08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

136<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

KujitunZa na KuMtunZa MtOtO baaDa Ya KujiFunGua<br />

Kama ulivyokuwa unakwenda kliniki kabla ya<br />

kujifungua, hakikisha unakwenda tena kwa uchunguzi<br />

baada ya kujifungua. Kama ulimzalia mtoto wako<br />

nyumbani hakikisha unakwenda kliniki kwa ajili<br />

ya uchunguzi ndani ya siku tatu. Kama ulimzalia<br />

mtoto wako hospitalini nenda baada ya wiki sita ili<br />

mkunga aone kama tumbo lako linarudia hali yake<br />

ya awali. Mkunga anatakiwa pia kuangalia kama<br />

huna maambukizo ya magonjwa au hutokwi na damu<br />

sana.Kama ulipoteza damu nyingi wakati wa kuzaa<br />

mkunga atakupa dawa za madini ya chuma ili kusaidia<br />

kuongeza damu.<br />

Mkunga anaweza vilevile kujibu maswali mengi<br />

utakayokuwa nayo kuhusu kunyonyesha mtoto, kulala,<br />

kinga kwa mtoto, kuzuia mimba na mambo mengine.<br />

Mwanamke aliyezaa kwa mara ya kwanza mara nyingi<br />

anakuwa na maswali mengi hivyo kuongea na mkunga<br />

inaweza kukusaidia.<br />

KuhaRibiKa MiMba<br />

Mara nyingine mimba huwa inaharibika/inatoka yenyewe tu. Tunasema mimba imetoka kwa<br />

bahati mbaya. Fitasi inakufa na inatoka kupitia ukeni. Malaria au magonjwa ya ngono huweza<br />

kusababisha kuharibika mimba. Mimba inaweza kutoka vilevile kama fitasi ina matatizo.<br />

Kama mimba itakuwa imetoka mwanamke anahitaji kumwona mhudumu wa afya ili kuhakikisha<br />

hapati maambukizo kwenye tumbo la uzazi. Mhudumu wa afya anaweza pia akatambua<br />

kilichosabisha mimba kutoka na kutoa matibabu ya magonjwa kama ya ngono.<br />

Mimba inaweza vilevile kutolewa kwa makusudi kwa kupitia taratibu za kitabibu. Mimba inaweza<br />

kutolewa na mganga aliyesomea katika mazingira ya hali ya usafi. Kutoa mimba ni utaratibu<br />

salama kitabibu kwa ujumla na ni salama kuliko kuzaa. Katika nchi nyingi za Kiafrika ni kosa la<br />

jinai kutoa mimba isipokuwa katika mazingira ya matatizo kama kubakwa au kujamiiana kwa<br />

maharimu (ndugu wa karibu) au wakati ambapo maisha ya mwanamke yako hatarini kwa ajili<br />

ya mimba au fitasi si ya kawaida na hata akizaliwa mtoto hataishi. Uthibitisho wa kitabibu<br />

unatakiwa kuwepo kuwa mhusika alibakwa kulikuwepo kujamiiana kwa maharimu au fitasi si ya<br />

kawaida.<br />

Kutoa mimba kinyume cha sheria katika nchi nyingi barani Afrika ni hatari sana. Kutoa mimba<br />

kunafanywa katika mazingira machafu na ya hatari na mara nyingi watu wengi wanaotoa<br />

mimba hawajasomea. Kwa sababu kutoa mimba hakuruhusiwi, mtoaji mimba anaweza kutoa<br />

bila utaratibu, kwa haraka na kuogopa na katika mazingira na vifaa vichafu. Mambo yote haya<br />

yanamuweka mwanamke katika hatari kubwa. Kwa hakika, katika nchi nyingi za Afrika, robo ya<br />

vifo vya wanawake wajawazito vinasababishwa na matatizo ya ama mimba kutoka au kutoa<br />

