08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

66<br />

Kutatua tatizo na kufikiri kwa<br />

ubunifu: Ili kupata ufumbuzi wa<br />

matatizo kunahitaji kufikiri kwa<br />

ubunifu. Kufikiri kwa ubunifu ni uwezo<br />

wa kufikiri ufumbuzi wa tatizo usio<br />

wazi. Ni uwezo wa kusumbua akili<br />

yako ili kupata fumbuzi mbalimbali<br />

bila kujiwekea mipaka ya mazoea<br />

uliyoyasikia ya utatuzi wa jambo fulani.<br />

Kwa mfano: fikiria kuwa umepata<br />

mimba ukiwa unasoma shule. Wasichana<br />

wote unaowafahamu waliopata mimba<br />

waliacha shule na hawakuweza kumaliza<br />

masomo. Kufikiria kwa ubunifu maana<br />

yake ni kutokudhani kwamba lazima<br />

uache shule eti kwasababu wasichana<br />

wengine waliacha. Labda inawezekana<br />

ukakaa shuleni ukiwa na mimba. Au<br />

unaweza kurudi shuleni baada ya<br />

kujifungua mtoto. Labda kipo kituo kwa<br />

ajili ya vijana waliozaa ambako unaweza<br />

kuendelea na masomo au mafunzo.<br />

Kufikiri kwa ubunifu kunahusisha<br />

kuzungumza na watu wengine. (walimu,<br />

vijana washauri wazazi, shangazi,<br />

wajomba marafiki) na kuchunguza<br />

chaguzi zote zilizoko mbele yako.<br />

Stadi za makubaliano. Hizi ni stadi<br />

ambazo unahitaji ili kutatua tatizo au<br />

tofauti ulizonazo na watu wengine.<br />

Kwa mfano, unaweza ukataka kutoka<br />

na rafiki yako, lakini wazazi wako<br />

wanataka ukae nyumbani. Hali kama<br />

hii inahitaji stadi nzuri za makubaliano.<br />

Inaweza ikawa vigumu kukubaliana<br />

na wakati wingine kukatishwa tamaa.<br />

Unaweza kujisikia kama upasuke,<br />

kwamba umevunjika moyo kiasi cha<br />

kusema “potelea mbali” na kuondoka<br />

ukiwa umekasirika na kuchoshwa.<br />

Lakini unahitaji kuwa mvumilivu na<br />

mtulivu wakati unaeleza kwa nini<br />

unajisikia hivyo, na kile unachohitaji.<br />

Vilevile unahitaji kuwa mkweli, mtu<br />

unayeelewa na kuheshimu yale ambayo<br />

watu wengine wanayahisi na kuyahitaji.<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Je, unajua maana ya kutatua tatizo kwa<br />

ubunifu bila woga wala jazba?<br />

Anne ana umri wa miaka 16 na ni yatima.<br />

Anaishi na shangazi yake ambaye anamtaka<br />

afanye kazi dukani kwake kila siku baada ya<br />

kutoka shule. Hili ni tatizo kubwa kwa Anne.<br />

Hapati muda wa kutosha wa kujisomea.<br />

Ameanza kufadhaika kwa vile mitihani<br />

inakaribia. Hapati usingizi vizuri usiku kwa<br />

sababu ana wasiwasi sana kuhusu masomo.<br />

Ameanza kumchukia shangazi yake.<br />

Anashangaa iwapo shangazi yake anamwona<br />

kama kitendea kazi na kwamba hampendi<br />

wala kujali maisha yake ya baadaye.<br />

Anne anajitambua. Anajua kuwa anayo<br />

tabia ya kuficha hisia zake mpaka<br />

anapolipuka kwa hasira. Tabia hii haimsaidii<br />

sana. Shangazi yake naye anakasirika na<br />

kusema ameanza kukosa heshima.Safari hii<br />

anaamua kufanya mambo tofauti. Badala<br />

ya kumwambia shangazi yake kiugomvi<br />

“Hunipendi” anamweleza shangazi yake bila<br />

woga wala jazba “Ninawasiwasi sana kuhusu<br />

mitihani yangu lakini nataka pia kukusaidia<br />

kazi za dukani”. Hapa ameonyesha tabia ya<br />

kujiamini.<br />

Kwa kujieleza mwenyewe kwa njia hii,<br />

Anne amesimama imara na kuomba<br />

muda zaidi wa kujisomea. Lakini kwa<br />

wakati huo huo anaelewa shangazi yake<br />

anahitaji msaada wa dukani. Anaonyesha<br />

ushirikiano kwa shangazi yake ambaye ana<br />

majukumu mengine. Akifuata utaratibu huu,<br />

shangazi naye anaelewa pia. Kwa pamoja<br />

wanafikiri kwa ubunifu kutatua tatizo hili.<br />

Wanatengeneza ratiba inayompa Anne muda<br />

zaidi wa kujisomea jioni na pia kumsaidia<br />

shangazi yake jioni inapokuwa lazima.<br />

Inatia moyo kwa jinsi Anne alivyojisikia<br />

vizuri. Ghafla mfadhaiko unapungua na<br />

anaweza kuyafurahia maisha tena.<br />

Hata hivyo sio kila tatizo linaweza kujadiliwa na kufikia maelewano. Wakati mwingine<br />

