. Kwa wakati huu lenga katika kuwa<br />
mtu mwenye huruma na anayependeka. Ukijipenda, ni rahisi kupenda watu wengine na<br />
wewe mwenyewe kupendwa.<br />
91
92<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Sura ya 8<br />
urafiki na mapenzi<br />
Urafiki mzuri na mahusiano mazuri yanakusaidia ujisikie vizuri. Marafiki wazuri<br />
wanakusaidia kutatua matatizo, kukuonyesha mawazo mapya na kushiriki na wewe<br />
katika ndoto za maisha yako ya baadaye.<br />
Wakati mwingine watu unaofikiria ni marafiki zako wanaweza kukushinikiza kufanya<br />
jambo ambalo hulitaki, kama vile kujamiiana au kula madawa ya kulevya. Hii tunaita<br />
shinikizo la kundi rika. Mtu yeyote anayekushinikiza ufanye jambo ambalo hutaki<br />
kulifanya sio rafiki mzuri. Usiruhusu mtu yeyote akakushinikiza ufanye jambo ambalo<br />
unajua ni makosa na ni hatari kwako.<br />
Marafiki wazuri wanaweza wakawa wa jinsi moja au jinsi nyingine. Wavulana na wasichana<br />
wanaweza kuwa marafiki bila ya kuwa na mahusiano ya kimapenzi. Maneno<br />
“rafiki wa kiume” au “rafiki wa kike” sio lazima yamaanishe kwamba mahusiano ni ya<br />
kimapenzi. Marafiki wa jinsi tofauti wanaweza kuwa na urafiki wa karibu na kupendana<br />
sana bila ya ngono.<br />
Inaweza ikawa vigumu kuelewana na mtu wa jinsi nyingine kwa sababu wavulana na<br />
wasichana hawana uhakika nini mwingine anataka katika mahusiano. Kumbuka, watu<br />
wengi – wavulana na wasichana – wanataka mambo yanayofanana katika mahusiano.<br />
Wanataka heshima, uaminifu, ukweli, kuelewana na kujali.<br />
Kama unamtaka msichana au mvulana unayempenda, jaribu kuvuta subira na kuwa<br />
mkweli. Kuwa mwema. Toka, nenda ukamwone. Kama anaelekea kupenda nia yako,<br />
mwombe kama mnaweza kwenda kushiriki shughuli fulani kwa pamoja.<br />
Kujenga mahusiano mazuri kunachukua muda na uvumilivu. Ngono sio njia nzuri ya<br />
kujenga mahusiano. Ukweli ni kwamba ngono inaweza kuharibu mahusiano. Kujamiiana<br />
haina maana ya kwamba watu wawili wanapendana au urafiki wao ni wa karibu sana.<br />
Ngono bila urafiki wa kweli ni hatari kwa afya yako na moyo wako.<br />
Kumpenda mtu ni jambo nzuri sana, mapenzi yanakufanya ujisikie vizuri mwenyewe na<br />
mtu mwingine. Furahia hisia lakini usikimbilie jambo lolote. Kumbuka mapenzi yanahusu<br />
heshima na kujaliana. Mapenzi hata siku moja yasiwe sababu ya kufanya jambo<br />
ambalo litaweka afya na maisha yako ya baadaye hatarini. Mapenzi hayawezi kuwa<br />
kisingizio cha kufanya ngono isiyo salama.<br />
Mahusiano hayadumu milele. Kama ukiachwa, sio vizuri kulazimisha mahusiano. Kuwa<br />
mkweli kwa rafiki yako, lakini kuwa na huruma na umfikirie pia. Jaribu usiumize hisia<br />
zake.<br />
Kama mtu amekuacha, unaweza kuhuzunika sana na kujisikia mpweke. Lakini usikate<br />
tamaa. Siku moja utampata mtu mwingine sahihi wa kumpenda. Jipe muda wa kustahimili<br />
ulichopoteza. Usikimbilie mahusiano mapya na usieneze uzishi kuhusu mtu huyo.<br />
Ujinsia Na Ngono<br />
Kuna utata mwingi sana kuhusu neno ujinsia (sexuality) na kujamiiana. Watu wengi wanafikiri<br />
ujinsia maana yake ni kujamiiana. Wengine wanafikiri kwamba huwezi kuwa binadamu hai<br />
mwenye ujinsia na mwenye hisia za kimapenzi hadi uanze kujamiiana.<br />
Imani hizi si za kweli; kila mtu anao ujinsia tangu<br />
kuzaliwa hadi kufa.<br />
Kuwa na ujinsia kunaweza kumaanisha:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Kujisikia unavutia na mwili wako<br />
umejengeka vizuri.<br />
Kujisikia mwenye hisia za kuwa karibu na<br />
mtu fulani.<br />
Kufurahia kuguswa na kukumbatiwa.<br />
Kujishika mwili wako mwenyewe.<br />
Kuvutiwa na mtu mwingine.<br />
Kufikiria hadithi za kimapenzi akilini<br />
mwako.<br />
Kuwa na mawazo au hisia za kimapenzi.<br />
Wakati wa ujana balehe ndio muda ambao<br />
unaweza kuutambua zaidi ujinsia wako -<br />
unavyojisikia, unavyofikiri, unavyojiheshimu<br />
kama mvulana au msichana, na unachokitaka<br />
kuhusu uhusiano wa karibu au pendo la mtu.<br />
Ulipokuwa mdogo pengine hukufikiria kuhusu<br />
mambo haya lakini wakati wa ujana, unaweza<br />
kuanza kufahamu maana ya kuwa mwanaume<br />
au mwanamke. Pia unaweza kuanza kuvutiwa<br />
na watu wengine na kuanza kuona hisia za<br />
kimapenzi, matamanio na ndoto.<br />
UNAJUA maana ya “Ujinsia”?<br />
Ujinsia ni suala lenye utata kueleweka. Ni<br />
zaidi ya kujisikia hisia za kimapenzi au<br />
kujamiiana. Ujinsia ni pamoja na:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Kufahamu na kuwa na hisia kuhusiana<br />
na mwili wako na miili ya watu wengine.<br />
Uwezo wako na nia ya kuwa karibu na<br />
mtu mwingine.<br />
Uelewa wako kuhusu nini maana ya<br />
kuwa mwanamke au mwanaume.<br />
Hisia za mvutano wa kijinsia na watu<br />
wengine.<br />
Uwezo wako kimwili wa kuzaa.<br />
Ujinsia ni muhimu, unafurahisha, na ni<br />
sehemu ya asili ya kuwa mtu. Lakini wakati<br />
mwingine watu wanatumia ujinsia wao<br />
katika namna isiyofaa kwa kushawishi,<br />
kuamuru au kutania watu wengine. Hii ni<br />
pamoja na kuonyesha mapenzi kwa mzaha,<br />
upotoshaji na unyanyasaji kijinsia kama<br />
kubaka/kunajisi n.k. Usitumie ujinsia kama<br />
kifaa cha kupata kitu au kunyanyasa au<br />
kumuumiza mwingine.<br />
93<br />
SURA YA 9
94<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Haya ni mabadiliko ya kufurahisha, lakini yanaweza vile vile kukupoteza – hasa kwa kuwa kuna<br />
miiko mingi kuhusu ujinsia na jinsia. Kwa mfano, watu wengine wanafikiri kwamba kuwa na hisia<br />
ya mapenzi ni dalili kwamba lazima wajamiiane, lakini hii si kweli kwani hisia za kimapenzi ni<br />
sehemu ya kuwa binadamu. Kila mtu anahisia za kimapenzi.<br />
Sura hii inahusu ujinsia na jinsi watu wanavyoonyesha hisia za kijinsia. Kuna mambo mengi<br />
unahitaji kuyajua ili uweze kufanya maamuzi mazuri kuhusu ujinsia na ngono/kujamiiana.<br />
ujinSia WenYe aFYa njeMa<br />
Kuwa mtu mwenye afya njema kijinsia inamaanisha kuwa na uwezo wa kuonyesha hisia zako<br />
katika njia ambazo hazikuhatarishii wewe au mtu mwingine. Yaani huhatarishi hisia na afya yako<br />
na wala huhatarishi hisia za watu wengine na afya zao.<br />
Kama kijana balehe, unaweza kuanza kulifanyia kazi jambo la kuwa kijana mwenye afya njema ya<br />
kijinsia. Unaweza kuhakikisha unajibidiisha kujua kadri iwezekanavyo tofauti kati ya ukweli na<br />
uongo inapokuja kwenye suala la ngono/kujamiiana. Pata muda wa kujifunza kuhusu mwili wako,<br />
hisia zako na namna ya kuwa salama na mwenye afya kijinsia.<br />
Cha muhimu zaidi, pata muda wa kufikiria chaguo lako linaloendana na vitendo vya jinsia yako.<br />
Chaguo lako mojawapo linaweza kuwa “hakuna ngono” au “muda bado”. Unaweza kusubiri kabla ya<br />
hujakimbilia kujamiiana. Unaweza kuhakikisha unaelewa matokeo ya kufanya ngono isiyo salama<br />
na namna ya kujikinga.<br />
Mara nyingine inaweza ikawa vigumu kuwa na afya njema kijinsia. Hakuna mtu<br />
atakayekufundisha kuhusu afya njema, iwe shuleni au nyumbani.<br />
Njia kuu ya kupata habari ni kupitia kwa marafiki, kaka na dada zako, video, miziki, na magazeti.<br />
Hata hivyo njia hizi zinaweza kukuchanganya na kukupoteza.<br />
Magazeti, muziki, vitabu vya hadithi na matangazo yanatoa taarifa<br />
zinazo changanya kuhusu ngono.<br />
SURA YA 9 | UJINSIA NA NGONO<br />
Baadhi ya video nyingine na riwaya za mapenzi, ngono inakuwa kama jambo la kuvutia na halina<br />
matatizo. Ngono inakuwa kama kitu tu kinachotokea na hakuna mazungumzo kati ya watu<br />
wawili kama wanahitaji kufanya mapenzi au la, na watumie kondomu au wasitumie. Hata kama<br />
hawatumii kondomu, watu katika video na riwaya hawaonyeshi iwapo wanapata matatizo ya<br />
kupata mimba zisizohitajika au kupata magonjwa ya zinaa kama VVU/UKIMWI.<br />
Katika muziki, wanaume na wanawake wanaimba kama waliopoteza matumaini na hawajali<br />
kuhusu ngono. Wanaonekana kutojali kuhusu VVU au matatizo mengine. Wanachotaka ni<br />
mapenzi. “Mawazo yangu yananiambia “hapana” lakini mwili unaniambia “ndiyo” unaendelea<br />
wimbo fulani wa rapu. Mwingine unasema: “sijui umenifanya nini hadi ikanisababishia kupenda<br />
kama mwenda wazimu”.<br />
Muziki ni mzuri, unagusa hisia za ndani ya moyo kabisa.Video na riwaya vinaweza kukufanya<br />
uasi maisha yako ya kila siku, lakini havikusaidii ushughulikie mahusiano yako. Havikusaidii<br />
ujue kuzungumza na msichana au mvulana wako kuhusu iwapo mfanye au msifanye ngono. Na ni<br />
ukweli havikusaidii kukuwezesha uzungumze na mwenzi wako kuhusu kutumia kondomu.<br />
Hata mtu unayemfahamu anaweza akakuchanganya kuhusiana na jinsia na ujinsia. Wazazi wengi<br />
hawapendi kuzungumzia maswala ya ngono na watoto wao, hivyo inaweza kuwa vigumu kujifunza<br />
kutoka kwao.<br />
Gifty, kutoka Ghana (umri wa miaka 14)<br />
“Kwa nini wazazi wetu wanaona vigumu kutufundisha mambo ya<br />
ngono? Au ni kwa sababu wanafikiri tutajaribisha au vipi?”<br />
Vijana wengi na marafiki, wanaweza kusema kuwa wameshawahi kufanya ngono hata kama<br />
hawajawahi. Unaweza kuanza kufikiria na wewe ukafanye ngono ili ulingane nao. Wenzako<br />
wanaweza pia wakazua kwamba unahitaji ngono ili upone maumivu ya hedhi au kufanya uume<br />
uwe mkubwa na wenye nguvu. Lakini mambo haya si kweli. Kujamiiana hakuwezi kukuponya<br />
maumivu ya hedhi, na wala hakuwezi kufanya uume uwe mkubwa.<br />
Kwa nyie wavulana, kaka na wajomba zenu wanaweza kuwa walichukua hatua za hatari kuhusiana<br />
na mapenzi ambazo wanazijutia hivi sasa. Cha kushangaza ni kwamba wanawashawishi muanze<br />
ngono kuhakikisha kwamba nyie ni wanaume.<br />
Kwa nyie wasichana, hakuna ambaye amewahi kukusifia huko nyuma, lakini sasa wavulana<br />
wanakuambia wewe ni mzuri, na hii inakufanya ujisikie vizuri. Je, kwa hilo tu unatakiwa uonyeshe<br />
mapenzi kwao na kuwapa matumaini?<br />
Inaweza ikawa vigumu kwako kuona la maana kuhusu maelezo unayopata kuhusu ngono. Hata<br />
hivyo, jambo muhimu kuhusu afya njema ya ujinsia ni kuonyesha tofauti kati ya tabia yenye<br />
mapenzi yenye afya na njia ambazo zina madhara kwako na kwa wengine. Kabla hujachukua<br />
hatua katika hisia zako za kijinsia fikiria matokeo ya hatua za matendo yako. Je wewe au yeyote<br />
yule atakuwa hatarini kupata mimba isiyotakiwa, VVU/UKIMWI au magonjwa ya ngono? Je,<br />
kutenda kutokana na hisia kutasababisha matatizo, kama vile kutoelewana? au kutoeleweka<br />
kimawasiliano katika mahusiano? Je, itasababisha mimi au mwenzi wangu kujisikia vibaya? Je,<br />
hisia za mtu yeyote zitaathirika?Kuwa mwenye afya kijinsia kunamaanisha kupata muda wa<br />
kufikiri kuhusu jambo kabla ya kulifanya ili kufurahisha hisia zako za kijinsia.<br />
95
96<br />
hiSia Za KijinSia<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Mambo mengi utayagundua punde utakapoanza kusikia ashiki au kusisimuka kijinsia. Utayahisi<br />
mwili mzima. Kwa wanaume, dalili ya hisia ya kijinsia ni uume kusimama. Kwa wasichana, ni<br />
unyevunyevu ukeni. Hii inatokea kwa sababu damu ya ziada kutoka kwenye mishipa ya damu<br />
inaingia kwenye spongi maalum kwenye tishu ndani ya uke au uume. Kwa wavulana tishu<br />
za spongi zinavimba na kusababisha uume kuwa mrefu, mgumu, mpana na kusimama. Kwa<br />
wasichana, tishu za spongi zinavimba ndani ya kuta za uke na kusababisha utoaji wa majimaji,<br />
ambayo yanalainisha eneo la uchi na kusabisha lilowane.<br />
Unaweza kujisikia hisia za kijinsi zenye kusisimua kwa kusoma riwaya za kimapenzi au kumfikiria<br />
mvulana au msichana unayempenda. Kama ulikuwa na mvulana au msichana na mlikuwa<br />
mnashikanashikana, unaweza kusisimuka zaidi.<br />
Utafanya nini kuhusu hisia za kijinsi? Jambo la kwanza, huhitaji kufanya ngono unapopata hisia za<br />
kijinsi. Kujamiiana ni njia moja wapo ya namna watu wanavyoonyesha hisia za kimapenzi. Lakini<br />
zipo njia nyingi ambazo watu wanaweza kuonyesha hisia zao za kimapenzi - katika mazungumzo,<br />
kushikana mikono, kukumbatiana, kupakatana, kubusiana na kushikanashikana.<br />
Njia hizi za kuonyesha mapenzi zinaweza kuwa za kuridhisha na zina hatari ndogo sana<br />
ya kuambukizwa VVU (soma sura ya 10 zaidi juu ya VVU na magonjwa ya zinaa). Kupumua<br />
na mapigo ya moyo yanaweza kuongezeka. Mwili mzima unaweza ukajisikia kusisimuka na<br />
kuchangamka. Unaweza kuwa na hali hiyo ya kusisimua kwa masaa mengi. Huhitaji kwenda zaidi<br />
ya hapo. Mvulana hahitaji kumwambia msichana kuwa anahitaji kujamiiana nae eti kwa kuwa<br />
amesimamisha. Si kweli. Uume wako utaacha kusimama pindi utakapoacha kumpakata msichana.<br />
Ni muhimu kujua kwamba, si migusano yote inaleta hisia za kufanya ngono. Kama unasukumwa<br />
bila kupenda ili ufanye ngono, hutajisikia vizuri. Msisimko wa kijinsia unatokea watu<br />
wanapokuwa na furaha na wamepumzika (soma sura 12 zaidi juu ya unyanyasaji kijinsia na<br />
vitendo vya ngono visivyotakiwa).<br />
PunYetO<br />
Punyeto ni kitendo cha mtu kushika sehemu zake za siri – uume, uke, matiti au sehemu nyingine<br />
za mwili ambazo zinasisimka kijinsia. Punyeto ni mojawapo ya njia ambayo watu wanaelezea<br />
hisia zao za kijinsia.<br />
Wanaume kwa wanawake wanaweza kupunguza hisia za kutaka kujamiiana na bado wakapata<br />
starehe kwa kupiga punyeto. Kwa kweli watu wengi wanapiga punyeto kipindi fulani katika<br />
maisha yao. Wavulana wanapiga punyeto mara kwa mara kuliko wasichana. Wasichana na<br />
wavulana wengine wanaanza kupiga punyeto wakati bado watoto na wanaendelea kufanya hivyo<br />
maisha yao yote. Wengine wanaanza wanapobalehe; wengine wanaanza wakiwa watu wazima.<br />
Baadhi ya watu hawapigi punyeto, na wengine wanafikiria kuwa starehe ya ngono na kupiga<br />
punyeto ni kinyume na madhehebu yao au imani na utu wao.<br />
Katika mila nyingine, kuna uzushi mwingi<br />
ambao umekusudiwa kuwakatisha tamaa<br />
watu wasipige punyeto. Haya ni baadhi ya<br />
mambo yasiyo ya kweli kuhusu punyeto,<br />
kwamba:-<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Kupiga punyeto kunafanya upate kichaa.<br />
Kupiga punyeto kunafanya uote nywele<br />
kwenye kiganja cha mkono wako;<br />
kunasababisha vipele usoni au kupofuka<br />
macho.<br />
Punyeto linafanya upauke rangi ya mwili<br />
na inasabisha utumie mbegu zote za<br />
kiume.<br />
Punyeto linasababisha mtu awe dhaifu<br />
na kufanya mwanaume ashindwe kupata<br />
watoto.<br />
Punyeto linafanya uwe na majivuno na<br />
uwe mbinafsi.<br />
Hakuna ukweli kuhusu uzushi huu. Kutokana<br />
na utalaam wa kitabibu na kisayansi, punyeto<br />
linachukuliwa kama sehemu ya makuzi.<br />
Haijalishi kama utapiga punyeto au hupigi.<br />
Hakuna ushahidi wa kisayansi unaoonyesha<br />
kwamba punyeto ina athari mbaya kimwili<br />
ama kisaikolojia.<br />
Punyeto linaweza kuwa na matatizo iwapo<br />
tu:-<br />
•<br />
•<br />
SURA YA 9 | UJINSIA NA NGONO<br />
Limezidi mno – mtu hawezi kufanya kazi<br />
za kutwa mpaka apige punyeto.<br />
Linafanywa maeneo ya watu wote mahali<br />
ambapo watu wengine wanaweza kuona.<br />
UNAFAHAMU maana ya kilele?<br />
Kama ashiki na msisimko vitazidi<br />
kuongezeka, utakuwa unaelekea “kilele”.<br />
Kwa mvulana kuutambua kilele misuli yako<br />
ghafla inabana na kufanya sehemu zote<br />
za uume wako kusukuma mbegu za kiume<br />
nje ya uume. Kwa msichana misuli ya ndani<br />
na inayozunguka uke, mlango wa tumbo<br />
la uzazi na kisimi vinabana. Mara nyingine<br />
majimaji kidogo yanaweza kutoka, lakini<br />
hakojoi kama ilivyo kwa wavulana.<br />
Kilele ni kama kupiga chafya, hisia ya<br />
kukakamaa kwa misuli ikifuatiwa na<br />
kulegea. Kwa watu wengi ni muda mfupi<br />
tu kilele kinadumu kwa sekunde 10, lakini<br />
ni muda ambao unajisikia vizuri na raha na<br />
watu wengi wangependa kukionja.<br />
Kwa wasichana wengi, inawachukua muda<br />
kufikia kilele. Inahitajika kujua wapi na<br />
namna gani washikwe.Na wanahitaji wawe<br />
wanafurahia na kutuliza akili.<br />
Wavulana na wasichana, wote wanaweza<br />
kufikia kilele kwa kupiga punyeto. Hivi ni<br />
vizuri.Uko pekee yako, unaugundua mwili<br />
wako, na majimaji yanayotoka wakati mwili<br />
umesisimkwa hayatampa mtu yoyote<br />
mimba wala uambukizo.<br />
Unapofikia upeo wa raha ya kujamiiana<br />
kwa kushikana na kupakatana, ina ugumu<br />
kidogo. Kweli mko wawili na maji maji<br />
yanayotoka wakati wa kushikana yanaweza<br />
kuwa na VVU au magonjwa ya ngono. (soma<br />
sura ya 10 kuhusu magonjwa ya zinaa na<br />
VVU).<br />
Wataalam wa ujinsia wa binadamu wanaamini<br />
kwamba punyeto ni njia ya kawaida ya watu<br />
kufurahia na kuelezea ujinsia wao bila ya<br />
kujihatarisha katika mimba au magonjwa ya ngono, yakiwemo VVU/UKIMWI. Hakuna tatizo<br />
litakalo tokea mwilini mwako hata kama ukipiga punyeto sana. Kitu pekee kinachoweza kutokea<br />
ni viungo vya uzazi kuvimba kwa sababu ya kuvisugua mno.<br />
97
98<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
KuVutiWa na Mtu Wa jinSi KaMa YaKO<br />
Wakati wa kubalehe ndio wakati watu wengi wanapata kuelewa zaidi mwelekeo wao kijinsi.<br />
Mwelekeo wa kijinsi unahusu mtu ana hisia za kimapenzi na anavutiwa kimapenzi kwa nani.<br />
Watu wengi wanavutiwa kimapenzi na watu wa jinsi tofauti (kama mwanaume anavutiwa na<br />
mwanamke na mwanamke anavutiwa na mwanaume).<br />
Watu wengine wanajisikia kuvutiwa kimapenzi na watu wa jinsi sawa. Wanaume wengine<br />
wanavutiwa na wanaume wenzao na wanawake wengine kuvutiwa na wanawake wenzao. Huku<br />
kuvutiwa na jinsia sawa kunaitwa “ubasha” au “usenge” au “ushoga”.<br />
Nyakati fulani katika maisha yao, baadhi ya watu wanakuwa na hisia za kimapenzi, mawazo,<br />
ndoto na mvuto kwa mtu fulani wa jinsi moja. Marafiki wawili waliokaribu (pengine wavulana<br />
wawili au wasichana wawili) wanaweza kupendana – wanapenda kuwa pamoja na wakati<br />
mwingine wanajisikia kutamaniana kimwili. Watu wengine wanaona hisia hizi zinawachanganya<br />
na kuwafadhaisha. Hisia hizi ni za kawaida, na baadhi ya watu wanazipata hisia hizi wakati fulani<br />
katika kipindi cha maisha yao.<br />
Japokuwa baadhi ya watu wanavutiwa na watu wa jinsi sawa, madhehebu mengine ya dini na mila<br />
zingine zinafikiria ubasha ni jambo baya, si la kawaida na ni tabia ambayo inaweza kurekebishwa.<br />
Watalaam wengi wanafikiria kwamba mwelekeo wa kimapenzi wa jinsi moja si jambo ambalo<br />
wanaweza kulidhibiti kama isivyowezekana kudhibiti rangi ya ngozi au nywele zilivyo. Kwa<br />
maneno mengine ubasha / usenge sio chaguo la makusudi ambalo mtu anachagua, hivyo<br />
haiwezekani kulibadilisha aidha kwa kuswali, kwa utashi au kwa kufanya ngono na mtu wa jinsia<br />
tofauti.<br />
Katika kipindi cha balehe, watu wengine wanajikuta ni mabasha/wasenge. Kujitambua kunaweza<br />
kuwa kugumu. Unaweza kujiona uko tofauti kuliko mtu yeyote anayekuzunguka, na unaweza<br />
kujisikia mpweke mno. Kama unajisikia kitu kama hiki, jaribu kuonana na mtu ili uzungumze naye,<br />
kama mshauri nasaha wa vijana, mhudumu wa afya, mwalimu unayemwamini, au jamaa yako<br />
mkubwa – yeyote atakayeweza kukusaidia kujibu maswali yako na kupunguza hofu yako atakuwa<br />
amekusaidia.<br />
ubiKiRa<br />
Bikira ni mtu ambaye hajawahi kujamiiana. Kila mvulana na msichana amezaliwa bikira. Ubikira<br />
ni kinga nzuri dhidi ya VVU na magonjwa ya zinaa. Siku hizi wavulana na wasichana wengi<br />
wanaamua kubakia bikira hadi siku ya kuoa/kuolewa.<br />
Ruvimbo kutoka Zimbabwe (umri wa miaka 13)<br />
“Nitataka kutunza ubikira wangu. Sitafanya mapenzi na yeyote<br />
hata kwa kutumia kinga. Rafiki yangu wa kiume ni mtulivu<br />
na ndio maana ni mtu wangu.”<br />
Stabile, kutoka Zimbabwe (umri; miaka 19)<br />
“Bado mimi ni bikira. Bila shaka imani yangu kubwa ya dini<br />
inanisaidia katika suala hili.”<br />
SURA YA 9 | UJINSIA NA NGONO<br />
Susan, umri wa miaka 18 kutoka uganda<br />
“Ubikira ulifanya nionekane mwenye heshima. Wasichana wanatakiwa<br />
kutunza ubikira wao mpaka wanapoona wamepata watu wa kuwafaa.<br />
Ngono ni jambo unaloweza kuahirisha. Yakwepe mazingira yaliyo<br />
kinyume na kanuni ulizojiwekea na utaweza ukadumisha dhamira yako.”<br />
Watu wengi wanachanganyikiwa na kitu kinachosababisha wasichana wapoteze ubikira.<br />
Wanafikiri ubikira wa msichana unadhihirishwa na kizinda, ambacho ni tishu nyembamba ndani ya<br />
mlango wa uke. Kizinda kina shimo dogo na hakizibi kabisa uke kwa sababu damu ya hedhi lazima<br />
itoke kila mwezi. Wasichana wengine hawana kizinda kabisa. Pengine ni kwa vile hawakuzaliwa<br />
nacho au kilinyumbuka na kuchanika kabisa wakati wa michezo.<br />
Wasichana walio na tishu ya kizinda mara nyingine wanatoka damu wanapopoteza ubikira wao.<br />
Wasichana ambao wana tishu ndogo ya kizinda au hawana tishu ya kizinda wanaweza wasivuje<br />
damu watakapojamiiana. Kwa mara ya kwanza hii inawachanganya watu. Watu wanasema:<br />
“Hakuna damu, kwa hiyo hakuwa bikira”. Lakini anaweza kuwa alikuwa, hajawahi kufanya ngono<br />
hapo awali hivyo alikuwa bikira. Ubikira unapotea kwa kujamiiana. Hauwezi kupotea kutokana na<br />
michezo, kwa kutumia visodo, kupiga punyeto au shughuli yoyote ile. Japo ni kweli mambo haya<br />
yanaweza kurefusha au kuchana kizinda, hii haimaanishi msichana sio bikira. Watu wanaofikiria<br />
kuwa kizinda ndio usahihi wa kuwepo bikira wanakosea.<br />
UNAJUA ukweli kuhusu ubikira?<br />
Kuna uzushi mwingi kuhusu ubikira:<br />
1. Nimesikia kwamba msichana anaweza kupoteza ubikira kwa kucheza michezo. Je, hii<br />
ni kweli? Si kweli! Ubikira anaweza kupotea tu kwa kufanya ngono, kucheza michezo ni<br />
kuzuri kwa wasichana na haiwezi kumsababishia kupoteza ubikira.<br />
2. Kuna mitishamba mingine inaweza kurejesha ubikira? Hapana, hakuna mitishamba<br />
inayoweza kurejesha ubikira. Ukipotea, umepotea milele.<br />
3. Rafiki yangu anasema nikibaki bikira kwa muda mrefu, naweza kuugua magonjwa na<br />
mambo yasiyo ya kawaida? Siyo kweli! Unaweza kubakia na ubikira maisha yako yote<br />
bila matatizo yoyote mabaya.<br />
4. Ni kweli kwamba msichana akiwa bikira kwa muda mrefu sana, kizinda chake kitakuwa<br />
kigumu na atapata matatizo ya kufanya ngono? Huu ni upuuzi! Kizinda ni kipande<br />
kidogo na chembamba cha tishu. Hakiwi kigumu kadri unavyokua na wala unaposubiri<br />
kujamiianahudhuriki kamwe.<br />
5. Unawaweza kuwatambua bikira kwa kuwaangalia usoni? Si kweli! Huweza kumtambua<br />
bikira kwa kumwangalia kwa macho. Ni bikira peke yake anayejua hali yake.<br />
6. Baada ya kupoteza ubikira wako, unatakiwa uendelee na ngono. Si kweli. Unaweza<br />
kuacha kufanya ngono ukipenda.<br />
7. Nimesikia kwamba si vema kutumia kondomu ukiwa unajamiiana na msichana ambaye<br />
ni bikira kwa sababu unahitaji kutumia nguvu sana kuvunja ubikira wa msichana<br />
– kiasi kwamba utachana kondomu. Je huu ni ukweli? Hapana! Mvulana na msichana<br />
ambao ni bikira wanaweza kutumia kondomu bila matatizo. Kizinda ni tishu laini sana<br />
inayochanika kwa urahisi mno.<br />
99
100<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Kama walivyo wasichana, wavulana wanaweza kupoteza ubikira wao kwa kujamiiana. Watu<br />
wengine wanafikiri sio muhimu kwa wavulana kuwa bikira kama ilivyo kwa wasichana.Zaidi, video<br />
nyingi unazozitazama na riwaya nyingi unazosoma zinafanya ionekane muhimu kwa wanaume<br />
kuwa na uzoefu zaidi wa ngono. Mara nyingine inaonekana kana kwamba ili uonekane mwanaume<br />
lijali lazima ufanye ngono. Lakini kufanya ngono hakukufanyi uwe mwanaume zaidi. Kwa mvulana<br />
au msichana kutunza ubikira wako ni vizuri. Ni njia nzuri sana kwa kinga ya kweli dhidi ya VVU, na<br />
magonjwa ya ngono na mimba zisizotakiwa.<br />
KuPOteZa ubiKiRa<br />
Uwe mvulana au msichana, unapaswa wewe mwenyewe kuamua wakati gani upoteze ubikira<br />
wako. Usije kuwaruhusu watu wengine kukuamulia au kukushinikiza uupoteze. Chagua muda<br />
wako. Na chagua mtu anayefaa. Subiri hadi unakuwa na uhakika kwamba unaweza kujizuia dhidi<br />
ya magonjwa ya ngono, pamoja na VVU/UKIMWI na mimba zisizotakiwa.<br />
adam, kutoka uganda (umri wa miaka 13)<br />
“Nafikiri muda mzuri wa kuanza kujamiiana ni wakati nikiwa na umri wa<br />
miaka 20. Nitamaliza masomo yangu na pengine kufanya kazi.Hata kama<br />
muda huo ukifika nitatumia kondomu”.<br />
Mfune, kutoka Zambia (umri wa miaka 13)<br />
“Nitasubiri hadi nioe au nipate fedha za kunisaidia kwa sababu msichana<br />
ukipata mimba nitahitaji fedha za kulelea mtoto”.<br />
Mara nyingine wenzako wanaweza kukulazimisha kufanya ngono.<br />
Douglas, kutoka Zambia (umri wa miaka 12)<br />
“Vijana wengine wakubwa kwetu au waliojaliwa kuwa<br />
na miili mikubwa wanatucheka na kutuambia sisi ni bikira”.<br />
andrew, kutoka tanzania (umri wa miaka 17)<br />
“Rafiki yangu wa kiume ananicheka na kunisihi niwe na rafiki wa kike.<br />
Wanasema utaishije bila rafiki wa kike wewe sio mwanaume”.<br />
Mildred, kutoka uganda (umri wa miaka 17)<br />
“Wakati fulani, unajisikia umeachwa na marafiki zako wakianza<br />
kuzungumzia masuala ya ngono. Unaweza tu kuingilia mazungumzo yao<br />
kutokana na ulichosoma kwenye kitabu cha hadithi au ulichoona kwenye<br />
sinema. Kama huna mwelekeo mzuri unaweza ukadanganywa. Nimechagua<br />
kubakia bikira mpaka nimpate mwanaume mzuri wa kunifaa.”<br />
lois, kutoka tanzania (umri wa miaka 13)<br />
“Nazungumza na marafiki zangu kuhusu kufanya ngono. Wapo baadhi ya<br />
wasichana na wavulana wanaosema kwamba ukikataa kufanya ngono<br />
unafanana na mtu ambaye hakusoma”.<br />
Vijana balehe wengi siku hizi wanaelewa kwamba kufanya ngono ni uamuzi wao wenyewe na<br />
kwamba asiwepo mtu wa kuwalazimisha kufanya ngono.<br />
Patrick, kutoka uganda (umri wa miaka 17)<br />
“Marafiki zangu wote wanafanya ngono<br />
na marafiki zao wa kike, na kidogo tu<br />
niwafuate kutokana na kulazimishwa na<br />
marafiki zangu. Lakini niligundua kwamba<br />
sikuwa na uhakika na nilichanganyikiwa.<br />
Isitoshe ninataka kufanya mambo yangu<br />
mwenyewe. Nitasubiri.”<br />
lois, kutoka tanzania (umri wa miaka 13 )<br />
“Hakuna atakayenilazimisha kufanya<br />
ngono. Nitaamua mwenyewe”<br />
Milensu, kutoka Zambia (umri wa miaka<br />
13)<br />
“Sitafanya ngono kwa sababu itabidi nisubiri hadi niolewe nitakapokuwa tayari kwa<br />
matokeo ya kufanya ngono. Sitarajii rafiki zangu kunishinikiza nifanye ngono. Uamuzi ni<br />
wangu.”<br />
andrew, kutoka tanzania (umri wa miaka 17)<br />
“Kama nitataka kufanya ngono utakuwa ni utayari wangu mwenyewe. Rafiki zangu<br />
hawatanishawishi kufanya hivyo.”<br />
KujaMiiana<br />
Kujamiiana ni wakati mwanaume na mwanamke wana ileta miili yao karibu na mwanaume<br />
anasimamisha uume na unaingia ukeni kwa mwanamke.<br />
Kwa nini watu wanajamiiana? Kuna sababu nyingi – nzuri na mbaya. Zifuatazo ni baadhi ya<br />
sababu:<br />
•<br />
•<br />
SURA YA 9 | UJINSIA NA NGONO<br />
Simama imara dhidi ya shinikizo la kundi<br />
rika. usifanye mapenzi eti kwa sababu rafiki<br />
zako wanafikiri unatakiwa kufanya.<br />
Upendo na mapenzi ya dhati. Kwa watu wawili walio karibu sana, kujamiiana kunaweza kuleta<br />
mapenzi ya dhati na yenye upendo. Hata hivyo watu wengine wanafanya ngono kwa sababu<br />
wanafikiri itawaletea kupendana na mapenzi ya dhati kwenye uhusiano wao. Wanafikiri<br />
kujamiiana kutathibitisha mapenzi kati yao. Hii mara nyingi haisaidii. Mapenzi ya dhati<br />
yanakuja kwa kuzungumza mambo ya uaminifu na kushirikiana katika hisia. Ngono haiwezi<br />
kuwaunganisha watu pamoja kama hawakuwa karibu kabla. Kufanya ngono hakumaanishi<br />
watu wanapendana.<br />
Kuridhisha hamu ya mapenzi na mahitaji ya kimwili. Watu wengine wanafikiri kwamba<br />
unahitaji kujamiiana ili kukidhi hisia za kufanya mapenzi – kama unavyohitaji kunywa<br />
unaposikia kiu. Lakini kujamiiana hakuko hivyo. Ukweli wakati mwingine kujamiiana<br />
hakuridhishi kuliko kushikana mikono, kukumbatiana, kubusu, kama watu wawili hawana<br />
mahusiano ya karibu, kufanya ngono kunaweza kusiwaridhishe.<br />
101
102<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Kujaribu kumhodhi mvulana au msichana. Watu wengi wanafanya ngono kwa sababu<br />
wanaogopa kupoteza mahusianao iwapo hawatafanya ngono. Hii ni sababu moja<br />
mbaya ya kufanya ngono. Yeyote atakayekuacha kwa sababu eti hutaki kujamiiana,<br />
hakupendi (soma sura ya 12 kwa maelezo mengi kuhusu hili).<br />
Zawadi: Watu wengine wanafanya ngono kwa ajili ya kupata zawadi, fedha au<br />
upendeleo kama kupata alama nzuri shuleni. Hili linaweza kuwa tatizo gumu, kwa<br />
mfano kama mshirika wako ndiye anayekulipia ada ya shule. Lakini hizi ni sababu zisizo<br />
sahihi za kufanya ngono. Hazitakufanya ujisikie vizuri. Usitumie mwili wako kupata<br />
chochote kutoka kwa mtu yeyote hata kingekuwa kitu gani – fedha au zawadi au<br />
huduma za kipekee – huwezi kuvilinganisha na mwili wako.<br />
Kujisikia umekua. Wengi wanakimbilia kufanya ngono kwa kufikiri itawafanya wajione<br />
wamekua. Lakini kufanya ngono kwa kweli hakubadilishi chochote kuhusu ukuaji wako.<br />
Ngono haitakufanya ukomae na wala haitakufanya uwe mtu mzima.<br />
Kulingana nao au kuwafurahisha wenzio. Watu wengi wanahisi kana kwamba watu wote<br />
wanaowazunguka wanafanya ngono – kana kwamba wao peke yao ndio hawafanyi<br />
ngono. Hii inaweza kuwa tishio na vijana wengine wanafanya ngono kwa sababu<br />
wanafikiri vijana wengine wanafanya hivyo.Ukweli ni kwamba watu wengi hawasemi<br />
ukweli kuhusu ngono, na watu wengi wanatunga tu hadithi kwa sababu wanataka<br />
kuwafurahisha watu wengine.<br />
Kupata mtoto. Kujamiiana ndiyo njia pekee ya kufanya mapenzi ambayo inaweza<br />
kukupatia mtoto.<br />
Watu wengi wanataka watoto wakati fulani katika maisha yao, lakini ni wachache<br />
wanaotaka kuwa na mtoto wakati wa ujana balehe (soma sura 11).<br />
Kujamiiana ndiyo njia ambayo watu wengi duniani wanapa VVU. Kama huko tayari kujikinga<br />
wewe na mwenzio kwa kutumia kondomu wakati wote hujawa tayari kujamiiana.<br />
KuWeKa KiWanGO cha KujaMiiana.<br />
Watu wengine wanafikiri ngono ina nguvu na haiwezi kuzuiliwa na kwamba inatokea<br />
kama radi au mvua. Lakini ukweli ni kwamba – kufanya ngono – ni uamuzi wa makusudi.<br />
Unapofanya ngono sio kwamba ni jambo la asili lazima litokee. Ni wewe unayefanya<br />
uamuzi. Lakini pawe na maamuzi mengi kuhusu ngono. Lini? Nani? Kwa nini? Wapi? Mara<br />
ngapi? Kwa kutumia kondomu? Bila kondomu?<br />
Ngono ni uamuzi mzito. Ni uamuzi wako! Zuia sauti zote zinazosema “kila mtu” anafanya<br />
ngono. Jibu ni kwamba si kila mtu anafanya ngono. Na wewe sio kila mtu. Ni wewe tu.<br />
Kama unafanya uamuzi wa kufanya au kutofanya ngono, fikiria kuhusu hili: Uko tayari<br />
kuvumilia mahitaji ya ngono salama – matumizi sahihi na kutumia kondomu kila mara,<br />
ushauri kuhusu VVU, kupima, na mengineyo? Vijana wengi hawako tayari kubeba wajibu<br />
wote huo; Kuwa mwaminifu kwa nafsi yako. Kama unajiona huko tayari, unaweza kusema<br />
“Hapana” subiri mpaka utakapokuwa mkubwa.<br />
SURA YA 9 | UJINSIA NA NGONO<br />
Unahitaji vile vile kumtunza mwenzi wako, na yeye vile vile anatakiwa akutunze. Kutunzana<br />
kunachukua muda. Urafiki na kuwa karibu haujengeki kwa usiku mmoja. Kama hamjawa marafiki<br />
wa kweli unaweza kuona ngono ni kitu cha aibu. Hii ni dalili tosha kwamba huyo siyo mtu<br />
anayefaa au siyo muda sahihi kwako.<br />
