Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
172<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
<strong>Ndoto</strong> yako ni nini? Ungependa uwe nani? Unajifikiriaje mwenyewe katika miaka mitano ijayo?<br />
Katika miaka15? Utakuwa nani na utakuwa unafanya nini?<br />
Sura hii inahusu kutimiza ndoto zako. Inahusu kuzifikiria ndoto zako na kutafakari ni kwa vipi<br />
unaweza kuzifikia. Inahusu kufanya uamuzi mzuri wa busara na utakaokufikisha karibu na ndoto<br />
zako. Aidha, inahusu namna ya kumudu vipingamizi vitakavyojitokeza katika maisha.<br />
Si jambo rahisi kufanikisha ndoto. Inahitaji kufanya kazi kwa bidii na kuwa na dhamira/nia. Kwa<br />
hiyo, jambo muhimu ni kujishughulisha na kufanya kazi kwa bidii. Fanya vitendo! Usikae chini na<br />
kusubiri mambo yakutokee. Unatakiwa kuyajenga maisha yako ya baadaye.<br />
KuZitaMbua nDOtO ZaKO.<br />
Watu wengine wana ndoto nyingi sana na zinabadilika kila wakati. Kwa mfano mchukue Remijia<br />
wa Tanzania:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Alipokuwa na miaka 6 alitaka kuwa ofisa wa polisi.<br />
Alipokuwa na miaka 8 alitaka kuwa kapteni wa meli.<br />
Alipokuwa na miaka 10 alitaka kuwa rubani wa ndege.<br />
Alipokuwa na miaka 13 alitaka kuwa mwalimu.<br />
Sasa ana miaka 19 anataka kuwa mhandisi.<br />
Kwa nini ndoto hubadilikabadilika? Je, ni vibaya kuwa na ndoto nyingi<br />
zilizo tofauti? Hapana! <strong>Ndoto</strong> ni nzuri, zinatia hamasa na zinakufanya<br />
ufanye kazi kwa bidii. Zinakufanya uangalie maisha ya baadaye na<br />
uwe na mipango thabiti.<br />
Watu wengine wanaelekea kuwa na ndoto chache. Hawajui<br />
wangependa wawe nani wakiwa wakubwa. Wanapata shida kujifikiria<br />
watakuwa vipi miaka 5 ijayo.<br />
Kama yanakugusa, usihofu. Hili ni jambo la kawaida! Haina maana<br />
kuwa huna ndoto, bali ina maana kuwa bado hujafikiria ndoto zako ni<br />
zipi. Lakini, unaweza kuanza sasa kuzitambua ndoto zako.<br />
<strong>Ndoto</strong> za watu wengi zinaathiriwa na watu wanaowazunguka. Kwa<br />
hiyo, kwanza angalia unazungukwa na nini. Fikiria kuhusu watu<br />
walio ndani ya jamii. Ni nani unaowahusudu? Ni watu gani<br />
unaowaheshimu? Mtu anaweza kuwa mwalimu<br />
ambaye anajua majibu ya maswali yote<br />
yanayoulizwa. Anaweza kuwa ni daktari<br />
ambaye alijua kilichokuwa kinakufanya<br />
uumwe miezi michache iliyopita.<br />
Anaweza akawa mchungaji wa kanisa<br />
lako. Wanaweza kuwa wazazi wako.<br />
Pata muda wa kutafakari ndoto zako za baadaye<br />
SURA YA 14 | KUTIMIZA NDOTO ZAKO<br />
Pili, usiruhusu ndoto zako zikakwamishwa na mambo unayoyaona. Angalia hata nje ya jumuia<br />
yako. Kuna mtu ambaye umemsoma kwenye gazeti au kitabuni ambaye alifanya jambo ambalo<br />
linakushangaza? Pengine ni mwanasayansi ambaye anajifunza jinsi tembo wanavyowasiliana wao<br />
kwa wao. Pengine ni muuguzi anayewahudumia wakimbizi katikati ya uwanja wa vita. Wapo watu<br />
