08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

10<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Wavulana na wasichana wengine hukua haraka sana wakati wa balehe kiasi cha kwamba ngozi<br />

yao inashindwa kustahimili ukuaji haraka wa mifupa. Wakati mwingine inapotokea hivyo alama<br />

za misitari hutokea kwenye ngozi. Alama hizi zinaweza kupotea au zisionekane kiurahisi mtu<br />

anavyoendelea kukua, lakini zinaweza zisipotee moja kwa moja.<br />

Hata kama unajiona kukua haraka,bado balehe ni kitendo<br />

cha taratibu mno. Itachukua muda mrefu kabla hujawa<br />

mtu mzima kimwili na kifikra. Kwa wakati huu yafuatayo ni<br />

mambo ya kuzingatia.<br />

Kila Mtu YuKO tOFauti<br />

Kila mtu hufikia balehe kwa wakati tofauti na kwa kiwango<br />

tofauti. Matiti yako yanaweza kuchelewa kukua kuliko ya<br />

rafiki zako lakini wewe unaweza ukavunja ungo mapema<br />

au unaweza kuyapata yote haya baadaye sana. Matiti<br />

yanaweza yakakua na ukavunja ungo akiwa na umri wa<br />

miaka 12 na wewe matiti yanaweza kukua na ukavunja ungo<br />

ukiwa na umri wa miaka 15.<br />

Au kama wewe ni mvulana unaweza ukawa na rafiki yako<br />

ambaye sauti yake ili badilika kuwa nzito akiwa na umri wa<br />

miaka 13. Anaweza akawa ameota mavuzi na misuli wakati<br />

wewe hujakua hata sentimeta moja!<br />

Wavulana hawa wote wana umri wa miaka<br />

13,lakini wanakua kitofauti<br />

Wasichana hawa wote wana umri wa<br />

miaka 13,lakini wanakua kitofauti<br />

Kumbuka kila mtu yuko tofauti na kila yanapokutokea mabadiliko huu ndio wakati muafaka<br />

kwako.<br />

Kila Mtu ana MabaDiliKO YaKe<br />

Kwa kutumia kigezo cha afya, haitegemei kama mwili<br />

wako unakua haraka au taratibu kuliko rika lako.<br />

Mwili wako utabadilika muda utakapofikia. Hakuna<br />

unachoweza kufanya kuhusu muda wa mabadiliko.<br />

Wasichana na wavulana wengine wenye afya nzuri<br />

huchelewa kukua kuliko wenzao wa rika moja.<br />

Wasichana na wavulana wengine wanakua mapema<br />

kuliko wenzao wa rika moja na wala hawana kasoro<br />

yoyote na wana afya nzuri pia.<br />

Lakini hata hivyo unaweza kupata matatizo kama<br />

utakuwa tofauti na wengine.Kwa mfano: inaweza kuwa<br />

vigumu kwa msichana kuwa wa kwanza kuwa na matiti<br />

darasani, au mvulana kuwa wa mwisho kubadilika sauti.<br />

Hii inaweza kusababisha kutaniwa na unaweza kujisikia<br />

upo tofauti sana na kundi rika lako.<br />

SURA YA 2 | MABADILIKO YA MWILI<br />

Sherifan, kutoka Ghana (umri wa miaka 15)<br />

“Nilianza kuona mabadiliko katika mwili wangu nikiwa na miaka 11. Matiti<br />

yalianza kuota, nywele zikaota kwapani na kwenye via vya uzazi. Nilijisikia<br />

vibaya sana kwa sababu nilipata mabadiliko haya mapema sana na<br />

nilijiona niko tofauti sana na wenzangu wa rika moja”<br />

Sherry, kutoka Ghana (umri wa miaka 19)<br />

“Nilikuwa darasa la sita(6), sifahamu kama marafiki zangu walikuwa<br />

wanachelewa kukua au mimi nilikuwa nimewahi kukua, lakini nilijisikia<br />

vibaya matiti yalipoanza kukua. Niliwahi kumsikia mama akisema jinsi<br />

walivyokuwa wakitumia tapoli, “kifaa kidogo cha ubao kilichotumika kusaga<br />

pilipili”, kujaribu kuondoa uvimbe kwenye matiti wakati wa enzi zao.<br />

Kwa hiyo nilijaribu, kama mara tatu hivi. Lilikuwa ni jambo la kuchekesha,<br />

lakini hata hivyo haikusaidia kitu. Lakini sasa hivi waliokuwa wananitania<br />

wana matiti makubwa kuliko ya kwangu.”<br />

Kumbuka kuwa mambo haya yanaisha kadri muda unavyopita. Utakapofikisha miaka 20<br />

hakutakuwa na tofauti yoyote kwako au kwa mtu mwingine, iwapo sauti yako ilibadilika ukiwa na<br />

miaka 13 au miaka 17. Hakutakuwa na tofauti iwapo ulivunja ungo ukiwa na miaka 11 au miaka 16.<br />

Sherry, kutoka Ghana (umri; miaka 19)<br />

“Ebu tuyaache mambo yaende kama yalivyopangwa kwani hata kama<br />

hupendi huwezi kubadili kitu isipokuwa kujikubali tu.”<br />

Ingawa huwezi kuubadili mwili wako yapo mambo yanayokuhusu ambayo unaweza<br />

kuyabadili:<br />

1. Unaweza kuhakikisha kuwa wewe ni mtu mzuri. Hakikisha kuwa unafanya kazi kwa<br />

bidiii katika lolote utakalokuwa unafanya (shuleni, kazini na nyumbani). Unaweza<br />

ukakuza haiba yako, ucheshi wako,pia na tabia yako. Angalia kuwa wewe ni nani na<br />

unataka uweje baadaye na wala sio vile unavyoonekana.<br />

2. Jitahidi sana kutotilia maanani utani jaribu kupuuza na usiwaruhusu wanaokutania<br />

waone umefadhaika. Mwishowe watachoka kukutania.<br />

3. Heshima na kukubalika na rafiki zako visije vikakushawishi kufanya mambo ambayo<br />

sio mazuri kwako. Usiruhusu marafiki zako kukulazimisha kufanya mambo ambayo<br />

unajua sio sahihi, kama vile kutania watu wengine, kutumia madawa ya kulevya au<br />

kujiingiza kwenye mambo yanayoweza kukudhuru.<br />

4. Jielimishe mwenyewe kwa kutafuta taarifa sahihi. Hakihisha unafahamu wapi utapata<br />

taarifa unazozihitaji na majibu ya maswali yako yote wakati unapoupitia ujana<br />

11

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!