08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

138<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Utoaji mimba usio salama ni hatari sana. Unaweza kupoteza maisha yako.<br />

Kama wewe au yeyote unayefahamu anakabiliwa na mimba isiyotakiwa, tafuta msaada. Kuwa<br />

mwaminifu kwa wazazi /walezi kuhusu hali hiyo. Kama wazazi wako hawakusaidii tembelea kituo<br />

cha vijana na mwombe mshauri wa vijana ushauri kuhusu suala lako. Mwombe mshauri wa vijana<br />

akuelekeze wapi unaweza kwenda kuzungumza na mhudumu wa afya anayejali na mpole.<br />

Kama wewe au yeyote unayemjua alitoa mimba na hajisikii vizuri, nenda hospitali haraka. Kuvuja<br />

damu, homa ya baridi, homa na/au kutoka majimaji yenye harufu ni dalili kwamba kuna mahali<br />

pana matatizo makubwa. Afya yako na maisha yako yapo hatarini hivyo uchunguzi wa waganga<br />

ni muhimu sana. Hata kama sheria ni kali kiasi gani, wahudumu wa afya wana miiko ya kitalaamu<br />

ya kumsaidia yeyote atakayekuwa na matatizo. Usiache woga ukuzuie kupata matibabu na<br />

hatimaye ukapoteza uhai.<br />

Njia nzuri ya kujikinga mwenyewe dhidi ya matokeo ya kutoa mimba kwa njia isiyo salama ni<br />

kukwepa kupata mimba isiyopangwa ama kuepuka ngono nzembe.<br />

naMna Ya KuePuKa KuPata MiMba<br />

Njia ya uhakika kabisa ya kutopata mimba ni kuacha kufanya ngono. Uzuiaji huu una uhakika wa<br />

asilimia 100, na ni salama kihisia na kimwili. Kama hujamiiani, hakuna jinsi unavyoweza kupata<br />

mimba au kumpa mimba msichana.<br />

Ikiwa unajamiiana, hakikisha pia kuwa wewe na mwenzi wako mnatumia kondomu kujikinga dhidi<br />

ya mimba na magonjwa ya ngono. Unatakiwa pia kuomba msaada kutoka kliniki ya uzazi wa<br />

mpango. Unahitaji kuchukuwa hatua ili mwenzi wako asipate mtoto ambaye huwezi kumtunza<br />

kwa wakati huu.<br />

Kuna aina nyingi za dawa za kuzuia mimba ambazo ni salama kabisa kwa vijana (angalia<br />

kisanduku ukurasa wa 140). Njia yoyote utakayotumia, hakikisha unaitumia inavyotakiwa. Kwa<br />

mfano, kusahau kumeza kidonge kunaweza kusababisha upate mimba.<br />

SURA YA 11 | MIMBA NA UZUIAJI WA MIMBA<br />

je, ViDOnGe VYa KuZuia MiMba ni SalaMa?<br />

Uvumi kama huu ni uwongo na si wa<br />

kisayansi. Tangu miaka ya 1950, mamilioni<br />

kwa mamilioni ya wanawake wametumia<br />

dawa za vidonge za kuzuia mimba. Vidonge<br />

vya kuzuia mimba vimefanyiwa uchunguzi<br />

mkubwa katika historia ya dawa. Kwa<br />

kuyafuatilia maisha ya maelfu ya wanawake<br />

kwa miaka mingi waganga sasa wanajua<br />

kwamba vidonge vya kuzuia mimba havileti<br />

saratani. Uwezekano wa wanawake<br />

wanaomeza vidonge kupata saratani ya<br />

kokwa la mayai na uwezekano wa kupata<br />

saratani kwenye ngozi laini ya kuta za<br />

tumbo la uzazi ni mdogo kuliko wanawake<br />

ambao hawajawahi kutumia vidonge hivyo.<br />

Kuna uvumi mwingine kwamba kutumia vidonge vya kuzuia mimba wakati wa ujana balehe<br />

kunaweza kuharibu kokwa la mayai na kusababisha isiwezekane kupata mimba baadaye. Huu pia<br />

ni uzushi.Mwongozo wa kimataifa wa kutumia dawa za kuzuia mimba unasema vidonge ni vizuri<br />

kwa wanawake ambao bado hawajapata watoto. Ukweli ni kwamba ,mara nyingine vinatumika<br />

kuwasaidia vijana balehe kuwapunguzia maumivu makali wakati wa hedhi. Huhitaji kuwa na<br />

mtoto kwanza ndipo uanze kumeza vidonge. Vidonge havitaharibu kokwa la mayai.<br />

Wasichana na wanawake wengine wanapata kichefuchefu, matiti kuwa laini na kuongezeka<br />

uzito wanapoanza kumeza vidonge. Matokeo haya huwa yanatoweka baada ya mwezi mmoja au<br />

zaidi. Karibu wanawake wadogo na wanawake wa makamo wote wanaweza kumeza vidonge. Ni<br />

wanawake wa makamo tu ambao wanaovuta sigara, walio wanene sana au wanashinikizo la damu<br />

au magonjwa fulani kwenye mfumo wao wa damu wanashauriwa wasitumie njia ya homoni kuzuia<br />

mimba (vidonge vya kuzuia mimba, sindano na vipandikizi). Unatakiwa kumwona mtoa huduma ili<br />

akupime kama huna vidokezo vya mteja wa dawa za kuzuia mimba.<br />

KuZuia MiMba KWa DhaRuRa<br />

christine kutoka uganda (umri wa miaka 18)<br />

“Nimesikia kwamba vidonge vya kuzuia mimba vinasababisha<br />

saratani au pia ulemavu kwa mtoto”.<br />

Kuna njia moja zaidi ya kuzuia mimba ambayo hapana budi kuijua. Hii ni njia ya dharura ya kuzuia<br />

mimba. Njia ambayo unaweza kuitumia kuzuia mimba haraka baada ya kufanya ngono isiyo<br />

salama. Kwa mfano kama ulisahau kutumia kondomu au kama kondomu ilipasuka au ilitoka kwa<br />

bahati mbaya (jambo ambalo ni nadra sana kama ikitumika vizuri).<br />

Kinga ya dharura ya kuzuia mimba imeanza kupatikana sehemu nyingi siku hizi. Kama ukifanya<br />

ngono bila kinga na una wasiwasi wa kupata mimba unaweza kwenda kwa muhudumu wa afya na<br />

kumwomba kinga ya dharura ya kuzuia mimba. Ikiwa umebakwa omba kinga ya dharura ya kuzuia<br />

mimba kutoka kwenye kliniki ya mpango wa uzazi au kituo cha vijana karibu na wewe katika<br />

kipindi cha saa 72 (siku 3).<br />

139

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!