Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
116<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
VVu VinainGiaje MWilini?<br />
Njia kuu inayoeneza VVU ni kujamiiana na mgusano wa moja kwa moja na majimaji ya mwilini.<br />
Katika Afrika, zaidi ya asilimia 90 ya watu wanaoambukizwa VVU wanaambukizwa kwa njia<br />
ya kujamiiana. Ni rahisi sana kwa mwanamume kumwambukiza mwanamke kuliko mwanamke<br />
kumwambukiza mwanamume. Hii ni kwa sababu ngozi na misuli ya uke, kuzunguka kinembe na<br />
kuzunguka mashavu ya nje ya uke ni laini sana. Ngozi hii inapata michubuko, vidonda na kuchanika.<br />
Michaniko na michubuko ni midogo sana kiasi kwamba huwezi kuona kwa macho, lakini ni mikubwa<br />
kutosha VVU kupita kama ngozi laini inagusana na shahawa kutoka kwa mwanaume ambaye ana<br />
maambukizo.<br />
Mwanamume anapofanya ngono na mwanamke aliye na maambukizo ya VVU yuko hatarini vilevile<br />
kupata maambukizo. Uume unakutana na majimaji ya ukeni ambayo yana VVU. Kama mwanamke<br />
ana VVU, vinasafiri kupitia kwenye mrija wa uume. Iwapo hajatahiriwa VVU vinaweza kupita<br />
kwenye ngozi hii laini hususani kama vipo vidonda, michubuko au mikato.<br />
VVU vinaweza kuenea kwa njia nyingine vilevile. Njia hizi ni pamoja na:<br />
•<br />
•<br />
Mama kwa mtoto wakati wa mimba, au wakati wa kujifungua au wakati wa kunyonyesha.<br />
Mgusano wa damu ya mtu ambaye ana maambukizi. Inawezekana ikawa wakati wa kuongezewa<br />
damu, kujikata na kisu cha kuchangia au wakati watu wanaotumia dawa za kulevya<br />
wanachangia sindano.<br />
Siku hizi damu inayotumika kuwaongezea wagonjwa inachunguzwa kwa makini kuhakikisha<br />
kwamba haina maambukizo.Hata hivyo, sherehe nyingi za kimila kama kutahiri na kukata vitu<br />
mwilini zinaendelea kutumia njia ambazo siyo salama kama vile kuchangia kisu kimoja au wembe<br />
kwa watu wote wanaotegemewa kufanyiwa. Kamwe usichangie wembe na ndugu zako au marafiki<br />
zako na wala usichangie visu visivyochemshwa wakati wa sherehe ya kutahiri au tukio lolote la<br />
kimila.<br />
Bado haijathibitishwa kama mtu anaweza kupata VVU kupitia kwenye mate wakati wa kubusu.<br />
Hata hivyo, iwapo mtu ana mkato/kidonda mdomoni anaweza kupata maambukizo kwa kumbusu<br />
mtu ambaye anayo maambukizo ya VVU na anavyo vidonda vilevile. Kwa vile VVU vipo ndani ya<br />
shahawa na majimaji ya ukeni, kujamiiana kwa njia ya mdomoni hakuepushi hatari. Iwapo mtu ana<br />
mchubuko au kidonda mdomoni na wakati huohuo akapata shahawa au majimaji ya ukeni mdomoni,<br />
anaweza kupata VVU .<br />
VVU havienei kwa kugusana kwa kawaida kama vile kukumbatiana, kushikana mikono au kumgusa<br />
mtu mwenye maambukizo. VVU vinaishi kwa muda mfupi sana vinapokuwa nje ya mwili, kwa hiyo<br />
haviwezi kuenezwa kwa njia ya kumgusa mtu aliye na maambukizo au kuchangia vitu – kama beseni,<br />
vyombo vya kulia chakula, nguo, vitabu n.k.<br />
Wengi wetu tunao wagonjwa wenye UKIMWI ndani ya familia zetu na tunatakiwa kuwatunza<br />
wanapougua. Ni muhimu unapomhudumia mgonjwa kujikinga ili usipate maambukizo. Unachotakiwa<br />
kuhofia ni majimaji ya mwilini kama vile, majimaji yanayotoka kwenye vidonda, damu ya hedhi na<br />
uharo. Jilinde mwenyewe kwa kuvaa glovu unapomsaidia kuoga au unaposafisha kitu chochote<br />
