08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

iii<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO Utanguzi<br />

Shukurani za pekee kwa Bi Cordula Schuemer kwa utetezi kwa vijana na kuhakikisha kuwa vijana<br />

wanapata taarifa sahihi kuhusu masuala ya jinsia na afya ya uzazi.<br />

Kwa kuwa Kitabu hiki ni tafsiri ya kitabu “You, Your life, Your Dreams”, shirika la Ubora wa Afya<br />

kwa Familia Duniani (FCI) lingependa kuwashukuru wale wote waliohusika katika uchapishaji<br />

wa kitabu hiki kwa lugha ya kingereza.Hii inatia ndani udhamini wa shirika la Ford Foundation,<br />

European Commission, William and Flora Hewlette Foundation, John D.and Catherine T.<br />

MacArthur Foundation na Blanchette Hooker Rockefeller Charitable Fund.<br />

FCI ingependa pia kuwashukuru Adolescent Reproductive Health Education Project; CEDPA;<br />

FAWE, Hesperian Foundation na United Nations haswa UNICEF kwa matumizi ya picha zao. FCI<br />

inawapa shukrani Regina C. Faul-Doyle, Timothy Kiwala, Mashet Ndhlovu, ODIA na Philip Odida<br />

kwa michoro yao.<br />

Sehemu mbalimbali za kitabu “You, Your life, Your Dreams”, zilipata mchango kutoka kwa Eva<br />

Agutti, Grace Canada, Claire Mcminn, Edith Mukisa, Dr. Sarah Naikoba na Joy Oguttu. Maandishi,<br />

mifano na michoro ilichambuliwa na Dr. A. Ananie Arkutu, FRCOG, Ghana; Regina Goergen, GTZ,<br />

Tanzania; Muriithi Kinyua, <strong>Family</strong> Planning Private Sector, Kenya; Dr. Margaret Makumi,Ministry<br />

of Health, Kenya; Dr. Elizabeth Odera, Malezi Preparatory School, Kenya; Rehema Mwateba,<br />

Independent Consultant, Tanzania na Mary Waithaka, Nairobi Primary School, Kenya.<br />

Msaada katika kufanya majaribio ulitolewa na wawakilishi kutoka Ministry of Health Ghana;<br />

<strong>Family</strong> Planning Association of Kenya;Planned Parenthood Association of Ghana; Young<br />

Christian Women’s Association, Ghana. Shukrani pia kwa wawakilishi kutoka Kenya Association<br />

of Professional Counsellors; Kuleana Centre for Child Rights, Tanzania; Mathare Youth Sports<br />

Association, Kenya; Media Trust for Development, Zimbabwe; Naguru Teenage Health Centre,<br />

Uganda; The New Vision, Uganda na Trendsetters Newspaper, Zambia kwa kuwanukuu vijana<br />

balehe.<br />

FCI inawapa shukrani wafanyakazi wake wote kwa mchango wao mbalimbali katika kufanikisha<br />

uchapishaji wa kitabu ‘<strong>Wewe</strong>, <strong>Maisha</strong> <strong>Yako</strong>, <strong>Ndoto</strong> <strong>Zako</strong>’ kwa lugha ya kiingereza na Kiswahili.<br />

Kubalehe ni kipindi katika maisha ya wanadamu ambapo kijana anabadilika na kuwa mtu mzima.<br />

Kipindi hiki kina msisimko mkubwa, lakini pia ni kipindi chenye kuchanganya sana. Wakati wa<br />

kubalehe utaona mabadiliko mengi ya kimwili na kihisia, pia unaweza kuwa na maswali mengi<br />

kuhusu mwili wako na uhusiano wako na wengine.<br />

Kitabu hiki kimeandikwa kwa ajili ya vijana balehe, ambao wana umri kati ya miaka 14 na 19 ili<br />

kiwasaidie kukabiliana na changamoto nyingi zinazotokea wakati wa mabadiliko kutoka utoto<br />

kwenda utu uzima.Kitabu hiki kinatoa taarifa sahihi kuhusu mabadiliko yanayotokea katika<br />

kipindi cha balehe, pamoja na mambo mengine, kwa mfano: jinsi ya kuwa na afya njema ya kimwili<br />

na kihisia, kuepuka magonjwa yanayosababishwa na ngono zisizotakiwa, jinsi ya kupambana<br />

na misukumo ya kufanya ngono, na jinsi ya kujiepusha na matumizi mabaya ya vileo na dawa za<br />

kulevya. Pia, kitabu kinatoa ushauri kuhusu uhusiano mwema na wazazi, marafiki, wapenzi, jinsi<br />

ya kuweka malengo ya maisha, mbinu za kufaulu shuleni na maishani na jinsi ya kukabili vikwazo.<br />

Kitabu hiki kina taarifa nyingi lakini si lazima usome kurasa zote. Unaweza kuangalia katika<br />

sehemu inayoonyesha “Yaliyomo” na kuona mada zinazokupendeza zaidi. Ukizimaliza,<br />

unaweza kurudi tena kwenye “Yaliyomo” na kuchagua tena mada inayokuvutia. Pia, unaweza<br />

kufunuafunua tu kitabu na kuangalia sehemu zenye michoro, katuni na nukuu mbalimbali toka<br />

kwa vijana. Unaweza pia kuangalia sehemu maalumu zilizo na kichwa “je, Wafahamu”. Hizi<br />

zinatoa taarifa sahihi kuhusu mambo mbalimbali.<br />

Ingawa kitabu hiki kilikusudiwa zaidi kwa vijana ambao hawajaoa/kuolewa wenye umri wa miaka<br />

14 hadi 19, zipo pia sehemu za kitabu hiki zinazowafaa vijana wenye umri uliozidi na hata walio<br />

kwenye ndoa. Kisome kitabu hiki pamoja na marafiki zako, kaka na dada zako na wazazi wako.<br />

Ongea nao na jaribu kuona wao wanazichukuliaje mada zilizomo kwenye kitabu hiki.<br />

Furahia kitabu hiki na uwe salama!<br />

Molly Anyango<br />

Mshauri rika wa Vijana<br />

<strong>Family</strong> Planning Association of Kenya<br />

iv

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!