Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
22<br />
KuDinDa KWa uuMe<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
iwapo hujatahiriwa rudisha nyuma govi na safisha taratibu chini yake.<br />
Kwa kawaida uume ni laini na huninginia chini. Wakati unadinda, damu nyingi huelekea kwenye<br />
uume isivyo kawaida na damu kidogo hurudi. Hii husababisha uume kuwa mkubwa na mgumu,<br />
na kusimama. Uume uliodinda kwa kawaida hujikunja kidogo kuelekea juu, na unaweza kujikunjia<br />
upande mmoja.<br />
Uume unapokuwa umedinda unaweza ukashindwa kukojoa kiurahisi kwa sababu msuli hufunga<br />
kibofu cha mkojo. Itakubidi usubiri uume ulegee ndipo ukojoe.<br />
Uume unaweza kudinda iwapo utaguswa au kushikwa shikwa, au wakati umepata mhemuko wa<br />
kutaka kujamiiana au kwa kumuona mtu anayekuvutia. Uume unaweza kudinda kwa sababu ya<br />
kuwa na wasiwasi na mfadhaiko. Ni kawaida kwa wavulana kuamka asubuhi na uume uliodinda.<br />
Ukiwa usingizini uume unaweza kudinda mara 5 mpaka 7. Hii ni kawaida kabisa na haina madhara<br />
yoyote.<br />
Kudinda kwa Uume kunawatokea wanaume wote wa umri mbalimbali ikiwa ni pamoja na watoto<br />
wadogo na wazee. Wakati mwingine wavulana huhofu wanapodindisha mara kwa mara. Hali hii<br />
inawasumbua wakiwa darasani, ndani ya basi au hata wakati wa matembezi. Wakati mwingine<br />
zipo sababu za msingi za uume kudinda, kwa mfano, unaweza ukawa umekaa karibu na mtu<br />
anayekuvutia. Hata hivyo, kuna wakati uume unadinda bila sababu yoyote ya msingi.<br />
nfune kutoka Zambia (umri wa miaka 13)<br />
“Kudindisha kwa uume hakuzuiliki na hutokea mara kwa mara.<br />
Wakati mwingine ni dalili ya kuonyesha una msisimko wa<br />
kutaka kujamiiana. Hali hii naichukia sana hasa ninapokuwa<br />
shuleni au hadharani.”<br />
Tafadhali usiwe na wasiwasi, wewe ni wa kawaida, mwenye afya na homoni nyingi. Unaweza<br />
kufedheheka ikitokea darasani au hadharani, lakini wakati wote ni wewe peke yako unayefahamu<br />
kwamba umedindisha.<br />
Wakati mwingine wavulana wanadhani njia pekee ya kuthibiti uume kudinda ni kufanya ngono<br />
Hii sio kweli ni uzushi ikiwa ni sababu ya wavulana kufanya ngono. Uume kudinda sio dalili ya<br />
kwamba unahitaji kufanya ngono, la hasha.<br />
KuMWaGa Manii “KuKOjOa”<br />
SURA YA 3 | WAvULANA<br />
Unapofikia balehe unaweza kuanza kuona majimaji yenye rangi ya maziwa ambayo yananata na ni<br />
mazito, sio mepesi kama mkojo.<br />
Majimaji kama ute hutoka kupitia kwenye uume wakati mwanaume anapofikia mshindo. Kukojoa<br />
manii ni kilele cha msisimko wa kijinsia, wakati mwanaume anapokuwa amedindisha uume.<br />
Kumbuka ya kwamba sio lazima kukojoa manii kila uume unapokuwa umedinda. Kama utasubiri,<br />
uume utalegea wenyewe bila hata ya kukusababishia madhara yoyote.<br />
Majimaji kama ute yametengenezwa na vitu viwili. Karibia 10% ya majimaji ni mamilioni ya<br />
mbegu za kiume. Mbegu za kiume ni ndogo sana kiasi ambacho hatuwezi kuziona kwa macho<br />
labda kwa darubini. Ukiziona zinaonekana kuwa na kichwa cha mviringo na mkia mrefu na<br />
mwembamba.<br />
Asilimia 90 ya ute huo ni majimaji yenye rangi ya maziwa yanayoitwa shahawa. Shahawa<br />
huwezesha mbegu za kiume kuogelea na pia huzipa chakula na kuziwezesha kuwa hai. Shahawa<br />
sio chakula kwa wasichana, kama watu wengine wanavyozusha.<br />
Mbegu za kiume zinatengenezwa katika Korodani/Makende (angalia kielelezo uk 19). Shahawa,<br />
ambazo ni majimaji yenye rangi nyeupe/maziwa zinatengenezwa kwenye vifuko vya shahawa.<br />
Hizi ni tezi zilizopo nyuma ya kibofu cha mkojo. Mwanaume anapofikia mshindo mbegu za kiume<br />
zinachanganyika na shahawa kutoka kifuko cha shahawa. Mchanganyiko huu huitwa manii. Manii<br />
hupitia kwenye mirija ya kupitishia mbegu na kutoka nje ya uume kupitia kwenye tundu dogo<br />
lililopo kwenye kichwa cha uume.<br />
Inaweza kuonekana kana kwamba manii nyingi hutoka wakati mwanaume “anapokojoa” Ukweli<br />
ni kwamba kiasi kinachotoka ni kama kijiko kidogo cha chai kilichojaa. Usije ukadharau uwezo<br />
wa hiki kijiko kidogo cha chai kilichojaa manii;<br />
kinaweza kuwa na mbegu za kiume karibia<br />
milioni mia tano!. Kila mojawapo ya mbegu<br />
hizo inaweza kumfanya msichana apate mimba.<br />
Unapofikiria mbegu za kiume zipatazo milioni<br />
mia tano, utaelewa ni kwa namna gani msichana<br />
anavyoweza kupata mimba kirahisi.<br />
Iwapo mvulana au mwanaume ana maambukizi<br />
ya VVU, kijiko cha chai kimoja kilichojaa<br />
shahawa kinaweza kuwa na mamia kwa maelfu<br />
ya virusi vinavyosababisha UKIMWI.<br />
Mbegu ya kiume<br />
Kijiko kidogo cha chai kilichoja shahawa kina<br />
mamilioni ya mbegu za kiume na kinaweza kuwa na<br />
VVu iwapo mvulana atakuwa ana maambujizi.<br />
23