Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
88<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Marafiki wa Okakah walimwambia kwamba angempoteza rafiki yake wa kike iwapo asingefanya<br />
naye ngono, lakini ukweli ni kwamba ilikaribia kumpoteza rafiki yake wa kike kwa kumwambia<br />
wafanye ngono! Alichokuwa anaambiwa na rafiki zake haikuwa kweli.<br />
Kumbuka, watu wawili wanaweza kuwa na mahusiano ya karibu sana bila ya hata kufanya ngono.<br />
Wanaweza kubadilishana uzoefu; wanaweza kujifunza mambo mengi ya muhimu kuhusu kila<br />
mmoja wao – jinsi kila mtu anavyoona maisha, jinsi watakavyofanya maamuzi pamoja, kila mmoja<br />
atakuwa mwenzi na mzazi wa namna gani na namna kila mmoja anavyoiona mipango ya maisha ya<br />
mwenzake.<br />
Yote haya ni muhimu kabla hujaanza mahusiano ya kimapenzi na mtu yeyote. Mnatakiwa kwanza<br />
muwe marafiki wa kweli. Ngono bila urafiki wa kweli wakati wote ni hatari kwa afya yako na kwa<br />
moyo wako. Unaweza kuumia. Kwa hiyo kwa ajili ya mahusiano yenye afya na afya ya ujinsia –<br />
kuweni marafiki wa kweli kwanza.<br />
MaPenZi<br />
Ni vigumu kutafsiri mapenzi kwa sababu yanahusu hasa hisia. Mapenzi ni kitu kikubwa na kuna<br />
aina mbalimbali za mapenzi. Mapenzi kwa wazazi na marafiki, mapenzi kwa rafiki wa kiume au wa<br />
kike na mapenzi kwa jamii.<br />
Vile vile mapenzi ni hisia ngumu, na watu wanaweza kueleza maana ya mapenzi kwa njia tofauti<br />
kutegemeana na uzoefu wao na mahusiano yao ya kupenda. Mapenzi ni hisia yenye utata na watu<br />
hutoa tafsiri ya mapenzi kutegemeana na uzoefu wa mahusiano ya kimapenzi.<br />
Godfrey, kutoka Zimbabwe (umri wa miaka 19)<br />
“Siwezi kuyaelezea mapenzi. Ni vizuri sana kuwa katika mapenzi.”<br />
Patrick, kutoka Ghana (umri wa miaka 16)<br />
“Mapenzi ni muungano wa watu wawili ukiwa na sanaa ya<br />
kuelewana na kuwa mwaminifu kwa kila mtu.”<br />
Sherifan, kutoka Ghana (umri wa miaka 15)<br />
“Mapenzi ni kitu ambacho kipo kati ya watu wawili. Aidha<br />
mvulana au msichana. Mapenzi ni kushirikiana katika matatizo<br />
na kujaliana”.<br />
Stabisile, kutoka Zimbabwe (umri wa miaka 19)<br />
“Kuwa na mpenzi ni mojawapo ya vitu vizuri duniani”.<br />
jennifer, kutoka Ghana (umri wa miaka 17)<br />
“Mapenzi ni wewe, familia yako na marafiki kushirikiana<br />
mawazo pamoja. Hivi ndivyo ninavyofahamu kuhusu mapenzi.”<br />
SURA YA 8 | URAfIKI NA MApENZI<br />
Kuwa na mpenzi kunaweza kuwa kama uchawi.<br />
Unakutana na mtu maalumu halafu kila kitu<br />
kinabadilika. Jua linaonekana kung’ara zaidi, nyasi<br />
zinakuwa za kijani zaidi na unajiona kama unatembea<br />
hewani.<br />
Kuwa na mpenzi ni tofauti na kumpata rafiki mpya.<br />
Unapokuwa na mpenzi, unaweza kujisikia joto, na<br />
hisia zilizojaa. Unaweza kujisikia kutabasamu kila<br />
wakati kwa sababu mawazo ya yule unayempenda<br />
yanakufanya uwe na furaha. Unataka kuwa na mtu<br />
huyu kila wakati. Unapata njozi za mchana za tamaa<br />
ya mambo yasiyowezekana kuhusu mtu huyo. Kuna<br />
wakati unaweza kupoteza hamu ya kula au kukosa<br />
usingizi usiku.<br />
Sherry, kutoka Ghana (umri wa miaka 19)<br />
“Ni jambo la ajabu. Huelewi kinachokupata. Huwezi kuelezea.<br />
Unajaribu kuacha kumfikiria lakini unagundua mawazo hayawezi<br />
kutoka. Unaweza ukawa unasoma kwa ajili ya mtihani lakini unaona<br />
akili yako haiendani na macho yanavyoangalia ukurasa wa kitabu.”<br />
Sara, kutoka uganda (umri wa miaka 18)<br />
“Nina miaka 18 na yupo mvulana ninayempenda sana. Anapokuwa<br />
mbali na mimi, ninashindwa kuwa makini na kitu chochote.<br />
Anapokuwepo karibu na mimi ninatetemeka na siwezi kufanya<br />
kitu chochote cha maana,hata kama akiniambia nijifanye kama<br />
hayupo. Hisia hizi zinanifanya nichanganikiwe kabisa.”<br />
angela, kutoka Kenya (umri wa miaka 18)<br />
“Inasisimumua kuwa katika mapenzi.Hutaki kumuumiza.Unajisikia<br />
mpya kama vile kitu kimeongezeka.Wakati mwingine kujisomea<br />
inakuwa matatizo.Akikuandikia barua ,itasomwa kwa masaa.<br />
“Penzi la kwanza” ni mojawapo ya uzoefu mzito wa maisha. Kuwa na mpenzi sio sawa na<br />
uzoefu wowote ulioupata ukiwa mtoto. Ni kitu ambacho unatakiwa kukichukulia taratibu.<br />
Usikimbilie. Tunza moyo wako na wa wale unaowapenda wachukulie kwa uangalifu.<br />
Diana, kutoka Zambia (umri wa miaka 17)<br />
“Ninafikiri kuwa mapenzi yaje kikawaida kuliko inavyotokea kwa<br />
vijana ambao wanaenda kutafuta mapenzi badala ya kuacha mapenzi<br />
yawatafute. Watu wanatakiwa kuangaliana kwa njia chanya.<br />
Mapenzi yanaweza kupatikana bila kulazimisha ili usije ukajuta<br />
baadaye.”<br />
89