08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

130<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Kumbuka kuwa mimba inaweza kutokea kama utafanya ngono isiyo salama mara moja tu.<br />

Mimba inaweza kutokea kama mwanamume atakojoa shahawa zake karibu na uke hata kama<br />

hamkujamiiana! Shahawa zikimwagwa nje ya mlango wa uke bado zinaweza kuogelea hadi<br />

kwenye mlango wa mfuko wa uzazi hadi kwenye tumbo la uzazi na kwenye mirija ya kupitisha yai.<br />

Utadhani hakuna uwezekano, lakini inatokea.<br />

Dalili Za MiMba<br />

Dalili ya wazi kuwa mimba imetungwa ni kukosa kupata hedhi. Hii ni kwa sababu ukuta wa mfuko<br />

wa kizazi hautoi damu mwanamke akiwa na mimba. Utando laini unabaki ndani ya mfuko wa<br />

kizazi na unatengeneza kiota laini kwa ajili ya mtoto kukua. Kukosekana kwa hedhi haina maana<br />

kuwa umepata mimba. Wasichana waliobalehe wanaweza kuwa na hedhi isiyo ya kawaida. Kwa<br />

miaka mingi siku za hedhi kwa baadhi ya wasichana balehe, zinaweza kuchelewa au zikakosekana<br />

mwezi mzima bila sababu yoyote.<br />

Dalili nyingine za mimba:<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

Matiti kuwa laini<br />

Kichefuchefu (hali ya kutaka kutapika) na kuwa na mate mdomoni.<br />

Uchovu (kujisikia umechoka sana)<br />

Kutaka kukojoa mara kwa mara<br />

Kupendelea kula vitu fulani,wakati mwingine visivyo vya kawaida.<br />

Wanawake wachache huwa hawaoni dalili zozote kati ya hizo hapo juu. Kwa mfano, wanawake<br />

wengine hutoa damu kidogo sana wakati wa miezi mitatu ya mwanzo ya mimba zao na hivyo<br />

wanaweza kufikiri hedhi imekuwa na damu kidogo kuliko kawaida.<br />

Kama huna uhakika kuwa umepata au hujapata mimba, unaweza kufanya kipimo cha mimba.<br />

Katika sehemu nyingine, unaweza kununua kipimo cha mimba kwenye maduka ya dawa. Vilevile,<br />

unaweza kufanyiwa kipimo cha mimba kwenye kliniki. Mara nyingine kipimo kinafanywa kwa<br />

kupima mkojo na unaweza kugundua viini fulani ambavyo vinatengenezwa na mwili wakati wa<br />

mimba. Dakitari au nesi wa kituo cha afya anaweza vilevile akakufanyia uchunguzi wa mwili ili<br />

kuona kama una mimba au la.<br />

Mimba inachukuwa wiki 40 kabla ya mtoto kuzaliwa(toka mwanzo wa hedhi yako ya mwisho).<br />

Hadi utakapokosa hedhi yako - kama siku 28 baada ya siku ya mwisho ya siku zako za hedhi<br />

iliyopita - kibonge cha seli nyingi, yaani kiinitete kitakuwa kinakua katika mfuko wa kizazi kwa<br />

karibu wiki nzima.<br />

Kiinitete kinakua haraka sana. Wiki sita baada ya hedhi yako ya mwisho, ubongo na uti wa<br />

mgongo vinakuwa vimeanza kutengenezwa na moyo unaanza kupiga. Katika wiki 9 kiinitete<br />

kinaitwa fitasi. Katika wiki ya 12 fitasi inatambulika kama binadamu ila inakuwa na kichwa<br />

kikubwa. Katika wiki 20 (miezi 5) mwanamke anaweza akajisikia fitasi inachezacheza au<br />

kuzunguka ndani ya tumbo lake. Fitasi inaweza kugeuka au kusogea na inaweza pia ikashituka<br />

kukiwa na kelele zenye sauti ya juu.<br />

SURA YA 11 | MIMBA NA UZUIAJI WA MIMBA<br />

Ukuaji na maendeleo ya mtoto ndani ya tumbo la uzazi<br />

hataRi Za MiMba na uZaZi KWa WaSichana balehe<br />

Mimba ni hatari kwa kila mwanamke lakini ni hatari zaidi kwa wasichana balehe. Tatizo kubwa<br />

kwa wasichana chini ya miaka 20 ni nyonga. Mifupa inayozunguka mfereji wa kutolea mtoto<br />

haujakua vizuri. Wasichana wanaopata mimba katika umri mdogo wanapata taabu katika kuzaa<br />

kwa sababu mlango wa uzazi kwenye mifupa ya nyonga ni midogo mno na mtoto hawezi kupita.<br />

Tatizo hili linaitwa uzazi wa kukwama.<br />

Kama mtoto hawezi kutoka nje inabidi mtoto atolewe kwa njia ya upasuaji. Vijijini, wanawake<br />

wengi wenye matatizo kama haya huwa hawawezi kufika hospitali kwa muda unaotakiwa. Mtoto<br />

anaweza kufia tumboni. Isitoshe mfuko wa kizazi unaweza kuchanika kwa sababu ya kipindi<br />

kirefu cha uchungu na mwanamke anaweza kufa kwa kuvuja damu nyingi. Hii ni sababu mojawapo<br />

inayowafanya wasichana balehe wengi wadogo kufa wakati wa kuzaa.<br />

131

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!