08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

14<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Vijana wengine hawafurahii nywele mpya zinazoota mwilini hasa mavuzi yanapotokea kwa mara<br />

ya kwanza.<br />

Kumbuka ya kwamba mavuzi ni kitu cha asili na yana kazi yake, kwa hiyo iwapo unayo mengi au<br />

kidogo usihofu sana.<br />

Vilevile, nywele huota kwapani kipindi cha balehe, ingawa mara nyingi ni wakati wa mwisho<br />

wa kipindi cha balehe. Wasichana wengi hawaoti nywele kwapani mpaka baada ya matiti<br />

kuanza kuota na baada ya kuvunja ungo. Kwa wavulana nywele za kwapani kwa kawaida huanza<br />

kujitokeza mwaka mmoja au zaidi baada ya mavuzi kuota. Kama mavuzi, nywele za kwapani<br />

zina kazi maalum.Wakati wa balehe jasho linatoka sana na nywele husaidia kuzuia jasho lisitoke<br />

kwenye ngozi.<br />

Kwa kawaida,kwa wavulana, nywele za usoni huwa za mwisho kuota. Huanza kuota pembeni mwa<br />

midomo ya juu. Nywele zinazoota juu ya midomo ya juu (masharubu) huendelea kuota, na zingine<br />

huota sehemu ya juu ya kidevu na chini kidogo katikati ya midomo ya chini na mwisho zingine<br />

huota kwenye kidevu. Nywele hazioti kidevuni mpaka via vya uzazi vya mvulana viwe vimekomaa<br />

kabisa. Kwa wavulana wengi, nywele za usoni huanza kuota hasa wakiwa na umri kati ya miaka 14<br />

na 18.Lakini zinaweza kuanza kuota mapema zaidi au zikachelewa.<br />

uWeZO Wa KuFiKiRi<br />

balay, kutoka Kenya (umri, miaka 16)<br />

“Nilistushwa! Sikujua kama mtu anaweza kuota nywele<br />

sehemu zake za siri. Nilidhani ninaumwa, na nikamwuliza<br />

mama ambaye alinihakikishia kwamba ilikuwa ni jambo la<br />

kawaida.”<br />

Diana, kutoka Zambia (umri, miaka 17)<br />

“Zilipoota, nilijisemesha mwenyewe kwamba itabidi<br />

nikubaliane na hali halisi”<br />

Doglas, kutoka Zimbabwe (umri miaka 12)<br />

“Yalipoota mavuzi haikunifurahisha yalinifanya nionekane<br />

mbaya”<br />

bernard, kutoka Kenya (umri, miaka 17)<br />

“Marafiki zangu walinicheka ati kwa sababu mavuzi yalikuwa<br />

hayajaota.”<br />

Wakati mabadiliko dhahiri yanayotokea katika mwili kipindi cha balehe, akili nayo pia hubadilika<br />

bila ya kutambulika kiurahisi.Katika kipindi cha ujana balehe, uwezo wa akili unaongezeka sana<br />

hasa katika kufikiri kwa makini na kutoa maoni ya kina. Matokeo ya mabadiliko haya husababisha<br />

utambulisho binafsi kuanza kujengeka.Unaanza kujiona kama mtu wa kipekee. Unapenda kufikiri<br />

mwenyewe na kufanya maamuzi yako binafsi.<br />

SURA YA 2 | MABADILIKO YA MWILI<br />

Mara nyingi, kwa mara ya kwanza utayaona mambo tofauti na wazazi wako wanavyoyaona.<br />

Unaweza kujisikia kutaka kujua imani za wazazi wako na sababu zake. Unaweza kutaka kujaribu<br />

kuishi maisha yako mwenyewe kuliko kutegemea ya kuambiwa na wengine. Unaweza kujaribu<br />

mambo mapya mwenyewe na wakati mwingine kujaribu mambo ya hatari.<br />

Mabadiliko yote haya ya akili ni dalili nzuri za kuonyesha kwamba unaingia utu uzima.<br />

Hata hivyo haina maana ya kwamba tayari umeishakuwa mtu mzima. Ingawa uwezo wako<br />

wa kiakili unaongezeka sana, bado kuna mambo mengi unakuwa hujayajua. Ukweli hutaweza<br />

kuyajua yote, kwa hiyo ni muhimu kujua wapi uende na umwone nani kwa ajili ya taarifa<br />

unayoihitaji. Kutakuwepo wakati ambapo itakuwa muhimu kutumia uzoefu na maarifa kutoka<br />

kwa waliokuzidi umri. Hivyo basi unatakiwa kuuliza maswali, usidhani unayo majibu yote. Jitahidi<br />

kujifunza mengi iwezekanavyo.<br />

Vijana wengine hutaniwa wanapokuwa wameota mavuzi au wanapokosa kuota.<br />

15

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!