08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

20<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Tohara ni kitendo cha kuondoa ngozi iliyojikunja inayozunguka kichwa cha uume. Ngozi hii huitwa<br />

govi, hufunika kabisa kichwa cha uume lakini inaweza kuvutwa chini ya “mpini” (shafti).<br />

Kufuatana na mila na desturi za waafrika, pamoja na dini fulani fulani kama vile Waislamu na<br />

Wayahudi, watoto wanatahiriwa wakiwa na umri wa siku chache. Katika desturi nyingine za Afrika,<br />

wavulana wanatahiriwa wanapofikia balehe, utaratibu huu unachukuliwa kama utaratibu wa mpito<br />

kutoka utoto kwenda utu uzima.Zipo tamaduni nyingine Afrika ambazo mila haziruhusu kutahiri<br />

kabisa.<br />

Hakuna ubaya wowote wa kutahiri au kutokutahiriwa. Kutahiriwa ni utaratibu wa kidini au<br />

kiutamaduni/kimila. Iwapo katika jamii yenu hawatahiri ni sawa sawa tu.<br />

Je, kutahiri kunaleta tofauti zozote katika hisia ya kujamiiana? Ni vigumu sana kujua jambo<br />

hili kwani kila mwanaume anayo namna yake ya kujisikia. Lililo la uhakika ni kwamba wote,<br />

aliyetahiriwa na asiyetahiriwa wanaweza kufurahia ngono na wanaweza kuwafurahisha wapenzi<br />

wao.<br />

Wakati kutahiri ni utaratibu wa kidini au kimila/ kiutamaduni, watu wengine wanaamini kwamba<br />

kuna faida za kiafya iwapo mwanaume ametahiriwa kwa sababu ni rahisi kusafisha uume wake.<br />

Lakini zipo sababu zingine za kiafya zinazoweza kusababisha watu kutahiriwa. Wapo wavulana na<br />

wanaume wengine ambao govi linakuwa limeshikana sana na kichwa cha uume kiasi cha kwamba<br />

inawia vigumu kuivuta kwa chini. Hii inaweza kusababisha kuvimba kwa uume na maumivu<br />

makali. Namna pekee ya kutatua tatizo hili ni kutahiri.Watu wengine wanafikiri kwamba kutahiri<br />

kunasaidia kuzuia maambukizi ya VVU/UKIMWI na magonjwa mengine ya ngono. Ukweli ni<br />

kwamba, hata kama umetahiriwa unaweza kupata maambukizi ya VVU/UKIMWI na magonjwa ya<br />

ngono. Unashauriwa kufanya mapenzi salama wakati wote.<br />

Mambo yote haya yana maana gani kwako? Kama utamaduni wako hauruhusu wavulana kutahiriwa,<br />

Je, ungependa utahiriwe ili iwe rahisi kuuweka uume wako msafi? Jibu ni hapana unachotakiwa ni<br />

kuwa msafi, kumbuka kusafisha kwa ungalifu chini ya govi. Kwa kawaida haya ndiyo unayotakiwa<br />

kuyafanya. Hata hivyo wavulana ambao hawawezi kuviringisha govi na wale ambao husikia<br />

maumivu uume unapodinda, wanashauriwa kumweleza mfanyakazi wa afya kwa ushauri zaidi.<br />

Sasa hivi watu wengi wanatahiriwa katika vituo vya afya. Lakini sehemu nyingine wanatahiri<br />

wataalamu wa kienyeji (mangariba) kama sehemu ya sherehe. Wakati wowote inapotokea hivyo,<br />

inatakiwa vitumike vyombo visafi, vilivyochemshwa, ili kuua vijidudu kila baada ya kumtahiri<br />

mtu mmoja. Ni hatari sana kutumia kisu kimoja kutahiria wavulana wengi kwa sababu kama<br />

mmojawapo atakuwa na maambuziki ya VVU, kisu kinaweza kueneza maambukizi kwa wavulana<br />

wengine.<br />

Iwapo utatahiriwa kimila, hakikisha utaratibu wa kisasa unatumika ili kuzuia maambukizi ya VVU<br />

na magonjwa mengine yanayotokana na damu. Usikubaliane kabisa na mila/desturi na utamaduni<br />

utakaosababisha maambukizi ya VVU. Taratibu hizo zinaweza kubadilishwa ukawa salama.<br />

Kwa mfano, watu wa Mbale, Uganda walichukua hatua zifuatazo ili kuhakikisha wanatahiri<br />

kiusalama:<br />

• Kila aliyetaka kutahiriwa alilazimishwa kuja na kisu chake.<br />

• Lazima kisu kichemshwa kabla ya kutumika.<br />

• Lazima Mangariba waoshe mikono yao kwa uangalifu kabla na baada ya kumtahiri kila mtu.<br />

