08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

120<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

Tibu magonjwa yote yanapojitokeza.<br />

Pumzika na fanya mazoezi mepesi.<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Jiunge na jumuia au vikundi vya kusaidia watu wanaoishi na VVU/UKIMWI.<br />

Fanya ngono salama ili usimwambukize mtu mwingine virusi au mwenyewe kujiongezea<br />

virusi vipya mwilini mwako.<br />

Kuishi chanya maana yake ni kuishi kwa kadiri ya upeo wako kila siku. Kuishi chanya ni kitu<br />

ambacho kila mtu anatakiwa kufanya hata kama hatuna maambukizo ya VVU.<br />

Vilevile ni muhimu kuwasaidia watu wengine waishi kwa matumaini na VVU. Usiwaite watu<br />

wenye VVU au UKIMWI “waathirika” kwa sababu siyo waathirika. Ni kama watu wengine, walio<br />

na vitu vingi vya kufanya. Wanaweza kufanya kazi na kuchangia maendeleo. Wanahitaji upendo<br />

na kusikilizwa kama watu wengine. Mara kwa mara wanahitaji msaada wa pekee kutoka kwa<br />

marafiki wa karibu. Inawapasa ndugu kuwa na mtazamo unaowajali / usiowabagua watu wenye<br />

VVU. Kamwe usiwatanie, kuwanyanyapaa au kuwasumbua katika jamii.<br />

Ulikuwa unafahamu kwamba:<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

nGOnO SalaMa / MaPenZi SalaMa<br />

UKWELI KUHUSU VVU/UKIMWI<br />

Watu milioni 42 duniani wanaishi na VVU kwa sasa. Kati ya hawa karibu robo wana umri<br />

wa miaka kati ya 15 na 24. Watoto na vijana chini ya miaka 18 wanawakilisha zaidi ya<br />

asilimia 10 ya wanaoishi na VVU*.<br />

Nchi zilizoko Kusini mwa Jangwa la Sahara zimeathirika sana na VVU/UKIMWI, na<br />

UKIMWI ndiyo ugonjwa unaosababisha vifo vingi. Kati ya watu wote wanaoishi na VVU,<br />

milioni 29.4 ni kutoka eneo hili na kulikuwa na maambukizo mapya ya watu milioni 3.5.<br />

Kwa ujumla, VVU vinaenea kwa njia ya kujamiiana. Asilimia 90 ya maambukizo Afrika<br />

yanatokana na kujamiiana.<br />

Duniani kote, wapo watoto milioni 14 ambao ni yatima kwa sababu ya UKIMWI na kati ya<br />

hawa milioni 12.1 wanaishi Kusini mwa Jangwa la Sahara.<br />

Ugonjwa huu wa mlipuko unapunguza matarajio ya muda wa kuishi katika Afrika.<br />

Mwishoni mwa miaka ya 1990, watu Afrika walitarajia kwa wastani kuishi miaka 59. Lakini<br />

kutokana na VVU/UKIMWI, matarajio ya muda wa kuishi kwa watu wa Afrika itashuka<br />

hadi miaka 45 tu kufikia mwaka 2010.<br />

Ngono salama maana yake ni kufanya mapenzi ambayo yanapunguza uwezekano wa wewe<br />

kupata magonjwa ya ngono, ikiwa ni pamoja na VVU au mimba. Ukitaka mapenzi salama kwa<br />

asilimia mia moja (100%) basi uchaguzi ulio bora zaidi ni kupiga punyeto na kuacha kabisa<br />

kujamiiana. Kama ukisoma sura ya 9 utafahamu kwamba punyeto ni salama kabisa, upo peke<br />

yako. Majimaji ya sehemu za siri ni yako mwenyewe. Huwezi kupata maambukizo kutoka kwa mtu<br />

yeyote na wala huwezi kujipa au kumpa mtu mwingine mimba.<br />

Kubusu au kumkumbatia mwenzi wako<br />

ni mapenzi salama. Mpaka sasa hivi<br />

haijathibitishwa kama VVU vinaenezwa kwa<br />

njia ya kubusu au kukumbatia. Hata hivyo, kama<br />

mmojawapo ana maambukizo ya VVU na ana<br />

vidonda mdomoni anaweza kumwambukiza<br />

mwenzake. Vilevile kuna uwezekano wa<br />

maambukizo kutokea iwapo mtagusana via vya<br />

uzazi na kupata majimaji ya ukeni au shahawa<br />

mikononi. Kama una mikato au michubuko<br />

mikononi unaweza kupata maambukizi ya VVU<br />

kama mtu mwingine ana maambukizi.<br />

Kujamiiana kati ya watu wawili ambao wote<br />

hawana maambukizo ya magonjwa ya zinaa au<br />

VVU ni mapenzi salama. Lakini, bila shaka bado<br />

patakuwa na hofu ya mimba.Watu wengi hufikiria<br />

kwamba kwasababu wamekuwa na uhusiano na<br />

mtu kwa muda mrefu, wanaamini kuwa hawana<br />

VVU na magonjwa mengine ya ngono. Lakini<br />

mmoja wao akipima ndipo ukweli unadhihirika.<br />

Watu unaowaamini na kuwapenda wanaweza<br />

kukuambukiza magonjwa ya zinaa. Wanaweza<br />

wakawa hawajui kuwa wamekuambukiza.<br />

andrew kutoka tanzania (umri wa miaka 17)<br />

“Ninajiamini mwenyewe; sina maambukizo ya magonjwa ya ngono<br />

kwa sababu sijawahi kujamiiana na mtu yeyote.”<br />

anthony kutoka Kenya (umri wa miaka 15)<br />

“Sababu nzuri kuliko zote ya kumfanya kijana acheleweshe kuanza<br />

ngono ni kwamba ana uhakika wa kutopata UKIMWI na magonjwa<br />

mengine ya ngono.”<br />

Milensu kutoka Zambia (umri wa miaka 13)<br />

“Kusema “HAPANA” sitaki kujamiiana ni njia mojawapo ya kujikinga<br />

na hatari ya kupata magonjwa na inakufanya udhibiti maisha yako.”<br />

Kondomu vilevile ikitumika vema hufanya tendo la ngono kuwa salama. Kwa kweli kondomu ni<br />

muhimu katika kukulinda wewe na mwenzi wako. Hata kama hujaanza kujamiiana, ni vema usome<br />

somo linalofuata kwani kuna siku utahitaji kuzifahamu kondomu.<br />

KOnDOMu<br />

SURA YA 10 | KUTUNZA AfYA YAKO YA KIUJINSIA<br />

Hujachelewa kuanza kutumia kondomu.<br />

Kondomu ni mfuko laini uliotengenezwa kwa mpira ambao unavalishwa kwenye uume kabla ya<br />

kuanza kujamiiana. Mwanaume anapofikia mshindo, anakojoa shahawa ambazo hunaswa kwenye<br />

chuchu ya kondomu. Kwa vile shahawa zinakusanyika kwenye kondomu ina maana majimaji ya<br />

mwanaume hayamwingii mwanamke na wala uume haugusi majimaji ya ukeni kwa sababu uume<br />

umefunikwa na kondomu.<br />

121

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!