utalenga katika matokeo ambayo yatakufanya uwe salama, hata kama mtu mwingine<br />

hatafurahia. Mathalani, rafiki yako wa kike au wa kiume amekataa kutumia kondomu<br />

pamoja na kumshawishi kwa nguvu zote. Katika hali kama hii zingatia usalama wako.<br />

Ondoka sehemu hiyo ikibidi.<br />

Msimamo: Msimamo ni stadi ya msingi katika kuelewana na watu wengine. Msimamo<br />

maana yake kutetea na kuyaenzi yale unayoyaamini wewe mwenyewe. Kuwa muwazi na<br />

mwaminifu kwako mwenyewe na watu wengine kuhusu kile unachokihitaji na kukitaka.<br />

Watu ambao hawana msimamo juu ya maisha yao huwa ni wanyenyekevu. Hata kama<br />

wanatendewa vibaya, hawajitetei. Watu ambao hawana msimamo mara kwa mara<br />

wanakosa imani ya kujienzi na kutetea mahitaji yao na kulinda hisia zao au hata miili yao ili<br />

wasiumizwe.<br />

Msimamo ni tofauti sana na kuwa mgomvi. Watu wagomvi ni watundu na hawana huruma,<br />

hawajali watu wengine wanahisi nini. Sio vizuri kuwa mgomvi kwa faida ya afya ya hisia<br />

kwa sababu, kwa undani kabisa, utajisikia vibaya kutokuwa na huruma kwa wengine.<br />

Misingi ya msimamo:<br />

SURA YA 6 | UTUNZAJI AfYA YA AKILI NA MOYO<br />

• amua unachohisi au unachotaka na kiseme. Usiogope kuwa mkweli kuhusu hisia<br />

zako. Watu wanatakiwa kuziheshimu hisia hizo. Kwa mfano, labda ulijisikia vibaya na<br />

unakosa raha baada ya rafiki yako wa kiume kukugusa sehemu zako za siri. Unatakiwa<br />

kumwambia, “Nilikosa raha uliponigusa sehemu zangu za siri sitaki uniguse hivyo tena”.<br />

Mtu anayekupenda kweli hatataka kufanya vitendo ambavyo vinakukosesha raha.<br />

• Mtazame mtu machoni: Kumwangalia mtu machoni ni kudhihirisha msimamo wako.<br />

Inamjulisha mtu mwingine kwamba hutanii kuhusu kile unachokisema na kwamba<br />

unaangalia kama wanakusikiliza au hawakusikilizi. Tamaduni nyingi haziungi mkono<br />

kumwangalia mtu machoni wakati wa mazungumzo. Wakati mwingine katika maeneo<br />

mengine huliona jambo hili ni ufedhuli (kutokuwa na ustaarabu/heshima) kijana<br />

mdogo anapomwangalia mtu mzima moja kwa moja usoni. Unaweza kufuata mila na<br />

desturi, kama kupiga magoti, kuonyesha heshima lakini kwa wakati huo huo endelea<br />

kumwangalia mtu huyo usoni kama unataka kuonyesha ujasiri/msimamo wako.<br />

• usitoe visingizio. Hisia zako ni sababu tosha. Kwa mfano, kama hujisikii kufanya<br />

mapenzi lakini rafiki yako wa kike au kiume anakulazimisha, epuka kutumia watu<br />

wengine kama kisingizio. Usiseme, “mama yangu karibu atarudi nyumbani au tumbo<br />

linaniuma au ninaogopa kupata mimba au nina kazi ya kusoma kwa hiyo sio muda mzuri<br />

kwangu”. Unaweza ukamchanganya rafiki yako na visingizio hivi. Anaweza kudhani<br />

unataka kwenda sehemu nyingine, au kwamba labda unataka kutumia kondomu.<br />

Anaweza asitambue kwamba unachotaka kumwambia ni “siko tayari kufanya tendo hilo<br />

kwa hiyo sitaki”. Kwa hiyo basi sema kile unachotaka.<br />

• usisemewe na mtu mwingine. Iwapo hutaki kufanya jambo fulani, sema mwenyewe<br />

na usiulize mtu mwingine kama ni sawa. Kwa mfano, kama mtu ana kushawishi unywe<br />

pombe au madawa ya kulevya usiseme; “nisingependa, lakini kama unaona sawa …?<br />

Badala yake sema “Hapana, ninashukuru.<br />

67

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!