08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

160<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Ni rahisi kuanza kunywa pombe na usiifikirie sana kuhusu jambo hilo. Lakini fikiria tena! Pombe<br />

ni dawa ya kulevya kama dawa nyingine za kulevya. Pombe inadumaza mfumo wa mwili. Baada<br />

ya kunywa pombe kidogo, matendo yako yanaweza yakawa ya taratibu na inaweza ikakuwia<br />

vigumu kufikiri vizuri. Ukiongeza kidogo tena, unashindwa kusema vizuri na unaweza kuwa mkali<br />

na mchokozi. Kama siyo mzoefu wa pombe au kama unakunywa sana unaweza kutapika sana au<br />

ukapoteza fahamu.<br />

Athari za muda mrefu za unywaji sana pombe ni mbaya. Nadhani unawafahamu watu katika<br />

jamii ambao ni walevi sana na ambao hawawezi kuishi bila kunywa. Unaweza ukawa umeona jinsi<br />

inavyoharibu familia, watu kupoteza kazi, na inasababisha afya kuwa mbaya, kama kuharibu<br />

ubongo na kuleta ugonjwa wa ini.<br />

Pombe ni dawa ya kulevya maarufu sana<br />

ambayo inawafanya watu wastarehe na<br />

kusahau taabu zao. Hata hivyo, kujiona<br />

umestarehe mno na kutojitambua si jambo<br />

zuri kwani kunaweza kukufanya upate<br />

matatizo.<br />

Pombe kama ilivyo kwa dawa nyingine za<br />

kubadili hali ya mtu, inaondoa uwezo wa<br />

kujizuia na mambo unayoona yatakutia aibu<br />

mbele ya wenzio. Pombe inakupa ujasiri wa<br />

kuzungumza mambo ambayo baadaye utakuja<br />

yajutia.<br />

Kwa mfano, wasichana wengi wakiwa<br />

hawajanywa hawana ujasiri wa kwenda kwa<br />

mwanaume na kumbusu kwenye mdomo lakini<br />

msichana akiwa amekunywa pombe anaweza<br />

kujisikia huru sana; anajisikia kumbusu<br />

mvulana na anafanya hivyo.<br />

Pombe inaweza pia kumfanya mvulana afanye<br />

vitu ambavyo kwa kawaida asingelifanya. Kwa<br />

mfano, mvulana anaweza akaamua kutaka<br />

kujamiiana na msichana baada ya kunywa<br />

pombe. Hata kama rafiki yake wa kike anataka<br />

au hataki, anaweza kujaribu kumlazimisha<br />

kujamiiana naye. Pombe inamfanya asiweze<br />

kumfikiria rafiki yake wa kike anavyojisikia;<br />

inamfanya pia asiweze kufikiria matokeo ya<br />

jambo analotaka kutenda.<br />

Unapokunywa pombe, sheria zinazotawala<br />

tabia yako ya kawaida zinapungua. Uwezo<br />

wako wa kuamua mambo mazuri unapungua.<br />

Kwa hiyo, unapoteza uwezo wa kupima<br />

mambo. Kijana mmoja anasema haya kuhusu<br />

pombe:<br />

Pombe inaathiri uwezo wako wa kufanya<br />

uamuzi salama<br />

lazarus kutoka Zambia (umri wa miaka 15)<br />

“Ninapokunywa ninasahau hatari zote zinazonizunguka. Ninasahau kila<br />

kitu kuhusu kondomu. Hivyo huwa ninafanya ngono bila kinga kwa sababu<br />

ya kishawishi cha pombe. Ninajua nina uwezekano wa kuambukizwa.”<br />

Iwapo kinywaji cha kawaida kama pombe kinaweza kukuletea matatizo makubwa kama hayo,<br />

hebu fikiria kinachoweza kutokea kama ukitumia dawa kali zaidi kama kokeni.<br />

KutaWaliWa na DaWa<br />

Kadiri mtu anavyoanza mapema kutumia dawa, ndivyo anavyojiwekea nafasi ya kujenga matatizo<br />

makubwa yanayohusiana na dawa baadaye. Athari za dawa nyingi zinaongezeka kadiri muda<br />

unavyopita. Athari zinajijenga mwilini, kama bomu lililotegwa kwa muda maalumu likisubiri muda<br />

ufike lilipuke.<br />

Kuna dalili nyingi zinazojitokeza matumizi ya dawa zinapofikia kuwa matatizo makubwa.<br />

Dalili hizo ni:-<br />

•<br />

Je, unajua kwamba matumizi ya dawa za kulevya zina matatizo ya kipekee kwa<br />

wanawake na wasichana?<br />

Wakati dawa za kulevya zote zina madhara mwilini, nyingi zinawaathiri zaidi wanawake<br />

na wasichana kuliko wanaume. Kwa mfano, kuvuta sigara kunaleta madhara ya pekee kwa<br />

wanawake. Kunaweza:<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

SURA YA 13 | MATUMIZI MABAYA YA DAWA<br />

Kuleta matatizo ya kiafya kama mwanamke anatumia vidonge vya kuzuia mimba.<br />

Kupunguza miaka ya mwanamke ya kuzaa watoto kwa sababu tukio la hedhi kukoma<br />

litatokea mapema<br />

Kuongeza hatari ya mwanamke kupata saratani ya mlango wa mfuko wa kizazi na tumbo<br />

la uzazi.<br />

Kusababisha mifupa ya mwanamke kuwa dhaifu.<br />

Kusababisha iwe vigumu kwa mwanamke kupata mimba.<br />

Kuongeza hatari ya mimba kutoka kwa mwanamke mjamzito.<br />

Kufanya mwanamke azae mtoto mdogo sana au mtoto azaliwe mapema kabla ya wakati.<br />

Kumeza dawa na kunywa pombe wakati mwanamke ana mimba ni hatari kwa sababu inaweza<br />

kusababisha matatizo makubwa ya kiafya na ya mtoto kuzaliwa na kasoro, kama kuundwa<br />

vibaya kwa moyo, mifupa, kichwa na viungo muhimu vya ndani. Mtoto pia anaweza kuzaliwa<br />

na uzito mdogo, kukua taratibu na kutokuwa na uwezo wa kujifunza darasani. Matumizi<br />

mabaya ya dawa wakati wa ujauzito yanaweza kusababisha uzae mtoto ambaye tayari<br />

ameathirika na dawa na hivyo kuzoeleka mwilini mwake.<br />

Kumbuka, ukiwa unatumia dawa wakati wa ujauzito, mtoto wako pia anapata kiwango<br />

kikubwa kuliko wewe. Athari kwa mtoto zitakuwa kubwa zaidi kuliko kwako.<br />

Kuongopa kuhusu kiasi cha dawa unachotumia. Hii ni pamoja na kujidanganya mwenyewe<br />

kiasi gani cha dawa au pombe unayotumia.<br />

161

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!