08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

96<br />

hiSia Za KijinSia<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Mambo mengi utayagundua punde utakapoanza kusikia ashiki au kusisimuka kijinsia. Utayahisi<br />

mwili mzima. Kwa wanaume, dalili ya hisia ya kijinsia ni uume kusimama. Kwa wasichana, ni<br />

unyevunyevu ukeni. Hii inatokea kwa sababu damu ya ziada kutoka kwenye mishipa ya damu<br />

inaingia kwenye spongi maalum kwenye tishu ndani ya uke au uume. Kwa wavulana tishu<br />

za spongi zinavimba na kusababisha uume kuwa mrefu, mgumu, mpana na kusimama. Kwa<br />

wasichana, tishu za spongi zinavimba ndani ya kuta za uke na kusababisha utoaji wa majimaji,<br />

ambayo yanalainisha eneo la uchi na kusabisha lilowane.<br />

Unaweza kujisikia hisia za kijinsi zenye kusisimua kwa kusoma riwaya za kimapenzi au kumfikiria<br />

mvulana au msichana unayempenda. Kama ulikuwa na mvulana au msichana na mlikuwa<br />

mnashikanashikana, unaweza kusisimuka zaidi.<br />

Utafanya nini kuhusu hisia za kijinsi? Jambo la kwanza, huhitaji kufanya ngono unapopata hisia za<br />

kijinsi. Kujamiiana ni njia moja wapo ya namna watu wanavyoonyesha hisia za kimapenzi. Lakini<br />

zipo njia nyingi ambazo watu wanaweza kuonyesha hisia zao za kimapenzi - katika mazungumzo,<br />

kushikana mikono, kukumbatiana, kupakatana, kubusiana na kushikanashikana.<br />

Njia hizi za kuonyesha mapenzi zinaweza kuwa za kuridhisha na zina hatari ndogo sana<br />

ya kuambukizwa VVU (soma sura ya 10 zaidi juu ya VVU na magonjwa ya zinaa). Kupumua<br />

na mapigo ya moyo yanaweza kuongezeka. Mwili mzima unaweza ukajisikia kusisimuka na<br />

kuchangamka. Unaweza kuwa na hali hiyo ya kusisimua kwa masaa mengi. Huhitaji kwenda zaidi<br />

ya hapo. Mvulana hahitaji kumwambia msichana kuwa anahitaji kujamiiana nae eti kwa kuwa<br />

amesimamisha. Si kweli. Uume wako utaacha kusimama pindi utakapoacha kumpakata msichana.<br />

Ni muhimu kujua kwamba, si migusano yote inaleta hisia za kufanya ngono. Kama unasukumwa<br />

bila kupenda ili ufanye ngono, hutajisikia vizuri. Msisimko wa kijinsia unatokea watu<br />

wanapokuwa na furaha na wamepumzika (soma sura 12 zaidi juu ya unyanyasaji kijinsia na<br />

vitendo vya ngono visivyotakiwa).<br />

PunYetO<br />

Punyeto ni kitendo cha mtu kushika sehemu zake za siri – uume, uke, matiti au sehemu nyingine<br />

za mwili ambazo zinasisimka kijinsia. Punyeto ni mojawapo ya njia ambayo watu wanaelezea<br />

hisia zao za kijinsia.<br />

Wanaume kwa wanawake wanaweza kupunguza hisia za kutaka kujamiiana na bado wakapata<br />

starehe kwa kupiga punyeto. Kwa kweli watu wengi wanapiga punyeto kipindi fulani katika<br />

maisha yao. Wavulana wanapiga punyeto mara kwa mara kuliko wasichana. Wasichana na<br />

wavulana wengine wanaanza kupiga punyeto wakati bado watoto na wanaendelea kufanya hivyo<br />

maisha yao yote. Wengine wanaanza wanapobalehe; wengine wanaanza wakiwa watu wazima.<br />

