08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

114<br />

•<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Unajua kuhusu magonjwa ya zinaa? (Inaendelea)<br />

Virusi vya “human Papilloma,” Vinundu sehemu za siri (genital warts)<br />

Virusi hivi husababisha sugu kuota kwenye via vya uzazi. Virusi hivi vilivyofunikwa<br />

vinaweza visionekane kwa urahisi, hususani kama vitatokea kwenye njia ya uzazi ya<br />

mwanamke. Kawaida vinajitokeza wiki 3 hadi wiki 9 baada ya maambukizo. Kipindi hiki<br />

kirefu vijidudu hukaa tuli mwilini kabla ya kusababisha ugonjwa. Inamaanisha kwamba<br />

inaweza ikawa vigumu kufahamu maambukizo yalikotokea na yanaweza kuenea kwa watu<br />

wengine bila kujua. Vinundu sugu vinaweza kutibiwa na maji ya tindikali na hairuhusiwi<br />

kujamiiana mpaka vinundu vyote vimepotea. Wenzi wote wanatakiwa kuchunguzwa ili<br />

kuona kama hawana vinundu sugu. Wanawake wenye maambukizo haya wako katika hatari<br />

kubwa ya kupata kansa ya kizazi.<br />

• VVu/ uKiMWi : Huu ni ugonjwa unaosababishwa na virusi. VVU vinapoingia mwilini<br />

hushambulia kinga ya mwili ambayo kwa kawaida inalinda mwili usipate maambukizo.<br />

Inaweza ikachukua miaka mingi kuona dalili za maambukizo, lakini baada ya muda mrefu<br />

mtu anashindwa kuzuia maambukizo na hata magonjwa yaliyozoeleka ambayo<br />

VVu/uKiMWi<br />

VVu (Virusi Vya uKiMWi) ni Virusi vinavyosababisha UKIMWI (upungufu wa Kinga Mwilini)<br />

UKIMWI ni ugonjwa ambao kinga ya mwili dhidi ya magonjwa inaharibiwa hatua kwa hatua.<br />

VVU vikiingia kwenye mwili wa mwanadamu vinashambulia kinga ya mwili ambayo kwa kawaida<br />

inalinda mwili usipate maambukizo. Watu wenye maambukizo ya VVU wanaitwa watu wanaoishi<br />

na VVU/ UKIMWI. Baada ya muda mrefu mtu aliyepata maambukizo anashindwa kuzuia<br />

maambukizo hata ya magonjwa yaliyozoeleka ambayo kwa vyovyote vile yasingefikia hali mbaya.<br />

Mwili unaposhindwa kujikinga na magonjwa tunasema mtu ana UKIMWI. hakuna chanjo ya<br />

maambukizo ya VVu, na hakuna tiba mara utakapokuwa umepata maambukizo hayo.<br />

Inachukua muda mrefu mpaka dalili za VVU kuonekana. Matokeo yake ni kwamba, mtu ambaye<br />

ana maambukizo ya VVU anaweza akawa na afya nzuri kwa miaka mingi na anaweza asijue<br />

kwamba anayo maambukizo. Katika kipindi hiki anaweza kueneza VVU bila yeye kujua.<br />

Muda ambao mtu anaanza kuona dalili za virusi unategemea na uwezo wa nguvu ya kinga ya mwili<br />

na uimara wa virusi. Yapo makundi mengi ya VVU. Makundi mengine humfanya mtu augue haraka<br />

kuliko mengine. Kwa wastani inachukua miaka 5 hadi 10 kabla dalili zozote za VVU hazijajitokeza.<br />

Kwa vile virusi vinashambulia kinga ya mwili na kumfanya mtu ashambuliwe kiurahisi na<br />

magonjwa, dalili zinatofautiana sana kutegemeana na ugonjwa gani mtu anaougua.<br />

Hata hivyo dalili za kawaida ni:-<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

