08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

48<br />

utaFanYa nini na chunuSi<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Chunusi ni jambo la kawaida kwa vijana balehe. Kwa bahati mbaya , hakuna jinsi tunavyoweza<br />

kuzikwepa kabisa; wala hakuna matibabu ya ajabu ya kutibu chunusi. Hata hivyo, yapo mambo<br />

kadhaa ambayo unaweza kuyafanya ili kushughulikia chunusi.<br />

Ni jambo muhimu sana kutunza ngozi yako, hususani kama unaishi sehemu zenye joto, vumbi<br />

na unyevu unyevu. Unaweza kutumia sabuni ya kuogea na maji ya uvuguvugu kuosha taratibu<br />

sehemu za mwili wako zenye mafuta – usoni, shingoni, mabegani, mgongoni na juu ya kifua.<br />

Ukiosha sehemu hizi angalau mara moja kwa siku itasaidia kuondoa mafuta kwenye ngozi na<br />

kusababisha vinyweleo kuwa safi na wazi.<br />

Lakini usisugue sana ngozi yako au kutumia sabuni zenye nguvu na kali kwa sababu zinaweza<br />

kusumbua ngozi yako na kusababisha chunusi zaidi. Kamwe usitumie sabuni za kufulia, sabuni<br />

ya unga na dawa ya madoa, kwani zitaharibu ngozi yako. Jaribu kutoruhusu mafuta unayopaka<br />

kichwani yasifike usoni kwa sababu mafuta haya yanaweza kuzuia vinyweleo vya ngozi yako.<br />

Mwisho, kuwa mwangalifu na matumizi ya krimu za usoni na zile za kung’arisha ngozi. Ingawa<br />

zimeandikwa kwamba ukizitumia ngozi yako itakuwa nyororo na nzuri, krimu zingine zinaharibu<br />

ngozi kabisa. Kwa nyongeza, dawa nyingi za kulainisha ngozi zina vitu ambavyo si vizuri kwa afya<br />

yako.<br />

Ingawa wakati mwingine<br />

unashawishika kuminya<br />

chunusi,sio vizuri. Kama<br />

utafanya hivyo, usaha<br />

unaweza kutawanya<br />

maambukizi kwenye<br />

vinyweleo vingine, na<br />

vilevile unaweza kupata<br />

makovu ya kudumu.<br />

Chunusi zinasumbua,<br />

zinaweza kusababisha<br />

maumivu na uchungu, na<br />

zinaweza kuleta usumbufu<br />

wakati mwingine. Lakini ni<br />

sehemu ya ujana balehe.<br />

Vijana wengi wanajihisi<br />

Hata kama unafikiria kwamba chunusi zako ni mbaya, watu wengine<br />

hawajaziona bado.<br />

kuwa ni wao pekee wenye kusumbuliwa na matatizo ya ngozi, lakini hii ni kwa sababu hawajui<br />

kwamba hata wenzao wa rika moja wanazo chunusi. Za kwako zinaonekana zaidi kwako<br />

kuliko watu wengine wanavyoziona chunusi zako. Unaweza kudhani kilamtu anaziangalia, na<br />

anaangalia ngozi yako mbaya tu na wala hakuangalii wewe. Lakini hii sio kweli. Watu wengine<br />

wanayo mambo mengi ya kufikiria na kwa hakika wanachoangalia ni kujua wewe ni nani na wala<br />

sio ngozi yako inaonekanaje. Kwa hiyo, usivunjike moyo na usiache chunusi chache zikunyime<br />

raha! Hautakuwa nazo milele.<br />

utunZaji Wa nYWele<br />

Tunazo nywele mwili mzima, lakini zaidi kichwani, kwapani na maeneo yanayozunguka via vya<br />

uzazi. Kutunza nywele zako ni sehemu nyingine ya kutunza usafi na kutunza vizuri mwili wako.<br />

