08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

24<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Wavulana wengi wanakuwa na wasiwasi kwamba kondomu haiwezi kuhifadhi mbegu za kiume<br />

zipatazo milioni 500. Lakini mbegu za kiume ni ndogo sana na kwa hiyo kondomu inaweza<br />

kuzizuia zote ili mradi inavaliwa kwa usahihi (angalia sura ya 10 kwa maelezo zaidi kuhusu<br />

kondomu).<br />

Wavulana wengine wanakuwa na wasiwasi kwamba wakikojoa manii mara kwa mara<br />

watapunguza kiasi cha shahawa mwilini mwao. Wasiwasi wa kwamba wanaweza kuishiwa<br />

shahawa na hivyo kutokuwanazo za kutosha watakapozihitaji. Hili haliwezi kutokea hata mara<br />

moja kwani mwanaume anatengeneza mbegu za kiume na shahawa tangia kipindi cha balehe<br />

mpaka siku anayokufa.<br />

Vilevile kumbuka ya kwamba haiwezekani mbegu za kiume na shahawa zikalundikana au<br />

zikajenga shinikizo mwilini. Mwili wako ni kama mashine iliyokamilika, unazo njia za kuondoa<br />

mbegu za kiume na shahawa inayozidi, mojawapo ni ndoto nyevu.<br />

nDOtO nYeVu (“KuKOjOlea” KitanDani)<br />

Wakati mwingine wavulana wanakojoa manii<br />

kitandani wakiwa usingizini.Kitendo hiki kinaitwa<br />

“ndoto nyevu” wavulana wengi wanapopata ndoto<br />

nyevu huwa inakuwa ni mara yao ya kwanza shahawa<br />

kutoka mwilini mwao. Wanaweza kuamka na kukuta<br />

doa bichi kitandani au kwenye nguo.<br />

Kama hufahamu lolote kuhusu ndoto nyevu unaweza<br />

kuchanganyikiwa na kuwa na wasiwasi. Unaweza<br />

kufikiri umekojoa kitandani au damu inakutoka au<br />

unaumwa, lakini utaona kwamba majimaji yana rangi<br />

ya maziwa/meupe, na sio kama damu au mkojo.<br />

ndoto nyevu kwa mara ya Kwanza<br />

<strong>Ndoto</strong> nyevu hutokea usingizini tu. Ukisinzia kidogo mchana unaweza kupata ndoto nyevu, lakini<br />

wavulana wengi hupata ndoto nyevu usiku wakiwa usingizini. Wavulana wengi wanapojikuta<br />

wamekojoa manii huwa wanakumbuka kwamba walikuwa wanaota ndoto zinazohusiana na<br />

mapenzi. Lakini unaweza kupata ndoto nyevu hata kama hujaota ndoto za mapenzi.<br />

Karibu wavulana wengi wanafedheheka wakipata ndoto nyevu. Ni sahihi kufedheheka, lakini<br />

kumbuka ya kwamba ndoto nyevu ni za kawaida wakati wa ujana balehe. Vijana balehe wengi<br />

wanapata ndoto nyevu ingawa sio wote.<br />

Mvulana hawezi kujizuia kupata ndoto nyevu; ni za asili na ni za kawaida. Ni njia ambayo mwili<br />

unatoa nafasi kwa ajili ya mbegu za kiume mpya kutoka kwenye korodani. Kupata ndoto nyevu<br />

haimaanishi uanze kujamiiana.<br />

SURA YA 3 | WAvULANA<br />

adamu, kutoka uganda (umri, miaka 13)<br />

“Sidhani kupata ndoto nyevu kunamaanisha ninatakiwa kujamiiana. Ni<br />

kukua tu. Ninaona aibu tu kwa vile inabidi nibadilishe mashuka kila baada<br />

ya siku moja.”<br />

Wavulana wengine wanapoanza kupata ndoto nyevu wanaona ni tukio kubwa sana ambalo<br />

wanalifurahia.<br />

Panaito kutoka Kenya<br />

“Nilipopata ndoto nyevu kwa mara ya kwanza nilijisikia kama nimekomaa<br />

kijinsi. Nilifurahi kuwa mmojawapo wa wale ambao tayari walishapata.<br />

Lakini ningelikuwa sijapata taarifa, ningeweza hata kwenda kumuona<br />

daktari,ninamshukuru Mungu kwamba nilijua kilichokuwa kinatokea”.<br />

adamu kutoka uganda (umri, miaka 13)<br />

“Nilipopata ndoto nyevu kwa mara ya kwanza nilimwambia kaka yangu mkubwa<br />

ambaye alinihakikishia kwamba ilikuwa ni sehemu ya ukuaji.”<br />

Wavulana wengine hawawi na furaha sana wanapoanza kupata ndoto nyevu. Hili ni jambo la<br />

kawaida vilevile.<br />

nfune kutoka Zambia (umri wa miaka 13.”<br />

“Ninaona kama zinanichukiza”<br />

Wavulana wengine wanao marafiki wasio na huruma, ambao huwatania kuhusu kupata ndoto<br />

nyevu. Ni makosa kumtania au kumcheka mtu kwa vile amepata ndoto nyevu. <strong>Ndoto</strong> nyevu ni<br />

jambo la kawaida.<br />

bernard kutoka Kenya (umri wa miaka 17)<br />

“Nilipokuwa darasa la 8, sikutegemea kama ningeanza kukojoa manii<br />

mapema kiasi hicho. Nilimwambia rafiki yangu siri, badala ya kunieleza kwa<br />

nini yametokea, alinicheka. Nilijisikia kufedheheka. Sikutaka mtu yoyote<br />

afahamu, lakini aliwaeleza watu wengine, na wengine wakasema nilikuwa ninapiga<br />

punyeto. Nilimfuata rafiki yangu mwingine ambaye alikuwa mkubwa<br />

kwangu ambaye alinieleza kwamba ndoto nyevu ni kawaida.”<br />

Unatakiwa usiwe na wasiwasi kuhusu ndoto nyevu kwa vile ni jambo la kawaida halina kasoro.<br />

Unavyoendelea kuujua mwili wako ndivyo utakavyokuwa na raha na mabadiliko unavyokuwa<br />

unayapitia. Kwa kuongezea, ukiwa na taarifa iliyokamilika utaweza kuwasaidia wavulana wadogo<br />

kuelewa kitu gani kinawatokea wanapopitia ujana balehe.<br />

Yapo maelezo na mafunzo mengi mazuri ndani ya kitabu hiki,kwa hiyo usiachie kukisoma kitabu<br />

hiki kwa undani.<br />

25

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!