Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
20<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Tohara ni kitendo cha kuondoa ngozi iliyojikunja inayozunguka kichwa cha uume. Ngozi hii huitwa<br />
govi, hufunika kabisa kichwa cha uume lakini inaweza kuvutwa chini ya “mpini” (shafti).<br />
Kufuatana na mila na desturi za waafrika, pamoja na dini fulani fulani kama vile Waislamu na<br />
Wayahudi, watoto wanatahiriwa wakiwa na umri wa siku chache. Katika desturi nyingine za Afrika,<br />
wavulana wanatahiriwa wanapofikia balehe, utaratibu huu unachukuliwa kama utaratibu wa mpito<br />
kutoka utoto kwenda utu uzima.Zipo tamaduni nyingine Afrika ambazo mila haziruhusu kutahiri<br />
kabisa.<br />
Hakuna ubaya wowote wa kutahiri au kutokutahiriwa. Kutahiriwa ni utaratibu wa kidini au<br />
kiutamaduni/kimila. Iwapo katika jamii yenu hawatahiri ni sawa sawa tu.<br />
Je, kutahiri kunaleta tofauti zozote katika hisia ya kujamiiana? Ni vigumu sana kujua jambo<br />
hili kwani kila mwanaume anayo namna yake ya kujisikia. Lililo la uhakika ni kwamba wote,<br />
aliyetahiriwa na asiyetahiriwa wanaweza kufurahia ngono na wanaweza kuwafurahisha wapenzi<br />
wao.<br />
Wakati kutahiri ni utaratibu wa kidini au kimila/ kiutamaduni, watu wengine wanaamini kwamba<br />
kuna faida za kiafya iwapo mwanaume ametahiriwa kwa sababu ni rahisi kusafisha uume wake.<br />
Lakini zipo sababu zingine za kiafya zinazoweza kusababisha watu kutahiriwa. Wapo wavulana na<br />
wanaume wengine ambao govi linakuwa limeshikana sana na kichwa cha uume kiasi cha kwamba<br />
inawia vigumu kuivuta kwa chini. Hii inaweza kusababisha kuvimba kwa uume na maumivu<br />
makali. Namna pekee ya kutatua tatizo hili ni kutahiri.Watu wengine wanafikiri kwamba kutahiri<br />
kunasaidia kuzuia maambukizi ya VVU/UKIMWI na magonjwa mengine ya ngono. Ukweli ni<br />
kwamba, hata kama umetahiriwa unaweza kupata maambukizi ya VVU/UKIMWI na magonjwa ya<br />
ngono. Unashauriwa kufanya mapenzi salama wakati wote.<br />
Mambo yote haya yana maana gani kwako? Kama utamaduni wako hauruhusu wavulana kutahiriwa,<br />
Je, ungependa utahiriwe ili iwe rahisi kuuweka uume wako msafi? Jibu ni hapana unachotakiwa ni<br />
kuwa msafi, kumbuka kusafisha kwa ungalifu chini ya govi. Kwa kawaida haya ndiyo unayotakiwa<br />
kuyafanya. Hata hivyo wavulana ambao hawawezi kuviringisha govi na wale ambao husikia<br />
maumivu uume unapodinda, wanashauriwa kumweleza mfanyakazi wa afya kwa ushauri zaidi.<br />
Sasa hivi watu wengi wanatahiriwa katika vituo vya afya. Lakini sehemu nyingine wanatahiri<br />
wataalamu wa kienyeji (mangariba) kama sehemu ya sherehe. Wakati wowote inapotokea hivyo,<br />
inatakiwa vitumike vyombo visafi, vilivyochemshwa, ili kuua vijidudu kila baada ya kumtahiri<br />
mtu mmoja. Ni hatari sana kutumia kisu kimoja kutahiria wavulana wengi kwa sababu kama<br />
mmojawapo atakuwa na maambuziki ya VVU, kisu kinaweza kueneza maambukizi kwa wavulana<br />
wengine.<br />
Iwapo utatahiriwa kimila, hakikisha utaratibu wa kisasa unatumika ili kuzuia maambukizi ya VVU<br />
na magonjwa mengine yanayotokana na damu. Usikubaliane kabisa na mila/desturi na utamaduni<br />
utakaosababisha maambukizi ya VVU. Taratibu hizo zinaweza kubadilishwa ukawa salama.<br />
Kwa mfano, watu wa Mbale, Uganda walichukua hatua zifuatazo ili kuhakikisha wanatahiri<br />
kiusalama:<br />
