Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
148<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Unaweza kushawishika kuingia katika uhusiano na mtu mzima, hususani kama huna pesa za<br />
matumizi na wazazi wako hawawezi kukununulia vitu vya kukufurahisha na vilivyo vizuri. Hata<br />
hivyo, hakuna zawadi au kiasi cha pesa chenye thamani ya gharama utakayolipa.<br />
Iwapo mtu mzima, mwanaume au mwanamke anajaribu kukupatia zawadi au pesa na anashinikiza<br />
mjamiiane, kuwa jasiri. Sema “hapana” na ondoka bila kuchelewa. Waeleze wazazi au shangazi<br />
au mjomba au mwelimisha rika kilichotokea. Waombe wakusaidie uweze kuimudu hali hiyo.<br />
Usijaribu kutatua peke yako.<br />
Vijana wengine wanaingizwa katika uhusiano wa namna hii na wazazi wao. Hii ni kwa sababu<br />
wazazi ni maskini na hawawezi kulipa karo, chakula, nguo na vitu vingine. Hali kama hii ni ngumu<br />
kwa kijana yeyote. Iwapo utakuwa katika mazingira kama haya unahitaji kufikiri kiubunifu:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Ni nani unaweza kumwendea kwa ajili ya msaada? Unaweza kuzungumza na ndugu wengine<br />
kama vile shangazi, mjomba, babu, bibi au kaka au dada? Huenda wakakulipia karo au<br />
wakawasaidia wazazi wako kufanikisha yote. Unaweza kuzungumza na mtu yeyote ndani<br />
ya jamii, kama vile mtu wa kanisani, msikitini au kutoka kituo cha vijana? Hawa wanaweza<br />
kufahamu namna ya kutatua tatizo lako.<br />
Je, unaweza kuzungumza na mwalimu au mkuu wa shule? Waulize namna unavyoweza<br />
kulishughulikia tatizo lako. Pengine wanaweza kukusaidia kwa kukusamehe karo au kwa<br />
kukupatia kazi ya kufanya shuleni ili uweze kulipa karo.<br />
Je, unaweza kupata pesa? Unaweza kufanya kazi, kama kuuza mboga, karanga, bisi au<br />
peremende baada ya shule ili kupata pesa?<br />
Wapo watu wengine wanaokuzunguka ambao wanaweza kukusaidia ikiwa watajua tatizo lako.<br />
Kwa hiyo omba msaada na usijaribu kulitatua peke yako.<br />
unYanYaSaji KijinSia<br />
Margaret kutoka Zimbabwe (umri wa miaka 17)<br />
“Kitu kimoja ninachojua kuhusu wanaume ni kwamba wengi<br />
huwania kujifurahisha na mtu wa jinsi nyingine, na katika kufanya<br />
hivyo wanaweza kukuahidi hazina zote za maisha. Kwa<br />
hiyo, nimesema HAPANA kwa wanaume wengi na nitaendelea<br />
kufanya hivyo.”<br />
neema kutoka Kenya (umri wa miaka 15)<br />
“Alikuwepo mfanyabiashara mmoja aliyekuwa anajaribu<br />
kufanya urafiki na mimi lakini nilikataa. Mwanaume huyo alikuwa<br />
anawatuma wasichana wengine kujaribu kunishawishi,<br />
lakini nilikataa.”<br />
Aina yoyote ya kuguswa au kushikwashikwa kimapenzi bila ridhaa ya anayetendewa hivyo ni<br />
unyanyasaji kijinsia. Inaweza ikawa kushikwa matiti au sehemu za siri. Inaweza vilevile ikawa<br />
kujamiiana. Aina yoyote ya kukutana kimapenzi bila ya kupenda ni unyanyasaji pia.<br />
SURA YA 12 | NGONO YA KULAZIMISHWA NA NGONO BILA YA RIDHAA YAKO<br />
Unyanyasaji kijinsia mara nyingi unafanywa na<br />
mtu mzima anayemjua kijana na ana madaraka juu<br />
yake. Mtu mzima anaweza kuwa jirani, rafiki wa<br />
familia, mwalimu, kiongozi wa dini au kiongozi wa<br />
jamii. Mtu mzima anaweza akawa ndugu, kama vile<br />
mzazi, mzazi wa kambo, mjomba au shangazi, kaka<br />
au dada.<br />
Unyanyasaji kijinsia unaweza kuhusisha tishio,<br />
rushwa, udanganyifu, ujanja na vurugu. Mtu mzima<br />
anaweza kukutishia, au mtu mzima anaweza<br />
kukupatia zawadi ili kukufanya utoe ushirikiano.<br />
Mtu mzima anaweza pia kukudanganya au<br />
kukutegea ufanye jambo. Mtu mzima anaweza<br />
kukutishia kukudhuru wewe au familia yako iwapo<br />
utamwambia mtu yeyote kuhusu unyanyasaji<br />
kijinsia. Mtu mzima anaweza kukuchanganya akili<br />
kwa kusema uhusiano utakuwa wa siri.<br />
Unyanyasaji kijinsia ni jambo baya sana na linaweza kukufanya uchanganyikiwe. Hapa kuna<br />
mambo machache ya kuyaweka maanani:-<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Mwili wako ni wako.<br />
Unayo haki ya kuamua nani akushike, akushike vipi na wakati gani.<br />
Kugusana kwa aina yoyote kusikokubalika ni<br />
unyanyasaji kijinsia.<br />
Mtu yeyote asiangalie au kukushika sehemu zako za siri kwa namna ambavyo utajisikia<br />
vibaya.<br />
Amini hisia zako kuhusu kuguswa na amua nini kilicho chema kwako. Usimsikilize mtu<br />
anayejaribu kukushawishi vinginevyo.<br />
Mtu akikugusa ambavyo hupendelei, sema “hapana” kwa nguvu na kwa sauti. Kuwa jasiri.<br />
Tafuta mtu wa kumweleza kuhusu tukio. Ongea na mzazi, shangazi au mjomba, babu, bibi, rafiki,<br />
mwalimu au mama wa rafiki yako. Pata msaada.<br />
iwapo yupo mtu anakunyanyasa kijinsia au anakushinikiza ufanye naye ngono, tafuta msaada. Ongea<br />
na wazazi au mtu mwingine anayejali.<br />
149