08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

88<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Marafiki wa Okakah walimwambia kwamba angempoteza rafiki yake wa kike iwapo asingefanya<br />

naye ngono, lakini ukweli ni kwamba ilikaribia kumpoteza rafiki yake wa kike kwa kumwambia<br />

wafanye ngono! Alichokuwa anaambiwa na rafiki zake haikuwa kweli.<br />

Kumbuka, watu wawili wanaweza kuwa na mahusiano ya karibu sana bila ya hata kufanya ngono.<br />

Wanaweza kubadilishana uzoefu; wanaweza kujifunza mambo mengi ya muhimu kuhusu kila<br />

mmoja wao – jinsi kila mtu anavyoona maisha, jinsi watakavyofanya maamuzi pamoja, kila mmoja<br />

atakuwa mwenzi na mzazi wa namna gani na namna kila mmoja anavyoiona mipango ya maisha ya<br />

mwenzake.<br />

Yote haya ni muhimu kabla hujaanza mahusiano ya kimapenzi na mtu yeyote. Mnatakiwa kwanza<br />

muwe marafiki wa kweli. Ngono bila urafiki wa kweli wakati wote ni hatari kwa afya yako na kwa<br />

moyo wako. Unaweza kuumia. Kwa hiyo kwa ajili ya mahusiano yenye afya na afya ya ujinsia –<br />

kuweni marafiki wa kweli kwanza.<br />

MaPenZi<br />

Ni vigumu kutafsiri mapenzi kwa sababu yanahusu hasa hisia. Mapenzi ni kitu kikubwa na kuna<br />

aina mbalimbali za mapenzi. Mapenzi kwa wazazi na marafiki, mapenzi kwa rafiki wa kiume au wa<br />

kike na mapenzi kwa jamii.<br />

Vile vile mapenzi ni hisia ngumu, na watu wanaweza kueleza maana ya mapenzi kwa njia tofauti<br />

kutegemeana na uzoefu wao na mahusiano yao ya kupenda. Mapenzi ni hisia yenye utata na watu<br />

hutoa tafsiri ya mapenzi kutegemeana na uzoefu wa mahusiano ya kimapenzi.<br />

Godfrey, kutoka Zimbabwe (umri wa miaka 19)<br />

“Siwezi kuyaelezea mapenzi. Ni vizuri sana kuwa katika mapenzi.”<br />

Patrick, kutoka Ghana (umri wa miaka 16)<br />

“Mapenzi ni muungano wa watu wawili ukiwa na sanaa ya<br />

kuelewana na kuwa mwaminifu kwa kila mtu.”<br />

Sherifan, kutoka Ghana (umri wa miaka 15)<br />

“Mapenzi ni kitu ambacho kipo kati ya watu wawili. Aidha<br />

mvulana au msichana. Mapenzi ni kushirikiana katika matatizo<br />

na kujaliana”.<br />

Stabisile, kutoka Zimbabwe (umri wa miaka 19)<br />

“Kuwa na mpenzi ni mojawapo ya vitu vizuri duniani”.<br />

jennifer, kutoka Ghana (umri wa miaka 17)<br />

“Mapenzi ni wewe, familia yako na marafiki kushirikiana<br />

mawazo pamoja. Hivi ndivyo ninavyofahamu kuhusu mapenzi.”<br />

SURA YA 8 | URAfIKI NA MApENZI<br />

Kuwa na mpenzi kunaweza kuwa kama uchawi.<br />

Unakutana na mtu maalumu halafu kila kitu<br />

kinabadilika. Jua linaonekana kung’ara zaidi, nyasi<br />

zinakuwa za kijani zaidi na unajiona kama unatembea<br />

hewani.<br />

Kuwa na mpenzi ni tofauti na kumpata rafiki mpya.<br />

Unapokuwa na mpenzi, unaweza kujisikia joto, na<br />

hisia zilizojaa. Unaweza kujisikia kutabasamu kila<br />

wakati kwa sababu mawazo ya yule unayempenda<br />

yanakufanya uwe na furaha. Unataka kuwa na mtu<br />

huyu kila wakati. Unapata njozi za mchana za tamaa<br />

ya mambo yasiyowezekana kuhusu mtu huyo. Kuna<br />

wakati unaweza kupoteza hamu ya kula au kukosa<br />

usingizi usiku.<br />

Sherry, kutoka Ghana (umri wa miaka 19)<br />

“Ni jambo la ajabu. Huelewi kinachokupata. Huwezi kuelezea.<br />

Unajaribu kuacha kumfikiria lakini unagundua mawazo hayawezi<br />

kutoka. Unaweza ukawa unasoma kwa ajili ya mtihani lakini unaona<br />

akili yako haiendani na macho yanavyoangalia ukurasa wa kitabu.”<br />

Sara, kutoka uganda (umri wa miaka 18)<br />

“Nina miaka 18 na yupo mvulana ninayempenda sana. Anapokuwa<br />

mbali na mimi, ninashindwa kuwa makini na kitu chochote.<br />

Anapokuwepo karibu na mimi ninatetemeka na siwezi kufanya<br />

kitu chochote cha maana,hata kama akiniambia nijifanye kama<br />

hayupo. Hisia hizi zinanifanya nichanganikiwe kabisa.”<br />

angela, kutoka Kenya (umri wa miaka 18)<br />

“Inasisimumua kuwa katika mapenzi.Hutaki kumuumiza.Unajisikia<br />

mpya kama vile kitu kimeongezeka.Wakati mwingine kujisomea<br />

inakuwa matatizo.Akikuandikia barua ,itasomwa kwa masaa.<br />

“Penzi la kwanza” ni mojawapo ya uzoefu mzito wa maisha. Kuwa na mpenzi sio sawa na<br />

uzoefu wowote ulioupata ukiwa mtoto. Ni kitu ambacho unatakiwa kukichukulia taratibu.<br />

Usikimbilie. Tunza moyo wako na wa wale unaowapenda wachukulie kwa uangalifu.<br />

Diana, kutoka Zambia (umri wa miaka 17)<br />

“Ninafikiri kuwa mapenzi yaje kikawaida kuliko inavyotokea kwa<br />

vijana ambao wanaenda kutafuta mapenzi badala ya kuacha mapenzi<br />

yawatafute. Watu wanatakiwa kuangaliana kwa njia chanya.<br />

Mapenzi yanaweza kupatikana bila kulazimisha ili usije ukajuta<br />

baadaye.”<br />

89

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!