08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

52<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Mazoezi yana faida nyingine zaidi, yanaimarisha hisia<br />

zako, yanajenga kujiamini, yanakufanya ujisikie vizuri.<br />

Kama unajihisi kuwa na mfadhaiko, hali mbaya au<br />

huzuni, tembeatembea au cheza mchezo wa kurusha<br />

mpira.Fanya mchezo wa kukaa na kunyanyuka. Cheza<br />

mpirawa pete. Endesha baiskeli, ruka kamba, ogelea,<br />

Cheza mpira wa wavu au mpira wa meza. Fanya kitu<br />

chochote kitachofanya moyo wako uende kasi ili<br />

kuongeza morali.<br />

Mazoezi yanaweza pia yakawa njia nzuri ya kukufanya<br />

uwe hodari katika stadi muhimu za maisha, kama<br />

kujiamini, ushirikano na kufanya kazi kwa pamoja. Watu<br />

wengi kwanza hujifunza stadi hizi wakati wakicheza<br />

michezo au wakati wanapojiunga na timu.<br />

Kufanya mazoezi mengi haimaaanishi kuwa lazima<br />

ujiunge na klabu ya michezo. Kusaidia kazi za shambani,<br />

kwenye bustani au kuzunguka nyumba yanaweza kuwa mazoezi mazuri. Shughuli za nyumbani<br />

zinaweza kujenga mahusiano mazuri na wazazi wako.<br />

Baadhi ya watu ni wakimbiaji wazuri lakini wengine<br />

sio. Baadhi ya watu wana vipaji maalum vya mpira<br />

wa miguu, kukimbia kwa kasi au kuogelea vizuri,<br />

kama vile ambavyo watu wengine ni wazuri katika<br />

hisabati au katika kujifunza lugha. Hata kama wewe<br />

si mkimbiaji, unatakiwa kufanya mazoezi kwa wingi.<br />

Kila mtu ana mwili ambao unatakiwa autumie. Kwa<br />

mfano kwa kujinyoosha, kusukuma au kujaribu<br />

mambo kadhaa. Unaweza kujikuta unapofanya<br />

mazoezi unafurahi zaidi na zaidi. Unaweza ukawa<br />

mwana riadha bila ya wewe mwenyewe kujua!<br />

Iwapo hujazoea kufanya mazoezi, inaweza kuwa<br />

vigumu unapoanza. Unaweza kujikuta unashindwa<br />

kupumua wakati wa kukimbia. Mazoezi yanaweza<br />

Kuna njia nyingi nzuri za kufanya mazoezi kukufanya ujisikie vibaya na hivyo kutoendelea<br />

nayo. Kwa hiyo, anza taratibu. Tafuta mchezo<br />

unaoupenda na jenga nguvu zako, hivyo unaweza<br />

kufanya zaidi na zaidi. Nia ni kufanya moyo wako uende kasi, kujisikia kwamba unapumua<br />

haraka kuliko kawaida, na kuwa na joto mwilini. Jaribu kufanya hivi kwa angalau dakika 20, mara<br />

3 kwa wiki.<br />

Fanya mazoezi yako kila mara na utaona maendeleo mazuri.Ngozi yako itang’aa. Macho yako<br />

yatang’aa, utakuwa na furaha na raha. Utajiamini zaidi na kuwa na uwezo wa kuyakabili matatizo.<br />

Na kwa hakika utakuwa na nguvu na mwenye afya pia. Kwa hivyo endelea na mazoezi na usiache<br />

kufanya ati kwa sababu ni kipindi cha mitihani.Wakati wa mitihani ndio unahitaji kufanya mazoezi<br />

zaidi.<br />

SURA YA 5 | MABADILIKO YA MSINGI KATIKA KUTUNZA MWILI<br />

Ruvimbo kutoka Zimbabwe (umri;miaka 13)<br />

“Naendesha baiskeli ili kujishughulisha na<br />

kwa sababu za kiafya. Vijana wanatakiwa<br />

wajishughulishe, Dunia ina mambo mengi ya<br />

kufanya.”<br />

Godfrey, kutoka Zimbabwe (umri; miaka 19)<br />

“Napenda michezo, Nacheza mpira wa kikapu<br />

kuuweka mwili wangu imara na wenye afya<br />

nzuri.”<br />

Maumbile mazuri hupatikana kwa kufanya mazoezi;<br />

maumbile mabaya husababisha maumivu katika kifua na mgongo.<br />

MaPuMZiKO MaZuRi<br />

endelea na mpangilio wako wa mazoezi na<br />

utaona tofauti !<br />

Pamoja na chakula kizuri na mazoezi ya kutosha, unahitaji kupumzika vya kutosha. Kupumzika<br />

kunaruhusu mwili kuhifadhi zaidi nguvu. Kupumzika kunaweza kuwa katika hali ya kupumzika<br />

kimwili au kulala usingizi<br />

Tumia muda kupumzika kila siku kwa kusoma kitabu, kufanya kitu unachofurahia, kusikiliza redio,<br />

au kwa kutafakari maisha yako. Kwa kiwango kidogo, televisheni inaweza kukufanya upumzike,<br />

lakini usitumie muda mwingi kuangalia televisheni au video.<br />

Kulala ni njia muhimu ya kupumzika. Ni wakati wa kulala tu ndio moyo wako unapunguza mapigo<br />

na misuli yako inapumzika. Hii inaruhusu mwili wako kurudisha na kujiponya na hali ya mfadhiko<br />

au majeraha. Unahitaji kulala sana kipindi cha balehe kwa sababu mwili wako unatumia nguvu<br />

nyingi. Watu wengi wanahitaji kama kiasi cha masaa 8 ya kulala usiku mmoja. Baadhi ya watu<br />

wanahitaji pungufu, na baadhi ya watu wanahitaji zaidi. Kama, unajisikia kuchoka muda wote,<br />

hakikisha unakwenda kulala mapema. Mabadiliko yote yanayotokea mwilini mwako yanachosha,<br />

kwa hiyo hakikisha unaupa mwili wako nafasi ya kupumzika!<br />

53

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!