Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
166<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
naMna Ya KuShuGhuliKia ShiniKiZO la KutuMia DaWa<br />
Kumudu shinikizo kutoka kwenye kundirika linalotaka utumie dawa kama wao ni vigumu sana.<br />
Hapa kuna hadithi fupi ya kijana mmoja:-<br />
Je, maelezo haya yanakukumbusha wewe pia hali ambayo imewahi kukutokea ukiwa na wenzako?<br />
Hawa marafiki walikuwa wanahitaji sana Jeckton avute. Kwa nini walimshinikiza?<br />
Watu wengi wanataka kuungwa mkono wanapofanya jambo wanalofikiri siyo sahihi. Wanafikiri<br />
makosa yao yanakuwa madogo kama mtu mwingine anafanya nao. Marafiki zao wanapofanya<br />
jambo la kijasiri pamoja nao, hawajisikii kuogopa sana kuhusu hatari iliyopo. Kama wako katika<br />
kikundi wanajisikia kustarehe na kufurahia burudani wanazozipata kwenye dawa. Ndiyo maana<br />
watakushinikiza sana wewe.<br />
Hapa kuna vidokezo vya jinsi ya kushughulikia hali hiyo:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
jeckton kutoka Kenya (umri wa miaka 15)<br />
“Nilipokuwa na miaka 13, nilikuwa naelekea nyumbani nikiwa na<br />
baadhi ya marafiki zangu. Tulipita sehemu ambayo marafiki zangu<br />
mara nyingine wanaenda kukutana na baadhi ya marafiki zao.<br />
Tulipofika pale waliwakuta marafiki zao na wakapewa kifurushi<br />
cha bangi. Bila kupita muda, msichana mmoja akaanza kuvuta<br />
na akaniambia nivute pafu moja. Nilikataa, wakaanza kunicheka.<br />
Waliniita majina mabaya na wakaniambia niache kuwaaibisha.<br />
Waliniambia ilikuwa tamu sana na ingenifanya nijisikie vizuri. Kwa<br />
sababu sikutaka waelewe kwamba nilikuwa naogopa, niliamua kuvuta<br />
kidogo. Baada ya kuvuta kidogo, siwezi kusema yaliyotokea<br />
baada ya hapo maana sikumbuki tena. Nilichanganyikiwa kwa<br />
muda wa karibu siku tatu.”<br />
Kumbuka kwamba huhitaji kumfanya rafiki ajisikie vizuri kwa kumuunga mkono kufanya<br />
mambo ambayo siyo mazuri kwako.<br />
Kama ni rafiki wa kweli, unaweza kumwambia rafiki yako kuwa mambo anayoyafanya ni ya<br />
hatari.<br />
Uwe mwazi kwa wenzio kwamba hutaki kutumia dawa au kitu. Waonyeshe rafiki zako<br />
kwamba unazijua akili zako zilivyo na kwamba hata wakikusihi vipi hutabadilisha mawazo<br />
yako.<br />
Ondoka kama rafiki yako anazidi kukushinikiza au anaanza kukutukana ama kukucheka.<br />
Usiendelee kujadili suala hilo zaidi. Subiri hadi atakapokuwa hatumii dawa ndiyo mwanze<br />
kuzungumza kuhusu jambo hilo.<br />
Kofi kutoka Ghana (umri wa miaka 16)<br />
“Huwa nashinikizwa na marafiki zangu kutumia dawa za kulevya<br />
ninapokuwa nao, lakini ninajizuia mwenyewe na kuwaeleza kwa<br />
ujasiri kabisa kwamba nimeridhika bila ya kutumia dawa.”<br />
Mara nyingine tatizo linaweza kuwa kubwa zaidi kuliko kukataa shinikizo toka kwa marafiki.<br />
Unaweza kugundua kwamba rafiki yako analo tatizo kubwa la dawa au pombe, tatizo ambalo<br />
unaona linamharibia maisha yake. Hili nalo ni gumu kulitatua. Haya ni mambo machache<br />
unayoweza kufanya:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
SURA YA 13 | MATUMIZI MABAYA YA DAWA<br />
Zungumza na rafiki yako kuhusu matumizi ya dawa wakati hajanywa au hayuko katika hali ya<br />
ulevi.<br />
Usimlaumu au kumkosoa rafiki yako. Hii itazua mabishano baina yenu. Badala yake lenga<br />
katika matatizo ya dawa na mwonyeshe rafiki yako kwamba unaogopa. Jaribu kumsaidia<br />
rafiki yako aelewe kwamba ana matatizo.<br />
Jaribu kumsaidia rafiki yako apate msaada na jaribu kumsaidia akwepe sehemu ambayo<br />
atapata shinikizo la kutumia dawa au pombe.<br />
Margaret kutoka Kenya (umri wa miaka 16)<br />
“Wengi wa marafiki zangu walikuwa wameshaharibiwa na dawa;<br />
lakini baada ya kujua hatari na ukweli kuhusu dawa niliamua kuwasaidia<br />
marafiki zangu. Wengi wamebadilika na mimi ninafurahi.”<br />
Wakati mwingine watu wenye matatizo kutokana na dawa hawako tayari kukusikiliza wewe na<br />
ushauri wako. Wanaweza kuzikataa juhudi zako za kusaidia na wanaweza kukukasirikia. Mnaweza<br />
mkaishia kuwa na mabishano makali na rafiki zako, lakini angalau dhamira yako itakuwa wazi na<br />
utakuwa umejitahidi kuwasaidia.<br />
Wakati wote upo uwezekano wa urafiki kuvunjika kutokana na tabia yako ya kutokubaliana na<br />
tabia zao.<br />
hanifa kutoka tanzania (umri wa miaka 17)<br />
“Nilikuwa na rafiki ambaye nilimwamini sana kwa kipindi kirefu,<br />
lakini sikujua mambo aliyokuwa anayafanya kwa kificho. Siku<br />
moja nilimkuta na watu wenye sura za ajabu, macho yake yalikuwa<br />
mekundu. Niligundua alikuwa ananuka bangi. Nilijaribu kuzungumza<br />
naye mara kwa mara lakini hakunisikiliza. Hivyo nilimtaka<br />
achague ama kuacha kutumia alichokuwa anatumia au kuacha<br />
kuzungumza na mimi. Nilifikiri angefanya uamuzi sahihi lakini<br />
nilikuwa nimekosea aliacha kuzungumza na mimi.”<br />
Inaweza kuwa vigumu sana kumpoteza rafiki lakini angalau ulisimama kwenye kanuni zako,<br />
ulijaribu kumsaidia rafiki na wewe binafsi hukujihusisha na hatari ya dawa. Mara chache, baada<br />
ya muda, rafiki atabadilika.<br />
hanifa kutoka tanzania (umri wa miaka 17)<br />
“Baada ya miezi kadhaa, rafiki yangu aligundua madhara ya dawa<br />
hizo kwa maisha yake, na akaniomba tuendelee kuwa marafiki<br />
tena. Kwa sababu nilimwonea huruma nilikubali.”<br />
167