Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
98<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
KuVutiWa na Mtu Wa jinSi KaMa YaKO<br />
Wakati wa kubalehe ndio wakati watu wengi wanapata kuelewa zaidi mwelekeo wao kijinsi.<br />
Mwelekeo wa kijinsi unahusu mtu ana hisia za kimapenzi na anavutiwa kimapenzi kwa nani.<br />
Watu wengi wanavutiwa kimapenzi na watu wa jinsi tofauti (kama mwanaume anavutiwa na<br />
mwanamke na mwanamke anavutiwa na mwanaume).<br />
Watu wengine wanajisikia kuvutiwa kimapenzi na watu wa jinsi sawa. Wanaume wengine<br />
wanavutiwa na wanaume wenzao na wanawake wengine kuvutiwa na wanawake wenzao. Huku<br />
kuvutiwa na jinsia sawa kunaitwa “ubasha” au “usenge” au “ushoga”.<br />
Nyakati fulani katika maisha yao, baadhi ya watu wanakuwa na hisia za kimapenzi, mawazo,<br />
ndoto na mvuto kwa mtu fulani wa jinsi moja. Marafiki wawili waliokaribu (pengine wavulana<br />
wawili au wasichana wawili) wanaweza kupendana – wanapenda kuwa pamoja na wakati<br />
mwingine wanajisikia kutamaniana kimwili. Watu wengine wanaona hisia hizi zinawachanganya<br />
na kuwafadhaisha. Hisia hizi ni za kawaida, na baadhi ya watu wanazipata hisia hizi wakati fulani<br />
katika kipindi cha maisha yao.<br />
Japokuwa baadhi ya watu wanavutiwa na watu wa jinsi sawa, madhehebu mengine ya dini na mila<br />
zingine zinafikiria ubasha ni jambo baya, si la kawaida na ni tabia ambayo inaweza kurekebishwa.<br />
Watalaam wengi wanafikiria kwamba mwelekeo wa kimapenzi wa jinsi moja si jambo ambalo<br />
wanaweza kulidhibiti kama isivyowezekana kudhibiti rangi ya ngozi au nywele zilivyo. Kwa<br />
maneno mengine ubasha / usenge sio chaguo la makusudi ambalo mtu anachagua, hivyo<br />
haiwezekani kulibadilisha aidha kwa kuswali, kwa utashi au kwa kufanya ngono na mtu wa jinsia<br />
tofauti.<br />
Katika kipindi cha balehe, watu wengine wanajikuta ni mabasha/wasenge. Kujitambua kunaweza<br />
kuwa kugumu. Unaweza kujiona uko tofauti kuliko mtu yeyote anayekuzunguka, na unaweza<br />
kujisikia mpweke mno. Kama unajisikia kitu kama hiki, jaribu kuonana na mtu ili uzungumze naye,<br />
kama mshauri nasaha wa vijana, mhudumu wa afya, mwalimu unayemwamini, au jamaa yako<br />
mkubwa – yeyote atakayeweza kukusaidia kujibu maswali yako na kupunguza hofu yako atakuwa<br />
amekusaidia.<br />
ubiKiRa<br />
Bikira ni mtu ambaye hajawahi kujamiiana. Kila mvulana na msichana amezaliwa bikira. Ubikira<br />
ni kinga nzuri dhidi ya VVU na magonjwa ya zinaa. Siku hizi wavulana na wasichana wengi<br />
wanaamua kubakia bikira hadi siku ya kuoa/kuolewa.<br />
Ruvimbo kutoka Zimbabwe (umri wa miaka 13)<br />
“Nitataka kutunza ubikira wangu. Sitafanya mapenzi na yeyote<br />
hata kwa kutumia kinga. Rafiki yangu wa kiume ni mtulivu<br />
na ndio maana ni mtu wangu.”<br />
Stabile, kutoka Zimbabwe (umri; miaka 19)<br />
“Bado mimi ni bikira. Bila shaka imani yangu kubwa ya dini<br />
inanisaidia katika suala hili.”<br />
SURA YA 9 | UJINSIA NA NGONO<br />
Susan, umri wa miaka 18 kutoka uganda<br />
“Ubikira ulifanya nionekane mwenye heshima. Wasichana wanatakiwa<br />
