Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
184<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Kitu kibaya kuliko vingine vyote na ambacho kitakachokurudisha nyuma ni mtazamo wako<br />
mwenyewe. Siku nyingine unahisi kama hutaki kujaribu zaidi. Umechoka au unajisikia hufai ama<br />
ghafla unafikiri njia uliyochagua ni ngumu mno na kwamba matunda na mafanikio viko mbali<br />
sana.<br />
Mtazamo wako mwenyewe unaweza kuwa kikwazo. Vikwazo vyenyewe ni:<br />
• MaWaZO MabaYa. Unajiambia mwenyewe kwamba una bahati mbaya na kwamba u mjinga.<br />
Hapohapo unatumia mawazo haya kuwa sababu ya kushindwa kufanya jambo lolote.<br />
• KuOGOPa KuFanYa MaKOSa. Unahofu sana kufanya makosa kiasi cha kutojaribu kufanya<br />
kitu chochote.<br />
• KuOGOPa MaFaniKiO. Hujaribu kwa sababu unahofu kuwa mafanikio yatakufanya kivutio.<br />
• laKini SiWeZi. Unajiambia mwenye kwamba huwezi kabla hata ya kujaribu.<br />
• KuOGOPa KutORiDhiSha MateGeMeO Ya Watu WenGine. Unahofu sana kuhusu<br />
kuwasikitisha watu wengine kiasi cha kuchelea kujaribu.<br />
Jihadhari na vikwazo hivi: Usiruhusu vikunase.<br />
Kamwe hutajua una uwezo wa kufanya jambo mpaka ufanye bidii ya kufanya jambo hilo.<br />
Usilizungumzie tu au kutarajia kwamba litatokea. Anza kuyafanyia kazi malengo yako.<br />
Mara nyingi tunafikiri kwamba watu tunaowasikia wamefanikiwa wamezaliwa na vipaji vyao<br />
pamoja na stadi kiasi kwamba ilikuwa rahisi kwao kufikia pale walipo. Hata hivyo, ukiangalia<br />
walichofanya watu hawa utashangaa kiasi cha juhudi zao binafsi walizoweka katika kufanikisha<br />
ndoto zao.<br />
Wakati mwingine, tunadhani kwamba watu waliofanikiwa wana bahati. Upo msemo usemao:<br />
“Bahati ipo pale maandalizi yanapokutana na nafasi”.<br />
Hakikisha kwamba unajiweka tayari kwa lolote wakati wote. Ipo siku bahati itakuangukia<br />
Kumbuka kuwa mafanikio si kuwa nyota wa uigizaji ama kuwa na gari la kifahari au kuwa na pesa<br />
nyingi. Mafanikio ni jambo la nafsi. “Mafanikio yana maana tofauti kwa watu tofauti. Hata hivyo,<br />
watu wengi wanatafsiri mafanikio kuwa ni kujihisi vizuri na kile unachokifanya.<br />
Mwenye kuamua kiwango cha mafanikio yako ni wewe mwenyewe. Usisubiri watu wengine<br />
wakutafutie mafanikio. Mafanikio yako yataamuliwa na furaha yako, utajiri wa kiroho, busara<br />
zako, uwezo wako wa kubadilika kutegemeana na hali, ubunifu wako, nia na mtazamo wako<br />
kwa watu wengine. Umeshika funguo za maisha yako ya baadaye na ndoto zako. Fanya<br />
linalowezekana leo, usingoje kesho.<br />
SURA YA 14 | KUTIMIZA NDOTO ZAKO<br />
Sura ya 14<br />
Kutimiza ndoto zako<br />
Kutimiza ndoto zako kunategemea kufanya kazi kwa bidii sana na kwa nia. Usisubiri<br />
mambo yakutokee. Haya ni maisha yako ya sasa na ya baadaye. Unahitaji kuyajenga kwa<br />
dhati.<br />
Watu wengine wanajua wanataka kuwa nani na wanataka kufanya nini. Wanajua ndoto zao.<br />
Wengine hawajui wanataka kuwa nani. Hii haina maana kuwa hawana ndoto. Ina maana<br />
bado hawajajijua ni akina nani. Unaweza kuanza kutambua ndoto zako leo.<br />
• angalia watu wanaokuzunguka katika jumuia yako. Nani unamhusudu na<br />
kumheshimu? Watu hawa wanaweza kuwa mfano mzuri kwako.<br />
• angalia nje ya jumuia yako. Wapo watu wanaofanya mambo yanayovutia na yenye<br />
thamani kwa maisha yao. Hawa wanaweza kuwa mifano mizuri kwako.<br />
• Ziache fikra zako za ubunifu zipae angani. Usijiwekee mipaka kuhusu nini unaweza<br />
kufanya na kipi huwezi. Kama ni mvulana au ni msichana unaweza kufanya karibu kila<br />
kitu unachotaka kufanya kama jambo ukiliweka akilini na kuongeza juhudi.<br />
Zungumza na watu wanaofanya mambo yanayokuvutia. Waulize walifikaje pale walipo?<br />
Walihitaji elimu gani? Mafunzo gani walipata. Wanapenda nini zaidi kuhusu kazi zao? Na ni<br />
kitu gani hawakipendi sana kuhusu kazi zao?<br />
<strong>Ndoto</strong> zako ni malengo yako ya muda mrefu – mambo ambayo unafikiria kuyakamilisha<br />
baada ya muda mrefu. Lakini unahitaji vilevile malengo mahususi— mambo ambayo<br />
unaweza kuyakamilisha katika muda mfupi. Fikiria unachotaka kufanikisha wiki hii,<br />
mwezi huu na mwaka huu. Ukifanikisha malengo haya utajisikia vizuri. Utaona kuwa<br />
unapokiweka akilini kitu unaweza kufanikisha.<br />
Kuzifikia ndoto zako si jambo rahisi na siyo jambo la moja kwa moja lililonyooka.<br />
Hatua sahihi za kuchukua hazitakuwa wazi na unaweza kujikuta unakutana na vipingamizi<br />
ambavyo hukuvitegemea. Utahitaji kuwa na uwezo wa:<br />
• Kufanya uamuzi mzuri kwa kuangalia matokeo ya uchaguzi uliopo mbele yako.<br />
• Kulenga ndoto zako na kutoruhusu kujikatisha tamaa au kupotezwa na watu wengine.<br />
• Kufanya kazi kwa bidii kama upo shuleni au haupo shuleni. Tumia nafasi uliyonayo<br />
vizuri.<br />
• Kumudu vikwazo (mambo yatakayokurudisha nyuma), na kutokata tamaa. Palipo na<br />
nia pana njia.<br />
Mafanikio yako yanaamuliwa na wewe mwenyewe. Nia yako, ubunifu, busara, uwezo<br />
wa kukubali mabadiliko, mtazamo kuhusu watu wengine ni ufunguo wa maisha yako ya<br />
baadaye na ndoto zako.<br />
185