Kama wewe na mwenzi wako hamko tayari kwa kujamiiiana, ishia kwenye kubusiana, kushikana<br />
mikono au kukumbatiana. Weka kikomo na kubaliana nacho usifanye kitu chochote ambacho<br />
mwenzako anakiona hakifai.<br />
Unafahamu kama mahusiano yenu ni tayari kwa kujamiiana?<br />
Jibu maswali yafuatayo kiukweli kadri uwezavyo. Weka tiki kwenye jibu ulilolichagua.<br />
.1. Je, mimi na mwenzi wangu tunafahamiana vizuri<br />
Ndiyo Hapana Labda Sijui<br />
2. Je unajisikia tumeungana pamoja na kila mmoja wetu anajiona kuwa sehemu ya mwenzi katika<br />
maisha.<br />
Ndiyo Hapana Labda Sijui<br />
3. Je, kila mmoja amejikabidhi kwa mwenzie katika uhusiano wenu?<br />
Ndiyo Hapana Labda Sijui<br />
4. Je, tunaaminiana?<br />
Ndiyo Hapana Labda Sijui<br />
5. Je, tunawasiliana vizuri?<br />
Ndiyo Hapana Labda Sijui<br />
6. Je, tunaweza tukazungumza bila wasi wasi kuhusu ngono?<br />
Ndiyo Hapana Labda Sijui<br />
7. Je, tunafikiria kufanya ngono kwasababu kweli tunataka au kwa sababu tunashinikizwa kufanya<br />
ngono?<br />
Ndiyo Hapana Labda Sijui<br />
8. Je, tumezungumzia kuhusu njia gani tutatumia kuzuia mimba?<br />
Ndiyo Hapana Labda Sijui<br />
9. Je, tumezungumzia kuhusu kupima VVU kwetu wote?<br />
Ndiyo Hapana Labda Sijui<br />
10. Je, tumezungumzia namna ya kujikinga na magonjwa ya ngono pamoja na VVU/UKIMWI?<br />
Ndiyo Hapana Labda Sijui<br />
11. Je, tumekubaliana kutumia kondomu na njia za kuzuia mimba wakati wa kujamiiana?<br />
Ndiyo Hapana Labda Sijui<br />
12. Je, mwenzi wangu ataheshimu haki yangu ya kusema “ndiyo” au “hapana” kila tunapofanya<br />
ngono?<br />
Ndiyo Hapana Labda Sijui<br />
13. Je, nitaheshimu haki ya mwenzi wangu ya kusema “ndio” au “hapana” kwa kila tutakapotaka<br />
kufanya ngono?<br />
Ndiyo Hapana Labda Sijui<br />
14. Je, ushirikiano wa mahusiano ya kimapenzi yatakuwa salama na ya raha?<br />
Ndiyo Hapana Labda Sijui<br />
Kama ulijibu “hapana” “labda” au “sijui” kwa swali lolote, basi labda wewe na mwenzi wako hamko<br />
tayari kujamiiana. Ni vizuri kungoja.<br />
103
104<br />
uaMuZi Wa KutOFanYa nGOnO<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Vijana wengi wanachagua kutofanya ngono kwa sababu nzuri sana zifuatazo:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Wanaogopa kupata mimba na magonjwa ya ngono virusi vya UKIMWI na UKIMWI wenyewe<br />
na hawapendi kuhatarisha maisha yao.<br />
Bado ni wadogo mno hivyo wanajiona hawako tayari.<br />
Hawataki kuwaudhi wazazi wao.<br />
Wanaona tendo hilo ni kinyume cha maadili ya dini zao.<br />
Wako tayari kusubiri ili kushughulikia masomo yao.<br />
Wanataka kuhakikisha kuwa rafiki yake wa kiume au wa kike anampenda kikweli.<br />
Iwapo unakabiliwa na uamuzi wa kufanya ngono, kumbuka kwamba ngono inaweza kuwa na<br />
matokeo mabaya kama kuambukizwa VVU au mimba zisizotakiwa.Mambo haya yanaweza<br />
kukuharibia maisha yako milele. Unahitaji kufikiri kwa makini uamuzi wako. Kumbuka kuwa:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Kusubiri ndiyo njia nzuri na salama ya kubakia na afya.<br />
Unayo haki ya kusema “hapana” kwa ngono na kushikilia uamuzi wako.<br />
Ukiamua kusema “ndio” kwa ngono, lazima ujizoeze kufanya ngono salama ili kukwepa<br />
mimba, VVU, UKIMWI na magonjwa ya ngono. “Bila kondomu, hakuna ngono”.<br />
KuZunGuMZa na MWenZi WaKO KuhuSu nGOnO<br />
andrew, kutoka tanzania (umri wa miaka 17)<br />
“Mimi na marafiki zangu tunazungumza kuhusu ngono.<br />
Tunazungumza pia athari za ngono,kwa mfano iwapo<br />
msichana atapata mimba,tutapata matatizo makubwa,<br />
tutalazimishwa kuoa au kufukuzwa shule!”<br />
halima, kutoka Kenya (umri wa miaka 17)<br />
“Sababu nzuri sana za kuchelewa kufanya ngono ni kusubiri<br />
kupata mtu atakayefaa na kusubiri mpaka mnaoana.”<br />
Maamuzi kuhusu ngono yanahusu watu wawili na yanahitaji mawasiliano mazuri na makini. Ni<br />
jambo muhimu kumweleza wenzi wako kitu unachofanya na kitu ambacho hutaki kukifanya.<br />
Watu wengi wanajisikia vibaya na aibu kuzungumza<br />
masuala ya ngono, lakini mambo haya yanakuwa rahisi<br />
baada ya muda na kuyafanyia mazoezi. Hapa kuna<br />
baadhi ya vidokezo:<br />
•<br />
Fikiri ni kwa nini unataka au hutaki kufanya<br />
chochote: Jua sababu zako ni zipi ili uweze<br />
kuzieleza wazi kwa mwezi wako.<br />
• Fanya mazoezi kabla: Kama huna uhakika<br />
utazungumza nini kuhusu kujamiiana na rafiki<br />
yako wa kike au kiume jaribu kuzungumza na<br />
rafiki wa karibu unayemwamini au mshauri wa<br />
vijana kwanza. Waulize jinsi ya kulizungumzia<br />
suala hilo. Pata maoni ya namna ya<br />
kushughulikia hali hii.<br />
•<br />
SURA YA 9 | UJINSIA NA NGONO<br />
chagua muda mzuri na mahali muafaka:<br />
Chagua muda mzuri wa kuzungumza na rafiki<br />
yako wa kiume au wa kike, muda ambao kila<br />
mmoja wenu hana shughuli ya mambo mengine<br />
na wakati ambapo wote mnajisikia mmetulia<br />
na mmestarehe. Ni vizuri pia kuchagua sehemu nzuri. Chagua sehemu ambayo hutajali<br />
hata watu wengine wakiwasikia. Wakati huo huo chagua sehemu ambayo siyo ya kificho<br />
sana ambayo itamfanya msichana wako au mvulana wako apate wasiwasi na kupata<br />
mawazo potofu.<br />
• usingoje mpaka umepata joto la mahaba ndio uanze kuzungumzia ngono: Ni vigumu<br />
sana kuwa na mazungumzo kuhusu kujamiiana wakati mmoja au wote mnajisikia<br />
mmesisimka na katika hali ya kufanya ngono. Hakikisha mnazungumza aina gani<br />
ya mapenzi mnayataka kabla wewe na mwenzi wako kujikuta katika hali ya kuvutia<br />
kimapenzi.<br />
• Kuwa mkweli kuhusu unavyojisikia na jinsi unavyoona. Usiwatumie watu au sababu<br />
mbalimbali kama kisingizio. Kwa mfano kama hutaki kufanya ngono kwa sababu<br />
unataka kwanza kuolewa, usimwambie rafiki yako kwamba sitaki kufanya ngono kwa<br />
sababu naogopa kupata mimba au kwa sababu unaogopa kwamba mama atagundua.<br />
Ukimwambia rafiki yako wa kiume visingizio hivyo atafikiri kwamba unataka utumie<br />
kondomu au unataka uende kwake.Ili kukwepa kutoeleweka, kuwa muwazi na eleza<br />
moja kwa moja hisia zako.<br />
• Simama imara na usikubali kushinikizwa: Hata watu ambao unawaheshimu sana<br />
wanaweza kukushinikiza ufanye vitu ambavyo hutaki kuvifanya. Inaweza kuwa vigumu<br />
sana kuhimili shinikizo kwa sababu ni mtu unayempenda unataka awe na furaha.<br />
Kumbuka hata hivyo kwamba mtu anayekupenda hapaswi kufanya mambo ambayo<br />
yatakukosesha raha. Kama rafiki yako wa kiume au kike anakushinikiza pengine ni<br />
kwa sababu hawajui unajisikiaje au kwa sababu hawajali hisia zako kama ambavyo<br />
inawapasa. Simama kidete, na hakikisha wanaelewa unachokitaka.<br />
105
106<br />
• Zingatia hisia na silika yako: Kama<br />
moyoni mwako hujisikii kwamba<br />
kitu fulani hakikufai usikifanye.<br />
Ngoja mpaka utakapoona huna woga<br />
wowote, wasiwasi au vitu vinavyo<br />
kuhangaisha.<br />
•<br />
Wakati wote jiruhusu kubadilisha<br />
mawazo. Tuseme ulimwambia rafiki<br />
yako wa kiume kwamba utafanya<br />
ngono naye, lakini ukajiona huwezi kufanya.<br />
Unayo haki ya kubadili mawazo<br />
yako. Unayo sababu nzuri ya kujisikia<br />
unavyojisikia.<br />
Hata kama umewahi kufanya ngono kabla,<br />
unaweza wakati wowote kuamua kuacha.<br />
Hakuna tatizo lolote unapoamua kuacha.<br />
Huna haja ya kutoa sababu za kutosheleza<br />
kueleza kwa nini unaacha. <strong>Wewe</strong><br />
kumbuka tu, mtu anayo haki ya kubadili<br />
mawazo yake.<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
unayo haki ya kubadilisha mawazo<br />
wakati wowote.<br />
SURA YA 9 | UJINSIA NA NGONO<br />
Sura ya 9<br />
ujinSia na nGOnO<br />
Ujana ndio muda ambao unajitambua wewe mwenyewe kama mtu ambaye unapata<br />
hisia za kijinsia. Unajitambua zaidi kuhusu ujinsia wako – unajisikia, unajiheshimu kama<br />
mwanaume au mwanamke, unajua kitu gani unataka kuhusiana na mahusiano na watu<br />
wengine.<br />
Mtu kuwa na afya kiujinsia maana yake ni kuwa unaweza kuelezea ujinsia wako katika<br />
namna ambayo haikudhuru wewe au mtu mwingine. Ina maana kwamba haujihatarishi<br />
kama vile kufanya ngono isiyo salama, ambayo inaweza kusababisha mimba zisizohitajika<br />
au magonjwa ya zinaa, ukiwemo VVU/UKIMWI.<br />
Kila mtu ana hisia za kiujinsia na huhitaji kufanya ngono unapokuwa na hisia za kiujinsia.<br />
Ngono ni njia mojawapo ambayo watu wanaweza kuelezea hisia za kijinsia, kama<br />
kuzungumza, kushikana mikono, kukumbatiana, kubusiana n.k.<br />
Bikira ni mtu – msichana au mvulana – ambaye hajawahi kufanya ngono. Wasichana<br />
hawawezi kupoteza ubikira wao kwa kucheza michezo au kuvaa kisodo au shughuli<br />
nyingine yoyote.<br />
Kutunza ubikira wako na kusubiri kufanya ngono kutakuweka salama. Haitakuumiza<br />
kusubiri. Vijana wengi wanaamua kutofanya ngono, wanajiona ni wadogo mno na wanajisikia<br />
bado. Unayo haki ya kusema “hapana” kwa ngono.<br />
Watu wengi duniani wameambukizwa VVU kwa kupitia ngono. Kama huko tayari kujikinga<br />
wewe na mwenzi wako kwa kutumia kondomu kila mara,basi ujue huko tayari<br />
kufanya ngono.<br />
Kuzungumza kuhusu ngono na marafiki zako wa kike au kiume inaweza kuonekana kazi<br />
ngumu na ya aibu mwanzoni lakini ni vizuri kumwambia mwenzio unataka nini na kipi<br />
hutaki ili isije ikatokea kutoelewana. Chagua muda mzuri wa mazungumzo na usisubiri<br />
mpaka uwe “katika joto la mahaba”. Kuwa mkweli kuhusu hisia zako, na usijirahisi au<br />
kushinikizwa kufanya kitu ambacho hukihitaji.<br />
Kumbuka, hata kama umewahi kufanya ngono kabla, unaweza wakati wote ukaamua<br />
kuacha kufanya ngono. Hakuna matatizo yoyote yatakayokupata. Kama huwezi kujikinga<br />
na mimba zisizotakiwa, VVU/UKIMWI na magonjwa ya ngono, itakubidi uache<br />
kufanya ngono.<br />
107
108<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Kutunza Afya <strong>Yako</strong><br />
Ya Kiujinsia<br />
Stabisile kutoka Zimbabwe (umri: miaka 19)<br />
“Mwili wangu ni wa pekee kwangu. Ninaulinda dhidi ya magonjwa<br />
ya ngono, VVU na mimba.”<br />
Mwili wako vile vile ni wa pekee. Je, unaulinda? Yapo mambo mengi unayotakiwa kuyajua<br />
kuhusu kuishi na afya nzuri na kujilinda mwenyewe dhidi ya matatizo ya afya ya uzazi.<br />
Watu wengi wanapofikiria matatizo ya afya ya uzazi, wanafikiria magonjwa ya ngono na<br />
VVU/UKIMWI tu. Haya ni matatizo ya hatari kwa hiyo ni wazo zuri kujua namna ya kujitunza<br />
na jinsi ya kuepuka majanga.<br />
MaGOnjWa Ya nGOnO<br />
Magonjwa ya ngono ni magonjwa ambayo<br />
yanaambukizwa kwa njia ya kujamiiana<br />
au kwa kufanya ngono. Yapo magonjwa ya<br />
ngono yanayosabisha vidonda, uvimbe au<br />
malengelenge wakati yapo mengine ambayo<br />
hayaonyeshi dalili zozote.<br />
Magonjwa ya ngono yanaenea kwa kupitia<br />
mgusano wa majimaji ya watu wawili – shahawa,<br />
majimaji ya ukeni na damu – na kupitia mgusano<br />
na ngozi iliyoathirika. Magonjwa ya ngono<br />
yanaweza kuenezwa kutoka kwa mwanaume<br />
kwenda kwa mwanamke, na kutoka kwa<br />
mwanamke kwenda kwa mwanaume na hata<br />
kati ya watu wawili wa jinsi moja.<br />
Ugonjwa uenezao kwa ngono uliombaya zaidi<br />
kuliko yote ni VVU/UKIMWI. Hakuna sindano<br />
ya kinga na hakuna dawa unapokuwa umepata<br />
maambukizi. Watu wengi wanakufa ndani ya<br />
miaka 10 mpaka miaka 20 baada ya maambukizi<br />
ya VVU.<br />
109<br />
SURA YA 10
110<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Magonjwa mengine ya zinaa kama kaswende, klamidia na kisonono ni hatari vilevile. Magonjwa<br />
haya yanatibika na tunaweza kuyathibiti. Lakini yanaweza kuleta athari za muda mrefu:<br />
•<br />
•<br />
Kusababisha ugumba yaani kushindwa kupata watoto.<br />
Kusaidia virusi vya UKIMWI kuingia mwilini kwa urahisi.<br />
Kwa ufupi, zipo njia tatu za kuepuka magonjwa ya zinaa ikiwa ni pamoja na VVU.<br />
1. Usifanye ngono. Ahirisha kufanya mapenzi au acha kabisa kujamiiana.<br />
2. Unapojamiiana, hakikisha unatumia kondomu tangu mwanzo mpaka unapomaliza kitendo.<br />
3. Nenda na mpenzi/mwenzi wako kupima VVU. Kabla ya kuanza kujamiiana. Unaweza kupima<br />
VVU zaidi ya mara moja kutegemeana ni lini ulifanya ngono isiyo salama (bila kinga) ili<br />
kuhakikisha huna VVU. (Angalia ukurasa wa 116 kwa maelezo zaidi). Hakikisha kati yenu hakuna<br />
aliye na maambukizo ya VVU kabla ya kuanza kujamiiana. Kila mmoja wenu abakie mwaminifu<br />
kwa mwenzie.<br />
Mambo haya yanaonekana kuwa rahisi. Njia za kuwa salama ni hizo tatu. Lakini, yapo mengi ya<br />
kufikiria. Iwapo ulifanya ngono na baadaye ukaamua kuacha, bado utatakiwa kupima. Unaweza<br />
kuwa na ugonjwa uenezwao kwa ngono bila ya kujitambua.<br />
je, unajua kwa nini wasichana wako hatarini zaidi kupata maambukizo ya<br />
magonjwa ya zinaa hasa VVu/uKiMWi?<br />
Ingawa wote, wanaume na wanawake, wanaweza kupata maambukizo ya magonjwa ya zinaa,<br />
wanawake na wasichana wanapata maambukizo kwa urahisi zaidi kuliko wanaume/wavulana.<br />
Zipo sababu kadhaa kwa nini iwe hivyo:<br />
1. Uume wa mwanaume unaingia ndani ya uke na shahawa zake zinaweza kuwa na maambukizo.<br />
Zikikaa ndani ya mwili wa mwanamke zinaongeza uwezekano wa kupata maambukizo ndani ya<br />
tumbo la uzazi, mirija ya falopia na ovari.<br />
2. Kwa ujumla, wasichana wako hatarini kupata maambukizo ya magonjwa ya zinaa kwa sababu<br />
mlango wa mfuko wa uzazi wa msichana balehe ni laini zaidi kuliko wa mwanamke mtu mzima. Uke<br />
unaweza ukachanika wakati wa kujamiiana jambo ambalo linaweza kuongezea hatari ya kupata<br />
maambukizo ya magonjwa ya ngono.<br />
3. Wasichana wengi na wanawake wanafundishwa kuwa watiifu na wanyenyekevu kwa wanaume.<br />
Hawana stadi ya kujiamini ili kuwashawishi wenzi wao kutumia kondomu kwa ajili ya kinga.<br />
Wasichana balehe wengi, walioolewa au wasioolewa, wenzi wao wana umri mkubwa kuliko wao<br />
wenyewe. Mwenzi anapokuwa na umri mkubwa kuliko msichana, inaweza kumuwia vigumu hasa<br />
msichana kujikinga na maambukizi ya magonjwa ya zinaa na mimba. Katika jamii nyingi inaweza<br />
kumwia vigumu mwanamke kukataa kujamiiana na mme wake au kumsisitizia watumie kondomu<br />
hata kama anafikiri mwanaume wake anaweza akawa na mwanamke mwingine.<br />
4. Wanawake na wasichana wako kwenye hatari ya kufanya ngono bila kutaka. (kwa kulazimishwa<br />
au kubakwa), kuliko wanaume na wavulana. Katika mazingira magumu kama haya, inaweza kuwa<br />
vigumu kujikinga na maambukizi.<br />
5. Mambo ya kimila na utamaduni kama vile kufanya ngono kavu na kuweka dawa za kienyeji, nguo<br />
na vitu vingine ndani ya uke ili “kusafisha” au “kuubana” vyote hivi vinamwongezea mwanamke<br />
hatari ya kupata maambukizo ya magonjwa ya ngono. Kukausha uke kabla ya kujamiiana<br />
kunaweza kuongeza uwezekano wa kuchanika na kuchubuka wakati wa kujamiiana.<br />
Kama wewe na mwenzi wako mnatumia kondomu wakati wote mnapojamiiana ni vizuri sana.<br />
Endelea!Watu wengi wanaanza kwa kutumia kondomu. Lakini baada ya muda wanaanza<br />
kufikiri. “Ninamwaminimwenzi wangu, tunaweza kuacha kutumia kondomu”. Hii siyo sawa!<br />
Kabla hamjaacha kutumiakondomu, wote wawili mnahitaji kupima kwa ajili ya magonjwa ya<br />
ngono pamoja na angalau, kipimokimoja cha VVU. Hata kama wewe na mwenzi wako mmepima<br />
na hamna maambukizo ya magonjwaya ngono, ni vizuri zaidi kuendelea kutumia kondomu. Je,<br />
ikitokea kwamba mmoja wenu amejamiianana mtu mwingine? Vilevile unahitaji kuzuia mimba.<br />
utajuaje KaMa uMePata MaaMbuKiZO Ya MaGOnjWa Ya Zinaa?<br />
Watu wengi hasa wanawake ambao wamepata maambukizo ya magonjwa ya zinaa<br />
hawaonyeshidalili zozote zile. Kwa mfano, hakuna dalili yoyote ya kuonyesha kwamba umepata<br />
maambukizo yaVVU kwa mara ya kwanza. Magonjwa mengine ya ngono vilevile hayana dalili za<br />
wazi, kwa hiyo kilamtu inabidi afikirie hatari ya kupata maambukizo ya magonjwa ya zinaa. Kama<br />
umeshafanya ngonobila kinga unaweza kuwa umejiweka katika hatari ya kupata maambukizo.<br />
Ukipata kidonda au kiupele sehemu za siri ambacho kinapotea, unahitaji kumwona mhudumu<br />
wa afya.Yapo magonjwa ya zinaa mengine ambayo yana dalili zinazokuja na kupotea. Kidonda<br />
cha kaswendewakati wote kinapona na vidonda vinavyotokana na malengelenge vinapona na<br />
kujirudia. Kama umewahikupata kidonda, kiupele au lengelenge kwenye via vya uzazi, unatakiwa<br />
kumwona mhudumu wa afya.Hata kama dalili za ugonjwa wa ngono zinapotea, maambukizo<br />
yanakuwepo na wala hayawezi kuponabila kupata tiba sahihi.<br />
Kwa vyovyote vile,kama<br />
umeshaanzakujamiiana au bado, ni<br />
vizuri kufahamuvia vyako vya uzazi<br />
vikoje. Ikiwa unajuavikoje ukiwa mzima,<br />
itakuwa rahisikugundua tatizo mapema.<br />
Tumia kiookujiangalia sehemu zako za<br />
siri kiurahisi.Kwa mfano, kidonda cha<br />
kaswendehakiumi, kwa hiyo unaweza<br />
usigundueisipokuwa kama ukiangalia.<br />
Kwa wasichana, ni vema kufahamu<br />
mwonekano na harufu ya kawaida<br />
yamajimaji yako ya ukeni. Majimaji<br />
yaukeni ya kawaida:. Ni kama majimaji<br />
meupe ya yai.<br />
• Ni maangavu au meupe.<br />
• Yanatoa harufu ya kawaida au yenye<br />
afya na isiyochukiza.<br />
• Hayawashi.<br />
SURA YA 10 | KUTUNZA AfYA YAKO YA KIUJINSIA<br />
Magonjwa ya ngono mara kwa mara<br />
husababisha majimaji ya ukeni kuwa na<br />
rangi ya njano au kijani na hutoa harufu<br />
mbaya na kali.<br />
je, unazijua alama na dalili za magonjwa ya<br />
zinaa?<br />
Magonjwa mengine ya zinaa hayana dalili za wazi,<br />
hasa kwa wanawake, lakini mengine yanazo.<br />
Dalili za magonjwa ya zinaa kwa wanaume ni<br />
pamoja na:-<br />
• Kidonda, vidonda, upele au malengelenge juu<br />
aukuzunguka uume.<br />
• Uume kutoa usaha.<br />
• Maumivu makali wakati wa kukojoa.<br />
• Maumivu wakati wa kujamiiana.<br />
• Maumivu na kuvimba mapumbu.<br />
• Uvimbe usio wa kawaida au kuota vitu kwenye<br />
via vya uzazi<br />
Dalili za magonjwa ya zinaa kwa mwanamke:<br />
• Kutoka kwa majimaji ukeni ambayo ni mazito;<br />
yanawasha au yana harufu na rangi isiyo ya<br />
kawaida.<br />
• Maumivu sehemu za chini ya kitovu. . Maumivu<br />
wakati wa kujamiiana.<br />
• Kutokwa kwa damu ukeni kusiko kwa kawaida<br />
na bila mpangilio.<br />
• Kuwasha maeneo ya via vya uzazi.<br />
• Uvimbe usio wa kawaida na kuota vitu kwenye<br />
via vya uzazi.<br />
111
112<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Magonjwa mengine ambayo hayaambukizo kwa njia ya ngono vilevile husababisha kutoka kwa<br />
majimaji yasiyo ya kawaida. (soma mwisho wa sura hii kwa taarifa zaidi). Hata bikira anaweza<br />
kupatabaadhi ya maambukizo haya. Ukiona kitu chochote cha tofauti, mwone mhudumu wa afya.<br />
Iwapomwenzi wako ameona kitu chochote cha tofauti kwenye sehemu zake za siri unatakiwa na<br />
wewe uende ukafanyiwe uchunguzi wa afya hata kama unajisikia una afya nzuri.<br />
KWenDa KuchunGuZWa MaGOnjWa Ya Zinaa.<br />
Kama umefanya ngono bila kinga, unahitaji kwenda kufanyiwa uchunguzi wa magonjwa ya zinaa,<br />
hatakama unazo au huna dalili zozote.<br />
Kwenda kuchunguza magonjwa ya ngono kunaogopesha. Kwa bahati mbaya wahudumu wa<br />
afyawengine wanahukumu na huwa hawana huruma kwa vijana balehe. Wanafikiri hawatakiwi<br />
kufanyangono na wanawafahamisha hivyo! Siku hizi, kliniki nyingi zinatoza gharama kubwa kwa<br />
matibabu yamagonjwa ya zinaa, lakini zipo chache ambazo zinatoa huduma kwa gharama nafuu<br />
kwa vijana balehe.Kwa hiyo, ulizia na ujaribu kutafuta kituo cha afya vinavyowajali vijana balehe.<br />
Hata kama wahudumusiyo wema, shikilia msimamo wako na endelea kuomba unachokitaka.<br />
Haiwezekani kwamba watakataakukuhudumia. Kuwa jasiri.<br />
Kwenye vituo vya afya vizuri utapata vilevile elimu nasaha kuhusu uamuzi muhimu kama:-<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Je, unataka kuendelea kufanya ngono?<br />
Je, unataka kupima VVU?<br />
Je, utazungumza vipi na mwenzi wako kuhusu kutumia kondomu?<br />
Je, unatakiwa kutumia uzazi wa mpango? Njia ipi ni sahihi kwako?<br />
Kliniki nyingi zinatoa kondomu bure, kwa hiyo anza kuzitumia kiukweli na hakikisha mwenzi wako<br />
anapata matibabu yanayostahili.<br />
Ikiwa umepata maambukizo ya magonjwa ya<br />
ngono:<br />
•<br />
Mwenzi ambaye hajatibiwa<br />
atakuambukizatena. Hata kama<br />
umeachana naye badounatakiwa<br />
kumweleza aende kufanyiwauchunguzi<br />
na kutibiwa. Kama huwaambiina kama<br />
hawana dalili zozote, hawawezikujua<br />
kama wana maambukizo ya magonjwaya<br />
ngono mpaka hapo ugonjwa<br />
utakapokuwaumesababisha madhara ya<br />
kudumu kwenyevia vya uzazi. Inaweza<br />
ikawa vigumukumweleza rafiki yako<br />
wa zamani lakiniunahitaji kuwa jasiri<br />
kuongea na kumwelezamtu huyo kwamba<br />
aende kufanyiwauchunguzi. Kumwambia mwenzako inaweza kuwa<br />
vigumu lakini ni muhimu.<br />
•<br />
SURA YA 10 | KUTUNZA AfYA YAKO YA KIUJINSIA<br />
Hakikisha unameza dawa zote ulizopewa na mhudumu wa afya.<br />
• Usifanye ngono mpaka utakapoelezwa na mhudumu wa afya kwamba wewe na mwenzi wako<br />
mmepona.<br />
• Jadili kuhusu afya ya kijinsia na mwenzi wako ili muweze kujikinga.<br />
Kamwe usijitibu mwenyewe magonjwa ya ngono. Unahitaji kupata dawa sahihi au dawa kutoka<br />
kwa mhudumu wa afya. Ukitumia dawa isiyo sahihi itafanya vijidudu vinavyosababisha ugonjwa<br />
kuwa sugu.<br />
Kamwe usichangie dawa na rafiki yako. Kunywa dozi yote peke yako. Iwapo utakunywa sehemu<br />
tu ya dozi utawafanya wadudu wanaosababisha ugonjwa wawe sugu na vigumu kutibika.<br />
Unajua kuhusu magonjwa ya zinaa?<br />
Magonjwa yote ya zinaa yanawezesha kupata maambukizo ya VVu kiurahisi. Baadhi ya magonjwa ya zinaa<br />
ambayo yanasababishwa na vijidudu vya bakteria na yanaweza kutibika ni:-<br />
• chankroidi: Ugonjwa huu husababisha vidonda vyenye maumivu kwenye via vya uzazi na wakati<br />
mwingine kuvimba kwa tezi kwenye kinena. Tezi za limfu zinaweza kuvimba hadi kupasuka. Vidonda<br />
vinavyohusiana na chankroidi vinaongeza hatari ya kupata maambukizo ya VVU.<br />
• Klamidia – Ugonjwa huu unaenezwa kwa njia ya kujamiiana na unaweza kukaa bila kujitokeza kwa muda<br />
halafu ukaanza kuleta matatizo. Dalili zake ni pamoja na uume au uke kutoa uchafu, maumivu wakati<br />
wa kujamiiana (kwa wanawake) na uvimbe au maumivu kwenye mapumbu. Mara nyingi, ugonjwa huu<br />
hauonyeshi dalili – 70% ya wanawake na 25% ya wanaume hawaonyeshi dalili kabisa. Kama klamidia<br />
haijatibiwa, maambukizo yanaweza kuenea na kusababisha uvimbe ndani ya mfuko wa kizazi na<br />
unaweza kupata ugumba. Kwa wanaume, klamidia isipotibiwa inaweza kusabisha ugumba.<br />
• Kisonono: Ugonjwa huu husababisha kutokwa usaha wa rangi ya njano/kijani na maumivu makali wakati<br />
wa kukojoa. Hata hivyo, wanaume wengine hawapati dalili zozote. Wanawake wengine wanaweza kutoa<br />
uchafu lakini wengi wao hawana dalili. Iwapo maambukizo hayajagundulika na kutibiwa, yanaweza<br />
kuenea na kusababisha ugumba/utasa. Kama kisonono hakijatibiwa husababisha pia upofu kwa watoto.<br />
• Kaswende: Ugonjwa huu husababisha kidonda kidogo kisichouma. Dalili zinatokea kwenye via vya uzazi<br />
au mdomoni. Kidonda hutokea siku 9 mpaka siku 90 baada ya maambukizo. Kidonda hiki hupotea baada<br />
ya siku chache na kinaweza kisionekane tena. Maambukizo yanaweza kukaa bwete kwa muda. Baadaye<br />
kipele kisichowasha hutokea. Dalili nyingine ni pamoja na homa kiasi, uchovu, vidonda kooni, nywele<br />
kunyonyoka, kupungua uzito, kuvimba tezi, na misuli kuuma. Iwapo kaswende haikutibiwa inaweza<br />
kuleta matatizo makubwa maishani kama ugonjwa wa moyo hasa katika hatua za mwisho. Maambukizo<br />
yanaathiri ubongo pia. Wanawake wajawazito wanaweza kumwambukiza kaswende mtoto tumboni na<br />
hii inaweza kusababisha mimba kuharibika au kuzaa mtoto aliyekufa. Watoto wanaozaliwa na kaswende<br />
wanakuwa wagonjwa sana. Matibabu yanaweza kufanyika wakati wowote kaswende inapogundulika,<br />
lakini ikigundulika mapema matibabu yanachukua muda mfupi na yanafanikisha kutibu ugonjwa huo.<br />
• “trikomoniasisi” husababisha kutoka uchafu unaonuka, kuwasha na vijidonda kwa wanawake.<br />
Wanaume kwa kawaida hawaonyeshi dalili kabisa. Dalili zinaanza siku 3 mpaka siku 28 baada ya<br />
maambukizo.<br />
Magonjwa mengine ya zinaa yanasabishwa na virusi. Haya hayawezi kutibika kiurahisi au hayawezi kutibika<br />
kabisa. Nayo ni:-<br />
• Malengelenge (herpes): Hayawezi kutibiwa na Viuavijasumu. Ugonjwa huu unaenezwa kwa njia ya<br />
kujamiiana na kwa kugusana na ngozi iliyoathirika. Malengelenge husababisha vidonda vidogo kutoka<br />
kwenye via vya uzazi au kuzunguka mdomo. Vidonda vinaweza kuambatana na homa kali, maumivu ya<br />
kawaida na kuvimba tezi. Malengelenge hupasuka baada ya siku 2 hadi siku 4 na mwishowe hupona. Mtu<br />
akipata maambukizo hubakia hivyo maishani. Marudio ya mashambulizi yanategemea afya ya mtu. Watu<br />
wenye VVU wanashambuliwa mara kwa mara na malengelenge. Mtoto aliye na maambukizo ya ugonjwa<br />
wa malengelenge yuko hatarini kupata upofu, ubongo kuharibika na kifo kutokea. Kwa kuongezea,<br />
malengelenge huongeza hatari ya mimba kutoka au kuzaa mapema (uaviaji).<br />
113
114<br />
•<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Unajua kuhusu magonjwa ya zinaa? (Inaendelea)<br />
Virusi vya “human Papilloma,” Vinundu sehemu za siri (genital warts)<br />
Virusi hivi husababisha sugu kuota kwenye via vya uzazi. Virusi hivi vilivyofunikwa<br />
vinaweza visionekane kwa urahisi, hususani kama vitatokea kwenye njia ya uzazi ya<br />
mwanamke. Kawaida vinajitokeza wiki 3 hadi wiki 9 baada ya maambukizo. Kipindi hiki<br />
kirefu vijidudu hukaa tuli mwilini kabla ya kusababisha ugonjwa. Inamaanisha kwamba<br />
inaweza ikawa vigumu kufahamu maambukizo yalikotokea na yanaweza kuenea kwa watu<br />
wengine bila kujua. Vinundu sugu vinaweza kutibiwa na maji ya tindikali na hairuhusiwi<br />
kujamiiana mpaka vinundu vyote vimepotea. Wenzi wote wanatakiwa kuchunguzwa ili<br />
kuona kama hawana vinundu sugu. Wanawake wenye maambukizo haya wako katika hatari<br />
kubwa ya kupata kansa ya kizazi.<br />
• VVu/ uKiMWi : Huu ni ugonjwa unaosababishwa na virusi. VVU vinapoingia mwilini<br />
hushambulia kinga ya mwili ambayo kwa kawaida inalinda mwili usipate maambukizo.<br />
Inaweza ikachukua miaka mingi kuona dalili za maambukizo, lakini baada ya muda mrefu<br />
mtu anashindwa kuzuia maambukizo na hata magonjwa yaliyozoeleka ambayo<br />
VVu/uKiMWi<br />
VVu (Virusi Vya uKiMWi) ni Virusi vinavyosababisha UKIMWI (upungufu wa Kinga Mwilini)<br />
UKIMWI ni ugonjwa ambao kinga ya mwili dhidi ya magonjwa inaharibiwa hatua kwa hatua.<br />
VVU vikiingia kwenye mwili wa mwanadamu vinashambulia kinga ya mwili ambayo kwa kawaida<br />
inalinda mwili usipate maambukizo. Watu wenye maambukizo ya VVU wanaitwa watu wanaoishi<br />
na VVU/ UKIMWI. Baada ya muda mrefu mtu aliyepata maambukizo anashindwa kuzuia<br />
maambukizo hata ya magonjwa yaliyozoeleka ambayo kwa vyovyote vile yasingefikia hali mbaya.<br />
Mwili unaposhindwa kujikinga na magonjwa tunasema mtu ana UKIMWI. hakuna chanjo ya<br />
maambukizo ya VVu, na hakuna tiba mara utakapokuwa umepata maambukizo hayo.<br />
Inachukua muda mrefu mpaka dalili za VVU kuonekana. Matokeo yake ni kwamba, mtu ambaye<br />
ana maambukizo ya VVU anaweza akawa na afya nzuri kwa miaka mingi na anaweza asijue<br />
kwamba anayo maambukizo. Katika kipindi hiki anaweza kueneza VVU bila yeye kujua.<br />
Muda ambao mtu anaanza kuona dalili za virusi unategemea na uwezo wa nguvu ya kinga ya mwili<br />
na uimara wa virusi. Yapo makundi mengi ya VVU. Makundi mengine humfanya mtu augue haraka<br />
kuliko mengine. Kwa wastani inachukua miaka 5 hadi 10 kabla dalili zozote za VVU hazijajitokeza.<br />
Kwa vile virusi vinashambulia kinga ya mwili na kumfanya mtu ashambuliwe kiurahisi na<br />
magonjwa, dalili zinatofautiana sana kutegemeana na ugonjwa gani mtu anaougua.<br />
Hata hivyo dalili za kawaida ni:-<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Kuvimba tezi za limfu<br />
Kifua kikuu.<br />
Kupungua uzito sana na kuchoka .<br />
Kutoka jasho, hasa usiku.<br />
Homa za mara kwa mara<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Kuharisha kwa mfululizo.<br />
Kichefuchefu na kutapika.<br />
Kikohozi kikavu cha mfululizo.<br />
Upele mwilini na vidonda mdomoni.<br />
Hakuna dawa inayotibu VVU/UKIMWI. Lakini zipo dawa zinazowasaidia watu waishio na VVU<br />
kwa miaka mingi bila kuumwa na zinazopunguza makali ya VVU/ UKIMWI. “Anti – retrovirals”<br />
(ARVs) ni dawa zinazopunguza kuendelea kwa virusi. “ARVs” zinawawezesha watu kuishi maisha<br />
ya afya nzuri. Dawa hizi haziuwi virusi moja kwa moja. Zaidi ya hapo dawa hizi ni ghali sana,<br />
ingawa zipo kampuni ambazo zimeanza kutengeneza dawa zenye gharama nafuu na zenye ubora<br />
uliosawa na dawa zilizo ghali. Hata hivyo, ni vigumu kununua dawa hizi ambazo ni nafuu katika<br />
nchi nyingi za Afrika. Matokeo yake ni kuwa watu wengi hawazipati. Dawa hizi sasa zimeanza<br />
kupatikana katika nchi nyingi za Kiafrika kwa bei nafuu.<br />
Kwa hiyo, kitu cha kwanza ni kuzuia VVU kuingia mwilini mwako.<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
UKWELI KUHUSU VVU<br />
Zipo aina mbili za VVU zinazojulikana kama VVU 1 na VVU 2. VVU 1 inapatikana zaidi, na VVU<br />
2 inapatikana zaidi Afrika ya Magharibi kuliko VVU 1. Vyote, VVU 1 na VVU 2 vinasababisha<br />
UKIMWI. Hata hivyo, kipindi cha kuanzia maambukizo mpaka kufikia UKIMWI ni kirefu<br />
zaidi kwa yule mwenye aina ya VVU 2 kuliko VVU 1. Sasa hivi hakuna kinga kwa aina zote za<br />
VVU wala hakuna dawa ya UKIMWI. Watu wengi wanaopata maambukizo ya VVU wanafikia<br />
UKIMWI baada ya kuishi na VVU kwa miaka 5 hadi miaka 10. Kipindi hiki cha muda ni cha<br />
wastani, inategemea na mambo kadhaa, kama:-<br />
•<br />
•<br />
•<br />
SURA YA 10 | KUTUNZA AfYA YAKO YA KIUJINSIA<br />
Aina ya VVU (VVU 1 au VVU 2).<br />
Upatikanaji wa dawa na kutibu dalili zinazojitokeza sana, na pia kujiweka wazi na<br />
magonjwa mengine.<br />
Msaada wa kisaikolojia anaopewa mgonjwa.<br />
Kumbuka kwamba maambukizo ya VVU/ UKIMWI huibuka kwa njia tofauti kutegemea na<br />
maelezo binafsi. Mtu akigundulika ana virusi vya UKIMWI haimaanishi atakufa tu. Wapo watu<br />
ambao walipata maambukizo miaka 20 iliyopita na hadi leo hawajafikia hatua ya UKIMWI.<br />
Matumaini yapo!<br />
Kamwe usidhani mtu anavyoonekana ni salama kwa sababu ya vile anavyoonekana.<br />
Subiri vya kutosha kabla ya kuanza ngono kwa sababu kujamiiana ndiyo njia kuu<br />
inayoambukiza VVU.<br />
Kama unafanya ngono, tumia kondomu kila maraKondomu inaweza kukukinga usipate VVU<br />
na magonjwa mengine ya ngono.<br />
Wakati wote pima VVU kabla ya kuanza uhusiano wa kijinsia na mtu mpya na hakikisha<br />
mwenzi wako naye anapima VVU.<br />
Usichangie nyembe, sindano, vifaa vya kutogea au visu vya kutahiria.<br />
115
116<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
VVu VinainGiaje MWilini?<br />
Njia kuu inayoeneza VVU ni kujamiiana na mgusano wa moja kwa moja na majimaji ya mwilini.<br />
Katika Afrika, zaidi ya asilimia 90 ya watu wanaoambukizwa VVU wanaambukizwa kwa njia<br />
ya kujamiiana. Ni rahisi sana kwa mwanamume kumwambukiza mwanamke kuliko mwanamke<br />
kumwambukiza mwanamume. Hii ni kwa sababu ngozi na misuli ya uke, kuzunguka kinembe na<br />
