Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
30<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Rita kutoka uganda (umri, miaka 16)<br />
“Ninayapenda matiti yangu kwa sababu yananifanya nijisikie mwanamke<br />
haswa. Wasichana wakubwa ambao hawana matiti hutaniwa na<br />
kufananishwa na wanaume”<br />
Si vema watu kuwatania wasichana kuhusu matiti yao. Huu si ustaarabu. Msichana ajaribu kadri<br />
awezavyo kuwadharau na kutojali matusi yao.<br />
UNAJUA KUWA KUNA IMANI POTOFU NYINGI KUHUSU MATITI?<br />
Watu husema mambo mengi potofu kuhusu matiti, yafuatayo ni baadhi yake:<br />
1. Wasichana wenye matiti yaliyochongoka huvutia kingono. hii Si Kweli. Kuvutia kingono<br />
ipo kwenye akili ya anayejiona hivyo na si kwenye mwili wake.<br />
2. Kuweka jibini kwenye chuchu au kumfanya mdudu ang’ate chuchu hufanya matiti yakue<br />
haraka. hii si Kweli pia. Homoni ndizo zinazofanya matiti yakue. Hamna kitu chochote<br />
zaidi ya hicho kitakachobadilisha matiti.<br />
3. Wasichana wenye ngozi iliyo nyeusi kuzunguka chuchu zao wamewahi kufanya ngono.<br />
huu ni uongo! Kama ilivyo rangi ya ngozi yako, rangi ya mduara wa chuchu inatokana na<br />
tabia vinasaba ulivyorithi kutoka kwa wazazi wako.<br />
4. Matiti yanaweza kuwa makubwa kama wavulana watayashikashika. Si kweli! Ukubwa wa<br />
matiti unategemea tabia vinasaba ulizorithi kutoka kwa wazazi wako.<br />
5. Wasichana wenye matiti yaliyolala wameshawahi kufanya ngono au wameshawahi kutoa<br />
mimba. huu pia ni uongo! Matiti hulala/huanguka kutokana na uzito na maumbile. Kama<br />
una matiti makubwa uwezekano wa kulala au kuanguka kwa sababu ya uzito ni mkubwa<br />
zaidi.<br />
6. Kuvaa sidiria hufanya matiti kuanguka. uongo! Sidiria hushikilia matiti na huzuia ngozi na<br />
tishu za matiti kutanuka na kupunguza kunyumbuka.<br />
7. Wasichana wenye matiti makubwa watakuwa na maziwa mengi kwa ajili ya watoto wao.<br />
uongo! Uzalishwaji wa maziwa hautokani na ukubwa wa matiti; hata matiti madogo huzalisha<br />
maziwa yanayomtosheleza mtoto.<br />
naMna Ya KutunZa Matiti YaKO<br />
Matiti ni sehemu nyeti, kwa hiyo kuna vitu fulani ambavyo unatakiwa uvijue kuhusu utunzaji<br />
wake. Hata siku moja using’oe nywele zinazozunguka chuchu, zinaweza kusababisha madhara.<br />
Ni kawaida kuwa na vinyweleo hivyo. Kuna baadhi ya wasichana wanatokwa majimaji kwenye<br />
chuchu zao: hiki ni kitu cha kawaida. Lakini kama majimaji hayo yana damu au rangi ya kahawia<br />
unatakiwa kumwona daktari maana inaweza kuwa ni uambukizo.<br />
Kutunza matiti ni pamoja na kuhakikisha kuwa hakuna anayeyashika bila ridhaa yako. Mara nyingi<br />
wavulana na wanaume hugundua kwamba matiti ya wanawake yanavutia sana, lakini hata hivyo<br />
mtu hana ruhusa kuyashika labda upende mwenyewe.<br />
Matiti ya wanawake wengi ni rahisi sana kuhisi yanapoguswa.Kuguswa kunaweza kuleta ashiki ya<br />
kusisimua, na hii inaweza kusababisha utende usilotegemea au uponzeke.<br />
SiDiRia<br />
SURA YA 4 | WASICHANA<br />
Si lazima kuvaa sidiria kama una matiti madogo au yaliyosimama imara. Lakini kama matiti yako<br />
ni makubwa, unaweza ukajisikia vizuri kama ukivaa sidiria ambayo inasaidia matiti yasitikisike<br />
au kurukaruka unapotembea, kukimbia, kucheza dansi au kucheza michezo. Wasichana wengine<br />
waliobalehe wanafedheheka na matiti yao, hivyo kuvaa sidiria kunawafanya kutokuwa na<br />
wasiwasi na pia hupunguza kufedheheka/kujishuku.<br />
Ili kupata kipimo sahihi, wanawake wengi wanajaribisha namba mbalimbali za sidiria kuona ni ipi<br />
itamtosha vizuri. Unashauriwa kufanya hivyo.<br />
Wanawake wengine huwa wanachukuwa vipimo ili waweze kupata saizi ya sidiria. Ili uweze<br />
kupata vipimo vyako, unahitaji kujua saizi ya kifua chako pamoja na saizi ya titi.Pima kifua chako,<br />
chini kidogo ya matiti, ili upate saizi ya kifua. Kisha pima sehemu iliyojaa zaidi ya matiti ili kupata<br />
ukubwa wa titi, kama viko sawa unahitaji kikombe A. Kama kipimo cha matiti ni 2.5 Sm zaidi ya<br />
kifua unahitaji saizi ya titi B. Iwapo kipimo cha matiti ni 5 Sm zaidi ya kifua basi unahitaji saizi ya<br />
titi C.<br />
Via VYa uZaZi/SeheMu ZaKO Za SiRi<br />
Uke ndilo tundu pekee lililo kubwa kuliko matundu yote matatu katika eneo la via vya uzazi.<br />
Mashimo mengine ni tundu la mkojo (mbele ya uke) na mkundu (nyuma ya uke). Uke una kina cha<br />
sm 7 na upana wa sm 3 – 4. Ngozi yake ni laini iliyokunjamana.<br />
Uke wa mwanamke mtu mzima ni imara sana; hutanuka sana na una misuli imara. Wakati wa<br />
kuzaa mtoto uke unatanuka sana kuliko ukubwa wake wa kawaida ili kuruhusu mtoto kutoka<br />
tumboni mwa mama yake. Lakini uke wa msichana ni mwembamba na hauwezi kutanuka<br />
sana. Hii ni mojawapo ya sababu ya madhara<br />
yanayompata msichana aliyezaa angali mdogo.<br />
Uke wa msichana mdogo unaweza kuchanika<br />
au kupasuka wakati wa kuzaa. Hii husababisha<br />
matatizo makubwa sana. (Soma Sura ya 11).<br />
Katika kipindi cha balehe, kuta za uke zinaanza<br />
kutoa majimaji ukeni. Maji maji hayo ni mazito na<br />
yananata kuliko mate na yana kazi yake ambayo<br />
ni kuuweka uke safi, na kutengeneza mazingira<br />
mwafaka ambapo bakteria wazuri wanaozuia<br />
maambukizo ya magonjwa wanaweza kuishi.<br />
Wanawake wengi wanaanza kuona maji maji<br />
ukeni katika nyakati tofauti katika mzunguko<br />
wa mwezi na wakati wanapopata ashiki. Hii ni<br />
kawaida.<br />
Sehemu za siri za mwanamke kwa nje<br />
31