SURA YA 5 | MABADILIKO YA MSINGI KATIKA KUTUNZA MWILI<br />

Nywele zilizopo kichwani mwako ni rahisi kuzitunza hususani kama utakuwa unazipunguza kila<br />

mara. Hata kama unakata nywele kila mara na kuzisuka, unatakiwa kuziosha ili zisiwe na vumbi<br />

na ziwe safi. Kama uko shuleni, jaribu kutochangia chanio kwa sababu unaweza kupata chawa,<br />

maambukizi ya fangasi, na minyoo. Kama utachangia vitana, hakikisha unaviosha vizuri kwa maji<br />

ya moto yenye sabuni kabla na baada ya kutumia.<br />

Watu wengine wana matatizo ya mba, hali ambayo inasababishwa na ngozi ya nywele kuwa kavu<br />

mno.Mba unasababishwa na chembechembe ndogo za ngozi mfu, na watu wengine wenye mba<br />

nyingi wanatumia shampuu maalumu zenye dawa ili kuzuia mba.<br />

Ni vema kuoga mara kwa mara ili kuziweka safi nywele zilizopo kwenye mwili wako, nywele<br />

zilizopo kwenye kwapa, na nywele zilizopo kwenye maeneo ya via vya uzazi. Kama ulivyosoma<br />

sura ya 2 nywele hizi zinasaidia kuondoa jasho na uchafu kwenye mwili wako. Hata hivyo, sehemu<br />

nyingine za Afrika watu wananyoa nywele hizi kwa vile wanajisikia vizuri bila nywele hizo.<br />

Kama mila na tamaduni zako zinapinga kuwa na mavuzi yakate kwa kutumia mkasi. Usiziondoe<br />

zote kabisa kwa kutumia krimu ya kuondolea nywele au kwa kunyoa. Mafuta ya kunyolea nywele<br />

yanasumbua na kuumiza ngozi laini katika sehemu za siri. Pia kunyoa mavuzi kuna madhara<br />

yake. Kama unanyoa mavuzi, uwezekano wa kujikata ngozi ni mkubwa. Iwapo utajamiiana,<br />

mikato hii ni milango ya kupitishia VVU. Hii ni hatari. Tatizo lingine la kunyoa mavuzi ni wakati<br />

mavuzi yanaota tena. Nywele zinakuwa na incha kali kiasi cha kuweza kutoboa kondomu. Vilevile<br />

maeneo yanayozunguka via vya uzazi yaliyonyolewa yanaweza kupata maambukizi kidogo<br />

kwenye vinyweleo au sehemu ambazo mavuzi yanaota. Kunyoa mavuzi kiasi ni salama kidogo,<br />

lakini kuwa mwangalifu usiondoe nywele zote.<br />

liShe nZuRi<br />

Margareth, kutoka tanzania (umri; miaka 18,)<br />

“Nilipokuwa darasa la sita, nilianza kuota nywele sehemu za siri. Mama<br />

yangu aliniambia kuwa, zikikua na kuwa ndefu ninatakiwa nizipunguze na<br />

kuzisafisha vizuri, la sivyo nitanuka.”<br />

lois kutoka tanzania (umri; miaka 13)<br />

“Nimeona nywele kwenye kwapa, kwa vile sio muda mrefu nilipoziona<br />

sijazikata bado”<br />

Lishe nzuri ni muhimu kwa afya njema. Kula chakula chenye virutubisho ni muhimu katika maisha<br />

yote lakini ni muhimu zaidi wakati wa utoto na wakati wa balehe kipindi ambacho mwili wako<br />

unakua na unaongezeka kwa kasi sana.<br />

Mwili wako unahitaji chakula kizuri ili ukue na upate nguvu kwa ajili ya kufanya vizuri shuleni,<br />

kucheza michezo na kufanya kazi.<br />

Wakati mwingine vijana wadogo hawali mlo wenye lishe na wanasahau kula kwa wakati maalum<br />

uliopangwa. Wanaweza kuacha mlo kamili na badala yake wakakazania kula biskuti, chips,<br />

chokoleti, vitu vitamu na soda. Hivi vyakula havina lishe, na mwili wako unahitaji zaidi ya hivi ili<br />

uwe na afya.<br />

49

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!