08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

104<br />

uaMuZi Wa KutOFanYa nGOnO<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Vijana wengi wanachagua kutofanya ngono kwa sababu nzuri sana zifuatazo:<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

Wanaogopa kupata mimba na magonjwa ya ngono virusi vya UKIMWI na UKIMWI wenyewe<br />

na hawapendi kuhatarisha maisha yao.<br />

Bado ni wadogo mno hivyo wanajiona hawako tayari.<br />

Hawataki kuwaudhi wazazi wao.<br />

Wanaona tendo hilo ni kinyume cha maadili ya dini zao.<br />

Wako tayari kusubiri ili kushughulikia masomo yao.<br />

Wanataka kuhakikisha kuwa rafiki yake wa kiume au wa kike anampenda kikweli.<br />

Iwapo unakabiliwa na uamuzi wa kufanya ngono, kumbuka kwamba ngono inaweza kuwa na<br />

matokeo mabaya kama kuambukizwa VVU au mimba zisizotakiwa.Mambo haya yanaweza<br />

kukuharibia maisha yako milele. Unahitaji kufikiri kwa makini uamuzi wako. Kumbuka kuwa:<br />

•<br />

•<br />

•<br />

Kusubiri ndiyo njia nzuri na salama ya kubakia na afya.<br />

Unayo haki ya kusema “hapana” kwa ngono na kushikilia uamuzi wako.<br />

Ukiamua kusema “ndio” kwa ngono, lazima ujizoeze kufanya ngono salama ili kukwepa<br />

mimba, VVU, UKIMWI na magonjwa ya ngono. “Bila kondomu, hakuna ngono”.<br />

KuZunGuMZa na MWenZi WaKO KuhuSu nGOnO<br />

andrew, kutoka tanzania (umri wa miaka 17)<br />

“Mimi na marafiki zangu tunazungumza kuhusu ngono.<br />

Tunazungumza pia athari za ngono,kwa mfano iwapo<br />

msichana atapata mimba,tutapata matatizo makubwa,<br />

tutalazimishwa kuoa au kufukuzwa shule!”<br />

halima, kutoka Kenya (umri wa miaka 17)<br />

“Sababu nzuri sana za kuchelewa kufanya ngono ni kusubiri<br />

kupata mtu atakayefaa na kusubiri mpaka mnaoana.”<br />

Maamuzi kuhusu ngono yanahusu watu wawili na yanahitaji mawasiliano mazuri na makini. Ni<br />

jambo muhimu kumweleza wenzi wako kitu unachofanya na kitu ambacho hutaki kukifanya.<br />

Watu wengi wanajisikia vibaya na aibu kuzungumza<br />

masuala ya ngono, lakini mambo haya yanakuwa rahisi<br />

baada ya muda na kuyafanyia mazoezi. Hapa kuna<br />

baadhi ya vidokezo:<br />

•<br />

Fikiri ni kwa nini unataka au hutaki kufanya<br />

chochote: Jua sababu zako ni zipi ili uweze<br />

kuzieleza wazi kwa mwezi wako.<br />

• Fanya mazoezi kabla: Kama huna uhakika<br />

utazungumza nini kuhusu kujamiiana na rafiki<br />

yako wa kike au kiume jaribu kuzungumza na<br />

rafiki wa karibu unayemwamini au mshauri wa<br />

vijana kwanza. Waulize jinsi ya kulizungumzia<br />

suala hilo. Pata maoni ya namna ya<br />

kushughulikia hali hii.<br />

•<br />

SURA YA 9 | UJINSIA NA NGONO<br />

chagua muda mzuri na mahali muafaka:<br />

Chagua muda mzuri wa kuzungumza na rafiki<br />

yako wa kiume au wa kike, muda ambao kila<br />

mmoja wenu hana shughuli ya mambo mengine<br />

na wakati ambapo wote mnajisikia mmetulia<br />

na mmestarehe. Ni vizuri pia kuchagua sehemu nzuri. Chagua sehemu ambayo hutajali<br />

hata watu wengine wakiwasikia. Wakati huo huo chagua sehemu ambayo siyo ya kificho<br />

sana ambayo itamfanya msichana wako au mvulana wako apate wasiwasi na kupata<br />

mawazo potofu.<br />

• usingoje mpaka umepata joto la mahaba ndio uanze kuzungumzia ngono: Ni vigumu<br />

sana kuwa na mazungumzo kuhusu kujamiiana wakati mmoja au wote mnajisikia<br />

mmesisimka na katika hali ya kufanya ngono. Hakikisha mnazungumza aina gani<br />

ya mapenzi mnayataka kabla wewe na mwenzi wako kujikuta katika hali ya kuvutia<br />

kimapenzi.<br />

• Kuwa mkweli kuhusu unavyojisikia na jinsi unavyoona. Usiwatumie watu au sababu<br />

mbalimbali kama kisingizio. Kwa mfano kama hutaki kufanya ngono kwa sababu<br />

unataka kwanza kuolewa, usimwambie rafiki yako kwamba sitaki kufanya ngono kwa<br />

sababu naogopa kupata mimba au kwa sababu unaogopa kwamba mama atagundua.<br />

Ukimwambia rafiki yako wa kiume visingizio hivyo atafikiri kwamba unataka utumie<br />

kondomu au unataka uende kwake.Ili kukwepa kutoeleweka, kuwa muwazi na eleza<br />

moja kwa moja hisia zako.<br />

• Simama imara na usikubali kushinikizwa: Hata watu ambao unawaheshimu sana<br />

wanaweza kukushinikiza ufanye vitu ambavyo hutaki kuvifanya. Inaweza kuwa vigumu<br />

sana kuhimili shinikizo kwa sababu ni mtu unayempenda unataka awe na furaha.<br />

Kumbuka hata hivyo kwamba mtu anayekupenda hapaswi kufanya mambo ambayo<br />

yatakukosesha raha. Kama rafiki yako wa kiume au kike anakushinikiza pengine ni<br />

kwa sababu hawajui unajisikiaje au kwa sababu hawajali hisia zako kama ambavyo<br />

inawapasa. Simama kidete, na hakikisha wanaelewa unachokitaka.<br />

105

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!