Baadhi ya watu hawapigi punyeto, na wengine wanafikiria kuwa starehe ya ngono na kupiga<br />

punyeto ni kinyume na madhehebu yao au imani na utu wao.<br />

Katika mila nyingine, kuna uzushi mwingi<br />

ambao umekusudiwa kuwakatisha tamaa<br />

watu wasipige punyeto. Haya ni baadhi ya<br />

mambo yasiyo ya kweli kuhusu punyeto,<br />

kwamba:-<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

Kupiga punyeto kunafanya upate kichaa.<br />

Kupiga punyeto kunafanya uote nywele<br />

kwenye kiganja cha mkono wako;<br />

kunasababisha vipele usoni au kupofuka<br />

macho.<br />

Punyeto linafanya upauke rangi ya mwili<br />

na inasabisha utumie mbegu zote za<br />

kiume.<br />

Punyeto linasababisha mtu awe dhaifu<br />

na kufanya mwanaume ashindwe kupata<br />

watoto.<br />

Punyeto linafanya uwe na majivuno na<br />

uwe mbinafsi.<br />

Hakuna ukweli kuhusu uzushi huu. Kutokana<br />

na utalaam wa kitabibu na kisayansi, punyeto<br />

linachukuliwa kama sehemu ya makuzi.<br />

Haijalishi kama utapiga punyeto au hupigi.<br />

Hakuna ushahidi wa kisayansi unaoonyesha<br />

kwamba punyeto ina athari mbaya kimwili<br />

ama kisaikolojia.<br />

Punyeto linaweza kuwa na matatizo iwapo<br />

tu:-<br />

•<br />

•<br />

SURA YA 9 | UJINSIA NA NGONO<br />

Limezidi mno – mtu hawezi kufanya kazi<br />

za kutwa mpaka apige punyeto.<br />

Linafanywa maeneo ya watu wote mahali<br />

ambapo watu wengine wanaweza kuona.<br />

UNAFAHAMU maana ya kilele?<br />

Kama ashiki na msisimko vitazidi<br />

kuongezeka, utakuwa unaelekea “kilele”.<br />

Kwa mvulana kuutambua kilele misuli yako<br />

ghafla inabana na kufanya sehemu zote<br />

za uume wako kusukuma mbegu za kiume<br />

nje ya uume. Kwa msichana misuli ya ndani<br />

na inayozunguka uke, mlango wa tumbo<br />

la uzazi na kisimi vinabana. Mara nyingine<br />

majimaji kidogo yanaweza kutoka, lakini<br />

hakojoi kama ilivyo kwa wavulana.<br />

Kilele ni kama kupiga chafya, hisia ya<br />

kukakamaa kwa misuli ikifuatiwa na<br />

kulegea. Kwa watu wengi ni muda mfupi<br />

tu kilele kinadumu kwa sekunde 10, lakini<br />

ni muda ambao unajisikia vizuri na raha na<br />

watu wengi wangependa kukionja.<br />

Kwa wasichana wengi, inawachukua muda<br />

kufikia kilele. Inahitajika kujua wapi na<br />

namna gani washikwe.Na wanahitaji wawe<br />

wanafurahia na kutuliza akili.<br />

Wavulana na wasichana, wote wanaweza<br />

kufikia kilele kwa kupiga punyeto. Hivi ni<br />

vizuri.Uko pekee yako, unaugundua mwili<br />

wako, na majimaji yanayotoka wakati mwili<br />

umesisimkwa hayatampa mtu yoyote<br />

mimba wala uambukizo.<br />

Unapofikia upeo wa raha ya kujamiiana<br />

kwa kushikana na kupakatana, ina ugumu<br />

kidogo. Kweli mko wawili na maji maji<br />

yanayotoka wakati wa kushikana yanaweza<br />

kuwa na VVU au magonjwa ya ngono. (soma<br />

sura ya 10 kuhusu magonjwa ya zinaa na<br />

VVU).<br />

Wataalam wa ujinsia wa binadamu wanaamini<br />

kwamba punyeto ni njia ya kawaida ya watu<br />

kufurahia na kuelezea ujinsia wao bila ya<br />

kujihatarisha katika mimba au magonjwa ya ngono, yakiwemo VVU/UKIMWI. Hakuna tatizo<br />

litakalo tokea mwilini mwako hata kama ukipiga punyeto sana. Kitu pekee kinachoweza kutokea<br />

ni viungo vya uzazi kuvimba kwa sababu ya kuvisugua mno.<br />

97

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!