Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
58<br />
•<br />
•<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Kumbuka kuwa watu wengine wanakuthamini kutokana na vile ulivyo. Mtafute mtu ambaye<br />
atakuthamini – rafiki mpya, mwalimu, dada, kaka, mzazi au ndugu mwingine.<br />
Kuwa mvumilivu. Kujiheshimu hakujengeki katika siku moja.Unaweza kujisikia vizuri baada<br />
ya siku kadhaa.<br />
KujiaMini<br />
Unapokuwa unajenga kujienzi, unajenga kujiamini pia. Kujiamini ni jambo la msingi katika afya<br />
ya kihisia. Kama kujienzi maana yake kujisikia vizuri na ukamilifu kuhusu tabia yako na namna<br />
ulivyo, kujiamini maana yake kujisikia vizuri kuhusu uwezo wako wa kufanya mambo.<br />
Kujiamini ni jambo kubwa. Watu wanaojiamini<br />
wanajisikia huru kujaribu kufanya mambo<br />
mapya bila ya kuwa na wasiwasi mkubwa<br />
kama watashindwa. Hawaogopi kujiingiza<br />
katika mazingira mapya na kati ya watu wasio<br />
wafahamu. Hawajali hata kidogo watu wengine<br />
watawafikiriaje.<br />
Kujiamini kunavutia sana. Watu wanaojiamini<br />
mara kwa mara wanapendwa sana kwa sababu<br />
wanaonekana kufurahia maisha kwa kiwango<br />
kikubwa wanapopata changamoto mpya na<br />
uzoefu wa mambo mapya.<br />
Kujiamini kunajitosheleza. Kwa maneno mengine,<br />
kujiamini kunasabisha kujiamini zaidi. Hii maana<br />
yake ni kwamba kwa jinsi unavyojaribu kufanya<br />
mambo mapya ndivyo unavyozidi kujiamini. Hii<br />
inasababishwa na sababu mbili zifuatazo:<br />
1. Unajifunza kwamba unaweza kufanikiwa katika mambo mengi ambayo hukuwahi kufikiria<br />
ungeweza.<br />
2. Unajifunza kwamba hata kama unashindwa kufanya jambo fulani hakuna neno.<br />
Unapojiamini, wakati mwingine unaweza kushindwa, lakini mara nyingi utafanikiwa. Hii ni<br />
kwasababu unaposhindwa kufanya kitu, mara kwa mara ni kwa sababu unakuwa na wasiwasi<br />
au kiwewe. Unapojiamini hata hivyo unaweza kufanya mambo mapya. Kwa ujumla, wasiwasi na<br />
kutojiamini hakuleti matatizo makubwa katika kuwa makini kwa lolote unalojaribu kufanya.<br />
Lifanyie kazi suala la kujiamini, itakusaida maisha yako yote. Unaweza:-<br />
Kujifikiria kama mtu unayeweza – yule ambaye unaweza kufanikisha.<br />
•<br />
•<br />
Kujiamini kunakuwezesha kujaribu mambo<br />
mapya bila kuhofu kushindwa<br />
Jipe changamoto. Jaribu mambo mapya na uwe muwazi katika mambo ambayo hukuyazoea.<br />
Jizoeshe kusema “sifahamu jinsi ya kufanya kile lakini ningependa kujaribu”<br />
JE? Unafahamu kwa nini wasichana wana matatizo zaidi ya kujiheshimu na<br />
kujiamini kuliko wavulana?<br />
Wakati mwingine wasichana wana matatizo ya kujiamini na kujienzi kidogo kuliko wavulana<br />
wa rika moja. Kwa nini iwe hivi? Je, kujienzi na kujiamini kunahusiana na jinsi ya mtu?<br />
Jibu ni “Hapana” kujienzi na kujiamini hakuhusiani na jinsi ya mtu. Hata hivyo heshima na<br />
imani ya mtu inaweza kuathirika sana kwa namna au jinsi anavyotendewa na watu wengine<br />
– wazazi, wadogo zake, ndugu, walimu, majirani viongozi wa dini na viongozi ndani ya jamii,<br />
n.k.<br />
Kwa bahati mbaya katika utamaduni mwingine wavulana na wasichana wanatendewa<br />
tofauti kabisa; na hii inaweza kuathiri sana namna wanavyojiona na uwezo wao. Kwa mfano;<br />
katika familia zingine wavulana wanaweza kupewa nafasi zaidi katika elimu na mafunzo<br />
ya kazi; na walimu wakati mwingine wanawajali zaidi wavulana. Kwa upande mwingine<br />
wasichana wanaweza wasipate nafasi kama hiyo. Wanaweza wasiruhusiwe kucheza na<br />
wenzao au kucheza michezo kama kaka zao wanavyofanya. Zaidi ya hapo kazi ngumu<br />
wanazofanya nyumbani na shambani zinaweza zisionekane na wala zisitambulike. Matokeo<br />
yake wasichana na wanawake hujiona hawana thamani na wanaweza kuanza kuamini<br />
kwamba thamani yao ni ndogo kuliko ya wavulana na wanaume. Lakini hii sio kweli! Watu<br />
wote ni sawa. Iwapo wote watapata nafasi sawa, wasichana wanaweza kufanya vizuri<br />
shuleni, katika kazi na kitu chochote wanachotaka kufanya.<br />
Inaweza kuwa vigumu sana kama wewe ni msichana na unaishi katika mazingira ambayo<br />
mara kwa mara unajisikia huthaminiwi kama ambavyo mvulana anavyothaminiwa. Haya<br />
hapa ni mambo machache ambayo unaweza kufanya ili kuimudu hali hiyo:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
SURA YA 6 | UTUNZAJI AfYA YA AKILI NA MOYO<br />
Wakati wote kumbuka kwamba una thamani kubwa bila kujali watu wengine wanasema<br />
nini. <strong>Wewe</strong> una akili na uwezo sawa na mvulana yeyote.<br />
Jitahidi mara dufu katika kujenga kujienzi na kujiamini kwako.<br />
Jisifu mwenyewe na ridhika unapofanya kazi vizuri. Usisubiri kusifiwa na watu<br />
wengine ambao wanaweza wasikusifu.<br />
Tumia kila nafasi uliyo nayo kujifunza stadi mpya na fanya mengi kati ya hayo.<br />
Kumbuka, kila unapofanikisha jambo utakuwa unajihakikishia mwenyewe na watu<br />
wengine kwamba unayo thamani kama ambavyo wengine walivyo nayo.<br />
Tambua changamoto unazokumbana nazo; lakini usikate tamaa. Kama unaishi katika<br />
jamii ambayo wanawake wanadharauliwa sana usitegemee hali hiyo kubadilika katika<br />
siku moja, lakini hata hivyo lisikufanye ukate tamaa.<br />
Zungumza na wazazi wako au mtu mzima yeyote anayejali. Kwa mfano; kama wazazi<br />
wanataka kukuachisha shule au wanataka uolewe jaribu kutafuta mtu wa kuzungumza<br />
naye. Eleza namna elimu ilivyo ya muhimu kwako na waombe kama wanaweza<br />
kukusaidia kumudu hali hiyo.<br />
59