08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

124<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Anaweza kumfanya mwanamke ajisikie vibaya kwa kumuuliza ni kwa nini hamwamini. Lakini<br />

ikumbukwe kuwa yeyote anaweza kuwa na maambukizo ya magonjwa ya ngono ikiwa ni pamoja<br />

na VVU kutokana na uhusiano uliotangulia hata bila ya kuona dalili zozote. Kwa hiyo, ni kwa faida<br />

ya wote kutumia kondomu.<br />

Kondomu inatoa kinga kwa wale watakaohusika. Kuitumia kondomu ni alama ya kuaminiana,<br />

kuheshimiana na kujaliana.<br />

MatatiZO MenGine Ya aFYa Ya uZaZi<br />

je, unazifahamu kondomu za kike?<br />

Umewahi kusikia kuhusu kondomu za kike? Hii ni njia<br />

nyingine ya kujikinga dhidi ya VVU, magonjwa mengine<br />

ya ngono na mimba. Hiki ni kimfuko kilicholainishwa<br />

kama kondomu ya kawaida ya wanaume. Lakini, badala<br />

ya kufunika uume, inakinga uke kama kizuizi dhidi ya<br />

maambukizo.<br />

inavyofanya kazi: Kuna pete ndogo mbili; moja ni pete<br />

ndogo ndani ya kondomu na ya pili ipo upande uliowazi ambayo hukaa nje ya mwili. Pete hizi<br />

hushikilia kondomu ya kike ikae mahali pake. Kondomu ya kike, kama kondomu ya kiume<br />

inazuia mbegu za kiume kukutana moja kwa moja na uke. Kama uume unabakia ndani ya<br />

kondomu na pete ya nje inabakia mahali pake basi kondomu itafanya kazi.<br />

jinsi ya kutumia: Inaweza kuchukua muda ili kuweza kuivaa kondomu vizuri kama mazoezi<br />

yalivyo kwa kondomu za kiume. Lakini mwisho utazoea. Kwanza ikunje pete ya ndani iwe<br />

na alama ya nane (8). Kisha isukume ndani kiasi utachoweza mpaka utakapoona huwezi<br />

kuisukuma zaidi. Kondomu itakapokuwa imekaa sehemu yake, ongoza uume wa mwenzi<br />

wako ndani ya kondomu. Tumia kondomu ya kike moja kwa wakati mmoja. Usirudie kuitumia<br />

kondomu hiyo.<br />

jinsi ya kuitoa: Ni rahisi sana kuitoa. Sokota pete ya juu ili shahawa zisimwagike, halafu vuta<br />

kondomu nje na itupe ndani ya choo cha shimo au choma moto au fukia ndani ya shimo.<br />

Faida yake: Kondomu ya kike ni njia pekee ya kujikinga ambayo inadhibitiwa na mwanamke<br />

mwenyewe ili imlinde dhidi ya maambukizo ya magonjwa ya zinaa, VVU/ UKIMWI na mimba.<br />

Inakaa taratibu ndani ya uke na haibani uume unapoingia.<br />

Yapo matatizo ambayo yanatokea kwenye via vya uzazi lakini siyo magonjwa ya zinaa. Hata<br />

kama hujawahi kufanya ngono, yapo maambukizo ambayo unaweza kuyapata sehemu zako<br />

za siri. Unaweza ukapata maambukizo kwenye njia ya mkojo ambayo husababisha kuwashwa<br />

au maumivu unapokojoa mkojo. Ukiona uchafu wa ajabu unatoka au maumivu au damu wakati<br />

unapokojoa, unatakiwa kumwona mhudumu wa afya.<br />

KanDiDiaSiSi”<br />

Kama sehemu zako za siri zinawasha na unatokwa na uchafu wa ajabu ukeni unaweza ukawa na<br />

“kandidiasisi”. Hili ni tatizo la kawaida. Ugonjwa huu vilevile unaitwa maambukizo ya hamira na<br />

unasababishwa na kuvu wanaofanana na hamira wanaoitwa “kandida albicans”. Ugonjwa huu<br />

unawasumbua wasichana na wanawake wengi. Wavulana wanaweza kupata kandida chini ya govi.<br />

Kandida ni kiumbe kimojawapo ambacho kwa asili kinaishi juu ya mwili. Kwa kawaida kandida<br />

hakisababishi matatizo yoyote. Kinadhibitiwa na kinga ya mwili na bakteria wengine ambao<br />

kwa kawaida wanaishi ukeni. Lakini ikiwa kinga ya mwili imeshaharibiwa na haifanyi kazi vizuri,<br />

viumbe kandida huzaliana haraka . Mara kwa mara tatizo hili hutokea kabla au baada ya damu ya<br />

hedhi kutoka na wakati wa mimba.<br />

“Kandidiasisi” inaweza kuenea kwa njia ya kujamiiana na mtu ambaye ana kandida wengi. Lakini<br />

inaweza kusababishwa na mambo mengine vilevile. Mfadhaiko, kama vile mitihani, kifo ndani ya<br />

familia au mabishano yanaweza kuwa kichochezi cha “kandidiasisi”. Wakati mwingine unaweza<br />

kupata kandidiasisi ukinywa kiuavijasumu – Viuavijasumu vinaua bakteria ambao kwa kawaida<br />

wanaishi ukeni. Watu wanaoumwa kisukari na wale wenye VVU wanapata kandidiasisi mara kwa<br />

mara.<br />

“Kandidiasisi” si ugonjwa wa ngono kwa sababu hata bikira wanaupata. Joto linapozidi na<br />

unyevunyevu kuzunguka eneo la via vya uzazi vinaweza kusabisha kandidiasisi. Hii ina maana ya<br />

kwamba unaweza kujiletea mwenyewe “kandidiasisi” kwa kuvaa nguo zisizofaa. Kama, kwa mfano<br />

ukivaa nguo za nailoni, kaptura za kubana au suruali aina ya jeans zinazobana na kukaa kwa saa<br />

kadhaa huku umebananisha miguu, pengine kwenye basi, unatengeneza unyevuunyevu na joto<br />

ambalo kandida wanahitaji ili waishi.<br />

Dalili za kandidiasisi ni:-<br />

•<br />

•<br />

•<br />

SURA YA 10 | KUTUNZA AfYA YAKO YA KIUJINSIA<br />

Zungumza na mwenzi wako kuhusu matumizi ya Kondomu. eleza unavyojisikia na unachotaka.<br />

Kuwashwa kwenye via vya uzazi, wote; wasichana na wavulana.<br />

Usaha kutoka ukeni au chini ya govi unaofanana na maziwa yaliyoharibika.<br />

Kuvimba na kuwepo kwa utando telezi wa uke na midomo ya ndani au kichwa cha uume kuwa<br />

chekundu.<br />

Iwapo utapata mojawapo ya dalili hizi omba msaada kutoka kwa mhudumu wa afya mwenye ujuzi<br />

ambaye atakupatia matibatu yanayotakiwa. Matibabu yanayotakiwa kawaida ni:-<br />

125

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!