Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
160<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Ni rahisi kuanza kunywa pombe na usiifikirie sana kuhusu jambo hilo. Lakini fikiria tena! Pombe<br />
ni dawa ya kulevya kama dawa nyingine za kulevya. Pombe inadumaza mfumo wa mwili. Baada<br />
ya kunywa pombe kidogo, matendo yako yanaweza yakawa ya taratibu na inaweza ikakuwia<br />
vigumu kufikiri vizuri. Ukiongeza kidogo tena, unashindwa kusema vizuri na unaweza kuwa mkali<br />
na mchokozi. Kama siyo mzoefu wa pombe au kama unakunywa sana unaweza kutapika sana au<br />
ukapoteza fahamu.<br />
Athari za muda mrefu za unywaji sana pombe ni mbaya. Nadhani unawafahamu watu katika<br />
jamii ambao ni walevi sana na ambao hawawezi kuishi bila kunywa. Unaweza ukawa umeona jinsi<br />
inavyoharibu familia, watu kupoteza kazi, na inasababisha afya kuwa mbaya, kama kuharibu<br />
ubongo na kuleta ugonjwa wa ini.<br />
Pombe ni dawa ya kulevya maarufu sana<br />
ambayo inawafanya watu wastarehe na<br />
kusahau taabu zao. Hata hivyo, kujiona<br />
umestarehe mno na kutojitambua si jambo<br />
zuri kwani kunaweza kukufanya upate<br />
matatizo.<br />
Pombe kama ilivyo kwa dawa nyingine za<br />
kubadili hali ya mtu, inaondoa uwezo wa<br />
kujizuia na mambo unayoona yatakutia aibu<br />
mbele ya wenzio. Pombe inakupa ujasiri wa<br />
kuzungumza mambo ambayo baadaye utakuja<br />
yajutia.<br />
Kwa mfano, wasichana wengi wakiwa<br />
hawajanywa hawana ujasiri wa kwenda kwa<br />
mwanaume na kumbusu kwenye mdomo lakini<br />
msichana akiwa amekunywa pombe anaweza<br />
kujisikia huru sana; anajisikia kumbusu<br />
mvulana na anafanya hivyo.<br />
Pombe inaweza pia kumfanya mvulana afanye<br />
vitu ambavyo kwa kawaida asingelifanya. Kwa<br />
mfano, mvulana anaweza akaamua kutaka<br />
kujamiiana na msichana baada ya kunywa<br />
pombe. Hata kama rafiki yake wa kike anataka<br />
au hataki, anaweza kujaribu kumlazimisha<br />
kujamiiana naye. Pombe inamfanya asiweze<br />
kumfikiria rafiki yake wa kike anavyojisikia;<br />
inamfanya pia asiweze kufikiria matokeo ya<br />
jambo analotaka kutenda.<br />
Unapokunywa pombe, sheria zinazotawala<br />
tabia yako ya kawaida zinapungua. Uwezo<br />
wako wa kuamua mambo mazuri unapungua.<br />
Kwa hiyo, unapoteza uwezo wa kupima<br />
mambo. Kijana mmoja anasema haya kuhusu<br />
pombe:<br />
Pombe inaathiri uwezo wako wa kufanya<br />
uamuzi salama<br />
lazarus kutoka Zambia (umri wa miaka 15)<br />
“Ninapokunywa ninasahau hatari zote zinazonizunguka. Ninasahau kila<br />
kitu kuhusu kondomu. Hivyo huwa ninafanya ngono bila kinga kwa sababu<br />
ya kishawishi cha pombe. Ninajua nina uwezekano wa kuambukizwa.”<br />
Iwapo kinywaji cha kawaida kama pombe kinaweza kukuletea matatizo makubwa kama hayo,<br />
hebu fikiria kinachoweza kutokea kama ukitumia dawa kali zaidi kama kokeni.<br />
KutaWaliWa na DaWa<br />
Kadiri mtu anavyoanza mapema kutumia dawa, ndivyo anavyojiwekea nafasi ya kujenga matatizo<br />
makubwa yanayohusiana na dawa baadaye. Athari za dawa nyingi zinaongezeka kadiri muda<br />
unavyopita. Athari zinajijenga mwilini, kama bomu lililotegwa kwa muda maalumu likisubiri muda<br />
ufike lilipuke.<br />
Kuna dalili nyingi zinazojitokeza matumizi ya dawa zinapofikia kuwa matatizo makubwa.<br />
Dalili hizo ni:-<br />
•<br />
Je, unajua kwamba matumizi ya dawa za kulevya zina matatizo ya kipekee kwa<br />
wanawake na wasichana?<br />
Wakati dawa za kulevya zote zina madhara mwilini, nyingi zinawaathiri zaidi wanawake<br />
na wasichana kuliko wanaume. Kwa mfano, kuvuta sigara kunaleta madhara ya pekee kwa<br />
wanawake. Kunaweza:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
SURA YA 13 | MATUMIZI MABAYA YA DAWA<br />
Kuleta matatizo ya kiafya kama mwanamke anatumia vidonge vya kuzuia mimba.<br />
Kupunguza miaka ya mwanamke ya kuzaa watoto kwa sababu tukio la hedhi kukoma<br />
litatokea mapema<br />
Kuongeza hatari ya mwanamke kupata saratani ya mlango wa mfuko wa kizazi na tumbo<br />
la uzazi.<br />
Kusababisha mifupa ya mwanamke kuwa dhaifu.<br />
Kusababisha iwe vigumu kwa mwanamke kupata mimba.<br />
Kuongeza hatari ya mimba kutoka kwa mwanamke mjamzito.<br />
Kufanya mwanamke azae mtoto mdogo sana au mtoto azaliwe mapema kabla ya wakati.<br />
Kumeza dawa na kunywa pombe wakati mwanamke ana mimba ni hatari kwa sababu inaweza<br />
kusababisha matatizo makubwa ya kiafya na ya mtoto kuzaliwa na kasoro, kama kuundwa<br />
vibaya kwa moyo, mifupa, kichwa na viungo muhimu vya ndani. Mtoto pia anaweza kuzaliwa<br />
na uzito mdogo, kukua taratibu na kutokuwa na uwezo wa kujifunza darasani. Matumizi<br />
mabaya ya dawa wakati wa ujauzito yanaweza kusababisha uzae mtoto ambaye tayari<br />
ameathirika na dawa na hivyo kuzoeleka mwilini mwake.<br />
Kumbuka, ukiwa unatumia dawa wakati wa ujauzito, mtoto wako pia anapata kiwango<br />
kikubwa kuliko wewe. Athari kwa mtoto zitakuwa kubwa zaidi kuliko kwako.<br />
Kuongopa kuhusu kiasi cha dawa unachotumia. Hii ni pamoja na kujidanganya mwenyewe<br />
kiasi gani cha dawa au pombe unayotumia.<br />
161