Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
122<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Kama ikitumika kiusahihi na kwa kukubaliana, kondomu ni kinga<br />
kamili dhidi ya magonjwa ya ngono, ikiwa ni pamoja na VVu na<br />
uzuiaji wa mimba. Kondomu zinazuia vijidudu, bakteria na virusi<br />
vilivyo ndani ya uke kukutana na uume, na huzuia mbegu za kiume,<br />
bakteria na virusi ndani ya shahawa kuingia ukeni.<br />
Ijapokuwa kondomu zinaonekana nyembamba sana,<br />
zimetengengezwa na mpira imara (lateksi) na zimejaribiwa kwa<br />
kutumia nguvu za electroniki ili kuhakikisha kwamba kiwango chake<br />
ni cha juu. Watu wengine wanasema kwamba kondomu zina matundu<br />
madogo sana ambayo yanaweza kupitisha VVU. Hii siyo kweli. VVU<br />
haviwezi kupita kwenye kondomu. Hata hivyo, kondomu inaweza<br />
kuwa na matundu kama muda wa kutumika umekwisha au imetunzwa<br />
vibaya au imewekwa visivyo.<br />
Ni muhimu sana kufuata taratibu za matumizi ya kondomu kila mara<br />
na kila wakati unapozitumia:<br />
1.<br />
2.<br />
3.<br />
4.<br />
Seif, kutoka tanzania(umri wa miaka 13)<br />
“Ngono salama ni kutumia kondomu. Niliyasikia haya kutoka<br />
kwa watu na vilevile kwa kusoma magazeti. Sijawahi kufanya<br />
ngono”.<br />
Sospita, kutoka tanzania(umri wa miaka 13)<br />
“Nimesikia kuhusu kondomu. Nilisoma kwamba zinakukinga<br />
usipate maambukizo ya magonjwa ya ngono na VVU”.<br />
Godfrey, kutoka Zimbabwe(umri wa miaka 19)<br />
“Sina uhakika kama nitafanya mapenzi na mtu yeyote bila ya<br />
kutumia kondomu. Sioni kama hilo linaweza kutokea”.<br />
Chana pembezoni mwa pakiti kwa uangalifu. Usitumie meno na<br />
hakikisha kucha hazichani kondomu.<br />
Usiikunjue kondomu harakaharaka. Iweke kwanza kwenye kiganja<br />
chako na itasimama kama kofia.<br />
Valisha kondomu mara uume unapodinda vizuri na kabla<br />
haujagusa uke. Shika chuchu ya kondomu ukiwa unaiviringisha<br />
chini ya uume. Kondomu inatakiwa iende yenyewe kiurahisi. Kama<br />
haishuki kiurahisi basi jua umeigeuza ndani nje. Itupe kondomu<br />
hiyo na uchukue mpya. Usitumie kondomu iliyogeuzwa ndani nje<br />
kwa sababu inaweza ikawa na shahawa ambazo zina mbegu za<br />
kiume au vijidudu vinavyoambukiza magonjwa ya ngono.<br />
Endelea kushika chuchu ya kondomu wakati unaendelea<br />
kuiviringisha kondomu mpaka uifikishe kwenye shina kabisa. Hii<br />
nafasi ya ziada (chuchu) ni kwa ajili ya shahawa baada ya kukojoa<br />
(kufikia mshindo).<br />
5.<br />
6.<br />
Baada ya kukojoa, shika ukingo wenye bangili wa kondomu na toa<br />
uume toka kwenye uke. Hii itasaidia kuzuia kondomu isiteleze.<br />
Tupa kondomu kwenye choo cha shimo, choma au fukia ardhini.<br />
Usiache kondomu mahali ambapo watoto wataiona na wala usitupe<br />
kwenye choo cha kuvuta maji kwani itaelea.<br />
Yafuatayo ni maelezo zaidi ya jinsi ya kutumia kondomu kwa usahihi ili<br />
zisipasuke na wala zisiteleze na kutoka.<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
SURA YA 10 | KUTUNZA AfYA YAKO YA KIUJINSIA<br />
Angalia juu ya pakiti tarehe ya kwisha matumizi au tarehe ya<br />
kutengenezwa. Kama tarehe ya kwisha matumizi imepita, usiitumie!<br />
Kama tarehe ya kutengeneza ni zaidi ya miaka mitatu iliyopita,<br />
usiitumie! Kumbuka kuwa hata kondomu zinazotumika kuzuia mimba<br />
zisitumike zaidi ya miaka miwili baada ya tarehe ya kutengenezwa.<br />
Kamwe usitumie kondomu ambayo pakiti yake imetoboka. Zaidi ya<br />
hapo usitumie kondomu ambayo ganda lake lina rangi zilizochujuka<br />
au halina rangi kabisa au kama ganda ni gumu limekakamaa au linanata sana.<br />
Tunza kondomu sehemu ambayo kuna ubaridi kiasi, kiza na pakavu. Joto, mwanga na<br />
unyevuunyevu vinaharibu kondomu. Usitunze kondomu kwenye pochi au mfukoni.<br />
Ikiwezekana tumia kondomu zenye vilainishi au tumia vilainishi kama kondomu siyo laini.<br />
Vilainishi vinaweza kusaidia kondomu isipasuke au kuchanika wakati wa kujamiiana. Tumia<br />
vilainishi vyenye asili ya maji tu. Vilainishi vizuri ni pamoja na maji na dawa za kuulia mbegu<br />
za kiume. Majimaji ya ukeni ya asili yanaweza kuwa kilainishi. Kamwe usitumie vilainishi<br />
vyenye asili ya mafuta. Usitumie vaselini, mafuta ya maji (ya kupikia, ya watoto, ya nazi,<br />
petroli), jeli ya petroli, vipodozi vya aina zote, siagi, malai ya kokoa au majarini. Vyote hivi<br />
vinaweza kudhoofisha uimara wa kondomu.<br />
Usikunjue kondomu kabla ya kutumia. Kondomu ambayo imeshakunjuliwa ni vigumu kuivaa.<br />
Tumia kondomu mpya kila unapofanya ngono baada ya mshindo. Kamwe usitumie kondomu<br />
zaidi ya mara moja na usivae zaidi ya moja.<br />
Watu wachache wanadhurika kiafya na mipira aina ya “lateksi”. Hivyo kondomu hizi<br />
zinawasababishia viupele na ngozi kuwasha. Kama unalo tatizo kama hili, zipo kondomu ambazo<br />
hazitengenezwi kwa kutumia mpira wa “lateksi”. Tumia hizo. Zungumza na mhudumu wa afya<br />
namna ya kuzipata.<br />
Watu wengi wanaotumia kondomu wanasema zinawafanya wenza wote wawili wafurahie ngono.<br />
Wenza wote wanaweza kupumzika na kutulia zaidi wanapokuwa hawana hofu ya mimba au<br />
kupata magonjwa ya ngono. Wanaume wengine wanasema kondomu zinawasaidia wasifikie<br />
mshindo “wasikojoe” haraka na kuwafurahisha wenzi wao.<br />
Lakini pia wapo wanaume na wanawake ambao hawapendi kutumia kondomu kwa sababu wana<br />
hofu kuwa hawatafurahia ngono vizuri. Hivyo, mwanaume anaweza kumdanganya mpenzi wake<br />
kwamba hana ugonjwa hivyo kumtaka amwamini na asiwe na sababu yoyote ya kuwa na hofu.<br />
123