08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

12<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Pia, weka akilini haya: Watu wa umri wako mara nyingi wanajua taarifa nyingi za uongo kuliko za<br />

ukweli hasa inapokuwa ni za kuelezea balehe na kujamiiana. Marafiki zako wanaweza kukueleza<br />

mambo ambayo si ya kweli, hivyo unahitaji kufahamu wapi uende ili kupata ukweli. Kwa mfano,<br />

unaweza kuambiwa kwamba, matiti au uume utakua iwapo utajamiiana. Au unaweza kutaniwa<br />

kwamba matiti yako ni makubwa kwa sababu umekwishajamiiana. Hali kadhalika unaweza<br />

kusikia kwamba chunusi ni dalili za kwamba unatakiwa ujamiiane. Lakini hakuna lolote katika<br />

haya lenye ukweli. Yote ni uzushi/uwongo.<br />

Uzushi kama huu unaweza kuleta hatari zaidi kwa sababu unaongeza hofu. Uzushi kama huu<br />

unakufanya ufikirie kwamba unaweza kufanya mambo ili kubadilisha yale ambayo huwezi<br />

kuyadhibiti.<br />

VichOcheO (hOMOni)<br />

Ni kitu gani hudhibiti mabadiliko ndani ya mwili wako? Ni kitu gani hufanya ukue haraka au<br />

taratibu? Ni kitu gani hukufanya uongezeke?<br />

Mwili wako wakati wote unatengeneza homoni, ambazo ni kemikali tarishi maalumu ambayo<br />

huuambia mwili namna gani na lini ubadilike na kukua. Mfoko wa ukuaji wako husababishwa na<br />

homoni za ukuaji ambazo zinatoka kwenye ubongo kwa wingi.<br />

Pamoja na homoni za ukuaji, homoni za jinsi nazo huanza kutolewa wakati wa balehe. Kwa<br />

wasichana homoni za jinsia zinatengenezwa ndani ya ovari na kwa wavulana zainatengenezwa<br />

ndani ya korodani. Homoni za jinsi ndizo zinazosababisha tofauti katika maumbile ya mwanaume<br />

na mwanamke. Wasichana wanapoingia kipindi cha balehe nyonga zao huongezeka. Kawaida<br />

nyonga hukua haraka kuliko kifua . Nyonga ya msichana hupanuka na kujiviringa, na kiuno<br />

huonekana kidogo na chembamba. Matiti vilevile huanza kukua.<br />

Kwa wavulana, homoni za jinsia husababisha kifua kupanuka, mikono na miguu inakuwa minene<br />

yenye misuli. Matiti ya wavulana hayabadiliki sana kama ya wasichana yanavyobadilika wakati<br />

wa balehe, lakini hubadilika kidogo. Kwa wavulana wengine, matiti yao hukua kipindi cha balehe<br />

lakini kawaida hupotea kadri muda unavyokwenda.<br />

Homoni huathiri pia hisia zako. Vijana wengi hujisikia kuwa na hisia kali. Dakika moja tu anaweza<br />

kuwa na furaha na msisimko, lakini dakika inayofuata akawa na huzuni karibia kulia. Anaweza<br />

kujisikia vizuri siku moja na vibaya siku inayofuata. Mabadiliko haya katika hisia yanaitwa “hisia<br />

za kuyumba”.<br />

Kipindi cha balehe huwa kina ambatana na hisia kali<br />

SURA YA 2 | MABADILIKO YA MWILI<br />

Jambo hili huwatokea vijana wengi mara kwa mara. Wakati wa ujana balehe, utengenezaji wa<br />

homoni huongezeka ghafla, kitendo ambacho huwafanya vijana wengi wawe na hisia kali za aina<br />

mbalimbali.<br />

Baadaye katika maisha utengenezaji wa homoni utapungua na utajisikia unao uwezo wa kudhibiti<br />

hisia.<br />

Weka akilini kwamba mabadiliko yote ya kimwili, kihisia na kiakili yanayotokea wakati wa balehe<br />

yanasababishwa na homoni zinazotengenezwa na mwili wako. Hakuna unaloweza kufanya<br />

kuharakisha au kuchelewesha utengenezaji wa homoni. Jaribu kukumbuka tu kwamba wewe ni wa<br />

pekee na huna kasoro yoyote.<br />

Via VYa uZaZi “SeheMu Za SiRi”<br />

Pamoja na kuleta mabadiliko katika umbo la mvulana na msichana, homoni hufanya via vya<br />

uzazi kukua. Via vya uzazi maana yake ni zile sehemu za siri za mwili wako ambazo mara nyingi<br />

zinafunikwa na chupi/nguo za ndani.<br />

Kabla hujawa kijana balehe, sehemu za siri zilikuwa kwa ajili ya kujisaidia tu (kukojoa). Wakati wa<br />

ujana balehe hata hivyo, sehemu za siri zinakuwa kubwa. Kwa wasichana ngozi na tishu huwa laini<br />

na yenye mafuta mafuta, kwa wavulana uume huanza kurefuka na kunenepa. Korodani vilevile<br />

hukua na kuanza kutengeneza mbegu za kiume.<br />

Kipindi cha balehe via vya uzazi huanza kutengeneza majimaji pia.<br />

Wavulana huanza kutengeneza shahawa, majimaji yaliyo kama kamasi ambayo mbegu za kiume<br />

huogelea. Shahawa hutoka nje ya uume wakati mvulana anapofikia mshindo. Wasichana vilevile<br />

hutoa majimaji ya ukeni na damu ya hedhi. (soma sura ya 3 na ya 4 kwa maelezo zaidi kuhusu<br />

wavulana na wasichana)<br />

nYWele Za MWilini na MabaDiliKO Ya nGOZi<br />

Ngozi yako na nywele za mwilini hubadilika vilevile katika kipindi cha balehe. Kwa vijana wengi<br />

ngozi inakuwa na mafuta. Ngozi ya utotoni hupotea. Hii hupelekea chunusi kutoka, jambo ambalo<br />

ni tatizo la kawaida kwa vijana wengi (soma sura ya 5 kwa maelezo zaidi kuhusu utunzaji mzuri<br />

wa ngozi).<br />

Dalili nyingine ya balehe ni nywele kuota sehemu mpya za mwili. Wavulana na wasichana wote<br />

wanaweza kuota nywele kidogo miguuni na mikononi. Kwa kuongezea wavulana huota nywele<br />

sehemu za siri, usoni kifuani na kwapani. Wasichana vilevile huota nywele sehemu za siri na<br />

kwapani.<br />

Nywele zinazoota sehemu za siri zinaitwa mavuzi, watu wengine wana mavuzi mengi na wengine<br />

wanayo kidogo. Mavuzi husaidia kufanya eneo la via vya uzazi liwe safi, jambo ambalo ni zuri<br />

sana kwani ngozi inayozunguka via vya uzazi ni laini/nyororo sana na ni rahisi kuumia.Mavuzi<br />

husaidia kuzuia jasho na vitu vingine kutoka kwenye ngozi laini ya via vya uzazi.<br />

13

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!