08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

92<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Sura ya 8<br />

urafiki na mapenzi<br />

Urafiki mzuri na mahusiano mazuri yanakusaidia ujisikie vizuri. Marafiki wazuri<br />

wanakusaidia kutatua matatizo, kukuonyesha mawazo mapya na kushiriki na wewe<br />

katika ndoto za maisha yako ya baadaye.<br />

Wakati mwingine watu unaofikiria ni marafiki zako wanaweza kukushinikiza kufanya<br />

jambo ambalo hulitaki, kama vile kujamiiana au kula madawa ya kulevya. Hii tunaita<br />

shinikizo la kundi rika. Mtu yeyote anayekushinikiza ufanye jambo ambalo hutaki<br />

kulifanya sio rafiki mzuri. Usiruhusu mtu yeyote akakushinikiza ufanye jambo ambalo<br />

unajua ni makosa na ni hatari kwako.<br />

Marafiki wazuri wanaweza wakawa wa jinsi moja au jinsi nyingine. Wavulana na wasichana<br />

wanaweza kuwa marafiki bila ya kuwa na mahusiano ya kimapenzi. Maneno<br />

“rafiki wa kiume” au “rafiki wa kike” sio lazima yamaanishe kwamba mahusiano ni ya<br />

kimapenzi. Marafiki wa jinsi tofauti wanaweza kuwa na urafiki wa karibu na kupendana<br />

sana bila ya ngono.<br />

Inaweza ikawa vigumu kuelewana na mtu wa jinsi nyingine kwa sababu wavulana na<br />

wasichana hawana uhakika nini mwingine anataka katika mahusiano. Kumbuka, watu<br />

wengi – wavulana na wasichana – wanataka mambo yanayofanana katika mahusiano.<br />

Wanataka heshima, uaminifu, ukweli, kuelewana na kujali.<br />

Kama unamtaka msichana au mvulana unayempenda, jaribu kuvuta subira na kuwa<br />

mkweli. Kuwa mwema. Toka, nenda ukamwone. Kama anaelekea kupenda nia yako,<br />

mwombe kama mnaweza kwenda kushiriki shughuli fulani kwa pamoja.<br />

Kujenga mahusiano mazuri kunachukua muda na uvumilivu. Ngono sio njia nzuri ya<br />

kujenga mahusiano. Ukweli ni kwamba ngono inaweza kuharibu mahusiano. Kujamiiana<br />

haina maana ya kwamba watu wawili wanapendana au urafiki wao ni wa karibu sana.<br />

Ngono bila urafiki wa kweli ni hatari kwa afya yako na moyo wako.<br />

Kumpenda mtu ni jambo nzuri sana, mapenzi yanakufanya ujisikie vizuri mwenyewe na<br />

mtu mwingine. Furahia hisia lakini usikimbilie jambo lolote. Kumbuka mapenzi yanahusu<br />

heshima na kujaliana. Mapenzi hata siku moja yasiwe sababu ya kufanya jambo<br />

ambalo litaweka afya na maisha yako ya baadaye hatarini. Mapenzi hayawezi kuwa<br />

kisingizio cha kufanya ngono isiyo salama.<br />

Mahusiano hayadumu milele. Kama ukiachwa, sio vizuri kulazimisha mahusiano. Kuwa<br />

mkweli kwa rafiki yako, lakini kuwa na huruma na umfikirie pia. Jaribu usiumize hisia<br />

zake.<br />

Kama mtu amekuacha, unaweza kuhuzunika sana na kujisikia mpweke. Lakini usikate<br />

tamaa. Siku moja utampata mtu mwingine sahihi wa kumpenda. Jipe muda wa kustahimili<br />

ulichopoteza. Usikimbilie mahusiano mapya na usieneze uzishi kuhusu mtu huyo.<br />

Ujinsia Na Ngono<br />

Kuna utata mwingi sana kuhusu neno ujinsia (sexuality) na kujamiiana. Watu wengi wanafikiri<br />

ujinsia maana yake ni kujamiiana. Wengine wanafikiri kwamba huwezi kuwa binadamu hai<br />

mwenye ujinsia na mwenye hisia za kimapenzi hadi uanze kujamiiana.<br />

Imani hizi si za kweli; kila mtu anao ujinsia tangu<br />

kuzaliwa hadi kufa.<br />

Kuwa na ujinsia kunaweza kumaanisha:<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

Kujisikia unavutia na mwili wako<br />

umejengeka vizuri.<br />

Kujisikia mwenye hisia za kuwa karibu na<br />

mtu fulani.<br />

Kufurahia kuguswa na kukumbatiwa.<br />

Kujishika mwili wako mwenyewe.<br />

Kuvutiwa na mtu mwingine.<br />

Kufikiria hadithi za kimapenzi akilini<br />

mwako.<br />

Kuwa na mawazo au hisia za kimapenzi.<br />

Wakati wa ujana balehe ndio muda ambao<br />

unaweza kuutambua zaidi ujinsia wako -<br />

unavyojisikia, unavyofikiri, unavyojiheshimu<br />

kama mvulana au msichana, na unachokitaka<br />

kuhusu uhusiano wa karibu au pendo la mtu.<br />

Ulipokuwa mdogo pengine hukufikiria kuhusu<br />

mambo haya lakini wakati wa ujana, unaweza<br />

kuanza kufahamu maana ya kuwa mwanaume<br />

au mwanamke. Pia unaweza kuanza kuvutiwa<br />

na watu wengine na kuanza kuona hisia za<br />

kimapenzi, matamanio na ndoto.<br />

UNAJUA maana ya “Ujinsia”?<br />

Ujinsia ni suala lenye utata kueleweka. Ni<br />

zaidi ya kujisikia hisia za kimapenzi au<br />

kujamiiana. Ujinsia ni pamoja na:<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

Kufahamu na kuwa na hisia kuhusiana<br />

na mwili wako na miili ya watu wengine.<br />

Uwezo wako na nia ya kuwa karibu na<br />

mtu mwingine.<br />

Uelewa wako kuhusu nini maana ya<br />

kuwa mwanamke au mwanaume.<br />

Hisia za mvutano wa kijinsia na watu<br />

wengine.<br />

Uwezo wako kimwili wa kuzaa.<br />

Ujinsia ni muhimu, unafurahisha, na ni<br />

sehemu ya asili ya kuwa mtu. Lakini wakati<br />

mwingine watu wanatumia ujinsia wao<br />

katika namna isiyofaa kwa kushawishi,<br />

kuamuru au kutania watu wengine. Hii ni<br />

pamoja na kuonyesha mapenzi kwa mzaha,<br />

upotoshaji na unyanyasaji kijinsia kama<br />

kubaka/kunajisi n.k. Usitumie ujinsia kama<br />

kifaa cha kupata kitu au kunyanyasa au<br />

kumuumiza mwingine.<br />

93<br />

SURA YA 9

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!