kuzunguka mashavu ya nje ya uke ni laini sana. Ngozi hii inapata michubuko, vidonda na kuchanika.<br />
Michaniko na michubuko ni midogo sana kiasi kwamba huwezi kuona kwa macho, lakini ni mikubwa<br />
kutosha VVU kupita kama ngozi laini inagusana na shahawa kutoka kwa mwanaume ambaye ana<br />
maambukizo.<br />
Mwanamume anapofanya ngono na mwanamke aliye na maambukizo ya VVU yuko hatarini vilevile<br />
kupata maambukizo. Uume unakutana na majimaji ya ukeni ambayo yana VVU. Kama mwanamke<br />
ana VVU, vinasafiri kupitia kwenye mrija wa uume. Iwapo hajatahiriwa VVU vinaweza kupita<br />
kwenye ngozi hii laini hususani kama vipo vidonda, michubuko au mikato.<br />
VVU vinaweza kuenea kwa njia nyingine vilevile. Njia hizi ni pamoja na:<br />
•<br />
•<br />
Mama kwa mtoto wakati wa mimba, au wakati wa kujifungua au wakati wa kunyonyesha.<br />
Mgusano wa damu ya mtu ambaye ana maambukizi. Inawezekana ikawa wakati wa kuongezewa<br />
damu, kujikata na kisu cha kuchangia au wakati watu wanaotumia dawa za kulevya<br />
wanachangia sindano.<br />
Siku hizi damu inayotumika kuwaongezea wagonjwa inachunguzwa kwa makini kuhakikisha<br />
kwamba haina maambukizo.Hata hivyo, sherehe nyingi za kimila kama kutahiri na kukata vitu<br />
mwilini zinaendelea kutumia njia ambazo siyo salama kama vile kuchangia kisu kimoja au wembe<br />
kwa watu wote wanaotegemewa kufanyiwa. Kamwe usichangie wembe na ndugu zako au marafiki<br />
zako na wala usichangie visu visivyochemshwa wakati wa sherehe ya kutahiri au tukio lolote la<br />
kimila.<br />
Bado haijathibitishwa kama mtu anaweza kupata VVU kupitia kwenye mate wakati wa kubusu.<br />
Hata hivyo, iwapo mtu ana mkato/kidonda mdomoni anaweza kupata maambukizo kwa kumbusu<br />
mtu ambaye anayo maambukizo ya VVU na anavyo vidonda vilevile. Kwa vile VVU vipo ndani ya<br />
shahawa na majimaji ya ukeni, kujamiiana kwa njia ya mdomoni hakuepushi hatari. Iwapo mtu ana<br />
mchubuko au kidonda mdomoni na wakati huohuo akapata shahawa au majimaji ya ukeni mdomoni,<br />
anaweza kupata VVU .<br />
VVU havienei kwa kugusana kwa kawaida kama vile kukumbatiana, kushikana mikono au kumgusa<br />
mtu mwenye maambukizo. VVU vinaishi kwa muda mfupi sana vinapokuwa nje ya mwili, kwa hiyo<br />
haviwezi kuenezwa kwa njia ya kumgusa mtu aliye na maambukizo au kuchangia vitu – kama beseni,<br />
vyombo vya kulia chakula, nguo, vitabu n.k.<br />
Wengi wetu tunao wagonjwa wenye UKIMWI ndani ya familia zetu na tunatakiwa kuwatunza<br />
wanapougua. Ni muhimu unapomhudumia mgonjwa kujikinga ili usipate maambukizo. Unachotakiwa<br />
kuhofia ni majimaji ya mwilini kama vile, majimaji yanayotoka kwenye vidonda, damu ya hedhi na<br />
uharo. Jilinde mwenyewe kwa kuvaa glovu unapomsaidia kuoga au unaposafisha kitu chochote<br />
chenye damu au majimaji yoyote ya mwilini.<br />
utajuaje KaMa una VVu?<br />
Huwezi kujua kwa kujiangalia mwili. Huwezi kutambua kama watu wengine wana VVU kwa<br />
kuwaangalia. Hata kama watu wana UKIMWI – walipata maambukizo ya VVU muda mrefu na<br />
wamekuwa wagonjwa – huwezi kujua kama ni UKIMWI kwa kuwaangalia labda kama wewe ni<br />
SURA YA 10 | KUTUNZA AfYA YAKO YA KIUJINSIA<br />
mhudumu wa afya. Hii ni kwa sababu<br />
magonjwa mengi yanayoambatana<br />
na UKIMWI yanaweza kujitokeza<br />
yenyewe kwa watu ambao hawana<br />
VVU. Kwa mfano, unaweza kuugua<br />
kifua kikuu ukiwa na VVU au<br />
usipokuwa navyo.<br />
Ipo njia moja tu ya kujua kama una<br />
VVU. Katika nchi nyingi upimaji<br />
wa VVU unaambatana na ushauri<br />
nasaha – majadiliano ya undani na<br />
mtu aliyesomea, mwenye huruma<br />
na ambaye anaweza kukusaidia<br />
ili uweze kumudu hali yako ya<br />
kuwa na VVU na kujifunza jinsi<br />
ya kujihudumia. Kama hujapata<br />
maambukizo, mshauri anaweza kukuelimisha ufanye hadhari ili usipate maambukizo.<br />
Vipimo vya UKIMWI vinaaminika ni sahihi, salama na haviumi. Mhudumu wa afya anachukua<br />
damu kidogo kutoka kwenye mkono wako. Unaweza kupata majibu katika muda wa saa moja, au<br />
unaweza kuambiwa urudi baada ya wiki<br />
moja au mbili kutegemeana na kipimo<br />
Vipimo vya VVU vinafanyaje kazi?<br />
kinachotumika.<br />
Ili kujua kama ni kweli huna VVU,<br />
utaambiwa urudi kupima tena baada<br />
ya miezi 3 hadi 6 wakati kipindi cha<br />
kusubiri kimepita.<br />
KWa nini uPiMe VVu?<br />
Zipo sababu nyingi za kupima VVU.<br />
Iwapo mara kwa mara unakuwa na hofu<br />
kuhusu maambukizo ya VVU na una<br />
wasiwasi kutokana na mabadiliko ya<br />
afya yako mara kwa mara inawezekana<br />
njia pekee ya kutuliza akili ni kupima.<br />
Iwapo ulifanya ngono na mtu ambaye<br />
anaumwa na umesikia ana UKIMWI,<br />
hapo utahofu zaidi. Labda njia pekee<br />
ya kutuliza akili ni kupima na kujua<br />
kama umepata maambukizo au la.<br />
Kamwe usidhani kwamba umepata<br />
maambukizo, pima ili ujue.<br />
Mtu yeyote anaweza akawa ameambukizwa VVu<br />
bila kuwa na dalili. usitegemee muonekano wa<br />
mtu kuamua kuwa fulani hana VVu.<br />
Mtu anapokuwa na maambukizo mwili hushituka<br />
na kutoa askari ili kupigana na maambukizo.<br />
Kipimo cha VVU kimetengenezwa kutambua kama<br />
askari wa VVU wapo au hawapo ndani ya mwili wa<br />
binadamu. Ikiwa wapo wengi, maana yake mtu huyo<br />
ana maambukizo ya VVU na kwamba mwili unajaribu<br />
kupigana na maambukizo.<br />
Kwa kawaida askari wanaopimwa na kipimo<br />
cha VVU huonekana mwezi mmoja baada ya<br />
maambukizo. Hata hivyo, mara nyingi askari wa<br />
VVU hutokea baada ya muda zaidi – kama miezi<br />
3 hadi miezi 6 baada ya maambukizo. Katika<br />
kipindi hiki kipimo cha VVU hakitaona askari. Kwa<br />
maneno mengine, miezi 3 mpaka miezi 6 baada ya<br />
maambukizo, mtu anaweza kupima na kuonekana<br />
hana maambukizo ingawa anayo maambukizo.<br />
Vile vile, mtu huyu anaweza kuambukiza watu<br />
wengine katika kipindi hiki kabla askari wa VVU<br />
hawajaonekana kwenye kipimo.<br />
Kwa hiyo,- kama mtu yuko hatarini kupata VVU<br />
na akapima na kuonekana hana VVU, bado<br />
anashauriwa kurudia baada ya miezi 6 ili kuwa na<br />
uhakika kama hana maambukizo.<br />
117
118<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Unafahamu kuhusu kuishi kwa matumaini na VVU? V<br />
Hamza alijua ana VVU miaka minne iliyopita. Wakati huo alikuwa ana umri wa miaka 18 naye<br />
anaeleza hadithi yake: “Nilitoka viupele mwilini. Hii ilinisukuma nikapime. Ulikuwa wakati<br />
mgumu sana kwangu, lakini kwa msaada wa ushauri nasaha nilikubaliana na hali halisi.<br />
Niliweza kumaliza kozi yangu ya ufundi magari. Ushauri nilioupata uliniwezesha kuishi mpaka<br />
hivi sasa. Nimeweza kubadili tabia. Nimeacha kuvuta sigara na kunywa pombe. Ninaye rafiki<br />
wa kike ambaye ana VVU vilevile. Ili kuepuka kuongezea maambukizo, tunafanya ngono<br />
salama – tunatumia kondomu.<br />
Vilevile ninaepuka kuwa na mfadhaiko na ninatibu magonjwa madogomadogo<br />
yanayonishambulia. Kitu kimoja cha muhimu nilichojifunza ni kuepuka kujionea huruma,<br />
na hili ndilo linalonifariji. Ninajihusisha sana katika michezo ya kuigiza ambayo inatumika<br />
kuelimisha vijana kuhusu kujizuia na VVU/UKIMWI na kuwahudumia waathirika.<br />
Ninawashauri vijana wasubiri kufanya ngono mpaka watakapokuwa wakubwa. Wale ambao<br />
wamepata maambukizo wanatakiwa kuikubali hali na kujiunga katika mapambano ili kuokoa<br />
maisha ya wale ambao hawajapata maambukizo”.<br />
Hamza anaishi salama na VVU. Amekuwa jasiri na amekubaliana na hali yake. Anautunza<br />
mwili wake. Anaendelea na shughuli zake ametingwa, hapotezi muda. Ana upendo na maisha.<br />
Ana rafiki wa kike. Lakini anahakikisha hamwongezei maambukizo na wala yeye mwenyewe<br />
haongezewi maambukizo anatumia kondomu. Kuishi kwa matumaini kunaweza kukusaidia<br />
kuwa hai kwa muda mrefu.<br />
KuiShi KWa MatuMaini na VVu<br />
Kugundua kuwa una maambukizo ya VVU, siyo kitu rahisi kustahimili lakini unaweza kujifunza<br />
kumudu kuishi navyo. Utahitaji kupewa ushauri nasaha. Ni jambo zuri vilevile kumweleza mtu wa<br />
karibu yako ili usibebe mzigo peke yako.<br />
Kwa watu wengi ugonjwa unaendelea polepole, na wanaweza kuishi na VVU kwa muda wa miaka<br />
10 hadi 20. Kuwa na matumaini. Wanasayansi wengi wanalifanyia kazi suala la VVU. Siku moja<br />
wataweza kufanikisha utafiti huo.<br />
Ukigundua umepata maambukizo ya VVU ni muhimu sana “kuishi kwa matumaini”. Kuishi kwa<br />
matumaini kunaweza kuboresha sana nafasi yako ya kuwa na afya kwa muda mrefu. Kuishi kwa<br />
matumaini na VVu maana yake ni:-<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Kumweleza mwenzi wako (unayeshirikiana naye ngono kuwa wewe ni mwathirika).<br />
Kuwatunza kwa upendo wale wote unaowapenda, na kushiriki ibada za dini yako.<br />
Tumia muda wako katika kumcha Mungu.<br />
Kula chakula bora kama vile mboga za majani, maharage, samaki wa kukausha kwa sababu<br />
hivi vinasaidia kuboresha kinga ya mwili.<br />
Kuishi kwa matumaini, kuikubali hali ilivyo na kutokunyanyapaliwa.<br />
SURA YA 10 | KUTUNZA AfYA YAKO YA KIUJINSIA<br />
unafahamu kinachotokea unapokwenda kupima?<br />
Susan ana umri wa miaka 19, aliamua kwenda kupima na sasa<br />
anaeleza kilichotokea. “Niligundua kwamba rafiki yangu wa<br />
kiume amefanya ngono na msichana mwingine. Niliachana<br />
naye. Lakini bado nilikuwa na hofu kwamba ningeweza kuwa<br />
nimepata maambukizo ya VVU. Tumekuwa tukifanya ngono<br />
isiyo salama (bila kinga). Hilo lilikuwa ni kosa kubwa sana.<br />
Sasa nimegundua.<br />
Nilihofu sana kuhusu VVU! Nilijua kuna njia moja tu ya kutuliza<br />
akili yangu: kwenda kupima. Siku moja nilipata ujasiri wa<br />
kwenda. Nilienda kwenye kituo cha maelezo kuhusu UKIMWI<br />
mjini Kampala. Nilipofika getini, niliogopa. Nilisimama pale<br />
kwa muda mrefu. Mwisho niliingia ndani.<br />
Niliandikishwa, nikapewa namba yangu na nikaambiwa<br />
nimsubiri mshauri. Baada ya dakika tano, alikuja na<br />
akanichukua pamoja na wengine wanne tukaenda kwenye<br />
chumba kingine. Tulipewa ushauri nasaha kama kundi.<br />
Alituuliza tulikuwa tunajua nini kuhusu VVU/UKIMWI na alijibu<br />
maswali yetu.<br />
Kilichofuata, mimi na mshauri tulikutana faragha. Aliniuliza lini<br />
nilifanya ngono kwa mara ya mwisho, nilikuwa na marafiki wa<br />
kiume wangapi na kama nilitumia kinga. Aliniambia ninaweza<br />
kutoka nje wakati wowote kama ningaliamua kutopima. Lakini<br />
nilimweleza kwamba nataka kupima. Baada ya hapo alinipeleka chumba kingine ambako<br />
alinitoa damu kidogo kutoka kwenye mkono. Alifanya haraka sana na wala haikuuma.<br />
Baada ya damu kuchukuliwa nilienda kwenye chumba cha ushauri nasaha na mshauri<br />
alizungumza na kila mtu kuhusu nini maana ya kuwa na VVU au kutokuwa na VVU. Alituuliza<br />
ni kwa jinsi gani tutamudu iwapo majibu yatakapoonyesha kuwa tumeathirika, na jinsi<br />
tutakavyojilinda tusipate maambukizi zaidi au tusiwaambukize wengine. Alituuliza namna<br />
gani tutahakikisha tunabakia watulivu iwapo majibu yatatokea kuwa hasi.<br />
Baada ya kupewa ushauri nasaha kwa kikundi, tuliitwa kwenye chumba cha faragha kupewa<br />
majibu yetu. Nilikuwa wa kwanza kuitwa. Jasho lilikuwa linanitoka na mapigo ya moyo<br />
yalikuwa yanaenda mbio. Nilitaka kukimbia nitoke, lakini niliyahitaji majibu.<br />
‘Majibu yako ni mazuri, huna VVU’, niliambiwa na mshauri. Nilifumba macho, nikasali sala ya<br />
shukurani. -Niliapa kutofanya ngono tena bila kusisitizia matumizi ya kondomu. Mshauri<br />
aliniambia kwamba, kwa vile ni zaidi ya miezi sita tangu nilipofanya ngono kwa mara ya<br />
mwisho, ninaweza kuamini majibu haya na nisingehitaji kipimo kingine cha kuhakikisha<br />
kwamba nilikuwa sina VVU.<br />
Nilipotoka nje, nilijisikia nafuu na mwenye furaha. Na yote haya yalifanyika kwa muda wa<br />
saa moja tu”<br />
119
120<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Tibu magonjwa yote yanapojitokeza.<br />
Pumzika na fanya mazoezi mepesi.<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Jiunge na jumuia au vikundi vya kusaidia watu wanaoishi na VVU/UKIMWI.<br />
Fanya ngono salama ili usimwambukize mtu mwingine virusi au mwenyewe kujiongezea<br />
virusi vipya mwilini mwako.<br />
Kuishi chanya maana yake ni kuishi kwa kadiri ya upeo wako kila siku. Kuishi chanya ni kitu<br />
ambacho kila mtu anatakiwa kufanya hata kama hatuna maambukizo ya VVU.<br />
Vilevile ni muhimu kuwasaidia watu wengine waishi kwa matumaini na VVU. Usiwaite watu<br />
wenye VVU au UKIMWI “waathirika” kwa sababu siyo waathirika. Ni kama watu wengine, walio<br />
na vitu vingi vya kufanya. Wanaweza kufanya kazi na kuchangia maendeleo. Wanahitaji upendo<br />
na kusikilizwa kama watu wengine. Mara kwa mara wanahitaji msaada wa pekee kutoka kwa<br />
marafiki wa karibu. Inawapasa ndugu kuwa na mtazamo unaowajali / usiowabagua watu wenye<br />
VVU. Kamwe usiwatanie, kuwanyanyapaa au kuwasumbua katika jamii.<br />
Ulikuwa unafahamu kwamba:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
nGOnO SalaMa / MaPenZi SalaMa<br />
UKWELI KUHUSU VVU/UKIMWI<br />
Watu milioni 42 duniani wanaishi na VVU kwa sasa. Kati ya hawa karibu robo wana umri<br />
wa miaka kati ya 15 na 24. Watoto na vijana chini ya miaka 18 wanawakilisha zaidi ya<br />
asilimia 10 ya wanaoishi na VVU*.<br />
Nchi zilizoko Kusini mwa Jangwa la Sahara zimeathirika sana na VVU/UKIMWI, na<br />
UKIMWI ndiyo ugonjwa unaosababisha vifo vingi. Kati ya watu wote wanaoishi na VVU,<br />
milioni 29.4 ni kutoka eneo hili na kulikuwa na maambukizo mapya ya watu milioni 3.5.<br />
Kwa ujumla, VVU vinaenea kwa njia ya kujamiiana. Asilimia 90 ya maambukizo Afrika<br />
yanatokana na kujamiiana.<br />
Duniani kote, wapo watoto milioni 14 ambao ni yatima kwa sababu ya UKIMWI na kati ya<br />
hawa milioni 12.1 wanaishi Kusini mwa Jangwa la Sahara.<br />
Ugonjwa huu wa mlipuko unapunguza matarajio ya muda wa kuishi katika Afrika.<br />
Mwishoni mwa miaka ya 1990, watu Afrika walitarajia kwa wastani kuishi miaka 59. Lakini<br />
kutokana na VVU/UKIMWI, matarajio ya muda wa kuishi kwa watu wa Afrika itashuka<br />
hadi miaka 45 tu kufikia mwaka 2010.<br />
Ngono salama maana yake ni kufanya mapenzi ambayo yanapunguza uwezekano wa wewe<br />
kupata magonjwa ya ngono, ikiwa ni pamoja na VVU au mimba. Ukitaka mapenzi salama kwa<br />
asilimia mia moja (100%) basi uchaguzi ulio bora zaidi ni kupiga punyeto na kuacha kabisa<br />
kujamiiana. Kama ukisoma sura ya 9 utafahamu kwamba punyeto ni salama kabisa, upo peke<br />
yako. Majimaji ya sehemu za siri ni yako mwenyewe. Huwezi kupata maambukizo kutoka kwa mtu<br />
yeyote na wala huwezi kujipa au kumpa mtu mwingine mimba.<br />
Kubusu au kumkumbatia mwenzi wako<br />
ni mapenzi salama. Mpaka sasa hivi<br />
haijathibitishwa kama VVU vinaenezwa kwa<br />
njia ya kubusu au kukumbatia. Hata hivyo, kama<br />
mmojawapo ana maambukizo ya VVU na ana<br />
vidonda mdomoni anaweza kumwambukiza<br />
mwenzake. Vilevile kuna uwezekano wa<br />
maambukizo kutokea iwapo mtagusana via vya<br />
uzazi na kupata majimaji ya ukeni au shahawa<br />
mikononi. Kama una mikato au michubuko<br />
mikononi unaweza kupata maambukizi ya VVU<br />
kama mtu mwingine ana maambukizi.<br />
Kujamiiana kati ya watu wawili ambao wote<br />
hawana maambukizo ya magonjwa ya zinaa au<br />
VVU ni mapenzi salama. Lakini, bila shaka bado<br />
patakuwa na hofu ya mimba.Watu wengi hufikiria<br />
kwamba kwasababu wamekuwa na uhusiano na<br />
mtu kwa muda mrefu, wanaamini kuwa hawana<br />
VVU na magonjwa mengine ya ngono. Lakini<br />
mmoja wao akipima ndipo ukweli unadhihirika.<br />
Watu unaowaamini na kuwapenda wanaweza<br />
kukuambukiza magonjwa ya zinaa. Wanaweza<br />
wakawa hawajui kuwa wamekuambukiza.<br />
andrew kutoka tanzania (umri wa miaka 17)<br />
“Ninajiamini mwenyewe; sina maambukizo ya magonjwa ya ngono<br />
kwa sababu sijawahi kujamiiana na mtu yeyote.”<br />
anthony kutoka Kenya (umri wa miaka 15)<br />
“Sababu nzuri kuliko zote ya kumfanya kijana acheleweshe kuanza<br />
ngono ni kwamba ana uhakika wa kutopata UKIMWI na magonjwa<br />
mengine ya ngono.”<br />
Milensu kutoka Zambia (umri wa miaka 13)<br />
“Kusema “HAPANA” sitaki kujamiiana ni njia mojawapo ya kujikinga<br />
na hatari ya kupata magonjwa na inakufanya udhibiti maisha yako.”<br />
Kondomu vilevile ikitumika vema hufanya tendo la ngono kuwa salama. Kwa kweli kondomu ni<br />
muhimu katika kukulinda wewe na mwenzi wako. Hata kama hujaanza kujamiiana, ni vema usome<br />
somo linalofuata kwani kuna siku utahitaji kuzifahamu kondomu.<br />
KOnDOMu<br />
SURA YA 10 | KUTUNZA AfYA YAKO YA KIUJINSIA<br />
Hujachelewa kuanza kutumia kondomu.<br />
Kondomu ni mfuko laini uliotengenezwa kwa mpira ambao unavalishwa kwenye uume kabla ya<br />
kuanza kujamiiana. Mwanaume anapofikia mshindo, anakojoa shahawa ambazo hunaswa kwenye<br />
chuchu ya kondomu. Kwa vile shahawa zinakusanyika kwenye kondomu ina maana majimaji ya<br />
mwanaume hayamwingii mwanamke na wala uume haugusi majimaji ya ukeni kwa sababu uume<br />
umefunikwa na kondomu.<br />
121
122<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Kama ikitumika kiusahihi na kwa kukubaliana, kondomu ni kinga<br />
kamili dhidi ya magonjwa ya ngono, ikiwa ni pamoja na VVu na<br />
uzuiaji wa mimba. Kondomu zinazuia vijidudu, bakteria na virusi<br />
vilivyo ndani ya uke kukutana na uume, na huzuia mbegu za kiume,<br />
bakteria na virusi ndani ya shahawa kuingia ukeni.<br />
Ijapokuwa kondomu zinaonekana nyembamba sana,<br />
zimetengengezwa na mpira imara (lateksi) na zimejaribiwa kwa<br />
kutumia nguvu za electroniki ili kuhakikisha kwamba kiwango chake<br />
ni cha juu. Watu wengine wanasema kwamba kondomu zina matundu<br />
madogo sana ambayo yanaweza kupitisha VVU. Hii siyo kweli. VVU<br />
haviwezi kupita kwenye kondomu. Hata hivyo, kondomu inaweza<br />
kuwa na matundu kama muda wa kutumika umekwisha au imetunzwa<br />
vibaya au imewekwa visivyo.<br />
Ni muhimu sana kufuata taratibu za matumizi ya kondomu kila mara<br />
na kila wakati unapozitumia:<br />
1.<br />
2.<br />
3.<br />
4.<br />
Seif, kutoka tanzania(umri wa miaka 13)<br />
“Ngono salama ni kutumia kondomu. Niliyasikia haya kutoka<br />
kwa watu na vilevile kwa kusoma magazeti. Sijawahi kufanya<br />
ngono”.<br />
Sospita, kutoka tanzania(umri wa miaka 13)<br />
“Nimesikia kuhusu kondomu. Nilisoma kwamba zinakukinga<br />
usipate maambukizo ya magonjwa ya ngono na VVU”.<br />
Godfrey, kutoka Zimbabwe(umri wa miaka 19)<br />
“Sina uhakika kama nitafanya mapenzi na mtu yeyote bila ya<br />
kutumia kondomu. Sioni kama hilo linaweza kutokea”.<br />
Chana pembezoni mwa pakiti kwa uangalifu. Usitumie meno na<br />
hakikisha kucha hazichani kondomu.<br />
Usiikunjue kondomu harakaharaka. Iweke kwanza kwenye kiganja<br />
chako na itasimama kama kofia.<br />
Valisha kondomu mara uume unapodinda vizuri na kabla<br />
haujagusa uke. Shika chuchu ya kondomu ukiwa unaiviringisha<br />
chini ya uume. Kondomu inatakiwa iende yenyewe kiurahisi. Kama<br />
haishuki kiurahisi basi jua umeigeuza ndani nje. Itupe kondomu<br />
hiyo na uchukue mpya. Usitumie kondomu iliyogeuzwa ndani nje<br />
kwa sababu inaweza ikawa na shahawa ambazo zina mbegu za<br />
kiume au vijidudu vinavyoambukiza magonjwa ya ngono.<br />
Endelea kushika chuchu ya kondomu wakati unaendelea<br />
kuiviringisha kondomu mpaka uifikishe kwenye shina kabisa. Hii<br />
nafasi ya ziada (chuchu) ni kwa ajili ya shahawa baada ya kukojoa<br />
(kufikia mshindo).<br />
5.<br />
6.<br />
Baada ya kukojoa, shika ukingo wenye bangili wa kondomu na toa<br />
uume toka kwenye uke. Hii itasaidia kuzuia kondomu isiteleze.<br />
Tupa kondomu kwenye choo cha shimo, choma au fukia ardhini.<br />
Usiache kondomu mahali ambapo watoto wataiona na wala usitupe<br />
kwenye choo cha kuvuta maji kwani itaelea.<br />
Yafuatayo ni maelezo zaidi ya jinsi ya kutumia kondomu kwa usahihi ili<br />
zisipasuke na wala zisiteleze na kutoka.<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
SURA YA 10 | KUTUNZA AfYA YAKO YA KIUJINSIA<br />
Angalia juu ya pakiti tarehe ya kwisha matumizi au tarehe ya<br />
kutengenezwa. Kama tarehe ya kwisha matumizi imepita, usiitumie!<br />
Kama tarehe ya kutengeneza ni zaidi ya miaka mitatu iliyopita,<br />
usiitumie! Kumbuka kuwa hata kondomu zinazotumika kuzuia mimba<br />
zisitumike zaidi ya miaka miwili baada ya tarehe ya kutengenezwa.<br />
Kamwe usitumie kondomu ambayo pakiti yake imetoboka. Zaidi ya<br />
hapo usitumie kondomu ambayo ganda lake lina rangi zilizochujuka<br />
au halina rangi kabisa au kama ganda ni gumu limekakamaa au linanata sana.<br />
Tunza kondomu sehemu ambayo kuna ubaridi kiasi, kiza na pakavu. Joto, mwanga na<br />
unyevuunyevu vinaharibu kondomu. Usitunze kondomu kwenye pochi au mfukoni.<br />
Ikiwezekana tumia kondomu zenye vilainishi au tumia vilainishi kama kondomu siyo laini.<br />
Vilainishi vinaweza kusaidia kondomu isipasuke au kuchanika wakati wa kujamiiana. Tumia<br />
vilainishi vyenye asili ya maji tu. Vilainishi vizuri ni pamoja na maji na dawa za kuulia mbegu<br />
za kiume. Majimaji ya ukeni ya asili yanaweza kuwa kilainishi. Kamwe usitumie vilainishi<br />
vyenye asili ya mafuta. Usitumie vaselini, mafuta ya maji (ya kupikia, ya watoto, ya nazi,<br />
petroli), jeli ya petroli, vipodozi vya aina zote, siagi, malai ya kokoa au majarini. Vyote hivi<br />
vinaweza kudhoofisha uimara wa kondomu.<br />
Usikunjue kondomu kabla ya kutumia. Kondomu ambayo imeshakunjuliwa ni vigumu kuivaa.<br />
Tumia kondomu mpya kila unapofanya ngono baada ya mshindo. Kamwe usitumie kondomu<br />
zaidi ya mara moja na usivae zaidi ya moja.<br />
Watu wachache wanadhurika kiafya na mipira aina ya “lateksi”. Hivyo kondomu hizi<br />
zinawasababishia viupele na ngozi kuwasha. Kama unalo tatizo kama hili, zipo kondomu ambazo<br />
hazitengenezwi kwa kutumia mpira wa “lateksi”. Tumia hizo. Zungumza na mhudumu wa afya<br />
namna ya kuzipata.<br />
Watu wengi wanaotumia kondomu wanasema zinawafanya wenza wote wawili wafurahie ngono.<br />
Wenza wote wanaweza kupumzika na kutulia zaidi wanapokuwa hawana hofu ya mimba au<br />
kupata magonjwa ya ngono. Wanaume wengine wanasema kondomu zinawasaidia wasifikie<br />
mshindo “wasikojoe” haraka na kuwafurahisha wenzi wao.<br />
Lakini pia wapo wanaume na wanawake ambao hawapendi kutumia kondomu kwa sababu wana<br />
hofu kuwa hawatafurahia ngono vizuri. Hivyo, mwanaume anaweza kumdanganya mpenzi wake<br />
kwamba hana ugonjwa hivyo kumtaka amwamini na asiwe na sababu yoyote ya kuwa na hofu.<br />
123
124<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Anaweza kumfanya mwanamke ajisikie vibaya kwa kumuuliza ni kwa nini hamwamini. Lakini<br />
ikumbukwe kuwa yeyote anaweza kuwa na maambukizo ya magonjwa ya ngono ikiwa ni pamoja<br />
na VVU kutokana na uhusiano uliotangulia hata bila ya kuona dalili zozote. Kwa hiyo, ni kwa faida<br />
ya wote kutumia kondomu.<br />
Kondomu inatoa kinga kwa wale watakaohusika. Kuitumia kondomu ni alama ya kuaminiana,<br />
kuheshimiana na kujaliana.<br />
MatatiZO MenGine Ya aFYa Ya uZaZi<br />
je, unazifahamu kondomu za kike?<br />
Umewahi kusikia kuhusu kondomu za kike? Hii ni njia<br />
nyingine ya kujikinga dhidi ya VVU, magonjwa mengine<br />
ya ngono na mimba. Hiki ni kimfuko kilicholainishwa<br />
kama kondomu ya kawaida ya wanaume. Lakini, badala<br />
ya kufunika uume, inakinga uke kama kizuizi dhidi ya<br />
maambukizo.<br />
inavyofanya kazi: Kuna pete ndogo mbili; moja ni pete<br />
ndogo ndani ya kondomu na ya pili ipo upande uliowazi ambayo hukaa nje ya mwili. Pete hizi<br />
hushikilia kondomu ya kike ikae mahali pake. Kondomu ya kike, kama kondomu ya kiume<br />
inazuia mbegu za kiume kukutana moja kwa moja na uke. Kama uume unabakia ndani ya<br />
kondomu na pete ya nje inabakia mahali pake basi kondomu itafanya kazi.<br />
jinsi ya kutumia: Inaweza kuchukua muda ili kuweza kuivaa kondomu vizuri kama mazoezi<br />
yalivyo kwa kondomu za kiume. Lakini mwisho utazoea. Kwanza ikunje pete ya ndani iwe<br />
na alama ya nane (8). Kisha isukume ndani kiasi utachoweza mpaka utakapoona huwezi<br />
kuisukuma zaidi. Kondomu itakapokuwa imekaa sehemu yake, ongoza uume wa mwenzi<br />
wako ndani ya kondomu. Tumia kondomu ya kike moja kwa wakati mmoja. Usirudie kuitumia<br />
kondomu hiyo.<br />
jinsi ya kuitoa: Ni rahisi sana kuitoa. Sokota pete ya juu ili shahawa zisimwagike, halafu vuta<br />
kondomu nje na itupe ndani ya choo cha shimo au choma moto au fukia ndani ya shimo.<br />
Faida yake: Kondomu ya kike ni njia pekee ya kujikinga ambayo inadhibitiwa na mwanamke<br />
mwenyewe ili imlinde dhidi ya maambukizo ya magonjwa ya zinaa, VVU/ UKIMWI na mimba.<br />
Inakaa taratibu ndani ya uke na haibani uume unapoingia.<br />
Yapo matatizo ambayo yanatokea kwenye via vya uzazi lakini siyo magonjwa ya zinaa. Hata<br />
kama hujawahi kufanya ngono, yapo maambukizo ambayo unaweza kuyapata sehemu zako<br />
za siri. Unaweza ukapata maambukizo kwenye njia ya mkojo ambayo husababisha kuwashwa<br />
au maumivu unapokojoa mkojo. Ukiona uchafu wa ajabu unatoka au maumivu au damu wakati<br />
unapokojoa, unatakiwa kumwona mhudumu wa afya.<br />
KanDiDiaSiSi”<br />
Kama sehemu zako za siri zinawasha na unatokwa na uchafu wa ajabu ukeni unaweza ukawa na<br />
“kandidiasisi”. Hili ni tatizo la kawaida. Ugonjwa huu vilevile unaitwa maambukizo ya hamira na<br />
unasababishwa na kuvu wanaofanana na hamira wanaoitwa “kandida albicans”. Ugonjwa huu<br />
unawasumbua wasichana na wanawake wengi. Wavulana wanaweza kupata kandida chini ya govi.<br />
Kandida ni kiumbe kimojawapo ambacho kwa asili kinaishi juu ya mwili. Kwa kawaida kandida<br />
hakisababishi matatizo yoyote. Kinadhibitiwa na kinga ya mwili na bakteria wengine ambao<br />
kwa kawaida wanaishi ukeni. Lakini ikiwa kinga ya mwili imeshaharibiwa na haifanyi kazi vizuri,<br />
viumbe kandida huzaliana haraka . Mara kwa mara tatizo hili hutokea kabla au baada ya damu ya<br />
hedhi kutoka na wakati wa mimba.<br />
“Kandidiasisi” inaweza kuenea kwa njia ya kujamiiana na mtu ambaye ana kandida wengi. Lakini<br />
inaweza kusababishwa na mambo mengine vilevile. Mfadhaiko, kama vile mitihani, kifo ndani ya<br />
familia au mabishano yanaweza kuwa kichochezi cha “kandidiasisi”. Wakati mwingine unaweza<br />
kupata kandidiasisi ukinywa kiuavijasumu – Viuavijasumu vinaua bakteria ambao kwa kawaida<br />
wanaishi ukeni. Watu wanaoumwa kisukari na wale wenye VVU wanapata kandidiasisi mara kwa<br />
mara.<br />
“Kandidiasisi” si ugonjwa wa ngono kwa sababu hata bikira wanaupata. Joto linapozidi na<br />
unyevunyevu kuzunguka eneo la via vya uzazi vinaweza kusabisha kandidiasisi. Hii ina maana ya<br />
kwamba unaweza kujiletea mwenyewe “kandidiasisi” kwa kuvaa nguo zisizofaa. Kama, kwa mfano<br />
ukivaa nguo za nailoni, kaptura za kubana au suruali aina ya jeans zinazobana na kukaa kwa saa<br />
kadhaa huku umebananisha miguu, pengine kwenye basi, unatengeneza unyevuunyevu na joto<br />
ambalo kandida wanahitaji ili waishi.<br />
Dalili za kandidiasisi ni:-<br />
•<br />
•<br />
•<br />
SURA YA 10 | KUTUNZA AfYA YAKO YA KIUJINSIA<br />
Zungumza na mwenzi wako kuhusu matumizi ya Kondomu. eleza unavyojisikia na unachotaka.<br />
Kuwashwa kwenye via vya uzazi, wote; wasichana na wavulana.<br />
Usaha kutoka ukeni au chini ya govi unaofanana na maziwa yaliyoharibika.<br />
Kuvimba na kuwepo kwa utando telezi wa uke na midomo ya ndani au kichwa cha uume kuwa<br />
chekundu.<br />
Iwapo utapata mojawapo ya dalili hizi omba msaada kutoka kwa mhudumu wa afya mwenye ujuzi<br />
ambaye atakupatia matibatu yanayotakiwa. Matibabu yanayotakiwa kawaida ni:-<br />
125
126<br />
•<br />
•<br />
•<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Dawa za kupaka zinazotibu kuvu au wakati mwingine kidonge kinachotumbukizwa ndani ya uke. Iwapo<br />
umeishaanza ngono, mwenzi wako anatakiwa kutibiwa pia ili asikuambukize tena.<br />
Vilevile, unaweza kusafisha taratibu eneo la via vya uzazi na maji yenye chumvi kidogo. Kuwa safi<br />
kwa kusafisha mara mbili kwa siku. Usifute via vya uzazi kwa sababu utasababisha vidonda ambavyo<br />
itabidi vitibiwe. Usikune uke, na nawa mikono baada ya kushika sehemu za siri. Vaa nguo safi<br />
zilizokauka na chupi za pamba. Kumbuka kuanika chupi juani.<br />
Iwapo maambukizo ya “kandidiasisi” yanajirudiarudia ni vema kwenda kupima VVU. Maambukizi<br />
yanayojirudiarudia ni alama ya kinga kuwa dhaifu.<br />
MaaMbuKiZi KWenYe njia Ya MKOjO<br />
Wanawake na wanaume wanaweza kupata maambukizo kwenye njia ya mkojo, lakini zaidi kwa wanawake<br />
kwa sababu ni rahisi bakteria kuingia kwenye njia ya mkojo. Dalili za maambukizo ni:<br />
• Kutaka kukojoa mara kwa mara<br />
• Kusikia maumivu makali wakati wa kukojoa<br />
• Mkojo kuchanganyikana na damu.<br />
Maambukizi haya yanaweza kuepukwa kwa kujiweka safi hasa kwa kusafisha eneo la via vya uzazi kila siku<br />
na kuhakikisha unanawa baada ya kwenda haja kubwa. Wakati wote unasafisha kutoka mbele kuelekea<br />
nyuma. Ukisafisha kutoka nyuma kwenda mbele unaweza kusambaza bakteria kutoka kwenye mkundu<br />
kwenda kwenye tundu la mkojo. Hatua nyingine za kuchukua ili kuepuka maambukizo haya ni kunywa<br />
maji mengi; kukojoa mkojo mara kwa mara (usijaribu kubana mkojo kwa muda mrefu) na hasa baada ya<br />
kujamiiana, na kuvaa chupi za pamba na nguo pana zinazoweka sehemu za siri kavu.<br />
Iwapo unafikiri unayo maambukizo kwenye mrija wa kupitisha mkojo, kunywa maji mengi na nenda<br />
kamwone mhudumu wa afya kwa ajili ya matibabu. Usijamiiane mpaka dalili zote ziwe zimetoweka.<br />
KanSa / SaRatani Ya ShinGO Ya MlanGO Wa KiZaZi<br />
Saratani ya shingo ya mlango wa kizazi inaathiri mlango wa mfuko wa kizazi. Seli zinapokuwa na saratani<br />
zinaongezeka haraka kuliko seli za kawaida mwilini mwako. Seli za Saratani zinavamia na kuchukua nafasi<br />
ya tishu zilizo na afya mwilini mwako na hatimaye ugonjwa unaweza kuua. Ugonjwa huu unawapata sana<br />
wanawake wakubwa (zaidi ya miaka 40). Lakini sasa hivi unajitokeza hata kwa vijana wa umri mdogo.<br />
Saratani ya shingo ya mlango wa mfuko wa kizazi inaweza kuonekana mapema kwa kutumia utaratibu<br />
unaoitwa “Pap smea”. Mhudumu wa afya atatakiwa akusanye seli kwenye mlango wa mfuko wa kizazi. Kwa<br />
kutumia darubini, seli ambazo si za kawaida na ambazo zinaweza kuwa na saratani zinaangaliwa kama<br />
zipo. Ikiwa zipo seli ambazo si za kawaida zinaweza kuondolewa. Saratani ya mlango wa mfuko wa kizazi<br />
inatibika iwapo itagundulika mapema. Kwa vile ni muhimu kugundua mapema saratani hiyo, madaktari<br />
wanashauri kwamba wanawake wote ambao wanajamiiana wapime kipimo cha “pap smea” kila baada ya<br />
miaka mitatu mpaka mitano.<br />
Kama harufu mbaya au uchafu unatoka ukeni au kama damu inatoka unapojamiiana, mwone daktari kwa<br />
sababu hizi zinaweza kuwa dalili za kuwa na tatizo kwenye mlango wa mfuko wa kizazi.<br />
Unajiweka kwenye hatari ya kupata kansa ya kizazi ikiwa utaanza kufanya ngono katika umri mdogo (kabla<br />
ya miaka 20) au kama utashiriki ngono na watu zaidi ya watatu katika kipindi cha uhai wako.<br />
Kuweka sugu sehemu za siri kunaongeza kwa kiasi kikubwa hatari ya kupata kansa ya kizazi. Ugonjwa wa<br />
kansa ya kizazi ni sababu ya msingi ya kukufanya uamue kusubiri hadi ufike miaka 20 ndipo ufanye ngono.<br />
