Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
138<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Utoaji mimba usio salama ni hatari sana. Unaweza kupoteza maisha yako.<br />
Kama wewe au yeyote unayefahamu anakabiliwa na mimba isiyotakiwa, tafuta msaada. Kuwa<br />
mwaminifu kwa wazazi /walezi kuhusu hali hiyo. Kama wazazi wako hawakusaidii tembelea kituo<br />
cha vijana na mwombe mshauri wa vijana ushauri kuhusu suala lako. Mwombe mshauri wa vijana<br />
akuelekeze wapi unaweza kwenda kuzungumza na mhudumu wa afya anayejali na mpole.<br />
Kama wewe au yeyote unayemjua alitoa mimba na hajisikii vizuri, nenda hospitali haraka. Kuvuja<br />
damu, homa ya baridi, homa na/au kutoka majimaji yenye harufu ni dalili kwamba kuna mahali<br />
pana matatizo makubwa. Afya yako na maisha yako yapo hatarini hivyo uchunguzi wa waganga<br />
ni muhimu sana. Hata kama sheria ni kali kiasi gani, wahudumu wa afya wana miiko ya kitalaamu<br />
ya kumsaidia yeyote atakayekuwa na matatizo. Usiache woga ukuzuie kupata matibabu na<br />
hatimaye ukapoteza uhai.<br />
Njia nzuri ya kujikinga mwenyewe dhidi ya matokeo ya kutoa mimba kwa njia isiyo salama ni<br />
kukwepa kupata mimba isiyopangwa ama kuepuka ngono nzembe.<br />
naMna Ya KuePuKa KuPata MiMba<br />
Njia ya uhakika kabisa ya kutopata mimba ni kuacha kufanya ngono. Uzuiaji huu una uhakika wa<br />
asilimia 100, na ni salama kihisia na kimwili. Kama hujamiiani, hakuna jinsi unavyoweza kupata<br />
mimba au kumpa mimba msichana.<br />
Ikiwa unajamiiana, hakikisha pia kuwa wewe na mwenzi wako mnatumia kondomu kujikinga dhidi<br />
ya mimba na magonjwa ya ngono. Unatakiwa pia kuomba msaada kutoka kliniki ya uzazi wa<br />
mpango. Unahitaji kuchukuwa hatua ili mwenzi wako asipate mtoto ambaye huwezi kumtunza<br />
kwa wakati huu.<br />
Kuna aina nyingi za dawa za kuzuia mimba ambazo ni salama kabisa kwa vijana (angalia<br />
kisanduku ukurasa wa 140). Njia yoyote utakayotumia, hakikisha unaitumia inavyotakiwa. Kwa<br />
mfano, kusahau kumeza kidonge kunaweza kusababisha upate mimba.<br />
SURA YA 11 | MIMBA NA UZUIAJI WA MIMBA<br />
je, ViDOnGe VYa KuZuia MiMba ni SalaMa?<br />
Uvumi kama huu ni uwongo na si wa<br />
kisayansi. Tangu miaka ya 1950, mamilioni<br />
kwa mamilioni ya wanawake wametumia<br />
dawa za vidonge za kuzuia mimba. Vidonge<br />
vya kuzuia mimba vimefanyiwa uchunguzi<br />
mkubwa katika historia ya dawa. Kwa<br />
kuyafuatilia maisha ya maelfu ya wanawake<br />
kwa miaka mingi waganga sasa wanajua<br />
kwamba vidonge vya kuzuia mimba havileti<br />
saratani. Uwezekano wa wanawake<br />
wanaomeza vidonge kupata saratani ya<br />
kokwa la mayai na uwezekano wa kupata<br />
saratani kwenye ngozi laini ya kuta za<br />
tumbo la uzazi ni mdogo kuliko wanawake<br />
ambao hawajawahi kutumia vidonge hivyo.<br />
Kuna uvumi mwingine kwamba kutumia vidonge vya kuzuia mimba wakati wa ujana balehe<br />
kunaweza kuharibu kokwa la mayai na kusababisha isiwezekane kupata mimba baadaye. Huu pia<br />
ni uzushi.Mwongozo wa kimataifa wa kutumia dawa za kuzuia mimba unasema vidonge ni vizuri<br />
kwa wanawake ambao bado hawajapata watoto. Ukweli ni kwamba ,mara nyingine vinatumika<br />
kuwasaidia vijana balehe kuwapunguzia maumivu makali wakati wa hedhi. Huhitaji kuwa na<br />
mtoto kwanza ndipo uanze kumeza vidonge. Vidonge havitaharibu kokwa la mayai.<br />
Wasichana na wanawake wengine wanapata kichefuchefu, matiti kuwa laini na kuongezeka<br />
uzito wanapoanza kumeza vidonge. Matokeo haya huwa yanatoweka baada ya mwezi mmoja au<br />
zaidi. Karibu wanawake wadogo na wanawake wa makamo wote wanaweza kumeza vidonge. Ni<br />
wanawake wa makamo tu ambao wanaovuta sigara, walio wanene sana au wanashinikizo la damu<br />
au magonjwa fulani kwenye mfumo wao wa damu wanashauriwa wasitumie njia ya homoni kuzuia<br />
mimba (vidonge vya kuzuia mimba, sindano na vipandikizi). Unatakiwa kumwona mtoa huduma ili<br />
akupime kama huna vidokezo vya mteja wa dawa za kuzuia mimba.<br />
KuZuia MiMba KWa DhaRuRa<br />
christine kutoka uganda (umri wa miaka 18)<br />
“Nimesikia kwamba vidonge vya kuzuia mimba vinasababisha<br />
saratani au pia ulemavu kwa mtoto”.<br />
Kuna njia moja zaidi ya kuzuia mimba ambayo hapana budi kuijua. Hii ni njia ya dharura ya kuzuia<br />
mimba. Njia ambayo unaweza kuitumia kuzuia mimba haraka baada ya kufanya ngono isiyo<br />
salama. Kwa mfano kama ulisahau kutumia kondomu au kama kondomu ilipasuka au ilitoka kwa<br />
bahati mbaya (jambo ambalo ni nadra sana kama ikitumika vizuri).<br />
Kinga ya dharura ya kuzuia mimba imeanza kupatikana sehemu nyingi siku hizi. Kama ukifanya<br />
ngono bila kinga na una wasiwasi wa kupata mimba unaweza kwenda kwa muhudumu wa afya na<br />
kumwomba kinga ya dharura ya kuzuia mimba. Ikiwa umebakwa omba kinga ya dharura ya kuzuia<br />
mimba kutoka kwenye kliniki ya mpango wa uzazi au kituo cha vijana karibu na wewe katika<br />
kipindi cha saa 72 (siku 3).<br />
139