Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
120<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Tibu magonjwa yote yanapojitokeza.<br />
Pumzika na fanya mazoezi mepesi.<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Jiunge na jumuia au vikundi vya kusaidia watu wanaoishi na VVU/UKIMWI.<br />
Fanya ngono salama ili usimwambukize mtu mwingine virusi au mwenyewe kujiongezea<br />
virusi vipya mwilini mwako.<br />
Kuishi chanya maana yake ni kuishi kwa kadiri ya upeo wako kila siku. Kuishi chanya ni kitu<br />
ambacho kila mtu anatakiwa kufanya hata kama hatuna maambukizo ya VVU.<br />
Vilevile ni muhimu kuwasaidia watu wengine waishi kwa matumaini na VVU. Usiwaite watu<br />
wenye VVU au UKIMWI “waathirika” kwa sababu siyo waathirika. Ni kama watu wengine, walio<br />
na vitu vingi vya kufanya. Wanaweza kufanya kazi na kuchangia maendeleo. Wanahitaji upendo<br />
na kusikilizwa kama watu wengine. Mara kwa mara wanahitaji msaada wa pekee kutoka kwa<br />
marafiki wa karibu. Inawapasa ndugu kuwa na mtazamo unaowajali / usiowabagua watu wenye<br />
VVU. Kamwe usiwatanie, kuwanyanyapaa au kuwasumbua katika jamii.<br />
Ulikuwa unafahamu kwamba:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
nGOnO SalaMa / MaPenZi SalaMa<br />
UKWELI KUHUSU VVU/UKIMWI<br />
Watu milioni 42 duniani wanaishi na VVU kwa sasa. Kati ya hawa karibu robo wana umri<br />
wa miaka kati ya 15 na 24. Watoto na vijana chini ya miaka 18 wanawakilisha zaidi ya<br />
asilimia 10 ya wanaoishi na VVU*.<br />
Nchi zilizoko Kusini mwa Jangwa la Sahara zimeathirika sana na VVU/UKIMWI, na<br />
UKIMWI ndiyo ugonjwa unaosababisha vifo vingi. Kati ya watu wote wanaoishi na VVU,<br />
milioni 29.4 ni kutoka eneo hili na kulikuwa na maambukizo mapya ya watu milioni 3.5.<br />
Kwa ujumla, VVU vinaenea kwa njia ya kujamiiana. Asilimia 90 ya maambukizo Afrika<br />
yanatokana na kujamiiana.<br />
Duniani kote, wapo watoto milioni 14 ambao ni yatima kwa sababu ya UKIMWI na kati ya<br />
hawa milioni 12.1 wanaishi Kusini mwa Jangwa la Sahara.<br />
Ugonjwa huu wa mlipuko unapunguza matarajio ya muda wa kuishi katika Afrika.<br />
Mwishoni mwa miaka ya 1990, watu Afrika walitarajia kwa wastani kuishi miaka 59. Lakini<br />
kutokana na VVU/UKIMWI, matarajio ya muda wa kuishi kwa watu wa Afrika itashuka<br />
hadi miaka 45 tu kufikia mwaka 2010.<br />
Ngono salama maana yake ni kufanya mapenzi ambayo yanapunguza uwezekano wa wewe<br />
kupata magonjwa ya ngono, ikiwa ni pamoja na VVU au mimba. Ukitaka mapenzi salama kwa<br />
asilimia mia moja (100%) basi uchaguzi ulio bora zaidi ni kupiga punyeto na kuacha kabisa<br />
kujamiiana. Kama ukisoma sura ya 9 utafahamu kwamba punyeto ni salama kabisa, upo peke<br />
yako. Majimaji ya sehemu za siri ni yako mwenyewe. Huwezi kupata maambukizo kutoka kwa mtu<br />
yeyote na wala huwezi kujipa au kumpa mtu mwingine mimba.<br />
Kubusu au kumkumbatia mwenzi wako<br />
ni mapenzi salama. Mpaka sasa hivi<br />
haijathibitishwa kama VVU vinaenezwa kwa<br />
njia ya kubusu au kukumbatia. Hata hivyo, kama<br />
mmojawapo ana maambukizo ya VVU na ana<br />
vidonda mdomoni anaweza kumwambukiza<br />
mwenzake. Vilevile kuna uwezekano wa<br />
maambukizo kutokea iwapo mtagusana via vya<br />
uzazi na kupata majimaji ya ukeni au shahawa<br />
mikononi. Kama una mikato au michubuko<br />
mikononi unaweza kupata maambukizi ya VVU<br />
kama mtu mwingine ana maambukizi.<br />
Kujamiiana kati ya watu wawili ambao wote<br />
hawana maambukizo ya magonjwa ya zinaa au<br />
VVU ni mapenzi salama. Lakini, bila shaka bado<br />
patakuwa na hofu ya mimba.Watu wengi hufikiria<br />
kwamba kwasababu wamekuwa na uhusiano na<br />
mtu kwa muda mrefu, wanaamini kuwa hawana<br />
VVU na magonjwa mengine ya ngono. Lakini<br />
mmoja wao akipima ndipo ukweli unadhihirika.<br />
Watu unaowaamini na kuwapenda wanaweza<br />
kukuambukiza magonjwa ya zinaa. Wanaweza<br />
wakawa hawajui kuwa wamekuambukiza.<br />
andrew kutoka tanzania (umri wa miaka 17)<br />
“Ninajiamini mwenyewe; sina maambukizo ya magonjwa ya ngono<br />
kwa sababu sijawahi kujamiiana na mtu yeyote.”<br />
anthony kutoka Kenya (umri wa miaka 15)<br />
“Sababu nzuri kuliko zote ya kumfanya kijana acheleweshe kuanza<br />
ngono ni kwamba ana uhakika wa kutopata UKIMWI na magonjwa<br />
mengine ya ngono.”<br />
Milensu kutoka Zambia (umri wa miaka 13)<br />
“Kusema “HAPANA” sitaki kujamiiana ni njia mojawapo ya kujikinga<br />
na hatari ya kupata magonjwa na inakufanya udhibiti maisha yako.”<br />
Kondomu vilevile ikitumika vema hufanya tendo la ngono kuwa salama. Kwa kweli kondomu ni<br />
muhimu katika kukulinda wewe na mwenzi wako. Hata kama hujaanza kujamiiana, ni vema usome<br />
somo linalofuata kwani kuna siku utahitaji kuzifahamu kondomu.<br />
KOnDOMu<br />
SURA YA 10 | KUTUNZA AfYA YAKO YA KIUJINSIA<br />
Hujachelewa kuanza kutumia kondomu.<br />
Kondomu ni mfuko laini uliotengenezwa kwa mpira ambao unavalishwa kwenye uume kabla ya<br />
kuanza kujamiiana. Mwanaume anapofikia mshindo, anakojoa shahawa ambazo hunaswa kwenye<br />
chuchu ya kondomu. Kwa vile shahawa zinakusanyika kwenye kondomu ina maana majimaji ya<br />
mwanaume hayamwingii mwanamke na wala uume haugusi majimaji ya ukeni kwa sababu uume<br />
umefunikwa na kondomu.<br />
121