08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

84<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Katika kipindi cha ujana balehe, ni jambo la kawaida kuona vijana wakiwa katika makundi ya<br />

kirafiki, wakilazimika kufanya mambo fulani fulani katika kundi hilo au kuwa na mtazamo fulani<br />

kama unataka kujiunga au kubaki katika kundi hilo. . Jihadhari na shinikizo la kundi rika kwani<br />

lina nguvu sana kwa sababu unataka kupendwa na unataka kuwa sehemu ya kikundi; na unataka<br />

kuwafurahisha marafiki zako ndani ya kikundi na unataka kuhakikisha hubaki nyuma.<br />

Wakati wote hakikisha akili yako iko sawasawa na<br />

unakuwa mkweli. Usijihatarishe ati kwa sababu unataka<br />

kuwa na kundi la marafiki.<br />

Jambo jingine la kukumbuka: Unaweza ukatokea<br />

wakati fulani kipindi cha ujana ukajisikia kama vile<br />

huna marafiki wa karibu. Hii inaweza kukufanya ujisikie<br />

mpweke, mwenye huzuni na wasi wasi. Usihofu kuwa<br />

una tatizo lolote. Inawezekana wewe umekomaa kidogo<br />

kuliko wenzako wa umri mmoja. Labda unataka mambo<br />

tofauti na rafiki zako wa rika moja. Jinsi utakavyo kuwa<br />

unakua na kukutana na watu wapya, utatengeneza<br />

marafiki wazuri na wa nguvu. Kuwa mvumilivu. Ipo siku.!<br />

KueleWana na jinSia nYinGine<br />

Vijana wengi wanapata shida kuelewana na mtu wa<br />

jinsi nyingine. Hawajui jinsi ya kutendeana kwa heshima na inavyofaa, na hawajui wafanye nini<br />

wanapokuwa wamezungukwa na watu wa jinsi nyingine. Vifuatavyo ni vidokezo kwa wavulana:<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

Usimwangalie au kumpigia mlunzi msichana kwa sababu ya jinsi anavyoonekana, gauni<br />

alilovaa au namna anayotembea.<br />

Msikilize rafiki yako wa kike anachosema na elewa anaposema “hapana” ana maanisha<br />

“Hapana” na sio vinginevyo. Usijaribu kujishawishi mwenyewe kwamba anamaanisha “labda”<br />

au “ndio” wakati anaposema hapana.<br />

Usipitepite karibu na msalani wa wasichana na/au kuziba njia yao.<br />

Usiwanyanyase au kuwatisha kwa makusudi wasichana usiku au sehemu zisizo na watu.<br />

Usivumishe mambo mabaya kuhusu wasichana.<br />

Wasichana vile vile wanaweza kuwa na mtazamo mbaya kwa wavulana. Vifuatavyo ni<br />

vidokezo vya jinsi ya kuelewana na wavulana:<br />

Usiwatafute wavulana ili upate pesa au zawadi kutoka kwao.<br />

Wakati mwingine vijana wa rika lako<br />

wanaweza kukutenga kwenye kundi lao. hii<br />

inaweza kuwa vigumu na unaweza kufikiri<br />

ufanye lolote ili ujiunge nao. Kuwa mkweli<br />

na usijihatarishe kwa ajili ya kupata<br />

heshima yao.<br />

Kubali kwamba wavulana nao wanashawishika na wanazo hisia kama zako. Usiwacheke,<br />

kuwatania au kuwafanyia mzaha.<br />

Kuwa muwazi kwa wavulana. Yaweke wazi yale unayotaka kuyafanya na yale ambayo hutaki<br />

kuyafanya. Sema yale ambayo kweli unayafikiria na usiogope kujieleza. Kuwa na uhakika,<br />

jiamini, kama hutaki kufanya jambo fulani sema “HAPANA” na ng’ang’ania hivyo hivyo.<br />

