Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
66<br />
Kutatua tatizo na kufikiri kwa<br />
ubunifu: Ili kupata ufumbuzi wa<br />
matatizo kunahitaji kufikiri kwa<br />
ubunifu. Kufikiri kwa ubunifu ni uwezo<br />
wa kufikiri ufumbuzi wa tatizo usio<br />
wazi. Ni uwezo wa kusumbua akili<br />
yako ili kupata fumbuzi mbalimbali<br />
bila kujiwekea mipaka ya mazoea<br />
uliyoyasikia ya utatuzi wa jambo fulani.<br />
Kwa mfano: fikiria kuwa umepata<br />
mimba ukiwa unasoma shule. Wasichana<br />
wote unaowafahamu waliopata mimba<br />
waliacha shule na hawakuweza kumaliza<br />
masomo. Kufikiria kwa ubunifu maana<br />
yake ni kutokudhani kwamba lazima<br />
uache shule eti kwasababu wasichana<br />
wengine waliacha. Labda inawezekana<br />
ukakaa shuleni ukiwa na mimba. Au<br />
unaweza kurudi shuleni baada ya<br />
kujifungua mtoto. Labda kipo kituo kwa<br />
ajili ya vijana waliozaa ambako unaweza<br />
kuendelea na masomo au mafunzo.<br />
Kufikiri kwa ubunifu kunahusisha<br />
kuzungumza na watu wengine. (walimu,<br />
vijana washauri wazazi, shangazi,<br />
wajomba marafiki) na kuchunguza<br />
chaguzi zote zilizoko mbele yako.<br />
Stadi za makubaliano. Hizi ni stadi<br />
ambazo unahitaji ili kutatua tatizo au<br />
tofauti ulizonazo na watu wengine.<br />
Kwa mfano, unaweza ukataka kutoka<br />
na rafiki yako, lakini wazazi wako<br />
wanataka ukae nyumbani. Hali kama<br />
hii inahitaji stadi nzuri za makubaliano.<br />
Inaweza ikawa vigumu kukubaliana<br />
na wakati wingine kukatishwa tamaa.<br />
Unaweza kujisikia kama upasuke,<br />
kwamba umevunjika moyo kiasi cha<br />
kusema “potelea mbali” na kuondoka<br />
ukiwa umekasirika na kuchoshwa.<br />
Lakini unahitaji kuwa mvumilivu na<br />
mtulivu wakati unaeleza kwa nini<br />
unajisikia hivyo, na kile unachohitaji.<br />
Vilevile unahitaji kuwa mkweli, mtu<br />
unayeelewa na kuheshimu yale ambayo<br />
watu wengine wanayahisi na kuyahitaji.<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Je, unajua maana ya kutatua tatizo kwa<br />
ubunifu bila woga wala jazba?<br />
Anne ana umri wa miaka 16 na ni yatima.<br />
Anaishi na shangazi yake ambaye anamtaka<br />
afanye kazi dukani kwake kila siku baada ya<br />
kutoka shule. Hili ni tatizo kubwa kwa Anne.<br />
Hapati muda wa kutosha wa kujisomea.<br />
Ameanza kufadhaika kwa vile mitihani<br />
inakaribia. Hapati usingizi vizuri usiku kwa<br />
sababu ana wasiwasi sana kuhusu masomo.<br />
Ameanza kumchukia shangazi yake.<br />
Anashangaa iwapo shangazi yake anamwona<br />
kama kitendea kazi na kwamba hampendi<br />
wala kujali maisha yake ya baadaye.<br />
Anne anajitambua. Anajua kuwa anayo<br />
tabia ya kuficha hisia zake mpaka<br />
anapolipuka kwa hasira. Tabia hii haimsaidii<br />
sana. Shangazi yake naye anakasirika na<br />
kusema ameanza kukosa heshima.Safari hii<br />
anaamua kufanya mambo tofauti. Badala<br />
ya kumwambia shangazi yake kiugomvi<br />
“Hunipendi” anamweleza shangazi yake bila<br />
woga wala jazba “Ninawasiwasi sana kuhusu<br />
mitihani yangu lakini nataka pia kukusaidia<br />
kazi za dukani”. Hapa ameonyesha tabia ya<br />
kujiamini.<br />
Kwa kujieleza mwenyewe kwa njia hii,<br />
Anne amesimama imara na kuomba<br />
muda zaidi wa kujisomea. Lakini kwa<br />
wakati huo huo anaelewa shangazi yake<br />
anahitaji msaada wa dukani. Anaonyesha<br />
ushirikiano kwa shangazi yake ambaye ana<br />
majukumu mengine. Akifuata utaratibu huu,<br />
shangazi naye anaelewa pia. Kwa pamoja<br />
wanafikiri kwa ubunifu kutatua tatizo hili.<br />