mimba.<br />

SURA YA 11 | MIMBA NA UZUIAJI WA MIMBA<br />

Kutoa mimba kwa kutumia njia isiyo salama<br />

kunaweza kusababisha matatizo ya kiafya.<br />

Kifaa cha kutolea mimba kikiingizwa kwenye<br />

mlango wa mfuko wa kizazi kinaweza<br />

kikasababisha uharibifu kwenye kibofu<br />

cha mkojo au utumbo mdogo au mlango<br />

wa mfuko wa kizazi. Mfuko wa kizazi<br />

ulioharibika utatakiwa uondolewe. Maana<br />

yake, msichana hataweza kupata mtoto tena.<br />

Kutoa mimba kusiko salama vilevile<br />

kunaweza kusababisha kuvuja damu,<br />

maambukizo ya magonjwa na kifo. Kuingiza<br />

kifaa cha kutolea mimba kwenye mlango<br />

wa mfuko wa kizazi na kizazi kunaweza<br />

kusababisha kuvuja sana damu na msichana<br />

anaweza akavuja damu mpaka akafa. Miti<br />

shamba na vifaa vingine vinavyotumika<br />

kuanzisha uchungu mara nyingi siyo safi;<br />

vinaweza kuleta vijidudu vya maradhi katika<br />

mfuko wa kizazi. Kizazi na mirija ya kupitisha<br />

mayai ya mgonjwa vinaweza kuathirika sana<br />

kiasi cha kusababishiwa ugumba au kifo. Miti<br />

shamba, dawa au kemikali ambazo msichana<br />

anameza zinaweza kumfanya awe mgonjwa<br />

sana na anaweza akawa amejipa sumu<br />

mwenyewe.<br />

Je unajua matokeo ya utoaji mimba usio<br />

salama?<br />

Jane alipopata mimba alikuwa na miaka 15<br />

na alikuwa Kidato cha Tatu. Alitaka sana<br />

kuendelea na shule, aliishi na shangazi yake,<br />

ambaye alimpeleka kwa mtu aliyedai ni<br />

mganga anayefanya kazi kwenye hospitali<br />

kubwa mjini Kampala. Mtu huyu aliingiza<br />

kifaa kwenye uke. “Maji” yakatoka. Alisikia<br />

maumivu makali sana, lakini aliambiwa asilie<br />

kwa sababu hata hivyo “alitaka” mwenyewe<br />

kilichomtokea. Shughuli ilichukua dakika 15.<br />

Alirudi nyumbani na alitokwa na damu wiki<br />

nzima, akidhoofu kidogokidogo kila siku.<br />

Tumbo lake liliuma na uke ukawa unatoa<br />

majimaji yenye harufu mbaya. Baadaye<br />

alipelekwa kliniki inayohudumia vijana. Kliniki<br />

waligundua amechanika sehemu kubwa ya<br />

mfuko wa kizazi. Ilibidi afanyiwe upasuaji<br />

na kukaa hospitalini kwa muda wa wiki nne<br />

kutibu kidonda na maambukizo ya magonjwa.<br />

Jane bado hajui iwapo ataweza kupata watoto<br />

baadaye.<br />

Diana kutoka uganda (umri wa miaka 15)<br />

“Kutoa mimba ni hatari sana hasa kwa kutumia miti shamba. Ni<br />

afadhali usishiriki katika ngono kabisa”.<br />

nedina kutoka uganda (umri wa miaka 18)<br />

“Rafiki yangu wa kike akipata mimba nitamkatisha tamaa asitoe<br />

mimba kwa sababu ni hatari. Nitamsihi azae na kisha aendelee na<br />

masomo yake hapo baadaye”<br />

Kutoa mimba kunaweza kuleta matokeo ya kusikitisha kijamii. Watu wengine wakijua kwamba<br />

msichana ametoa mimba, anaweza kufukuzwa shule, kutoaminika au kufedheheshwa na marafiki<br />

au na familia.<br />

Hata hivyo, wasichana wengi wanaishia kutoa mimba kwa njia isiyo salama wanapojikuta<br />

wamepata mimba. Wanasahau hatari za kutoa mimba kwa sababu ya hofu, familia zao<br />

zitakapogundua ujauzito wao. Wanakata tamaa ya kuendelea na masomo. Marafiki zao wa kiume<br />

wanaweza kuwa wamewaacha au kuwalazimisha watoe mimba.<br />

137

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!