kutunza ubikira wao mpaka wanapoona wamepata watu wa kuwafaa.<br />
Ngono ni jambo unaloweza kuahirisha. Yakwepe mazingira yaliyo<br />
kinyume na kanuni ulizojiwekea na utaweza ukadumisha dhamira yako.”<br />
Watu wengi wanachanganyikiwa na kitu kinachosababisha wasichana wapoteze ubikira.<br />
Wanafikiri ubikira wa msichana unadhihirishwa na kizinda, ambacho ni tishu nyembamba ndani ya<br />
mlango wa uke. Kizinda kina shimo dogo na hakizibi kabisa uke kwa sababu damu ya hedhi lazima<br />
itoke kila mwezi. Wasichana wengine hawana kizinda kabisa. Pengine ni kwa vile hawakuzaliwa<br />
nacho au kilinyumbuka na kuchanika kabisa wakati wa michezo.<br />
Wasichana walio na tishu ya kizinda mara nyingine wanatoka damu wanapopoteza ubikira wao.<br />
Wasichana ambao wana tishu ndogo ya kizinda au hawana tishu ya kizinda wanaweza wasivuje<br />
damu watakapojamiiana. Kwa mara ya kwanza hii inawachanganya watu. Watu wanasema:<br />
“Hakuna damu, kwa hiyo hakuwa bikira”. Lakini anaweza kuwa alikuwa, hajawahi kufanya ngono<br />
hapo awali hivyo alikuwa bikira. Ubikira unapotea kwa kujamiiana. Hauwezi kupotea kutokana na<br />
michezo, kwa kutumia visodo, kupiga punyeto au shughuli yoyote ile. Japo ni kweli mambo haya<br />
yanaweza kurefusha au kuchana kizinda, hii haimaanishi msichana sio bikira. Watu wanaofikiria<br />
kuwa kizinda ndio usahihi wa kuwepo bikira wanakosea.<br />
UNAJUA ukweli kuhusu ubikira?<br />
Kuna uzushi mwingi kuhusu ubikira:<br />
1. Nimesikia kwamba msichana anaweza kupoteza ubikira kwa kucheza michezo. Je, hii<br />
ni kweli? Si kweli! Ubikira anaweza kupotea tu kwa kufanya ngono, kucheza michezo ni<br />
kuzuri kwa wasichana na haiwezi kumsababishia kupoteza ubikira.<br />
2. Kuna mitishamba mingine inaweza kurejesha ubikira? Hapana, hakuna mitishamba<br />
inayoweza kurejesha ubikira. Ukipotea, umepotea milele.<br />
3. Rafiki yangu anasema nikibaki bikira kwa muda mrefu, naweza kuugua magonjwa na<br />
mambo yasiyo ya kawaida? Siyo kweli! Unaweza kubakia na ubikira maisha yako yote<br />
bila matatizo yoyote mabaya.<br />
4. Ni kweli kwamba msichana akiwa bikira kwa muda mrefu sana, kizinda chake kitakuwa<br />
kigumu na atapata matatizo ya kufanya ngono? Huu ni upuuzi! Kizinda ni kipande<br />
kidogo na chembamba cha tishu. Hakiwi kigumu kadri unavyokua na wala unaposubiri<br />
kujamiianahudhuriki kamwe.<br />
5. Unawaweza kuwatambua bikira kwa kuwaangalia usoni? Si kweli! Huweza kumtambua<br />
bikira kwa kumwangalia kwa macho. Ni bikira peke yake anayejua hali yake.<br />
6. Baada ya kupoteza ubikira wako, unatakiwa uendelee na ngono. Si kweli. Unaweza<br />
kuacha kufanya ngono ukipenda.<br />
7. Nimesikia kwamba si vema kutumia kondomu ukiwa unajamiiana na msichana ambaye<br />
ni bikira kwa sababu unahitaji kutumia nguvu sana kuvunja ubikira wa msichana<br />
– kiasi kwamba utachana kondomu. Je huu ni ukweli? Hapana! Mvulana na msichana<br />
ambao ni bikira wanaweza kutumia kondomu bila matatizo. Kizinda ni tishu laini sana<br />
inayochanika kwa urahisi mno.<br />
99