Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
48<br />
utaFanYa nini na chunuSi<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Chunusi ni jambo la kawaida kwa vijana balehe. Kwa bahati mbaya , hakuna jinsi tunavyoweza<br />
kuzikwepa kabisa; wala hakuna matibabu ya ajabu ya kutibu chunusi. Hata hivyo, yapo mambo<br />
kadhaa ambayo unaweza kuyafanya ili kushughulikia chunusi.<br />
Ni jambo muhimu sana kutunza ngozi yako, hususani kama unaishi sehemu zenye joto, vumbi<br />
na unyevu unyevu. Unaweza kutumia sabuni ya kuogea na maji ya uvuguvugu kuosha taratibu<br />
sehemu za mwili wako zenye mafuta – usoni, shingoni, mabegani, mgongoni na juu ya kifua.<br />
Ukiosha sehemu hizi angalau mara moja kwa siku itasaidia kuondoa mafuta kwenye ngozi na<br />
kusababisha vinyweleo kuwa safi na wazi.<br />
Lakini usisugue sana ngozi yako au kutumia sabuni zenye nguvu na kali kwa sababu zinaweza<br />
kusumbua ngozi yako na kusababisha chunusi zaidi. Kamwe usitumie sabuni za kufulia, sabuni<br />
ya unga na dawa ya madoa, kwani zitaharibu ngozi yako. Jaribu kutoruhusu mafuta unayopaka<br />
kichwani yasifike usoni kwa sababu mafuta haya yanaweza kuzuia vinyweleo vya ngozi yako.<br />
Mwisho, kuwa mwangalifu na matumizi ya krimu za usoni na zile za kung’arisha ngozi. Ingawa<br />
zimeandikwa kwamba ukizitumia ngozi yako itakuwa nyororo na nzuri, krimu zingine zinaharibu<br />
ngozi kabisa. Kwa nyongeza, dawa nyingi za kulainisha ngozi zina vitu ambavyo si vizuri kwa afya<br />
yako.<br />
Ingawa wakati mwingine<br />
unashawishika kuminya<br />
chunusi,sio vizuri. Kama<br />
utafanya hivyo, usaha<br />
unaweza kutawanya<br />
maambukizi kwenye<br />
vinyweleo vingine, na<br />
vilevile unaweza kupata<br />
makovu ya kudumu.<br />
Chunusi zinasumbua,<br />
zinaweza kusababisha<br />
maumivu na uchungu, na<br />
zinaweza kuleta usumbufu<br />
wakati mwingine. Lakini ni<br />
sehemu ya ujana balehe.<br />
Vijana wengi wanajihisi<br />
Hata kama unafikiria kwamba chunusi zako ni mbaya, watu wengine<br />
hawajaziona bado.<br />
kuwa ni wao pekee wenye kusumbuliwa na matatizo ya ngozi, lakini hii ni kwa sababu hawajui<br />
kwamba hata wenzao wa rika moja wanazo chunusi. Za kwako zinaonekana zaidi kwako<br />
kuliko watu wengine wanavyoziona chunusi zako. Unaweza kudhani kilamtu anaziangalia, na<br />
anaangalia ngozi yako mbaya tu na wala hakuangalii wewe. Lakini hii sio kweli. Watu wengine<br />
wanayo mambo mengi ya kufikiria na kwa hakika wanachoangalia ni kujua wewe ni nani na wala<br />
sio ngozi yako inaonekanaje. Kwa hiyo, usivunjike moyo na usiache chunusi chache zikunyime<br />
raha! Hautakuwa nazo milele.<br />
utunZaji Wa nYWele<br />
Tunazo nywele mwili mzima, lakini zaidi kichwani, kwapani na maeneo yanayozunguka via vya<br />
uzazi. Kutunza nywele zako ni sehemu nyingine ya kutunza usafi na kutunza vizuri mwili wako.<br />
SURA YA 5 | MABADILIKO YA MSINGI KATIKA KUTUNZA MWILI<br />
