08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

98<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

KuVutiWa na Mtu Wa jinSi KaMa YaKO<br />

Wakati wa kubalehe ndio wakati watu wengi wanapata kuelewa zaidi mwelekeo wao kijinsi.<br />

Mwelekeo wa kijinsi unahusu mtu ana hisia za kimapenzi na anavutiwa kimapenzi kwa nani.<br />

Watu wengi wanavutiwa kimapenzi na watu wa jinsi tofauti (kama mwanaume anavutiwa na<br />

mwanamke na mwanamke anavutiwa na mwanaume).<br />

Watu wengine wanajisikia kuvutiwa kimapenzi na watu wa jinsi sawa. Wanaume wengine<br />

wanavutiwa na wanaume wenzao na wanawake wengine kuvutiwa na wanawake wenzao. Huku<br />

kuvutiwa na jinsia sawa kunaitwa “ubasha” au “usenge” au “ushoga”.<br />

Nyakati fulani katika maisha yao, baadhi ya watu wanakuwa na hisia za kimapenzi, mawazo,<br />

ndoto na mvuto kwa mtu fulani wa jinsi moja. Marafiki wawili waliokaribu (pengine wavulana<br />

wawili au wasichana wawili) wanaweza kupendana – wanapenda kuwa pamoja na wakati<br />

mwingine wanajisikia kutamaniana kimwili. Watu wengine wanaona hisia hizi zinawachanganya<br />

na kuwafadhaisha. Hisia hizi ni za kawaida, na baadhi ya watu wanazipata hisia hizi wakati fulani<br />

katika kipindi cha maisha yao.<br />

Japokuwa baadhi ya watu wanavutiwa na watu wa jinsi sawa, madhehebu mengine ya dini na mila<br />

zingine zinafikiria ubasha ni jambo baya, si la kawaida na ni tabia ambayo inaweza kurekebishwa.<br />

Watalaam wengi wanafikiria kwamba mwelekeo wa kimapenzi wa jinsi moja si jambo ambalo<br />

wanaweza kulidhibiti kama isivyowezekana kudhibiti rangi ya ngozi au nywele zilivyo. Kwa<br />

maneno mengine ubasha / usenge sio chaguo la makusudi ambalo mtu anachagua, hivyo<br />

haiwezekani kulibadilisha aidha kwa kuswali, kwa utashi au kwa kufanya ngono na mtu wa jinsia<br />

tofauti.<br />

Katika kipindi cha balehe, watu wengine wanajikuta ni mabasha/wasenge. Kujitambua kunaweza<br />

kuwa kugumu. Unaweza kujiona uko tofauti kuliko mtu yeyote anayekuzunguka, na unaweza<br />

kujisikia mpweke mno. Kama unajisikia kitu kama hiki, jaribu kuonana na mtu ili uzungumze naye,<br />

kama mshauri nasaha wa vijana, mhudumu wa afya, mwalimu unayemwamini, au jamaa yako<br />

mkubwa – yeyote atakayeweza kukusaidia kujibu maswali yako na kupunguza hofu yako atakuwa<br />

amekusaidia.<br />

ubiKiRa<br />

Bikira ni mtu ambaye hajawahi kujamiiana. Kila mvulana na msichana amezaliwa bikira. Ubikira<br />

ni kinga nzuri dhidi ya VVU na magonjwa ya zinaa. Siku hizi wavulana na wasichana wengi<br />

wanaamua kubakia bikira hadi siku ya kuoa/kuolewa.<br />

Ruvimbo kutoka Zimbabwe (umri wa miaka 13)<br />

“Nitataka kutunza ubikira wangu. Sitafanya mapenzi na yeyote<br />

hata kwa kutumia kinga. Rafiki yangu wa kiume ni mtulivu<br />

na ndio maana ni mtu wangu.”<br />

Stabile, kutoka Zimbabwe (umri; miaka 19)<br />

“Bado mimi ni bikira. Bila shaka imani yangu kubwa ya dini<br />

inanisaidia katika suala hili.”<br />

SURA YA 9 | UJINSIA NA NGONO<br />

Susan, umri wa miaka 18 kutoka uganda<br />

“Ubikira ulifanya nionekane mwenye heshima. Wasichana wanatakiwa<br />

kutunza ubikira wao mpaka wanapoona wamepata watu wa kuwafaa.<br />

Ngono ni jambo unaloweza kuahirisha. Yakwepe mazingira yaliyo<br />

kinyume na kanuni ulizojiwekea na utaweza ukadumisha dhamira yako.”<br />

Watu wengi wanachanganyikiwa na kitu kinachosababisha wasichana wapoteze ubikira.<br />

