Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
114<br />
•<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Unajua kuhusu magonjwa ya zinaa? (Inaendelea)<br />
Virusi vya “human Papilloma,” Vinundu sehemu za siri (genital warts)<br />
Virusi hivi husababisha sugu kuota kwenye via vya uzazi. Virusi hivi vilivyofunikwa<br />
vinaweza visionekane kwa urahisi, hususani kama vitatokea kwenye njia ya uzazi ya<br />
mwanamke. Kawaida vinajitokeza wiki 3 hadi wiki 9 baada ya maambukizo. Kipindi hiki<br />
kirefu vijidudu hukaa tuli mwilini kabla ya kusababisha ugonjwa. Inamaanisha kwamba<br />
inaweza ikawa vigumu kufahamu maambukizo yalikotokea na yanaweza kuenea kwa watu<br />
wengine bila kujua. Vinundu sugu vinaweza kutibiwa na maji ya tindikali na hairuhusiwi<br />
kujamiiana mpaka vinundu vyote vimepotea. Wenzi wote wanatakiwa kuchunguzwa ili<br />
kuona kama hawana vinundu sugu. Wanawake wenye maambukizo haya wako katika hatari<br />
kubwa ya kupata kansa ya kizazi.<br />
• VVu/ uKiMWi : Huu ni ugonjwa unaosababishwa na virusi. VVU vinapoingia mwilini<br />
hushambulia kinga ya mwili ambayo kwa kawaida inalinda mwili usipate maambukizo.<br />
Inaweza ikachukua miaka mingi kuona dalili za maambukizo, lakini baada ya muda mrefu<br />
mtu anashindwa kuzuia maambukizo na hata magonjwa yaliyozoeleka ambayo<br />
VVu/uKiMWi<br />
VVu (Virusi Vya uKiMWi) ni Virusi vinavyosababisha UKIMWI (upungufu wa Kinga Mwilini)<br />
UKIMWI ni ugonjwa ambao kinga ya mwili dhidi ya magonjwa inaharibiwa hatua kwa hatua.<br />
VVU vikiingia kwenye mwili wa mwanadamu vinashambulia kinga ya mwili ambayo kwa kawaida<br />
inalinda mwili usipate maambukizo. Watu wenye maambukizo ya VVU wanaitwa watu wanaoishi<br />
na VVU/ UKIMWI. Baada ya muda mrefu mtu aliyepata maambukizo anashindwa kuzuia<br />
maambukizo hata ya magonjwa yaliyozoeleka ambayo kwa vyovyote vile yasingefikia hali mbaya.<br />
Mwili unaposhindwa kujikinga na magonjwa tunasema mtu ana UKIMWI. hakuna chanjo ya<br />
maambukizo ya VVu, na hakuna tiba mara utakapokuwa umepata maambukizo hayo.<br />
Inachukua muda mrefu mpaka dalili za VVU kuonekana. Matokeo yake ni kwamba, mtu ambaye<br />
ana maambukizo ya VVU anaweza akawa na afya nzuri kwa miaka mingi na anaweza asijue<br />
kwamba anayo maambukizo. Katika kipindi hiki anaweza kueneza VVU bila yeye kujua.<br />
Muda ambao mtu anaanza kuona dalili za virusi unategemea na uwezo wa nguvu ya kinga ya mwili<br />
na uimara wa virusi. Yapo makundi mengi ya VVU. Makundi mengine humfanya mtu augue haraka<br />
kuliko mengine. Kwa wastani inachukua miaka 5 hadi 10 kabla dalili zozote za VVU hazijajitokeza.<br />
Kwa vile virusi vinashambulia kinga ya mwili na kumfanya mtu ashambuliwe kiurahisi na<br />
magonjwa, dalili zinatofautiana sana kutegemeana na ugonjwa gani mtu anaougua.<br />
Hata hivyo dalili za kawaida ni:-<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Kuvimba tezi za limfu<br />
