08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

172<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

<strong>Ndoto</strong> yako ni nini? Ungependa uwe nani? Unajifikiriaje mwenyewe katika miaka mitano ijayo?<br />

Katika miaka15? Utakuwa nani na utakuwa unafanya nini?<br />

Sura hii inahusu kutimiza ndoto zako. Inahusu kuzifikiria ndoto zako na kutafakari ni kwa vipi<br />

unaweza kuzifikia. Inahusu kufanya uamuzi mzuri wa busara na utakaokufikisha karibu na ndoto<br />

zako. Aidha, inahusu namna ya kumudu vipingamizi vitakavyojitokeza katika maisha.<br />

Si jambo rahisi kufanikisha ndoto. Inahitaji kufanya kazi kwa bidii na kuwa na dhamira/nia. Kwa<br />

hiyo, jambo muhimu ni kujishughulisha na kufanya kazi kwa bidii. Fanya vitendo! Usikae chini na<br />

kusubiri mambo yakutokee. Unatakiwa kuyajenga maisha yako ya baadaye.<br />

KuZitaMbua nDOtO ZaKO.<br />

Watu wengine wana ndoto nyingi sana na zinabadilika kila wakati. Kwa mfano mchukue Remijia<br />

wa Tanzania:<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

Alipokuwa na miaka 6 alitaka kuwa ofisa wa polisi.<br />

Alipokuwa na miaka 8 alitaka kuwa kapteni wa meli.<br />

Alipokuwa na miaka 10 alitaka kuwa rubani wa ndege.<br />

Alipokuwa na miaka 13 alitaka kuwa mwalimu.<br />

Sasa ana miaka 19 anataka kuwa mhandisi.<br />

Kwa nini ndoto hubadilikabadilika? Je, ni vibaya kuwa na ndoto nyingi<br />

zilizo tofauti? Hapana! <strong>Ndoto</strong> ni nzuri, zinatia hamasa na zinakufanya<br />

ufanye kazi kwa bidii. Zinakufanya uangalie maisha ya baadaye na<br />

uwe na mipango thabiti.<br />

Watu wengine wanaelekea kuwa na ndoto chache. Hawajui<br />

wangependa wawe nani wakiwa wakubwa. Wanapata shida kujifikiria<br />

watakuwa vipi miaka 5 ijayo.<br />

Kama yanakugusa, usihofu. Hili ni jambo la kawaida! Haina maana<br />

kuwa huna ndoto, bali ina maana kuwa bado hujafikiria ndoto zako ni<br />

zipi. Lakini, unaweza kuanza sasa kuzitambua ndoto zako.<br />

<strong>Ndoto</strong> za watu wengi zinaathiriwa na watu wanaowazunguka. Kwa<br />

hiyo, kwanza angalia unazungukwa na nini. Fikiria kuhusu watu<br />

walio ndani ya jamii. Ni nani unaowahusudu? Ni watu gani<br />

unaowaheshimu? Mtu anaweza kuwa mwalimu<br />

ambaye anajua majibu ya maswali yote<br />

yanayoulizwa. Anaweza kuwa ni daktari<br />

ambaye alijua kilichokuwa kinakufanya<br />

uumwe miezi michache iliyopita.<br />

Anaweza akawa mchungaji wa kanisa<br />

lako. Wanaweza kuwa wazazi wako.<br />

Pata muda wa kutafakari ndoto zako za baadaye<br />

SURA YA 14 | KUTIMIZA NDOTO ZAKO<br />

Pili, usiruhusu ndoto zako zikakwamishwa na mambo unayoyaona. Angalia hata nje ya jumuia<br />

yako. Kuna mtu ambaye umemsoma kwenye gazeti au kitabuni ambaye alifanya jambo ambalo<br />

linakushangaza? Pengine ni mwanasayansi ambaye anajifunza jinsi tembo wanavyowasiliana wao<br />

kwa wao. Pengine ni muuguzi anayewahudumia wakimbizi katikati ya uwanja wa vita. Wapo watu<br />

