08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

116<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

VVu VinainGiaje MWilini?<br />

Njia kuu inayoeneza VVU ni kujamiiana na mgusano wa moja kwa moja na majimaji ya mwilini.<br />

Katika Afrika, zaidi ya asilimia 90 ya watu wanaoambukizwa VVU wanaambukizwa kwa njia<br />

ya kujamiiana. Ni rahisi sana kwa mwanamume kumwambukiza mwanamke kuliko mwanamke<br />

kumwambukiza mwanamume. Hii ni kwa sababu ngozi na misuli ya uke, kuzunguka kinembe na<br />

kuzunguka mashavu ya nje ya uke ni laini sana. Ngozi hii inapata michubuko, vidonda na kuchanika.<br />

Michaniko na michubuko ni midogo sana kiasi kwamba huwezi kuona kwa macho, lakini ni mikubwa<br />

kutosha VVU kupita kama ngozi laini inagusana na shahawa kutoka kwa mwanaume ambaye ana<br />

maambukizo.<br />

Mwanamume anapofanya ngono na mwanamke aliye na maambukizo ya VVU yuko hatarini vilevile<br />

kupata maambukizo. Uume unakutana na majimaji ya ukeni ambayo yana VVU. Kama mwanamke<br />

ana VVU, vinasafiri kupitia kwenye mrija wa uume. Iwapo hajatahiriwa VVU vinaweza kupita<br />

kwenye ngozi hii laini hususani kama vipo vidonda, michubuko au mikato.<br />

VVU vinaweza kuenea kwa njia nyingine vilevile. Njia hizi ni pamoja na:<br />

•<br />

•<br />

Mama kwa mtoto wakati wa mimba, au wakati wa kujifungua au wakati wa kunyonyesha.<br />

Mgusano wa damu ya mtu ambaye ana maambukizi. Inawezekana ikawa wakati wa kuongezewa<br />

damu, kujikata na kisu cha kuchangia au wakati watu wanaotumia dawa za kulevya<br />

wanachangia sindano.<br />

Siku hizi damu inayotumika kuwaongezea wagonjwa inachunguzwa kwa makini kuhakikisha<br />

kwamba haina maambukizo.Hata hivyo, sherehe nyingi za kimila kama kutahiri na kukata vitu<br />

mwilini zinaendelea kutumia njia ambazo siyo salama kama vile kuchangia kisu kimoja au wembe<br />

kwa watu wote wanaotegemewa kufanyiwa. Kamwe usichangie wembe na ndugu zako au marafiki<br />

zako na wala usichangie visu visivyochemshwa wakati wa sherehe ya kutahiri au tukio lolote la<br />

kimila.<br />

Bado haijathibitishwa kama mtu anaweza kupata VVU kupitia kwenye mate wakati wa kubusu.<br />

Hata hivyo, iwapo mtu ana mkato/kidonda mdomoni anaweza kupata maambukizo kwa kumbusu<br />

mtu ambaye anayo maambukizo ya VVU na anavyo vidonda vilevile. Kwa vile VVU vipo ndani ya<br />

shahawa na majimaji ya ukeni, kujamiiana kwa njia ya mdomoni hakuepushi hatari. Iwapo mtu ana<br />

mchubuko au kidonda mdomoni na wakati huohuo akapata shahawa au majimaji ya ukeni mdomoni,<br />

anaweza kupata VVU .<br />

VVU havienei kwa kugusana kwa kawaida kama vile kukumbatiana, kushikana mikono au kumgusa<br />

mtu mwenye maambukizo. VVU vinaishi kwa muda mfupi sana vinapokuwa nje ya mwili, kwa hiyo<br />

haviwezi kuenezwa kwa njia ya kumgusa mtu aliye na maambukizo au kuchangia vitu – kama beseni,<br />

vyombo vya kulia chakula, nguo, vitabu n.k.<br />

Wengi wetu tunao wagonjwa wenye UKIMWI ndani ya familia zetu na tunatakiwa kuwatunza<br />

wanapougua. Ni muhimu unapomhudumia mgonjwa kujikinga ili usipate maambukizo. Unachotakiwa<br />

kuhofia ni majimaji ya mwilini kama vile, majimaji yanayotoka kwenye vidonda, damu ya hedhi na<br />

uharo. Jilinde mwenyewe kwa kuvaa glovu unapomsaidia kuoga au unaposafisha kitu chochote<br />

chenye damu au majimaji yoyote ya mwilini.<br />

utajuaje KaMa una VVu?<br />

Huwezi kujua kwa kujiangalia mwili. Huwezi kutambua kama watu wengine wana VVU kwa<br />

kuwaangalia. Hata kama watu wana UKIMWI – walipata maambukizo ya VVU muda mrefu na<br />

wamekuwa wagonjwa – huwezi kujua kama ni UKIMWI kwa kuwaangalia labda kama wewe ni<br />

