Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
iii<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO Utanguzi<br />
Shukurani za pekee kwa Bi Cordula Schuemer kwa utetezi kwa vijana na kuhakikisha kuwa vijana<br />
wanapata taarifa sahihi kuhusu masuala ya jinsia na afya ya uzazi.<br />
Kwa kuwa Kitabu hiki ni tafsiri ya kitabu “You, Your life, Your Dreams”, shirika la Ubora wa Afya<br />
kwa Familia Duniani (FCI) lingependa kuwashukuru wale wote waliohusika katika uchapishaji<br />
wa kitabu hiki kwa lugha ya kingereza.Hii inatia ndani udhamini wa shirika la Ford Foundation,<br />
European Commission, William and Flora Hewlette Foundation, John D.and Catherine T.<br />
MacArthur Foundation na Blanchette Hooker Rockefeller Charitable Fund.<br />
FCI ingependa pia kuwashukuru Adolescent Reproductive Health Education Project; CEDPA;<br />
FAWE, Hesperian Foundation na United Nations haswa UNICEF kwa matumizi ya picha zao. FCI<br />
inawapa shukrani Regina C. Faul-Doyle, Timothy Kiwala, Mashet Ndhlovu, ODIA na Philip Odida<br />
kwa michoro yao.<br />
Sehemu mbalimbali za kitabu “You, Your life, Your Dreams”, zilipata mchango kutoka kwa Eva<br />
Agutti, Grace Canada, Claire Mcminn, Edith Mukisa, Dr. Sarah Naikoba na Joy Oguttu. Maandishi,<br />
mifano na michoro ilichambuliwa na Dr. A. Ananie Arkutu, FRCOG, Ghana; Regina Goergen, GTZ,<br />
Tanzania; Muriithi Kinyua, <strong>Family</strong> Planning Private Sector, Kenya; Dr. Margaret Makumi,Ministry<br />
of Health, Kenya; Dr. Elizabeth Odera, Malezi Preparatory School, Kenya; Rehema Mwateba,<br />
Independent Consultant, Tanzania na Mary Waithaka, Nairobi Primary School, Kenya.<br />
Msaada katika kufanya majaribio ulitolewa na wawakilishi kutoka Ministry of Health Ghana;<br />
<strong>Family</strong> Planning Association of Kenya;Planned Parenthood Association of Ghana; Young<br />
Christian Women’s Association, Ghana. Shukrani pia kwa wawakilishi kutoka Kenya Association<br />
of Professional Counsellors; Kuleana Centre for Child Rights, Tanzania; Mathare Youth Sports<br />
Association, Kenya; Media Trust for Development, Zimbabwe; Naguru Teenage Health Centre,<br />
Uganda; The New Vision, Uganda na Trendsetters Newspaper, Zambia kwa kuwanukuu vijana<br />
balehe.<br />
FCI inawapa shukrani wafanyakazi wake wote kwa mchango wao mbalimbali katika kufanikisha<br />
uchapishaji wa kitabu ‘<strong>Wewe</strong>, <strong>Maisha</strong> <strong>Yako</strong>, <strong>Ndoto</strong> <strong>Zako</strong>’ kwa lugha ya kiingereza na Kiswahili.<br />
Kubalehe ni kipindi katika maisha ya wanadamu ambapo kijana anabadilika na kuwa mtu mzima.<br />
Kipindi hiki kina msisimko mkubwa, lakini pia ni kipindi chenye kuchanganya sana. Wakati wa<br />
kubalehe utaona mabadiliko mengi ya kimwili na kihisia, pia unaweza kuwa na maswali mengi<br />
kuhusu mwili wako na uhusiano wako na wengine.<br />
Kitabu hiki kimeandikwa kwa ajili ya vijana balehe, ambao wana umri kati ya miaka 14 na 19 ili<br />
kiwasaidie kukabiliana na changamoto nyingi zinazotokea wakati wa mabadiliko kutoka utoto<br />
kwenda utu uzima.Kitabu hiki kinatoa taarifa sahihi kuhusu mabadiliko yanayotokea katika<br />
kipindi cha balehe, pamoja na mambo mengine, kwa mfano: jinsi ya kuwa na afya njema ya kimwili<br />
na kihisia, kuepuka magonjwa yanayosababishwa na ngono zisizotakiwa, jinsi ya kupambana<br />
na misukumo ya kufanya ngono, na jinsi ya kujiepusha na matumizi mabaya ya vileo na dawa za<br />
kulevya. Pia, kitabu kinatoa ushauri kuhusu uhusiano mwema na wazazi, marafiki, wapenzi, jinsi<br />
ya kuweka malengo ya maisha, mbinu za kufaulu shuleni na maishani na jinsi ya kukabili vikwazo.<br />
Kitabu hiki kina taarifa nyingi lakini si lazima usome kurasa zote. Unaweza kuangalia katika<br />
sehemu inayoonyesha “Yaliyomo” na kuona mada zinazokupendeza zaidi. Ukizimaliza,<br />
unaweza kurudi tena kwenye “Yaliyomo” na kuchagua tena mada inayokuvutia. Pia, unaweza<br />
kufunuafunua tu kitabu na kuangalia sehemu zenye michoro, katuni na nukuu mbalimbali toka<br />
kwa vijana. Unaweza pia kuangalia sehemu maalumu zilizo na kichwa “je, Wafahamu”. Hizi<br />
zinatoa taarifa sahihi kuhusu mambo mbalimbali.<br />
Ingawa kitabu hiki kilikusudiwa zaidi kwa vijana ambao hawajaoa/kuolewa wenye umri wa miaka<br />
14 hadi 19, zipo pia sehemu za kitabu hiki zinazowafaa vijana wenye umri uliozidi na hata walio<br />
kwenye ndoa. Kisome kitabu hiki pamoja na marafiki zako, kaka na dada zako na wazazi wako.<br />
Ongea nao na jaribu kuona wao wanazichukuliaje mada zilizomo kwenye kitabu hiki.<br />
Furahia kitabu hiki na uwe salama!<br />
Molly Anyango<br />
Mshauri rika wa Vijana<br />
<strong>Family</strong> Planning Association of Kenya<br />
iv