Pia, ni sababu ya kukufanya uamue kuwa na mpenzi mmoja na utumie kondomu kila mara.<br />
Sura ya 10<br />
Kujali na Kuhudumia afya yako ya kijinsia<br />
Magonjwa ya zinaa au maambukizo yatokanayo na ngono ni maambukizo ambayo yanaenea<br />
kwa njia ya kujamiiana. Yanaenea kwa njia ya majimaji ya watu wawili kama vile shahawa,<br />
majimaji ya ukeni na damu.<br />
Magonjwa mengi ya zinaa yanatibika, lakini bado yanaweza kuharibu via vya uzazi na<br />
kufanya mtu asizae. Dalili za magonjwa ya ngono ni pamoja na:-<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Vidonda, malengelenge, uvimbe na vipele sehemu za siri.<br />
Usaha kutoka kwenye uume.<br />
Usaha wenye rangi ya ajabu na harufu mbaya kutoka ukeni.<br />
• Maumivu wakati wa kujamiiana au wakati wa kukojoa.<br />
Magonjwa mengine ya ngono hayatibiki. UKIMWI ni mmojawapo wa magonjwa ya ngono<br />
ambayo hayatibiki. VVU husababisha upungufu wa kinga mwilini. Maambukizo ya VVU<br />
yanasababisha UKIMWI. (Upungufu wa Kinga Mwilini) Ugonjwa huu unasababisha kinga ya<br />
mwili (mfumo wa kinga mwilini dhidi ya magonjwa) ushindwe kufanya kazi. hakuna dawa ya<br />
kuzuia maambukizo ya VVu, na hakuna dawa ya kutibu uKiMWi.<br />
haiwezekani kumtambua mtu mwenye maambukizo ya VVu kwa kumwangalia tu. Mtu<br />
anaweza kuwa na afya yake kwa muda mrefu kabla dalili hazijaanza kujitokeza. Mtu anaweza<br />
asifahamu kama amepata maambukizo kwa miaka kadhaa. usije ukadhani kwamba mtu<br />
hana VVu, na usije ukadhani kwamba mtu anavyo VVu. ni muhimu kupima.<br />
Iwapo una wasiwasi kuhusu magonjwa ya ngono, ni jambo jema kwenda kupima na kupata<br />
matibabu kama yanatakiwa. Usije ukajitibu mwenyewe na dawa na wala usichangie dawa na<br />
mtu mwingine.<br />
Iwapo utafahamu kwamba umepata maambukizo ya VVU, pata ushauri. Usijaribu kukabili<br />
tatizo hili peke yako. Kama utajitunza vizuri unaweza kuwa na afya nzuri na kuishi maisha<br />
yenye manufaa.<br />
Zipo njia zitakazokuepusha kupata maambukizo ya magonjwa ya ngono pamoja na VVU:-<br />
•<br />
•<br />
SURA YA 10 | KUTUNZA AfYA YAKO YA KIUJINSIA<br />
Acha kabisa kujamiiana. Ishia kubusu na kukumbatiana tu.<br />
Iwapo umeshaanza kujamiiana tumia kondomu kila mara ili kujikinga. Hakikisha unajua<br />
jinsi ya kutumia kondomu kiusahihi.<br />
Siyo kweli kwamba matatizo yote yaliyopo kwenye via vya uzazi ni magonjwa ya ngono. Yapo<br />
maambukizo kama kandidiasisi na maambukizo ya njia ya mkojo ambayo hayasababishwi na<br />
kujamiiana. Haya husababisha pia matatizo katika sehemu za siri. Kwa ujumla, maambukizo<br />
haya yanaweza kuepukwa kwa kuimarisha usafi sehemu za siri. Iwapo unasikia maumivu au<br />
muwasho sehemu za siri mwone mhudumu wa afya.<br />
127
128<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Mimba inatokana na watu wawili, mwanaume na mwanamke. Wote wawili wanawajibika. Sura<br />
hii haihusu wasichana peke yao. Wavulana wanatakiwa kusoma pia. Mimba na kuzuia mimba<br />
zisizotakiwa ni wajibu wenu wote wawili msichana na mvulana.<br />
MiMba inatOKeaje?<br />
Mimba na uzuiaji wa<br />
mimba<br />
Mwanamume na mwanamke watakapofanya<br />
ngono isiyo na kinga, kuna uwezekano wa<br />
mwanamke kupata mimba. Mwanamume<br />
anapokojoa shahawa ndani ya uke, shahawa<br />
hizo zinaingia kwenye uke na kuogelea kwenda<br />
kwenye mlango wa mfuko wa kizazi. Zikitoka<br />
kwenye mfuko wa kizazi zitaogelea hadi kwenye<br />
mirija ya kupitisha yai na hapo zinaweza kuishi<br />
kwa muda wa siku 3 hadi 5<br />
Kama yai litakuwa limeshaingia kwenye mirija<br />
ya kupitisha yai au litafika hapo katika kipindi<br />
cha siku 3 hadi 5, moja ya mbegu za kiume<br />
inaweza kuliingia yai na kulirutubisha. Seli mpya<br />
ijulikanayo kama Zaigoti inaundwa ikiwa ni<br />
muungano wa yai na mbegu ya kiume. Zaigoti<br />
hugawanyika sehemu mbili kutengeneza seli<br />
mbili zinazofanana. Seli mbili hizi zinagawanyika<br />
kufanya seli 4, nazo seli nne zinagawanyika mara<br />
mbili kutengeneza seli 8, na kuendelea. Mara<br />
kibonge cha seli nyingi kinatokea.<br />
Kibonge cha seli kinasafiri kutoka kwenye mirija<br />
ya kupitishia yai kwenda kujishikiza kwenye<br />
kuta za mfuko wa kizazi. Kitendo cha seli<br />
kujishikiza kwenye ukuta wa mfuko wa kizazi<br />
kinaitwa “Upandikizaji”. Upandikizaji unatokea<br />
wiki 3 baada ya hedhi yako ya mwisho. Huu ndio<br />
mwanzo wa mimba.<br />
Mbegu za kiume zikiogelea kwenye ukuta wa<br />
tumbo la uzazi kwenda kwenye yai<br />
Mwanzo wa mimba: yai lililoovushwa<br />
likipandikizwa kwenye ukuta wa tumbo la uzazi<br />
129<br />
SURA YA 11
130<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Kumbuka kuwa mimba inaweza kutokea kama utafanya ngono isiyo salama mara moja tu.<br />
Mimba inaweza kutokea kama mwanamume atakojoa shahawa zake karibu na uke hata kama<br />
hamkujamiiana! Shahawa zikimwagwa nje ya mlango wa uke bado zinaweza kuogelea hadi<br />
kwenye mlango wa mfuko wa uzazi hadi kwenye tumbo la uzazi na kwenye mirija ya kupitisha yai.<br />
Utadhani hakuna uwezekano, lakini inatokea.<br />
Dalili Za MiMba<br />
Dalili ya wazi kuwa mimba imetungwa ni kukosa kupata hedhi. Hii ni kwa sababu ukuta wa mfuko<br />
wa kizazi hautoi damu mwanamke akiwa na mimba. Utando laini unabaki ndani ya mfuko wa<br />
kizazi na unatengeneza kiota laini kwa ajili ya mtoto kukua. Kukosekana kwa hedhi haina maana<br />
kuwa umepata mimba. Wasichana waliobalehe wanaweza kuwa na hedhi isiyo ya kawaida. Kwa<br />
miaka mingi siku za hedhi kwa baadhi ya wasichana balehe, zinaweza kuchelewa au zikakosekana<br />
mwezi mzima bila sababu yoyote.<br />
Dalili nyingine za mimba:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Matiti kuwa laini<br />
Kichefuchefu (hali ya kutaka kutapika) na kuwa na mate mdomoni.<br />
Uchovu (kujisikia umechoka sana)<br />
Kutaka kukojoa mara kwa mara<br />
Kupendelea kula vitu fulani,wakati mwingine visivyo vya kawaida.<br />
Wanawake wachache huwa hawaoni dalili zozote kati ya hizo hapo juu. Kwa mfano, wanawake<br />
wengine hutoa damu kidogo sana wakati wa miezi mitatu ya mwanzo ya mimba zao na hivyo<br />
wanaweza kufikiri hedhi imekuwa na damu kidogo kuliko kawaida.<br />
Kama huna uhakika kuwa umepata au hujapata mimba, unaweza kufanya kipimo cha mimba.<br />
Katika sehemu nyingine, unaweza kununua kipimo cha mimba kwenye maduka ya dawa. Vilevile,<br />
unaweza kufanyiwa kipimo cha mimba kwenye kliniki. Mara nyingine kipimo kinafanywa kwa<br />
kupima mkojo na unaweza kugundua viini fulani ambavyo vinatengenezwa na mwili wakati wa<br />
mimba. Dakitari au nesi wa kituo cha afya anaweza vilevile akakufanyia uchunguzi wa mwili ili<br />
kuona kama una mimba au la.<br />
Mimba inachukuwa wiki 40 kabla ya mtoto kuzaliwa(toka mwanzo wa hedhi yako ya mwisho).<br />
Hadi utakapokosa hedhi yako - kama siku 28 baada ya siku ya mwisho ya siku zako za hedhi<br />
iliyopita - kibonge cha seli nyingi, yaani kiinitete kitakuwa kinakua katika mfuko wa kizazi kwa<br />
karibu wiki nzima.<br />
Kiinitete kinakua haraka sana. Wiki sita baada ya hedhi yako ya mwisho, ubongo na uti wa<br />
mgongo vinakuwa vimeanza kutengenezwa na moyo unaanza kupiga. Katika wiki 9 kiinitete<br />
kinaitwa fitasi. Katika wiki ya 12 fitasi inatambulika kama binadamu ila inakuwa na kichwa<br />
kikubwa. Katika wiki 20 (miezi 5) mwanamke anaweza akajisikia fitasi inachezacheza au<br />
kuzunguka ndani ya tumbo lake. Fitasi inaweza kugeuka au kusogea na inaweza pia ikashituka<br />
kukiwa na kelele zenye sauti ya juu.<br />
SURA YA 11 | MIMBA NA UZUIAJI WA MIMBA<br />
Ukuaji na maendeleo ya mtoto ndani ya tumbo la uzazi<br />
hataRi Za MiMba na uZaZi KWa WaSichana balehe<br />
Mimba ni hatari kwa kila mwanamke lakini ni hatari zaidi kwa wasichana balehe. Tatizo kubwa<br />
kwa wasichana chini ya miaka 20 ni nyonga. Mifupa inayozunguka mfereji wa kutolea mtoto<br />
haujakua vizuri. Wasichana wanaopata mimba katika umri mdogo wanapata taabu katika kuzaa<br />
kwa sababu mlango wa uzazi kwenye mifupa ya nyonga ni midogo mno na mtoto hawezi kupita.<br />
Tatizo hili linaitwa uzazi wa kukwama.<br />
Kama mtoto hawezi kutoka nje inabidi mtoto atolewe kwa njia ya upasuaji. Vijijini, wanawake<br />
wengi wenye matatizo kama haya huwa hawawezi kufika hospitali kwa muda unaotakiwa. Mtoto<br />
anaweza kufia tumboni. Isitoshe mfuko wa kizazi unaweza kuchanika kwa sababu ya kipindi<br />
kirefu cha uchungu na mwanamke anaweza kufa kwa kuvuja damu nyingi. Hii ni sababu mojawapo<br />
inayowafanya wasichana balehe wengi wadogo kufa wakati wa kuzaa.<br />
131
132<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Uchungu wa muda mrefu unaweza kusababisha matatizo mengi. Baada ya saa nyingi za uchungu,<br />
kichwa cha mtoto kinaweza kunyoosha au kuchana uke, na kusababisha shimo kati ya uke na<br />
kibofu cha mkojo au kati ya uke na mkundu. Shimo hili linaitwa Fistula. Kwa sababu ya shimo<br />
hilo, msichana au mwanamke hawezi kuzuia mkojo au kinyesi. Mkojo au kinyesi wakati wote<br />
vitakuwa vinavuja kupitia shimo hilo na kushuka chini ya miguu. Matokeo yake msichana au<br />
mwanamke atakuwa ananuka vibaya na anaweza kuvimba miguu kutokana na mwasho wa mara<br />
kwa mara unaosababishwa na mkojo kwenye ngozi. Katika jamii zingine msichana au mwanamke<br />
wa aina hiyo hutengwa na jamii. Jibu pekee ni kumtafuta mganga mtalaamu wa upasuaji kuweza<br />
kuziba shimo. Inaweza kuwa vigumu kumpata mtalaamu wa operesheni hii, na siyo mara zote<br />
inafanikiwa.<br />
Pia kutokana na uchungu wa muda mrefu kwa wasichana wadogo kuna hatari ya kupungukiwa<br />
damu (damu dhaifu), kupata shinikizo la damu na kifafa cha mimba. Mambo haya yanaweza<br />
kusababisha uchovu, maambukizo ya magonjwa, kuumia na kifo. Wasichana wadogo pia wako<br />
hatarini kuzaa kabla ya wakati wake au kuzaa watoto wenye uzito wa chini kuliko inavyotakiwa.<br />
Kupunguza hatari ya matatizo haya unahitaji kujitunza vizuri wakati wa ujauzito mimba isije<br />
ikaharibu mwili wako na kukusababishia ulemavu wa maisha.<br />
KuStahiMili MiMba KatiKa uMRi<br />
MDOGO.<br />
Miezi tisa ya mimba ni muda wa uchovu<br />
mkubwa kwa mwili wa msichana. Kinaweza<br />
pia kuwa kipindi cha msongo na uchovu.<br />
Hata kwa wasichana walioolewa ambao<br />
wanataka kuanzisha familia, kipindi cha<br />
mimba ni kipindi ambacho matunzo maalumu<br />
yanahitajika.<br />
Kupata mtoto kwa msichana asiyeolewa<br />
kunaweza kukawa na matatizo mengi<br />
mbalimbali. Mara nyingine familia ya<br />
msichana inaweza kutoa msaada na<br />
kumsaidia katika hali ngumu aliyonayo.<br />
Kwa wasichana wengi,mimba inamaanisha<br />
mwisho wa masomo yao<br />
Watamsaidia kulea mtoto, watampeleka shule kumalizia masomo yake. Ni jambo zuri sana<br />
familia wanapotoa msaada. Lakini kwa bahati mbaya, si jambo la kawaida.<br />
Mara nyingi, mimba isiyotakiwa inasababisha msururu wa matukio. Wazazi wa msichana<br />
wanaweza ama kumwachisha shule kwa sababu ya kukasirishwa na kukatishwa tamaa, anaweza<br />
kupigwa na kufukuzwa nyumbani au anaweza kutishwa mno na vitisho vya wazazi wake akaamua<br />
kutoroka yeye mwenyewe. <strong>Maisha</strong> yake yanakuwa ni ya huzuni, maisha ya baadaye ya mtoto<br />
yatakuwa hatarini, kwa vile amezaliwa na msichana mwenye huzuni ambaye hakuwa tayari kulea.<br />
Wasichana wengi wanaokabiliwa na mimba zisizotakiwa wanajaribu kuzitoa kinyume cha sheria.<br />
Pamoja na kwamba wanajua kutoa mimba ni hatari, wanapendelea kuhatarisha maisha yao kuliko<br />
kufukuzwa shuleni au nyumbani. Kila mwaka barani Afrika, maelfu ya wasichana wanakufa au<br />
wanaharibu viungo vyao vya uzazi kwa sababu ya kutoa mimba zisizo salama. Katika nchi nyingi<br />
za Afrika kutoa mimba ni kinyume cha sheria (soma zaidi mwisho wa sura hii).<br />
SURA YA 11 | MIMBA NA UZUIAJI WA MIMBA<br />
Wakati mwingine mvulana aliyempa mimba msichana anaweza<br />
kupata matatizo pia. Anaweza kupigwa na baba au kaka wa msichana.<br />
Anaweza kufukuzwa shuleni au kwenye jamii. Anaweza kulazimishwa<br />
kumwoa msichana na kumtunza mtoto na hivyo hataweza kuendelea<br />
na masomo yake na malengo yake ya kazi. Pengine atalazimika kulipa<br />
faini kubwa kwa wazazi wa msichana.<br />
Ukigundua unakabiliwa na mimba isiyotakiwa, usijihukumu<br />
mwenyewe, na usijaribu kuikabili hali hiyo kimyakimya. Mtafute mtu<br />
yeyote anayeweza kukusaidia kufanya uamuzi mzuri uzungumze naye.<br />
Katika hali hiyo usifanye uamuzi wa haraka bila kutafuta maelezo na<br />
ushauri unaotakiwaau bila kufikiri kwa makini uchague lipi.<br />
Japo itaonekana ni vigumu, ni muhimu kuwataarifu wazazi wako<br />
au walezi kuhusu hiyo mimba. Utahitaji msaada wao wakati huu na<br />
baadaye, hasa kama utahitaji kuendelea na masomo. Unayo haki ya<br />
kupata elimu lakini unaweza kuhitaji msaada wa watu wengine ili<br />
urudi shuleni.<br />
Je, unajua kuwa mvulana naye anawajibu kuhusu mimba?<br />
Usijaribu kukaa kimya<br />
unapopata mimba.<br />
Unahitaji matunzo<br />
mengi na msaada.<br />
Wavulana wengi hawafikirii kuhusu uwezekano wao kuwa baba wakati wanapojamiiana. Hata<br />
hivyo, watu wawili wanahusika ili kupata mimba na kwa hiyo mvulana anao wajibu sawa na<br />
msichana.<br />
Kama umekwishaanza kujamiiana unatakiwa kuwajibika na kuwa mwangalifu. Usitegemee<br />
kalenda kwamba ni njia inayoweza kukusaidia kujikinga wewe na rafiki yako wa kike. “Hakuna<br />
siku salama kwa wasichana balehe”. Unaweza kumpa mimba kwa urahisi rafiki yako wa kike na<br />
mimba ya utotoni inaweza kuwa hatari na ikahatarisha maisha na afya ya rafiki yako wa kike.<br />
Inaweza kuwa vibaya pia kwa maisha yake ya baadaye, na maisha yako pia kwa kulazimishwa<br />
kuacha masomo ili umtunze mtoto. Kwa hiyo, usifanye mambo ya hatari kijinsi. Kama ukiamua,<br />
fanya ngono salama kama kukumbatiana au hakikisha kwamba wewe na rafiki yako wa kike<br />
mnatumia njia za kuzuia mimba vizuri kila mnapojamiiana. Ni afadhali kuwa mwangalifu<br />
kimwenendo, kimatendo, kifedha na vyovyote inavyowezekana kuliko kujutia baadaye.<br />
Kama utakuwa baba bila kutarajia, kubali kuwajibika kwa vitendo vyako. Jifikirie kama<br />
baba mwenye wajibu na tenda kama baba. Zungumza na rafiki yako wa kike kuhusu jinsi<br />
utakavyosaidia kumtunza mtoto. Muulize jinsi utakavyoweza kusaidia ili aweze kuilea vema<br />
mimba yenu (kama vile kumsindikiza kliniki, kumsaidia kazi n.k). Hata kama wewe na msichana<br />
hamna uhusiano wa karibu, usimkimbie, zungumza naye jinsi utakavyohusika katika maisha ya<br />
mtoto.<br />
Unatakiwa pia kuwa mwazi kwa wazazi wako kuhusu jambo hili na waeleze wakusaidie katika<br />
mazungumzo ya kushirikiana na wajibu wa kumlea mtoto na matunzo ya mama na mtoto. Zaidi<br />
ya yote usirudie kufanya kosa kama hilo tena.<br />
133
134<br />
KujitunZa WaKati Wa ujauZitO<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Kwa sababu mimba inaleta uchovu mkubwa katika mwili wako na ni hatari kwa afya yako ni vizuri<br />
upate matunzo yanayofaa.<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Anza kwenda kliniki ya wazazi mapema unapojijua umepata mimba; usingoje hadi mimba<br />
ionekane. Sababu za kuwepo kliniki ya wazazi ni kuhakikisha wewe na mtoto wako mko<br />
katika hali nzuri. Kliniki ya wazazi ni muhimu kuweza kutambua matatizo mapema na<br />
kuyatibu mapema.<br />
Jiwekee utaratibu. Fuata ratiba ya kwenda kliniki ya<br />
wazazi.<br />
Nenda mara nyingi kadiri wakunga watakavyokwambia.<br />
Tumia chandarua ili kujikinga na malaria.<br />
Pata mapumziko kwa wingi<br />
Fikiria utakula nini na hakikisha unakula vyakula vya<br />
kujenga mwili kama maharage na mayai. Kula matunda<br />
kwa wingi na mboga za majani. Utahitaji vilevile madini<br />
kama kalsiamu. Kalsiamu inapatikana katika maziwa<br />
lakini ile yenye gharama nafuu inapatikana toka kwenye<br />
samaki wadogo wanaoliwa na miiba yake (dagaa).<br />
Pata madini ya ziada ya chuma yanayotolewa hospitalini au kliniki. Mwili wako unahitaji<br />
madini ya chuma kwa wingi ili uwe na nguvu na afya wakati wa ujauzito.<br />
Hakikisha unakwenda kliniki ya akina mama na unapata chanjo za lazima mapema.<br />
MiMba na VVu<br />
cissy kutoka uganda (umri wa miaka 17)<br />
“Haikuwa rahisi mara ya kwanza nilipogundua nilikuwa na mimba. Sikuwahi<br />
kufikiria ingeliweza kunitokea. Nilizungumza na rafiki yangu wa<br />
karibu akanishauri nionane na mshauri ambaye alinisihi nisitoe mimba,<br />
kitu nilichotaka kufanya. Niliwapoteza marafiki zangu, lakini niliyakubali<br />
makosa yangu, na sasa nina mtoto wa kike. Sitakubali kurudia tena kosa”.<br />
Hakikisha unakwenda kliniki ya akina<br />
mama na unapata chanjo za muhimu<br />
mapema.<br />
Ni muhimu mno kujikinga dhidi ya maambukizo ya ugonjwa wa UKIMWI wakati una mimba na<br />
baadaye wakati unanyonyesha. Hii ni kwa sababu ukiambukizwa nyakati hizi, kuna uwezekano<br />
wa kumwambukiza mtoto VVU. Sisitiza matumizi ya kondomu na mwenzi wako. <strong>Wewe</strong> na mwenzi<br />
wako mnaweza kwenda kupima VVU pamoja. Kama mmoja wenu au wote mna VVU, mnatakiwa<br />
kutumia kondomu wakati wote mnapojamiiana. Iwapo wote vipimo vitaonyesha hamna VVU<br />
mnatakiwa kuwa waminifu na kuendelea kutumia njia ya uzazi wa mpango ya chaguo lenu ikiwa ni<br />
pamoja na kutumia kondomu.<br />
Ukigundua una VVU wakati wa ujauzito, mwambie daktari. Siku hizi kuna dawa ambayo unaweza<br />
kutumia ukiwa mjamzito ili kupunguza maambukizi kwa mtoto. Kwa kawaida, karibu asilimia 30<br />
ya watoto waliozaliwa na mama walio na virusi vya UKIMWI / VVU wanakuwa wameambukizwa<br />
VVU. Lakini kwa kutumia dawa, unaweza kupunguza hatari ya maambukizo hayo.<br />
Vilevile unatakiwa kuzungumza na tabibu wako kuhusu kunyonyesha mtoto kwa sababu kuna<br />
hatari ya kumwambukiza VVU kupitia kwenye maziwa ya mama. Huduma za dawa za kupunguza<br />
makali ya VVU kwa mama wajawazito zinapatikana. Watoa huduma katika vituo vya tiba<br />
wanaweza kukueleza jinsi mpango wa huduma hizo ulivyo katika ngazi ya Wilaya.<br />
MaanDaliZi Ya KujiFunGua<br />
Kama kijana balehe, unatakiwa kufanya maandalizi ya kujifungulia mtoto hospitalini ambako<br />
wapo wataalamu wa kutosha na vifaa vya kutosha kuweza kushughulikia matatizo yoyote<br />
yanayoweza kujitokeza.Usijaribu kujifungulia nyumbani au kwa wakunga wa jadi. Jitahidi kadiri<br />
iwezekanavyo kujifungulia katika kituo cha afya chenye vifaa bora, mahali ambapo wanaweza<br />
wakafanya upasuaji kuondoa mtoto kupitia tumboni kama italazimu.<br />
Mkunga au mwanamke wa makamo atakushauri vitu unavyovihitaji kwa ajili ya mtoto wako<br />
kama: nepi, nguo na blanketi. Hii itategemea sehemu unayoishi na utaratibu wa afya wa nchi<br />
hiyo. Unaweza kuhitajiwa upeleke vifaa kama pamba, glavu za plastiki, wembe mpya, sirinji<br />
mpya, sindano, sabuni na dawa za kuua wadudu. Unaweza kulazimika kuandaa usafiri wa kwenda<br />
hospitali.<br />
Jaribu kuwa na mwanamke wa makamo mwaminifu wakati wa kipindi cha uchungu, pengine mama<br />
yako mzazi, dada yako mkubwa au shangazi. Hii inaweza kukuliwaza na kukusaidia kwani uchungu<br />
unaweza kuchukua muda mrefu. Mkunga anaweza asiwe na wewe muda wote.<br />
Je, unafahamu kuwa wanawake waliokeketwa wana mahitaji<br />
maalumu wakati wa kujifungua?<br />
Tohara ya wanawake ambayo pia inajulikana kama “female genital mutilation (FGM)” inaweza<br />
kusababisha matatizo ya kipekee kwa wanawake wenye mimba. Tohara mbaya sana ni<br />
“mfyato/ ufyataji”, ambayo uke unashonwa na linaachwa tundu dogo tu kwa ajili ya mkojo na<br />
damu ya hedhi kupita. Tundu hilo lazima lifunguliwe wakati wa kuzaa mtoto ili kichwa cha<br />
mtoto kiweze kupita. Utaratibu huu, lazima ufanywe na mtaalamu wa mambo ya afya ili kuzuia<br />
matatizo zaidi. Makovu yatokanayo na tohara yanaweza vilevile kusababisha viungo vya uzazi<br />
kuchanika wakati wa kuzaa, kwa sababu ngozi haiwezi kutanuka kirahisi. Damu nyingi inaweza<br />
kuvuja.<br />
Kama mtoto hawezi kutoka, inawezekana kukawa na matatizo makubwa. Wakati mtoto<br />
amezuiwa, kuta za uke, kibofu au mkundu vinaweza kupasuka. Kutokana na hali hiyo mkojo na<br />
kinyesi vinaweza kuwa vinavuja wakati wote kupitia ukeni. Wanawake wengi wametengwa na<br />
wenzi wao kwa sababu ya harufu mbaya.<br />
nini cha kufanya.<br />
SURA YA 11 | MIMBA NA UZUIAJI WA MIMBA<br />
Jiandae mapema kwa ajili ya kujifungua. Wakati wa nusu ya kipindi cha pili cha mimba,<br />
unatakiwa umwone mkunga kwenye kituo cha afya ambaye amesomea kuzalisha wanawake<br />
waliotahiriwa. Mkunga anaweza akakueleza kama kuna hatari ya kupata matatizo, au uke<br />
unatakiwa kuongezwa. Panga kuzalia katika mazingira mazuri ya afya. Kujifungulia mtoto<br />
nyumbani ni hatari mno.<br />
135
136<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
KujitunZa na KuMtunZa MtOtO baaDa Ya KujiFunGua<br />
Kama ulivyokuwa unakwenda kliniki kabla ya<br />
kujifungua, hakikisha unakwenda tena kwa uchunguzi<br />
baada ya kujifungua. Kama ulimzalia mtoto wako<br />
nyumbani hakikisha unakwenda kliniki kwa ajili<br />
ya uchunguzi ndani ya siku tatu. Kama ulimzalia<br />
mtoto wako hospitalini nenda baada ya wiki sita ili<br />
mkunga aone kama tumbo lako linarudia hali yake<br />
ya awali. Mkunga anatakiwa pia kuangalia kama<br />
huna maambukizo ya magonjwa au hutokwi na damu<br />
sana.Kama ulipoteza damu nyingi wakati wa kuzaa<br />
mkunga atakupa dawa za madini ya chuma ili kusaidia<br />
kuongeza damu.<br />
Mkunga anaweza vilevile kujibu maswali mengi<br />
utakayokuwa nayo kuhusu kunyonyesha mtoto, kulala,<br />
kinga kwa mtoto, kuzuia mimba na mambo mengine.<br />
Mwanamke aliyezaa kwa mara ya kwanza mara nyingi<br />
anakuwa na maswali mengi hivyo kuongea na mkunga<br />
inaweza kukusaidia.<br />
KuhaRibiKa MiMba<br />
Mara nyingine mimba huwa inaharibika/inatoka yenyewe tu. Tunasema mimba imetoka kwa<br />
bahati mbaya. Fitasi inakufa na inatoka kupitia ukeni. Malaria au magonjwa ya ngono huweza<br />
kusababisha kuharibika mimba. Mimba inaweza kutoka vilevile kama fitasi ina matatizo.<br />
Kama mimba itakuwa imetoka mwanamke anahitaji kumwona mhudumu wa afya ili kuhakikisha<br />
hapati maambukizo kwenye tumbo la uzazi. Mhudumu wa afya anaweza pia akatambua<br />
kilichosabisha mimba kutoka na kutoa matibabu ya magonjwa kama ya ngono.<br />
Mimba inaweza vilevile kutolewa kwa makusudi kwa kupitia taratibu za kitabibu. Mimba inaweza<br />
kutolewa na mganga aliyesomea katika mazingira ya hali ya usafi. Kutoa mimba ni utaratibu<br />
salama kitabibu kwa ujumla na ni salama kuliko kuzaa. Katika nchi nyingi za Kiafrika ni kosa la<br />
jinai kutoa mimba isipokuwa katika mazingira ya matatizo kama kubakwa au kujamiiana kwa<br />
maharimu (ndugu wa karibu) au wakati ambapo maisha ya mwanamke yako hatarini kwa ajili<br />
ya mimba au fitasi si ya kawaida na hata akizaliwa mtoto hataishi. Uthibitisho wa kitabibu<br />
unatakiwa kuwepo kuwa mhusika alibakwa kulikuwepo kujamiiana kwa maharimu au fitasi si ya<br />
kawaida.<br />
Kutoa mimba kinyume cha sheria katika nchi nyingi barani Afrika ni hatari sana. Kutoa mimba<br />
kunafanywa katika mazingira machafu na ya hatari na mara nyingi watu wengi wanaotoa<br />
mimba hawajasomea. Kwa sababu kutoa mimba hakuruhusiwi, mtoaji mimba anaweza kutoa<br />
bila utaratibu, kwa haraka na kuogopa na katika mazingira na vifaa vichafu. Mambo yote haya<br />
yanamuweka mwanamke katika hatari kubwa. Kwa hakika, katika nchi nyingi za Afrika, robo ya<br />
vifo vya wanawake wajawazito vinasababishwa na matatizo ya ama mimba kutoka au kutoa<br />
mimba.<br />
SURA YA 11 | MIMBA NA UZUIAJI WA MIMBA<br />
Kutoa mimba kwa kutumia njia isiyo salama<br />
kunaweza kusababisha matatizo ya kiafya.<br />
Kifaa cha kutolea mimba kikiingizwa kwenye<br />
mlango wa mfuko wa kizazi kinaweza<br />
kikasababisha uharibifu kwenye kibofu<br />
cha mkojo au utumbo mdogo au mlango<br />
wa mfuko wa kizazi. Mfuko wa kizazi<br />
ulioharibika utatakiwa uondolewe. Maana<br />
yake, msichana hataweza kupata mtoto tena.<br />
Kutoa mimba kusiko salama vilevile<br />
kunaweza kusababisha kuvuja damu,<br />
maambukizo ya magonjwa na kifo. Kuingiza<br />
kifaa cha kutolea mimba kwenye mlango<br />
wa mfuko wa kizazi na kizazi kunaweza<br />
kusababisha kuvuja sana damu na msichana<br />
anaweza akavuja damu mpaka akafa. Miti<br />
shamba na vifaa vingine vinavyotumika<br />
kuanzisha uchungu mara nyingi siyo safi;<br />
vinaweza kuleta vijidudu vya maradhi katika<br />
mfuko wa kizazi. Kizazi na mirija ya kupitisha<br />
mayai ya mgonjwa vinaweza kuathirika sana<br />
kiasi cha kusababishiwa ugumba au kifo. Miti<br />
shamba, dawa au kemikali ambazo msichana<br />
anameza zinaweza kumfanya awe mgonjwa<br />
sana na anaweza akawa amejipa sumu<br />
mwenyewe.<br />
Je unajua matokeo ya utoaji mimba usio<br />
salama?<br />
Jane alipopata mimba alikuwa na miaka 15<br />
na alikuwa Kidato cha Tatu. Alitaka sana<br />
kuendelea na shule, aliishi na shangazi yake,<br />
ambaye alimpeleka kwa mtu aliyedai ni<br />
mganga anayefanya kazi kwenye hospitali<br />
kubwa mjini Kampala. Mtu huyu aliingiza<br />
kifaa kwenye uke. “Maji” yakatoka. Alisikia<br />
maumivu makali sana, lakini aliambiwa asilie<br />
kwa sababu hata hivyo “alitaka” mwenyewe<br />
kilichomtokea. Shughuli ilichukua dakika 15.<br />
Alirudi nyumbani na alitokwa na damu wiki<br />
nzima, akidhoofu kidogokidogo kila siku.<br />
Tumbo lake liliuma na uke ukawa unatoa<br />
majimaji yenye harufu mbaya. Baadaye<br />
alipelekwa kliniki inayohudumia vijana. Kliniki<br />
waligundua amechanika sehemu kubwa ya<br />
mfuko wa kizazi. Ilibidi afanyiwe upasuaji<br />
na kukaa hospitalini kwa muda wa wiki nne<br />
kutibu kidonda na maambukizo ya magonjwa.<br />
Jane bado hajui iwapo ataweza kupata watoto<br />
baadaye.<br />
Diana kutoka uganda (umri wa miaka 15)<br />
“Kutoa mimba ni hatari sana hasa kwa kutumia miti shamba. Ni<br />
afadhali usishiriki katika ngono kabisa”.<br />
nedina kutoka uganda (umri wa miaka 18)<br />
“Rafiki yangu wa kike akipata mimba nitamkatisha tamaa asitoe<br />
mimba kwa sababu ni hatari. Nitamsihi azae na kisha aendelee na<br />
masomo yake hapo baadaye”<br />
Kutoa mimba kunaweza kuleta matokeo ya kusikitisha kijamii. Watu wengine wakijua kwamba<br />
msichana ametoa mimba, anaweza kufukuzwa shule, kutoaminika au kufedheheshwa na marafiki<br />
au na familia.<br />
Hata hivyo, wasichana wengi wanaishia kutoa mimba kwa njia isiyo salama wanapojikuta<br />
wamepata mimba. Wanasahau hatari za kutoa mimba kwa sababu ya hofu, familia zao<br />
zitakapogundua ujauzito wao. Wanakata tamaa ya kuendelea na masomo. Marafiki zao wa kiume<br />
wanaweza kuwa wamewaacha au kuwalazimisha watoe mimba.<br />
137
138<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Utoaji mimba usio salama ni hatari sana. Unaweza kupoteza maisha yako.<br />
Kama wewe au yeyote unayefahamu anakabiliwa na mimba isiyotakiwa, tafuta msaada. Kuwa<br />
mwaminifu kwa wazazi /walezi kuhusu hali hiyo. Kama wazazi wako hawakusaidii tembelea kituo<br />
cha vijana na mwombe mshauri wa vijana ushauri kuhusu suala lako. Mwombe mshauri wa vijana<br />
akuelekeze wapi unaweza kwenda kuzungumza na mhudumu wa afya anayejali na mpole.<br />
Kama wewe au yeyote unayemjua alitoa mimba na hajisikii vizuri, nenda hospitali haraka. Kuvuja<br />
damu, homa ya baridi, homa na/au kutoka majimaji yenye harufu ni dalili kwamba kuna mahali<br />
pana matatizo makubwa. Afya yako na maisha yako yapo hatarini hivyo uchunguzi wa waganga<br />
ni muhimu sana. Hata kama sheria ni kali kiasi gani, wahudumu wa afya wana miiko ya kitalaamu<br />
ya kumsaidia yeyote atakayekuwa na matatizo. Usiache woga ukuzuie kupata matibabu na<br />
hatimaye ukapoteza uhai.<br />
Njia nzuri ya kujikinga mwenyewe dhidi ya matokeo ya kutoa mimba kwa njia isiyo salama ni<br />
kukwepa kupata mimba isiyopangwa ama kuepuka ngono nzembe.<br />
naMna Ya KuePuKa KuPata MiMba<br />
Njia ya uhakika kabisa ya kutopata mimba ni kuacha kufanya ngono. Uzuiaji huu una uhakika wa<br />
asilimia 100, na ni salama kihisia na kimwili. Kama hujamiiani, hakuna jinsi unavyoweza kupata<br />
mimba au kumpa mimba msichana.<br />
Ikiwa unajamiiana, hakikisha pia kuwa wewe na mwenzi wako mnatumia kondomu kujikinga dhidi<br />
ya mimba na magonjwa ya ngono. Unatakiwa pia kuomba msaada kutoka kliniki ya uzazi wa<br />
mpango. Unahitaji kuchukuwa hatua ili mwenzi wako asipate mtoto ambaye huwezi kumtunza<br />
kwa wakati huu.<br />
Kuna aina nyingi za dawa za kuzuia mimba ambazo ni salama kabisa kwa vijana (angalia<br />
kisanduku ukurasa wa 140). Njia yoyote utakayotumia, hakikisha unaitumia inavyotakiwa. Kwa<br />
mfano, kusahau kumeza kidonge kunaweza kusababisha upate mimba.<br />
SURA YA 11 | MIMBA NA UZUIAJI WA MIMBA<br />
je, ViDOnGe VYa KuZuia MiMba ni SalaMa?<br />
Uvumi kama huu ni uwongo na si wa<br />
kisayansi. Tangu miaka ya 1950, mamilioni<br />
kwa mamilioni ya wanawake wametumia<br />
dawa za vidonge za kuzuia mimba. Vidonge<br />
vya kuzuia mimba vimefanyiwa uchunguzi<br />
mkubwa katika historia ya dawa. Kwa<br />
kuyafuatilia maisha ya maelfu ya wanawake<br />
kwa miaka mingi waganga sasa wanajua<br />
kwamba vidonge vya kuzuia mimba havileti<br />
saratani. Uwezekano wa wanawake<br />
wanaomeza vidonge kupata saratani ya<br />
kokwa la mayai na uwezekano wa kupata<br />
saratani kwenye ngozi laini ya kuta za<br />
tumbo la uzazi ni mdogo kuliko wanawake<br />
ambao hawajawahi kutumia vidonge hivyo.<br />
Kuna uvumi mwingine kwamba kutumia vidonge vya kuzuia mimba wakati wa ujana balehe<br />
kunaweza kuharibu kokwa la mayai na kusababisha isiwezekane kupata mimba baadaye. Huu pia<br />
ni uzushi.Mwongozo wa kimataifa wa kutumia dawa za kuzuia mimba unasema vidonge ni vizuri<br />
kwa wanawake ambao bado hawajapata watoto. Ukweli ni kwamba ,mara nyingine vinatumika<br />
kuwasaidia vijana balehe kuwapunguzia maumivu makali wakati wa hedhi. Huhitaji kuwa na<br />
mtoto kwanza ndipo uanze kumeza vidonge. Vidonge havitaharibu kokwa la mayai.<br />
Wasichana na wanawake wengine wanapata kichefuchefu, matiti kuwa laini na kuongezeka<br />
uzito wanapoanza kumeza vidonge. Matokeo haya huwa yanatoweka baada ya mwezi mmoja au<br />
zaidi. Karibu wanawake wadogo na wanawake wa makamo wote wanaweza kumeza vidonge. Ni<br />
wanawake wa makamo tu ambao wanaovuta sigara, walio wanene sana au wanashinikizo la damu<br />
au magonjwa fulani kwenye mfumo wao wa damu wanashauriwa wasitumie njia ya homoni kuzuia<br />
mimba (vidonge vya kuzuia mimba, sindano na vipandikizi). Unatakiwa kumwona mtoa huduma ili<br />
akupime kama huna vidokezo vya mteja wa dawa za kuzuia mimba.<br />
KuZuia MiMba KWa DhaRuRa<br />
christine kutoka uganda (umri wa miaka 18)<br />
“Nimesikia kwamba vidonge vya kuzuia mimba vinasababisha<br />
saratani au pia ulemavu kwa mtoto”.<br />
Kuna njia moja zaidi ya kuzuia mimba ambayo hapana budi kuijua. Hii ni njia ya dharura ya kuzuia<br />
mimba. Njia ambayo unaweza kuitumia kuzuia mimba haraka baada ya kufanya ngono isiyo<br />
salama. Kwa mfano kama ulisahau kutumia kondomu au kama kondomu ilipasuka au ilitoka kwa<br />
bahati mbaya (jambo ambalo ni nadra sana kama ikitumika vizuri).<br />
Kinga ya dharura ya kuzuia mimba imeanza kupatikana sehemu nyingi siku hizi. Kama ukifanya<br />
