Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
12<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Pia, weka akilini haya: Watu wa umri wako mara nyingi wanajua taarifa nyingi za uongo kuliko za<br />
ukweli hasa inapokuwa ni za kuelezea balehe na kujamiiana. Marafiki zako wanaweza kukueleza<br />
mambo ambayo si ya kweli, hivyo unahitaji kufahamu wapi uende ili kupata ukweli. Kwa mfano,<br />
unaweza kuambiwa kwamba, matiti au uume utakua iwapo utajamiiana. Au unaweza kutaniwa<br />
kwamba matiti yako ni makubwa kwa sababu umekwishajamiiana. Hali kadhalika unaweza<br />
kusikia kwamba chunusi ni dalili za kwamba unatakiwa ujamiiane. Lakini hakuna lolote katika<br />
haya lenye ukweli. Yote ni uzushi/uwongo.<br />
Uzushi kama huu unaweza kuleta hatari zaidi kwa sababu unaongeza hofu. Uzushi kama huu<br />
unakufanya ufikirie kwamba unaweza kufanya mambo ili kubadilisha yale ambayo huwezi<br />
kuyadhibiti.<br />
VichOcheO (hOMOni)<br />
Ni kitu gani hudhibiti mabadiliko ndani ya mwili wako? Ni kitu gani hufanya ukue haraka au<br />
taratibu? Ni kitu gani hukufanya uongezeke?<br />
Mwili wako wakati wote unatengeneza homoni, ambazo ni kemikali tarishi maalumu ambayo<br />
huuambia mwili namna gani na lini ubadilike na kukua. Mfoko wa ukuaji wako husababishwa na<br />
homoni za ukuaji ambazo zinatoka kwenye ubongo kwa wingi.<br />
Pamoja na homoni za ukuaji, homoni za jinsi nazo huanza kutolewa wakati wa balehe. Kwa<br />
wasichana homoni za jinsia zinatengenezwa ndani ya ovari na kwa wavulana zainatengenezwa<br />
ndani ya korodani. Homoni za jinsi ndizo zinazosababisha tofauti katika maumbile ya mwanaume<br />
na mwanamke. Wasichana wanapoingia kipindi cha balehe nyonga zao huongezeka. Kawaida<br />
nyonga hukua haraka kuliko kifua . Nyonga ya msichana hupanuka na kujiviringa, na kiuno<br />
huonekana kidogo na chembamba. Matiti vilevile huanza kukua.<br />
Kwa wavulana, homoni za jinsia husababisha kifua kupanuka, mikono na miguu inakuwa minene<br />
yenye misuli. Matiti ya wavulana hayabadiliki sana kama ya wasichana yanavyobadilika wakati<br />
wa balehe, lakini hubadilika kidogo. Kwa wavulana wengine, matiti yao hukua kipindi cha balehe<br />
lakini kawaida hupotea kadri muda unavyokwenda.<br />
Homoni huathiri pia hisia zako. Vijana wengi hujisikia kuwa na hisia kali. Dakika moja tu anaweza<br />
kuwa na furaha na msisimko, lakini dakika inayofuata akawa na huzuni karibia kulia. Anaweza<br />
kujisikia vizuri siku moja na vibaya siku inayofuata. Mabadiliko haya katika hisia yanaitwa “hisia<br />
za kuyumba”.<br />
Kipindi cha balehe huwa kina ambatana na hisia kali<br />
SURA YA 2 | MABADILIKO YA MWILI<br />
Jambo hili huwatokea vijana wengi mara kwa mara. Wakati wa ujana balehe, utengenezaji wa<br />
homoni huongezeka ghafla, kitendo ambacho huwafanya vijana wengi wawe na hisia kali za aina<br />
mbalimbali.<br />
Baadaye katika maisha utengenezaji wa homoni utapungua na utajisikia unao uwezo wa kudhibiti<br />
hisia.<br />
Weka akilini kwamba mabadiliko yote ya kimwili, kihisia na kiakili yanayotokea wakati wa balehe<br />
yanasababishwa na homoni zinazotengenezwa na mwili wako. Hakuna unaloweza kufanya<br />
kuharakisha au kuchelewesha utengenezaji wa homoni. Jaribu kukumbuka tu kwamba wewe ni wa<br />
pekee na huna kasoro yoyote.<br />
Via VYa uZaZi “SeheMu Za SiRi”<br />
Pamoja na kuleta mabadiliko katika umbo la mvulana na msichana, homoni hufanya via vya<br />
uzazi kukua. Via vya uzazi maana yake ni zile sehemu za siri za mwili wako ambazo mara nyingi<br />
zinafunikwa na chupi/nguo za ndani.<br />
Kabla hujawa kijana balehe, sehemu za siri zilikuwa kwa ajili ya kujisaidia tu (kukojoa). Wakati wa<br />
ujana balehe hata hivyo, sehemu za siri zinakuwa kubwa. Kwa wasichana ngozi na tishu huwa laini<br />
na yenye mafuta mafuta, kwa wavulana uume huanza kurefuka na kunenepa. Korodani vilevile<br />
hukua na kuanza kutengeneza mbegu za kiume.<br />
Kipindi cha balehe via vya uzazi huanza kutengeneza majimaji pia.<br />
Wavulana huanza kutengeneza shahawa, majimaji yaliyo kama kamasi ambayo mbegu za kiume<br />
huogelea. Shahawa hutoka nje ya uume wakati mvulana anapofikia mshindo. Wasichana vilevile<br />
hutoa majimaji ya ukeni na damu ya hedhi. (soma sura ya 3 na ya 4 kwa maelezo zaidi kuhusu<br />
wavulana na wasichana)<br />
nYWele Za MWilini na MabaDiliKO Ya nGOZi<br />
Ngozi yako na nywele za mwilini hubadilika vilevile katika kipindi cha balehe. Kwa vijana wengi<br />
ngozi inakuwa na mafuta. Ngozi ya utotoni hupotea. Hii hupelekea chunusi kutoka, jambo ambalo<br />
ni tatizo la kawaida kwa vijana wengi (soma sura ya 5 kwa maelezo zaidi kuhusu utunzaji mzuri<br />
wa ngozi).<br />
Dalili nyingine ya balehe ni nywele kuota sehemu mpya za mwili. Wavulana na wasichana wote<br />
wanaweza kuota nywele kidogo miguuni na mikononi. Kwa kuongezea wavulana huota nywele<br />
sehemu za siri, usoni kifuani na kwapani. Wasichana vilevile huota nywele sehemu za siri na<br />
kwapani.<br />
Nywele zinazoota sehemu za siri zinaitwa mavuzi, watu wengine wana mavuzi mengi na wengine<br />
wanayo kidogo. Mavuzi husaidia kufanya eneo la via vya uzazi liwe safi, jambo ambalo ni zuri<br />
sana kwani ngozi inayozunguka via vya uzazi ni laini/nyororo sana na ni rahisi kuumia.Mavuzi<br />
husaidia kuzuia jasho na vitu vingine kutoka kwenye ngozi laini ya via vya uzazi.<br />
13