08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

148<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Unaweza kushawishika kuingia katika uhusiano na mtu mzima, hususani kama huna pesa za<br />

matumizi na wazazi wako hawawezi kukununulia vitu vya kukufurahisha na vilivyo vizuri. Hata<br />

hivyo, hakuna zawadi au kiasi cha pesa chenye thamani ya gharama utakayolipa.<br />

Iwapo mtu mzima, mwanaume au mwanamke anajaribu kukupatia zawadi au pesa na anashinikiza<br />

mjamiiane, kuwa jasiri. Sema “hapana” na ondoka bila kuchelewa. Waeleze wazazi au shangazi<br />

au mjomba au mwelimisha rika kilichotokea. Waombe wakusaidie uweze kuimudu hali hiyo.<br />

Usijaribu kutatua peke yako.<br />

Vijana wengine wanaingizwa katika uhusiano wa namna hii na wazazi wao. Hii ni kwa sababu<br />

wazazi ni maskini na hawawezi kulipa karo, chakula, nguo na vitu vingine. Hali kama hii ni ngumu<br />

kwa kijana yeyote. Iwapo utakuwa katika mazingira kama haya unahitaji kufikiri kiubunifu:<br />

•<br />

•<br />

•<br />

Ni nani unaweza kumwendea kwa ajili ya msaada? Unaweza kuzungumza na ndugu wengine<br />

kama vile shangazi, mjomba, babu, bibi au kaka au dada? Huenda wakakulipia karo au<br />

wakawasaidia wazazi wako kufanikisha yote. Unaweza kuzungumza na mtu yeyote ndani<br />

ya jamii, kama vile mtu wa kanisani, msikitini au kutoka kituo cha vijana? Hawa wanaweza<br />

kufahamu namna ya kutatua tatizo lako.<br />

Je, unaweza kuzungumza na mwalimu au mkuu wa shule? Waulize namna unavyoweza<br />

kulishughulikia tatizo lako. Pengine wanaweza kukusaidia kwa kukusamehe karo au kwa<br />

kukupatia kazi ya kufanya shuleni ili uweze kulipa karo.<br />

Je, unaweza kupata pesa? Unaweza kufanya kazi, kama kuuza mboga, karanga, bisi au<br />

peremende baada ya shule ili kupata pesa?<br />

Wapo watu wengine wanaokuzunguka ambao wanaweza kukusaidia ikiwa watajua tatizo lako.<br />

Kwa hiyo omba msaada na usijaribu kulitatua peke yako.<br />

unYanYaSaji KijinSia<br />

Margaret kutoka Zimbabwe (umri wa miaka 17)<br />

“Kitu kimoja ninachojua kuhusu wanaume ni kwamba wengi<br />

huwania kujifurahisha na mtu wa jinsi nyingine, na katika kufanya<br />

hivyo wanaweza kukuahidi hazina zote za maisha. Kwa<br />

hiyo, nimesema HAPANA kwa wanaume wengi na nitaendelea<br />

kufanya hivyo.”<br />

neema kutoka Kenya (umri wa miaka 15)<br />

“Alikuwepo mfanyabiashara mmoja aliyekuwa anajaribu<br />

kufanya urafiki na mimi lakini nilikataa. Mwanaume huyo alikuwa<br />

anawatuma wasichana wengine kujaribu kunishawishi,<br />

lakini nilikataa.”<br />

Aina yoyote ya kuguswa au kushikwashikwa kimapenzi bila ridhaa ya anayetendewa hivyo ni<br />

unyanyasaji kijinsia. Inaweza ikawa kushikwa matiti au sehemu za siri. Inaweza vilevile ikawa<br />

kujamiiana. Aina yoyote ya kukutana kimapenzi bila ya kupenda ni unyanyasaji pia.<br />

SURA YA 12 | NGONO YA KULAZIMISHWA NA NGONO BILA YA RIDHAA YAKO<br />

Unyanyasaji kijinsia mara nyingi unafanywa na<br />

mtu mzima anayemjua kijana na ana madaraka juu<br />

yake. Mtu mzima anaweza kuwa jirani, rafiki wa<br />

familia, mwalimu, kiongozi wa dini au kiongozi wa<br />

jamii. Mtu mzima anaweza akawa ndugu, kama vile<br />

mzazi, mzazi wa kambo, mjomba au shangazi, kaka<br />

au dada.<br />

Unyanyasaji kijinsia unaweza kuhusisha tishio,<br />

rushwa, udanganyifu, ujanja na vurugu. Mtu mzima<br />

anaweza kukutishia, au mtu mzima anaweza<br />

kukupatia zawadi ili kukufanya utoe ushirikiano.<br />

Mtu mzima anaweza pia kukudanganya au<br />

kukutegea ufanye jambo. Mtu mzima anaweza<br />

kukutishia kukudhuru wewe au familia yako iwapo<br />

utamwambia mtu yeyote kuhusu unyanyasaji<br />

kijinsia. Mtu mzima anaweza kukuchanganya akili<br />

kwa kusema uhusiano utakuwa wa siri.<br />

Unyanyasaji kijinsia ni jambo baya sana na linaweza kukufanya uchanganyikiwe. Hapa kuna<br />

mambo machache ya kuyaweka maanani:-<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

Mwili wako ni wako.<br />

Unayo haki ya kuamua nani akushike, akushike vipi na wakati gani.<br />

Kugusana kwa aina yoyote kusikokubalika ni<br />

unyanyasaji kijinsia.<br />

Mtu yeyote asiangalie au kukushika sehemu zako za siri kwa namna ambavyo utajisikia<br />

vibaya.<br />

Amini hisia zako kuhusu kuguswa na amua nini kilicho chema kwako. Usimsikilize mtu<br />

anayejaribu kukushawishi vinginevyo.<br />

Mtu akikugusa ambavyo hupendelei, sema “hapana” kwa nguvu na kwa sauti. Kuwa jasiri.<br />

Tafuta mtu wa kumweleza kuhusu tukio. Ongea na mzazi, shangazi au mjomba, babu, bibi, rafiki,<br />

mwalimu au mama wa rafiki yako. Pata msaada.<br />

iwapo yupo mtu anakunyanyasa kijinsia au anakushinikiza ufanye naye ngono, tafuta msaada. Ongea<br />

na wazazi au mtu mwingine anayejali.<br />

149

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!