08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

30<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Rita kutoka uganda (umri, miaka 16)<br />

“Ninayapenda matiti yangu kwa sababu yananifanya nijisikie mwanamke<br />

haswa. Wasichana wakubwa ambao hawana matiti hutaniwa na<br />

kufananishwa na wanaume”<br />

Si vema watu kuwatania wasichana kuhusu matiti yao. Huu si ustaarabu. Msichana ajaribu kadri<br />

awezavyo kuwadharau na kutojali matusi yao.<br />

UNAJUA KUWA KUNA IMANI POTOFU NYINGI KUHUSU MATITI?<br />

Watu husema mambo mengi potofu kuhusu matiti, yafuatayo ni baadhi yake:<br />

1. Wasichana wenye matiti yaliyochongoka huvutia kingono. hii Si Kweli. Kuvutia kingono<br />

ipo kwenye akili ya anayejiona hivyo na si kwenye mwili wake.<br />

2. Kuweka jibini kwenye chuchu au kumfanya mdudu ang’ate chuchu hufanya matiti yakue<br />

haraka. hii si Kweli pia. Homoni ndizo zinazofanya matiti yakue. Hamna kitu chochote<br />

zaidi ya hicho kitakachobadilisha matiti.<br />

3. Wasichana wenye ngozi iliyo nyeusi kuzunguka chuchu zao wamewahi kufanya ngono.<br />

huu ni uongo! Kama ilivyo rangi ya ngozi yako, rangi ya mduara wa chuchu inatokana na<br />

tabia vinasaba ulivyorithi kutoka kwa wazazi wako.<br />

4. Matiti yanaweza kuwa makubwa kama wavulana watayashikashika. Si kweli! Ukubwa wa<br />

matiti unategemea tabia vinasaba ulizorithi kutoka kwa wazazi wako.<br />

5. Wasichana wenye matiti yaliyolala wameshawahi kufanya ngono au wameshawahi kutoa<br />

mimba. huu pia ni uongo! Matiti hulala/huanguka kutokana na uzito na maumbile. Kama<br />

una matiti makubwa uwezekano wa kulala au kuanguka kwa sababu ya uzito ni mkubwa<br />

zaidi.<br />

6. Kuvaa sidiria hufanya matiti kuanguka. uongo! Sidiria hushikilia matiti na huzuia ngozi na<br />

tishu za matiti kutanuka na kupunguza kunyumbuka.<br />

7. Wasichana wenye matiti makubwa watakuwa na maziwa mengi kwa ajili ya watoto wao.<br />

uongo! Uzalishwaji wa maziwa hautokani na ukubwa wa matiti; hata matiti madogo huzalisha<br />

maziwa yanayomtosheleza mtoto.<br />

naMna Ya KutunZa Matiti YaKO<br />

Matiti ni sehemu nyeti, kwa hiyo kuna vitu fulani ambavyo unatakiwa uvijue kuhusu utunzaji<br />

wake. Hata siku moja using’oe nywele zinazozunguka chuchu, zinaweza kusababisha madhara.<br />

Ni kawaida kuwa na vinyweleo hivyo. Kuna baadhi ya wasichana wanatokwa majimaji kwenye<br />

chuchu zao: hiki ni kitu cha kawaida. Lakini kama majimaji hayo yana damu au rangi ya kahawia<br />

unatakiwa kumwona daktari maana inaweza kuwa ni uambukizo.<br />

Kutunza matiti ni pamoja na kuhakikisha kuwa hakuna anayeyashika bila ridhaa yako. Mara nyingi<br />

wavulana na wanaume hugundua kwamba matiti ya wanawake yanavutia sana, lakini hata hivyo<br />

mtu hana ruhusa kuyashika labda upende mwenyewe.<br />

Matiti ya wanawake wengi ni rahisi sana kuhisi yanapoguswa.Kuguswa kunaweza kuleta ashiki ya<br />

kusisimua, na hii inaweza kusababisha utende usilotegemea au uponzeke.<br />

SiDiRia<br />

SURA YA 4 | WASICHANA<br />

Si lazima kuvaa sidiria kama una matiti madogo au yaliyosimama imara. Lakini kama matiti yako<br />

ni makubwa, unaweza ukajisikia vizuri kama ukivaa sidiria ambayo inasaidia matiti yasitikisike<br />

au kurukaruka unapotembea, kukimbia, kucheza dansi au kucheza michezo. Wasichana wengine<br />

waliobalehe wanafedheheka na matiti yao, hivyo kuvaa sidiria kunawafanya kutokuwa na<br />

wasiwasi na pia hupunguza kufedheheka/kujishuku.<br />

Ili kupata kipimo sahihi, wanawake wengi wanajaribisha namba mbalimbali za sidiria kuona ni ipi<br />

itamtosha vizuri. Unashauriwa kufanya hivyo.<br />

Wanawake wengine huwa wanachukuwa vipimo ili waweze kupata saizi ya sidiria. Ili uweze<br />

kupata vipimo vyako, unahitaji kujua saizi ya kifua chako pamoja na saizi ya titi.Pima kifua chako,<br />

chini kidogo ya matiti, ili upate saizi ya kifua. Kisha pima sehemu iliyojaa zaidi ya matiti ili kupata<br />

ukubwa wa titi, kama viko sawa unahitaji kikombe A. Kama kipimo cha matiti ni 2.5 Sm zaidi ya<br />

kifua unahitaji saizi ya titi B. Iwapo kipimo cha matiti ni 5 Sm zaidi ya kifua basi unahitaji saizi ya<br />

titi C.<br />

Via VYa uZaZi/SeheMu ZaKO Za SiRi<br />

Uke ndilo tundu pekee lililo kubwa kuliko matundu yote matatu katika eneo la via vya uzazi.<br />

Mashimo mengine ni tundu la mkojo (mbele ya uke) na mkundu (nyuma ya uke). Uke una kina cha<br />

sm 7 na upana wa sm 3 – 4. Ngozi yake ni laini iliyokunjamana.<br />

Uke wa mwanamke mtu mzima ni imara sana; hutanuka sana na una misuli imara. Wakati wa<br />

kuzaa mtoto uke unatanuka sana kuliko ukubwa wake wa kawaida ili kuruhusu mtoto kutoka<br />

tumboni mwa mama yake. Lakini uke wa msichana ni mwembamba na hauwezi kutanuka<br />

sana. Hii ni mojawapo ya sababu ya madhara<br />

yanayompata msichana aliyezaa angali mdogo.<br />

Uke wa msichana mdogo unaweza kuchanika<br />

au kupasuka wakati wa kuzaa. Hii husababisha<br />

matatizo makubwa sana. (Soma Sura ya 11).<br />

Katika kipindi cha balehe, kuta za uke zinaanza<br />

kutoa majimaji ukeni. Maji maji hayo ni mazito na<br />

yananata kuliko mate na yana kazi yake ambayo<br />

ni kuuweka uke safi, na kutengeneza mazingira<br />

mwafaka ambapo bakteria wazuri wanaozuia<br />

maambukizo ya magonjwa wanaweza kuishi.<br />

Wanawake wengi wanaanza kuona maji maji<br />

ukeni katika nyakati tofauti katika mzunguko<br />

wa mwezi na wakati wanapopata ashiki. Hii ni<br />

kawaida.<br />

Sehemu za siri za mwanamke kwa nje<br />

31

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!