08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

142<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Hata hivyo, njia pekee nzuri ya kujikinga ni kuacha kujamiiana au kuacha zinaa. Lakini kama<br />

unavyoweza kuona hapo juu, yeyote ambaye anajamiiana, njia nzuri ya kuzuia mimba ni kutumia<br />

vipandikizi, sindano na kondomu.<br />

Stabisile kutoka Zimbabwe (umri wa miaka 19)<br />

“Kama mwanamume anakataa kutumia kondomu, huyo anapoteza<br />

muda.<br />

” cathy kutoka uganda (umri wa miaka 17)<br />

“Ninapendekeza matumizi ya kondomu ili kukwepa maambukizo<br />

ya VVU/UKIMWI, magonjwa ya zinaa na kuzuia mimba<br />

zisizotakiwa”.<br />

Kondomu ni nzuri kwa kuzuia mimba, na zinakusaidia kukukinga wewe na mwenzi wako dhidi ya<br />

magonjwa ya zinaa/UKIMWI. Unaweza kufanya ziwe kinga nzuri zaidi kwa kuchanganya vidonge<br />

na njia nyingine ya kuzuia mimba.<br />

iwapo yeyote anasema hataki kutumia kondomu jiandae kwa jibu zuri! na jiandae kuondoka kama<br />

atakataa kutumia kondomu.<br />

Sura ya 11<br />

Mimba na uzuiaji wa mimba<br />

Wakati wote mwanaume na mwanamke wakijamiiana bila kinga, mimba inaweza kutokea.<br />

Mimba inaweza ikatokea mara ya kwanza tu mnapojamiiana bila kinga.<br />

Mimba inaweza kutungwa kama mbegu moja inakutana na yai na kulirutubisha ndani ya<br />

mwanamke. Kama yai litarutubishwa, linajishikiza kwenye kuta za mfuko wa kizazi. Huu ndio<br />

mwanzo wa mimba.<br />

Dalili za mimba ni pamoja na:<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

Kukosa siku zako za hedhi<br />

Kujaa na kuuma kwa matiti<br />

Kichefuchefu<br />

Kuwa mchovu<br />

SURA YA 11 | MIMBA NA UZUIAJI WA MIMBA<br />

Kutaka kukojoa mara kwa mara.<br />

Mimba ni hatari hasa kwa wasichana balehe kwa sababu miili yao bado haijakomaa.<br />

Wasichana wadogo wanakabiliwa na matatizo makubwa ya afya wakati wa mimba na wakati<br />

wa kuzaa kuliko wanawake wa makamo. Kwa hiyo, ni jambo la muhimu hasa kwa msichana<br />

mdogo kupata matunzo sahihi wakati wa mimba. Inashauriwa kuzalia hospitalini mahali<br />

ambapo kuna wahudumu wa afya wa kutosha na vifaa vinavyoweza kumudu matatizo yoyote<br />

ya uzazi.<br />

Wasichana balehe wengi wanapata mimba kwa makosa. Wanaamua kutoa mimba kwasababu<br />

wanataka kuendelea na shule au kwa sababu hawataki kuwaaibisha wazazi wao. Hata hivyo,<br />

katika nchi nyingi za Afrika kutoa mimba ni kinyume cha sheria na si salama hata kidogo.<br />

Kutoa mimba kusiko salama kunaweza kusababisha matatizo makubwa kiafya, kuanzia<br />

maambukizo ya magonjwa, uharibu wa via vya uzazi, kuvuja damu sana, ugumba na vifo. njia<br />

sahihi ya kukwepa mimba ni kuacha ngono. Kuacha kabisa ni salama kwa asilimia 100.<br />

Iwapo unashiriki kujamiiana, wewe na mwenzi wako mnatakiwa wakati wote kujikinga dhidi<br />

ya mimba na magonjwa ya ngono pamoja na VVU/UKIMWI. Njia zote za kuzuia mimba ni<br />

salama kwa vijana.<br />

Kama umesahau kutumia kinga ya mimba au kama kondomu itatoka au kupasuka, nenda<br />

haraka kwenye kliniki waombe kinga ya dharura ya kuzuia mimba. Inaweza kuzuia mimba<br />

ikiwa itatumika katika kipindi cha saa 72 cha kujamiiana bila kinga.<br />

Mimba inahusu watu wawili yaani mwanamume na mwanamke. Wavulana na wanaume pia<br />

watu wazima, wote wanalo jukumu la kuzuia mimba.<br />

143

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!