ngono bila kinga na una wasiwasi wa kupata mimba unaweza kwenda kwa muhudumu wa afya na<br />
kumwomba kinga ya dharura ya kuzuia mimba. Ikiwa umebakwa omba kinga ya dharura ya kuzuia<br />
mimba kutoka kwenye kliniki ya mpango wa uzazi au kituo cha vijana karibu na wewe katika<br />
kipindi cha saa 72 (siku 3).<br />
139
140<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Je, unajua njia zipi za kuzuia mimba ambazo ni salama kwa vijana?<br />
Njia zote hizi za kuzuia mimba ni salama kwa vijana:<br />
Kondomu: Kondomu ni mpira laini ambao huwekwa kwenye uume<br />
uliosimama kabla ya kujamiiana. Mwanaume anapotoa shahawa (“anafikia<br />
mshindo”) zinanaswa nchani mwa kondomu. Majimaji toka kwa mwanaume<br />
hayamwingii mwanamke na majimaji toka kwa mwanamke hayagusi uume<br />
wa mwanaume. Kondomu zinatoa kinga nzuri dhidi ya magonjwa ya ngono, pamoja na VVU/ UKIMWI<br />
na huzuia mimba. Bei ya kondomu ni ndogo na zinawasaidia wanaume wengine kuchelewa kutoa<br />
shahawa mapema.<br />
Vidonge: Vidonge vina kiasi kidogo sana cha homoni. Homoni hii huzuia uovishaji<br />
kutoka kwenye makokwa ya mayai. Mwanamke aliyeingia kwenye hedhi<br />
anapomeza kidonge lakini kidonge kinafanya hedhi ya mwanamke kuwa nyepesi<br />
na maumivu kuwa mepesi. Pia matokeo ya kuzuia mimba kwa kutumia vidonge<br />
ni mazuri sana, lakini lazima umeze kila siku. Ukikosa kumeza zaidi ya siku moja<br />
unaweza kupata mimba kwa sababu rutuba inarudi pindi unapoacha kumeza<br />
vidonge. Vidonge havizuii VVU au mangojwa mengine ya zinaa. Kwa hiyo, ni vizuri<br />
iwapo unatumia kondomu, uwe na mwenzi mmoja tu na wote muwe mmepima na kuthibitisha hamna<br />
magonjwa ya ngono/VVU.<br />
Sindano: Sindano ina homoni ambazo zinazuia yai kurutubishwa. Huanza<br />
kufanya kazi katika muda wa saa 24 na hutoa kinga dhidi ya mimba kwa<br />
muda wa miezi mitatu. Kudunga sindano ni rahisi kwa sababu huhitaji<br />
kukumbuka kumeza kidonge kila siku au kufanya chochote kabla ya<br />
kujamiiana. Sindano pia inatunza siri, hakuna anayeweza kujua kwamba<br />
unatumia mtindo huu kwa kuzuia mimba. Sindano zinafanya siku zako za<br />
hedhi ziwe nyepesi na zenye maumivu kidogo ambapo zinaweza kuwasaidia<br />
vijana wanaopata maumivu au hedhi nzito. Unapoacha kudunga sindano, huwi na rutuba tena mara<br />
moja, kwa sababu homoni zinakaa mwilini kwa muda . Wanawake wengi wanakuwa na rutuba tena<br />
ndani ya mwaka mmoja wanapoacha kutumia sindano, lakini wengine wanapata mimba mapema.<br />
Sindano hazizuii magonjwa ya zinaa/VVU hivyo zinafaa tu kama unatumia kondomu au kama unaye<br />
mwenzi mmoja na wote mmepima magonjwa ya ngono/VVU.<br />
Vipandikizi: Vipandikizi ni vimrija vidogo vinavyowekwa ndani ya ngozi kwenye<br />
mkono chini kidogo ya bega. Vimirija hivyo huwa vinatoa homoni inayozuia yai<br />
kurutubishwa. Kama ilivyo kwa sindano huhitaji kukumbuka kumeza vidonge<br />
au kufanya lolote kabla ya kujamiiana. Vipandikizi vinadumu miaka mitano.<br />
Lakini vinaweza kuondolewa mapema. Ni kinga nzuri sana kuzuia mimba, lakini<br />
haizuii magonjwa ya zinaa/VVU. Kwa hiyo unatakiwa kutumia kondomu au kuhakikisha kuwa wewe na<br />
mwenzi wako hamna magonjwa ya ngono/VVU.<br />
Dawa ya kuulia mbegu za kiume (vidonge mafuta au krimu na povu): Dawa<br />
hizi zinaua mbegu za mwanaume kabla hazijaingia ndani ya mfuko wa kizazi,<br />
lakini hazimuumizi mwanaume au mwanamke. Zipo aina mbalimbali za dawa<br />
na zinaingizwa ukeni kabla ya kujamiiana. Dawa hizi zitumike na kondomu kwa<br />
sababu zina kinga ndogo sana dhidi ya magonjwa ya zinaa/VVU. Zaidi ya hapo,<br />
hazina kinga madhubuti kama ya vidonge au sindano katika kuzuia mimba.<br />
Tofauti na vidonge na sindano, huhitaji kuzipata kutoka kwa mhudumu wa afya; unaweza kupata moja<br />
kwa moja toka kwenye maduka ya dawa. Hii inaweza kuwa bahati kama una aibu kwenda kliniki, lakini<br />
kumbuka kutumia kondomu.<br />
Unapotumia vidonge vya dharura inakubidi umeze kiasi cha mchanganyiko wa vidonge vya kuzuia<br />
mimba baada ya saa 12 katika kipindi cha saa 72 za kufanya ngono bila kinga. Kinga ya dharura ya<br />
kuzuia mimba haifanyi kazi mimba inapokuwa imetungwa. Ndio maana ni muhimu kuipata haraka<br />
baada ya ngono isiyo na kinga. Usijaribu kunywa dawa hizi bila ushauri wa mhudumu wa afya<br />
mwenye ujuzi.<br />
KinGa MaRa Mbili<br />
SURA YA 11 | MIMBA NA UZUIAJI WA MIMBA<br />
Je, unafahamu kuwa wanawake waliokeketwa wana mahitaji<br />
Kuchomoa/kurusha: Kuchomoa au kurusha ni wakati mwanaume anatoa uume nje ya uke<br />
kabla ya kukojoa shahawa. Njia hii sio salama kwa sababu wanaume wengi hawawezi kuutoa<br />
uume kwa wakati unaotakiwa. Mara nyingi wanaume hawajui kwamba wanakaribia kukojoa<br />
mpaka wanapokuwa wamekaribia sana. Pia, matone machache ya shahawa yanaweza kutoka<br />
kabla ya kukojoa na matone machache haya yanatosha kusababisha mimba. Kuchomoa<br />
hakuleti kinga dhidi ya VVU/UKIMWI na magonjwa mengine ya zinaa.<br />
“Siku salama”: Wanawake wengine wanasubiri siku ambazo wanajua kwamba hawana rutuba.<br />
Utaratibu huu unafaa kwa wanawake ambao hedhi zao ni za kawaida na wenzi wao wana<br />
ushirikiano. Wasichana wa umri mdogo wengi hawana hedhi za kawaida hivyo si rahisi kujua<br />
siku salama. Kama ilivyo kwa njia ya kuchomoa, siku salama hazileti kinga dhidi ya magonjwa<br />
ya zinaa/VVU.<br />
Kitanzi: Kitanzi kinatumbukizwa kwenye tumbo la uzazi na mhudumu wa afya. Ni rahisi<br />
kukiingiza kwa mwanamke ambaye amewahi kuzaa, kwa hiyo haipendekezwi kwa vijana.<br />
Kitanzi kinaweza kusababisha ugonjwa wa ngono ukue na kufikia hali ya kutisha. Kwa vile<br />
vijana ni rahisi sana kuambukizwa magonjwa ya zinaa, wasitumie kitanzi. Kitanzi hakitoi kinga<br />
dhidi ya magonjwa ya zinaa/VVU.<br />
Kufunga kizazi: Kukata au kufunga mirija ya kupitishia mbegu ya wanaume na wanawake ni<br />
njia ya kudumu ya kuzuia mimba. Unafanyika upasuaji ambapo mirija ya kupitishia shahawa na<br />
yai inazibwa. Njia hii inawahusu wanaume na wanawake ambao wanafikiri wamepata idadi ya<br />
watoto inayowatosha. Njia hii haifai kwa vijana kwa sababu huwezi kupata watoto baada ya<br />
upasuaji. Kufunga kizazi hakutoi kinga dhidi ya magonjwa ya zinaa/VVU.<br />
Ugonjwa wa UKIMWI umebadilisha mawazo ya watu wengi kuhusu njia za kuzuia mimba.<br />
Zamani watu walilenga katika kuangalia ni njia zipi zinaleta matokeo bora katika kuzuia mimba.<br />
Hawakujali sana kama njia ya kuzuia mimba ilitoa kinga dhidi ya magonjwa ya zinaa/VVU.<br />
Leo mambo ni tofauti. Kupata VVU ni maafa makubwa kuliko kupata mimba isiyotakiwa. Siku<br />
hizi watu wanazungumzia kuhusu kinga mara mbili. Kinga mara mbili ni wakati unatumia njia<br />
ambayo matokeo yake hupunguza hatari ya mambukizo ya magonjwa ya zinaa/VVU/UKIMWI, na<br />
wakati huohuo, unatumia njia nyingine ambayo matokeo yake ni mazuri katika kukinga mimba<br />
zisizotakiwa.<br />
Angalia njia mbalimbali hapa chini uone jinsi zinavyotoa kinga dhidi ya mimba na magonjwa<br />
mengine ya ngono pamoja na VVU.<br />
141
142<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Hata hivyo, njia pekee nzuri ya kujikinga ni kuacha kujamiiana au kuacha zinaa. Lakini kama<br />
unavyoweza kuona hapo juu, yeyote ambaye anajamiiana, njia nzuri ya kuzuia mimba ni kutumia<br />
vipandikizi, sindano na kondomu.<br />
Stabisile kutoka Zimbabwe (umri wa miaka 19)<br />
“Kama mwanamume anakataa kutumia kondomu, huyo anapoteza<br />
muda.<br />
” cathy kutoka uganda (umri wa miaka 17)<br />
“Ninapendekeza matumizi ya kondomu ili kukwepa maambukizo<br />
ya VVU/UKIMWI, magonjwa ya zinaa na kuzuia mimba<br />
zisizotakiwa”.<br />
Kondomu ni nzuri kwa kuzuia mimba, na zinakusaidia kukukinga wewe na mwenzi wako dhidi ya<br />
magonjwa ya zinaa/UKIMWI. Unaweza kufanya ziwe kinga nzuri zaidi kwa kuchanganya vidonge<br />
na njia nyingine ya kuzuia mimba.<br />
iwapo yeyote anasema hataki kutumia kondomu jiandae kwa jibu zuri! na jiandae kuondoka kama<br />
atakataa kutumia kondomu.<br />
Sura ya 11<br />
Mimba na uzuiaji wa mimba<br />
Wakati wote mwanaume na mwanamke wakijamiiana bila kinga, mimba inaweza kutokea.<br />
Mimba inaweza ikatokea mara ya kwanza tu mnapojamiiana bila kinga.<br />
Mimba inaweza kutungwa kama mbegu moja inakutana na yai na kulirutubisha ndani ya<br />
mwanamke. Kama yai litarutubishwa, linajishikiza kwenye kuta za mfuko wa kizazi. Huu ndio<br />
mwanzo wa mimba.<br />
Dalili za mimba ni pamoja na:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Kukosa siku zako za hedhi<br />
Kujaa na kuuma kwa matiti<br />
Kichefuchefu<br />
Kuwa mchovu<br />
SURA YA 11 | MIMBA NA UZUIAJI WA MIMBA<br />
Kutaka kukojoa mara kwa mara.<br />
Mimba ni hatari hasa kwa wasichana balehe kwa sababu miili yao bado haijakomaa.<br />
Wasichana wadogo wanakabiliwa na matatizo makubwa ya afya wakati wa mimba na wakati<br />
wa kuzaa kuliko wanawake wa makamo. Kwa hiyo, ni jambo la muhimu hasa kwa msichana<br />
mdogo kupata matunzo sahihi wakati wa mimba. Inashauriwa kuzalia hospitalini mahali<br />
ambapo kuna wahudumu wa afya wa kutosha na vifaa vinavyoweza kumudu matatizo yoyote<br />
ya uzazi.<br />
Wasichana balehe wengi wanapata mimba kwa makosa. Wanaamua kutoa mimba kwasababu<br />
wanataka kuendelea na shule au kwa sababu hawataki kuwaaibisha wazazi wao. Hata hivyo,<br />
katika nchi nyingi za Afrika kutoa mimba ni kinyume cha sheria na si salama hata kidogo.<br />
Kutoa mimba kusiko salama kunaweza kusababisha matatizo makubwa kiafya, kuanzia<br />
maambukizo ya magonjwa, uharibu wa via vya uzazi, kuvuja damu sana, ugumba na vifo. njia<br />
sahihi ya kukwepa mimba ni kuacha ngono. Kuacha kabisa ni salama kwa asilimia 100.<br />
Iwapo unashiriki kujamiiana, wewe na mwenzi wako mnatakiwa wakati wote kujikinga dhidi<br />
ya mimba na magonjwa ya ngono pamoja na VVU/UKIMWI. Njia zote za kuzuia mimba ni<br />
salama kwa vijana.<br />
Kama umesahau kutumia kinga ya mimba au kama kondomu itatoka au kupasuka, nenda<br />
haraka kwenye kliniki waombe kinga ya dharura ya kuzuia mimba. Inaweza kuzuia mimba<br />
ikiwa itatumika katika kipindi cha saa 72 cha kujamiiana bila kinga.<br />
Mimba inahusu watu wawili yaani mwanamume na mwanamke. Wavulana na wanaume pia<br />
watu wazima, wote wanalo jukumu la kuzuia mimba.<br />
143
144<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Ngono ya kulazimishwa na<br />
Ngono bila ya ridhaa yako<br />
Wakati mwingine watu yaani wanaume kwa wanawake na wavulana kwa wasichana wanajamiiana<br />
huku kiukweli hawapendi kufanya hivyo. Wanaweza kushinikizwa na rafiki wa kiume au kike<br />
kujamiiana kama ushahidi wa mapenzi yao. Wanaweza kushinikizwa kufanya ngono ili kulipa<br />
zawadi au pesa walizopokea. Au wanaweza kulazimishwa kujamiiana na mtu ambaye ni mkubwa<br />
au ana nguvu zaidi.<br />
Ngono isiyotakiwa ni hatari. Itakuweka katika hatari ya kupata mimba na magonjwa ya ngono<br />
ikiwa ni pamoja na UKIMWI. Vilevile, inakuweka katika hatari ya kupata magonjwa ya hisia.<br />
Unaweza kupata maumivu makali sana ya kihoro iwapo utajamiiana bila ridhaa yako.<br />
Njia nzuri ya kukwepa ngono za namna hii ni<br />
kuyakimbia mazingira mabaya yanayoweza<br />
kusababisha ukaingia katika mtego.<br />
ShiniKiZO KutOKa KWa RaFiKi Wa<br />
KiuMe au Wa KiKe<br />
Wakati mwingine wavulana wanawaambia wasichana<br />
wajamiiane kama ushahidi wa mapenzi yao. Vilevile,<br />
wasichana wanawaambia wavulana vivyohivyo.<br />
Watu wengine wanafikia hatua ya kutishia kuvunja<br />
uhusiano pindi mwenzi atakapokataa kujamiiana.<br />
Inaweza kuwa vigumu iwapo mtu unayempenda na<br />
kumjali akikwambia mjamiiane. Unaweza kudhani<br />
njia pekee ya kuendeleza urafiki ni kumkubalia<br />
mfanye ngono. Unaweza kudhani ni vema kumkubalia<br />
kwa sababu unamjali na unataka afurahi.<br />
Ngono kamwe isitumike kama ushahidi wa<br />
mapenzi.<br />
145<br />
SURA YA 12
146<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Katika mazingira kama haya, inaweza kuwa vigumu sana kujua tofauti ya kile anachokitaka na<br />
kile wewe unachokitaka. Ni rahisi kuchanganyikiwa lipi ni sahihi kwako.<br />
Iwapo rafiki yako wa kiume au wa kike anashinikiza mjamiiane, fikiria maswali yafuatayo:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Unathamini nini? Je, unaamini kwamba ni sahihi kujamiiana wakati huu katika maisha yako?<br />
Au je, huoni ni vyema usubiri mpaka baadaye, kama vile utakapoolewa au kuoa?<br />
Unajisikia vizuri kuhusu wazo la kujamiiana au wazo hilo linakufanya ukose raha?<br />
Unajisikia kama unaweza kukataa kujamiiana au hili linaenda kinyume na kile unachofikiri<br />
ni sahihi kwa msichana au mvulana kufanya? Kwa mfano, katika maeneo mengine, ni vigumu<br />
sana msichana kusema “HAPANA” kwa mvulana au mwanaume kwa sababu amefundishwa<br />
kwamba wakati wote anatakiwa kuwa mnyenyekevu kwa mwanaume. Katika maeneo<br />
mengine inaweza kuwa vigumu sana kwa mvulana kusema “HAPANA” kwa sababu amelelewa<br />
kuamini kwamba mwanaume wakati wote anatakiwa kujamiiana. Hivyo mtu anaweza kuhisi<br />
kwamba kwa kusema hapana inaweza kuleta matatizo.<br />
Unafikiri mwenzi wako ataendelea kukupenda na kukuheshimu kama ukikataa?<br />
Majibu ya maswali haya yatakueleza mengi kuhusu kama ujamiaane au usijamiiane na rafiki<br />
yako. Uwe msichana au mvulana, wote mnayo haki ya kukataa kujamiiana. Ni wewe unayetakiwa<br />
kufanya uamuzi mwenyewe kuhusu kujamiiana. Kama huamini kwamba ngono inakufaa wakati<br />
huu wa maisha yako, usifanye; bila hata kujali rafiki yako wa kiume au kike anasema nini.<br />
Kama hujisikii kufurahia wazo la ngono na hauko tayari kufanya, usifanye. Iwapo unafikiria rafiki<br />
yako wa kike au wa kiume hatakupenda ukikataa kujamiiana, ukweli ni kwamba hakupendi kama<br />
atakuchukia. Hakuna mtu ambaye anakupenda kweli atakulazimisha kufanya jambo ambalo<br />
unahisi ni baya kwako.<br />
Iwapo huna uhakika kama rafiki yako wa kike au wa kiume atakuwa na wewe ukikataa kujamiiana,<br />
labda jambo la maana la kufanya ni kusubiri na kuona. Mwambie rafiki yako kwamba unampenda<br />
lakini umeamua kwamba hauko tayari kujamiiana. Kama akisema ni sawa, basi unaweza ukatuliza<br />
moyo na kutulia. Unaweza kufurahia uhusiano wenu mzuri bila kukimbilia kufanya ngono.<br />
Hata hivyo, iwapo rafiki yako wa kike au kiume ataamua kukuacha, hii inaweza kuwa ngumu kwa<br />
sababu inakuonyesha kwamba rafiki yako alikuwa hakupendi. Unaweza kujisikia una huzuni na<br />
mpweke. Unaweza kufikiri ulifanya uamuzi usio sahihi, lakini hukufanya! Ulifanya kilichokuwa<br />
sahihi kwako. Katika kufanya uamuzi ukakuta rafiki yako wa kiume au wa kike alitaka kukutumia<br />
na wala hakuwa anakujali, bila shaka uvumbuzi huu utakuhuzunisha, lakini ni afadhali kuvumbua<br />
mapema kwani ingekuwa vibaya zaidi kama ungegundua baada ya kujamiiana.<br />
ShiniKiZO KutOKa KWa Watu WaZiMa<br />
Wakati mwingine watu wazima ikiwa ni pamoja na waliooa au kuolewa, wanawalazimisha vijana<br />
kufanya ngono. Mara nyingi wanaume, watu wazima (wazee) wanapenda kuwa na uhusiano wa<br />
kimapenzi na wasichana wadogo.<br />
SURA YA 12 | NGONO YA KULAZIMISHWA NA NGONO BILA YA RIDHAA YAKO<br />
Wakati mwingine vilevile wapo wanawake watu<br />
wazima wanaopenda kuwa na uhusiano wa<br />
kimapenzi na wavulana wa umri mdogo.<br />
Mara kwa mara mtu mzima hutoa zawadi, pesa<br />
au huduma maalumu kwa kijana. Mtu mzima<br />
anaweza kutoa pesa kwa ajili ya karo, nguo au<br />
peremende. Iwapo mtu mzima ni kama mwalimu<br />
au dereva wa basi, anaweza kuahidi kumpa<br />
alama nzuri au kumpakia kwenye gari bure.<br />
Lakini zawadi zote hizi siyo bure. Baada ya<br />
muda mtu mzima atadai “malipo” kwa zawadi<br />
alizotoa. Kawaida kijana “atalipa” kwa njia ya<br />
ngono.<br />
effie Kutoka Kenya ( umri wa miaka 16)<br />
“Nilikuwa na rafiki yangu ambaye alikuwa na umri wa miaka<br />
15. Rafiki yangu alikuwa na uhusiano na mtu mzima ambaye<br />
alikuwa anampa kila alichotaka, na mama yake alifahamu kuhusu<br />
uhusiano huo na wala hakujali. Siku moja akiwa anaelekea shuleni<br />
aliona gari la mzee huyo. Aliamua kumpa lifti mpaka shuleni,<br />
lakini wakiwa njiani kuelekea shuleni yule mwanaume alipita njia<br />
nyingine na akampeleka msichana kwenye nyumba ya kulala<br />
wageni na akajamiiana naye kwa nguvu”.<br />
Ingawa inaweza kufurahisha kuona mtu mzima anavutiwa na wewe na inaweza kukufanya ujisikie<br />
unapendeza na ni wa maana, uhusiano wa namna hii ni mbaya sana. Unaweza kuwa hatari kwako<br />
kwa vile:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Unaweza kupata maambukizo ya magonjwa ya<br />
zinaa, VVU/UKIMWI na mimba.<br />
Unaweza kukatisha masomo yako.<br />
Unaweza kuwa chanzo cha hasira kwa mke wake<br />
au mume wake ambaye anaweza kukushambulia<br />
au kukudhuru.<br />
Umri unapopishana sana na kipato kinapotofautiana,<br />
vilevile uhusiano hauwi sawa. Unaweza kujisikia<br />
huna mamlaka. Unaweza kuogopa kusema hapana<br />
unapoombwa ngono kwa sababu unajua ulichukua<br />
pesa au zawadi. Unaweza vilevile kuogopa<br />
kumwambia mtu mzima kutumia kondomu.<br />
Huu ni uhusiano wa hatari sana unaweza kuharibu<br />
maisha yako ya baadaye au milele!<br />
Watu wazima wanaweza kukupatia pesa au<br />
zawadi kwa ajili ya ngono. uhusiano huu ni<br />
hatari kwako<br />
KWa nini unaniPa<br />
MiMi hiZi PeSa?<br />
SitaZichuKua!<br />
aSante.<br />
Kataa kupokea zawadi na pesa. usijiingize<br />
katika deni na mtu.<br />
147
148<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Unaweza kushawishika kuingia katika uhusiano na mtu mzima, hususani kama huna pesa za<br />
matumizi na wazazi wako hawawezi kukununulia vitu vya kukufurahisha na vilivyo vizuri. Hata<br />
hivyo, hakuna zawadi au kiasi cha pesa chenye thamani ya gharama utakayolipa.<br />
Iwapo mtu mzima, mwanaume au mwanamke anajaribu kukupatia zawadi au pesa na anashinikiza<br />
mjamiiane, kuwa jasiri. Sema “hapana” na ondoka bila kuchelewa. Waeleze wazazi au shangazi<br />
au mjomba au mwelimisha rika kilichotokea. Waombe wakusaidie uweze kuimudu hali hiyo.<br />
Usijaribu kutatua peke yako.<br />
Vijana wengine wanaingizwa katika uhusiano wa namna hii na wazazi wao. Hii ni kwa sababu<br />
wazazi ni maskini na hawawezi kulipa karo, chakula, nguo na vitu vingine. Hali kama hii ni ngumu<br />
kwa kijana yeyote. Iwapo utakuwa katika mazingira kama haya unahitaji kufikiri kiubunifu:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Ni nani unaweza kumwendea kwa ajili ya msaada? Unaweza kuzungumza na ndugu wengine<br />
kama vile shangazi, mjomba, babu, bibi au kaka au dada? Huenda wakakulipia karo au<br />
wakawasaidia wazazi wako kufanikisha yote. Unaweza kuzungumza na mtu yeyote ndani<br />
ya jamii, kama vile mtu wa kanisani, msikitini au kutoka kituo cha vijana? Hawa wanaweza<br />
kufahamu namna ya kutatua tatizo lako.<br />
Je, unaweza kuzungumza na mwalimu au mkuu wa shule? Waulize namna unavyoweza<br />
kulishughulikia tatizo lako. Pengine wanaweza kukusaidia kwa kukusamehe karo au kwa<br />
kukupatia kazi ya kufanya shuleni ili uweze kulipa karo.<br />
Je, unaweza kupata pesa? Unaweza kufanya kazi, kama kuuza mboga, karanga, bisi au<br />
peremende baada ya shule ili kupata pesa?<br />
Wapo watu wengine wanaokuzunguka ambao wanaweza kukusaidia ikiwa watajua tatizo lako.<br />
Kwa hiyo omba msaada na usijaribu kulitatua peke yako.<br />
unYanYaSaji KijinSia<br />
Margaret kutoka Zimbabwe (umri wa miaka 17)<br />
“Kitu kimoja ninachojua kuhusu wanaume ni kwamba wengi<br />
huwania kujifurahisha na mtu wa jinsi nyingine, na katika kufanya<br />
hivyo wanaweza kukuahidi hazina zote za maisha. Kwa<br />
hiyo, nimesema HAPANA kwa wanaume wengi na nitaendelea<br />
kufanya hivyo.”<br />
neema kutoka Kenya (umri wa miaka 15)<br />
“Alikuwepo mfanyabiashara mmoja aliyekuwa anajaribu<br />
kufanya urafiki na mimi lakini nilikataa. Mwanaume huyo alikuwa<br />
anawatuma wasichana wengine kujaribu kunishawishi,<br />
lakini nilikataa.”<br />
Aina yoyote ya kuguswa au kushikwashikwa kimapenzi bila ridhaa ya anayetendewa hivyo ni<br />
unyanyasaji kijinsia. Inaweza ikawa kushikwa matiti au sehemu za siri. Inaweza vilevile ikawa<br />
kujamiiana. Aina yoyote ya kukutana kimapenzi bila ya kupenda ni unyanyasaji pia.<br />
SURA YA 12 | NGONO YA KULAZIMISHWA NA NGONO BILA YA RIDHAA YAKO<br />
Unyanyasaji kijinsia mara nyingi unafanywa na<br />
mtu mzima anayemjua kijana na ana madaraka juu<br />
yake. Mtu mzima anaweza kuwa jirani, rafiki wa<br />
familia, mwalimu, kiongozi wa dini au kiongozi wa<br />
jamii. Mtu mzima anaweza akawa ndugu, kama vile<br />
mzazi, mzazi wa kambo, mjomba au shangazi, kaka<br />
au dada.<br />
Unyanyasaji kijinsia unaweza kuhusisha tishio,<br />
rushwa, udanganyifu, ujanja na vurugu. Mtu mzima<br />
anaweza kukutishia, au mtu mzima anaweza<br />
kukupatia zawadi ili kukufanya utoe ushirikiano.<br />
Mtu mzima anaweza pia kukudanganya au<br />
kukutegea ufanye jambo. Mtu mzima anaweza<br />
kukutishia kukudhuru wewe au familia yako iwapo<br />
utamwambia mtu yeyote kuhusu unyanyasaji<br />
kijinsia. Mtu mzima anaweza kukuchanganya akili<br />
kwa kusema uhusiano utakuwa wa siri.<br />
Unyanyasaji kijinsia ni jambo baya sana na linaweza kukufanya uchanganyikiwe. Hapa kuna<br />
mambo machache ya kuyaweka maanani:-<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Mwili wako ni wako.<br />
Unayo haki ya kuamua nani akushike, akushike vipi na wakati gani.<br />
Kugusana kwa aina yoyote kusikokubalika ni<br />
unyanyasaji kijinsia.<br />
Mtu yeyote asiangalie au kukushika sehemu zako za siri kwa namna ambavyo utajisikia<br />
vibaya.<br />
Amini hisia zako kuhusu kuguswa na amua nini kilicho chema kwako. Usimsikilize mtu<br />
anayejaribu kukushawishi vinginevyo.<br />
Mtu akikugusa ambavyo hupendelei, sema “hapana” kwa nguvu na kwa sauti. Kuwa jasiri.<br />
Tafuta mtu wa kumweleza kuhusu tukio. Ongea na mzazi, shangazi au mjomba, babu, bibi, rafiki,<br />
mwalimu au mama wa rafiki yako. Pata msaada.<br />
iwapo yupo mtu anakunyanyasa kijinsia au anakushinikiza ufanye naye ngono, tafuta msaada. Ongea<br />
na wazazi au mtu mwingine anayejali.<br />
149
150<br />
KuDhaliliSha KijinSia<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Unyanyasaji kijinsia hauishii katika kushikashika au kugusa mwili. Wakati mwingine matusi ya<br />
nguoni na utazamwaji wa kifuska vinaweza kumfanya mtu ajisikie vibaya.<br />
Aina yoyote ya kitu kisichovutia kijinsia unaitwa udhalilishaji kijinsia. Mifano ya udhalilishaji<br />
kijinsia ni:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Kumwita msichana “mchafu”,anajirahisisha au mkarimu kwa sababu tu ya uvumi kwamba<br />
amekuwa na wapenzi wengi.<br />
Kupiga miluzi au kutoa maoni juu ya mwonekano wa mtu anapopita mbele yako.<br />
Utani wa kimapenzi kama vile utani kuhusu matiti au mwili wa msichana.<br />
Udhalilishaji kijinsia unaweza kutokea mahali popote – shuleni, mtaani, sokoni, kanisani au<br />
nyumbani.Udhalilishaji kijinsia mara nyingi unatokea kwenye mabasi wakati wa kwenda shuleni<br />
au wakati wa kurudi nyumbani. Wadhalilishaji wanaweza kuwa wageni au watu unaowafahamu,<br />
kama mwalimu, jirani, ndugu au mtu mnayefanya naye kazi au mwanafunzi.<br />
Udhalilishaji kijinsia ni jambo zito. Maneno tu yanaweza kuharibu heshima yako. Yanaweza<br />
kukufanya ujisikie kudhalilika na kukosa raha. Yanaweza vilevile kukufanya uogope.<br />
Kuogopa kwa sababu ya kudhalilishwa kijinsia ni jambo la kawaida na la asili. Hisia hizi ni silika<br />
inayokueleza uwe mwangalifu. Watu wanaotoa maneno mabaya kijinsia, kwa vyovyote vile<br />
hawajali hisia zako. Hawajali kama yanakuumiza. Maneno machafu ya kijinsia yanaweza kuwa ni<br />
onyo kwamba, jambo baya zaidi linakuja.<br />
Njia nzuri ya kumudu udhalilishaji kijinsia ni kuwaepuka watu wanaotoa maneno machafu ya<br />
kijinsia. Usionyeshe unaogopa. Kuwa mtulivu na mwenye kujiamini, na ondoka sehemu hiyo.<br />
Jaribu kuepuka hali kama hii baadaye. Kwa mfano, kama kuna mtu anakusumbua unapokwenda<br />
shuleni, jaribu kubadilisha njia au muda unaokwenda.<br />
Njia nyingine za kumudu udhalilishaji kijinsia ni pamoja na:<br />
•<br />
•<br />
Kutojilaumu. Kumbuka, hakuna mwenye haki ya kukunyanyasa kwa vile unavyoonekana,<br />
ulivyovaa au tabia yako ya mapenzi iliyopita.<br />
Kuongea na mtu. Usinyamaze kimya; zungumza na mzazi, shangazi, mjomba, mwelimishaji<br />
rika au mwalimu unayemwamini. Waombe wakusaidie kuishughulikia hali hiyo.<br />
ubaKaji<br />
Ubakaji ni kitendo cha kutumia nguvu ambacho mtu analazimishwa kujamiiana.Waathirika wa<br />
ubakaji mara nyingi ni wanawake, hata hivyo, wakati mwingine wavulana na wanaume wanabakwa<br />
vilevile.<br />
Ubakaji ni kitendo cha kulazimisha, utumiaji wa nguvu, kufedhehesha na ukatili. Watu wengi<br />
wanadhani kwamba wabakaji ni wageni wenye vurugu. Hata hivyo hili ni jambo ambalo sio la<br />
kawaida, kubakwa na mtu asiyejulikana ni mara chache sana. Wengi waliobakwa wanawafahamu<br />
SURA YA 12 | NGONO YA KULAZIMISHWA NA NGONO BILA YA RIDHAA YAKO<br />
waliowashambulia. Kawaida mshambuliaji anaweza kuwa ni rafiki wa kiume, jirani, ndugu au rafiki<br />
wa familia.<br />
beth kutoka Kenya (umri wa miaka 15)<br />
“Ilikuwa tarehe 16 mwezi wa Novemba nilipomtembelea rafiki<br />
yangu. Hakuwa mpenzi wangu, alikuwa rafiki wa kawaida. Kawaida<br />
nilikuwa ninaenda huko na kukaa naye siku nzima. Lakini siku<br />
hiyo alibadilika. Alinivutia kitandani na tukaanza kupambana.<br />
Alitaka kunilazimisha tujamiiane lakini nilikataa. Baadaye alianza<br />
kusema maneno matamu na hakutaka kunisikiliza. Kisha niliruka<br />
pembeni na kumweleza kwamba sitaki nipate mimba kwa sababu<br />
mimi ningali mdogo. Nilitoka nje ya nyumba nikimuaga kwa heri.<br />
Tangu siku hiyo sijarudi tena kwenye nyumba ya mvulana huyo.”<br />
Ubakaji mwingi kwa vijana ni ule wa miadi na rafiki yako na ule wa watu uliowazoea. Ubakaji<br />
wa aina hii hutokea pale rafiki wa kiume anapomlazimisha rafiki wa kike wajamiiane bila ya<br />
ridhaa yake. Pengine walikuwa wanakumbatiana na kubusiana lakini baadaye rafiki wa kiume<br />
akamlazimisha msichana wajamiiane.<br />
Ulikuwa unafahamu kwamba mambo mengi yanayozungumzwa<br />
kuhusu ubakaji siyo ya kweli?<br />
Kuna uzushi kuhusu ubakaji kama ifuatavyo:<br />
• Wasichana wanafurahia. hii siyo kweli! Ubakaji unatisha na unaleta kihoro. Unaumiza<br />
kimwili na kihisia. Hakuna mtu ambaye anaweza kufurahia kubakwa.<br />
•<br />
•<br />
Wasichana wanaomba kubakwa wanapovaa nguo zinazochochea ashiki au<br />
wanapotembea kwa namna ya kuchochea ashiki. Siyo kweli! Hakuna mtu anayeomba<br />
kubakwa.<br />
Mwanaume hawezi kushitakiwa kwa vile msichana au mwanamke alikuwa amemchochea<br />
kwa nguo yake fupi au kwa kukaa kifuska. Siyo kweli! Wanaume wote wanao uwezo wa<br />
kudhibiti hamu ya kujamiiana. Wale wanaosema hawawezi, wanadanganya na lazima<br />
waadhibiwe.<br />
• Msichana au mwanamke akisema “hapana” ukweli anamaanisha “ndiyo”. Siyo kweli!<br />
Mwanamke akisema “hapana” anamaanisha “hapana” Hamaanishi “ndio” au “labda”.<br />
•<br />
Iwapo msichana au mwanamke amebakwa, yeye ndiye wa kulaumiwa kwa sababu<br />
angeweza kuzuia. uongo! Mwathirika kamwe hawezi kulaumiwa. Mbakaji anawajibika<br />
kwa kubaka na ana makosa. Kamwe usimlaumu aliyebakwa.<br />
Ubakaji wa miadi na ule wa watu uliowazoea ni ubakaji wa kutumia nguvu, unaumiza, unakosesha<br />
raha na ni makosa. Hata kama mvulana na msichana walikuwa wanaelewana, mvulana hana haki<br />
ya kumlazimisha msichana kufanya zaidi ya kile anachotaka.<br />
151
152<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Hata kama wameshawahi kujamiiana kabla, lakini kwa sasa msichana hataki, mvulana hana haki<br />
ya kumlazimisha. Hata kama msichana alikuwa anavaa nguo zinazochochea ashiki, mvulana hana<br />
haki ya kumlazimisha. Katika mazingira yote haya, kitendo cha mvulana kubaka ni kosa la jinai.<br />
naana kutoka Ghana (umri wa miaka 16)<br />
“Rafiki yangu alijamiiana kwa sababu rafiki yake wa kiume<br />
alimlazimisha. Hakutaka kujamiiana lakini hakuwa jasiri kwa<br />
sababu mpaka rafiki yake anafikia kushika matiti yake hakukataa.<br />
Kwa hiyo, kijana aliendelea na kumwingilia na akashika<br />
mimba.”<br />
Wakati mwingine wasichana wanaonyesha ishara zinazochanganya. Wanaweza kujionyesha<br />
kama vile wanafurahia kinachotokea, kwa hiyo mvulana anakuwa haelewi ni wakati gani anasema<br />
hataki aendelee zaidi. Hata kama msichana hatoi ishara za wazi, mvulana hana haki ya kumbaka.<br />
Kamwe kubaka si adhabu halali kwa msichana ambaye alikuwa anatoa ishara zinazochanganya.<br />
Wavulana wengine ambao wanawabaka marafiki zao wa kike wana imani potofu kwamba<br />
mwanaume atafanya kile anachotaka bila ya kujali msichana anataka nini. Wavulana wengine<br />
wana imani potofu kwamba wasichana wanaposema “hapana” wanamaanisha “ndiyo”. Hakuna<br />
lililo la kweli kati ya haya.<br />
Mwanaume wa kweli anajali na kumfikiria mtu mwingine. Husikiliza mwenzi wake anachosema na<br />
hafanyi mzaha. Wavulana wanahitaji kujifunza kuamini yale wasichana wanayoyasema. Msichana<br />
akisema “hapana” anamaanisha “hapana”. Msichana akisema “acha” mvulana lazima aache.<br />
Regina kutoka uganda (umri wa miaka 15)<br />
“Nilikuwa na rafiki wa kiume. Siku moja alinialika nyumbani<br />
kwake kwa ajili ya chakula cha mchana. Nilipokwenda, nilimkuta<br />
anashughulika kutengeneza chakula. Tulikula chakula<br />
pamoja na kuosha vyombo. Nilimweleza kwamba ningependa<br />
kuondoka, lakini alinisisitizia nikae kwa muda. Aliniambia<br />
kwamba kulikuwa na sinema moja nzuri sana; kwa kweli<br />
ilikuwa ni nzuri na inavutia. Lakini katikati ya sinema aliniomba<br />
nimbusu na kujaribu kunilazimisha tujamiiane. Lakini<br />
nilikataa. Nilimwambia siwezi na kumwomba aniache, ama<br />
sivyo ningepiga kelele ya kuomba msaada. Alihofu sana na<br />
akaniacha. Nilimwambia kwamba, kwasababu ya tabia yake<br />
urafiki wetu umekwisha”.<br />
Kila mtu anaweza kujifunza jinsi ya kupunguza uwezekano wa kubakwa. Kama ni msichana<br />
au mvulana, kitu cha muhimu zaidi ni kuamini hisia zako. Kwa mfano, kama mtu anakufanya<br />
ukose raha au anakutishia, zingatia hisia zako na zifanyie kazi. Mwache huyo mtu au ondoka<br />
katika mazingira hayo mara moja, hata kama hakuna sababu iliyowazi ya kukufanya ukose raha.<br />
Unaweza ukawa unapata dalili zenye hila ambazo ni ishara muhimu za kukuonya. Kamwe usipuuze<br />
hisia hizi. Zisikilize hisia zako na uzifanyie kazi.<br />
SURA YA 12 | NGONO YA KULAZIMISHWA NA NGONO BILA YA RIDHAA YAKO<br />
Njia Nyingine za kujilinda dhidi ya ubakaji:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Usikae peke yako na mtu usiyemjua na kumwamini. Ukienda kutembea fuatana na kikundi<br />
cha marafiki na kaa na kikundi hicho.<br />
Usiende au kuendelea kukaa nyumbani<br />
kwa mtu kama hakuna mtu mwingine.<br />
Usiende sehemu za upweke ambako<br />
hakuna watu wengine jirani.<br />
Iwapo katika eneo lenu watu wanabakwa<br />
sana, beba mchanganyiko wa mchanga<br />
au pilipili iliyosagwa ili uweze kumtupia<br />
machoni mtu anayekusumbua.<br />
Kama una matembezi, hakikisha (wazazi<br />
marafiki, shangazi, mjomba) wanajua<br />
unakokwenda na muda unaotegemea<br />
kurudi.<br />
Kuwa jasiri na kusema “HAPANA” kwa<br />
