08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

26<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Sura ya 3<br />

WaVulana<br />

Katika kipindi cha balehe mvulana anategemea mabadiliko mengi kutokea. Mabadiliko<br />

haya ni ya taratibu na hutokea katika umri tofauti kwa wavulana tofauti. Yafuatayo ni<br />

mabadiliko ambayo unaweza kuyategemea:<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

Mwili wako utakua , hasa mifupa ya mabegani, mikono, miguu na nyayo. Vilevile misuli<br />

itajengeka na utakuwa na nguvu.<br />

Sauti itabadilika halafu itakuwa nzito kadri vinyuzi sauti vinavyokuwa vinene na<br />

kurefuka.<br />

Uume wako utaongezeka na mapumbu yataanza kuninginia chini.<br />

Uume wako utadinda mara kwa mara.<br />

Unaweza kupata ndoto nyevu (kukojoa manii usingizini) usiku.<br />

Unapopitia mabadiliko haya elewa kwamba:<br />

Kila ukubwa wa uume ni sahihi.<br />

Hakuna ubaya wowote kutahiriwa na wala hakuna ubaya wowote kutokutahiriwa kwa<br />

mwanaume.<br />

Oga na kusafisha uume wako kila siku. Kila mara rudisha nyuma govi na kusafisha chini<br />

yake iwapo hujatahiriwa.<br />

Sio lazima kujamiiana eti kwa vile uume umedinda.<br />

<strong>Ndoto</strong> nyevu ni tukio la kawaida, huwapata wengi, hakuna haja ya kuwa na wasiwasi, sio<br />

dalili ya kwamba unatakiwa kuanza kujamiiana.<br />

Wakati wowote mabadiliko haya yanapotokea mwilini mwako ndio wakati mwafaka. <strong>Wewe</strong><br />

ni wa kipekee na uko kawaida kabisa.<br />

Wasichana<br />

Sura ya pili ilielezea kidogo kuhusu mabadiliko ya msichana wakati wa balehe. Sura hii inatoa<br />

maelezo ya kina na naamini utayafurahia kuyasoma.<br />

MauMbile na uKubWa Wa MWili<br />

Wasichana wengi huanza kukua haraka haraka wanapokaribia umri wa miaka 10 hadi 11. Lakini<br />

wapo wasichana wanaoanza kukua wakiwa chini ya umri huu au umri mkubwa zaidi ya huu. Miguu<br />

mara nyingi huwa ndiyo sehemu ya mwili inayokua haraka. Unaweza kuwa mfupi, lakini ukajikuta<br />

miguu yako ghafla imekuwa mikubwa sana! Usijali sehemu nyingine ya mwili itakua na kulingana<br />

na hiyo miguu mikubwa. Mwili wako unakua kwa wakati wake.<br />

Mifupa mingine itaanza kukua pia kila mmoja kwa wakati wake. Mikono na miguu yako inaweza<br />

kutangulia kukua haraka wakati sehemu ya uti wa mgongo ikiwa inakua taratibu zaidi.<br />

Mabadiliko mengine unayoweza kuyahisi ni kuanza kukua nyonga. Mifupa ya nyonga inakuwa<br />

mikubwa, na laini, tishu zenye mafuta hukua kwenye nyonga, mapaja na matako. Kadri nyonga<br />

inavyozidi kupanuka, kiuno kitaonekana chembamba ukilinganisha na sehemu zingine. Mwili<br />

utakuwa wa mviringo, ukionyesha umbo la kike.<br />

Matiti YaKO<br />

catheryn, kutoka Ghana (umri, miaka 15)<br />

“Nilikuwa na miaka 10 nilipoanza kuhisi mabadiliko ya mwili wangu.<br />

Watu waliniambia bila mabadiliko hayo nisingeliweza kuwa<br />

mwanamke kwa hiyo nilifurahi. Nilikuwa naingia katika kundi la<br />

wanawake hivyo sikuwa na budi kujihadhari.”<br />

Wasichana wengine wanaanza kuota matiti wakiwa na umri kati ya miaka 8 au 9, lakini wengine<br />

yanachelewa kuota. Kuota kwa matiti kunasababishwa na homoni inayoitwa estrojeni.<br />

Estrojeni inasababisha tishu ndani ya matiti kukua ili siku moja utakapokuwa na mtoto, uweze<br />

kutengeneza na kuhifadhi maziwa.<br />

Kabla matiti yako hayajaanza kukua, pengine chuchu zako zitakuwa kubwa na kusimama kuliko<br />

zilivyokuwa awali. Mabadiliko mengine unayoweza kuyaona ni duara jeusi na kubwa la ngozi<br />

litakalozunguka chuchu zao.<br />

27<br />

SURA YA 4

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!