Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
124<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Anaweza kumfanya mwanamke ajisikie vibaya kwa kumuuliza ni kwa nini hamwamini. Lakini<br />
ikumbukwe kuwa yeyote anaweza kuwa na maambukizo ya magonjwa ya ngono ikiwa ni pamoja<br />
na VVU kutokana na uhusiano uliotangulia hata bila ya kuona dalili zozote. Kwa hiyo, ni kwa faida<br />
ya wote kutumia kondomu.<br />
Kondomu inatoa kinga kwa wale watakaohusika. Kuitumia kondomu ni alama ya kuaminiana,<br />
kuheshimiana na kujaliana.<br />
MatatiZO MenGine Ya aFYa Ya uZaZi<br />
je, unazifahamu kondomu za kike?<br />
Umewahi kusikia kuhusu kondomu za kike? Hii ni njia<br />
nyingine ya kujikinga dhidi ya VVU, magonjwa mengine<br />
ya ngono na mimba. Hiki ni kimfuko kilicholainishwa<br />
kama kondomu ya kawaida ya wanaume. Lakini, badala<br />
ya kufunika uume, inakinga uke kama kizuizi dhidi ya<br />
maambukizo.<br />
inavyofanya kazi: Kuna pete ndogo mbili; moja ni pete<br />
ndogo ndani ya kondomu na ya pili ipo upande uliowazi ambayo hukaa nje ya mwili. Pete hizi<br />
hushikilia kondomu ya kike ikae mahali pake. Kondomu ya kike, kama kondomu ya kiume<br />
inazuia mbegu za kiume kukutana moja kwa moja na uke. Kama uume unabakia ndani ya<br />
kondomu na pete ya nje inabakia mahali pake basi kondomu itafanya kazi.<br />
jinsi ya kutumia: Inaweza kuchukua muda ili kuweza kuivaa kondomu vizuri kama mazoezi<br />
yalivyo kwa kondomu za kiume. Lakini mwisho utazoea. Kwanza ikunje pete ya ndani iwe<br />
na alama ya nane (8). Kisha isukume ndani kiasi utachoweza mpaka utakapoona huwezi<br />
kuisukuma zaidi. Kondomu itakapokuwa imekaa sehemu yake, ongoza uume wa mwenzi<br />
wako ndani ya kondomu. Tumia kondomu ya kike moja kwa wakati mmoja. Usirudie kuitumia<br />
kondomu hiyo.<br />
jinsi ya kuitoa: Ni rahisi sana kuitoa. Sokota pete ya juu ili shahawa zisimwagike, halafu vuta<br />
kondomu nje na itupe ndani ya choo cha shimo au choma moto au fukia ndani ya shimo.<br />
Faida yake: Kondomu ya kike ni njia pekee ya kujikinga ambayo inadhibitiwa na mwanamke<br />
mwenyewe ili imlinde dhidi ya maambukizo ya magonjwa ya zinaa, VVU/ UKIMWI na mimba.<br />
Inakaa taratibu ndani ya uke na haibani uume unapoingia.<br />
Yapo matatizo ambayo yanatokea kwenye via vya uzazi lakini siyo magonjwa ya zinaa. Hata<br />
kama hujawahi kufanya ngono, yapo maambukizo ambayo unaweza kuyapata sehemu zako<br />
za siri. Unaweza ukapata maambukizo kwenye njia ya mkojo ambayo husababisha kuwashwa<br />
au maumivu unapokojoa mkojo. Ukiona uchafu wa ajabu unatoka au maumivu au damu wakati<br />
unapokojoa, unatakiwa kumwona mhudumu wa afya.<br />
KanDiDiaSiSi”<br />
Kama sehemu zako za siri zinawasha na unatokwa na uchafu wa ajabu ukeni unaweza ukawa na<br />
“kandidiasisi”. Hili ni tatizo la kawaida. Ugonjwa huu vilevile unaitwa maambukizo ya hamira na<br />
unasababishwa na kuvu wanaofanana na hamira wanaoitwa “kandida albicans”. Ugonjwa huu<br />
unawasumbua wasichana na wanawake wengi. Wavulana wanaweza kupata kandida chini ya govi.<br />
Kandida ni kiumbe kimojawapo ambacho kwa asili kinaishi juu ya mwili. Kwa kawaida kandida<br />
hakisababishi matatizo yoyote. Kinadhibitiwa na kinga ya mwili na bakteria wengine ambao<br />
kwa kawaida wanaishi ukeni. Lakini ikiwa kinga ya mwili imeshaharibiwa na haifanyi kazi vizuri,<br />
viumbe kandida huzaliana haraka . Mara kwa mara tatizo hili hutokea kabla au baada ya damu ya<br />
hedhi kutoka na wakati wa mimba.<br />
“Kandidiasisi” inaweza kuenea kwa njia ya kujamiiana na mtu ambaye ana kandida wengi. Lakini<br />
inaweza kusababishwa na mambo mengine vilevile. Mfadhaiko, kama vile mitihani, kifo ndani ya<br />
familia au mabishano yanaweza kuwa kichochezi cha “kandidiasisi”. Wakati mwingine unaweza<br />
kupata kandidiasisi ukinywa kiuavijasumu – Viuavijasumu vinaua bakteria ambao kwa kawaida<br />
wanaishi ukeni. Watu wanaoumwa kisukari na wale wenye VVU wanapata kandidiasisi mara kwa<br />
mara.<br />
“Kandidiasisi” si ugonjwa wa ngono kwa sababu hata bikira wanaupata. Joto linapozidi na<br />
unyevunyevu kuzunguka eneo la via vya uzazi vinaweza kusabisha kandidiasisi. Hii ina maana ya<br />
kwamba unaweza kujiletea mwenyewe “kandidiasisi” kwa kuvaa nguo zisizofaa. Kama, kwa mfano<br />
ukivaa nguo za nailoni, kaptura za kubana au suruali aina ya jeans zinazobana na kukaa kwa saa<br />
kadhaa huku umebananisha miguu, pengine kwenye basi, unatengeneza unyevuunyevu na joto<br />
ambalo kandida wanahitaji ili waishi.<br />
Dalili za kandidiasisi ni:-<br />
•<br />
•<br />
•<br />
SURA YA 10 | KUTUNZA AfYA YAKO YA KIUJINSIA<br />
Zungumza na mwenzi wako kuhusu matumizi ya Kondomu. eleza unavyojisikia na unachotaka.<br />
Kuwashwa kwenye via vya uzazi, wote; wasichana na wavulana.<br />
Usaha kutoka ukeni au chini ya govi unaofanana na maziwa yaliyoharibika.<br />
Kuvimba na kuwepo kwa utando telezi wa uke na midomo ya ndani au kichwa cha uume kuwa<br />
chekundu.<br />
Iwapo utapata mojawapo ya dalili hizi omba msaada kutoka kwa mhudumu wa afya mwenye ujuzi<br />
ambaye atakupatia matibatu yanayotakiwa. Matibabu yanayotakiwa kawaida ni:-<br />
125