08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

166<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

naMna Ya KuShuGhuliKia ShiniKiZO la KutuMia DaWa<br />

Kumudu shinikizo kutoka kwenye kundirika linalotaka utumie dawa kama wao ni vigumu sana.<br />

Hapa kuna hadithi fupi ya kijana mmoja:-<br />

Je, maelezo haya yanakukumbusha wewe pia hali ambayo imewahi kukutokea ukiwa na wenzako?<br />

Hawa marafiki walikuwa wanahitaji sana Jeckton avute. Kwa nini walimshinikiza?<br />

Watu wengi wanataka kuungwa mkono wanapofanya jambo wanalofikiri siyo sahihi. Wanafikiri<br />

makosa yao yanakuwa madogo kama mtu mwingine anafanya nao. Marafiki zao wanapofanya<br />

jambo la kijasiri pamoja nao, hawajisikii kuogopa sana kuhusu hatari iliyopo. Kama wako katika<br />

kikundi wanajisikia kustarehe na kufurahia burudani wanazozipata kwenye dawa. Ndiyo maana<br />

watakushinikiza sana wewe.<br />

Hapa kuna vidokezo vya jinsi ya kushughulikia hali hiyo:<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

jeckton kutoka Kenya (umri wa miaka 15)<br />

“Nilipokuwa na miaka 13, nilikuwa naelekea nyumbani nikiwa na<br />

baadhi ya marafiki zangu. Tulipita sehemu ambayo marafiki zangu<br />

mara nyingine wanaenda kukutana na baadhi ya marafiki zao.<br />

Tulipofika pale waliwakuta marafiki zao na wakapewa kifurushi<br />

cha bangi. Bila kupita muda, msichana mmoja akaanza kuvuta<br />

na akaniambia nivute pafu moja. Nilikataa, wakaanza kunicheka.<br />

Waliniita majina mabaya na wakaniambia niache kuwaaibisha.<br />

Waliniambia ilikuwa tamu sana na ingenifanya nijisikie vizuri. Kwa<br />

sababu sikutaka waelewe kwamba nilikuwa naogopa, niliamua kuvuta<br />

kidogo. Baada ya kuvuta kidogo, siwezi kusema yaliyotokea<br />

baada ya hapo maana sikumbuki tena. Nilichanganyikiwa kwa<br />

muda wa karibu siku tatu.”<br />

Kumbuka kwamba huhitaji kumfanya rafiki ajisikie vizuri kwa kumuunga mkono kufanya<br />

mambo ambayo siyo mazuri kwako.<br />

Kama ni rafiki wa kweli, unaweza kumwambia rafiki yako kuwa mambo anayoyafanya ni ya<br />

hatari.<br />

Uwe mwazi kwa wenzio kwamba hutaki kutumia dawa au kitu. Waonyeshe rafiki zako<br />

kwamba unazijua akili zako zilivyo na kwamba hata wakikusihi vipi hutabadilisha mawazo<br />

yako.<br />

Ondoka kama rafiki yako anazidi kukushinikiza au anaanza kukutukana ama kukucheka.<br />

Usiendelee kujadili suala hilo zaidi. Subiri hadi atakapokuwa hatumii dawa ndiyo mwanze<br />

kuzungumza kuhusu jambo hilo.<br />

Kofi kutoka Ghana (umri wa miaka 16)<br />

“Huwa nashinikizwa na marafiki zangu kutumia dawa za kulevya<br />

ninapokuwa nao, lakini ninajizuia mwenyewe na kuwaeleza kwa<br />

ujasiri kabisa kwamba nimeridhika bila ya kutumia dawa.”<br />

Mara nyingine tatizo linaweza kuwa kubwa zaidi kuliko kukataa shinikizo toka kwa marafiki.<br />

Unaweza kugundua kwamba rafiki yako analo tatizo kubwa la dawa au pombe, tatizo ambalo<br />

unaona linamharibia maisha yake. Hili nalo ni gumu kulitatua. Haya ni mambo machache<br />

unayoweza kufanya:<br />

•<br />

•<br />

•<br />

SURA YA 13 | MATUMIZI MABAYA YA DAWA<br />

Zungumza na rafiki yako kuhusu matumizi ya dawa wakati hajanywa au hayuko katika hali ya<br />

ulevi.<br />

Usimlaumu au kumkosoa rafiki yako. Hii itazua mabishano baina yenu. Badala yake lenga<br />

katika matatizo ya dawa na mwonyeshe rafiki yako kwamba unaogopa. Jaribu kumsaidia<br />

rafiki yako aelewe kwamba ana matatizo.<br />

Jaribu kumsaidia rafiki yako apate msaada na jaribu kumsaidia akwepe sehemu ambayo<br />

atapata shinikizo la kutumia dawa au pombe.<br />

Margaret kutoka Kenya (umri wa miaka 16)<br />

“Wengi wa marafiki zangu walikuwa wameshaharibiwa na dawa;<br />

lakini baada ya kujua hatari na ukweli kuhusu dawa niliamua kuwasaidia<br />

marafiki zangu. Wengi wamebadilika na mimi ninafurahi.”<br />

Wakati mwingine watu wenye matatizo kutokana na dawa hawako tayari kukusikiliza wewe na<br />

ushauri wako. Wanaweza kuzikataa juhudi zako za kusaidia na wanaweza kukukasirikia. Mnaweza<br />

mkaishia kuwa na mabishano makali na rafiki zako, lakini angalau dhamira yako itakuwa wazi na<br />

utakuwa umejitahidi kuwasaidia.<br />

Wakati wote upo uwezekano wa urafiki kuvunjika kutokana na tabia yako ya kutokubaliana na<br />

tabia zao.<br />

hanifa kutoka tanzania (umri wa miaka 17)<br />

“Nilikuwa na rafiki ambaye nilimwamini sana kwa kipindi kirefu,<br />

lakini sikujua mambo aliyokuwa anayafanya kwa kificho. Siku<br />

moja nilimkuta na watu wenye sura za ajabu, macho yake yalikuwa<br />

mekundu. Niligundua alikuwa ananuka bangi. Nilijaribu kuzungumza<br />

naye mara kwa mara lakini hakunisikiliza. Hivyo nilimtaka<br />

achague ama kuacha kutumia alichokuwa anatumia au kuacha<br />

kuzungumza na mimi. Nilifikiri angefanya uamuzi sahihi lakini<br />

nilikuwa nimekosea aliacha kuzungumza na mimi.”<br />

Inaweza kuwa vigumu sana kumpoteza rafiki lakini angalau ulisimama kwenye kanuni zako,<br />

ulijaribu kumsaidia rafiki na wewe binafsi hukujihusisha na hatari ya dawa. Mara chache, baada<br />

ya muda, rafiki atabadilika.<br />

hanifa kutoka tanzania (umri wa miaka 17)<br />

“Baada ya miezi kadhaa, rafiki yangu aligundua madhara ya dawa<br />

hizo kwa maisha yake, na akaniomba tuendelee kuwa marafiki<br />

tena. Kwa sababu nilimwonea huruma nilikubali.”<br />

167

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!