Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
24<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Wavulana wengi wanakuwa na wasiwasi kwamba kondomu haiwezi kuhifadhi mbegu za kiume<br />
zipatazo milioni 500. Lakini mbegu za kiume ni ndogo sana na kwa hiyo kondomu inaweza<br />
kuzizuia zote ili mradi inavaliwa kwa usahihi (angalia sura ya 10 kwa maelezo zaidi kuhusu<br />
kondomu).<br />
Wavulana wengine wanakuwa na wasiwasi kwamba wakikojoa manii mara kwa mara<br />
watapunguza kiasi cha shahawa mwilini mwao. Wasiwasi wa kwamba wanaweza kuishiwa<br />
shahawa na hivyo kutokuwanazo za kutosha watakapozihitaji. Hili haliwezi kutokea hata mara<br />
moja kwani mwanaume anatengeneza mbegu za kiume na shahawa tangia kipindi cha balehe<br />
mpaka siku anayokufa.<br />
Vilevile kumbuka ya kwamba haiwezekani mbegu za kiume na shahawa zikalundikana au<br />
zikajenga shinikizo mwilini. Mwili wako ni kama mashine iliyokamilika, unazo njia za kuondoa<br />
mbegu za kiume na shahawa inayozidi, mojawapo ni ndoto nyevu.<br />
nDOtO nYeVu (“KuKOjOlea” KitanDani)<br />
Wakati mwingine wavulana wanakojoa manii<br />
kitandani wakiwa usingizini.Kitendo hiki kinaitwa<br />
“ndoto nyevu” wavulana wengi wanapopata ndoto<br />
nyevu huwa inakuwa ni mara yao ya kwanza shahawa<br />
kutoka mwilini mwao. Wanaweza kuamka na kukuta<br />
doa bichi kitandani au kwenye nguo.<br />
Kama hufahamu lolote kuhusu ndoto nyevu unaweza<br />
kuchanganyikiwa na kuwa na wasiwasi. Unaweza<br />
kufikiri umekojoa kitandani au damu inakutoka au<br />
unaumwa, lakini utaona kwamba majimaji yana rangi<br />
ya maziwa/meupe, na sio kama damu au mkojo.<br />
ndoto nyevu kwa mara ya Kwanza<br />
<strong>Ndoto</strong> nyevu hutokea usingizini tu. Ukisinzia kidogo mchana unaweza kupata ndoto nyevu, lakini<br />
wavulana wengi hupata ndoto nyevu usiku wakiwa usingizini. Wavulana wengi wanapojikuta<br />
wamekojoa manii huwa wanakumbuka kwamba walikuwa wanaota ndoto zinazohusiana na<br />
mapenzi. Lakini unaweza kupata ndoto nyevu hata kama hujaota ndoto za mapenzi.<br />
Karibu wavulana wengi wanafedheheka wakipata ndoto nyevu. Ni sahihi kufedheheka, lakini<br />
kumbuka ya kwamba ndoto nyevu ni za kawaida wakati wa ujana balehe. Vijana balehe wengi<br />
wanapata ndoto nyevu ingawa sio wote.<br />
Mvulana hawezi kujizuia kupata ndoto nyevu; ni za asili na ni za kawaida. Ni njia ambayo mwili<br />
unatoa nafasi kwa ajili ya mbegu za kiume mpya kutoka kwenye korodani. Kupata ndoto nyevu<br />
haimaanishi uanze kujamiiana.<br />
SURA YA 3 | WAvULANA<br />
adamu, kutoka uganda (umri, miaka 13)<br />
“Sidhani kupata ndoto nyevu kunamaanisha ninatakiwa kujamiiana. Ni<br />
kukua tu. Ninaona aibu tu kwa vile inabidi nibadilishe mashuka kila baada<br />
ya siku moja.”<br />
Wavulana wengine wanapoanza kupata ndoto nyevu wanaona ni tukio kubwa sana ambalo<br />
wanalifurahia.<br />
Panaito kutoka Kenya<br />
“Nilipopata ndoto nyevu kwa mara ya kwanza nilijisikia kama nimekomaa<br />
kijinsi. Nilifurahi kuwa mmojawapo wa wale ambao tayari walishapata.<br />
Lakini ningelikuwa sijapata taarifa, ningeweza hata kwenda kumuona<br />
daktari,ninamshukuru Mungu kwamba nilijua kilichokuwa kinatokea”.<br />
adamu kutoka uganda (umri, miaka 13)<br />
“Nilipopata ndoto nyevu kwa mara ya kwanza nilimwambia kaka yangu mkubwa<br />
ambaye alinihakikishia kwamba ilikuwa ni sehemu ya ukuaji.”<br />
Wavulana wengine hawawi na furaha sana wanapoanza kupata ndoto nyevu. Hili ni jambo la<br />
kawaida vilevile.<br />
nfune kutoka Zambia (umri wa miaka 13.”<br />
“Ninaona kama zinanichukiza”<br />
Wavulana wengine wanao marafiki wasio na huruma, ambao huwatania kuhusu kupata ndoto<br />
nyevu. Ni makosa kumtania au kumcheka mtu kwa vile amepata ndoto nyevu. <strong>Ndoto</strong> nyevu ni<br />
jambo la kawaida.<br />
bernard kutoka Kenya (umri wa miaka 17)<br />
“Nilipokuwa darasa la 8, sikutegemea kama ningeanza kukojoa manii<br />
mapema kiasi hicho. Nilimwambia rafiki yangu siri, badala ya kunieleza kwa<br />
nini yametokea, alinicheka. Nilijisikia kufedheheka. Sikutaka mtu yoyote<br />
afahamu, lakini aliwaeleza watu wengine, na wengine wakasema nilikuwa ninapiga<br />
punyeto. Nilimfuata rafiki yangu mwingine ambaye alikuwa mkubwa<br />
kwangu ambaye alinieleza kwamba ndoto nyevu ni kawaida.”<br />
Unatakiwa usiwe na wasiwasi kuhusu ndoto nyevu kwa vile ni jambo la kawaida halina kasoro.<br />
Unavyoendelea kuujua mwili wako ndivyo utakavyokuwa na raha na mabadiliko unavyokuwa<br />
unayapitia. Kwa kuongezea, ukiwa na taarifa iliyokamilika utaweza kuwasaidia wavulana wadogo<br />
kuelewa kitu gani kinawatokea wanapopitia ujana balehe.<br />
Yapo maelezo na mafunzo mengi mazuri ndani ya kitabu hiki,kwa hiyo usiachie kukisoma kitabu<br />
hiki kwa undani.<br />
25