Kuvimba tezi za limfu<br />

Kifua kikuu.<br />

Kupungua uzito sana na kuchoka .<br />

Kutoka jasho, hasa usiku.<br />

Homa za mara kwa mara<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

Kuharisha kwa mfululizo.<br />

Kichefuchefu na kutapika.<br />

Kikohozi kikavu cha mfululizo.<br />

Upele mwilini na vidonda mdomoni.<br />

Hakuna dawa inayotibu VVU/UKIMWI. Lakini zipo dawa zinazowasaidia watu waishio na VVU<br />

kwa miaka mingi bila kuumwa na zinazopunguza makali ya VVU/ UKIMWI. “Anti – retrovirals”<br />

(ARVs) ni dawa zinazopunguza kuendelea kwa virusi. “ARVs” zinawawezesha watu kuishi maisha<br />

ya afya nzuri. Dawa hizi haziuwi virusi moja kwa moja. Zaidi ya hapo dawa hizi ni ghali sana,<br />

ingawa zipo kampuni ambazo zimeanza kutengeneza dawa zenye gharama nafuu na zenye ubora<br />

uliosawa na dawa zilizo ghali. Hata hivyo, ni vigumu kununua dawa hizi ambazo ni nafuu katika<br />

nchi nyingi za Afrika. Matokeo yake ni kuwa watu wengi hawazipati. Dawa hizi sasa zimeanza<br />

kupatikana katika nchi nyingi za Kiafrika kwa bei nafuu.<br />

Kwa hiyo, kitu cha kwanza ni kuzuia VVU kuingia mwilini mwako.<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

UKWELI KUHUSU VVU<br />

Zipo aina mbili za VVU zinazojulikana kama VVU 1 na VVU 2. VVU 1 inapatikana zaidi, na VVU<br />

2 inapatikana zaidi Afrika ya Magharibi kuliko VVU 1. Vyote, VVU 1 na VVU 2 vinasababisha<br />

UKIMWI. Hata hivyo, kipindi cha kuanzia maambukizo mpaka kufikia UKIMWI ni kirefu<br />

zaidi kwa yule mwenye aina ya VVU 2 kuliko VVU 1. Sasa hivi hakuna kinga kwa aina zote za<br />

VVU wala hakuna dawa ya UKIMWI. Watu wengi wanaopata maambukizo ya VVU wanafikia<br />

UKIMWI baada ya kuishi na VVU kwa miaka 5 hadi miaka 10. Kipindi hiki cha muda ni cha<br />

wastani, inategemea na mambo kadhaa, kama:-<br />

•<br />

•<br />

•<br />

SURA YA 10 | KUTUNZA AfYA YAKO YA KIUJINSIA<br />

Aina ya VVU (VVU 1 au VVU 2).<br />

Upatikanaji wa dawa na kutibu dalili zinazojitokeza sana, na pia kujiweka wazi na<br />

magonjwa mengine.<br />

Msaada wa kisaikolojia anaopewa mgonjwa.<br />

Kumbuka kwamba maambukizo ya VVU/ UKIMWI huibuka kwa njia tofauti kutegemea na<br />

maelezo binafsi. Mtu akigundulika ana virusi vya UKIMWI haimaanishi atakufa tu. Wapo watu<br />

ambao walipata maambukizo miaka 20 iliyopita na hadi leo hawajafikia hatua ya UKIMWI.<br />

Matumaini yapo!<br />

Kamwe usidhani mtu anavyoonekana ni salama kwa sababu ya vile anavyoonekana.<br />

Subiri vya kutosha kabla ya kuanza ngono kwa sababu kujamiiana ndiyo njia kuu<br />

inayoambukiza VVU.<br />

Kama unafanya ngono, tumia kondomu kila maraKondomu inaweza kukukinga usipate VVU<br />

na magonjwa mengine ya ngono.<br />

Wakati wote pima VVU kabla ya kuanza uhusiano wa kijinsia na mtu mpya na hakikisha<br />

mwenzi wako naye anapima VVU.<br />

Usichangie nyembe, sindano, vifaa vya kutogea au visu vya kutahiria.<br />

115

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!