SURA YA 10 | KUTUNZA AfYA YAKO YA KIUJINSIA<br />

mhudumu wa afya. Hii ni kwa sababu<br />

magonjwa mengi yanayoambatana<br />

na UKIMWI yanaweza kujitokeza<br />

yenyewe kwa watu ambao hawana<br />

VVU. Kwa mfano, unaweza kuugua<br />

kifua kikuu ukiwa na VVU au<br />

usipokuwa navyo.<br />

Ipo njia moja tu ya kujua kama una<br />

VVU. Katika nchi nyingi upimaji<br />

wa VVU unaambatana na ushauri<br />

nasaha – majadiliano ya undani na<br />

mtu aliyesomea, mwenye huruma<br />

na ambaye anaweza kukusaidia<br />

ili uweze kumudu hali yako ya<br />

kuwa na VVU na kujifunza jinsi<br />

ya kujihudumia. Kama hujapata<br />

maambukizo, mshauri anaweza kukuelimisha ufanye hadhari ili usipate maambukizo.<br />

Vipimo vya UKIMWI vinaaminika ni sahihi, salama na haviumi. Mhudumu wa afya anachukua<br />

damu kidogo kutoka kwenye mkono wako. Unaweza kupata majibu katika muda wa saa moja, au<br />

unaweza kuambiwa urudi baada ya wiki<br />

moja au mbili kutegemeana na kipimo<br />

Vipimo vya VVU vinafanyaje kazi?<br />

kinachotumika.<br />

Ili kujua kama ni kweli huna VVU,<br />

utaambiwa urudi kupima tena baada<br />

ya miezi 3 hadi 6 wakati kipindi cha<br />

kusubiri kimepita.<br />

KWa nini uPiMe VVu?<br />

Zipo sababu nyingi za kupima VVU.<br />

Iwapo mara kwa mara unakuwa na hofu<br />

kuhusu maambukizo ya VVU na una<br />

wasiwasi kutokana na mabadiliko ya<br />

afya yako mara kwa mara inawezekana<br />

njia pekee ya kutuliza akili ni kupima.<br />

Iwapo ulifanya ngono na mtu ambaye<br />

anaumwa na umesikia ana UKIMWI,<br />

hapo utahofu zaidi. Labda njia pekee<br />

ya kutuliza akili ni kupima na kujua<br />

kama umepata maambukizo au la.<br />

Kamwe usidhani kwamba umepata<br />

maambukizo, pima ili ujue.<br />

Mtu yeyote anaweza akawa ameambukizwa VVu<br />

bila kuwa na dalili. usitegemee muonekano wa<br />

mtu kuamua kuwa fulani hana VVu.<br />

Mtu anapokuwa na maambukizo mwili hushituka<br />

na kutoa askari ili kupigana na maambukizo.<br />

Kipimo cha VVU kimetengenezwa kutambua kama<br />

askari wa VVU wapo au hawapo ndani ya mwili wa<br />

binadamu. Ikiwa wapo wengi, maana yake mtu huyo<br />

ana maambukizo ya VVU na kwamba mwili unajaribu<br />

kupigana na maambukizo.<br />

Kwa kawaida askari wanaopimwa na kipimo<br />

cha VVU huonekana mwezi mmoja baada ya<br />

maambukizo. Hata hivyo, mara nyingi askari wa<br />

VVU hutokea baada ya muda zaidi – kama miezi<br />

3 hadi miezi 6 baada ya maambukizo. Katika<br />

kipindi hiki kipimo cha VVU hakitaona askari. Kwa<br />

maneno mengine, miezi 3 mpaka miezi 6 baada ya<br />

maambukizo, mtu anaweza kupima na kuonekana<br />

hana maambukizo ingawa anayo maambukizo.<br />

Vile vile, mtu huyu anaweza kuambukiza watu<br />

wengine katika kipindi hiki kabla askari wa VVU<br />

hawajaonekana kwenye kipimo.<br />

Kwa hiyo,- kama mtu yuko hatarini kupata VVU<br />

na akapima na kuonekana hana VVU, bado<br />

anashauriwa kurudia baada ya miezi 6 ili kuwa na<br />

uhakika kama hana maambukizo.<br />

117

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!