08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

58<br />

•<br />

•<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Kumbuka kuwa watu wengine wanakuthamini kutokana na vile ulivyo. Mtafute mtu ambaye<br />

atakuthamini – rafiki mpya, mwalimu, dada, kaka, mzazi au ndugu mwingine.<br />

Kuwa mvumilivu. Kujiheshimu hakujengeki katika siku moja.Unaweza kujisikia vizuri baada<br />

ya siku kadhaa.<br />

KujiaMini<br />

Unapokuwa unajenga kujienzi, unajenga kujiamini pia. Kujiamini ni jambo la msingi katika afya<br />

ya kihisia. Kama kujienzi maana yake kujisikia vizuri na ukamilifu kuhusu tabia yako na namna<br />

ulivyo, kujiamini maana yake kujisikia vizuri kuhusu uwezo wako wa kufanya mambo.<br />

Kujiamini ni jambo kubwa. Watu wanaojiamini<br />

wanajisikia huru kujaribu kufanya mambo<br />

mapya bila ya kuwa na wasiwasi mkubwa<br />

kama watashindwa. Hawaogopi kujiingiza<br />

katika mazingira mapya na kati ya watu wasio<br />

wafahamu. Hawajali hata kidogo watu wengine<br />

watawafikiriaje.<br />

Kujiamini kunavutia sana. Watu wanaojiamini<br />

mara kwa mara wanapendwa sana kwa sababu<br />

wanaonekana kufurahia maisha kwa kiwango<br />

kikubwa wanapopata changamoto mpya na<br />

uzoefu wa mambo mapya.<br />

Kujiamini kunajitosheleza. Kwa maneno mengine,<br />

kujiamini kunasabisha kujiamini zaidi. Hii maana<br />

yake ni kwamba kwa jinsi unavyojaribu kufanya<br />

mambo mapya ndivyo unavyozidi kujiamini. Hii<br />

inasababishwa na sababu mbili zifuatazo:<br />

1. Unajifunza kwamba unaweza kufanikiwa katika mambo mengi ambayo hukuwahi kufikiria<br />

ungeweza.<br />

2. Unajifunza kwamba hata kama unashindwa kufanya jambo fulani hakuna neno.<br />

Unapojiamini, wakati mwingine unaweza kushindwa, lakini mara nyingi utafanikiwa. Hii ni<br />

kwasababu unaposhindwa kufanya kitu, mara kwa mara ni kwa sababu unakuwa na wasiwasi<br />

au kiwewe. Unapojiamini hata hivyo unaweza kufanya mambo mapya. Kwa ujumla, wasiwasi na<br />

kutojiamini hakuleti matatizo makubwa katika kuwa makini kwa lolote unalojaribu kufanya.<br />

Lifanyie kazi suala la kujiamini, itakusaida maisha yako yote. Unaweza:-<br />

Kujifikiria kama mtu unayeweza – yule ambaye unaweza kufanikisha.<br />

•<br />

•<br />

Kujiamini kunakuwezesha kujaribu mambo<br />

mapya bila kuhofu kushindwa<br />

Jipe changamoto. Jaribu mambo mapya na uwe muwazi katika mambo ambayo hukuyazoea.<br />

Jizoeshe kusema “sifahamu jinsi ya kufanya kile lakini ningependa kujaribu”<br />

JE? Unafahamu kwa nini wasichana wana matatizo zaidi ya kujiheshimu na<br />

kujiamini kuliko wavulana?<br />

Wakati mwingine wasichana wana matatizo ya kujiamini na kujienzi kidogo kuliko wavulana<br />

wa rika moja. Kwa nini iwe hivi? Je, kujienzi na kujiamini kunahusiana na jinsi ya mtu?<br />

Jibu ni “Hapana” kujienzi na kujiamini hakuhusiani na jinsi ya mtu. Hata hivyo heshima na<br />

imani ya mtu inaweza kuathirika sana kwa namna au jinsi anavyotendewa na watu wengine<br />

– wazazi, wadogo zake, ndugu, walimu, majirani viongozi wa dini na viongozi ndani ya jamii,<br />

n.k.<br />

Kwa bahati mbaya katika utamaduni mwingine wavulana na wasichana wanatendewa<br />

tofauti kabisa; na hii inaweza kuathiri sana namna wanavyojiona na uwezo wao. Kwa mfano;<br />

katika familia zingine wavulana wanaweza kupewa nafasi zaidi katika elimu na mafunzo<br />

ya kazi; na walimu wakati mwingine wanawajali zaidi wavulana. Kwa upande mwingine<br />

wasichana wanaweza wasipate nafasi kama hiyo. Wanaweza wasiruhusiwe kucheza na<br />

wenzao au kucheza michezo kama kaka zao wanavyofanya. Zaidi ya hapo kazi ngumu<br />

wanazofanya nyumbani na shambani zinaweza zisionekane na wala zisitambulike. Matokeo<br />

yake wasichana na wanawake hujiona hawana thamani na wanaweza kuanza kuamini<br />

kwamba thamani yao ni ndogo kuliko ya wavulana na wanaume. Lakini hii sio kweli! Watu<br />

wote ni sawa. Iwapo wote watapata nafasi sawa, wasichana wanaweza kufanya vizuri<br />

shuleni, katika kazi na kitu chochote wanachotaka kufanya.<br />

Inaweza kuwa vigumu sana kama wewe ni msichana na unaishi katika mazingira ambayo<br />

mara kwa mara unajisikia huthaminiwi kama ambavyo mvulana anavyothaminiwa. Haya<br />

hapa ni mambo machache ambayo unaweza kufanya ili kuimudu hali hiyo:<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

SURA YA 6 | UTUNZAJI AfYA YA AKILI NA MOYO<br />

Wakati wote kumbuka kwamba una thamani kubwa bila kujali watu wengine wanasema<br />

nini. <strong>Wewe</strong> una akili na uwezo sawa na mvulana yeyote.<br />

Jitahidi mara dufu katika kujenga kujienzi na kujiamini kwako.<br />

Jisifu mwenyewe na ridhika unapofanya kazi vizuri. Usisubiri kusifiwa na watu<br />

wengine ambao wanaweza wasikusifu.<br />

Tumia kila nafasi uliyo nayo kujifunza stadi mpya na fanya mengi kati ya hayo.<br />

Kumbuka, kila unapofanikisha jambo utakuwa unajihakikishia mwenyewe na watu<br />

wengine kwamba unayo thamani kama ambavyo wengine walivyo nayo.<br />

Tambua changamoto unazokumbana nazo; lakini usikate tamaa. Kama unaishi katika<br />

jamii ambayo wanawake wanadharauliwa sana usitegemee hali hiyo kubadilika katika<br />

siku moja, lakini hata hivyo lisikufanye ukate tamaa.<br />

Zungumza na wazazi wako au mtu mzima yeyote anayejali. Kwa mfano; kama wazazi<br />

wanataka kukuachisha shule au wanataka uolewe jaribu kutafuta mtu wa kuzungumza<br />

naye. Eleza namna elimu ilivyo ya muhimu kwako na waombe kama wanaweza<br />

kukusaidia kumudu hali hiyo.<br />

59

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!