Ijue mipaka yako. Kabla hujaenda<br />
sauti na kwa nguvu<br />
kwenye miadi yako, fikiria kile<br />
unachotaka kukifanya na kile ambacho hutaki kukifanya. Usijaribu kufikiria wakati tayari<br />
upo na rafiki yako na mnakumbatiana na kubusiana.<br />
Kuwa mwazi kuhusu mipaka yako. Ikiwa hutaki kujamiiana mweleze rafiki yako bila kuficha,<br />
hasa uhusiano unapoanza ili kuhakikisha kwamba wote mna mategemeo yanayofanana.<br />
Unapotoka kwa ajili ya miadi; hakikisha unazo pesa za kwako ili uweze kurudi nyumbani<br />
kama miadi itageuka kuwa michungu.<br />
Gawana gharama na rafiki yako. Usimwache akafikiri anakudai ngono kama malipo ya pesa<br />
alizotumia kwa ajili yako.<br />
Usinywe pombe wala dawa za kulevya. Pombe na dawa za kulevya zinaweza kukufanya<br />
ushindwe kuwa mwazi kuhusu mipaka yako. Unaweza kushindwa kujimudu.<br />
Usikubali kinywaji kutoka kwa mtu usiyemjua na usiache kinywaji chako unapokwenda<br />
chooni kwa sababu mtu anaweza kuweka dawa za kulevya ndani ya kinywaji chako.<br />
Kama umetoka na rafiki yako naye akaanza kukushinikiza, kataa kwa nguvu. Usimwachie<br />
mwanya wowote wa yeye kudhani unamaanisha ndio wakati unaposema hapana. Sema<br />
kwa nguvu na kwa sauti kubwa na mwangalie moja kwa moja machoni. Usitabasamu wala<br />
usiangalie pembeni kwa aibu. Usimwonyeshe rafiki yako alama ya kuwa unataka ushawishike<br />
au kubembelezwa.<br />
Iwapo upo katika hali mbaya na kuna mtu anajaribu kukuzidi nguvu unaweza kupigana naye,<br />
bila kujali jinsia na ukubwa wa umbo. Unazo nguvu na akili ya kupigana. Tumia kila ulichonacho<br />
kujilinda. Piga ukelele mkubwa kwa mfululizo kuomba msaada.<br />
153
154<br />
Njia za kujilinda ni pamoja na:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Silaha nzuri uliyonayo ni vidole vyako na kucha. Mchome kwa nguvu kwa kutumia vidole<br />
ndani ya macho ya mshambuliaji. Usihofu kumuumiza. Alikuwa na nia ya kukuumiza.<br />
Tumia goti kumpiga teke la nguvu kwenye sehemu za siri. Iwapo utatumia nguvu, ataumia<br />
sana na kumsababishia maumivu mara mbili.<br />
Iwapo mtu huyo yuko juu yako na anausukumiza uso chini kwenye ardhi, tumia kisigino<br />
kumpiga teke kwenye mifupa ya chini ya mgongo, juu kidogo ya matako.<br />
Iwapo unazidiwa nguvu, tulia, jaribu kumdanganya mshambuliaji kwa kumshikashika. Halafu<br />
mchome machoni au piga mapumbu. Kimbia mara mbakaji atakapotulia kidogo kwa sababu<br />
ya maumivu.<br />
Kitu cha KuFanYa ubaKaji uKitOKea<br />
Wakati mwingine pamoja na jitihada zote za kujaribu kujitetea ubakaji unatokea, msichana au<br />
mvulana anaweza kuzidiwa nguvu na mshambuliaji na ukashindwa kujinasua. Hii ni hali mbaya<br />
sana, kwa hiyo ni muhimu kujua cha kufanya baada ya hapo.<br />
Ubakaji ukitokea kwako au kwa mtu unayemfahamu, haya ndiyo unatakiwa kufanya:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Tumia nguvu zako zote kumsukuma na kupigana<br />
Pata huduma ya matibabu haraka iwezekenavyo. Lazima upime vipimo kuhakikisha kwamba<br />
upo salama na kwamba majeraha yote yanatibiwa.<br />
Mwombe mzazi, shangazi, mdogo wako au rafiki wa karibu akusindikize kliniki / hospitalini<br />
au polisi ili ukapate msaada. Mtafute mtu ambaye ana nguvu, anajali na anategemewa.<br />
Mtu unayemwamini na ambaye hatasema kwa watu wengine.<br />
Usioge kabla ya kwenda kutibiwa. Ingawa wazo la kwanza la mtu ni kuoga vizuri, siyo vizuri<br />
kufanya hivyo. Watalaamu wanashauri kwamba mtu aliyebakwa asinawe hata mikono yake<br />
kwa sababu inaweza kuharibu ushahidi (uchafu, shahawa, majimaji ya mwili, nywele n.k.)<br />
ambavyo vingetumika kuhakikisha kwamba ubakaji umetokea na ni nani aliyefanya hivyo.<br />
SURA YA 12 | NGONO YA KULAZIMISHWA NA NGONO BILA YA RIDHAA YAKO<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Vaa au weka ndani ya sanduku, nguo zilizovaliwa wakati ubakaji unatokea. Nguo hizi<br />
zitatumika kama ushahidi kuhakikisha kwamba ubakaji umetokea.<br />
Jaribu kumtafuta mhudumu wa afya ambaye ni wa jinsi yako akuchunguze mara utakapofika<br />
kituo cha afya. Iwapo wewe ni msichana mwombe mhudumu msichana akuchunguze.<br />
Mhudumu anatakiwa achunguze kama kuna mikato, michaniko au michubuko. Na anaweza<br />
kuchukua sampuli ya shahawa ukeni.<br />
Omba dawa za dharura za kuzuia mimba (angalia Sura ya 11 kwa taarifa zaidi kuhusu<br />
kuzuia mimba kwa dharura). Omba vilevile upime vipimo vya magonjwa ya ngono na VVU.<br />
Kipimo cha VVU utahitajika kukirudia baada ya miezi 3 hadi 6 ili kuhakikisha maambukizo<br />
hayajatokea. (angalia Sura ya 10 kwa taarifa zaidi kuhusu VVU na magonjwa mengine ya<br />
zinaa).<br />
Mwombe mhudumu wa afya aandike kila kitu anachokiona. Taarifa hii inaweza kusaidia<br />
kuhakikisha kwamba ulibakwa.<br />
Mwombe mhudumu wa afya akushauri wapi uende kutoa taarifa ya kubakwa. Iwapo<br />
mhudumu wa afya hajui, nenda kwenye kituo cha vijana au kikundi cha wanawake. Waombe<br />
ushauri namna ya kutoa taarifa kuhusu ubakaji na wapi unaweza kupata ushauri wa kisheria<br />
kama unataka kumshitaki mbakaji.<br />
Iwapo unataka kutoa taarifa kuhusu ubakaji fanya hivyo mapema iwezekanavyo. Nchi nyingi<br />
zimeweka sheria na adhabu kali kwa mtu atakayepatikana na kosa la kubaka. Ukiamua kutoa<br />
taarifa polisi au kwa viongozi wa kijiji, fanya hivyo bila kuchelewa. Unahitaji kuwa jasiri kutoa<br />
taarifa ya ubakaji kwa sababu inaumiza na kuhuzunisha kuzungumzia yaliyotokea lakini<br />
lazima utoe taarifa hiyo. Usipofanya hivyo ataondoka na kuwa huru na anaweza kumuumiza<br />
mtu mwingine.<br />
Pata nasaha. Lazima umpate mtu wa kuzungumza naye kuhusu hisia zako za hofu, huzuni,<br />
hasira na maumivu. Mtaalamu wa nasaha anaweza kukusaidia kuchambua hisia zako ili uweze<br />
kuendelea na maisha yako ya kila siku.<br />
Ni muhimu kujua kwamba katika nchi nyingi ni kosa mwanamke kutoa mimba ambayo ni matokeo<br />
ya kubakwa. Iwapo unafikiri kwamba umepata mimba, zungumza na mhudumu wa afya au waone<br />
kikundi cha akina mama ili kujua uchaguzi ulionao.<br />
Inaweza ikakuchukua muda mrefu kupona kimwili na kihisia baada ya kubakwa. Kuwa mvumilivu.<br />
Jambo la muhimu zaidi usijilaumu au kufikiria uliwajibika kwa ubakaji huo. Halikuwa kosa lako.<br />
155
156<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Sura ya 12<br />
ngono ya kulazimishwa na ngono bila ridhaa yako<br />
Ngono isiyotakiwa ni hatari; inakuweka katika uwezekano mkubwa wa kupata mimba<br />
isiyotakiwa na magonjwa ya zinaa na VVU/UKIMWI. Inaweza kuwa mbaya vilevile kwa afya<br />
ya hisia zako. Inaumiza sana na kuleta kiwewe ukijamiiana bila ya ridhaa yako.<br />
Ngono isiyotakiwa inajumuisha mambo mengi tofauti. Inaweza ikawa:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Kushikwa au kuguswa kijinsia bila ya ridhaa yako. Hii ni kunyanyaswa kijinsia.<br />
Matusi ya kijinsia yasiyotakiwa ni udhalilishaji kijinsia.<br />
Kulazimishwa ngono; huu ni ubakaji. Mbakaji anaweza akawa mgeni kabisa, lakini<br />
kawaida ni watu ambao wanafahamika kwa anayebakwa – kama rafiki wa kiume, rafiki,<br />
jirani au ndugu.<br />
Njia nzuri ya kujilinda ni kujifunza jinsi ya kugundua na kuepuka mazingira ambayo utakuwa<br />
hatarini kulazimishwa ngono:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Epuka uhusiano na watu wazima. Uhusiano huu unakuweka katika uwezekano mkubwa<br />
wa kupata magonjwa ya ngono na mimba kwa sababu uhusiano huu hauna usawa.<br />
Unaweza usiwe na nguvu ya kusema “hapana” ukiombwa ngono au kumlazimisha mtu<br />
mzima atumie kondomu.<br />
Amini hisia zako. Iwapo kuna mtu anakufanya ujisikie vibaya au uwe mwenye wasiwasi,<br />
mwache mtu huyo mara moja. Hisia zako ni ishara muhimu, usizipuuzie.<br />
Usije hata siku moja ukawa peke yako na mtu ambaye humwelewi vizuri na kumwamini.<br />
Usiende nyumbani kwa mtu kama hakuna mtu mwingine. Fuatana na kundi la marafiki na<br />
kaa nalo.<br />
Jua mipaka yako na hakikisha rafiki yako wa kiume au wa kike anaielewa mipaka hiyo.<br />
Usiwaruhusu watu wengine wakupatie zawadi au watumie pesa kwa ajili yako kwa<br />
sababu wanaweza kukuomba urudishe msaada huo kwa kufanya nao ngono.<br />
Usinywe pombe au kutumia dawa za kulevya.<br />
Kuwa jasiri, usiwachanganye watu kwamba unaposema hapana unamaanisha ndio.<br />
Usitoe ishara yoyote kwamba unataka kushawishiwa na kubembelezwa kwanza.<br />
Wakati mwingine ubakaji unatokea licha ya mtu kujitahidi kujilinda. Iwapo hili litatokea,<br />
unahitaji kupata matibabu na ushauri moja kwa moja. Mhudumu wa afya anaweza kukupatia<br />
dawa ya dharura ya kuzuia mimba. Usioge kwanza kwa sababu itakuwa vigumu kuhakikisha<br />
kwamba ulibakwa. Tunza nguo ulizokuwa umevaa wakati ubakaji unatokea.<br />
Jambo la muhimu zaidi, usijilaumu. Halikuwa kosa lako. Jipe muda wa kupona kimwili na<br />
kihisia.<br />
Matumizi mabaya ya dawa<br />
Mara nyingine watu hutumia dawa na viini kadhaa ambavyo haviponyi magonjwa. Dawa hizi<br />
zinabadili jinsi mtu anavyojisikia na anavyofikiri. Zinaweza kumfanya mtu awe mcheshi zaidi,<br />
mwerevu, mpole, jasiri na anayefurahisha kuwa naye. Dawa hizi zinaweza kumfanya mtu asiwe<br />
mwoga na asifadhaike. Lakini hisia hizi zinadumu kwa muda mfupi sana na hivyo kutumia dawa<br />
kama njia ya kujifurahisha na kufanikisha mambo yako ni hatari sana. Kutumia dawa kwa njia hii<br />
kunaitwa “matumizi mabaya ya dawa.”<br />
Matumizi mabaya ya dawa ni tatizo kubwa linalotukabili. Dawa zingine kama pombe na sigara ni<br />
sehemu katika maisha yetu ya kila siku kiasi kwamba hatufikirii kama ni dawa za kulevya. Lakini<br />
pombe na sigara ni dawa za kulevya na mara nyingi watu wanazitumia vibaya.<br />
Dawa zinadhuru akili yako, mwili wako, na uhusiano wako na watu wengine. Zinaweza kukufanya<br />
mgonjwa na usipate mafanikio katika maisha yako yote. Zinaweza kusababisha ufanye<br />
vibaya shuleni, upoteze marafiki na ukosane na wazazi wako. Zitakufanya utumie pesa yote<br />
utakayofanikiwa kuipata.<br />
Dawa zinaweza kufanya iwe vigumu kwako kufanikisha mpango wa kufanya ngono salama.<br />
Wakati wote unatakiwa kuwa makini kuhusu ngono. Unahitaji kuwa na uwezo wa kusema “Hakuna<br />
kujamiiana, hakuna kabisa”.; au “ninataka busu tu na sitaki kujamiiana,” au “nitatumia kondomu<br />
tu.” Dawa zinafanya ubongo usifanye kazi vizuri. Zinaweza kukufanya ufanye mambo ya hatari<br />
kama kufanya ngono isiyo salama. Kutokana na hiyo unaweza ukaishia kupata magonjwa ya zinaa<br />
pamoja na VVU/UKIMWI. Unaweza ukaishia kupata mimba au kumpa mimba msichana.<br />
aina Ya DaWa na Vitu aMbaVYO VinatuMiKa VibaYa<br />
Kuna aina nyingi za dawa zinazotumiwa vibaya na watu.<br />
Zinaweza zikasababisha matatizo ya kweli. Zifuatazo ni baadhi tu ya dawa zinazojulikana na<br />
baadhi ya matatizo yanayoweza kukupata.<br />
Marijuana ambayo majina yake kadhaa ni bangi, hashi, poti, majani, gugu, acapulco gold au<br />
fimbo ya thai. Dawa zote hizi zinatokana na mimea. Kwa kawaida watu wanavuta majani lakini<br />
mara nyingine ipo dawa ya nguvu zaidi inayotengenezwa kutokana na mashina ya mimea.<br />
157<br />
SURA YA 13
158<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Bangi inaweza kumfanya mtu ajisikie ameburudika na kufurahi, au inaweza kumfanya mtu ajisikie<br />
kutetemeka sana na kuogopa. Kuvuta bangi kunaweza kusababisha macho yawe mekundu,<br />
midomo na koo kuwa mikavu na hamu ya kula kuongezeka. Unaweza kujisikia usingizi, na<br />
wasiwasi wako kutoweka katika muda ambao ulevi umekolea. Lakini ujue utashindwa kufanya<br />
uamuzi hata ule ulio mdogo!<br />
Kuvuta sana na matumizi ya muda mrefu ya bangi yana madhara kwenye mapafu na yanaweza<br />
kusababisha saratani. Uvutaji unaweza vilevile kuathiri kumbukumbu na uwezo wa kuwa makini<br />
na kuelewa mambo. Inawezekana kuwa vigumu kuendelea na masomo au kuwa na maendeleo<br />
mazuri ya kazi kwa sababu kumbukumbu na usikivu vinakuwa vimepungua.<br />
Khat, gat, miraa au mirungi ni aina ya jani linalotafunwa maeneo ya pembezoni mwa Afrika na<br />
karibu Afrika ya Mashariki yote. Hii ni dawa maarufu sana katika baadhi ya jumuia kwa sababu<br />
inafanya ujisikie kuwa macho zaidi, mwenye nguvu na mwenye kujiamini. Vilevile, inapunguza<br />
njaa. Athari mbaya za kutafuna jani hili ni pamoja na kuwa na wasiwasi, uchokozi, uhanithi (kama<br />
mwanaume hawezi kusimamisha uume) na maono ya vitu<br />
ambavyo havipo.<br />
Petroli, gundi, rangi, tina na bidhaa za viwandani<br />
zinazowekwa kwenye makopo ya kupuliza. Mara nyingine<br />
zinavutwa ili kujiweka katika hali ya ulevi. Vitu hivyo vinaweza<br />
kufanya ujisikie joto, njaa kidogo, hupunguza woga na<br />
kukufanya mwenye furaha angalau kwa muda. Baada ya kuvuta<br />
vitu hivyo, unajisikia usingizi na unajiona haupo kabisa kwenye<br />
mazingira yanayokuzunguka. Kwa kuwa vitu hivyo ni rahisi sana<br />
kununua, vinakuwa kivutio kikubwa kwa vijana wa mitaani.<br />
Dawa hizi zinaweza kusababisha kichefuchefu na kutapika.<br />
Unaweza kupoteza mwelekeo na ukachanganyikiwa na<br />
usiweze kudhibiti hatari zinazokuzunguka. Kwa hiyo, unaweza<br />
kugongwa na gari kwasababu utashindwa vitu rahisi kama<br />
kuvuka barabara.<br />
Kuvuta kwa muda mrefu kunaweza kusababisha ukakosa<br />
fahamu (kuzimia au kufariki), kukabwa roho (kushindwa<br />
kupumua) na kifo. Matumizi ya mara kwa mara ya vitu hivi<br />
yanaweza kukuharibu mapafu, ubongo na viungo vingine<br />
muhimu vya mwili.<br />
Dawa za kutuliza ni pamoja na valiumu na mandraksi: Dawa<br />
hizi zinaweza kukufanya ujisikie mwenye usingizi au kama<br />
umepumzika vile na uko shwari. Zinapunguza mapigo ya moyo na kupunguza kupumua.Ukizidisha<br />
zinaweza kukuua kwa haraka na kiurahisi.<br />
Dawa zenye kuleta njozi, kama “angel dust,” LSD (pia yanaitwa tindikali, mchemraba wa sukari,<br />
dragoni na magugu yanayoua). Dawa hizi zinaweza kukufanya uhisi mambo ambayo hayapo.<br />
Dawa hizi zinasababisha kutetemeka, kupoteza hamu ya kula, kupoteza usingizi na kupandisha<br />
joto la mwili. Mtumiaji anaweza pia kuwa na wasiwasi, tabia ya vurugu, mfadhaiko na wazimu<br />
(ugonjwa wa akili usiotibika.) Wakati uko katika hali ya ulevi kwa sababu ya dawa na unahisi<br />
kwamba unaweza ukajiumiza. Matumizi ya muda mrefu yanaweza kuleta matatizo ya kupoteza<br />
kumbukumbu, na ukizidisha zinaweza kusababisha kutetemeka, kupoteza fahamu na hatimaye<br />
kifo.<br />
“Dawa kali” (narcotics) zikijumuisha dawa kama heroini (pia inaitwa junki, sukari ya kahawia<br />
na smak) na kokeini (inaitwa koki, crak na barafu). Katika Bara la Afrika dawa kali ni matatizo<br />
makubwa, na watu wengi wanazitumia. Mara nyingi zinatumika kwa kujidunga sindano inayoenda<br />
moja kwa moja kwenye mishipa ya damu. Dawa hizi ni rahisi sana kuzizoea mwilini. Ukianza<br />
kuzitumia inaweza ikakuwia vigumu kuziacha. Watu ambao wamezizoea wanaona kana kwamba<br />
hawawezi kuishi bila dawa hizo.<br />
Dawa hizi zimepigwa marufuku kabisa, na ili kuzipata shurti ufuatane na watu ambao wanavunja<br />
sheria. Dawa hizi ni ghali sana hivyo watu wengine wanaozitumia wanaanza kuiba fedha ili<br />
wapate fedha ya kutosha kuweza kuzinunua. Watu wengine wanauza miili yao ili kupata fedha<br />
ya kutosha kununua dawa hizi. Watu wengine wanaotumia dawa hizi hutumia sindano kwa<br />
kujichoma ili waweze kuzizoea mwilini. Wale wanaochangia sindano wana hatari kubwa ya kupata<br />
mambukizo ya VVU.<br />
SiGaRa na POMbe<br />
SURA YA 13 | MATUMIZI MABAYA YA DAWA<br />
Watu wengi wanapofikiria dawa za kulevya huwa hawaorodheshi pombe na sigara. Hata hivyo,<br />
pombe na sigara mara nyingi vinatumiwa vibaya kama dawa nyingine za kulevya na zina athari<br />
zake.<br />
tumbaku, sigara (vilevile zinaitwa, dragis, batis, na fegi) na “mitemba”. Nikotini ni kiambato<br />
kichochezi katika tumbaku, sigara na mitemba. Nikotini haikufanyi ujisikie uko juujuu kama ilivyo<br />
bangi au pombe na wala haiharibu uwezo wako wa kuamua. Inaweza kukufanya ujisikie mwenye<br />
nguvu nyingi na inapunguza hamu yako ya kula.<br />
Hatari moja kubwa ya nikotini ni kwamba inazoeleka sana mwilini. Umewahi kuona wavutaji<br />
wakitaka kuacha kuvuta?. Wanakuwa wanyonge, hawawezi kulala au kuunganisha mawazo,<br />
wanaudhika upesi na wanakuwa na hasira na wasiwasi. Kujisikia kwa namna hii kunaudhi kiasi<br />
kwamba watu wengi wanashindwa kuacha kuvuta na wanajaribu tena na tena kabla ya kufanikiwa<br />
kuiacha tabia hii.<br />
Siyo tu kwamba nikotini inazoeleka sana mwilini bali pia ni hatari kwa afya yako.Uvutaji<br />
umeonekana kusababisha matatizo mengi ikiwa ni pamoja na saratani ya koo, ulimi, mapafu,<br />
matiti na utumbo mkubwa. Uvutaji unaharibu moyo na mishipa ya damu katika mwili na inaweza<br />
kuleta hatari ya kupata shinikizo la damu, kiharusi na ugonjwa wa moyo.<br />
Pia uvutaji sigara umeonekana kusababisha uhanithi kwa wanaume. Hii ni kwa sababu uvutaji<br />
unaharibu mishipa ya damu katika uume kama unavyoharibu mishipa ya damu mingine mwilini.<br />
Pombe ni dawa ya kulevya maarufu sana Afrika na kwa kweli dunia nzima. Tofauti na dawa<br />
zingine za kulevya, pombe imehalalishwa kisheria na inapatikana kwa aina mbalimbali na kwa bei<br />
ndogo.Kwa hiyo pombe ni dawa ya kulevya ambayo kuna uwezekano wa kukumbana nayo. Mara<br />
nyingi ndani ya nyumba, mmoja wa wazazi wako au wote wanaweza wakawa wanakunywa pombe.<br />
Inaweza ikawa rahisi kwako kuipata na haitaonekana kama kitu cha kutisha kwa sababu ni kitu<br />
cha kawaida katika jamii.<br />
159
160<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Ni rahisi kuanza kunywa pombe na usiifikirie sana kuhusu jambo hilo. Lakini fikiria tena! Pombe<br />
ni dawa ya kulevya kama dawa nyingine za kulevya. Pombe inadumaza mfumo wa mwili. Baada<br />
ya kunywa pombe kidogo, matendo yako yanaweza yakawa ya taratibu na inaweza ikakuwia<br />
vigumu kufikiri vizuri. Ukiongeza kidogo tena, unashindwa kusema vizuri na unaweza kuwa mkali<br />
na mchokozi. Kama siyo mzoefu wa pombe au kama unakunywa sana unaweza kutapika sana au<br />
ukapoteza fahamu.<br />
Athari za muda mrefu za unywaji sana pombe ni mbaya. Nadhani unawafahamu watu katika<br />
jamii ambao ni walevi sana na ambao hawawezi kuishi bila kunywa. Unaweza ukawa umeona jinsi<br />
inavyoharibu familia, watu kupoteza kazi, na inasababisha afya kuwa mbaya, kama kuharibu<br />
ubongo na kuleta ugonjwa wa ini.<br />
Pombe ni dawa ya kulevya maarufu sana<br />
ambayo inawafanya watu wastarehe na<br />
kusahau taabu zao. Hata hivyo, kujiona<br />
umestarehe mno na kutojitambua si jambo<br />
zuri kwani kunaweza kukufanya upate<br />
matatizo.<br />
Pombe kama ilivyo kwa dawa nyingine za<br />
kubadili hali ya mtu, inaondoa uwezo wa<br />
kujizuia na mambo unayoona yatakutia aibu<br />
mbele ya wenzio. Pombe inakupa ujasiri wa<br />
kuzungumza mambo ambayo baadaye utakuja<br />
yajutia.<br />
Kwa mfano, wasichana wengi wakiwa<br />
hawajanywa hawana ujasiri wa kwenda kwa<br />
mwanaume na kumbusu kwenye mdomo lakini<br />
msichana akiwa amekunywa pombe anaweza<br />
kujisikia huru sana; anajisikia kumbusu<br />
mvulana na anafanya hivyo.<br />
Pombe inaweza pia kumfanya mvulana afanye<br />
vitu ambavyo kwa kawaida asingelifanya. Kwa<br />
mfano, mvulana anaweza akaamua kutaka<br />
kujamiiana na msichana baada ya kunywa<br />
pombe. Hata kama rafiki yake wa kike anataka<br />
au hataki, anaweza kujaribu kumlazimisha<br />
kujamiiana naye. Pombe inamfanya asiweze<br />
kumfikiria rafiki yake wa kike anavyojisikia;<br />
inamfanya pia asiweze kufikiria matokeo ya<br />
jambo analotaka kutenda.<br />
Unapokunywa pombe, sheria zinazotawala<br />
tabia yako ya kawaida zinapungua. Uwezo<br />
wako wa kuamua mambo mazuri unapungua.<br />
Kwa hiyo, unapoteza uwezo wa kupima<br />
mambo. Kijana mmoja anasema haya kuhusu<br />
pombe:<br />
Pombe inaathiri uwezo wako wa kufanya<br />
uamuzi salama<br />
lazarus kutoka Zambia (umri wa miaka 15)<br />
“Ninapokunywa ninasahau hatari zote zinazonizunguka. Ninasahau kila<br />
kitu kuhusu kondomu. Hivyo huwa ninafanya ngono bila kinga kwa sababu<br />
ya kishawishi cha pombe. Ninajua nina uwezekano wa kuambukizwa.”<br />
Iwapo kinywaji cha kawaida kama pombe kinaweza kukuletea matatizo makubwa kama hayo,<br />
hebu fikiria kinachoweza kutokea kama ukitumia dawa kali zaidi kama kokeni.<br />
KutaWaliWa na DaWa<br />
Kadiri mtu anavyoanza mapema kutumia dawa, ndivyo anavyojiwekea nafasi ya kujenga matatizo<br />
makubwa yanayohusiana na dawa baadaye. Athari za dawa nyingi zinaongezeka kadiri muda<br />
unavyopita. Athari zinajijenga mwilini, kama bomu lililotegwa kwa muda maalumu likisubiri muda<br />
ufike lilipuke.<br />
Kuna dalili nyingi zinazojitokeza matumizi ya dawa zinapofikia kuwa matatizo makubwa.<br />
Dalili hizo ni:-<br />
•<br />
Je, unajua kwamba matumizi ya dawa za kulevya zina matatizo ya kipekee kwa<br />
wanawake na wasichana?<br />
Wakati dawa za kulevya zote zina madhara mwilini, nyingi zinawaathiri zaidi wanawake<br />
na wasichana kuliko wanaume. Kwa mfano, kuvuta sigara kunaleta madhara ya pekee kwa<br />
wanawake. Kunaweza:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
SURA YA 13 | MATUMIZI MABAYA YA DAWA<br />
Kuleta matatizo ya kiafya kama mwanamke anatumia vidonge vya kuzuia mimba.<br />
Kupunguza miaka ya mwanamke ya kuzaa watoto kwa sababu tukio la hedhi kukoma<br />
litatokea mapema<br />
Kuongeza hatari ya mwanamke kupata saratani ya mlango wa mfuko wa kizazi na tumbo<br />
la uzazi.<br />
Kusababisha mifupa ya mwanamke kuwa dhaifu.<br />
Kusababisha iwe vigumu kwa mwanamke kupata mimba.<br />
Kuongeza hatari ya mimba kutoka kwa mwanamke mjamzito.<br />
Kufanya mwanamke azae mtoto mdogo sana au mtoto azaliwe mapema kabla ya wakati.<br />
Kumeza dawa na kunywa pombe wakati mwanamke ana mimba ni hatari kwa sababu inaweza<br />
kusababisha matatizo makubwa ya kiafya na ya mtoto kuzaliwa na kasoro, kama kuundwa<br />
vibaya kwa moyo, mifupa, kichwa na viungo muhimu vya ndani. Mtoto pia anaweza kuzaliwa<br />
na uzito mdogo, kukua taratibu na kutokuwa na uwezo wa kujifunza darasani. Matumizi<br />
mabaya ya dawa wakati wa ujauzito yanaweza kusababisha uzae mtoto ambaye tayari<br />
ameathirika na dawa na hivyo kuzoeleka mwilini mwake.<br />
Kumbuka, ukiwa unatumia dawa wakati wa ujauzito, mtoto wako pia anapata kiwango<br />
kikubwa kuliko wewe. Athari kwa mtoto zitakuwa kubwa zaidi kuliko kwako.<br />
Kuongopa kuhusu kiasi cha dawa unachotumia. Hii ni pamoja na kujidanganya mwenyewe<br />
kiasi gani cha dawa au pombe unayotumia.<br />
161
162<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Kuficha dawa ili watu wengine wasizione.<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Kuwa na matatizo ya fedha kwa sababu zote zimetumika kwa dawa.<br />
Kujiaibisha mwenyewe na wengine hadharani kwa kufanya vitendo vya aibu.<br />
Iwapo wewe au mtu yeyote unayemfahamu anaanza kuacha kufanya mambo anayoyapenda,<br />
anatumia muda kidogo kwenye kazi za shuleni, anakwepa kuwajibika, anataka sherehe na<br />
anataka kupigana baada ya kunywa au akiwa amelewa basi matumizi ya dawa yanamfanya aingie<br />
katika matatizo makubwa na anahitaji asaidiwe ili aache au unahitaji kusaidiwa ili uache.<br />
irinne kutoka Zambia (umri wa miaka 16)<br />
“Rafiki yangu alikuwa anatumia dawa, na dawa zikamzoea<br />
mwilini. Hakuwa anaweza kukaa hata saa moja bila kuzitumia.<br />
Alizizoea hadi wakati fulani akizikosa alikuwa anapigana hovyo<br />
na ndugu zake na majirani.”<br />
Moja ya matatizo makubwa ya kutumia dawa ni mwili kutawaliwa<br />
na dawa hizo. Mwili unapozoea dawa hizo inabidi uzitegemee ili<br />
uweze kufanya kazi za kila siku. Dalili za mwili kuzoea dawa ni<br />
pamoja na:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Kujisikia kana kwamba dawa ni muhimu ili kukamilisha siku.<br />
Kutaka zaidi na zaidi dawa ili uweze kujisikia ipasavyo.<br />
Kuanza kuona mabadiliko mabovu ya tabia kama vile hasira,<br />
wasiwasi, vurugu za ghafla.<br />
Kupoteza fahamu (kuzimia) baada ya kuzitumia.<br />
Salome kutoka Kenya (umri wa miaka 17)<br />
“Mmoja wa marafiki zangu ambaye alizoea<br />
kutumia dawa aliugua sana. Pua yake ilikuwa<br />
inatoa damu wakati wowote. Mara nyingine<br />
alikuwa anaanguka chini.”<br />
Mara mwili unapokuwa umetawaliwa na dawa, unahitaji zaidi na zaidi dawa hizo ili uweze<br />
kujisikia vizuri. Hii ni gharama na inaharibu mwili wako. Kwa dawa kali kama kokeini na heroini,<br />
mara zinapozoeleka mwilini, ukizikosa unaugua sana. Ukiacha kutumia, moja kwa moja, utapata<br />
dalili zisizopendeza, kama kutetemeka, kichefuchefu, kutapika, maumivu na shida katika kupata<br />
usingizi na kula. Hali hii inaweza ikawa mbaya kiasi kwamba utataka kurudia tena kutumia dawa<br />
hizo.<br />
Dalili hizi za kujisikia vibaya zinaitwa “dalili za kujitoa”. Ni hisia za mwili kutokana na dawa<br />
kuondolewa mwilini. Kwa sababu mwili wako umekuwa tegemezi kwa dawa hizi, mwili unaugua<br />
kwa kukosa dawa hizo.<br />
SURA YA 13 | MATUMIZI MABAYA YA DAWA<br />
julia kutoka Ghana (umri wa miaka 17)<br />
“Niliacha kutumia dawa rafiki yangu mpenzi aliponishauri kuhusu<br />
hatari za dawa. Mara ya kwanza nilidharau, lakini baada ya muda<br />
nilijaribu kujidhibiti mwenyewe. Niliambiwa na rafiki yangu nisizitumie<br />
kwa wiki moja, lakini nilimweleza nisingaliweza bila dawa<br />
hizo. Hata hivyo, namshukuru Mungu kwamba wiki nzima sikuzitumia<br />
na sasa najua naweza kuishi bila dawa hizo.”<br />
Kuyashinda mazoea ni vigumu sana na watu tofauti wanao uzoefu tofauti. Watu wengine wana<br />
uwezo wa kuacha kutumia dawa mara moja. Watu wengine wanahitaji kuacha taratibu, kwa<br />
kupunguza kiwango cha kutumia. Hii inasaidia kuulinda mwili kutokana na mshituko wa kuacha<br />
ghafla. Kuacha kidogo kidogo kunasaidia kuruhusu mwili kuanza kujitoa kwenye dawa.<br />
Omari kutoka tanzania (umri wa miaka 18) “<br />
Niliacha kutumia dawa baada ya kushuhudia athari zinazotokana<br />
na kujihusisha katika kutumia dawa. Baadhi ya marafiki zangu<br />
wamefariki kutokana na maambukizo ya kifua au maradhi mengine.<br />
Ilibidi niende kupata ushauri dhidi ya dawa na kwa kufanya<br />
hivyo nimeweza kuacha.”<br />
Kushinda utegemezi wa dawa za kulevya kunahitaji nguvu kubwa na dhamira, ujasiri na<br />
uamuzi thabiti. Kuna wakati ambapo utajisikia kama vile huwezi. Kwa hiyo ni jambo muhimu<br />
kutafuta msaada na kuungwa mkono. Zungumza na mshauri wa vijana au mhudumu wa afya<br />
kuangalia kama kuna msaada wa vikundi au mpango unaoweza kujiunga nao. Jambo la muhimu<br />
zaidi usishirikiane na watu ambao watakurudisha nyuma. Usishirikiane na watu ambao<br />
hawatakusaidia kuacha tabia yako.<br />
KWa nini Watu WanaanZa KutuMia DaWa?<br />
Njia iliyo wazi na sahihi ya kuepuka kupata matatizo ya kutawaliwa na dawa ni kutokuanza<br />
kutumia dawa kabisa. Kwa hiyo, ni vizuri kuelewa ni kwa nini watu wanaanza kutumia dawa, ili<br />
uwe mwangalifu na kuhakikisha kuwa kamwe huangukii katika mitego hiyo.<br />
Kuna sababu nyingi zinazowafanya vijana kuanza kutumia dawa kama<br />
kokeini na heroini au hizi zilizozoeleka kama pombe na sigara:<br />
Kwanza, vijana wengi wanatumia dawa kwa sababu wenzao<br />
wa rika moja wanafanya hivyo na kwa sababu<br />
wanataka kuonekana sawa katika kundi.<br />
Makundi mengine yanatumia dawa<br />
kama sehemu ya utambulisho wa kundi<br />
lao. Kama unataka kuwa sehemu ya<br />
kundi, unaweza kupata msukumo wa<br />
kutumia dawa kama wanayotumia<br />
wenzako.<br />
163
164<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Wenzako wanaweza kukuomba ujaribu kutumia dawa na kudharau athari zake. Wanaweza<br />
wakakasirika au wakakutukana kama hujaribishi kuvuta.<br />
Margaret kutoka Kenya (umri wa miaka 16)<br />
“Nilikuwa na miaka 13 nilipoanza kutumia dawa. Marafiki zangu<br />
walianza kuvuta bangi. Waliniambia nivute pafu moja tu, lakini<br />
nilikataa. Wakaanza kunicheka, na kwa vile sikutaka kuambiwa<br />
kuwa ni mwoga, niliamua kuvuta pafu moja.”<br />
Pili, wengi wanatumia dawa kwa sababu wanataka kukwepa matatizo katika maisha yao.<br />
Labda waligombana na wazazi wao au pengine marafiki wamewaumiza kihisia. Wanaweza kuwa<br />
wanajisikia wenye huzuni, wasiwasi au wamezidiwa na matatizo. Dawa zinaweza kuonekana<br />
kama njia rahisi ya kuepukana na matatizo.<br />
Marion kutoka Zimbabwe (umri wa<br />
miaka 17)<br />
“Baadhi ya marafiki zangu walianza<br />
kutumia dawa kwa sababu ya<br />
matatizo nyumbani au nje.”<br />
Francis kutoka uganda (umri wa<br />
miaka 15)<br />
“Baadhi ya marafiki zangu<br />
wamepoteza wazazi wao kutokana<br />
na UKIMWI na wanatumia dawa<br />
kusahau matatizo yao.”<br />
tatu, wengine wanatumia dawa za kulevya kwa sababu<br />
wanataka waonekane tofauti na vile walivyo. Vijana<br />
wengi hawajisikii ni wazuri vya kutosha kama walivyo.<br />
Wanataka wawe na ujasiri wa ajabu, waongee kwa sauti ya<br />
juu, waonekane wanavutia na wamekua. Dawa zinaweza<br />
kuwafanya wawe watu tofauti.<br />
juma kutoka Kenya (umri wa miaka 17)<br />
“Ninao marafiki ambao wanatumia dawa kila wakati, kama<br />
dawa zinazoathiri akili na bangi. Wanatumia dawa hizi ili<br />
wajisikie watu wazima na bora kuliko wenzao. Lakini dawa hizi<br />
zimewasababishia wasizingatie kazi zao, ndoto, malengo na<br />
tamaa zao za baadaye.”<br />
nne, watu wengine wanafikiri dawa zitawafanya wapate ujasiri wa kufanya mambo ambayo<br />
wanaogopa kuyafanya. Kuna mazingira mengi katika maisha yanayohitaji ujasiri. Unaweza<br />
ukawa mwoga kuongea darasani au unaweza kuwa mwoga kumwendea msichana au mvulana<br />
unayempenda. Dawa zinaweza kuonekana kama njia rahisi kuushinda woga huu.<br />
tano, vijana wengine wanaamini kuwa dawa zitawafanya wawe werevu zaidi. Wanafikiri dawa<br />
zitawasaidia wakae macho ili waweze kujisomea kwa muda mrefu na vizuri<br />
Sita, vijana wengi wanatumia dawa kwa sababu ya kuchoshwa na maisha. Wanataka kuwa na<br />
furaha na hawajui kitu gani kingine kitawafurahisha.<br />
Saba, vijana wengine wanatumia dawa kwa sababu wamepoteza matumaini. Hawajisikii kama<br />
wana mpango wa maisha ya baadaye. Wanatumia dawa kwa sababu wanajiona kana kwamba<br />
hawajali kitakachowatokea.<br />
Hizi ni baadhi tu ya sababu za baadhi ya vijana kutumia dawa za kulevya. Lakini hakuna sababu<br />
hata moja inayothibitisha uhalali wa matumizi ya dawa. Kutumia dawa ni njia mbaya ya kutatua<br />
matatizo. Dawa zinafanya matatizo kuwa magumu zaidi. Ujana ni kazi ngumu, na kuna mambo<br />
mengi ungetaka kufanikisha unapokuwa kijana shuleni na nje ya shule. Unahitaji kujifunza namna<br />
ya kuvumilia matatizo, namna ya kushughulikia hisia zako, namna ya kuwa na urafiki usio na<br />
madhara, namna ya kushughulikia mabadiliko ya mwili wako. Orodha ya mambo unayopaswa<br />
kuyashinda au kuyaweza wakati wa ujana wako haina mwisho.<br />
Tatizo la dawa ni kwamba zinaweza kuingilia utaratibu wako mzima wa kupata stadi na utaalamu.<br />
Zinakusimamisha kujifunza namna ya kuvumilia mfadhaiko wa kila siku. Zinakuzuia kujifunza<br />
stadi za maisha utakazozihitaji utakapokuwa mtu mzima.<br />
Kumbuka:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
SURA YA 13 | MATUMIZI MABAYA YA DAWA<br />
Huhitaji dawa ili upendwe na watu.<br />
Huhitaji dawa kuwa jasiri na shupavu.<br />
Huhitaji dawa ili kumudu huzuni au maudhi.<br />
