08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

44<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Sura ya Nne<br />

Wasichana<br />

Wakati wa kubalehe, msichana ategemee mabadiliko mengi ya mwili. Yafuatayo ni baadhi<br />

tu ya mabadiliko yanayoweza kutokea:<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

Mwili utaongezeka urefu; nyonga itapanuka, mifupa ya mikono, miguu itarefuka.<br />

Msichana atapata umbo la mviringo la kike.<br />

Matiti yatakua na chuchu itaongezeka ukubwa na kuwa na rangi nyeusi.<br />

Sehemu za siri zitakomaa na kuta za uke zitaanza kutoa majimaji.<br />

Damu ya hedhi itaanza kuonekana kila mwezi.<br />

Dalili hizi hutokea kwa muda muafaka ambao ni tofauti kwa kila msichana. Wakati<br />

mabadiliko haya yanatokea, kuna vitu vichache vya kuzingatia:<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

Kwamba matiti yana ukubwa unaotofautiana kwa kila mwanamke. Matiti yote<br />

yanavutia hivyo yalivyo na ni muhimu kwa kunyonyesha watoto.<br />

Safisha sehemu za siri- ila sio ndani ya uke- kila siku. Vaa chupi zilizotengenezwa kwa<br />

kitambaa cha pamba.<br />

Ni muhimu kuifahamu harufu na hali ya kawaida ya majimaji ya uke ili inapotokea<br />

mabadiliko ujue kuwa ni dalili za maambukizi.<br />

Siku za hedhi kwa msichana anayebalehe hubadilika badilika hivyo hakuna “siku<br />

salama’ za kutopata mimba wala hakuna siku salama ambazo hutaambukizwa VVU au<br />

magonjwa mengine ya ngono.<br />

Ingawa wakati wa hedhi ni kawaida kuumwa tumbo, kuvimba au kujisikia vibaya,<br />

hali hii isifanye msichana akakosa raha. Mazoezi na vyakula vyenye chumvi kidogo<br />

husaidia kupunguza maumivu. Kama maumivu yanakuwa makali na damu nyingi sana<br />

inatoka, kamuone mhudumu wa afya.<br />

Mabadiliko Ya Msingi<br />

Katika Kutunza Mwili<br />

Sura hii inazungumzia jinsi ya kutunza afya ya mwili wako kwa ujumla. Hili linaweza kuonekana<br />

kama sio muhimu ukilinganisha na mambo mengine yaliyomo katika kitabu hiki, lakini ni muhimu<br />

kujua jinsi ya kuishi na afya njema. Kwa kweli matatizo mengi ya afya yanaweza kuepukwa kama<br />

ukila vizuri, ukifanya mazoezi, ukiwa msafi na ukijisikia vizuri.<br />

Ni wajibu wako kuangalia mambo haya kila siku, na kuonekana na kujisikia vizuri iwezekanavyo.<br />

Mwili wako ndio utakaokuwa nao katika kipindi chote cha uhai wako. Kwa hiyo unatakiwa<br />

kuutunza kweli kweli!<br />

jiWeKe MSaFi, nuKia ViZuRi.<br />

Kila mtu anataka kuonekana msafi,<br />

lakini kujihisi kuwa na mvuto<br />

inaonekana ni muhimu hususani katika<br />

kipindi cha ujana balehe kwa sababu<br />

ya mabadiliko makubwa yanayotokea<br />

katika mwili. Sio tu mwili unabadilika<br />

umbo wakati wa balehe, lakini vilevile<br />

unaanza kutoa harufu mpya, majimaji<br />

mapya na hofu mpya hasa kwa vijana.<br />

Hivyo kujizoesha kuwa msafi inaweza<br />

kuwa ni njia nzuri ya kujisikia raha ili<br />

kukabiliana na mabadiliko haya yote<br />

yanayotokea.<br />

Oga angalau mara moja kwa siku ili kujisikia<br />

vizuri na safi.<br />

Sandra, kutoka uganda (umri ; miaka 13)<br />

“Siku zote oga, fua na piga pasi nguo ili uonekane nadhifu.”<br />

Usafi mzuri wa mwili hususani wakati wa balehe ni muhimu kwa sababu ngozi yako inaanza<br />

kutoa majimaji zaidi kuliko ilivyokuwa wakati ukiwa mtoto, na baadhi ya haya majimaji yanaweza<br />

kusababisha harufu mbaya kama huogi.<br />

Majimaji utakayoyaona zaidi ni ya jasho. Jasho linatokana na tezi zilizopo kwenye ngozi. Tezi za<br />

jasho zinakuwa hai zaidi wakati unapofikia balehe.<br />

45<br />

SURA YA 5

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!