Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
130<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Kumbuka kuwa mimba inaweza kutokea kama utafanya ngono isiyo salama mara moja tu.<br />
Mimba inaweza kutokea kama mwanamume atakojoa shahawa zake karibu na uke hata kama<br />
hamkujamiiana! Shahawa zikimwagwa nje ya mlango wa uke bado zinaweza kuogelea hadi<br />
kwenye mlango wa mfuko wa uzazi hadi kwenye tumbo la uzazi na kwenye mirija ya kupitisha yai.<br />
Utadhani hakuna uwezekano, lakini inatokea.<br />
Dalili Za MiMba<br />
Dalili ya wazi kuwa mimba imetungwa ni kukosa kupata hedhi. Hii ni kwa sababu ukuta wa mfuko<br />
wa kizazi hautoi damu mwanamke akiwa na mimba. Utando laini unabaki ndani ya mfuko wa<br />
kizazi na unatengeneza kiota laini kwa ajili ya mtoto kukua. Kukosekana kwa hedhi haina maana<br />
kuwa umepata mimba. Wasichana waliobalehe wanaweza kuwa na hedhi isiyo ya kawaida. Kwa<br />
miaka mingi siku za hedhi kwa baadhi ya wasichana balehe, zinaweza kuchelewa au zikakosekana<br />
mwezi mzima bila sababu yoyote.<br />
Dalili nyingine za mimba:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Matiti kuwa laini<br />
Kichefuchefu (hali ya kutaka kutapika) na kuwa na mate mdomoni.<br />
Uchovu (kujisikia umechoka sana)<br />
Kutaka kukojoa mara kwa mara<br />
Kupendelea kula vitu fulani,wakati mwingine visivyo vya kawaida.<br />
Wanawake wachache huwa hawaoni dalili zozote kati ya hizo hapo juu. Kwa mfano, wanawake<br />
wengine hutoa damu kidogo sana wakati wa miezi mitatu ya mwanzo ya mimba zao na hivyo<br />
wanaweza kufikiri hedhi imekuwa na damu kidogo kuliko kawaida.<br />
Kama huna uhakika kuwa umepata au hujapata mimba, unaweza kufanya kipimo cha mimba.<br />
Katika sehemu nyingine, unaweza kununua kipimo cha mimba kwenye maduka ya dawa. Vilevile,<br />
unaweza kufanyiwa kipimo cha mimba kwenye kliniki. Mara nyingine kipimo kinafanywa kwa<br />
kupima mkojo na unaweza kugundua viini fulani ambavyo vinatengenezwa na mwili wakati wa<br />
mimba. Dakitari au nesi wa kituo cha afya anaweza vilevile akakufanyia uchunguzi wa mwili ili<br />
kuona kama una mimba au la.<br />
Mimba inachukuwa wiki 40 kabla ya mtoto kuzaliwa(toka mwanzo wa hedhi yako ya mwisho).<br />
Hadi utakapokosa hedhi yako - kama siku 28 baada ya siku ya mwisho ya siku zako za hedhi<br />
iliyopita - kibonge cha seli nyingi, yaani kiinitete kitakuwa kinakua katika mfuko wa kizazi kwa<br />
karibu wiki nzima.<br />
Kiinitete kinakua haraka sana. Wiki sita baada ya hedhi yako ya mwisho, ubongo na uti wa<br />
mgongo vinakuwa vimeanza kutengenezwa na moyo unaanza kupiga. Katika wiki 9 kiinitete<br />
kinaitwa fitasi. Katika wiki ya 12 fitasi inatambulika kama binadamu ila inakuwa na kichwa<br />
kikubwa. Katika wiki 20 (miezi 5) mwanamke anaweza akajisikia fitasi inachezacheza au<br />
kuzunguka ndani ya tumbo lake. Fitasi inaweza kugeuka au kusogea na inaweza pia ikashituka<br />
kukiwa na kelele zenye sauti ya juu.<br />
SURA YA 11 | MIMBA NA UZUIAJI WA MIMBA<br />
Ukuaji na maendeleo ya mtoto ndani ya tumbo la uzazi<br />
hataRi Za MiMba na uZaZi KWa WaSichana balehe<br />
Mimba ni hatari kwa kila mwanamke lakini ni hatari zaidi kwa wasichana balehe. Tatizo kubwa<br />
kwa wasichana chini ya miaka 20 ni nyonga. Mifupa inayozunguka mfereji wa kutolea mtoto<br />
haujakua vizuri. Wasichana wanaopata mimba katika umri mdogo wanapata taabu katika kuzaa<br />
kwa sababu mlango wa uzazi kwenye mifupa ya nyonga ni midogo mno na mtoto hawezi kupita.<br />
Tatizo hili linaitwa uzazi wa kukwama.<br />
Kama mtoto hawezi kutoka nje inabidi mtoto atolewe kwa njia ya upasuaji. Vijijini, wanawake<br />
wengi wenye matatizo kama haya huwa hawawezi kufika hospitali kwa muda unaotakiwa. Mtoto<br />
anaweza kufia tumboni. Isitoshe mfuko wa kizazi unaweza kuchanika kwa sababu ya kipindi<br />
kirefu cha uchungu na mwanamke anaweza kufa kwa kuvuja damu nyingi. Hii ni sababu mojawapo<br />
inayowafanya wasichana balehe wengi wadogo kufa wakati wa kuzaa.<br />
131