MaZOeZi Ya uSaFi<br />

SURA YA 3 | WAvULANA<br />

JE UNAFAHAMU KUHUSU TOHARA? Je, ulikuwa unajua kwamba kuna uzushi mwingi kuhusu uume?<br />

Yafuatayo ni maelezo mbalimbali ya uzushi kuhusu uume:<br />

1. Iwapo huufanyii mazoezi uume kwa kujamiiana, uume wako hautafanya kazi na utakuwa<br />

mdogo. huu ni uongo! Kujamiana sio “mazoezi” ya uume. Uume hauhitaji mazoezi yoyote.<br />

Utafanya kazi vizuri bila hata ya kujamiiana.Kutojamiiana au subira kamwe haviwezi<br />

kuudhuru uume wako.<br />

2. Uume unaongezeka ukubwa kila unapofanya ngono mara nyingi. Sio kweli! Ukubwa wa<br />

uume wako utategemea sifa urizorithi kutoka kwa wazazi wako, na wala sio unachofanya<br />

na uume wako.<br />

3. Uume mdogo hauwezi kumridhisha mwanamke. Sio kweli! Ukubwa wa uume unaathari<br />

ndogo sana kwa mwanamke kufurahia ngono. Hii ni kwa sababu hisia za kutaka kujamiiana<br />

kwa mwanamke zipo kwenye kinembe na eneo linalozunguka uke.Uke wenyewe hauna<br />

mishipa mingi ya fahamu kwa hiyo haujisikii sana<br />

4. Wavulana wenye uume mdogo hawawezi kutumia kondomu. Sio kweli! kondomu<br />

zimetengenezwa kwa jinsi ya kubana, hivyo kila mtu anaweza kuzitumia vema.<br />

5. Lazima ujamiiane kila uume unapodinda. Si kweli! Kwa vyovyote vile hii sio kweli kabisa.<br />

Kwa mfano utafanya nini kama uume wako ungedinda darasani? Uume utalegea wenyewe.<br />

Kamwe huwezi kudhurika kwa kutokufanya ngono uume unapokuwa umedinda.<br />

6. Wavulana wenye dole gumba kubwa wana uume mkubwa. Sio kweli! Watu wengi husema<br />

mambo kama haya ikiwa ni pamoja na wavulana wenye pua kubwa, miguu mikubwa,<br />

masikio n.k, lakini sio kweli. Hakuna mahusiano yoyote kati ya ukubwa wa uume na viungo<br />

vingine vyovyote vya mwili wako. Hakuna jinsi unavyoweza kufahamu ukubwa wa uume<br />

kwa kumwangalia tu.<br />

7. Mbegu za kiume zikizidi zinasababisha mgongo kuuma, kichaa, kichwa kuuma, kuwa<br />

hanithi na kuota chunusi. Sio kweli! Hata kama korodani zinatengeneza mamilioni ya<br />

mbegu za kiume, haiwezekani mbegu hizo kujazana na kusababisha matatizo. Zaidi ya<br />

hapo mbegu za kiume haziwezi kwenda sehemu nyingine ya mwili.<br />

8. <strong>Ndoto</strong> nyevu ni dalili ya kwamba unahitaji kujamiiana. Sio kweli! <strong>Ndoto</strong> nyevu ni njia<br />

mojawapo ya mwili kupunguza mbegu za kiume na shahawa. Sio dalili ya kwamba unahitaji<br />

kujamiiana. Mwili wako unaweza kujirekebisha wenyewe bila ya wewe kujihatarisha kwa<br />

vyovyote vile.<br />

Ni muhimu kuosha na kusafisha uume wako kila siku, uwe umetahiri au la. Hii ni lazima iwe<br />

desturi kama unavyofanya kwa sehemu nyingine za mwili wako. Unatakiwa vile vile kuosha<br />

mapumbu, katikati ya mapumbu na mapaja na katikati ya matako.<br />

Kama hujatahiriwa, unatakiwa kurudisha nyuma govi na kusafisha eneo hilo kwa utaratibu.<br />

Unaweza kuhisi viuvimbe vidogo mwanzoni mwa kichwa cha uume viuvimbe hivyo ni matezi<br />

yanayotoa majimaji meupe yanayoitwa smegma. Smegma inasaidia govi kuteleza nyuma<br />

kiulaini. Hata hivyo, iwapo Smegma itajaa chini ya govi inaweza kusababisha harufu mbaya au<br />

maambukizi. Ni muhimu wakati wote eneo la chini ya govi liwe ni safi .<br />

21

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!