08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

146<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Katika mazingira kama haya, inaweza kuwa vigumu sana kujua tofauti ya kile anachokitaka na<br />

kile wewe unachokitaka. Ni rahisi kuchanganyikiwa lipi ni sahihi kwako.<br />

Iwapo rafiki yako wa kiume au wa kike anashinikiza mjamiiane, fikiria maswali yafuatayo:<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

Unathamini nini? Je, unaamini kwamba ni sahihi kujamiiana wakati huu katika maisha yako?<br />

Au je, huoni ni vyema usubiri mpaka baadaye, kama vile utakapoolewa au kuoa?<br />

Unajisikia vizuri kuhusu wazo la kujamiiana au wazo hilo linakufanya ukose raha?<br />

Unajisikia kama unaweza kukataa kujamiiana au hili linaenda kinyume na kile unachofikiri<br />

ni sahihi kwa msichana au mvulana kufanya? Kwa mfano, katika maeneo mengine, ni vigumu<br />

sana msichana kusema “HAPANA” kwa mvulana au mwanaume kwa sababu amefundishwa<br />

kwamba wakati wote anatakiwa kuwa mnyenyekevu kwa mwanaume. Katika maeneo<br />

mengine inaweza kuwa vigumu sana kwa mvulana kusema “HAPANA” kwa sababu amelelewa<br />

kuamini kwamba mwanaume wakati wote anatakiwa kujamiiana. Hivyo mtu anaweza kuhisi<br />

kwamba kwa kusema hapana inaweza kuleta matatizo.<br />

Unafikiri mwenzi wako ataendelea kukupenda na kukuheshimu kama ukikataa?<br />

Majibu ya maswali haya yatakueleza mengi kuhusu kama ujamiaane au usijamiiane na rafiki<br />

yako. Uwe msichana au mvulana, wote mnayo haki ya kukataa kujamiiana. Ni wewe unayetakiwa<br />

kufanya uamuzi mwenyewe kuhusu kujamiiana. Kama huamini kwamba ngono inakufaa wakati<br />

huu wa maisha yako, usifanye; bila hata kujali rafiki yako wa kiume au kike anasema nini.<br />

Kama hujisikii kufurahia wazo la ngono na hauko tayari kufanya, usifanye. Iwapo unafikiria rafiki<br />

yako wa kike au wa kiume hatakupenda ukikataa kujamiiana, ukweli ni kwamba hakupendi kama<br />

atakuchukia. Hakuna mtu ambaye anakupenda kweli atakulazimisha kufanya jambo ambalo<br />

unahisi ni baya kwako.<br />

Iwapo huna uhakika kama rafiki yako wa kike au wa kiume atakuwa na wewe ukikataa kujamiiana,<br />

labda jambo la maana la kufanya ni kusubiri na kuona. Mwambie rafiki yako kwamba unampenda<br />

lakini umeamua kwamba hauko tayari kujamiiana. Kama akisema ni sawa, basi unaweza ukatuliza<br />

moyo na kutulia. Unaweza kufurahia uhusiano wenu mzuri bila kukimbilia kufanya ngono.<br />

Hata hivyo, iwapo rafiki yako wa kike au kiume ataamua kukuacha, hii inaweza kuwa ngumu kwa<br />

sababu inakuonyesha kwamba rafiki yako alikuwa hakupendi. Unaweza kujisikia una huzuni na<br />

mpweke. Unaweza kufikiri ulifanya uamuzi usio sahihi, lakini hukufanya! Ulifanya kilichokuwa<br />

sahihi kwako. Katika kufanya uamuzi ukakuta rafiki yako wa kiume au wa kike alitaka kukutumia<br />

na wala hakuwa anakujali, bila shaka uvumbuzi huu utakuhuzunisha, lakini ni afadhali kuvumbua<br />

mapema kwani ingekuwa vibaya zaidi kama ungegundua baada ya kujamiiana.<br />

ShiniKiZO KutOKa KWa Watu WaZiMa<br />

Wakati mwingine watu wazima ikiwa ni pamoja na waliooa au kuolewa, wanawalazimisha vijana<br />

kufanya ngono. Mara nyingi wanaume, watu wazima (wazee) wanapenda kuwa na uhusiano wa<br />

kimapenzi na wasichana wadogo.<br />

SURA YA 12 | NGONO YA KULAZIMISHWA NA NGONO BILA YA RIDHAA YAKO<br />

Wakati mwingine vilevile wapo wanawake watu<br />

wazima wanaopenda kuwa na uhusiano wa<br />

kimapenzi na wavulana wa umri mdogo.<br />

Mara kwa mara mtu mzima hutoa zawadi, pesa<br />

au huduma maalumu kwa kijana. Mtu mzima<br />

anaweza kutoa pesa kwa ajili ya karo, nguo au<br />

peremende. Iwapo mtu mzima ni kama mwalimu<br />

au dereva wa basi, anaweza kuahidi kumpa<br />

alama nzuri au kumpakia kwenye gari bure.<br />

Lakini zawadi zote hizi siyo bure. Baada ya<br />

muda mtu mzima atadai “malipo” kwa zawadi<br />

alizotoa. Kawaida kijana “atalipa” kwa njia ya<br />

ngono.<br />

effie Kutoka Kenya ( umri wa miaka 16)<br />

“Nilikuwa na rafiki yangu ambaye alikuwa na umri wa miaka<br />

15. Rafiki yangu alikuwa na uhusiano na mtu mzima ambaye<br />

alikuwa anampa kila alichotaka, na mama yake alifahamu kuhusu<br />

uhusiano huo na wala hakujali. Siku moja akiwa anaelekea shuleni<br />

aliona gari la mzee huyo. Aliamua kumpa lifti mpaka shuleni,<br />

lakini wakiwa njiani kuelekea shuleni yule mwanaume alipita njia<br />

nyingine na akampeleka msichana kwenye nyumba ya kulala<br />

wageni na akajamiiana naye kwa nguvu”.<br />

Ingawa inaweza kufurahisha kuona mtu mzima anavutiwa na wewe na inaweza kukufanya ujisikie<br />

unapendeza na ni wa maana, uhusiano wa namna hii ni mbaya sana. Unaweza kuwa hatari kwako<br />

kwa vile:<br />

•<br />

•<br />

•<br />

Unaweza kupata maambukizo ya magonjwa ya<br />

zinaa, VVU/UKIMWI na mimba.<br />

Unaweza kukatisha masomo yako.<br />

Unaweza kuwa chanzo cha hasira kwa mke wake<br />

au mume wake ambaye anaweza kukushambulia<br />

au kukudhuru.<br />

Umri unapopishana sana na kipato kinapotofautiana,<br />

vilevile uhusiano hauwi sawa. Unaweza kujisikia<br />

huna mamlaka. Unaweza kuogopa kusema hapana<br />

unapoombwa ngono kwa sababu unajua ulichukua<br />

pesa au zawadi. Unaweza vilevile kuogopa<br />

kumwambia mtu mzima kutumia kondomu.<br />

Huu ni uhusiano wa hatari sana unaweza kuharibu<br />

maisha yako ya baadaye au milele!<br />

Watu wazima wanaweza kukupatia pesa au<br />

zawadi kwa ajili ya ngono. uhusiano huu ni<br />

hatari kwako<br />

KWa nini unaniPa<br />

MiMi hiZi PeSa?<br />

SitaZichuKua!<br />

aSante.<br />

Kataa kupokea zawadi na pesa. usijiingize<br />

katika deni na mtu.<br />

147

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!