Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
174<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Kwa mfano unaweza kupata fursa ya kuona jinsi utaratibu wa kazi za ofisini zinavyokuwa na<br />
utaweza kupata hisia nzuri kuhusu kazi wanazozifanya. Unaweza kujua kwamba kazi hiyo<br />
inakufaa au haikufai. Kwa vyovyote itakavyokuwa, uvumbuzi utakuwa muhimu. Kwa jinsi<br />
utakavyokuwa unaendelea utajifunza stadi mpya, utajenga mvuto mpya na utajiamini.<br />
Unapofikiria kuhusu aina ya kazi ambayo ungependa kufanya, vilevile fikiria kuhusu hatua<br />
utakazozichukua. Kwa mfano, fikiria kuhusu watu wenye sifa nzuri uliowachagua. Unafikiri<br />
walifanya nini hadi kufikia hapo walipo? Walihitaji aina gani ya elimu? Aina gani ya mafunzo kwa<br />
vitendo waliyapata?<br />
Njia bora ya kujua namna gani watu walivyofikia hapo walipo ni kuwauliza. Iwapo wapo watu<br />
ambao unawaheshimu na ambao mafanikio yao unayahusudu, waulize kama wanao muda<br />
wakuambie jinsi walivyofikia pale walipo. Kabla hamjakutana, andika orodha ya maswali ambayo<br />
ungependa kuwauliza, Kwa mfano; ni kitu gani kilisababisha kuchagua kazi wanayoifanya na ni<br />
aina gani ya elimu na mafunzo waliyapata. Wanapenda nini zaidi kuhusu kazi yao? Ni kitu gani<br />
hawakipendi?n.k.<br />
Watu wengi wanafurahi sana na kujisikia sifa wakati mtu mwingine anavutiwa na mafanikio yake<br />
na pale wanapoombwa ushauri. Kawaida watu watakuwa na shauku ya kukueleza habari zao na<br />
kukusaidia njia utakayochagua. Unahitaji ujasiri kumwendea mtu mzima ambaye humjui vizuri,<br />
lakini utashangaa wengi wao watakuwa wazuri na watakusaidia, wanaweza kukushauri jinsi ya<br />
kupanga kazi yako.<br />
KuWeKa MalenGO<br />
Ni vema kuweka malengo, mambo unayoyategemea kwa maisha ya baadaye. Vilevile, unahitaji<br />
kujiwekea malengo mahususi ambayo yanaweza kukamilishwa katika muda mfupi.<br />
Lengo ni kuwa na jambo unalotaka kulifanyia kazi. Kuna aina mbili za malengo. Malengo ya muda<br />
mfupi na mrefu. <strong>Ndoto</strong> zako ni malengo ya muda mrefu. Haya ni mambo unayoyawazia kutokea<br />
baadaye katika muda mrefu.Malengo ya muda mfupi ni mambo ya muda mfupi. Ni mambo<br />
yatakayotokea kesho, juma lijalo au mwaka kesho. Malengo ya muda mfupi ya baadhi ya vijana<br />
balehe ni haya yafuatayo:-<br />
Sofia kutoka uganda (umri wa miaka 14)<br />
“ Itakapofikia mwisho wa mwaka wa kwanza wa sekondari,<br />
ninataka kushika namba za juu, nusu ya darasa.”<br />
essie kutoka Ghana (umri wa miaka 15)<br />
“Nitakapofikia umri wa miaka 16 ninataka kujua jinsi ya kutumia<br />
kompyuta.”<br />
Francis kutoka Kenya (umri wa miaka 16)<br />
“Mwakani ninataka kupiga solo katika kwaya ya kanisa”.<br />
Miriam kutoka Zambia (umri wa miaka 16)<br />
“Ninataka kufanya vizuri katika mitihani yangu ili niandikishwe<br />
katika shule nitakayoichagua.”<br />
Patrick kutoka Zimbabwe (umri wa miaka 18)<br />
“Ninataka kujifunza jinsi ya kuzungumza mbele ya kadamnasi.”<br />
Una malengo gani? Ni mambo gani ambayo ungependa kuyafanya ifikapo mwisho wa mwaka<br />
huu? Je, mwisho wa mwaka ujao?<br />
Malengo yana manufaa sana. Unapokamilisha lengo<br />
unaweza kulifuta kwenye orodha. Inakupa hisia ya mafanikio<br />
na furaha ya kukamilisha jambo. Inakufanya ujisikie<br />
vizuri. Inakuonyesha kwamba unapofikiria kitu unaweza<br />
kufanikisha.<br />
Malengo yanatakiwa yawe halisi na ambayo yanawezekana<br />
kutekelezeka- mambo ambayo unaweza kufanikisha. Wakati<br />
mwingine watu huweka malengo ambayo si halisi, kama vile<br />
kuwa tajiri sana. Watu wengi hawawi matajiri na hata wale<br />
wanaokuwa matajiri pengine walikuwa na malengo halisi<br />
kama vile kuanza biashara zao. Waliendesha biashara kwa<br />
muda mrefu kiasi cha kufanikiwa sana.<br />
Wakati mwingine watu wanaweka malengo yasiyofaa,<br />
mathalani kuhusu mambo ya kufanya mapenzi. Vijana balehe<br />
wengine wanajiambia:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
“Likizo hii lazima nipoteze ubikira wangu.”<br />
“Lazima nijamiiane nikifikisha umri wa miaka 16”<br />
Nitajaribu kujamiiana na msichana mwingine zaidi ya rafiki yangu wa kike.”<br />
Malengo kama haya hayana manufaa. Ukiyafanikisha pengine hutajisikia vizuri. Hebu fikiria:<br />
Hivi kweli kujamiiana ndilo lengo lako? Je, umeweka lengo hili kwa sababu tu unapata shinikizo<br />
ili usiwapoteze marafiki? Je, unafikiri marafiki zako wote wanajamiiana, hivyo wewe unabaki<br />
nyuma? Hizi siyo sababu nzuri za kujiwekea malengo.<br />
Fikiria kile ambacho wewe mwenyewe unataka kufanikiwa na weka maanani mwongozo huu wa<br />
kuweka malengo:-<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
SURA YA 14 | KUTIMIZA NDOTO ZAKO<br />
Hakikisha malengo yako ni mazuri na yana manufaa.<br />
Hakikisha malengo ni halisi na yanatekelezeka.<br />
Hakikisha hayakuingizi katika hatari yoyote<br />
Hakikisha ni malengo yako wewe na siyo ya mtu mwingine.<br />
Ukifanikisha lengo utajisikia vizuri<br />
175