Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
142<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Hata hivyo, njia pekee nzuri ya kujikinga ni kuacha kujamiiana au kuacha zinaa. Lakini kama<br />
unavyoweza kuona hapo juu, yeyote ambaye anajamiiana, njia nzuri ya kuzuia mimba ni kutumia<br />
vipandikizi, sindano na kondomu.<br />
Stabisile kutoka Zimbabwe (umri wa miaka 19)<br />
“Kama mwanamume anakataa kutumia kondomu, huyo anapoteza<br />
muda.<br />
” cathy kutoka uganda (umri wa miaka 17)<br />
“Ninapendekeza matumizi ya kondomu ili kukwepa maambukizo<br />
ya VVU/UKIMWI, magonjwa ya zinaa na kuzuia mimba<br />
zisizotakiwa”.<br />
Kondomu ni nzuri kwa kuzuia mimba, na zinakusaidia kukukinga wewe na mwenzi wako dhidi ya<br />
magonjwa ya zinaa/UKIMWI. Unaweza kufanya ziwe kinga nzuri zaidi kwa kuchanganya vidonge<br />
na njia nyingine ya kuzuia mimba.<br />
iwapo yeyote anasema hataki kutumia kondomu jiandae kwa jibu zuri! na jiandae kuondoka kama<br />
atakataa kutumia kondomu.<br />
Sura ya 11<br />
Mimba na uzuiaji wa mimba<br />
Wakati wote mwanaume na mwanamke wakijamiiana bila kinga, mimba inaweza kutokea.<br />
Mimba inaweza ikatokea mara ya kwanza tu mnapojamiiana bila kinga.<br />
Mimba inaweza kutungwa kama mbegu moja inakutana na yai na kulirutubisha ndani ya<br />
mwanamke. Kama yai litarutubishwa, linajishikiza kwenye kuta za mfuko wa kizazi. Huu ndio<br />
mwanzo wa mimba.<br />
Dalili za mimba ni pamoja na:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Kukosa siku zako za hedhi<br />
Kujaa na kuuma kwa matiti<br />
Kichefuchefu<br />
Kuwa mchovu<br />
SURA YA 11 | MIMBA NA UZUIAJI WA MIMBA<br />
Kutaka kukojoa mara kwa mara.<br />
Mimba ni hatari hasa kwa wasichana balehe kwa sababu miili yao bado haijakomaa.<br />
Wasichana wadogo wanakabiliwa na matatizo makubwa ya afya wakati wa mimba na wakati<br />
wa kuzaa kuliko wanawake wa makamo. Kwa hiyo, ni jambo la muhimu hasa kwa msichana<br />
mdogo kupata matunzo sahihi wakati wa mimba. Inashauriwa kuzalia hospitalini mahali<br />
ambapo kuna wahudumu wa afya wa kutosha na vifaa vinavyoweza kumudu matatizo yoyote<br />
ya uzazi.<br />
Wasichana balehe wengi wanapata mimba kwa makosa. Wanaamua kutoa mimba kwasababu<br />
wanataka kuendelea na shule au kwa sababu hawataki kuwaaibisha wazazi wao. Hata hivyo,<br />
katika nchi nyingi za Afrika kutoa mimba ni kinyume cha sheria na si salama hata kidogo.<br />
Kutoa mimba kusiko salama kunaweza kusababisha matatizo makubwa kiafya, kuanzia<br />
maambukizo ya magonjwa, uharibu wa via vya uzazi, kuvuja damu sana, ugumba na vifo. njia<br />
sahihi ya kukwepa mimba ni kuacha ngono. Kuacha kabisa ni salama kwa asilimia 100.<br />
Iwapo unashiriki kujamiiana, wewe na mwenzi wako mnatakiwa wakati wote kujikinga dhidi<br />
ya mimba na magonjwa ya ngono pamoja na VVU/UKIMWI. Njia zote za kuzuia mimba ni<br />
salama kwa vijana.<br />
Kama umesahau kutumia kinga ya mimba au kama kondomu itatoka au kupasuka, nenda<br />
haraka kwenye kliniki waombe kinga ya dharura ya kuzuia mimba. Inaweza kuzuia mimba<br />
ikiwa itatumika katika kipindi cha saa 72 cha kujamiiana bila kinga.<br />
Mimba inahusu watu wawili yaani mwanamume na mwanamke. Wavulana na wanaume pia<br />
watu wazima, wote wanalo jukumu la kuzuia mimba.<br />
143