Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
14<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Vijana wengine hawafurahii nywele mpya zinazoota mwilini hasa mavuzi yanapotokea kwa mara<br />
ya kwanza.<br />
Kumbuka ya kwamba mavuzi ni kitu cha asili na yana kazi yake, kwa hiyo iwapo unayo mengi au<br />
kidogo usihofu sana.<br />
Vilevile, nywele huota kwapani kipindi cha balehe, ingawa mara nyingi ni wakati wa mwisho<br />
wa kipindi cha balehe. Wasichana wengi hawaoti nywele kwapani mpaka baada ya matiti<br />
kuanza kuota na baada ya kuvunja ungo. Kwa wavulana nywele za kwapani kwa kawaida huanza<br />
kujitokeza mwaka mmoja au zaidi baada ya mavuzi kuota. Kama mavuzi, nywele za kwapani<br />
zina kazi maalum.Wakati wa balehe jasho linatoka sana na nywele husaidia kuzuia jasho lisitoke<br />
kwenye ngozi.<br />
Kwa kawaida,kwa wavulana, nywele za usoni huwa za mwisho kuota. Huanza kuota pembeni mwa<br />
midomo ya juu. Nywele zinazoota juu ya midomo ya juu (masharubu) huendelea kuota, na zingine<br />
huota sehemu ya juu ya kidevu na chini kidogo katikati ya midomo ya chini na mwisho zingine<br />
huota kwenye kidevu. Nywele hazioti kidevuni mpaka via vya uzazi vya mvulana viwe vimekomaa<br />
kabisa. Kwa wavulana wengi, nywele za usoni huanza kuota hasa wakiwa na umri kati ya miaka 14<br />
na 18.Lakini zinaweza kuanza kuota mapema zaidi au zikachelewa.<br />
uWeZO Wa KuFiKiRi<br />
balay, kutoka Kenya (umri, miaka 16)<br />
“Nilistushwa! Sikujua kama mtu anaweza kuota nywele<br />
sehemu zake za siri. Nilidhani ninaumwa, na nikamwuliza<br />
mama ambaye alinihakikishia kwamba ilikuwa ni jambo la<br />
kawaida.”<br />
Diana, kutoka Zambia (umri, miaka 17)<br />
“Zilipoota, nilijisemesha mwenyewe kwamba itabidi<br />
nikubaliane na hali halisi”<br />
Doglas, kutoka Zimbabwe (umri miaka 12)<br />
“Yalipoota mavuzi haikunifurahisha yalinifanya nionekane<br />
mbaya”<br />
bernard, kutoka Kenya (umri, miaka 17)<br />
“Marafiki zangu walinicheka ati kwa sababu mavuzi yalikuwa<br />
hayajaota.”<br />
Wakati mabadiliko dhahiri yanayotokea katika mwili kipindi cha balehe, akili nayo pia hubadilika<br />
bila ya kutambulika kiurahisi.Katika kipindi cha ujana balehe, uwezo wa akili unaongezeka sana<br />
hasa katika kufikiri kwa makini na kutoa maoni ya kina. Matokeo ya mabadiliko haya husababisha<br />
utambulisho binafsi kuanza kujengeka.Unaanza kujiona kama mtu wa kipekee. Unapenda kufikiri<br />
mwenyewe na kufanya maamuzi yako binafsi.<br />
SURA YA 2 | MABADILIKO YA MWILI<br />
Mara nyingi, kwa mara ya kwanza utayaona mambo tofauti na wazazi wako wanavyoyaona.<br />
Unaweza kujisikia kutaka kujua imani za wazazi wako na sababu zake. Unaweza kutaka kujaribu<br />
kuishi maisha yako mwenyewe kuliko kutegemea ya kuambiwa na wengine. Unaweza kujaribu<br />
mambo mapya mwenyewe na wakati mwingine kujaribu mambo ya hatari.<br />
Mabadiliko yote haya ya akili ni dalili nzuri za kuonyesha kwamba unaingia utu uzima.<br />
Hata hivyo haina maana ya kwamba tayari umeishakuwa mtu mzima. Ingawa uwezo wako<br />
wa kiakili unaongezeka sana, bado kuna mambo mengi unakuwa hujayajua. Ukweli hutaweza<br />
kuyajua yote, kwa hiyo ni muhimu kujua wapi uende na umwone nani kwa ajili ya taarifa<br />
unayoihitaji. Kutakuwepo wakati ambapo itakuwa muhimu kutumia uzoefu na maarifa kutoka<br />
kwa waliokuzidi umri. Hivyo basi unatakiwa kuuliza maswali, usidhani unayo majibu yote. Jitahidi<br />
kujifunza mengi iwezekanavyo.<br />
Vijana wengine hutaniwa wanapokuwa wameota mavuzi au wanapokosa kuota.<br />
15