Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
136<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
KujitunZa na KuMtunZa MtOtO baaDa Ya KujiFunGua<br />
Kama ulivyokuwa unakwenda kliniki kabla ya<br />
kujifungua, hakikisha unakwenda tena kwa uchunguzi<br />
baada ya kujifungua. Kama ulimzalia mtoto wako<br />
nyumbani hakikisha unakwenda kliniki kwa ajili<br />
ya uchunguzi ndani ya siku tatu. Kama ulimzalia<br />
mtoto wako hospitalini nenda baada ya wiki sita ili<br />
mkunga aone kama tumbo lako linarudia hali yake<br />
ya awali. Mkunga anatakiwa pia kuangalia kama<br />
huna maambukizo ya magonjwa au hutokwi na damu<br />
sana.Kama ulipoteza damu nyingi wakati wa kuzaa<br />
mkunga atakupa dawa za madini ya chuma ili kusaidia<br />
kuongeza damu.<br />
Mkunga anaweza vilevile kujibu maswali mengi<br />
utakayokuwa nayo kuhusu kunyonyesha mtoto, kulala,<br />
kinga kwa mtoto, kuzuia mimba na mambo mengine.<br />
Mwanamke aliyezaa kwa mara ya kwanza mara nyingi<br />
anakuwa na maswali mengi hivyo kuongea na mkunga<br />
inaweza kukusaidia.<br />
KuhaRibiKa MiMba<br />
Mara nyingine mimba huwa inaharibika/inatoka yenyewe tu. Tunasema mimba imetoka kwa<br />
bahati mbaya. Fitasi inakufa na inatoka kupitia ukeni. Malaria au magonjwa ya ngono huweza<br />
kusababisha kuharibika mimba. Mimba inaweza kutoka vilevile kama fitasi ina matatizo.<br />
Kama mimba itakuwa imetoka mwanamke anahitaji kumwona mhudumu wa afya ili kuhakikisha<br />
hapati maambukizo kwenye tumbo la uzazi. Mhudumu wa afya anaweza pia akatambua<br />
kilichosabisha mimba kutoka na kutoa matibabu ya magonjwa kama ya ngono.<br />
Mimba inaweza vilevile kutolewa kwa makusudi kwa kupitia taratibu za kitabibu. Mimba inaweza<br />
kutolewa na mganga aliyesomea katika mazingira ya hali ya usafi. Kutoa mimba ni utaratibu<br />
salama kitabibu kwa ujumla na ni salama kuliko kuzaa. Katika nchi nyingi za Kiafrika ni kosa la<br />
jinai kutoa mimba isipokuwa katika mazingira ya matatizo kama kubakwa au kujamiiana kwa<br />
maharimu (ndugu wa karibu) au wakati ambapo maisha ya mwanamke yako hatarini kwa ajili<br />
ya mimba au fitasi si ya kawaida na hata akizaliwa mtoto hataishi. Uthibitisho wa kitabibu<br />
unatakiwa kuwepo kuwa mhusika alibakwa kulikuwepo kujamiiana kwa maharimu au fitasi si ya<br />
kawaida.<br />
Kutoa mimba kinyume cha sheria katika nchi nyingi barani Afrika ni hatari sana. Kutoa mimba<br />
kunafanywa katika mazingira machafu na ya hatari na mara nyingi watu wengi wanaotoa<br />
mimba hawajasomea. Kwa sababu kutoa mimba hakuruhusiwi, mtoaji mimba anaweza kutoa<br />
bila utaratibu, kwa haraka na kuogopa na katika mazingira na vifaa vichafu. Mambo yote haya<br />
yanamuweka mwanamke katika hatari kubwa. Kwa hakika, katika nchi nyingi za Afrika, robo ya<br />
vifo vya wanawake wajawazito vinasababishwa na matatizo ya ama mimba kutoka au kutoa<br />
mimba.<br />
SURA YA 11 | MIMBA NA UZUIAJI WA MIMBA<br />
Kutoa mimba kwa kutumia njia isiyo salama<br />
kunaweza kusababisha matatizo ya kiafya.<br />
