Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
96<br />
hiSia Za KijinSia<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Mambo mengi utayagundua punde utakapoanza kusikia ashiki au kusisimuka kijinsia. Utayahisi<br />
mwili mzima. Kwa wanaume, dalili ya hisia ya kijinsia ni uume kusimama. Kwa wasichana, ni<br />
unyevunyevu ukeni. Hii inatokea kwa sababu damu ya ziada kutoka kwenye mishipa ya damu<br />
inaingia kwenye spongi maalum kwenye tishu ndani ya uke au uume. Kwa wavulana tishu<br />
za spongi zinavimba na kusababisha uume kuwa mrefu, mgumu, mpana na kusimama. Kwa<br />
wasichana, tishu za spongi zinavimba ndani ya kuta za uke na kusababisha utoaji wa majimaji,<br />
ambayo yanalainisha eneo la uchi na kusabisha lilowane.<br />
Unaweza kujisikia hisia za kijinsi zenye kusisimua kwa kusoma riwaya za kimapenzi au kumfikiria<br />
mvulana au msichana unayempenda. Kama ulikuwa na mvulana au msichana na mlikuwa<br />
mnashikanashikana, unaweza kusisimuka zaidi.<br />
Utafanya nini kuhusu hisia za kijinsi? Jambo la kwanza, huhitaji kufanya ngono unapopata hisia za<br />
kijinsi. Kujamiiana ni njia moja wapo ya namna watu wanavyoonyesha hisia za kimapenzi. Lakini<br />
zipo njia nyingi ambazo watu wanaweza kuonyesha hisia zao za kimapenzi - katika mazungumzo,<br />
kushikana mikono, kukumbatiana, kupakatana, kubusiana na kushikanashikana.<br />
Njia hizi za kuonyesha mapenzi zinaweza kuwa za kuridhisha na zina hatari ndogo sana<br />
ya kuambukizwa VVU (soma sura ya 10 zaidi juu ya VVU na magonjwa ya zinaa). Kupumua<br />
na mapigo ya moyo yanaweza kuongezeka. Mwili mzima unaweza ukajisikia kusisimuka na<br />
kuchangamka. Unaweza kuwa na hali hiyo ya kusisimua kwa masaa mengi. Huhitaji kwenda zaidi<br />
ya hapo. Mvulana hahitaji kumwambia msichana kuwa anahitaji kujamiiana nae eti kwa kuwa<br />
amesimamisha. Si kweli. Uume wako utaacha kusimama pindi utakapoacha kumpakata msichana.<br />
Ni muhimu kujua kwamba, si migusano yote inaleta hisia za kufanya ngono. Kama unasukumwa<br />
bila kupenda ili ufanye ngono, hutajisikia vizuri. Msisimko wa kijinsia unatokea watu<br />
wanapokuwa na furaha na wamepumzika (soma sura 12 zaidi juu ya unyanyasaji kijinsia na<br />
vitendo vya ngono visivyotakiwa).<br />
PunYetO<br />
Punyeto ni kitendo cha mtu kushika sehemu zake za siri – uume, uke, matiti au sehemu nyingine<br />
za mwili ambazo zinasisimka kijinsia. Punyeto ni mojawapo ya njia ambayo watu wanaelezea<br />
hisia zao za kijinsia.<br />
Wanaume kwa wanawake wanaweza kupunguza hisia za kutaka kujamiiana na bado wakapata<br />
starehe kwa kupiga punyeto. Kwa kweli watu wengi wanapiga punyeto kipindi fulani katika<br />
maisha yao. Wavulana wanapiga punyeto mara kwa mara kuliko wasichana. Wasichana na<br />
wavulana wengine wanaanza kupiga punyeto wakati bado watoto na wanaendelea kufanya hivyo<br />
maisha yao yote. Wengine wanaanza wanapobalehe; wengine wanaanza wakiwa watu wazima.<br />
Baadhi ya watu hawapigi punyeto, na wengine wanafikiria kuwa starehe ya ngono na kupiga<br />
punyeto ni kinyume na madhehebu yao au imani na utu wao.<br />