Nywele zilizopo kichwani mwako ni rahisi kuzitunza hususani kama utakuwa unazipunguza kila<br />
mara. Hata kama unakata nywele kila mara na kuzisuka, unatakiwa kuziosha ili zisiwe na vumbi<br />
na ziwe safi. Kama uko shuleni, jaribu kutochangia chanio kwa sababu unaweza kupata chawa,<br />
maambukizi ya fangasi, na minyoo. Kama utachangia vitana, hakikisha unaviosha vizuri kwa maji<br />
ya moto yenye sabuni kabla na baada ya kutumia.<br />
Watu wengine wana matatizo ya mba, hali ambayo inasababishwa na ngozi ya nywele kuwa kavu<br />
mno.Mba unasababishwa na chembechembe ndogo za ngozi mfu, na watu wengine wenye mba<br />
nyingi wanatumia shampuu maalumu zenye dawa ili kuzuia mba.<br />
Ni vema kuoga mara kwa mara ili kuziweka safi nywele zilizopo kwenye mwili wako, nywele<br />
zilizopo kwenye kwapa, na nywele zilizopo kwenye maeneo ya via vya uzazi. Kama ulivyosoma<br />
sura ya 2 nywele hizi zinasaidia kuondoa jasho na uchafu kwenye mwili wako. Hata hivyo, sehemu<br />
nyingine za Afrika watu wananyoa nywele hizi kwa vile wanajisikia vizuri bila nywele hizo.<br />
Kama mila na tamaduni zako zinapinga kuwa na mavuzi yakate kwa kutumia mkasi. Usiziondoe<br />
zote kabisa kwa kutumia krimu ya kuondolea nywele au kwa kunyoa. Mafuta ya kunyolea nywele<br />
yanasumbua na kuumiza ngozi laini katika sehemu za siri. Pia kunyoa mavuzi kuna madhara<br />
yake. Kama unanyoa mavuzi, uwezekano wa kujikata ngozi ni mkubwa. Iwapo utajamiiana,<br />
mikato hii ni milango ya kupitishia VVU. Hii ni hatari. Tatizo lingine la kunyoa mavuzi ni wakati<br />
mavuzi yanaota tena. Nywele zinakuwa na incha kali kiasi cha kuweza kutoboa kondomu. Vilevile<br />
maeneo yanayozunguka via vya uzazi yaliyonyolewa yanaweza kupata maambukizi kidogo<br />
kwenye vinyweleo au sehemu ambazo mavuzi yanaota. Kunyoa mavuzi kiasi ni salama kidogo,<br />
lakini kuwa mwangalifu usiondoe nywele zote.<br />
liShe nZuRi<br />
Margareth, kutoka tanzania (umri; miaka 18,)<br />
“Nilipokuwa darasa la sita, nilianza kuota nywele sehemu za siri. Mama<br />
yangu aliniambia kuwa, zikikua na kuwa ndefu ninatakiwa nizipunguze na<br />
kuzisafisha vizuri, la sivyo nitanuka.”<br />
lois kutoka tanzania (umri; miaka 13)<br />
“Nimeona nywele kwenye kwapa, kwa vile sio muda mrefu nilipoziona<br />
sijazikata bado”<br />
Lishe nzuri ni muhimu kwa afya njema. Kula chakula chenye virutubisho ni muhimu katika maisha<br />
yote lakini ni muhimu zaidi wakati wa utoto na wakati wa balehe kipindi ambacho mwili wako<br />
unakua na unaongezeka kwa kasi sana.<br />
Mwili wako unahitaji chakula kizuri ili ukue na upate nguvu kwa ajili ya kufanya vizuri shuleni,<br />
kucheza michezo na kufanya kazi.<br />
Wakati mwingine vijana wadogo hawali mlo wenye lishe na wanasahau kula kwa wakati maalum<br />
uliopangwa. Wanaweza kuacha mlo kamili na badala yake wakakazania kula biskuti, chips,<br />
chokoleti, vitu vitamu na soda. Hivi vyakula havina lishe, na mwili wako unahitaji zaidi ya hivi ili<br />
uwe na afya.<br />
49