Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
16<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Sura ya 2<br />
MabaDiliKO KatiKa MWili WaKO<br />
Ujana, ambao kawaida huanzia umri kati ya miaka 10 na 16 ni mabadiliko ya hatua kutoka<br />
utoto kuingia utu uzima. Kila mtu anaanza kubadilika wakati wake. Wakati watu wengine<br />
hukua haraka zaidi, wengine hukua taratibu. Tunatofautiana, na hakuna unaloweza kufanya<br />
kuthibiti muda wa mabadiliko hayo.<br />
Ni yapi uyategemee unapobadilika kutoka msichana na kuwa mwanamke au kutoka<br />
mvulana na kuwa mwanaume?<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Mfoko wa ukuaji; viganja, nyayo, miguu, mikono, nyonga kifua vyote vitaongezeka<br />
ukubwa mwili utatengeneza homoni, kemikali maalumu ambazo hutoa ujumbe namna<br />
mwili utakavyokua na kubadilika.<br />
Via vya uzazi (au sehemu za siri) vitakuwa vikubwa na vitaanza kutengeneza majimaji<br />
(giligili).<br />
Ngozi inaweza kuwa na mafuta zaidi.<br />
Utaanza kuota mavuzi na nywele kidogo kwapani, miguuni, mikononi na kama ni<br />
mvulana, usoni pia.<br />
Utaanza kupata hisia nzito mbali mbali.<br />
Uwezo wa kufikiri utaongezeka.<br />
Bila ya kujali mabadiliko yanatokea haraka au taratibu, wakati gani yanaanza, jaribu<br />
kukumbuka kwamba mabadiliko haya ni ya kawaida na hayana kasoro yoyote.<br />
Inaweza kuchukua muda mrefu kuyazoea mabadiliko haya kwa hiyo kuwa mvumilivu na<br />
usihofu.<br />
Wavulana<br />
Katika sura ya pili umesoma baadhi ya mabadiliko kadhaa ambayo wavulana wanayapata katika<br />
kipindi cha balehe. Sura hii itakupa maelezo zaidi kuhusu mabadiliko haya.<br />
uMbO na uKubWa Wa MWili<br />
Mfoko wa ukuaji kwa wavulana wengi unaanza kati ya miaka 12 na 13. Hata hivyo wavulana<br />
wengine wanaanza ukuaji mapema zaidi na wengine wanachelewa. Wakati wa mfoko wa ukuaji,<br />
mwili wako utaanza kuwa mrefu zaidi na mkubwa.<br />
Sehemu mojawapo ya mwili wako itakayoanza kukua ni miguu. Ukweli ni kwamba, mifupa ya<br />
miguu inakua haraka zaidi kuliko sehemu zingine za mwili. Hivyo basi miguu inaweza kukua hadi<br />
mwisho kabla ya sehemu zingine kukua sana. Iwapo utajisikia kama vile unakuwa mzito ghafla,<br />
inawezekana ni kwa sababu ya miguu yako imekuwa mikubwa kuliko ilivyokuwa muda mfupi<br />
uliopita. Unatakiwa kuwa mvumilivu kwani hali hii inaweza kukuchukua muda kabla hujaizoea<br />
Mifupa mingine ya mwili nayo itakuwa zaidi kuliko mingine na kusababisha umbo la mwili<br />
kubadilika. Kwa mfano, mabega yatakua zaidi wakati nyonga inaweza kukua kidogo tu. Nyonga<br />
yako inaweza kuonekana nyembamba ukilinganisha na upana wa mabega. Inawezekana miguu na<br />
mikono ikakua zaidi kuliko uti wa mgongo, hivyo basi miguu inaweza kuwa mirefu ukilinganisha<br />
na kifua au kiwiliwili. Matokeo yake umbo lako litakuwa tofauti sana na lile la mvulana mdogo.<br />
Misuli vile vile inakuwa, hasa ile ya miguuni na mikononi. Kadri misuli inavyokua, ndivyo<br />
unavyokuwa na nguvu zaidi. Mlundikano wa misuli na mafuta utasababisha kifua kuwa kikubwa.<br />
Vile vile wavulana wengi hugundua kwamba kuna mabadiliko ya chuchu na matiti katika kipindi<br />
cha balehe. Chuchu huongezeka na kuwa kubwa kidogo. Miduara inayozinguka chuchu nayo huwa<br />
mikubwa na rangi yake kuwa nyeusi kidogo.<br />
Wavulana wengine wanajikuta matiti yao yamevimba na yanauma. Kwa wachache, uvimbe<br />
huzidi, hivyo kuwasababishia wasiwasi kuwa wataota matiti makubwa kama wanawake. Usiwe<br />
na wasiwasi, haya ni mambo ya kawaida uvimbe na ulaini unasababishwa na homoni ndani ya<br />
mwili. Uvimbe unaweza ukadumu mwaka mmoja au mwaka mmoja na nusu, lakini baada ya hapo<br />
hupungua kwa vile mwili unaacha kutengeneza homoni nyingi.<br />
Wakati wa mabadiliko yote haya unatakiwa kuwa mvumilivu kwani mwili wako hauna matatizo<br />
yoyote, na wewe ni wa kawaida kabisa. Hata kama hukui haraka ukilinganisha na rafiki zako<br />
wanavyokua, usiwe na wasiwasi utakua tu, muda bado. Ni wakati gani unaanza kukua na kiasi<br />
gani utakua,inategemea sifa bainifu unazorithi kutoka kwa wazazi wako. Hata ukichelewa<br />
17<br />
SURA YA 3