Wanafikiri ubikira wa msichana unadhihirishwa na kizinda, ambacho ni tishu nyembamba ndani ya<br />

mlango wa uke. Kizinda kina shimo dogo na hakizibi kabisa uke kwa sababu damu ya hedhi lazima<br />

itoke kila mwezi. Wasichana wengine hawana kizinda kabisa. Pengine ni kwa vile hawakuzaliwa<br />

nacho au kilinyumbuka na kuchanika kabisa wakati wa michezo.<br />

Wasichana walio na tishu ya kizinda mara nyingine wanatoka damu wanapopoteza ubikira wao.<br />

Wasichana ambao wana tishu ndogo ya kizinda au hawana tishu ya kizinda wanaweza wasivuje<br />

damu watakapojamiiana. Kwa mara ya kwanza hii inawachanganya watu. Watu wanasema:<br />

“Hakuna damu, kwa hiyo hakuwa bikira”. Lakini anaweza kuwa alikuwa, hajawahi kufanya ngono<br />

hapo awali hivyo alikuwa bikira. Ubikira unapotea kwa kujamiiana. Hauwezi kupotea kutokana na<br />

michezo, kwa kutumia visodo, kupiga punyeto au shughuli yoyote ile. Japo ni kweli mambo haya<br />

yanaweza kurefusha au kuchana kizinda, hii haimaanishi msichana sio bikira. Watu wanaofikiria<br />

kuwa kizinda ndio usahihi wa kuwepo bikira wanakosea.<br />

UNAJUA ukweli kuhusu ubikira?<br />

Kuna uzushi mwingi kuhusu ubikira:<br />

1. Nimesikia kwamba msichana anaweza kupoteza ubikira kwa kucheza michezo. Je, hii<br />

ni kweli? Si kweli! Ubikira anaweza kupotea tu kwa kufanya ngono, kucheza michezo ni<br />

kuzuri kwa wasichana na haiwezi kumsababishia kupoteza ubikira.<br />

2. Kuna mitishamba mingine inaweza kurejesha ubikira? Hapana, hakuna mitishamba<br />

inayoweza kurejesha ubikira. Ukipotea, umepotea milele.<br />

3. Rafiki yangu anasema nikibaki bikira kwa muda mrefu, naweza kuugua magonjwa na<br />

mambo yasiyo ya kawaida? Siyo kweli! Unaweza kubakia na ubikira maisha yako yote<br />

bila matatizo yoyote mabaya.<br />

4. Ni kweli kwamba msichana akiwa bikira kwa muda mrefu sana, kizinda chake kitakuwa<br />

kigumu na atapata matatizo ya kufanya ngono? Huu ni upuuzi! Kizinda ni kipande<br />

kidogo na chembamba cha tishu. Hakiwi kigumu kadri unavyokua na wala unaposubiri<br />

kujamiianahudhuriki kamwe.<br />

5. Unawaweza kuwatambua bikira kwa kuwaangalia usoni? Si kweli! Huweza kumtambua<br />

bikira kwa kumwangalia kwa macho. Ni bikira peke yake anayejua hali yake.<br />

6. Baada ya kupoteza ubikira wako, unatakiwa uendelee na ngono. Si kweli. Unaweza<br />

kuacha kufanya ngono ukipenda.<br />

7. Nimesikia kwamba si vema kutumia kondomu ukiwa unajamiiana na msichana ambaye<br />

ni bikira kwa sababu unahitaji kutumia nguvu sana kuvunja ubikira wa msichana<br />

– kiasi kwamba utachana kondomu. Je huu ni ukweli? Hapana! Mvulana na msichana<br />

ambao ni bikira wanaweza kutumia kondomu bila matatizo. Kizinda ni tishu laini sana<br />

inayochanika kwa urahisi mno.<br />

99

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!