Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
44<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Sura ya Nne<br />
Wasichana<br />
Wakati wa kubalehe, msichana ategemee mabadiliko mengi ya mwili. Yafuatayo ni baadhi<br />
tu ya mabadiliko yanayoweza kutokea:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Mwili utaongezeka urefu; nyonga itapanuka, mifupa ya mikono, miguu itarefuka.<br />
Msichana atapata umbo la mviringo la kike.<br />
Matiti yatakua na chuchu itaongezeka ukubwa na kuwa na rangi nyeusi.<br />
Sehemu za siri zitakomaa na kuta za uke zitaanza kutoa majimaji.<br />
Damu ya hedhi itaanza kuonekana kila mwezi.<br />
Dalili hizi hutokea kwa muda muafaka ambao ni tofauti kwa kila msichana. Wakati<br />
mabadiliko haya yanatokea, kuna vitu vichache vya kuzingatia:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Kwamba matiti yana ukubwa unaotofautiana kwa kila mwanamke. Matiti yote<br />
yanavutia hivyo yalivyo na ni muhimu kwa kunyonyesha watoto.<br />
Safisha sehemu za siri- ila sio ndani ya uke- kila siku. Vaa chupi zilizotengenezwa kwa<br />
kitambaa cha pamba.<br />
Ni muhimu kuifahamu harufu na hali ya kawaida ya majimaji ya uke ili inapotokea<br />
mabadiliko ujue kuwa ni dalili za maambukizi.<br />
Siku za hedhi kwa msichana anayebalehe hubadilika badilika hivyo hakuna “siku<br />
salama’ za kutopata mimba wala hakuna siku salama ambazo hutaambukizwa VVU au<br />
magonjwa mengine ya ngono.<br />
Ingawa wakati wa hedhi ni kawaida kuumwa tumbo, kuvimba au kujisikia vibaya,<br />
hali hii isifanye msichana akakosa raha. Mazoezi na vyakula vyenye chumvi kidogo<br />
husaidia kupunguza maumivu. Kama maumivu yanakuwa makali na damu nyingi sana<br />
inatoka, kamuone mhudumu wa afya.<br />
Mabadiliko Ya Msingi<br />
Katika Kutunza Mwili<br />
Sura hii inazungumzia jinsi ya kutunza afya ya mwili wako kwa ujumla. Hili linaweza kuonekana<br />
kama sio muhimu ukilinganisha na mambo mengine yaliyomo katika kitabu hiki, lakini ni muhimu<br />
kujua jinsi ya kuishi na afya njema. Kwa kweli matatizo mengi ya afya yanaweza kuepukwa kama<br />
ukila vizuri, ukifanya mazoezi, ukiwa msafi na ukijisikia vizuri.<br />
Ni wajibu wako kuangalia mambo haya kila siku, na kuonekana na kujisikia vizuri iwezekanavyo.<br />
Mwili wako ndio utakaokuwa nao katika kipindi chote cha uhai wako. Kwa hiyo unatakiwa<br />
kuutunza kweli kweli!<br />
jiWeKe MSaFi, nuKia ViZuRi.<br />
Kila mtu anataka kuonekana msafi,<br />
lakini kujihisi kuwa na mvuto<br />
inaonekana ni muhimu hususani katika<br />
kipindi cha ujana balehe kwa sababu<br />
ya mabadiliko makubwa yanayotokea<br />
katika mwili. Sio tu mwili unabadilika<br />
umbo wakati wa balehe, lakini vilevile<br />
unaanza kutoa harufu mpya, majimaji<br />
mapya na hofu mpya hasa kwa vijana.<br />
Hivyo kujizoesha kuwa msafi inaweza<br />
kuwa ni njia nzuri ya kujisikia raha ili<br />
kukabiliana na mabadiliko haya yote<br />
yanayotokea.<br />
Oga angalau mara moja kwa siku ili kujisikia<br />
vizuri na safi.<br />
Sandra, kutoka uganda (umri ; miaka 13)<br />
“Siku zote oga, fua na piga pasi nguo ili uonekane nadhifu.”<br />
Usafi mzuri wa mwili hususani wakati wa balehe ni muhimu kwa sababu ngozi yako inaanza<br />
kutoa majimaji zaidi kuliko ilivyokuwa wakati ukiwa mtoto, na baadhi ya haya majimaji yanaweza<br />
kusababisha harufu mbaya kama huogi.<br />
Majimaji utakayoyaona zaidi ni ya jasho. Jasho linatokana na tezi zilizopo kwenye ngozi. Tezi za<br />
jasho zinakuwa hai zaidi wakati unapofikia balehe.<br />
45<br />
SURA YA 5