• Kila aliyetaka kutahiriwa alilazimishwa kuja na kisu chake.<br />
• Lazima kisu kichemshwa kabla ya kutumika.<br />
• Lazima Mangariba waoshe mikono yao kwa uangalifu kabla na baada ya kumtahiri kila mtu.<br />
MaZOeZi Ya uSaFi<br />
SURA YA 3 | WAvULANA<br />
JE UNAFAHAMU KUHUSU TOHARA? Je, ulikuwa unajua kwamba kuna uzushi mwingi kuhusu uume?<br />
Yafuatayo ni maelezo mbalimbali ya uzushi kuhusu uume:<br />
1. Iwapo huufanyii mazoezi uume kwa kujamiiana, uume wako hautafanya kazi na utakuwa<br />
mdogo. huu ni uongo! Kujamiana sio “mazoezi” ya uume. Uume hauhitaji mazoezi yoyote.<br />
Utafanya kazi vizuri bila hata ya kujamiiana.Kutojamiiana au subira kamwe haviwezi<br />
kuudhuru uume wako.<br />
2. Uume unaongezeka ukubwa kila unapofanya ngono mara nyingi. Sio kweli! Ukubwa wa<br />
uume wako utategemea sifa urizorithi kutoka kwa wazazi wako, na wala sio unachofanya<br />
na uume wako.<br />
3. Uume mdogo hauwezi kumridhisha mwanamke. Sio kweli! Ukubwa wa uume unaathari<br />
ndogo sana kwa mwanamke kufurahia ngono. Hii ni kwa sababu hisia za kutaka kujamiiana<br />
kwa mwanamke zipo kwenye kinembe na eneo linalozunguka uke.Uke wenyewe hauna<br />
mishipa mingi ya fahamu kwa hiyo haujisikii sana<br />
4. Wavulana wenye uume mdogo hawawezi kutumia kondomu. Sio kweli! kondomu<br />
zimetengenezwa kwa jinsi ya kubana, hivyo kila mtu anaweza kuzitumia vema.<br />
5. Lazima ujamiiane kila uume unapodinda. Si kweli! Kwa vyovyote vile hii sio kweli kabisa.<br />
Kwa mfano utafanya nini kama uume wako ungedinda darasani? Uume utalegea wenyewe.<br />
Kamwe huwezi kudhurika kwa kutokufanya ngono uume unapokuwa umedinda.<br />
6. Wavulana wenye dole gumba kubwa wana uume mkubwa. Sio kweli! Watu wengi husema<br />
mambo kama haya ikiwa ni pamoja na wavulana wenye pua kubwa, miguu mikubwa,<br />
masikio n.k, lakini sio kweli. Hakuna mahusiano yoyote kati ya ukubwa wa uume na viungo<br />
vingine vyovyote vya mwili wako. Hakuna jinsi unavyoweza kufahamu ukubwa wa uume<br />
kwa kumwangalia tu.<br />
7. Mbegu za kiume zikizidi zinasababisha mgongo kuuma, kichaa, kichwa kuuma, kuwa<br />
hanithi na kuota chunusi. Sio kweli! Hata kama korodani zinatengeneza mamilioni ya<br />
mbegu za kiume, haiwezekani mbegu hizo kujazana na kusababisha matatizo. Zaidi ya<br />
hapo mbegu za kiume haziwezi kwenda sehemu nyingine ya mwili.<br />
8. <strong>Ndoto</strong> nyevu ni dalili ya kwamba unahitaji kujamiiana. Sio kweli! <strong>Ndoto</strong> nyevu ni njia<br />
mojawapo ya mwili kupunguza mbegu za kiume na shahawa. Sio dalili ya kwamba unahitaji<br />
kujamiiana. Mwili wako unaweza kujirekebisha wenyewe bila ya wewe kujihatarisha kwa<br />
vyovyote vile.<br />
Ni muhimu kuosha na kusafisha uume wako kila siku, uwe umetahiri au la. Hii ni lazima iwe<br />
desturi kama unavyofanya kwa sehemu nyingine za mwili wako. Unatakiwa vile vile kuosha<br />
mapumbu, katikati ya mapumbu na mapaja na katikati ya matako.<br />
Kama hujatahiriwa, unatakiwa kurudisha nyuma govi na kusafisha eneo hilo kwa utaratibu.<br />
Unaweza kuhisi viuvimbe vidogo mwanzoni mwa kichwa cha uume viuvimbe hivyo ni matezi<br />
yanayotoa majimaji meupe yanayoitwa smegma. Smegma inasaidia govi kuteleza nyuma<br />
kiulaini. Hata hivyo, iwapo Smegma itajaa chini ya govi inaweza kusababisha harufu mbaya au<br />
maambukizi. Ni muhimu wakati wote eneo la chini ya govi liwe ni safi .<br />
21