08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

22<br />

KuDinDa KWa uuMe<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

iwapo hujatahiriwa rudisha nyuma govi na safisha taratibu chini yake.<br />

Kwa kawaida uume ni laini na huninginia chini. Wakati unadinda, damu nyingi huelekea kwenye<br />

uume isivyo kawaida na damu kidogo hurudi. Hii husababisha uume kuwa mkubwa na mgumu,<br />

na kusimama. Uume uliodinda kwa kawaida hujikunja kidogo kuelekea juu, na unaweza kujikunjia<br />

upande mmoja.<br />

Uume unapokuwa umedinda unaweza ukashindwa kukojoa kiurahisi kwa sababu msuli hufunga<br />

kibofu cha mkojo. Itakubidi usubiri uume ulegee ndipo ukojoe.<br />

Uume unaweza kudinda iwapo utaguswa au kushikwa shikwa, au wakati umepata mhemuko wa<br />

kutaka kujamiiana au kwa kumuona mtu anayekuvutia. Uume unaweza kudinda kwa sababu ya<br />

kuwa na wasiwasi na mfadhaiko. Ni kawaida kwa wavulana kuamka asubuhi na uume uliodinda.<br />

Ukiwa usingizini uume unaweza kudinda mara 5 mpaka 7. Hii ni kawaida kabisa na haina madhara<br />

yoyote.<br />

Kudinda kwa Uume kunawatokea wanaume wote wa umri mbalimbali ikiwa ni pamoja na watoto<br />

wadogo na wazee. Wakati mwingine wavulana huhofu wanapodindisha mara kwa mara. Hali hii<br />

inawasumbua wakiwa darasani, ndani ya basi au hata wakati wa matembezi. Wakati mwingine<br />

zipo sababu za msingi za uume kudinda, kwa mfano, unaweza ukawa umekaa karibu na mtu<br />

anayekuvutia. Hata hivyo, kuna wakati uume unadinda bila sababu yoyote ya msingi.<br />

nfune kutoka Zambia (umri wa miaka 13)<br />

“Kudindisha kwa uume hakuzuiliki na hutokea mara kwa mara.<br />

Wakati mwingine ni dalili ya kuonyesha una msisimko wa<br />

kutaka kujamiiana. Hali hii naichukia sana hasa ninapokuwa<br />

shuleni au hadharani.”<br />

Tafadhali usiwe na wasiwasi, wewe ni wa kawaida, mwenye afya na homoni nyingi. Unaweza<br />

kufedheheka ikitokea darasani au hadharani, lakini wakati wote ni wewe peke yako unayefahamu<br />

kwamba umedindisha.<br />

Wakati mwingine wavulana wanadhani njia pekee ya kuthibiti uume kudinda ni kufanya ngono<br />

Hii sio kweli ni uzushi ikiwa ni sababu ya wavulana kufanya ngono. Uume kudinda sio dalili ya<br />

kwamba unahitaji kufanya ngono, la hasha.<br />

KuMWaGa Manii “KuKOjOa”<br />

SURA YA 3 | WAvULANA<br />

Unapofikia balehe unaweza kuanza kuona majimaji yenye rangi ya maziwa ambayo yananata na ni<br />

mazito, sio mepesi kama mkojo.<br />

Majimaji kama ute hutoka kupitia kwenye uume wakati mwanaume anapofikia mshindo. Kukojoa<br />

manii ni kilele cha msisimko wa kijinsia, wakati mwanaume anapokuwa amedindisha uume.<br />

Kumbuka ya kwamba sio lazima kukojoa manii kila uume unapokuwa umedinda. Kama utasubiri,<br />

uume utalegea wenyewe bila hata ya kukusababishia madhara yoyote.<br />

Majimaji kama ute yametengenezwa na vitu viwili. Karibia 10% ya majimaji ni mamilioni ya<br />

mbegu za kiume. Mbegu za kiume ni ndogo sana kiasi ambacho hatuwezi kuziona kwa macho<br />

labda kwa darubini. Ukiziona zinaonekana kuwa na kichwa cha mviringo na mkia mrefu na<br />

mwembamba.<br />

Asilimia 90 ya ute huo ni majimaji yenye rangi ya maziwa yanayoitwa shahawa. Shahawa<br />

huwezesha mbegu za kiume kuogelea na pia huzipa chakula na kuziwezesha kuwa hai. Shahawa<br />

sio chakula kwa wasichana, kama watu wengine wanavyozusha.<br />

Mbegu za kiume zinatengenezwa katika Korodani/Makende (angalia kielelezo uk 19). Shahawa,<br />

ambazo ni majimaji yenye rangi nyeupe/maziwa zinatengenezwa kwenye vifuko vya shahawa.<br />

Hizi ni tezi zilizopo nyuma ya kibofu cha mkojo. Mwanaume anapofikia mshindo mbegu za kiume<br />

zinachanganyika na shahawa kutoka kifuko cha shahawa. Mchanganyiko huu huitwa manii. Manii<br />

hupitia kwenye mirija ya kupitishia mbegu na kutoka nje ya uume kupitia kwenye tundu dogo<br />

lililopo kwenye kichwa cha uume.<br />

Inaweza kuonekana kana kwamba manii nyingi hutoka wakati mwanaume “anapokojoa” Ukweli<br />

ni kwamba kiasi kinachotoka ni kama kijiko kidogo cha chai kilichojaa. Usije ukadharau uwezo<br />

wa hiki kijiko kidogo cha chai kilichojaa manii;<br />

kinaweza kuwa na mbegu za kiume karibia<br />

milioni mia tano!. Kila mojawapo ya mbegu<br />

hizo inaweza kumfanya msichana apate mimba.<br />

Unapofikiria mbegu za kiume zipatazo milioni<br />

mia tano, utaelewa ni kwa namna gani msichana<br />

anavyoweza kupata mimba kirahisi.<br />

Iwapo mvulana au mwanaume ana maambukizi<br />

ya VVU, kijiko cha chai kimoja kilichojaa<br />

shahawa kinaweza kuwa na mamia kwa maelfu<br />

ya virusi vinavyosababisha UKIMWI.<br />

Mbegu ya kiume<br />

Kijiko kidogo cha chai kilichoja shahawa kina<br />

mamilioni ya mbegu za kiume na kinaweza kuwa na<br />

VVu iwapo mvulana atakuwa ana maambujizi.<br />

23

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!