Maryann kutoka Kenya (umri wa miaka 15)<br />
“Rafiki yangu Katty aliambiwa na msichana mwingine kwamba<br />
akivuta bangi anaweza kumuuliza mwalimu maswali magumu ambayo<br />
hawezi kuyajibu. Lakini mambo yalimgeukia Katty upande<br />
mwingine. Akaanza kushindwa kuyamudu masomo. Sasa hivi ni<br />
mtu aliyekata tamaa na kuacha shule. Angependa apewe nafasi<br />
tena kurudia shule lakini baba yake hataki kusikia habari hizo.<br />
Anasema kwamba alishindwa alipopewa fursa.”<br />
Unaweza ukaishi bila dawa na pombe. Ndani yako unazo nguvu na nyenzo za ndani za<br />
kushughulikia hali na matatizo yoyote yale. Unahitaji kutafuta nguvu za ziada ndani yako ili<br />
kushinda tatizo hili.<br />
Kwa tatizo lolote unaloliona, msaada unaweza kupatikana. Unaweza kuzungumza na mshauri<br />
wako, mwalimu unayemwamini au mtu katika kanisa lako au msikiti wako. Zungumza na wazazi,<br />
shangazi au mjomba, kaka mkubwa au dada au rafiki unayemwamini. Msaada unapatikana<br />
ukiutafuta.<br />
165
166<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
naMna Ya KuShuGhuliKia ShiniKiZO la KutuMia DaWa<br />
Kumudu shinikizo kutoka kwenye kundirika linalotaka utumie dawa kama wao ni vigumu sana.<br />
Hapa kuna hadithi fupi ya kijana mmoja:-<br />
Je, maelezo haya yanakukumbusha wewe pia hali ambayo imewahi kukutokea ukiwa na wenzako?<br />
Hawa marafiki walikuwa wanahitaji sana Jeckton avute. Kwa nini walimshinikiza?<br />
Watu wengi wanataka kuungwa mkono wanapofanya jambo wanalofikiri siyo sahihi. Wanafikiri<br />
makosa yao yanakuwa madogo kama mtu mwingine anafanya nao. Marafiki zao wanapofanya<br />
jambo la kijasiri pamoja nao, hawajisikii kuogopa sana kuhusu hatari iliyopo. Kama wako katika<br />
kikundi wanajisikia kustarehe na kufurahia burudani wanazozipata kwenye dawa. Ndiyo maana<br />
watakushinikiza sana wewe.<br />
Hapa kuna vidokezo vya jinsi ya kushughulikia hali hiyo:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
jeckton kutoka Kenya (umri wa miaka 15)<br />
“Nilipokuwa na miaka 13, nilikuwa naelekea nyumbani nikiwa na<br />
baadhi ya marafiki zangu. Tulipita sehemu ambayo marafiki zangu<br />
mara nyingine wanaenda kukutana na baadhi ya marafiki zao.<br />
Tulipofika pale waliwakuta marafiki zao na wakapewa kifurushi<br />
cha bangi. Bila kupita muda, msichana mmoja akaanza kuvuta<br />
na akaniambia nivute pafu moja. Nilikataa, wakaanza kunicheka.<br />
Waliniita majina mabaya na wakaniambia niache kuwaaibisha.<br />
Waliniambia ilikuwa tamu sana na ingenifanya nijisikie vizuri. Kwa<br />
sababu sikutaka waelewe kwamba nilikuwa naogopa, niliamua kuvuta<br />
kidogo. Baada ya kuvuta kidogo, siwezi kusema yaliyotokea<br />
baada ya hapo maana sikumbuki tena. Nilichanganyikiwa kwa<br />
muda wa karibu siku tatu.”<br />
Kumbuka kwamba huhitaji kumfanya rafiki ajisikie vizuri kwa kumuunga mkono kufanya<br />
mambo ambayo siyo mazuri kwako.<br />
Kama ni rafiki wa kweli, unaweza kumwambia rafiki yako kuwa mambo anayoyafanya ni ya<br />
hatari.<br />
Uwe mwazi kwa wenzio kwamba hutaki kutumia dawa au kitu. Waonyeshe rafiki zako<br />
kwamba unazijua akili zako zilivyo na kwamba hata wakikusihi vipi hutabadilisha mawazo<br />
yako.<br />
Ondoka kama rafiki yako anazidi kukushinikiza au anaanza kukutukana ama kukucheka.<br />
Usiendelee kujadili suala hilo zaidi. Subiri hadi atakapokuwa hatumii dawa ndiyo mwanze<br />
kuzungumza kuhusu jambo hilo.<br />
Kofi kutoka Ghana (umri wa miaka 16)<br />
“Huwa nashinikizwa na marafiki zangu kutumia dawa za kulevya<br />
ninapokuwa nao, lakini ninajizuia mwenyewe na kuwaeleza kwa<br />
ujasiri kabisa kwamba nimeridhika bila ya kutumia dawa.”<br />
Mara nyingine tatizo linaweza kuwa kubwa zaidi kuliko kukataa shinikizo toka kwa marafiki.<br />
Unaweza kugundua kwamba rafiki yako analo tatizo kubwa la dawa au pombe, tatizo ambalo<br />
unaona linamharibia maisha yake. Hili nalo ni gumu kulitatua. Haya ni mambo machache<br />
unayoweza kufanya:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
SURA YA 13 | MATUMIZI MABAYA YA DAWA<br />
Zungumza na rafiki yako kuhusu matumizi ya dawa wakati hajanywa au hayuko katika hali ya<br />
ulevi.<br />
Usimlaumu au kumkosoa rafiki yako. Hii itazua mabishano baina yenu. Badala yake lenga<br />
katika matatizo ya dawa na mwonyeshe rafiki yako kwamba unaogopa. Jaribu kumsaidia<br />
rafiki yako aelewe kwamba ana matatizo.<br />
Jaribu kumsaidia rafiki yako apate msaada na jaribu kumsaidia akwepe sehemu ambayo<br />
atapata shinikizo la kutumia dawa au pombe.<br />
Margaret kutoka Kenya (umri wa miaka 16)<br />
“Wengi wa marafiki zangu walikuwa wameshaharibiwa na dawa;<br />
lakini baada ya kujua hatari na ukweli kuhusu dawa niliamua kuwasaidia<br />
marafiki zangu. Wengi wamebadilika na mimi ninafurahi.”<br />
Wakati mwingine watu wenye matatizo kutokana na dawa hawako tayari kukusikiliza wewe na<br />
ushauri wako. Wanaweza kuzikataa juhudi zako za kusaidia na wanaweza kukukasirikia. Mnaweza<br />
mkaishia kuwa na mabishano makali na rafiki zako, lakini angalau dhamira yako itakuwa wazi na<br />
utakuwa umejitahidi kuwasaidia.<br />
Wakati wote upo uwezekano wa urafiki kuvunjika kutokana na tabia yako ya kutokubaliana na<br />
tabia zao.<br />
hanifa kutoka tanzania (umri wa miaka 17)<br />
“Nilikuwa na rafiki ambaye nilimwamini sana kwa kipindi kirefu,<br />
lakini sikujua mambo aliyokuwa anayafanya kwa kificho. Siku<br />
moja nilimkuta na watu wenye sura za ajabu, macho yake yalikuwa<br />
mekundu. Niligundua alikuwa ananuka bangi. Nilijaribu kuzungumza<br />
naye mara kwa mara lakini hakunisikiliza. Hivyo nilimtaka<br />
achague ama kuacha kutumia alichokuwa anatumia au kuacha<br />
kuzungumza na mimi. Nilifikiri angefanya uamuzi sahihi lakini<br />
nilikuwa nimekosea aliacha kuzungumza na mimi.”<br />
Inaweza kuwa vigumu sana kumpoteza rafiki lakini angalau ulisimama kwenye kanuni zako,<br />
ulijaribu kumsaidia rafiki na wewe binafsi hukujihusisha na hatari ya dawa. Mara chache, baada<br />
ya muda, rafiki atabadilika.<br />
hanifa kutoka tanzania (umri wa miaka 17)<br />
“Baada ya miezi kadhaa, rafiki yangu aligundua madhara ya dawa<br />
hizo kwa maisha yake, na akaniomba tuendelee kuwa marafiki<br />
tena. Kwa sababu nilimwonea huruma nilikubali.”<br />
167
168<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Kama una wasiwasi kuhusu rafiki yako, jaribu kumsaidia lakini kama rafiki anakataa msaada<br />
wako urafiki hautadumu, usijilaumu. Ulifanya jambo ulilopaswa kwa kadiri ulivyoweza.<br />
Kuacha DaWa<br />
Vijana wengi wanakua katika mazingira ambayo yanazungukwa na aina mbalimbali za dawa<br />
za kulevya. Lakini siyo kila kijana katika sehemu hizi anajihusisha na dawa hizo. Wengine<br />
wanajihusisha, baadhi hawajihusishi. Wengi wanakataa dawa na shinikizo kutoka kundirika kwa<br />
sababu wanayaona matatizo yanayoletwa na dawa za kulevya. Vijana hawa wana msimamo,<br />
wanafikiri wakati wote, na wanajitegemea. Wanakaa kimya, safi na wanafanya mambo<br />
wanayoyaona mazuri kwao.<br />
anthony kutoka Zambia (umri wa miaka 16)<br />
“Nafikiri vijana wanapaswa kujishughulisha na mambo wanayoyapenda<br />
na siyo kukaa bila shughuli kwasababu ubongo<br />
usioshughulishwa ni karakana ya kufikiri maovu. Wanatakiwa<br />
kuwakwepa marafiki wabaya na makundi mabaya. Vilevile, ni<br />
vizuri kwa afya yako kukaa mbali na dawa za kulevya.”<br />
Prisca kutoka Kenya (umri wa miaka 14)<br />
“Yakwepe makundi mabaya yanayotumia dawa na jihusishe na<br />
shughuli za vijana.”<br />
Dawa na pombe zipo tele kila mahali na zinaweza kuwa rahisi kupatikana. Lakini kuwepo<br />
kwa dawa haimanishi kwamba ni lazima uzitumie. Unaweza kuwa mtulivu, fanya mambo yako<br />
mwenyewe na kaa mbali na dawa za kulevya.<br />
Kuwa thabiti. Jitazame kwa uaminifu kujijua wewe ni nani na jinsi unavyotaka uendeshe maisha<br />
yako. Jua kipi ni muhimu kwako, na malengo yako ya baadaye ni yapi na utayapataje malengo<br />
hayo? Fikiria wapi dawa na pombe vinaingia katika mipango yako. Je, vitakusaidia ufanikishe<br />
mipango yako ya baadaye au vitakuzuia?<br />
Vifuatavyo ni vidokezo kutoka kwa vijana kuhusu namna ya kuepukana na dawa:<br />
• Jishughulishe: Jihusishe katika shughuli mbalimbali kama vile michezo au vikundi vya sanaa.<br />
Shughuli hizo zitachukua muda wa kukaa bure na zitakufanya ujisikie vizuri. Hutachoshwa na<br />
hutahitaji kutafuta dawa za kulevya kama kiburudisho.<br />
• Kuwa tofauti: Usitumie dawa ili ufanane na makundi. Kuwa mwenyewe. Fanya yale<br />
yanayokupendeza.<br />
• Jiheshimu: Usitumie dawa za kulevya au pombe kwa ajili ya kufurahisha watu wengine au<br />
kupata ujasiri wa kufanya kitu. Jiheshimu na watu wengine watakuheshimu. Na ukishajua<br />
watu wanakuheshimu utapata ujasiri kwa lolote unalotaka kufanya.<br />
SURA YA 13 | MATUMIZI MABAYA YA DAWA<br />
• Tafuta kukubalika kwenye manufaa: Kuna njia nyingi za kujisikia umekubalika na unapendwa<br />
na watu wengine. Kuna njia nyingi zinazokubalika kuliko kutumia dawa au pombe. Jiunge<br />
na makundi ya watu waliokusudia kufanya jambo fulani, kama kuimba, michezo, maigizo,<br />
kusoma au kusafisha maeneo ya jirani. Tafuta watu watakaokupenda vile ulivyo. Tafuta nini<br />
unaweza kufanya. Tafuta watu ambao hawapotezi muda wao kubwia dawa.<br />
• Jithamini:<br />
Tambua thamani yako. Itetee thamani hiyo.<br />
• Kuwa na nia ya kufanikiwa katika mambo yako: Je, nini ndoto zako? Tazama maisha yako ya<br />
baadaye na ona wapi unataka kwenda. Dawa hazitakusaidia kwenda unakotaka kufika.<br />
• Tumia kila chembe hai ndani ya ubongo wako: Usiruhusu chembe hai za ubongo wako<br />
zikauawa na dawa za kulevya. Soma kwa bidii na fanya vizuri katika kazi zako za shuleni.<br />
• Pata msaada wa kitaalamu: Kama unapata shinikizo la kutumia dawa, nenda kazungumze<br />
na mshauri wa vijana.Pata msaada kama unafikiria unalo tatizo la dawa. Jaribu kutafuta<br />
mshauri na matibabu. Hujachelewa sana kuacha kutumia dawa za kulevya hata kama<br />
umekuwa unatumia muda mrefu. Msaada unapatikana lakini unatakiwa kuchukua hatua ya<br />
kwanza kuutafuta msaada huo.<br />
169
170<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Sura ya 13<br />
Matumizi Mabaya ya Dawa<br />
Kutumia dawa bila sababu za kiafya na kupata hali ya aina fulani kunaitwa matumizi<br />
mabaya ya dawa. Kuna aina nyingi za dawa na vitu vinavyotumika vibaya kama bangi,<br />
miraa, petroli, gundi na dawa kali kama kokeini na heroini. Pombe na sigara nazo pia ni<br />
dawa na mara nyingi zinatumika vibaya.<br />
Dawa zinaweza kuwa na athari nyingi zenye kuleta madhara. Matumizi ya dawa hufanya<br />
mwili uzoee hali ambayo huwezi kufanya chochote bila ya kuzitumia. Dawa pia zinaweza<br />
kuharibu ubongo wako, moyo, mishipa ya damu, na mapafu. Matumizi ya dawa wakati wa<br />
ujauzito yanaweza kuleta matatizo makubwa kwa mtoto.<br />
Vilevile dawa zinaweza kusababisha matatizo mengine. Dawa nyingi zinaweza kukufanya<br />
usifikiri vizuri na usiwe na uamuzi mzuri. Kutokana na hilo, unaweza kuwa hatarini kupata<br />
matatizo ya muda mrefu. Unaweza kufanya ngono bila kinga na kuishia kupata mimba<br />
zisizotakiwa au kumpa msichana mimba na magonjwa ya zinaa kama VVU/UKIMWI.<br />
Zipo sababu nyingi zinazowafanya vijana watumie dawa:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Kujumuika na kundirika.<br />
Kuyakimbia matatizo.<br />
Kuishinda huzuni.<br />
Kujaribu kujibadilisha walivyo ili kuonekana tofauti.<br />
Kutafuta ujasiri wa kuhimili hali ngumu au changamoto.<br />
Kujifurahisha.<br />
Kumudu hali ya kupoteza matumaini.<br />
Hakuna hata sababu moja ambayo ni nzuri ili kuhalalisha matumizi ya dawa. Dawa<br />
zitafanya matatizo yako kuwa magumu zaidi.Unaweza wakati wote kuyavumilia matatizo<br />
bila kuwa na dawa ndani yako. Una utashi wa kuyashughulikia matatizo au hali yoyote ile.<br />
Dawa zinaweza zikaharibu maisha yako ya baadaye. achana na dawa na jishughulishe.<br />
Jihusishe na michezo na mambo mengine ya jumuia. Hutahitaji kutafuta tena furaha au<br />
burudani kutokana na dawa. Kuwa tofauti. Usifanye jambo la hatari ili ulingane na wenzio.<br />
Jiamini na fanya kilicho sahihi kwako. Kama unajiheshimu watu wengine watakuheshimu<br />
pia.<br />
Kama unapata msukumo wa kutumia dawa au kama unafikiri una tatizo la dawa, pata<br />
msaada. Dawa ni kitu chenye nguvu. Usijaribu kupigana na dawa peke yako. Msaada upo<br />
wakati wote, lakini unapaswa kuchukua hatua ya kwanza ya kuomba msaada.<br />
Kutimiza ndoto zako<br />
Kila mtu anazo ndoto za maisha yake ya baadaye, ndoto za kufanya jambo kubwa na kuwa mtu<br />
muhimu na aliyefanikiwa. <strong>Ndoto</strong> hizi zinaonyesha lengo la kupata kitu fulani. Haya ni malengo<br />
yetu na matamanio yetu. Ni maono tuliyonayo kwa ajili yetu wenyewe na kwa ajili ya maisha ya<br />
baadaye.<br />
Zifuatazo ni baadhi ya ndoto chache za vijana balehe:<br />
Sherifa kutoka Ghana (umri wa miaka 15)<br />
“Ninataka kuwa bibi shamba na ninataka kuwa mtu maarufu.”<br />
Omari kutoka tanzania (umri wa miaka 18)<br />
“Ningependa niwe mtu ambaye watu wanakuja kwangu kwa ushauri,<br />
mtu mwenye ndoa imara na pengine kazi kama meneja ofisini.”<br />
naana kutoka Ghana (umri wa miaka 17)<br />
“Ninataka kuwa daktari, hususani kushughulikia wanawake na watoto.”<br />
Patrick kutoka Kenya (umri wa miaka 16)<br />
“Ninafikiria kuwa na shamba dogo<br />
la mifugo lenye ardhi ya kutosha ili<br />
wazazi wangu wakae huko pamoja<br />
na mimi. Ningependa niwe na mke na<br />
nipate watoto watatu.”<br />
Milensu kutoka Zambia (umri wa miaka<br />
13)<br />
“Ninafikiria kuwa na nyumba yangu<br />
mjini ikiwa na sofa sebuleni. Ninataka<br />
kuwa muuguzi, niwe na kliniki yangu na<br />
niheshimiwe na jamii yangu.”<br />
171<br />
SURA YA 14
172<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
<strong>Ndoto</strong> yako ni nini? Ungependa uwe nani? Unajifikiriaje mwenyewe katika miaka mitano ijayo?<br />
Katika miaka15? Utakuwa nani na utakuwa unafanya nini?<br />
Sura hii inahusu kutimiza ndoto zako. Inahusu kuzifikiria ndoto zako na kutafakari ni kwa vipi<br />
unaweza kuzifikia. Inahusu kufanya uamuzi mzuri wa busara na utakaokufikisha karibu na ndoto<br />
zako. Aidha, inahusu namna ya kumudu vipingamizi vitakavyojitokeza katika maisha.<br />
Si jambo rahisi kufanikisha ndoto. Inahitaji kufanya kazi kwa bidii na kuwa na dhamira/nia. Kwa<br />
hiyo, jambo muhimu ni kujishughulisha na kufanya kazi kwa bidii. Fanya vitendo! Usikae chini na<br />
kusubiri mambo yakutokee. Unatakiwa kuyajenga maisha yako ya baadaye.<br />
KuZitaMbua nDOtO ZaKO.<br />
Watu wengine wana ndoto nyingi sana na zinabadilika kila wakati. Kwa mfano mchukue Remijia<br />
wa Tanzania:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Alipokuwa na miaka 6 alitaka kuwa ofisa wa polisi.<br />
Alipokuwa na miaka 8 alitaka kuwa kapteni wa meli.<br />
Alipokuwa na miaka 10 alitaka kuwa rubani wa ndege.<br />
Alipokuwa na miaka 13 alitaka kuwa mwalimu.<br />
Sasa ana miaka 19 anataka kuwa mhandisi.<br />
Kwa nini ndoto hubadilikabadilika? Je, ni vibaya kuwa na ndoto nyingi<br />
zilizo tofauti? Hapana! <strong>Ndoto</strong> ni nzuri, zinatia hamasa na zinakufanya<br />
ufanye kazi kwa bidii. Zinakufanya uangalie maisha ya baadaye na<br />
uwe na mipango thabiti.<br />
Watu wengine wanaelekea kuwa na ndoto chache. Hawajui<br />
wangependa wawe nani wakiwa wakubwa. Wanapata shida kujifikiria<br />
watakuwa vipi miaka 5 ijayo.<br />
Kama yanakugusa, usihofu. Hili ni jambo la kawaida! Haina maana<br />
kuwa huna ndoto, bali ina maana kuwa bado hujafikiria ndoto zako ni<br />
zipi. Lakini, unaweza kuanza sasa kuzitambua ndoto zako.<br />
<strong>Ndoto</strong> za watu wengi zinaathiriwa na watu wanaowazunguka. Kwa<br />
hiyo, kwanza angalia unazungukwa na nini. Fikiria kuhusu watu<br />
walio ndani ya jamii. Ni nani unaowahusudu? Ni watu gani<br />
unaowaheshimu? Mtu anaweza kuwa mwalimu<br />
ambaye anajua majibu ya maswali yote<br />
yanayoulizwa. Anaweza kuwa ni daktari<br />
ambaye alijua kilichokuwa kinakufanya<br />
uumwe miezi michache iliyopita.<br />
Anaweza akawa mchungaji wa kanisa<br />
lako. Wanaweza kuwa wazazi wako.<br />
Pata muda wa kutafakari ndoto zako za baadaye<br />
SURA YA 14 | KUTIMIZA NDOTO ZAKO<br />
Pili, usiruhusu ndoto zako zikakwamishwa na mambo unayoyaona. Angalia hata nje ya jumuia<br />
yako. Kuna mtu ambaye umemsoma kwenye gazeti au kitabuni ambaye alifanya jambo ambalo<br />
linakushangaza? Pengine ni mwanasayansi ambaye anajifunza jinsi tembo wanavyowasiliana wao<br />
kwa wao. Pengine ni muuguzi anayewahudumia wakimbizi katikati ya uwanja wa vita. Wapo watu<br />
wengi wanaofanya mambo mengi mazuri yanayovutia na yenye manufaa na maisha yao. Watu<br />
hawa wanaweza kuwa mfano mzuri wa kuigwa. Wanaweza kukuanzishia ndoto kuhusu maisha<br />
yako ya baadaye.<br />
Tatu, yaruhusu mawazo yako “yapae angani” usijiwekee mipaka ya vitu ambavyo unaweza<br />
kufanya au ambavyo huwezi kuvifanya. Kwa mfano, usiiache ndoto kwa sababu ya mawazo<br />
yaliyopitwa na wakati, kama mawazo kuhusu kazi wanazoweza kufanya wanaume pekee au<br />
wanawake pekee. Mambo yanaenda yakibadilika. Wanawake siku hizi wanafanya kazi ambazo<br />
mama zao hawakuwahi kufikiria kuzifanya. Sasa hivi wanawake wanaweza kuwa wahandisi,<br />
marubani, madaktari, wanariadha, wanasayansi, maprofesa, wanaanga, Marais, waandishi wa<br />
habari n.k. Kama ni mvulana au msichana, unaweza kuwa mtu unayetaka kuwa, ikiwa utadhamiria<br />
na kufanya kazi kwa bidii.<br />
MiPanGO Ya baaDaYe KuhuSu KaZi<br />
Vijana balehe wachache wana vipaji vya ziada katika taaluma fulani, kama hisabati, muziki au<br />
kuchora. Utafikiri kipaji kimewachagua. Wanakuwa wataalamu wazuri wa hisabati, wasanii,<br />
walimu na viongozi wa kwaya au wasanifu majengo.<br />
Watu wengine wanapendelea kitu kimoja tangu utoto wao, na mvuto huo mkubwa unarahisisha<br />
sana wakati wa kutoa uamuzi kuhusu watakuwa nani. Unaweza kumsikia mzazi akisema “wakati<br />
wote tulijua kwamba John atakuwa mganga wa mifugo. Alianza kuwahudumia wanyama wadogo<br />
alipokuwa na umri wa miaka minne tu.<br />
Watu kama hawa, maisha yao yanaonekana kuwa rahisi. Inaonekana kana kwamba njia yao ya<br />
kazi imenyooka. Uamuzi wao unaonekana kuwa ni rahisi kwa sababu wanajua kabisa wanataka<br />
kufanya nini, na wanacho kipaji katika eneo hilo maalumu.<br />
Wengi hatuko hivyo. Wengi ni watu wa kawaida, wenye akili ambao tunaweza kufanya vizuri<br />
katika mambo tofauti. Uwezekano wa kuwa nani au kufanya nini ni matokeo ya mchanganyiko wa<br />
yale tunayoyapenda na tusiyoyapenda, uwezo wetu na utayari wa kufanya kazi kwa bidii na fursa<br />
tunazopata.<br />
Kufanikisha ndoto kwa watu wengi ni njia ndefu yenye kona nyingi. Wakati wote siyo moja kwa<br />
moja na hatua sahihi za kuchukua haziko wazi. Zaidi ya hapo vikwazo visivyotegemewa vinaweza<br />
kujitokeza njiani. Ni mambo ambayo yanatakiwa kushughulikiwa kwa makini sana.<br />
Jitahidi kujitokeza kwenye kazi nyingi iwezekanavyo. Bila kufanya hivyo huwezi kufahamu nafasi<br />
gani zipo duniani kwa ajili yako? Katika nchi nyingine, vijana balehe wanajitolea kufanya kazi<br />
katika mashirika mbalimbali wakati wa likizo. Wakati mwingine wanapata malipo kidogo ya<br />
kutosha usafiri kwenda na kutoka nyumbani. Lakini mara nyingi hawapati chochote. Wanajitolea<br />
tu.<br />
Usifikiri kwamba kwa vile jambo fulani siyo la shule na siyo la kazi ya kulipwa basi halina<br />
thamani. Iwapo unaweza kupata kazi ya kujitolea, pengine unaweza kupata uzoefu mzuri na<br />
wenye manufaa.<br />
173
174<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Kwa mfano unaweza kupata fursa ya kuona jinsi utaratibu wa kazi za ofisini zinavyokuwa na<br />
utaweza kupata hisia nzuri kuhusu kazi wanazozifanya. Unaweza kujua kwamba kazi hiyo<br />
inakufaa au haikufai. Kwa vyovyote itakavyokuwa, uvumbuzi utakuwa muhimu. Kwa jinsi<br />
utakavyokuwa unaendelea utajifunza stadi mpya, utajenga mvuto mpya na utajiamini.<br />
Unapofikiria kuhusu aina ya kazi ambayo ungependa kufanya, vilevile fikiria kuhusu hatua<br />
utakazozichukua. Kwa mfano, fikiria kuhusu watu wenye sifa nzuri uliowachagua. Unafikiri<br />
walifanya nini hadi kufikia hapo walipo? Walihitaji aina gani ya elimu? Aina gani ya mafunzo kwa<br />
vitendo waliyapata?<br />
Njia bora ya kujua namna gani watu walivyofikia hapo walipo ni kuwauliza. Iwapo wapo watu<br />
ambao unawaheshimu na ambao mafanikio yao unayahusudu, waulize kama wanao muda<br />
wakuambie jinsi walivyofikia pale walipo. Kabla hamjakutana, andika orodha ya maswali ambayo<br />
ungependa kuwauliza, Kwa mfano; ni kitu gani kilisababisha kuchagua kazi wanayoifanya na ni<br />
aina gani ya elimu na mafunzo waliyapata. Wanapenda nini zaidi kuhusu kazi yao? Ni kitu gani<br />
hawakipendi?n.k.<br />
Watu wengi wanafurahi sana na kujisikia sifa wakati mtu mwingine anavutiwa na mafanikio yake<br />
na pale wanapoombwa ushauri. Kawaida watu watakuwa na shauku ya kukueleza habari zao na<br />
kukusaidia njia utakayochagua. Unahitaji ujasiri kumwendea mtu mzima ambaye humjui vizuri,<br />
lakini utashangaa wengi wao watakuwa wazuri na watakusaidia, wanaweza kukushauri jinsi ya<br />
kupanga kazi yako.<br />
KuWeKa MalenGO<br />
Ni vema kuweka malengo, mambo unayoyategemea kwa maisha ya baadaye. Vilevile, unahitaji<br />
kujiwekea malengo mahususi ambayo yanaweza kukamilishwa katika muda mfupi.<br />
Lengo ni kuwa na jambo unalotaka kulifanyia kazi. Kuna aina mbili za malengo. Malengo ya muda<br />
mfupi na mrefu. <strong>Ndoto</strong> zako ni malengo ya muda mrefu. Haya ni mambo unayoyawazia kutokea<br />
baadaye katika muda mrefu.Malengo ya muda mfupi ni mambo ya muda mfupi. Ni mambo<br />
yatakayotokea kesho, juma lijalo au mwaka kesho. Malengo ya muda mfupi ya baadhi ya vijana<br />
balehe ni haya yafuatayo:-<br />
Sofia kutoka uganda (umri wa miaka 14)<br />
“ Itakapofikia mwisho wa mwaka wa kwanza wa sekondari,<br />
ninataka kushika namba za juu, nusu ya darasa.”<br />
essie kutoka Ghana (umri wa miaka 15)<br />
“Nitakapofikia umri wa miaka 16 ninataka kujua jinsi ya kutumia<br />
kompyuta.”<br />
Francis kutoka Kenya (umri wa miaka 16)<br />
“Mwakani ninataka kupiga solo katika kwaya ya kanisa”.<br />
Miriam kutoka Zambia (umri wa miaka 16)<br />
“Ninataka kufanya vizuri katika mitihani yangu ili niandikishwe<br />
katika shule nitakayoichagua.”<br />
Patrick kutoka Zimbabwe (umri wa miaka 18)<br />
“Ninataka kujifunza jinsi ya kuzungumza mbele ya kadamnasi.”<br />
Una malengo gani? Ni mambo gani ambayo ungependa kuyafanya ifikapo mwisho wa mwaka<br />
huu? Je, mwisho wa mwaka ujao?<br />
Malengo yana manufaa sana. Unapokamilisha lengo<br />
unaweza kulifuta kwenye orodha. Inakupa hisia ya mafanikio<br />
na furaha ya kukamilisha jambo. Inakufanya ujisikie<br />
vizuri. Inakuonyesha kwamba unapofikiria kitu unaweza<br />
kufanikisha.<br />
Malengo yanatakiwa yawe halisi na ambayo yanawezekana<br />
kutekelezeka- mambo ambayo unaweza kufanikisha. Wakati<br />
mwingine watu huweka malengo ambayo si halisi, kama vile<br />
kuwa tajiri sana. Watu wengi hawawi matajiri na hata wale<br />
wanaokuwa matajiri pengine walikuwa na malengo halisi<br />
kama vile kuanza biashara zao. Waliendesha biashara kwa<br />
muda mrefu kiasi cha kufanikiwa sana.<br />
Wakati mwingine watu wanaweka malengo yasiyofaa,<br />
mathalani kuhusu mambo ya kufanya mapenzi. Vijana balehe<br />
wengine wanajiambia:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
“Likizo hii lazima nipoteze ubikira wangu.”<br />
“Lazima nijamiiane nikifikisha umri wa miaka 16”<br />
Nitajaribu kujamiiana na msichana mwingine zaidi ya rafiki yangu wa kike.”<br />
Malengo kama haya hayana manufaa. Ukiyafanikisha pengine hutajisikia vizuri. Hebu fikiria:<br />
Hivi kweli kujamiiana ndilo lengo lako? Je, umeweka lengo hili kwa sababu tu unapata shinikizo<br />
ili usiwapoteze marafiki? Je, unafikiri marafiki zako wote wanajamiiana, hivyo wewe unabaki<br />
nyuma? Hizi siyo sababu nzuri za kujiwekea malengo.<br />
Fikiria kile ambacho wewe mwenyewe unataka kufanikiwa na weka maanani mwongozo huu wa<br />
kuweka malengo:-<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
SURA YA 14 | KUTIMIZA NDOTO ZAKO<br />
Hakikisha malengo yako ni mazuri na yana manufaa.<br />
Hakikisha malengo ni halisi na yanatekelezeka.<br />
Hakikisha hayakuingizi katika hatari yoyote<br />
Hakikisha ni malengo yako wewe na siyo ya mtu mwingine.<br />
Ukifanikisha lengo utajisikia vizuri<br />
175
176<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Baada ya kuyatambua malengo yako, fikiria jinsi utakavyoyafanikisha. Weka mpango mzuri<br />
mwenyewe. Halafu jiulize maswali haya manne:<br />
Kwa nini? Ni sababu gani zinakufanya uwe na lengo hili?. Kwa nini unataka kulifanikisha?<br />
namna gani? Hatua gani utakazozichukua kufanikisha lengo hili? Utafanya nini?<br />
lini? Utamaliza lini kila hatua uliyoiweka katika kufanikisha lengo? Utafanikisha lengo lako lini?<br />
nini? Utahitaji nini ili kufanikisha lengo lako?<br />
Kwa mfano: Tuchukulie labda unataka kufanya vizuri zaidi katika somo la Hisabati. Kwa nini<br />
unataka kufanya vizuri zaidi? Pengine ni kwa sababu unajua unaweza kufanya vizuri zaidi kuliko<br />
ulivyowahi kufanya siku za nyuma. Unafaulu sana katika masomo mengine isipokuwa Hisabati.<br />
Una akili, na wala huhitaji kusoma sana ili ufanye vizuri masomo mengine. Hata hivyo, unaona<br />
Hisabati ni ngumu zaidi.<br />
ni kwa namna gani utaboresha alama zako<br />
za Hisabati? Labda utaanza kufanya marudio<br />
zaidi, kwa kupata msaada wa ziada baada<br />
ya masomo na baada ya mazoezi ya maswali<br />
zaidi.<br />
lini utachukua hatua zote hizi? Labda<br />
utaamua kutumia saa moja nzima kila siku<br />
kujifunza Hisabati baada ya kutoka shule na<br />
saa mbili siku za mwisho wa wiki.<br />
utahitaji nini kikusaidie uboreshe alama<br />
katika Hisabati? Labda unahitaji muda zaidi.<br />
Pengine huwa unamsaidia shangazi yako<br />
shughuli za dukani kila siku jioni. Mweleze<br />
shangazi yako kuhusu lengo lako na mwombe<br />
kama anaweza kukuachia mapema ili uweze<br />
kujisomea. Pengine unahitaji maswali mengi<br />
ili ufanye mazoezi. Mwombe mwalimu wako<br />
akupe maswali ya ziada ya kufanya nyumbani.<br />
Ukipanga vizuri na kufanya kazi kwa bidii unaweza kutimiza malengo yako.<br />
KuFanYa uaMuZi MZuRi (Wa buSaRa).<br />
Panga mipango vizuri ili uweze kufikia<br />
malengo na ndoto zako<br />
Kufanya uamuzi mzuri kunaweza kukusaidia kutimiza malengo yako na hatimaye kufanikisha<br />
ndoto zako. Uamuzi mzuri haimaanishi kuwa ukiwa na miaka 13 unaweza kufanya uamuzi sahihi<br />
kuhusu utakuwa nani maishani mwako. Kufikiria utakuwa nani siyo uamuzi. Hiyo ni ndoto na ni<br />
lengo la muda mrefu.<br />
Kufanya uamuzi ni tofauti. Uamuzi ni uchaguzi kati ya njia moja au nyingine zinazowezekana<br />
kutumika. Kufanya uamuzi ni kitendo cha kila siku. Utafanya mamia ya uamuzi mpaka ufikie<br />
mafanikio ya ndoto zako.<br />
Je, uende nyumbani baada ya masomo<br />
ukajisomee au ubaki shuleni kucheza<br />
na wenzako? Je, ukubali kujamiiana<br />
na rafiki yako wa kike au usubiri?<br />
Unatakiwa ufanye uamuzi wa busara<br />
kila siku.<br />
Mojawapo ya mambo muhimu katika<br />
kufanya uamuzi ni kuangalia mbele<br />
na kuona kitu gani kinaweza kutokea<br />
iwapo utafanya kitu fulani. Tunaita<br />
kutabiri matokeo yanayoweza kutokea.<br />
Jinsi unavyoweza kutabiri matokeo<br />
mapema ndivyo utakavyofanya<br />
uamuzi mzuri utakaoleta matokeo<br />
unayoyataka.<br />
Kwa mfano, labda unataka kuamua<br />
uende nyumbani kwa rafiki yako baada<br />
ya kutoka shuleni. Iwapo utaenda<br />
nyumbani kwao itasaidia kuimarisha<br />
urafiki wenu kwa vile msichana<br />
huyu anajulikana sana shuleni na<br />
amewaalika wasichana wengi kwao.<br />
Kwa muda mrefu umekuwa unataka<br />
kuwa rafiki na kikundi hiki kwa hiyo<br />
unafurahi sana kualikwa ili kupata<br />
wasaa wa kuwa nao.<br />
SURA YA 14 | KUTIMIZA NDOTO ZAKO<br />
1.<br />
2.<br />
3.<br />
4.<br />
5.<br />
6.<br />
7.<br />
Je, Unafahamu hatua muhimu za kuchukua<br />
unapofanya uamuzi?<br />
Fafanua tatizo, hali au suala ambalo unahitaji<br />
kufanyiwa uamuzi.<br />
Tambua uchaguzi wote wenye kuwezekana au<br />
njia utakazotumia.<br />
Fikiria matokeo ya kila utakalochagua.<br />
Fikiria maadili na imani yako kuhusu<br />
kinachostahili na ambacho hakistahili ni jambo<br />
gani la kufanya linaloendana na maadili yako.<br />
Fikiria jinsi uamuzi wako unavyoweza kuathiri<br />
watu wengine.<br />
Chagua jambo la kufanya ambalo kigezo chake ni<br />
ufahamu wako, maadili, thamani, malezi ya kidini<br />
na malengo yako.<br />
Tathmini uamuzi wako na jinsi unavyojisikia amua<br />
kama ulifikiria kwa uangalifu na chunguza tena ili<br />
uweze kujisikia safi na uchaguzi ulioufanya.<br />
Kwa upande mwingine, mama yako anaweza kukasirika kama ukienda bila ya kuomba ruhusa.<br />
Zaidi ya hapo unakabiliwa na mtihani wiki ijayo na ulikuwa umeahidi ungeanza kujisomea<br />
mapema. Ukienda nyumbani kwa huyu msichana, utakuwa na muda mfupi wa kujisomea kwa ajili<br />
ya mitihani, na unaweza kupata maksi chache.<br />
Toa uamuzi wako binafsi. Usiruhusu watu wengine wafanye kwa ajili yako.<br />
177
178<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Uamuzi kama huu unaweza kuwa mgumu. Masomo yako na uhusiano mzuri na mama ni muhimu<br />
kwako. Lakini wakati huohuo, unataka kuwa na urafiki na kikundi hiki cha wasichana. Hayo ni<br />
muhimu kwako vilevile. Vyovyote vile, itabidi upime vipengele vyote na kuona ni kipi kizuri<br />
kwako. Kitu gani kitakuwa kizuri kwa muda mrefu. Lolote utakaloamua hakikisha ni uamuzi wako.<br />
Hakikisha unachagua jambo moja kwa sababu ndilo unalolitaka – siyo kwa sababu kuna mtu<br />
anakulazimisha kufanya hivyo.<br />
Mara kwa mara tathmini uamuzi wako na jinsi unavyojisikia kuhusu uamuzi huo. Je, unajisikia<br />
kama uliyefanya uamuzi sahihi? Kama sio, utafanya nini ili uyabadilishe? Kwa mfano, labda<br />
unaamua kuanza kujamiiana na rafiki yako wa kiume lakini unajua ulikuwa siyo uamuzi sahihi<br />
kwako. Unahofu kubwa ya kupata mimba na kuwasikitisha wazazi. Unajua kwamba wewe na<br />
rafiki yako wa kiume mngetumia dawa za kuzuia mimba lakini kitu ambacho kingefaa zaidi ni<br />
kutojamiiana.<br />
Uamuzi mwingine unaweza kubadilishwa. Kwa hiyo, ni muhimu kutathmini mara kwa mara.<br />
Unaweza kuamua kuacha kujamiiana. Kamwe usiseme nimechelewa kufanya uamuzi mzuri.<br />
ZinGatia bila KuYuMba KatiKa MalenGO na nDOtO ZaKO.<br />
Wakati mwingine inakuwa vigumu kubaki umelenga katika makusudio au ndoto zako. Wakati<br />
mwingine matokeo unayoyataka yanaonekana kuwa mbali na hayafikiki. Unaweza kuhisi<br />
kushawishika kufurahia maisha sasa na kuacha maisha ya baadaye yawe yatakavyokuwa.<br />
Unaweza kuamua kuacha kusoma kwa bidii, na<br />
badala yake ukawa unafurahi na marafiki zako<br />
tu.<br />
Wakati mwingine watu wanaweza kukukatisha<br />
tamaa. Wanaweza kukufanya ufikiri hutaweza<br />
kufikia ndoto zako. Kwa mfano, vijana wengine<br />
wanapata msukumo mkubwa wa kuoa au<br />
kuolewa mapema na kuanza kuzaa watoto.<br />
Vilevile inaweza kuwa vigumu kama unafuata<br />
njia ambayo siyo ya kawaida - kufuatilia ndoto<br />