Kifaa cha kutolea mimba kikiingizwa kwenye<br />
mlango wa mfuko wa kizazi kinaweza<br />
kikasababisha uharibifu kwenye kibofu<br />
cha mkojo au utumbo mdogo au mlango<br />
wa mfuko wa kizazi. Mfuko wa kizazi<br />
ulioharibika utatakiwa uondolewe. Maana<br />
yake, msichana hataweza kupata mtoto tena.<br />
Kutoa mimba kusiko salama vilevile<br />
kunaweza kusababisha kuvuja damu,<br />
maambukizo ya magonjwa na kifo. Kuingiza<br />
kifaa cha kutolea mimba kwenye mlango<br />
wa mfuko wa kizazi na kizazi kunaweza<br />
kusababisha kuvuja sana damu na msichana<br />
anaweza akavuja damu mpaka akafa. Miti<br />
shamba na vifaa vingine vinavyotumika<br />
kuanzisha uchungu mara nyingi siyo safi;<br />
vinaweza kuleta vijidudu vya maradhi katika<br />
mfuko wa kizazi. Kizazi na mirija ya kupitisha<br />
mayai ya mgonjwa vinaweza kuathirika sana<br />
kiasi cha kusababishiwa ugumba au kifo. Miti<br />
shamba, dawa au kemikali ambazo msichana<br />
anameza zinaweza kumfanya awe mgonjwa<br />
sana na anaweza akawa amejipa sumu<br />
mwenyewe.<br />
Je unajua matokeo ya utoaji mimba usio<br />
salama?<br />
Jane alipopata mimba alikuwa na miaka 15<br />
na alikuwa Kidato cha Tatu. Alitaka sana<br />
kuendelea na shule, aliishi na shangazi yake,<br />
ambaye alimpeleka kwa mtu aliyedai ni<br />
mganga anayefanya kazi kwenye hospitali<br />
kubwa mjini Kampala. Mtu huyu aliingiza<br />
kifaa kwenye uke. “Maji” yakatoka. Alisikia<br />
maumivu makali sana, lakini aliambiwa asilie<br />
kwa sababu hata hivyo “alitaka” mwenyewe<br />
kilichomtokea. Shughuli ilichukua dakika 15.<br />
Alirudi nyumbani na alitokwa na damu wiki<br />
nzima, akidhoofu kidogokidogo kila siku.<br />
Tumbo lake liliuma na uke ukawa unatoa<br />
majimaji yenye harufu mbaya. Baadaye<br />
alipelekwa kliniki inayohudumia vijana. Kliniki<br />
waligundua amechanika sehemu kubwa ya<br />
mfuko wa kizazi. Ilibidi afanyiwe upasuaji<br />
na kukaa hospitalini kwa muda wa wiki nne<br />
kutibu kidonda na maambukizo ya magonjwa.<br />
Jane bado hajui iwapo ataweza kupata watoto<br />
baadaye.<br />
Diana kutoka uganda (umri wa miaka 15)<br />
“Kutoa mimba ni hatari sana hasa kwa kutumia miti shamba. Ni<br />
afadhali usishiriki katika ngono kabisa”.<br />
nedina kutoka uganda (umri wa miaka 18)<br />
“Rafiki yangu wa kike akipata mimba nitamkatisha tamaa asitoe<br />
mimba kwa sababu ni hatari. Nitamsihi azae na kisha aendelee na<br />
masomo yake hapo baadaye”<br />
Kutoa mimba kunaweza kuleta matokeo ya kusikitisha kijamii. Watu wengine wakijua kwamba<br />
msichana ametoa mimba, anaweza kufukuzwa shule, kutoaminika au kufedheheshwa na marafiki<br />
au na familia.<br />
Hata hivyo, wasichana wengi wanaishia kutoa mimba kwa njia isiyo salama wanapojikuta<br />
wamepata mimba. Wanasahau hatari za kutoa mimba kwa sababu ya hofu, familia zao<br />
zitakapogundua ujauzito wao. Wanakata tamaa ya kuendelea na masomo. Marafiki zao wa kiume<br />
wanaweza kuwa wamewaacha au kuwalazimisha watoe mimba.<br />
137