chenye damu au majimaji yoyote ya mwilini.<br />
utajuaje KaMa una VVu?<br />
Huwezi kujua kwa kujiangalia mwili. Huwezi kutambua kama watu wengine wana VVU kwa<br />
kuwaangalia. Hata kama watu wana UKIMWI – walipata maambukizo ya VVU muda mrefu na<br />
wamekuwa wagonjwa – huwezi kujua kama ni UKIMWI kwa kuwaangalia labda kama wewe ni<br />
SURA YA 10 | KUTUNZA AfYA YAKO YA KIUJINSIA<br />
mhudumu wa afya. Hii ni kwa sababu<br />
magonjwa mengi yanayoambatana<br />
na UKIMWI yanaweza kujitokeza<br />
yenyewe kwa watu ambao hawana<br />
VVU. Kwa mfano, unaweza kuugua<br />
kifua kikuu ukiwa na VVU au<br />
usipokuwa navyo.<br />
Ipo njia moja tu ya kujua kama una<br />
VVU. Katika nchi nyingi upimaji<br />
wa VVU unaambatana na ushauri<br />
nasaha – majadiliano ya undani na<br />
mtu aliyesomea, mwenye huruma<br />
na ambaye anaweza kukusaidia<br />
ili uweze kumudu hali yako ya<br />
kuwa na VVU na kujifunza jinsi<br />
ya kujihudumia. Kama hujapata<br />
maambukizo, mshauri anaweza kukuelimisha ufanye hadhari ili usipate maambukizo.<br />
Vipimo vya UKIMWI vinaaminika ni sahihi, salama na haviumi. Mhudumu wa afya anachukua<br />
damu kidogo kutoka kwenye mkono wako. Unaweza kupata majibu katika muda wa saa moja, au<br />
unaweza kuambiwa urudi baada ya wiki<br />
moja au mbili kutegemeana na kipimo<br />
Vipimo vya VVU vinafanyaje kazi?<br />
kinachotumika.<br />
Ili kujua kama ni kweli huna VVU,<br />
utaambiwa urudi kupima tena baada<br />
ya miezi 3 hadi 6 wakati kipindi cha<br />
kusubiri kimepita.<br />
KWa nini uPiMe VVu?<br />
Zipo sababu nyingi za kupima VVU.<br />
Iwapo mara kwa mara unakuwa na hofu<br />
kuhusu maambukizo ya VVU na una<br />
wasiwasi kutokana na mabadiliko ya<br />
afya yako mara kwa mara inawezekana<br />
njia pekee ya kutuliza akili ni kupima.<br />
Iwapo ulifanya ngono na mtu ambaye<br />
anaumwa na umesikia ana UKIMWI,<br />
hapo utahofu zaidi. Labda njia pekee<br />
ya kutuliza akili ni kupima na kujua<br />
kama umepata maambukizo au la.<br />
Kamwe usidhani kwamba umepata<br />
maambukizo, pima ili ujue.<br />
Mtu yeyote anaweza akawa ameambukizwa VVu<br />
bila kuwa na dalili. usitegemee muonekano wa<br />
mtu kuamua kuwa fulani hana VVu.<br />
Mtu anapokuwa na maambukizo mwili hushituka<br />
na kutoa askari ili kupigana na maambukizo.<br />
Kipimo cha VVU kimetengenezwa kutambua kama<br />
askari wa VVU wapo au hawapo ndani ya mwili wa<br />
binadamu. Ikiwa wapo wengi, maana yake mtu huyo<br />
ana maambukizo ya VVU na kwamba mwili unajaribu<br />
kupigana na maambukizo.<br />
Kwa kawaida askari wanaopimwa na kipimo<br />
cha VVU huonekana mwezi mmoja baada ya<br />
maambukizo. Hata hivyo, mara nyingi askari wa<br />
VVU hutokea baada ya muda zaidi – kama miezi<br />
3 hadi miezi 6 baada ya maambukizo. Katika<br />
kipindi hiki kipimo cha VVU hakitaona askari. Kwa<br />
maneno mengine, miezi 3 mpaka miezi 6 baada ya<br />
maambukizo, mtu anaweza kupima na kuonekana<br />
hana maambukizo ingawa anayo maambukizo.<br />
Vile vile, mtu huyu anaweza kuambukiza watu<br />
wengine katika kipindi hiki kabla askari wa VVU<br />
hawajaonekana kwenye kipimo.<br />
Kwa hiyo,- kama mtu yuko hatarini kupata VVU<br />
na akapima na kuonekana hana VVU, bado<br />
anashauriwa kurudia baada ya miezi 6 ili kuwa na<br />
uhakika kama hana maambukizo.<br />
117