Wanatengeneza ratiba inayompa Anne muda<br />
zaidi wa kujisomea jioni na pia kumsaidia<br />
shangazi yake jioni inapokuwa lazima.<br />
Inatia moyo kwa jinsi Anne alivyojisikia<br />
vizuri. Ghafla mfadhaiko unapungua na<br />
anaweza kuyafurahia maisha tena.<br />
Hata hivyo sio kila tatizo linaweza kujadiliwa na kufikia maelewano. Wakati mwingine<br />
utalenga katika matokeo ambayo yatakufanya uwe salama, hata kama mtu mwingine<br />
hatafurahia. Mathalani, rafiki yako wa kike au wa kiume amekataa kutumia kondomu<br />
pamoja na kumshawishi kwa nguvu zote. Katika hali kama hii zingatia usalama wako.<br />
Ondoka sehemu hiyo ikibidi.<br />
Msimamo: Msimamo ni stadi ya msingi katika kuelewana na watu wengine. Msimamo<br />
maana yake kutetea na kuyaenzi yale unayoyaamini wewe mwenyewe. Kuwa muwazi na<br />
mwaminifu kwako mwenyewe na watu wengine kuhusu kile unachokihitaji na kukitaka.<br />
Watu ambao hawana msimamo juu ya maisha yao huwa ni wanyenyekevu. Hata kama<br />
wanatendewa vibaya, hawajitetei. Watu ambao hawana msimamo mara kwa mara<br />
wanakosa imani ya kujienzi na kutetea mahitaji yao na kulinda hisia zao au hata miili yao ili<br />
wasiumizwe.<br />
Msimamo ni tofauti sana na kuwa mgomvi. Watu wagomvi ni watundu na hawana huruma,<br />
hawajali watu wengine wanahisi nini. Sio vizuri kuwa mgomvi kwa faida ya afya ya hisia<br />
kwa sababu, kwa undani kabisa, utajisikia vibaya kutokuwa na huruma kwa wengine.<br />
Misingi ya msimamo:<br />
SURA YA 6 | UTUNZAJI AfYA YA AKILI NA MOYO<br />
• amua unachohisi au unachotaka na kiseme. Usiogope kuwa mkweli kuhusu hisia<br />
zako. Watu wanatakiwa kuziheshimu hisia hizo. Kwa mfano, labda ulijisikia vibaya na<br />
unakosa raha baada ya rafiki yako wa kiume kukugusa sehemu zako za siri. Unatakiwa<br />
kumwambia, “Nilikosa raha uliponigusa sehemu zangu za siri sitaki uniguse hivyo tena”.<br />
Mtu anayekupenda kweli hatataka kufanya vitendo ambavyo vinakukosesha raha.<br />
• Mtazame mtu machoni: Kumwangalia mtu machoni ni kudhihirisha msimamo wako.<br />
Inamjulisha mtu mwingine kwamba hutanii kuhusu kile unachokisema na kwamba<br />
unaangalia kama wanakusikiliza au hawakusikilizi. Tamaduni nyingi haziungi mkono<br />
kumwangalia mtu machoni wakati wa mazungumzo. Wakati mwingine katika maeneo<br />
mengine huliona jambo hili ni ufedhuli (kutokuwa na ustaarabu/heshima) kijana<br />
mdogo anapomwangalia mtu mzima moja kwa moja usoni. Unaweza kufuata mila na<br />
desturi, kama kupiga magoti, kuonyesha heshima lakini kwa wakati huo huo endelea<br />
kumwangalia mtu huyo usoni kama unataka kuonyesha ujasiri/msimamo wako.<br />
• usitoe visingizio. Hisia zako ni sababu tosha. Kwa mfano, kama hujisikii kufanya<br />
mapenzi lakini rafiki yako wa kike au kiume anakulazimisha, epuka kutumia watu<br />
wengine kama kisingizio. Usiseme, “mama yangu karibu atarudi nyumbani au tumbo<br />
linaniuma au ninaogopa kupata mimba au nina kazi ya kusoma kwa hiyo sio muda mzuri<br />
kwangu”. Unaweza ukamchanganya rafiki yako na visingizio hivi. Anaweza kudhani<br />
unataka kwenda sehemu nyingine, au kwamba labda unataka kutumia kondomu.<br />
Anaweza asitambue kwamba unachotaka kumwambia ni “siko tayari kufanya tendo hilo<br />
kwa hiyo sitaki”. Kwa hiyo basi sema kile unachotaka.<br />
• usisemewe na mtu mwingine. Iwapo hutaki kufanya jambo fulani, sema mwenyewe<br />
na usiulize mtu mwingine kama ni sawa. Kwa mfano, kama mtu ana kushawishi unywe<br />
pombe au madawa ya kulevya usiseme; “nisingependa, lakini kama unaona sawa …?<br />
Badala yake sema “Hapana, ninashukuru.<br />
67