08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

6<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Ukijua unachokithamini itakusaidia kuwa mkweli kwako binafsi, hata wakati mtu mwingine<br />

anapokulazimisha kufanya kitendo unachodhani ni makosa. Maadili yako yatakusaidia kuchagua<br />

lililojema kwako; ambalo wakati mwingine, baada ya kuchagua, itabidi uishi nalo daima.<br />

StaDi Za MaiSha<br />

Unahitaji stadi za maisha pia ili uwe salama. Kusema kweli<br />

“Stadi za maisha” zinaweza kuwa stadi za kuokoa maisha,<br />

kama vile uwezo wa :-<br />

Kuelezea hisia zako. Hisia zako ni muhimu, lakini watu<br />

wengine hawawezi kujua unavyojisikia mpaka uwaeleze.<br />

Jifunze jinsi ya kuwafanya watu wengine wajue kile<br />

unachofikiri na unachokitaka kwa kusema moja kwa<br />

moja na kutumia sentensi zinazoanzia na “mimi” – “mimi<br />

ninataka” “mimi ningelipenda” “mimi ninahitaji”“mimi<br />

Sipendi” ………… .” Fanya mazoezi ya kutumia sentensi<br />

zinazoanza na<br />

“mimi” mpaka utakapozoea na kujisikia huru kuzitumia.<br />

tetea hoja yako. Una uhuru wa kufikiri na kujihisi<br />

unavyopenda. Ni vema kujifunza jinsi ya kuwasilisha<br />

mawazo yako kwa wengine bila ya kuwaudhi au kuwafanya<br />

wajisikie vibaya, usionyeshe uadui, ugomvi wala kukosoa<br />

sana.<br />

tetea unachoamini bila kujali wanayosema watu wengine.<br />

Kila mtu ana imani na yaliyo sahihi na yasiyo sahihi, mazuri<br />

na mabaya. Imani hizi zinaitwa kanuni. Wakati mwingine<br />

unaweza ukawa unajua kanuni zako lakini mambo yanaweza<br />

yasiwe wazi sana kiasi cha kukufanya utumie muda<br />

kufikiria lipi ni sahihi kwako na ni kwa nini.<br />

Iwapo unao uhakika wa usahihi wa kile unachofikiria na kwa<br />

nini unakifanya, na kwa nini hupendelei kukifanya utaweza<br />

kusimama imara na lile unaloamini. Hivyo basi msimamo<br />

wa namna hii utakupa heshima mbele za watu.<br />

jihadhari na yanayotokana na shinikizo.<br />

Kuwa na msimamo wa pekee ndiyo<br />

stadi za <strong>Maisha</strong>.<br />

Jinsi unavyoelekea kwenye utu uzima unatakiwa kufanya maamuzi mengi peke yako. Wakati<br />

mwingine watu wengine wanaweza kukuhimiza na kukusukuma kufanya maamuzi fulani na<br />

ukushawishika kufanya hivyo.<br />

Lakini ufahamu kuwa kufanya maamuzi mazuri maana yake ni kupima chaguo zote zilizopo na<br />

kufikiria matokeo kwa kila chaguo.Inaweza ikawa kazi ngumu iwapo kuna mtu anakuharakisha au<br />

anakushinikiza uamue haraka. Kitu muhimu katika kufanya maamuzi bora ni kuwa na uhakika wa<br />

kanuni zako na malengo yako ya maisha kwa ujumla.<br />

SURA YA 1 | UJANA BALEHE: BADILIKO KUBWA CHANGAMOTO KUBWA<br />

Jambo lingine la muhimu katika kufanya<br />

maamuzi ni kujipa muda wa kutosha.<br />

Kumbuka,unaweza kumueleza mtu kwamba<br />

“ninahitaji kufikiria zaidi kuhusu jambo hili na<br />

nisubiri nitakujibu”<br />

Stadi hizi za maisha zina majina yake, kama<br />

vile “kuongea bila woga wala jazba”<br />

“Mawazo yenye ubunifu” “Kutatua matatizo”,<br />

“Kufanya maamuzi” na“Kujitambua”.<br />

Stadi za maisha ni muhimu sana. Ukweli ni<br />

kwamba stadi za maisha ni muhimu kama<br />

ilivyo kuufahamu “ukweli.” Kuufahamu “ukweli<br />

wa mambo” peke yake hakuwezi kukulinda<br />

hadi uwe pia na stadi za maisha. Kwa mfano<br />

unaweza ukafahamu kwamba kujamiiana bila<br />

kinga kunaweza kukusababisha mimba na<br />

magonjwa ya zinaa ikiwa ni pamoja na VVU/<br />

UKIMWI. Vilevile unaweza ukawa umeamua<br />

kwamba hutaki kujamiiana, lakini bado ukawa<br />

huna uwezo wa kujieleza na kutetea hoja zako<br />

kwa rafiki yako wa kiume.<br />

Unahitaji Stadi za maisha ili uutumie<br />

ukweli unaoufahamu kusimama imara<br />

katika yale unayoyataka na kuyaamini,<br />

hasa pale inapotokea watu unaowajali na<br />

kuwaheshimuwanatofautiana na wewe.<br />

je, unazo Stadi za maisha? Unaweza<br />

ukasimama imara na kuwa na msimamo kwa<br />

yale unayoyaamini kuwa ni sahihi hata kama<br />

marafiki zako wanawaza tofauti? Unao ujasiri<br />

wa kutosha kutetea afya yako au maisha<br />

yako? Anza kuzitumia stadi zako kadri<br />

unavyoendelea kusoma kitabu hiki.<br />

Kufanya maamuzi mazuri na kusimama imara kwa<br />

unachokiamini ni stadi bora za maisha<br />

7

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!