•<br />

SURA YA 8 | URAfIKI NA MApENZI<br />

Usianzishe uzushi kuhusu wavulana.<br />

Mara nyingi wasichana na wavulana wanaishia katika mahusiano mabaya kwa sababu hawana<br />

uelewa na uzoefu wa namna ya kuishi na jinsia nyingine. Wavulana hawajui wasichana<br />

wanataka nini kutoka kwa wavulana na wasichana vile vile hawajui wavulana wanataka nini<br />

kutoka wasichana. Hapa kuna vidokezo vichache vitakavyokusaidia:<br />

• Wasichana wanataka upendo, kujaliwa, uaminifu na heshima. Wasichana wanapata<br />

hofu kama wavulana hawawaheshimu. Wanapenda wavulana wanaotumia muda kuwasikiliza<br />

bila mzaha.<br />

• Kuwa pamoja: Wasichana wanaona kwamba kuwa pamoja na kujumuika na wavulana<br />

kunafurahisha na kusisimua. Pia wanawapenda wavulana ambao wanaweza kuwasaidia<br />

wanapopata matatizo na ambao wanaweza kustarehe, kutaniana na kucheka nao.<br />

• uhuru: Wasichana wanataka kupewa nafasi ya kufikiri wenyewe.Wanawapenda wavulana<br />

wanaotambua kwamba wasichana wana akili na wanapenda kuzitumia.<br />

• Wavulana wanaojiamini: Wasichana wanawahusudu wavulana ambao wanajiamini na<br />

ambao hawawaogopi wasichana.<br />

• Wavulana wasiojifanya: Wasichana wanawapenda wavulana ambao hawaigi wengine<br />

na kujifanya wana hali fulani kumbe sio. Wavulana wanataka nini? Wavulana wengi wanayataka<br />

yale yote ambayo wasichana wanayataka katika mahusiano.<br />

• Wavulana wanataka upendo, kujaliwa, uaminifu na heshima. Wavulana wengi wanapenda<br />

kuwa na msichana anayejali na kusaidia – mtu anayesikiliza, aliye na heshima na<br />

asiye na mzaha<br />

• Kuwa pamoja: Kila mtu anapenda kujumuika. Wasichana na wavulana pia wanataka mtu<br />

ambaye wanaweza kutumia muda naye kucheka, kusimuliana hadithi na kuzungumza<br />

kuhusu maoni yao, ndoto na hata malengo.<br />

• uhuru: Wavulana wengi wanasukumwa kutenda mambo kinguvu. Wanatenda kama vile<br />

hawana hisia na hawajisikii kitu. Wanataka mtu ambaye wanaweza kushirikiana naye<br />

kimawazo na kihisia.<br />

• Wasichana wanaojiamini: Tofauti na ambavyo wasichana wengi wanavyoamini, wavulana<br />

wanawapenda wasichana wanaojiamini– wasichana ambao hawaogopi kujieleza<br />

wenyewe kwa uhuru.<br />

• Wasichana wasiojifanya: Wavulana wanawapenda wasichana ambao ni halisi - wasichana<br />

ambao hawaigi mambo ya wengine kama kukomaa, kujisikia au kuringa.<br />

Msingi wa mahusiano mazuri ni urafiki wa nguvu – sio tu jinsi mtu anavyoonekana au mvuto<br />

wa kimapenzi. Katika uhusiano mzuri, hakuna mtu anayejaribu kumdhibiti mwenzake au<br />

kumlazimisha katika kufanya mambo. Pia hakuna mtu ambaye anamnyonya mwenzake au<br />

kumtumia mwenzie kwa namna yoyote ile.<br />

Kumbuka kuwa mahusiano mazuri na ya kudumu hayaji katika muda mfupi. Inachukua muda<br />

kufahamiana kikweli kweli na kujenga urafiki wa nguvu.<br />

KUANZA MAHUSIANO NA MTU UNAYEMPENDA.<br />

Ujana balehe ni wakati ambao unaweza kuanza kujisikia una hamu au unavutiwa na watu<br />

wengine. Unaweza kumuona mtu shuleni kwako ambaye anaonekana mzuri na unafikiria<br />

ungependa muwe marafiki.<br />

85

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!