wengi wanaofanya mambo mengi mazuri yanayovutia na yenye manufaa na maisha yao. Watu<br />

hawa wanaweza kuwa mfano mzuri wa kuigwa. Wanaweza kukuanzishia ndoto kuhusu maisha<br />

yako ya baadaye.<br />

Tatu, yaruhusu mawazo yako “yapae angani” usijiwekee mipaka ya vitu ambavyo unaweza<br />

kufanya au ambavyo huwezi kuvifanya. Kwa mfano, usiiache ndoto kwa sababu ya mawazo<br />

yaliyopitwa na wakati, kama mawazo kuhusu kazi wanazoweza kufanya wanaume pekee au<br />

wanawake pekee. Mambo yanaenda yakibadilika. Wanawake siku hizi wanafanya kazi ambazo<br />

mama zao hawakuwahi kufikiria kuzifanya. Sasa hivi wanawake wanaweza kuwa wahandisi,<br />

marubani, madaktari, wanariadha, wanasayansi, maprofesa, wanaanga, Marais, waandishi wa<br />

habari n.k. Kama ni mvulana au msichana, unaweza kuwa mtu unayetaka kuwa, ikiwa utadhamiria<br />

na kufanya kazi kwa bidii.<br />

MiPanGO Ya baaDaYe KuhuSu KaZi<br />

Vijana balehe wachache wana vipaji vya ziada katika taaluma fulani, kama hisabati, muziki au<br />

kuchora. Utafikiri kipaji kimewachagua. Wanakuwa wataalamu wazuri wa hisabati, wasanii,<br />

walimu na viongozi wa kwaya au wasanifu majengo.<br />

Watu wengine wanapendelea kitu kimoja tangu utoto wao, na mvuto huo mkubwa unarahisisha<br />

sana wakati wa kutoa uamuzi kuhusu watakuwa nani. Unaweza kumsikia mzazi akisema “wakati<br />

wote tulijua kwamba John atakuwa mganga wa mifugo. Alianza kuwahudumia wanyama wadogo<br />

alipokuwa na umri wa miaka minne tu.<br />

Watu kama hawa, maisha yao yanaonekana kuwa rahisi. Inaonekana kana kwamba njia yao ya<br />

kazi imenyooka. Uamuzi wao unaonekana kuwa ni rahisi kwa sababu wanajua kabisa wanataka<br />

kufanya nini, na wanacho kipaji katika eneo hilo maalumu.<br />

Wengi hatuko hivyo. Wengi ni watu wa kawaida, wenye akili ambao tunaweza kufanya vizuri<br />

katika mambo tofauti. Uwezekano wa kuwa nani au kufanya nini ni matokeo ya mchanganyiko wa<br />

yale tunayoyapenda na tusiyoyapenda, uwezo wetu na utayari wa kufanya kazi kwa bidii na fursa<br />

tunazopata.<br />

Kufanikisha ndoto kwa watu wengi ni njia ndefu yenye kona nyingi. Wakati wote siyo moja kwa<br />

moja na hatua sahihi za kuchukua haziko wazi. Zaidi ya hapo vikwazo visivyotegemewa vinaweza<br />

kujitokeza njiani. Ni mambo ambayo yanatakiwa kushughulikiwa kwa makini sana.<br />

Jitahidi kujitokeza kwenye kazi nyingi iwezekanavyo. Bila kufanya hivyo huwezi kufahamu nafasi<br />

gani zipo duniani kwa ajili yako? Katika nchi nyingine, vijana balehe wanajitolea kufanya kazi<br />

katika mashirika mbalimbali wakati wa likizo. Wakati mwingine wanapata malipo kidogo ya<br />

kutosha usafiri kwenda na kutoka nyumbani. Lakini mara nyingi hawapati chochote. Wanajitolea<br />

tu.<br />

Usifikiri kwamba kwa vile jambo fulani siyo la shule na siyo la kazi ya kulipwa basi halina<br />

thamani. Iwapo unaweza kupata kazi ya kujitolea, pengine unaweza kupata uzoefu mzuri na<br />

wenye manufaa.<br />

173

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!