08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

122<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Kama ikitumika kiusahihi na kwa kukubaliana, kondomu ni kinga<br />

kamili dhidi ya magonjwa ya ngono, ikiwa ni pamoja na VVu na<br />

uzuiaji wa mimba. Kondomu zinazuia vijidudu, bakteria na virusi<br />

vilivyo ndani ya uke kukutana na uume, na huzuia mbegu za kiume,<br />

bakteria na virusi ndani ya shahawa kuingia ukeni.<br />

Ijapokuwa kondomu zinaonekana nyembamba sana,<br />

zimetengengezwa na mpira imara (lateksi) na zimejaribiwa kwa<br />

kutumia nguvu za electroniki ili kuhakikisha kwamba kiwango chake<br />

ni cha juu. Watu wengine wanasema kwamba kondomu zina matundu<br />

madogo sana ambayo yanaweza kupitisha VVU. Hii siyo kweli. VVU<br />

haviwezi kupita kwenye kondomu. Hata hivyo, kondomu inaweza<br />

kuwa na matundu kama muda wa kutumika umekwisha au imetunzwa<br />

vibaya au imewekwa visivyo.<br />

Ni muhimu sana kufuata taratibu za matumizi ya kondomu kila mara<br />

na kila wakati unapozitumia:<br />

1.<br />

2.<br />

3.<br />

4.<br />

Seif, kutoka tanzania(umri wa miaka 13)<br />

“Ngono salama ni kutumia kondomu. Niliyasikia haya kutoka<br />

kwa watu na vilevile kwa kusoma magazeti. Sijawahi kufanya<br />

ngono”.<br />

Sospita, kutoka tanzania(umri wa miaka 13)<br />

“Nimesikia kuhusu kondomu. Nilisoma kwamba zinakukinga<br />

usipate maambukizo ya magonjwa ya ngono na VVU”.<br />

Godfrey, kutoka Zimbabwe(umri wa miaka 19)<br />

“Sina uhakika kama nitafanya mapenzi na mtu yeyote bila ya<br />

kutumia kondomu. Sioni kama hilo linaweza kutokea”.<br />

Chana pembezoni mwa pakiti kwa uangalifu. Usitumie meno na<br />

hakikisha kucha hazichani kondomu.<br />

Usiikunjue kondomu harakaharaka. Iweke kwanza kwenye kiganja<br />

chako na itasimama kama kofia.<br />

Valisha kondomu mara uume unapodinda vizuri na kabla<br />

haujagusa uke. Shika chuchu ya kondomu ukiwa unaiviringisha<br />

chini ya uume. Kondomu inatakiwa iende yenyewe kiurahisi. Kama<br />

haishuki kiurahisi basi jua umeigeuza ndani nje. Itupe kondomu<br />

hiyo na uchukue mpya. Usitumie kondomu iliyogeuzwa ndani nje<br />

kwa sababu inaweza ikawa na shahawa ambazo zina mbegu za<br />

kiume au vijidudu vinavyoambukiza magonjwa ya ngono.<br />

Endelea kushika chuchu ya kondomu wakati unaendelea<br />

kuiviringisha kondomu mpaka uifikishe kwenye shina kabisa. Hii<br />

nafasi ya ziada (chuchu) ni kwa ajili ya shahawa baada ya kukojoa<br />

(kufikia mshindo).<br />

5.<br />

6.<br />

Baada ya kukojoa, shika ukingo wenye bangili wa kondomu na toa<br />

uume toka kwenye uke. Hii itasaidia kuzuia kondomu isiteleze.<br />

Tupa kondomu kwenye choo cha shimo, choma au fukia ardhini.<br />

Usiache kondomu mahali ambapo watoto wataiona na wala usitupe<br />

kwenye choo cha kuvuta maji kwani itaelea.<br />

Yafuatayo ni maelezo zaidi ya jinsi ya kutumia kondomu kwa usahihi ili<br />

zisipasuke na wala zisiteleze na kutoka.<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

SURA YA 10 | KUTUNZA AfYA YAKO YA KIUJINSIA<br />

Angalia juu ya pakiti tarehe ya kwisha matumizi au tarehe ya<br />

kutengenezwa. Kama tarehe ya kwisha matumizi imepita, usiitumie!<br />

Kama tarehe ya kutengeneza ni zaidi ya miaka mitatu iliyopita,<br />

usiitumie! Kumbuka kuwa hata kondomu zinazotumika kuzuia mimba<br />

zisitumike zaidi ya miaka miwili baada ya tarehe ya kutengenezwa.<br />

Kamwe usitumie kondomu ambayo pakiti yake imetoboka. Zaidi ya<br />

hapo usitumie kondomu ambayo ganda lake lina rangi zilizochujuka<br />

au halina rangi kabisa au kama ganda ni gumu limekakamaa au linanata sana.<br />

Tunza kondomu sehemu ambayo kuna ubaridi kiasi, kiza na pakavu. Joto, mwanga na<br />

unyevuunyevu vinaharibu kondomu. Usitunze kondomu kwenye pochi au mfukoni.<br />

Ikiwezekana tumia kondomu zenye vilainishi au tumia vilainishi kama kondomu siyo laini.<br />

Vilainishi vinaweza kusaidia kondomu isipasuke au kuchanika wakati wa kujamiiana. Tumia<br />

vilainishi vyenye asili ya maji tu. Vilainishi vizuri ni pamoja na maji na dawa za kuulia mbegu<br />

za kiume. Majimaji ya ukeni ya asili yanaweza kuwa kilainishi. Kamwe usitumie vilainishi<br />

vyenye asili ya mafuta. Usitumie vaselini, mafuta ya maji (ya kupikia, ya watoto, ya nazi,<br />

petroli), jeli ya petroli, vipodozi vya aina zote, siagi, malai ya kokoa au majarini. Vyote hivi<br />

vinaweza kudhoofisha uimara wa kondomu.<br />

Usikunjue kondomu kabla ya kutumia. Kondomu ambayo imeshakunjuliwa ni vigumu kuivaa.<br />

Tumia kondomu mpya kila unapofanya ngono baada ya mshindo. Kamwe usitumie kondomu<br />

zaidi ya mara moja na usivae zaidi ya moja.<br />

Watu wachache wanadhurika kiafya na mipira aina ya “lateksi”. Hivyo kondomu hizi<br />

zinawasababishia viupele na ngozi kuwasha. Kama unalo tatizo kama hili, zipo kondomu ambazo<br />

hazitengenezwi kwa kutumia mpira wa “lateksi”. Tumia hizo. Zungumza na mhudumu wa afya<br />

namna ya kuzipata.<br />

Watu wengi wanaotumia kondomu wanasema zinawafanya wenza wote wawili wafurahie ngono.<br />

Wenza wote wanaweza kupumzika na kutulia zaidi wanapokuwa hawana hofu ya mimba au<br />

kupata magonjwa ya ngono. Wanaume wengine wanasema kondomu zinawasaidia wasifikie<br />

mshindo “wasikojoe” haraka na kuwafurahisha wenzi wao.<br />

Lakini pia wapo wanaume na wanawake ambao hawapendi kutumia kondomu kwa sababu wana<br />

hofu kuwa hawatafurahia ngono vizuri. Hivyo, mwanaume anaweza kumdanganya mpenzi wake<br />

kwamba hana ugonjwa hivyo kumtaka amwamini na asiwe na sababu yoyote ya kuwa na hofu.<br />

123

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!