Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
52<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Mazoezi yana faida nyingine zaidi, yanaimarisha hisia<br />
zako, yanajenga kujiamini, yanakufanya ujisikie vizuri.<br />
Kama unajihisi kuwa na mfadhaiko, hali mbaya au<br />
huzuni, tembeatembea au cheza mchezo wa kurusha<br />
mpira.Fanya mchezo wa kukaa na kunyanyuka. Cheza<br />
mpirawa pete. Endesha baiskeli, ruka kamba, ogelea,<br />
Cheza mpira wa wavu au mpira wa meza. Fanya kitu<br />
chochote kitachofanya moyo wako uende kasi ili<br />
kuongeza morali.<br />
Mazoezi yanaweza pia yakawa njia nzuri ya kukufanya<br />
uwe hodari katika stadi muhimu za maisha, kama<br />
kujiamini, ushirikano na kufanya kazi kwa pamoja. Watu<br />
wengi kwanza hujifunza stadi hizi wakati wakicheza<br />
michezo au wakati wanapojiunga na timu.<br />
Kufanya mazoezi mengi haimaaanishi kuwa lazima<br />
ujiunge na klabu ya michezo. Kusaidia kazi za shambani,<br />
kwenye bustani au kuzunguka nyumba yanaweza kuwa mazoezi mazuri. Shughuli za nyumbani<br />
zinaweza kujenga mahusiano mazuri na wazazi wako.<br />
Baadhi ya watu ni wakimbiaji wazuri lakini wengine<br />
sio. Baadhi ya watu wana vipaji maalum vya mpira<br />
wa miguu, kukimbia kwa kasi au kuogelea vizuri,<br />
kama vile ambavyo watu wengine ni wazuri katika<br />
hisabati au katika kujifunza lugha. Hata kama wewe<br />
si mkimbiaji, unatakiwa kufanya mazoezi kwa wingi.<br />
Kila mtu ana mwili ambao unatakiwa autumie. Kwa<br />
mfano kwa kujinyoosha, kusukuma au kujaribu<br />
mambo kadhaa. Unaweza kujikuta unapofanya<br />
mazoezi unafurahi zaidi na zaidi. Unaweza ukawa<br />
mwana riadha bila ya wewe mwenyewe kujua!<br />
Iwapo hujazoea kufanya mazoezi, inaweza kuwa<br />
vigumu unapoanza. Unaweza kujikuta unashindwa<br />
kupumua wakati wa kukimbia. Mazoezi yanaweza<br />
Kuna njia nyingi nzuri za kufanya mazoezi kukufanya ujisikie vibaya na hivyo kutoendelea<br />
nayo. Kwa hiyo, anza taratibu. Tafuta mchezo<br />
unaoupenda na jenga nguvu zako, hivyo unaweza<br />
kufanya zaidi na zaidi. Nia ni kufanya moyo wako uende kasi, kujisikia kwamba unapumua<br />
haraka kuliko kawaida, na kuwa na joto mwilini. Jaribu kufanya hivi kwa angalau dakika 20, mara<br />
3 kwa wiki.<br />
Fanya mazoezi yako kila mara na utaona maendeleo mazuri.Ngozi yako itang’aa. Macho yako<br />
yatang’aa, utakuwa na furaha na raha. Utajiamini zaidi na kuwa na uwezo wa kuyakabili matatizo.<br />
Na kwa hakika utakuwa na nguvu na mwenye afya pia. Kwa hivyo endelea na mazoezi na usiache<br />
kufanya ati kwa sababu ni kipindi cha mitihani.Wakati wa mitihani ndio unahitaji kufanya mazoezi<br />
zaidi.<br />
SURA YA 5 | MABADILIKO YA MSINGI KATIKA KUTUNZA MWILI<br />
Ruvimbo kutoka Zimbabwe (umri;miaka 13)<br />
“Naendesha baiskeli ili kujishughulisha na<br />
kwa sababu za kiafya. Vijana wanatakiwa<br />
wajishughulishe, Dunia ina mambo mengi ya<br />
kufanya.”<br />
Godfrey, kutoka Zimbabwe (umri; miaka 19)<br />
“Napenda michezo, Nacheza mpira wa kikapu<br />
kuuweka mwili wangu imara na wenye afya<br />
nzuri.”<br />
Maumbile mazuri hupatikana kwa kufanya mazoezi;<br />
maumbile mabaya husababisha maumivu katika kifua na mgongo.<br />
MaPuMZiKO MaZuRi<br />
endelea na mpangilio wako wa mazoezi na<br />
utaona tofauti !<br />
Pamoja na chakula kizuri na mazoezi ya kutosha, unahitaji kupumzika vya kutosha. Kupumzika<br />
kunaruhusu mwili kuhifadhi zaidi nguvu. Kupumzika kunaweza kuwa katika hali ya kupumzika<br />
kimwili au kulala usingizi<br />
Tumia muda kupumzika kila siku kwa kusoma kitabu, kufanya kitu unachofurahia, kusikiliza redio,<br />
au kwa kutafakari maisha yako. Kwa kiwango kidogo, televisheni inaweza kukufanya upumzike,<br />
lakini usitumie muda mwingi kuangalia televisheni au video.<br />
Kulala ni njia muhimu ya kupumzika. Ni wakati wa kulala tu ndio moyo wako unapunguza mapigo<br />
na misuli yako inapumzika. Hii inaruhusu mwili wako kurudisha na kujiponya na hali ya mfadhiko<br />
au majeraha. Unahitaji kulala sana kipindi cha balehe kwa sababu mwili wako unatumia nguvu<br />
nyingi. Watu wengi wanahitaji kama kiasi cha masaa 8 ya kulala usiku mmoja. Baadhi ya watu<br />
wanahitaji pungufu, na baadhi ya watu wanahitaji zaidi. Kama, unajisikia kuchoka muda wote,<br />
hakikisha unakwenda kulala mapema. Mabadiliko yote yanayotokea mwilini mwako yanachosha,<br />
kwa hiyo hakikisha unaupa mwili wako nafasi ya kupumzika!<br />
53