Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
146<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Katika mazingira kama haya, inaweza kuwa vigumu sana kujua tofauti ya kile anachokitaka na<br />
kile wewe unachokitaka. Ni rahisi kuchanganyikiwa lipi ni sahihi kwako.<br />
Iwapo rafiki yako wa kiume au wa kike anashinikiza mjamiiane, fikiria maswali yafuatayo:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Unathamini nini? Je, unaamini kwamba ni sahihi kujamiiana wakati huu katika maisha yako?<br />
Au je, huoni ni vyema usubiri mpaka baadaye, kama vile utakapoolewa au kuoa?<br />
Unajisikia vizuri kuhusu wazo la kujamiiana au wazo hilo linakufanya ukose raha?<br />
Unajisikia kama unaweza kukataa kujamiiana au hili linaenda kinyume na kile unachofikiri<br />
ni sahihi kwa msichana au mvulana kufanya? Kwa mfano, katika maeneo mengine, ni vigumu<br />
sana msichana kusema “HAPANA” kwa mvulana au mwanaume kwa sababu amefundishwa<br />
kwamba wakati wote anatakiwa kuwa mnyenyekevu kwa mwanaume. Katika maeneo<br />
mengine inaweza kuwa vigumu sana kwa mvulana kusema “HAPANA” kwa sababu amelelewa<br />
kuamini kwamba mwanaume wakati wote anatakiwa kujamiiana. Hivyo mtu anaweza kuhisi<br />
kwamba kwa kusema hapana inaweza kuleta matatizo.<br />
Unafikiri mwenzi wako ataendelea kukupenda na kukuheshimu kama ukikataa?<br />
Majibu ya maswali haya yatakueleza mengi kuhusu kama ujamiaane au usijamiiane na rafiki<br />
yako. Uwe msichana au mvulana, wote mnayo haki ya kukataa kujamiiana. Ni wewe unayetakiwa<br />
kufanya uamuzi mwenyewe kuhusu kujamiiana. Kama huamini kwamba ngono inakufaa wakati<br />
huu wa maisha yako, usifanye; bila hata kujali rafiki yako wa kiume au kike anasema nini.<br />
Kama hujisikii kufurahia wazo la ngono na hauko tayari kufanya, usifanye. Iwapo unafikiria rafiki<br />
yako wa kike au wa kiume hatakupenda ukikataa kujamiiana, ukweli ni kwamba hakupendi kama<br />
atakuchukia. Hakuna mtu ambaye anakupenda kweli atakulazimisha kufanya jambo ambalo<br />
unahisi ni baya kwako.<br />
Iwapo huna uhakika kama rafiki yako wa kike au wa kiume atakuwa na wewe ukikataa kujamiiana,<br />
labda jambo la maana la kufanya ni kusubiri na kuona. Mwambie rafiki yako kwamba unampenda<br />
lakini umeamua kwamba hauko tayari kujamiiana. Kama akisema ni sawa, basi unaweza ukatuliza<br />
moyo na kutulia. Unaweza kufurahia uhusiano wenu mzuri bila kukimbilia kufanya ngono.<br />
Hata hivyo, iwapo rafiki yako wa kike au kiume ataamua kukuacha, hii inaweza kuwa ngumu kwa<br />
sababu inakuonyesha kwamba rafiki yako alikuwa hakupendi. Unaweza kujisikia una huzuni na<br />
mpweke. Unaweza kufikiri ulifanya uamuzi usio sahihi, lakini hukufanya! Ulifanya kilichokuwa<br />
sahihi kwako. Katika kufanya uamuzi ukakuta rafiki yako wa kiume au wa kike alitaka kukutumia<br />
na wala hakuwa anakujali, bila shaka uvumbuzi huu utakuhuzunisha, lakini ni afadhali kuvumbua<br />
mapema kwani ingekuwa vibaya zaidi kama ungegundua baada ya kujamiiana.<br />
ShiniKiZO KutOKa KWa Watu WaZiMa<br />
Wakati mwingine watu wazima ikiwa ni pamoja na waliooa au kuolewa, wanawalazimisha vijana<br />
kufanya ngono. Mara nyingi wanaume, watu wazima (wazee) wanapenda kuwa na uhusiano wa<br />
kimapenzi na wasichana wadogo.<br />
SURA YA 12 | NGONO YA KULAZIMISHWA NA NGONO BILA YA RIDHAA YAKO<br />
Wakati mwingine vilevile wapo wanawake watu<br />
wazima wanaopenda kuwa na uhusiano wa<br />
kimapenzi na wavulana wa umri mdogo.<br />
Mara kwa mara mtu mzima hutoa zawadi, pesa<br />
au huduma maalumu kwa kijana. Mtu mzima<br />
anaweza kutoa pesa kwa ajili ya karo, nguo au<br />
peremende. Iwapo mtu mzima ni kama mwalimu<br />
au dereva wa basi, anaweza kuahidi kumpa<br />
alama nzuri au kumpakia kwenye gari bure.<br />
Lakini zawadi zote hizi siyo bure. Baada ya<br />
muda mtu mzima atadai “malipo” kwa zawadi<br />
alizotoa. Kawaida kijana “atalipa” kwa njia ya<br />
ngono.<br />
effie Kutoka Kenya ( umri wa miaka 16)<br />
“Nilikuwa na rafiki yangu ambaye alikuwa na umri wa miaka<br />
15. Rafiki yangu alikuwa na uhusiano na mtu mzima ambaye<br />
alikuwa anampa kila alichotaka, na mama yake alifahamu kuhusu<br />
uhusiano huo na wala hakujali. Siku moja akiwa anaelekea shuleni<br />
aliona gari la mzee huyo. Aliamua kumpa lifti mpaka shuleni,<br />
lakini wakiwa njiani kuelekea shuleni yule mwanaume alipita njia<br />
nyingine na akampeleka msichana kwenye nyumba ya kulala<br />
wageni na akajamiiana naye kwa nguvu”.<br />
Ingawa inaweza kufurahisha kuona mtu mzima anavutiwa na wewe na inaweza kukufanya ujisikie<br />
unapendeza na ni wa maana, uhusiano wa namna hii ni mbaya sana. Unaweza kuwa hatari kwako<br />
kwa vile:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Unaweza kupata maambukizo ya magonjwa ya<br />
zinaa, VVU/UKIMWI na mimba.<br />
Unaweza kukatisha masomo yako.<br />
Unaweza kuwa chanzo cha hasira kwa mke wake<br />
au mume wake ambaye anaweza kukushambulia<br />
au kukudhuru.<br />
Umri unapopishana sana na kipato kinapotofautiana,<br />
vilevile uhusiano hauwi sawa. Unaweza kujisikia<br />
huna mamlaka. Unaweza kuogopa kusema hapana<br />
unapoombwa ngono kwa sababu unajua ulichukua<br />
pesa au zawadi. Unaweza vilevile kuogopa<br />
kumwambia mtu mzima kutumia kondomu.<br />
Huu ni uhusiano wa hatari sana unaweza kuharibu<br />
maisha yako ya baadaye au milele!<br />
Watu wazima wanaweza kukupatia pesa au<br />
zawadi kwa ajili ya ngono. uhusiano huu ni<br />
hatari kwako<br />
KWa nini unaniPa<br />
MiMi hiZi PeSa?<br />
SitaZichuKua!<br />
aSante.<br />
Kataa kupokea zawadi na pesa. usijiingize<br />
katika deni na mtu.<br />
147