Katika mila nyingine, kuna uzushi mwingi<br />
ambao umekusudiwa kuwakatisha tamaa<br />
watu wasipige punyeto. Haya ni baadhi ya<br />
mambo yasiyo ya kweli kuhusu punyeto,<br />
kwamba:-<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Kupiga punyeto kunafanya upate kichaa.<br />
Kupiga punyeto kunafanya uote nywele<br />
kwenye kiganja cha mkono wako;<br />
kunasababisha vipele usoni au kupofuka<br />
macho.<br />
Punyeto linafanya upauke rangi ya mwili<br />
na inasabisha utumie mbegu zote za<br />
kiume.<br />
Punyeto linasababisha mtu awe dhaifu<br />
na kufanya mwanaume ashindwe kupata<br />
watoto.<br />
Punyeto linafanya uwe na majivuno na<br />
uwe mbinafsi.<br />
Hakuna ukweli kuhusu uzushi huu. Kutokana<br />
na utalaam wa kitabibu na kisayansi, punyeto<br />
linachukuliwa kama sehemu ya makuzi.<br />
Haijalishi kama utapiga punyeto au hupigi.<br />
Hakuna ushahidi wa kisayansi unaoonyesha<br />
kwamba punyeto ina athari mbaya kimwili<br />
ama kisaikolojia.<br />
Punyeto linaweza kuwa na matatizo iwapo<br />
tu:-<br />
•<br />
•<br />
SURA YA 9 | UJINSIA NA NGONO<br />
Limezidi mno – mtu hawezi kufanya kazi<br />
za kutwa mpaka apige punyeto.<br />
Linafanywa maeneo ya watu wote mahali<br />
ambapo watu wengine wanaweza kuona.<br />
UNAFAHAMU maana ya kilele?<br />
Kama ashiki na msisimko vitazidi<br />
kuongezeka, utakuwa unaelekea “kilele”.<br />
Kwa mvulana kuutambua kilele misuli yako<br />
ghafla inabana na kufanya sehemu zote<br />
za uume wako kusukuma mbegu za kiume<br />
nje ya uume. Kwa msichana misuli ya ndani<br />
na inayozunguka uke, mlango wa tumbo<br />
la uzazi na kisimi vinabana. Mara nyingine<br />
majimaji kidogo yanaweza kutoka, lakini<br />
hakojoi kama ilivyo kwa wavulana.<br />
Kilele ni kama kupiga chafya, hisia ya<br />
kukakamaa kwa misuli ikifuatiwa na<br />
kulegea. Kwa watu wengi ni muda mfupi<br />
tu kilele kinadumu kwa sekunde 10, lakini<br />
ni muda ambao unajisikia vizuri na raha na<br />
watu wengi wangependa kukionja.<br />
Kwa wasichana wengi, inawachukua muda<br />
kufikia kilele. Inahitajika kujua wapi na<br />
namna gani washikwe.Na wanahitaji wawe<br />
wanafurahia na kutuliza akili.<br />
Wavulana na wasichana, wote wanaweza<br />
kufikia kilele kwa kupiga punyeto. Hivi ni<br />
vizuri.Uko pekee yako, unaugundua mwili<br />
wako, na majimaji yanayotoka wakati mwili<br />
umesisimkwa hayatampa mtu yoyote<br />
mimba wala uambukizo.<br />
Unapofikia upeo wa raha ya kujamiiana<br />
kwa kushikana na kupakatana, ina ugumu<br />
kidogo. Kweli mko wawili na maji maji<br />
yanayotoka wakati wa kushikana yanaweza<br />
kuwa na VVU au magonjwa ya ngono. (soma<br />
sura ya 10 kuhusu magonjwa ya zinaa na<br />
VVU).<br />
Wataalam wa ujinsia wa binadamu wanaamini<br />
kwamba punyeto ni njia ya kawaida ya watu<br />
kufurahia na kuelezea ujinsia wao bila ya<br />
kujihatarisha katika mimba au magonjwa ya ngono, yakiwemo VVU/UKIMWI. Hakuna tatizo<br />
litakalo tokea mwilini mwako hata kama ukipiga punyeto sana. Kitu pekee kinachoweza kutokea<br />
ni viungo vya uzazi kuvimba kwa sababu ya kuvisugua mno.<br />
97