wengi wanaofanya mambo mengi mazuri yanayovutia na yenye manufaa na maisha yao. Watu<br />
hawa wanaweza kuwa mfano mzuri wa kuigwa. Wanaweza kukuanzishia ndoto kuhusu maisha<br />
yako ya baadaye.<br />
Tatu, yaruhusu mawazo yako “yapae angani” usijiwekee mipaka ya vitu ambavyo unaweza<br />
kufanya au ambavyo huwezi kuvifanya. Kwa mfano, usiiache ndoto kwa sababu ya mawazo<br />
yaliyopitwa na wakati, kama mawazo kuhusu kazi wanazoweza kufanya wanaume pekee au<br />
wanawake pekee. Mambo yanaenda yakibadilika. Wanawake siku hizi wanafanya kazi ambazo<br />
mama zao hawakuwahi kufikiria kuzifanya. Sasa hivi wanawake wanaweza kuwa wahandisi,<br />
marubani, madaktari, wanariadha, wanasayansi, maprofesa, wanaanga, Marais, waandishi wa<br />
habari n.k. Kama ni mvulana au msichana, unaweza kuwa mtu unayetaka kuwa, ikiwa utadhamiria<br />
na kufanya kazi kwa bidii.<br />
MiPanGO Ya baaDaYe KuhuSu KaZi<br />
Vijana balehe wachache wana vipaji vya ziada katika taaluma fulani, kama hisabati, muziki au<br />
kuchora. Utafikiri kipaji kimewachagua. Wanakuwa wataalamu wazuri wa hisabati, wasanii,<br />
walimu na viongozi wa kwaya au wasanifu majengo.<br />
Watu wengine wanapendelea kitu kimoja tangu utoto wao, na mvuto huo mkubwa unarahisisha<br />
sana wakati wa kutoa uamuzi kuhusu watakuwa nani. Unaweza kumsikia mzazi akisema “wakati<br />
wote tulijua kwamba John atakuwa mganga wa mifugo. Alianza kuwahudumia wanyama wadogo<br />
alipokuwa na umri wa miaka minne tu.<br />
Watu kama hawa, maisha yao yanaonekana kuwa rahisi. Inaonekana kana kwamba njia yao ya<br />
kazi imenyooka. Uamuzi wao unaonekana kuwa ni rahisi kwa sababu wanajua kabisa wanataka<br />
kufanya nini, na wanacho kipaji katika eneo hilo maalumu.<br />
Wengi hatuko hivyo. Wengi ni watu wa kawaida, wenye akili ambao tunaweza kufanya vizuri<br />
katika mambo tofauti. Uwezekano wa kuwa nani au kufanya nini ni matokeo ya mchanganyiko wa<br />
yale tunayoyapenda na tusiyoyapenda, uwezo wetu na utayari wa kufanya kazi kwa bidii na fursa<br />
tunazopata.<br />
Kufanikisha ndoto kwa watu wengi ni njia ndefu yenye kona nyingi. Wakati wote siyo moja kwa<br />
moja na hatua sahihi za kuchukua haziko wazi. Zaidi ya hapo vikwazo visivyotegemewa vinaweza<br />
kujitokeza njiani. Ni mambo ambayo yanatakiwa kushughulikiwa kwa makini sana.<br />
Jitahidi kujitokeza kwenye kazi nyingi iwezekanavyo. Bila kufanya hivyo huwezi kufahamu nafasi<br />
gani zipo duniani kwa ajili yako? Katika nchi nyingine, vijana balehe wanajitolea kufanya kazi<br />
katika mashirika mbalimbali wakati wa likizo. Wakati mwingine wanapata malipo kidogo ya<br />
kutosha usafiri kwenda na kutoka nyumbani. Lakini mara nyingi hawapati chochote. Wanajitolea<br />
tu.<br />
Usifikiri kwamba kwa vile jambo fulani siyo la shule na siyo la kazi ya kulipwa basi halina<br />
thamani. Iwapo unaweza kupata kazi ya kujitolea, pengine unaweza kupata uzoefu mzuri na<br />
wenye manufaa.<br />
173