Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
10<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Wavulana na wasichana wengine hukua haraka sana wakati wa balehe kiasi cha kwamba ngozi<br />
yao inashindwa kustahimili ukuaji haraka wa mifupa. Wakati mwingine inapotokea hivyo alama<br />
za misitari hutokea kwenye ngozi. Alama hizi zinaweza kupotea au zisionekane kiurahisi mtu<br />
anavyoendelea kukua, lakini zinaweza zisipotee moja kwa moja.<br />
Hata kama unajiona kukua haraka,bado balehe ni kitendo<br />
cha taratibu mno. Itachukua muda mrefu kabla hujawa<br />
mtu mzima kimwili na kifikra. Kwa wakati huu yafuatayo ni<br />
mambo ya kuzingatia.<br />
Kila Mtu YuKO tOFauti<br />
Kila mtu hufikia balehe kwa wakati tofauti na kwa kiwango<br />
tofauti. Matiti yako yanaweza kuchelewa kukua kuliko ya<br />
rafiki zako lakini wewe unaweza ukavunja ungo mapema<br />
au unaweza kuyapata yote haya baadaye sana. Matiti<br />
yanaweza yakakua na ukavunja ungo akiwa na umri wa<br />
miaka 12 na wewe matiti yanaweza kukua na ukavunja ungo<br />
ukiwa na umri wa miaka 15.<br />
Au kama wewe ni mvulana unaweza ukawa na rafiki yako<br />
ambaye sauti yake ili badilika kuwa nzito akiwa na umri wa<br />
miaka 13. Anaweza akawa ameota mavuzi na misuli wakati<br />
wewe hujakua hata sentimeta moja!<br />
Wavulana hawa wote wana umri wa miaka<br />
13,lakini wanakua kitofauti<br />
Wasichana hawa wote wana umri wa<br />
miaka 13,lakini wanakua kitofauti<br />
Kumbuka kila mtu yuko tofauti na kila yanapokutokea mabadiliko huu ndio wakati muafaka<br />
kwako.<br />
Kila Mtu ana MabaDiliKO YaKe<br />
Kwa kutumia kigezo cha afya, haitegemei kama mwili<br />
wako unakua haraka au taratibu kuliko rika lako.<br />
Mwili wako utabadilika muda utakapofikia. Hakuna<br />
unachoweza kufanya kuhusu muda wa mabadiliko.<br />
Wasichana na wavulana wengine wenye afya nzuri<br />
huchelewa kukua kuliko wenzao wa rika moja.<br />
Wasichana na wavulana wengine wanakua mapema<br />
kuliko wenzao wa rika moja na wala hawana kasoro<br />
yoyote na wana afya nzuri pia.<br />
Lakini hata hivyo unaweza kupata matatizo kama<br />
utakuwa tofauti na wengine.Kwa mfano: inaweza kuwa<br />
vigumu kwa msichana kuwa wa kwanza kuwa na matiti<br />
darasani, au mvulana kuwa wa mwisho kubadilika sauti.<br />
Hii inaweza kusababisha kutaniwa na unaweza kujisikia<br />
upo tofauti sana na kundi rika lako.<br />
SURA YA 2 | MABADILIKO YA MWILI<br />
Sherifan, kutoka Ghana (umri wa miaka 15)<br />
“Nilianza kuona mabadiliko katika mwili wangu nikiwa na miaka 11. Matiti<br />
yalianza kuota, nywele zikaota kwapani na kwenye via vya uzazi. Nilijisikia<br />
vibaya sana kwa sababu nilipata mabadiliko haya mapema sana na<br />
nilijiona niko tofauti sana na wenzangu wa rika moja”<br />
Sherry, kutoka Ghana (umri wa miaka 19)<br />
“Nilikuwa darasa la sita(6), sifahamu kama marafiki zangu walikuwa<br />
wanachelewa kukua au mimi nilikuwa nimewahi kukua, lakini nilijisikia<br />
vibaya matiti yalipoanza kukua. Niliwahi kumsikia mama akisema jinsi<br />
walivyokuwa wakitumia tapoli, “kifaa kidogo cha ubao kilichotumika kusaga<br />
pilipili”, kujaribu kuondoa uvimbe kwenye matiti wakati wa enzi zao.<br />
Kwa hiyo nilijaribu, kama mara tatu hivi. Lilikuwa ni jambo la kuchekesha,<br />
lakini hata hivyo haikusaidia kitu. Lakini sasa hivi waliokuwa wananitania<br />
wana matiti makubwa kuliko ya kwangu.”<br />
Kumbuka kuwa mambo haya yanaisha kadri muda unavyopita. Utakapofikisha miaka 20<br />
hakutakuwa na tofauti yoyote kwako au kwa mtu mwingine, iwapo sauti yako ilibadilika ukiwa na<br />
miaka 13 au miaka 17. Hakutakuwa na tofauti iwapo ulivunja ungo ukiwa na miaka 11 au miaka 16.<br />
Sherry, kutoka Ghana (umri; miaka 19)<br />
“Ebu tuyaache mambo yaende kama yalivyopangwa kwani hata kama<br />
hupendi huwezi kubadili kitu isipokuwa kujikubali tu.”<br />
Ingawa huwezi kuubadili mwili wako yapo mambo yanayokuhusu ambayo unaweza<br />
kuyabadili:<br />
1. Unaweza kuhakikisha kuwa wewe ni mtu mzuri. Hakikisha kuwa unafanya kazi kwa<br />
bidiii katika lolote utakalokuwa unafanya (shuleni, kazini na nyumbani). Unaweza<br />
ukakuza haiba yako, ucheshi wako,pia na tabia yako. Angalia kuwa wewe ni nani na<br />
unataka uweje baadaye na wala sio vile unavyoonekana.<br />
2. Jitahidi sana kutotilia maanani utani jaribu kupuuza na usiwaruhusu wanaokutania<br />
waone umefadhaika. Mwishowe watachoka kukutania.<br />
3. Heshima na kukubalika na rafiki zako visije vikakushawishi kufanya mambo ambayo<br />
sio mazuri kwako. Usiruhusu marafiki zako kukulazimisha kufanya mambo ambayo<br />
unajua sio sahihi, kama vile kutania watu wengine, kutumia madawa ya kulevya au<br />
kujiingiza kwenye mambo yanayoweza kukudhuru.<br />
4. Jielimishe mwenyewe kwa kutafuta taarifa sahihi. Hakihisha unafahamu wapi utapata<br />
taarifa unazozihitaji na majibu ya maswali yako yote wakati unapoupitia ujana<br />
11