ambayo iko tofauti na za rika lako. Inaweza kuwa<br />
vigumu zaidi kama unafuatilia kazi ambayo watu<br />
wengi wa jinsi yako hawapendi.<br />
Simama imara katika ndoto yako.<br />
usikubali kuyumbishwa<br />
aromo kutoka uganda (umri wa miaka 19)<br />
“Rafiki zangu mara kwa mara wananitania kwamba kazi ya uhandisi<br />
na umakanika ni kazi ya wanaume na kwamba hakuna mwanaume<br />
atakayenioa. Lakini ninataka kufika hapo na kuona itakavyokuwa.<br />
Siwasikilizi na ninasoma kwa bidii. Mambo mengine yatafuata<br />
baadaye.”<br />
Sherry kutoka Ghana (umri wa miaka 19)<br />
“Ninataka kuwa mhandisi sanifu majengo. Baba yangu ni mkandarasi<br />
wa ujenzi na aliniambia ni fani nzuri. Jinsi Ghana inavyobadilika,<br />
kutakuwa na ujenzi mwingi na fani hii itakuwa nzuri.<br />
Lakini itakuwa vigumu kwa mwanamke pekee. Kutakuwa na ubaguzi.<br />
Hata mjomba hakubaliani na jambo hili kwa sababu anasema<br />
wanawake ni dhaifu. Anasema asingemwajiri mwanamke kama<br />
angepata nafasi ya kuajiri. Ananishauri niende kusoma fani ya<br />
uhasibu.”<br />
Inaweza kuwa vigumu kuendelea na malengo yako wakati watu wengine wanakukatisha tamaa<br />
na kukwambia huwezi kufanya kitu hicho. Vivyohivyo, ni ngumu kubakia na lengo wakati watu<br />
wengine wanakwambia fanya upesi na uwe na furaha. Bila ya kujali watu wengine wanasema nini,<br />
bakia mkweli na ndoto zako.<br />
Iwapo watu watakwambia kwamba<br />
huwezi kufanya kwa sababu ni<br />
mwanamke au ni mwanaume, zidisha<br />
kufanya kazi mara mbili ya ulivyozoea.<br />
Unaweza kufanya kazi yoyote ambayo<br />
akili yako inakutuma na unayoimudu.<br />
Wanaume na wanawake wana uwezo<br />
sawa wa kufanya kazi, hata kama<br />
hawapewi nafasi sawa wakati wote.<br />
Iwapo unashinikizwa na wazazi wako<br />
uolewe au uoe au uache masomo<br />
mapema, jaribu kupata ushauri kutoka<br />
kwa mwalimu, shangazi, mjomba,<br />
kiongozi wa jamii ama mtu mmoja kutoka<br />
kanisani kwako au msikitini. Waombe watu hawa ushauri na uone kama wanaweza kukusaidia<br />
uzungumze na wazazi kuhusu umuhimu wa elimu na mafunzo. <strong>Ndoto</strong> zako ni muhimu, na itakuwa<br />
vigumu kuzifuatilia wakati unahudumia familia.<br />
KuFanYa ViZuRi KatiKa MaSOMO Shuleni<br />
Kufanya vizuri shuleni kunahitaji bidii na nia. Elimu ni ufunguo wa maisha. Welewa ni zawadi<br />
nzuri zaidi ambayo unaweza kujipatia mwenyewe. Jaribu kubaki shuleni kwa muda mrefu<br />
iwezekanavyo. Kila mwaka utapata ufahamu zaidi na stadi zaidi zitakazokusaidia ufanikishe<br />
ndoto zako.<br />
Vifuatavyo ni vidokezo vichache vya kukusaidia kufanya vizuri katika elimu:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Jiwekee utaratibu mzuri wa kufanya mambo yako.<br />
Jiandae kwa ajili ya masomo. Usiache muda wa mazoezi ya masomo hadi dakika za mwisho.<br />
Weka muda wa kujisomea<br />
SURA YA 14 | KUTIMIZA NDOTO ZAKO<br />
Weka muda wa kujifurahisha na kupumzika. Kufanya kazi wakati wote bila ya kucheza<br />
kunamfanya mtu achoke na asiwe mchangamfu. Kwa hiyo, kuwa mwangalifu kupanga muda<br />
wa kujifurahisha, kufanya mazoezi na muda kwa ajili ya marafiki na familia.<br />
Kula vizuri na pata muda wa kulala usingizi ili usisinzie darasani.<br />
iwapo unashinikizwa kwamba uolewe “mapema”<br />
zungumza na mtu mmoja kama mwalimu,<br />
ambaye anaweza kukusaidia.<br />
179
180<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Shiriki darasani. Hata kama unaona aibu, unahitaji kujifunza kuzungumza. Mwonyeshe mwalimu<br />
wako kwamba unasikiliza kwa makini na unafanya kazi kwa bidii. Hii ni muhimu kwa wasichana.<br />
Wasichana wengine wanaogopa kuongea darasani na wanawaacha wavulana peke yao<br />
wasikilizwe.<br />
Unajua jinsi ya kujiandaa vizuri kwa ajili ya mitihani?<br />
Katika shule nyingi, mambo mengi yanategemea matokeo ya mitihani, kama ilivyo Kidato cha<br />
Nne na cha Sita. Hapa kuna vidokezo vichache vya namna ya kujiandaa kwa ajili ya mitihani:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Wasichana zungumzeni darasani msikae tu kimya na kuwaacha wavulana peke yao<br />
wasikilizwe na mwalimu<br />
Pitia tena madaftari kila siku kwa makini. Usisubiri mpaka siku ya mwisho.<br />
Panga ratiba yako ya kila siku na kumbuka muda wa kufanya kazi za shule.<br />
Andika muhtasari “tini” ili uweze kukumbuka vipengele muhimu siku ya mitihani.<br />
Tumia muda wa ziada katika masomo yanayokushinda na jaribu kupitia marudio kwa<br />
msaada wa mwalimu.<br />
Ukianza kupata mfadhaiko, pumzika. Cheza michezo au soma kitabu cha hadithi. Karuke<br />
kamba au nenda katembee ili kutuliza mishipa ya fahamu.<br />
Kitu muhimu siku ya mtihani ni kutulia!<br />
Fika kwenye chumba cha mtihani muda uliopangwa. Ukichelewa utakuwa na wasiwasi na<br />
itakuwa vigumu kufikiri kwa makini.<br />
Ukipewa karatasi za mtihani usifanye kitu chochote dakika chache za mwamzo. Acha<br />
mapigo ya moyo wako yashuke kidogo kwa sababu ukirukia moja kwa moja kujibu maswali<br />
unaweza kufanya makosa ya kijinga.<br />
Soma maelezo na maswali kwa uangalifu mkubwa ili kuhakikisha umeelewa maswali.<br />
Mtahini atakayesoma majibu yako ataangalia ni jinsi gani umetafsiri swali. Panga majibu<br />
na weka hoja zako vizuri.<br />
Anza kujibu maswali ambayo ni rahisi kwako. Hii itakuongezea hali ya kujiamini. Watahini<br />
hawatakuadhibu kwa kutojibu maswali kwa mpangilio uliopo ili mradi umejibu maswali<br />
vizuri na umeandika namba ya kila swali. Usianze na swali gumu kuliko yote kwani<br />
litakufanya upoteze matumaini ya kujiamini. Pia, utapoteza muda mwingi kufikiria majibu.<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Kuacha Shule.<br />
SURA YA 14 | KUTIMIZA NDOTO ZAKO<br />
Unajua jinsi ya kujiandaa vizuri kwa ajili ya mitihani? (Endelea)<br />
Usiangalie huku na huku unapofanya mtihani. Unaweza kupata wasiwasi na hofu ukiona<br />
wanafunzi wenzako wanaandika haraka. Usitetemeke unapoona watahiniwa wengi<br />
wanaomba karatasi za ziada. Walimu hawaangalii kiasi gani ulichoandika bali ni kwa<br />
namna gani umelijibu swali na kwa jinsi gani mawazo ya majibu yako yalivyopangiliwa.<br />
Watu wengine wanaandika upuuzi mtupu!<br />
Kumbuka mwandiko ni muhimu uwe mzuri kwani mtahini anahitaji kusoma ulichoandika.<br />
Baada ya mtihani, epuka kujadili majibu na wenzako. Ukizungumzia unaweza ukajikuta<br />
unajihisi kwamba majibu yako siyo mazuri ya kutosha na hii haitakusaidia kujiandaa kwa<br />
mitihani itakayofuata.<br />
Utakapopata karatasi za majibu ziangalie kwa makini. Angalia maswali ambayo ulikosea<br />
kujibu ili ujue wapi unatakiwa kufanya kazi kwa bidii. Fikiri kuhusu aina ya maswali<br />
yanayokupa matatizo ili ujiandae vizuri zaidi safari ijayo. Usisahau kuangalia maswali uliyojibu<br />
kiusahihi na kujipongeza kwa kazi nzuri.<br />
Vijana balehe wengi wanalazimika kuacha shule kabla ya kumaliza masomo. Labda wazazi<br />
hawana uwezo wa kuwalipia karo au pengine wanapata mimba kwa makosa na wanalazimika<br />
kuacha shule.<br />
Hali hizi ni ngumu, lakini haimaanishi kwamba utashindwa maisha sehemu nyingine. Itakubidi<br />
kufikiria upya ndoto na malengo yako. Kama ni mbunifu na unayo maarifa unaweza kushinda<br />
maisha. Usifikiri maisha yako sasa yamekwisha, ila:<br />
• angalia watu wanaokuzunguka. Vijana wengine ambao hawapo shuleni wanazikamilisha vipi<br />
ndoto zao? Wanafanya nini?<br />
• angalia nafasi na rasilimali zilizopo kwa ajili yako. Hata kama huwezi kuendelea na shule,<br />
zipo njia nyingine za kupata mafunzo mazuri. Kwa mfano, kama uliacha shule kwa sababu<br />
ya mimba, tafuta kama kuna kituo cha akinamama ambako unaweza kwenda kwa ajili ya<br />
mafunzo na kozi. Pengine kunaweza kuwa na mfuko wa mkopo kwa jamii wa kusaidia watu<br />
kuanza miradi midogomidogo ya kuongeza kipato.<br />
• Omba ushauri kwa watu. Kutoka kwa wazazi, mjomba, shangazi, majirani, viongozi ndani<br />
ya jumuia au hata mwalimu wako wa zamani. Watu hawa wanaweza kuwa na maoni mazuri<br />
kuhusu kazi au mambo ambayo ungeweza kuyafanya.<br />
• Fikiria upya malengo yako na mikakati kwa ajili ya kuyatimiza. Labda haitawezekana<br />
kuwa daktari, lakini kuna mambo chungu nzima ambayo unaweza kuyafanya vizuri. Unaweza<br />
kuamua kuanzisha biashara ndogo. Je, utafanyaje? Labda unaweza kuunda kikundi na rafiki<br />
zako. Mwombe kila mtu achangie kwenye mfuko wa pamoja utakaotumika kama pesa za<br />
mtaji kwa ajili ya biashara. Pengine unaweza kuzungumza na wafanyabiashara wakupe<br />
ushauri jinsi walivyofanikiwa na namna ya kuanza. Unaweza ukawaalika wawekezaji kwenye<br />
biashara yako kama unaweza kuwashawishi kwamba ni wazo zuri.<br />
181
182<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
• Kuwa mbunifu.<br />
Kama rafiki zako wote wanauza magazeti mitaani au kwenye taa za<br />
barabarani, unaweza kufikiria kuuza kitu kingine au kufanya jambo jingine. Kuungana nao<br />
kuuza magazeti kunaweza kufanya usipate kipato cha kutosha ili kuweka akiba ya pesa ya<br />
kuanzishia shughuli nyingine.<br />
Kutatua ViPinGaMiZi<br />
Kama upo shuleni au upo nje ya shule, siyo kila mara mambo yataenda kama ulivyopanga. Wakati<br />
mwingine kizuizi kikubwa hutokea katika mchakato na kusababisha ugumu katika kufanikisha<br />
malengo uliyojiwekea. Vizuizi hivi<br />
vinasababisha ugumu na mara nyingine<br />
vinakurudisha nyuma kabisa.<br />
Unafahamu jinsi ya kuvikabili vipingamizi?<br />
Vipingamizi vinaweza kuwa vigumu na<br />
kukatisha tamaa, lakini vinatokea kwa<br />
kila mtu. Jinsi utakavyochukulia vizuizi<br />
vya maisha visivyoepukika ndivyo jinsi<br />
vitaamua ni kwa namna gani utafanya<br />
vizuri kuzifikia ndoto zako yawezekana<br />
isiwe ile ndoto yako ya mwanzo lakini<br />
ikawa ni ndoto nzuri pia.<br />
Vipingamizi vinaweza kutokea kwa<br />
sababu ya matukio yaliyo nje ya<br />
uwezo wako – mambo ambayo huwezi<br />
kuyadhibiti, kama vile mabadiliko<br />
katika hali ya kiuchumi ya familia<br />
yako. Pengine biashara ya baba yako<br />
imeanguka au mama yako ameugua<br />
na hivyo hawawezi kulipa karo. Jambo<br />
kama hili likitokea itabidi utumie nguvu<br />
zako zote ulizo nazo kupata ufumbuzi.<br />
Je, yupo ndugu yeyote ambaye<br />
anaweza kukusaidia kulipa karo? Je,<br />
shule inaweza kukupunguzia karo kwa<br />
sababu umekuwa mwanafunzi mzuri?<br />
Je, unaweza kuhamia shule ambayo ni<br />
nafuu kidogo?<br />
Wakati mwingine unaweza kupata<br />
vipingamizi ambavyo viko nje kabisa ya<br />
uwezo wako. Labda zipo nafasi 20 za<br />
Chuo Kikuu kwa wanafunzi wa wilaya<br />
yako kusomea uhandisi. Ushindani ni<br />
mkubwa mwaka huu. Wanafunzi 80<br />
wanashindania nafasi hizo. <strong>Wewe</strong> ni wa<br />
21 katika mitihani.<br />
Unafahamu jinsi ya kuvikabili vizuizi? Wakati<br />
wote Tom alitaka kuwa daktari. Lakini vita<br />
vilitokea katika eneo lake alipokuwa na umri<br />
wa miaka 15, na hakufanya mitihani. Hatimaye<br />
alipofanya hakuweza kumudu kununua kitabu cha<br />
Kemia na ilibidi asome muhtasari “tini”. Hakufaulu<br />
kuingia shule ya udaktari.<br />
Tom alisikitika sana lakini aliendelea kupendelea<br />
mambo ya afya. Kwa hiyo wazazi wake<br />
walimhimiza afanye kozi ya mambo ya elimu ya<br />
afya. Tom alijisikia mbadala huu ni dhaifu. Lakini<br />
alifanya kazi kwa bidii na baada ya miaka miwili<br />
alifuzu kozi hiyo. Baada ya hapo alipata kazi kama<br />
mkaguzi msaidizi wa afya katika eneo dogo la<br />
Wilaya iliyoko nje ya mji. Alifanya vizuri kazini<br />
kwake na baadaye aliajiriwa na shirika moja<br />
ambalo walimpeleka kupata mafunzo kadhaa.<br />
Mwaka jana Tom alipandishwa cheo akawa<br />
Mratibu wa mradi wa Shirika la Afya kwenye<br />
wilaya tatu. Anawasimamia madaktari watatu.<br />
Tom amefanikiwa. Siri ya mafanikio yake ni<br />
pamoja na:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Kuwa mkweli kuhusu kupendelea masuala ya<br />
afya.<br />
Kukubali na kuwa tayari kufanya jambo<br />
lingine baada ya mpango wa kwanza<br />
kushindikana.<br />
Uwezo wake mkubwa wa kufanya kazi na<br />
kujituma katika yote anayofanya.<br />
Hii inaweza kukuwia vigumu. Utalishughulikia namna gani tatizo hili? Tukio mojawapo ni<br />
kufadhaika sana na kukata tamaa. Njia ya ufumbuzi ni kuwa na mtazamo wa kushinda. Unaweza<br />
kushughulikia namna gani hali hii? Umekosa nafasi hii kwa pointi moja tu! Je, ipo kozi nyingine<br />
Chuo Kikuu ambayo unaweza kuanza nayo halafu uhamie uhandisi baadaye? Je, kuna Chuo Kikuu<br />
kingine? Unaweza kurudia mitihani? Wanafunzi wote 20 wataenda Chuo Kikuu? Je, ukifuatilia<br />
kwa karibu zaidi utaipata nafasi hiyo au la?<br />
Kipingamizi chochote kitakachokupata kisikuvunje moyo na wala usikate tamaa. Jaribu kutatua<br />
tatizo. Upo usemi kwamba “penye nia pana njia” ambao unamaanisha kuwa endapo una nia ya kitu<br />
utatafuta njia ya kufanikisha.<br />
Wakati mwingine vipingamizi<br />
vinatokea kwa sababu ya matatizo<br />
uliyonayo. Aidha, nguvu yako<br />
haiendani na njia uliyochagua au kwa<br />
sababu ya mtazamo wako na namna<br />
unavyolishughulikia jambo lenyewe.<br />
Vipingamizi vinavyosababishwa<br />
na udhaifu wako ni vigumu<br />
kuvishughulikia. Moyo wako unaweza<br />
kutaka kufanya kitu lakini ikatokea<br />
kuwa hufai kufanya jambo hilo.<br />
Kwa mfano, moyo wako ulipenda<br />
kuwa daktari lakini biolojia na<br />
kemia unashindwa kumudu. Huwezi<br />
kukumbuka mambo haya hata<br />
kama utakariri masomo hayo mara<br />
kwa mara. Unafanya vibaya katika<br />
majaribio ya masomo haya, ingawa<br />
unafanya vizuri katika masomo<br />
mengine.<br />
Jambo kama hili likitokea unatakiwa<br />
kujikosoa mwenyewe. Fikiria kuhusu<br />
uwezo wako na udhaifu wako.<br />
Wapi unafanya vizuri. Ufanye nini<br />
kitakachokuwa sawa na uwezo wako?<br />
SURA YA 14 | KUTIMIZA NDOTO ZAKO<br />
Kutambua uwezo wako na jinsi ya<br />
kufanya zaidi ya uwezo wako inaweza<br />
kuwa vigumu. Ni vigumu kujiona<br />
wewe mwenyewe, na kujua aina zako<br />
za uwezo. Kama unapata matatizo<br />
kutambua jaribu kuzungumza na mtu<br />
unayemfahamu – mzazi, kaka, dada,<br />
shangazi , mwalimu au mshauri. Watu<br />
hawa wanaweza kuwa wameona uwezo wako ambao wewe hujauona.<br />
Ni kwa vipi utautumia uwezo wako wote?<br />
Susan alikuwa na uhakika kuwa atakuwa mwandishi<br />
wa habari. Alipata kazi ya kujitolea kwenye gazeti<br />
moja la wanawake. Wafanyakazi wenzake walimpa<br />
kazi ya kuandika na kumpa mapendekezo ya namna<br />
ya kuandika makala. Lakini kila alichoandika<br />
kilikuwa kibaya japo alijitahidi sana. Mawazo<br />
yalipotea kila alipojaribu kuandika, na ilimchukua<br />
saa nzima kuandika aya moja.<br />
Alikaa hapo kwa muda wa miezi mitatu bila ya<br />
kuandika makala yoyote. Susan alianza kuingiwa na<br />
hofu. Alikuwa anatumaini kufanya kozi ya uandishi<br />
wa habari baada ya kumaliza Kidato cha Sita.<br />
Ingawa wafanyakazi wote pale walikuwa wazuri<br />
kwake, mwanamke mmoja ambaye alibuni gazeti<br />
alikuwa mzuri zaidi. Susan aliamua kwenda<br />
kuzungumza naye na kumwomba ushauri. Yule<br />
mwanamke alimwambia Susan asihofu sana. Vilevile<br />
alimshauri Susan ajaribu mambo mengine pale.<br />
Halafu akamwacha Susan ajaribu mikono yake<br />
kwenye kompyuta na ikatokea kwamba Susan<br />
alikuwa na jicho zuri kwa picha na ramani. Kwa<br />
furaha, Susan alibadilisha na kusoma kozi ya usanifu<br />
wa grafu.<br />
Ingawa uandishi wa habari hakuufanikisha, Susan<br />
alipata kazi nyingine ambayo aliipenda kweli. Susan<br />
alikuwa na uwezo wa kubadili mawazo. Hakukata<br />
tamaa badala yake alifanya kila kazi kwa uwezo<br />
wake na kwa nafasi iliyojitokeza.<br />
183
184<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Kitu kibaya kuliko vingine vyote na ambacho kitakachokurudisha nyuma ni mtazamo wako<br />
mwenyewe. Siku nyingine unahisi kama hutaki kujaribu zaidi. Umechoka au unajisikia hufai ama<br />
ghafla unafikiri njia uliyochagua ni ngumu mno na kwamba matunda na mafanikio viko mbali<br />
sana.<br />
Mtazamo wako mwenyewe unaweza kuwa kikwazo. Vikwazo vyenyewe ni:<br />
• MaWaZO MabaYa. Unajiambia mwenyewe kwamba una bahati mbaya na kwamba u mjinga.<br />
Hapohapo unatumia mawazo haya kuwa sababu ya kushindwa kufanya jambo lolote.<br />
• KuOGOPa KuFanYa MaKOSa. Unahofu sana kufanya makosa kiasi cha kutojaribu kufanya<br />
kitu chochote.<br />
• KuOGOPa MaFaniKiO. Hujaribu kwa sababu unahofu kuwa mafanikio yatakufanya kivutio.<br />
• laKini SiWeZi. Unajiambia mwenye kwamba huwezi kabla hata ya kujaribu.<br />
• KuOGOPa KutORiDhiSha MateGeMeO Ya Watu WenGine. Unahofu sana kuhusu<br />
kuwasikitisha watu wengine kiasi cha kuchelea kujaribu.<br />
Jihadhari na vikwazo hivi: Usiruhusu vikunase.<br />
Kamwe hutajua una uwezo wa kufanya jambo mpaka ufanye bidii ya kufanya jambo hilo.<br />
Usilizungumzie tu au kutarajia kwamba litatokea. Anza kuyafanyia kazi malengo yako.<br />
Mara nyingi tunafikiri kwamba watu tunaowasikia wamefanikiwa wamezaliwa na vipaji vyao<br />
pamoja na stadi kiasi kwamba ilikuwa rahisi kwao kufikia pale walipo. Hata hivyo, ukiangalia<br />
walichofanya watu hawa utashangaa kiasi cha juhudi zao binafsi walizoweka katika kufanikisha<br />
ndoto zao.<br />
Wakati mwingine, tunadhani kwamba watu waliofanikiwa wana bahati. Upo msemo usemao:<br />
“Bahati ipo pale maandalizi yanapokutana na nafasi”.<br />
Hakikisha kwamba unajiweka tayari kwa lolote wakati wote. Ipo siku bahati itakuangukia<br />
Kumbuka kuwa mafanikio si kuwa nyota wa uigizaji ama kuwa na gari la kifahari au kuwa na pesa<br />
nyingi. Mafanikio ni jambo la nafsi. “Mafanikio yana maana tofauti kwa watu tofauti. Hata hivyo,<br />
watu wengi wanatafsiri mafanikio kuwa ni kujihisi vizuri na kile unachokifanya.<br />
Mwenye kuamua kiwango cha mafanikio yako ni wewe mwenyewe. Usisubiri watu wengine<br />
wakutafutie mafanikio. Mafanikio yako yataamuliwa na furaha yako, utajiri wa kiroho, busara<br />
zako, uwezo wako wa kubadilika kutegemeana na hali, ubunifu wako, nia na mtazamo wako<br />
kwa watu wengine. Umeshika funguo za maisha yako ya baadaye na ndoto zako. Fanya<br />
linalowezekana leo, usingoje kesho.<br />
SURA YA 14 | KUTIMIZA NDOTO ZAKO<br />
Sura ya 14<br />
Kutimiza ndoto zako<br />
Kutimiza ndoto zako kunategemea kufanya kazi kwa bidii sana na kwa nia. Usisubiri<br />
mambo yakutokee. Haya ni maisha yako ya sasa na ya baadaye. Unahitaji kuyajenga kwa<br />
dhati.<br />
Watu wengine wanajua wanataka kuwa nani na wanataka kufanya nini. Wanajua ndoto zao.<br />
Wengine hawajui wanataka kuwa nani. Hii haina maana kuwa hawana ndoto. Ina maana<br />
bado hawajajijua ni akina nani. Unaweza kuanza kutambua ndoto zako leo.<br />
• angalia watu wanaokuzunguka katika jumuia yako. Nani unamhusudu na<br />
kumheshimu? Watu hawa wanaweza kuwa mfano mzuri kwako.<br />
• angalia nje ya jumuia yako. Wapo watu wanaofanya mambo yanayovutia na yenye<br />
thamani kwa maisha yao. Hawa wanaweza kuwa mifano mizuri kwako.<br />
• Ziache fikra zako za ubunifu zipae angani. Usijiwekee mipaka kuhusu nini unaweza<br />
kufanya na kipi huwezi. Kama ni mvulana au ni msichana unaweza kufanya karibu kila<br />
kitu unachotaka kufanya kama jambo ukiliweka akilini na kuongeza juhudi.<br />
Zungumza na watu wanaofanya mambo yanayokuvutia. Waulize walifikaje pale walipo?<br />
Walihitaji elimu gani? Mafunzo gani walipata. Wanapenda nini zaidi kuhusu kazi zao? Na ni<br />
kitu gani hawakipendi sana kuhusu kazi zao?<br />
<strong>Ndoto</strong> zako ni malengo yako ya muda mrefu – mambo ambayo unafikiria kuyakamilisha<br />
baada ya muda mrefu. Lakini unahitaji vilevile malengo mahususi— mambo ambayo<br />
unaweza kuyakamilisha katika muda mfupi. Fikiria unachotaka kufanikisha wiki hii,<br />
mwezi huu na mwaka huu. Ukifanikisha malengo haya utajisikia vizuri. Utaona kuwa<br />
unapokiweka akilini kitu unaweza kufanikisha.<br />
Kuzifikia ndoto zako si jambo rahisi na siyo jambo la moja kwa moja lililonyooka.<br />
Hatua sahihi za kuchukua hazitakuwa wazi na unaweza kujikuta unakutana na vipingamizi<br />
ambavyo hukuvitegemea. Utahitaji kuwa na uwezo wa:<br />
• Kufanya uamuzi mzuri kwa kuangalia matokeo ya uchaguzi uliopo mbele yako.<br />
• Kulenga ndoto zako na kutoruhusu kujikatisha tamaa au kupotezwa na watu wengine.<br />
• Kufanya kazi kwa bidii kama upo shuleni au haupo shuleni. Tumia nafasi uliyonayo<br />
vizuri.<br />
• Kumudu vikwazo (mambo yatakayokurudisha nyuma), na kutokata tamaa. Palipo na<br />
nia pana njia.<br />
Mafanikio yako yanaamuliwa na wewe mwenyewe. Nia yako, ubunifu, busara, uwezo<br />
wa kukubali mabadiliko, mtazamo kuhusu watu wengine ni ufunguo wa maisha yako ya<br />
baadaye na ndoto zako.<br />
185
186<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Faharasa<br />
amali [kutaamali] matendo, kazi, mazowea<br />
angavu -eupe, safi, -enye kuelimika, enye akili nzuri<br />
ari hali ya kuwa na moyo wa hima katika kukamilisha jambo,<br />
kutokubali kushindwa<br />
ashki tamaa ya kiume au kike, hamu, nyege, uchu<br />
asi kataa kutii amri, pinga kanuni au sheria<br />
baini [kubainisha] tambua au fahamu jambo lililokuwa limefumbwa<br />
bwete bure, rahisi<br />
changamoto kitu au jambo linalotia ari<br />
chunusi [Acne] ugonjwa wa uvimbe<br />
dinda kwa uume simama kwa uume, disa, inuka<br />
disisha/ dindisha [kusimamisha] simama kwa uume, inuka<br />
enzi [Kujienzi] onyesha heshima au mapenzi, penda<br />
fufu fuvu/bupuri, bakaa ya mifupa baada ya mwili kuoza<br />
ghali -enye bei kubwa, siyo rahisi<br />
giligili kioevu kizito kinachoteleza, ute au gole<br />
govi ngozi ambayo huziba dhakari kwa mbele kwa asiyetahiriwa<br />
187
188<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
haiba heba, uvutio wa heshima, mwenendo wa kupendeza, sura<br />
nzuri, urembo, uzuri<br />
harimu [ma] ndugu wasioweza kuingiliana kimwili kwa mfano mtu<br />
na dada yake<br />
hasi ondoa au haribu mapumbu ya mwanaume au mnyama dume<br />
kinyume cha kitu -(chanya)<br />
hadhari uangalifu<br />
hedhi damu inayomtoka mwanamke katika siku zake za mwezi<br />
hodhi jirundikia mali au bidhaa<br />
homoni kemikali zinazosisimua mwili<br />
ishi kwa matumaini kuishi kwa matumaini. Hali ya mwathirika kuendelea<br />
kuishi kwa kujipa moyo<br />
jinsi, jeni Kijinsi viini urithi ambavyo hurithisha tabia na maumbile ya<br />
kiumbe, -a kike au a-kiume<br />
Jinsia uhusiano kati ya wanawake na wanaume unaojumuisha<br />
mambo mengi, mfano mgawanyo wa kazi n.k.<br />
kalori [Calories] kipimo cha joto<br />
kandida [albicans] aina ya kuvu ambayo hupatikana mdomoni, ngozi, utumbo,<br />
ukeni<br />
kandidia [kandidiasisi] vijidudu/ vimelea vinavyosababisha ugonjwa wa kuvu<br />
kanuni desturi, sheria, amri, taratibu za lazima<br />
kemi muziki/ nyimbo zenye mahadhi ya rapu.<br />
kiambato kitu kinachoambatanakihoro huzuni kubwa kwa ajili ya<br />
kufiwa au jambo la msiba,<br />
kilele sehemu ya juu kabisa, kiwango cha juu cha mafanikio,<br />
kufikia kilele katika mapenzi (mshindo)<br />
kilenge, kijusi, [Fitasi] mimba changa ya wiki tano au zaidi<br />
fARASA<br />
kinembe kinyama kilichojitokeza kwenye tupu ya mbele ya<br />
mwanamke (kisimi)<br />
kipindi fiche kipindi ambacho mwenye virusi vya UKIMWI/ VVU<br />
hajaonyesha dalili za ugonjwa<br />
kiwango cha kujamiiana idadi ya matendo ya ngono mtu ayafanyayo kwa muda<br />
fulani<br />
kizinda kizuizi chembamba cha nyama au mwili<br />
kojoa toa mkojo, toa shahawa, katika ngono ni mshindo.<br />
kokwa [la Mayai] mbegu za uzazi za mwanaume<br />
konokono Mnyama anayeteleza na anayetambaa polepole<br />
kuvu fangasi, husababisha vimelea na vijidudu<br />
Kuzitambua ndoto zako Kuwa na mawazo halisi ya kufikirika kimaisha<br />
kweza [Kujiweka Juu] kujitukuza, kutaka watu wakuone,<br />
lateksi gundi<br />
limfu kioevu ambacho asilimia kubwa ni maji yenye virutubisho<br />
mbalimbali mwilini<br />
malai mafuta yanayotumika kupaka usoni<br />
manukato marashi ya majimaji ya urembo yanayonukia<br />
mavuzi nywele ziotazo manenani<br />
mfoko kutoka kwa kitu ghafla na kwa nguvu<br />
mfyato kushona uke na kuacha tundu dogo kwa ajili ya kutolea<br />
mkojo na hedhi<br />
miadi makubaliano ya kukutana, ahadi<br />
189
190<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
mkakamao msinyao/kushupaa kwa mwili, kujikaza kwa musuli wa<br />
mwili baada ya jambo fulani<br />
morali msisimko anaopata mtu<br />
mshindo Tendo la kumwaga shahawa kwa mwanaume<br />
msongo kuwa au kutingwa na mawazo mengi yasiyo na utatuzi wa<br />
papo hapo<br />
mustakabali uelekeo wa jambo baadaye<br />
nasaha mawaidha, mwongozo anaopewa mtu kuhusu jambo fulani<br />
nata shika na gandaganda kama vile gundi na ulimbo gandama<br />
ndoto nyevu kutoka shahawa (mbegu za uzazi) mvulana akiwa usingizini<br />
ngono tendo la kuingiliana kimwili kati ya mwanamke na<br />
mwanamume.<br />
nyonga umbo la mfupa lenye umbile la beseni lililopo katika kitako<br />
cha mgongo<br />
nyumbuka kuvutika kama mpira<br />
odorono mafuta ya manukato yapakwayo kwapani<br />
ovisha/ uovishaji kuachiwa kwa yai / kutoka kwa yai kutoka kwenye mfuko<br />
wa mayai kwa ajili ya kurutubishwa. Lisiporutubishwa huwa<br />
hedhi.<br />
pangusa ugonjwa uenezwao kwa njia ya ngono unaojitokeza kama<br />
kidonda sehemu za siri.<br />
“pap smea” kipimo cha saratani<br />
pumbaa [pumbazika] zubaa bila kusema neno, bumbuwazi<br />
punyeto kitendo cha kujichua na kufika kilele ili kukidhi haja ya<br />
mapenzi<br />
riwaya hadithi ndefu yenye visa zaidi ya kimoja.<br />
fARASA<br />
sebamu “Sebum” mnyeso wa mafuta kutoka kwenye tezi za kwenye ngozi<br />
shankaroidi[Chankroidi]pangusa ugonjwa wa zinaa unaoleta maumivu makali sehemu za siri,<br />
wakati mwingine kuvimba kwa tezi hadi kupasuka.<br />
sifa-bainifu maelezo ya pekee yanayotambulisha kitu kilivyo<br />
sirinji bomba la kupigia sindano<br />
smegma mnyeso wa mafuta kutoka kwenye tezi za kwenye ngozi<br />
kwenye paji la uso<br />
sodo [tampon] kifaa kinachotumiwa na wanawake kujihifadhi wakati wa<br />
hedhi (pedi)<br />
sponji sifongo<br />
stadi maarifa ya utendaji wa jambo fulani<br />
thamini familia heshima na kupenda familia<br />
ugumba hali ya kushindwa kuzaa - utasa<br />
uhanga [dalili za kujitoa] kufanya jambo kwa nia nzuri au mbaya kwa faida/ hasara ya<br />
wengine<br />
ujinsia hali ya kuwa na jinsia moja<br />
ungo hali ya uzima anayokuwa nayo msichana kabla hajaingiliwa<br />
na mwanaume<br />
unyong’onyevu hali ya kuchoka anayokuwa nayo mtu<br />
uovishaji utaratibu wa kujitoa kwa yai kutoka katika mirija ya uzazi<br />
ushirikiali hali ya kuhisi au kuelewa hisia za mtu mwingine<br />
utashi hali ya kutaka (matamanio)<br />
utoko uchafu wa ukeni<br />
uvumi jambo linalosemwa lisilo na ukweli<br />
via vya uzazi viungo vya uzazi<br />
191
192<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
virigua fanya ghasia, fujo, sumbua<br />
vunja ungo hatua inayoendana na mabadiliko ya kibiolojia kutoka<br />
utoto kwenda utu uzima (msichana)<br />
VVU virusi vya UKIMWI<br />
wajibu [Kuwajibika] jukumu, kazi, shughuli<br />
weka wasilisha kitu mahali, tua, peleka<br />
Marejeleo<br />
Am I ready to have sex? Planned Parenthood of New York City, Inc., New York. 1998.<br />
Je, niko tayari kufanya ngono?<br />
Birth Control Choices for Teens. Planned Parenthood Federation of America, New York, 1997.<br />
Njia za Kupanga Uzazi Kwa Vijana?<br />
Changing Bodies, Changing Lives, edited by Ruth Bell and the Teen Book Project, 3rd Edition,<br />
RandomHouse, 1998.<br />
Mabadiliko ya Miili, Mabadili ya <strong>Maisha</strong><br />
Choose a Future! Issues and Options for Adolescent Girls. Centre for Development and Population<br />
Activities (CEDPA), Washington, D.C., 1996.<br />
Chagua <strong>Maisha</strong> yako ya Usoni! Masuala na Maamuzi ya Wasichana balehe<br />
Contraceptive Technology. 17th ed., written by R.A. Hatcher et al. Ardent Media, Inc., New<br />
York,1998.<br />
Tekinolojia ya Uzuiaji Mimba<br />
The Education of Girls and Women in Africa, Forum for African Women Educationalists (FAWE),<br />
Nairobi, Kenya.<br />
Elimu ya Wasichana na Wanawake Afrika<br />
“Feeling Good about Growing Up.” Planned Parenthood Federation of America, New York, 1993.<br />
Kujisikia Vema Kuhusu Kuwa Mtu Mzima<br />
Filling the Gaps: Hard to Teach Topics in Sexuality Education. Sexuality Information and Education<br />
Council of the United States (SIECUS), New York, 1998.<br />
Kuyajaza Mapengo: Mada Nyeti kufundisha katika Elimu ya Kijinsia<br />
Guidelines for Comprehensive Sexuality Education. 2nd ed. Sexuality Information and Education<br />
Council of the United States (SIECUS), New York, 1996.<br />
Maelekezo ya Elimu Mwafaka ya Mambo ya Kijinsia<br />
Healthy Women, Healthy Mothers: An Information Guide, written by A.A. Arkutu. <strong>Family</strong> <strong>Care</strong><br />
<strong>International</strong>, New York, 1995.<br />
Wanawake wa Afya Bora, Akina Mama wa Afya Bora: Habari ya Maelekezo<br />
193
194<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
HIV Testing. Straight Talk, Vol. 7, No. 8, August 1998.<br />
Kupima Virusi vya Ukimwi<br />
Life Planning Education: A Youth Development Program. Advocates for Youth, Washington,<br />
D.C., 1995.<br />
Elimu ya Kupanga <strong>Maisha</strong>:Mradi wa Maendeleo wa Vijana<br />
Now What do I do? How to Give Your Pre-Teens Your Messages. Sexuality Information and EducationCouncil<br />
of the United States (SIECUS), New York, 1996.<br />
Sasa Nifanye Nini? Jinsi ya Kuwapa Habari Vijana Wako Ambao Hawajabalehe<br />
The Preteen’s First Book about Love, Sex and AIDS, written by Michelle Harrison, M.D., American<br />
Psychiatric Press, Inc., Washington, D.C., 1995.<br />
Kitabu cha Kwanza kwa Vijana ambao Hawajabalehe Kuhusu Mapenzi, Ngono and Ukimwi<br />
Red Card or Yellow—Are You Still in the Game? Being Young and Coping with Sexual and<br />
Reproductive Health in Tanzania. Swedish Association for Sex Education (RFSU), Stockholm,<br />
1995.<br />
Kadi Nyekundu au ya Kijani- Je Ungali Mchezoni? Kuwa Mchanga na kukabiliana na Afya ya<br />
Uzazi Tanzania<br />
Responsible Teenage Sexuality, Planned Parenthood of South Africa (PPASA), 1992.<br />
Afya Bora ya Kijinsia kwa Vijana balehe<br />
Sexually Transmitted Infections: The Facts. New York: Planned Parenthood Federation of<br />
America, 1997.<br />
Magonjwa ya Zinaa: Ukweli wa Mambo<br />
Stay off drugs and Alcohol. Straight Talk, Vol. 7, No. 9, September, 1999.<br />
Usiyakaribie Madawa ya Kulevya na Pombe<br />
Sugar Daddies and Sugar Mummies. Straight Talk, Vol. 7, No. 10, October 1999.<br />
Baba na Mama Sukari<br />
Talking with our Children about Sex and Growing up, Unicef and Government of Uganda, Kampala,<br />
Uganda.<br />
Kuzungumza na Watoto Wetu Kuhusu Ngono na Utu Uzima<br />
What’s Happening to My Body? A Book for Boys, written by Lynda Madaras. Newmarket Press,<br />
New York,1988.<br />
Ni Nini Kinachofanyika katika Mwili Wangu, Kitabu cha Wavulana<br />
What’s Happening to My Body? A Book for Girls, written by Lynda Madaras. Newmarket Press,<br />
New York,1988.<br />
Ni Nini Kinachofanyika katika Mwili Wangu, Kitabu cha Wasichana<br />
Where Women Have No Doctor: A Health Guide for Women, written by A.A. Burns et al. The<br />
Hesperian Foundation, Berkeley, 1997.<br />
Mahali Wanawake Hawana Daktari, Maelekezo ya Afya kwa Wanawake.