08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

184<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Kitu kibaya kuliko vingine vyote na ambacho kitakachokurudisha nyuma ni mtazamo wako<br />

mwenyewe. Siku nyingine unahisi kama hutaki kujaribu zaidi. Umechoka au unajisikia hufai ama<br />

ghafla unafikiri njia uliyochagua ni ngumu mno na kwamba matunda na mafanikio viko mbali<br />

sana.<br />

Mtazamo wako mwenyewe unaweza kuwa kikwazo. Vikwazo vyenyewe ni:<br />

• MaWaZO MabaYa. Unajiambia mwenyewe kwamba una bahati mbaya na kwamba u mjinga.<br />

Hapohapo unatumia mawazo haya kuwa sababu ya kushindwa kufanya jambo lolote.<br />

• KuOGOPa KuFanYa MaKOSa. Unahofu sana kufanya makosa kiasi cha kutojaribu kufanya<br />

kitu chochote.<br />

• KuOGOPa MaFaniKiO. Hujaribu kwa sababu unahofu kuwa mafanikio yatakufanya kivutio.<br />

• laKini SiWeZi. Unajiambia mwenye kwamba huwezi kabla hata ya kujaribu.<br />

• KuOGOPa KutORiDhiSha MateGeMeO Ya Watu WenGine. Unahofu sana kuhusu<br />

kuwasikitisha watu wengine kiasi cha kuchelea kujaribu.<br />

Jihadhari na vikwazo hivi: Usiruhusu vikunase.<br />

Kamwe hutajua una uwezo wa kufanya jambo mpaka ufanye bidii ya kufanya jambo hilo.<br />

Usilizungumzie tu au kutarajia kwamba litatokea. Anza kuyafanyia kazi malengo yako.<br />

Mara nyingi tunafikiri kwamba watu tunaowasikia wamefanikiwa wamezaliwa na vipaji vyao<br />

pamoja na stadi kiasi kwamba ilikuwa rahisi kwao kufikia pale walipo. Hata hivyo, ukiangalia<br />

walichofanya watu hawa utashangaa kiasi cha juhudi zao binafsi walizoweka katika kufanikisha<br />

ndoto zao.<br />

Wakati mwingine, tunadhani kwamba watu waliofanikiwa wana bahati. Upo msemo usemao:<br />

“Bahati ipo pale maandalizi yanapokutana na nafasi”.<br />

Hakikisha kwamba unajiweka tayari kwa lolote wakati wote. Ipo siku bahati itakuangukia<br />

Kumbuka kuwa mafanikio si kuwa nyota wa uigizaji ama kuwa na gari la kifahari au kuwa na pesa<br />

nyingi. Mafanikio ni jambo la nafsi. “Mafanikio yana maana tofauti kwa watu tofauti. Hata hivyo,<br />

watu wengi wanatafsiri mafanikio kuwa ni kujihisi vizuri na kile unachokifanya.<br />

Mwenye kuamua kiwango cha mafanikio yako ni wewe mwenyewe. Usisubiri watu wengine<br />

wakutafutie mafanikio. Mafanikio yako yataamuliwa na furaha yako, utajiri wa kiroho, busara<br />

zako, uwezo wako wa kubadilika kutegemeana na hali, ubunifu wako, nia na mtazamo wako<br />

kwa watu wengine. Umeshika funguo za maisha yako ya baadaye na ndoto zako. Fanya<br />

linalowezekana leo, usingoje kesho.<br />

SURA YA 14 | KUTIMIZA NDOTO ZAKO<br />

Sura ya 14<br />

Kutimiza ndoto zako<br />

Kutimiza ndoto zako kunategemea kufanya kazi kwa bidii sana na kwa nia. Usisubiri<br />

mambo yakutokee. Haya ni maisha yako ya sasa na ya baadaye. Unahitaji kuyajenga kwa<br />

dhati.<br />

Watu wengine wanajua wanataka kuwa nani na wanataka kufanya nini. Wanajua ndoto zao.<br />

Wengine hawajui wanataka kuwa nani. Hii haina maana kuwa hawana ndoto. Ina maana<br />

bado hawajajijua ni akina nani. Unaweza kuanza kutambua ndoto zako leo.<br />

• angalia watu wanaokuzunguka katika jumuia yako. Nani unamhusudu na<br />

kumheshimu? Watu hawa wanaweza kuwa mfano mzuri kwako.<br />

• angalia nje ya jumuia yako. Wapo watu wanaofanya mambo yanayovutia na yenye<br />

thamani kwa maisha yao. Hawa wanaweza kuwa mifano mizuri kwako.<br />

• Ziache fikra zako za ubunifu zipae angani. Usijiwekee mipaka kuhusu nini unaweza<br />

kufanya na kipi huwezi. Kama ni mvulana au ni msichana unaweza kufanya karibu kila<br />

kitu unachotaka kufanya kama jambo ukiliweka akilini na kuongeza juhudi.<br />

Zungumza na watu wanaofanya mambo yanayokuvutia. Waulize walifikaje pale walipo?<br />

Walihitaji elimu gani? Mafunzo gani walipata. Wanapenda nini zaidi kuhusu kazi zao? Na ni<br />

kitu gani hawakipendi sana kuhusu kazi zao?<br />

<strong>Ndoto</strong> zako ni malengo yako ya muda mrefu – mambo ambayo unafikiria kuyakamilisha<br />

baada ya muda mrefu. Lakini unahitaji vilevile malengo mahususi— mambo ambayo<br />

unaweza kuyakamilisha katika muda mfupi. Fikiria unachotaka kufanikisha wiki hii,<br />

mwezi huu na mwaka huu. Ukifanikisha malengo haya utajisikia vizuri. Utaona kuwa<br />

unapokiweka akilini kitu unaweza kufanikisha.<br />

Kuzifikia ndoto zako si jambo rahisi na siyo jambo la moja kwa moja lililonyooka.<br />

Hatua sahihi za kuchukua hazitakuwa wazi na unaweza kujikuta unakutana na vipingamizi<br />

ambavyo hukuvitegemea. Utahitaji kuwa na uwezo wa:<br />

• Kufanya uamuzi mzuri kwa kuangalia matokeo ya uchaguzi uliopo mbele yako.<br />

• Kulenga ndoto zako na kutoruhusu kujikatisha tamaa au kupotezwa na watu wengine.<br />

• Kufanya kazi kwa bidii kama upo shuleni au haupo shuleni. Tumia nafasi uliyonayo<br />

vizuri.<br />

• Kumudu vikwazo (mambo yatakayokurudisha nyuma), na kutokata tamaa. Palipo na<br />

nia pana njia.<br />

Mafanikio yako yanaamuliwa na wewe mwenyewe. Nia yako, ubunifu, busara, uwezo<br />

wa kukubali mabadiliko, mtazamo kuhusu watu wengine ni ufunguo wa maisha yako ya<br />

baadaye na ndoto zako.<br />

185

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!