08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

16<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Sura ya 2<br />

MabaDiliKO KatiKa MWili WaKO<br />

Ujana, ambao kawaida huanzia umri kati ya miaka 10 na 16 ni mabadiliko ya hatua kutoka<br />

utoto kuingia utu uzima. Kila mtu anaanza kubadilika wakati wake. Wakati watu wengine<br />

hukua haraka zaidi, wengine hukua taratibu. Tunatofautiana, na hakuna unaloweza kufanya<br />

kuthibiti muda wa mabadiliko hayo.<br />

Ni yapi uyategemee unapobadilika kutoka msichana na kuwa mwanamke au kutoka<br />

mvulana na kuwa mwanaume?<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

Mfoko wa ukuaji; viganja, nyayo, miguu, mikono, nyonga kifua vyote vitaongezeka<br />

ukubwa mwili utatengeneza homoni, kemikali maalumu ambazo hutoa ujumbe namna<br />

mwili utakavyokua na kubadilika.<br />

Via vya uzazi (au sehemu za siri) vitakuwa vikubwa na vitaanza kutengeneza majimaji<br />

(giligili).<br />

Ngozi inaweza kuwa na mafuta zaidi.<br />

Utaanza kuota mavuzi na nywele kidogo kwapani, miguuni, mikononi na kama ni<br />

mvulana, usoni pia.<br />

Utaanza kupata hisia nzito mbali mbali.<br />

Uwezo wa kufikiri utaongezeka.<br />

Bila ya kujali mabadiliko yanatokea haraka au taratibu, wakati gani yanaanza, jaribu<br />

kukumbuka kwamba mabadiliko haya ni ya kawaida na hayana kasoro yoyote.<br />

Inaweza kuchukua muda mrefu kuyazoea mabadiliko haya kwa hiyo kuwa mvumilivu na<br />

usihofu.<br />

Wavulana<br />

Katika sura ya pili umesoma baadhi ya mabadiliko kadhaa ambayo wavulana wanayapata katika<br />

kipindi cha balehe. Sura hii itakupa maelezo zaidi kuhusu mabadiliko haya.<br />

uMbO na uKubWa Wa MWili<br />

Mfoko wa ukuaji kwa wavulana wengi unaanza kati ya miaka 12 na 13. Hata hivyo wavulana<br />

wengine wanaanza ukuaji mapema zaidi na wengine wanachelewa. Wakati wa mfoko wa ukuaji,<br />

mwili wako utaanza kuwa mrefu zaidi na mkubwa.<br />

Sehemu mojawapo ya mwili wako itakayoanza kukua ni miguu. Ukweli ni kwamba, mifupa ya<br />

miguu inakua haraka zaidi kuliko sehemu zingine za mwili. Hivyo basi miguu inaweza kukua hadi<br />

mwisho kabla ya sehemu zingine kukua sana. Iwapo utajisikia kama vile unakuwa mzito ghafla,<br />

inawezekana ni kwa sababu ya miguu yako imekuwa mikubwa kuliko ilivyokuwa muda mfupi<br />

uliopita. Unatakiwa kuwa mvumilivu kwani hali hii inaweza kukuchukua muda kabla hujaizoea<br />

Mifupa mingine ya mwili nayo itakuwa zaidi kuliko mingine na kusababisha umbo la mwili<br />

kubadilika. Kwa mfano, mabega yatakua zaidi wakati nyonga inaweza kukua kidogo tu. Nyonga<br />

yako inaweza kuonekana nyembamba ukilinganisha na upana wa mabega. Inawezekana miguu na<br />

mikono ikakua zaidi kuliko uti wa mgongo, hivyo basi miguu inaweza kuwa mirefu ukilinganisha<br />

na kifua au kiwiliwili. Matokeo yake umbo lako litakuwa tofauti sana na lile la mvulana mdogo.<br />

Misuli vile vile inakuwa, hasa ile ya miguuni na mikononi. Kadri misuli inavyokua, ndivyo<br />

unavyokuwa na nguvu zaidi. Mlundikano wa misuli na mafuta utasababisha kifua kuwa kikubwa.<br />

Vile vile wavulana wengi hugundua kwamba kuna mabadiliko ya chuchu na matiti katika kipindi<br />

cha balehe. Chuchu huongezeka na kuwa kubwa kidogo. Miduara inayozinguka chuchu nayo huwa<br />

mikubwa na rangi yake kuwa nyeusi kidogo.<br />

Wavulana wengine wanajikuta matiti yao yamevimba na yanauma. Kwa wachache, uvimbe<br />

huzidi, hivyo kuwasababishia wasiwasi kuwa wataota matiti makubwa kama wanawake. Usiwe<br />

na wasiwasi, haya ni mambo ya kawaida uvimbe na ulaini unasababishwa na homoni ndani ya<br />

mwili. Uvimbe unaweza ukadumu mwaka mmoja au mwaka mmoja na nusu, lakini baada ya hapo<br />

hupungua kwa vile mwili unaacha kutengeneza homoni nyingi.<br />

Wakati wa mabadiliko yote haya unatakiwa kuwa mvumilivu kwani mwili wako hauna matatizo<br />

yoyote, na wewe ni wa kawaida kabisa. Hata kama hukui haraka ukilinganisha na rafiki zako<br />

wanavyokua, usiwe na wasiwasi utakua tu, muda bado. Ni wakati gani unaanza kukua na kiasi<br />

gani utakua,inategemea sifa bainifu unazorithi kutoka kwa wazazi wako. Hata ukichelewa<br />

17<br />

SURA YA 3

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!