Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
26<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Sura ya 3<br />
WaVulana<br />
Katika kipindi cha balehe mvulana anategemea mabadiliko mengi kutokea. Mabadiliko<br />
haya ni ya taratibu na hutokea katika umri tofauti kwa wavulana tofauti. Yafuatayo ni<br />
mabadiliko ambayo unaweza kuyategemea:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Mwili wako utakua , hasa mifupa ya mabegani, mikono, miguu na nyayo. Vilevile misuli<br />
itajengeka na utakuwa na nguvu.<br />
Sauti itabadilika halafu itakuwa nzito kadri vinyuzi sauti vinavyokuwa vinene na<br />
kurefuka.<br />
Uume wako utaongezeka na mapumbu yataanza kuninginia chini.<br />
Uume wako utadinda mara kwa mara.<br />
Unaweza kupata ndoto nyevu (kukojoa manii usingizini) usiku.<br />
Unapopitia mabadiliko haya elewa kwamba:<br />
Kila ukubwa wa uume ni sahihi.<br />
Hakuna ubaya wowote kutahiriwa na wala hakuna ubaya wowote kutokutahiriwa kwa<br />
mwanaume.<br />
Oga na kusafisha uume wako kila siku. Kila mara rudisha nyuma govi na kusafisha chini<br />
yake iwapo hujatahiriwa.<br />
Sio lazima kujamiiana eti kwa vile uume umedinda.<br />
<strong>Ndoto</strong> nyevu ni tukio la kawaida, huwapata wengi, hakuna haja ya kuwa na wasiwasi, sio<br />
dalili ya kwamba unatakiwa kuanza kujamiiana.<br />
Wakati wowote mabadiliko haya yanapotokea mwilini mwako ndio wakati mwafaka. <strong>Wewe</strong><br />
ni wa kipekee na uko kawaida kabisa.<br />
Wasichana<br />
Sura ya pili ilielezea kidogo kuhusu mabadiliko ya msichana wakati wa balehe. Sura hii inatoa<br />
maelezo ya kina na naamini utayafurahia kuyasoma.<br />
MauMbile na uKubWa Wa MWili<br />
Wasichana wengi huanza kukua haraka haraka wanapokaribia umri wa miaka 10 hadi 11. Lakini<br />
wapo wasichana wanaoanza kukua wakiwa chini ya umri huu au umri mkubwa zaidi ya huu. Miguu<br />
mara nyingi huwa ndiyo sehemu ya mwili inayokua haraka. Unaweza kuwa mfupi, lakini ukajikuta<br />
miguu yako ghafla imekuwa mikubwa sana! Usijali sehemu nyingine ya mwili itakua na kulingana<br />
na hiyo miguu mikubwa. Mwili wako unakua kwa wakati wake.<br />
Mifupa mingine itaanza kukua pia kila mmoja kwa wakati wake. Mikono na miguu yako inaweza<br />
kutangulia kukua haraka wakati sehemu ya uti wa mgongo ikiwa inakua taratibu zaidi.<br />
Mabadiliko mengine unayoweza kuyahisi ni kuanza kukua nyonga. Mifupa ya nyonga inakuwa<br />
mikubwa, na laini, tishu zenye mafuta hukua kwenye nyonga, mapaja na matako. Kadri nyonga<br />
inavyozidi kupanuka, kiuno kitaonekana chembamba ukilinganisha na sehemu zingine. Mwili<br />
utakuwa wa mviringo, ukionyesha umbo la kike.<br />
Matiti YaKO<br />
catheryn, kutoka Ghana (umri, miaka 15)<br />
“Nilikuwa na miaka 10 nilipoanza kuhisi mabadiliko ya mwili wangu.<br />
Watu waliniambia bila mabadiliko hayo nisingeliweza kuwa<br />
mwanamke kwa hiyo nilifurahi. Nilikuwa naingia katika kundi la<br />
wanawake hivyo sikuwa na budi kujihadhari.”<br />
Wasichana wengine wanaanza kuota matiti wakiwa na umri kati ya miaka 8 au 9, lakini wengine<br />
yanachelewa kuota. Kuota kwa matiti kunasababishwa na homoni inayoitwa estrojeni.<br />
Estrojeni inasababisha tishu ndani ya matiti kukua ili siku moja utakapokuwa na mtoto, uweze<br />
kutengeneza na kuhifadhi maziwa.<br />
Kabla matiti yako hayajaanza kukua, pengine chuchu zako zitakuwa kubwa na kusimama kuliko<br />
zilivyokuwa awali. Mabadiliko mengine unayoweza kuyaona ni duara jeusi na kubwa la ngozi<br />
litakalozunguka chuchu zao.<br />
27<br />
SURA YA 4