Kifua kikuu.<br />
Kupungua uzito sana na kuchoka .<br />
Kutoka jasho, hasa usiku.<br />
Homa za mara kwa mara<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Kuharisha kwa mfululizo.<br />
Kichefuchefu na kutapika.<br />
Kikohozi kikavu cha mfululizo.<br />
Upele mwilini na vidonda mdomoni.<br />
Hakuna dawa inayotibu VVU/UKIMWI. Lakini zipo dawa zinazowasaidia watu waishio na VVU<br />
kwa miaka mingi bila kuumwa na zinazopunguza makali ya VVU/ UKIMWI. “Anti – retrovirals”<br />
(ARVs) ni dawa zinazopunguza kuendelea kwa virusi. “ARVs” zinawawezesha watu kuishi maisha<br />
ya afya nzuri. Dawa hizi haziuwi virusi moja kwa moja. Zaidi ya hapo dawa hizi ni ghali sana,<br />
ingawa zipo kampuni ambazo zimeanza kutengeneza dawa zenye gharama nafuu na zenye ubora<br />
uliosawa na dawa zilizo ghali. Hata hivyo, ni vigumu kununua dawa hizi ambazo ni nafuu katika<br />
nchi nyingi za Afrika. Matokeo yake ni kuwa watu wengi hawazipati. Dawa hizi sasa zimeanza<br />
kupatikana katika nchi nyingi za Kiafrika kwa bei nafuu.<br />
Kwa hiyo, kitu cha kwanza ni kuzuia VVU kuingia mwilini mwako.<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
UKWELI KUHUSU VVU<br />
Zipo aina mbili za VVU zinazojulikana kama VVU 1 na VVU 2. VVU 1 inapatikana zaidi, na VVU<br />
2 inapatikana zaidi Afrika ya Magharibi kuliko VVU 1. Vyote, VVU 1 na VVU 2 vinasababisha<br />
UKIMWI. Hata hivyo, kipindi cha kuanzia maambukizo mpaka kufikia UKIMWI ni kirefu<br />
zaidi kwa yule mwenye aina ya VVU 2 kuliko VVU 1. Sasa hivi hakuna kinga kwa aina zote za<br />
VVU wala hakuna dawa ya UKIMWI. Watu wengi wanaopata maambukizo ya VVU wanafikia<br />
UKIMWI baada ya kuishi na VVU kwa miaka 5 hadi miaka 10. Kipindi hiki cha muda ni cha<br />
wastani, inategemea na mambo kadhaa, kama:-<br />
•<br />
•<br />
•<br />
SURA YA 10 | KUTUNZA AfYA YAKO YA KIUJINSIA<br />
Aina ya VVU (VVU 1 au VVU 2).<br />
Upatikanaji wa dawa na kutibu dalili zinazojitokeza sana, na pia kujiweka wazi na<br />
magonjwa mengine.<br />
Msaada wa kisaikolojia anaopewa mgonjwa.<br />
Kumbuka kwamba maambukizo ya VVU/ UKIMWI huibuka kwa njia tofauti kutegemea na<br />
maelezo binafsi. Mtu akigundulika ana virusi vya UKIMWI haimaanishi atakufa tu. Wapo watu<br />
ambao walipata maambukizo miaka 20 iliyopita na hadi leo hawajafikia hatua ya UKIMWI.<br />
Matumaini yapo!<br />
Kamwe usidhani mtu anavyoonekana ni salama kwa sababu ya vile anavyoonekana.<br />
Subiri vya kutosha kabla ya kuanza ngono kwa sababu kujamiiana ndiyo njia kuu<br />
inayoambukiza VVU.<br />
Kama unafanya ngono, tumia kondomu kila maraKondomu inaweza kukukinga usipate VVU<br />
na magonjwa mengine ya ngono.<br />
Wakati wote pima VVU kabla ya kuanza uhusiano wa kijinsia na mtu mpya na hakikisha<br />
mwenzi wako naye anapima VVU.<br />
Usichangie nyembe, sindano, vifaa vya kutogea au visu vya kutahiria.<br />
115