08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

2<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Mwonekano wako mpya na kujitambua kwako kunawafanya wazazi, shangazi zako na wajomba<br />

kuwa na wasiwasi kwa sababu wasingependa upate matatizo na wala wasingependa ufanye<br />

makosa makubwa kama vile kupata mimba (au kwa kumpa mimba rafiki wa kike) wakati ungali<br />

unasoma. Zaidi ya yote wanakuwa na wasiwasi kwa sababu wanafahamu kwamba umri kati ya 10-<br />

19 unaweza kuwa na athari kubwa katika ukuaji wako na aina ya maisha utakayokuwa nayo.<br />

nini Maana Ya ujana balehe?<br />

• Ujana balehe ni kipindi ambacho unabadilika na kukua kimwili na kiakili kutoka utoto na<br />

kuingia utu uzima. Wakati wa ujana balehe mambo yafuatayo hutokea:<br />

• Mwili wako utabadilika kwa jinsi unavyopenda uwe au wakati mwingine hata usivyopenda<br />

uwe.<br />

• Utaanza kupata hisia za kutaka kujamiiana, na unaweza usijue ufanye nini baada ya kupata<br />

hisia hizo.<br />

• Utaanza kufikiri bila ya kumtegemea mtu mwingine na kutaka kufanya maamuzi peke yako.<br />

• Hisia zako kuhusu familia na mahusiano yako na wazazi, yanaweza kubadilika kwa uzuri<br />

au kwa ubaya. Wazazi wanaweza kukupa majukumu zaidi ambayo ni dalili nzuri kwamba<br />

wanakuamini na kukutegemea. Lakini wanaweza vilevile wakaanza kuwa wakali hata<br />

kutokuruhusu ukutane na marafiki zako. Wakati mwingine watajaribu kufanya maamuzi<br />

kuhusu masomo na mustakabali wa maisha yako ya baadaye. Wanaweza wakaonyesha<br />

kuwa na upendo mdogo kwako kuliko walivyokuwa huko nyuma na unaweza vilevile usipate<br />

mahusiano yenye upendo kama ulivyokuwa ukiwa mtoto.<br />

• Marafiki zako, na hata yale wanayofikiria, vinaweza kuwa vya muhimu zaidi kuliko ilivyokuwa<br />

awali.<br />

• Hisia zako zinaweza kuwa na utata zaidi kuliko ulivyozoea na wakati mwingine wewe<br />

mwenyewe unaweza usifahamu hasa kile unachohisi au ni kwa nini unahisi hivyo.<br />

• Kwa hakika unaweza kuhisi kutaka kupendwa au kuwa karibu na mtu mwingine.<br />

• Unaweza kukumbana na maamuzi mazito na zinaweza kuwepo nyakati ambapo hujui umtake<br />

nani ushauri.<br />

Ujana balehe ni kipindi maalum kwa kila mtu, kote duniani – mashariki au magharibi,kaskazini<br />

au kusini.Lakini pia ni kipindi chenye changamoto. Hiki ni kipindi cha mabadiliko makubwa, na<br />

mabadiliko makubwa huchukua muda. Utakutana na mambo mengi ya kuyafanyia maamuzi<br />

unapopitia ujana balehe na maamuzi mengine utakayofanya yatadumu nawe katika maisha yako<br />

yote.<br />

Yapo mambo mengi sana ambayo unaweza kuyafanya ili kupitia salama ujana balehe. Hivyo<br />

ni vema uelewe mwili wako na mabadiliko yanayotokea .Ni vema ujielewe na pia uelewe kile<br />

unachokitaka katika maisha. Tumia muda kufikiria maisha yako ya baadaye na kupanga<br />

yatakuwaje. Utu uzima una majukumu makubwa hivyo basi ni lazima kujiandaa vema wakati wa<br />

ujana balehe.<br />

Wakati wa ujana usiwe mpweke na kufanya mambo peke yako. Umezungukwa na watu<br />

wanaoshughulikia matatizo muhimu kila siku. Unao ndugu wengi, kama akina shangazi, wajomba,<br />

binamu na wengi wengineo, amabao unaweza kuwaomba ushauri. Pia kwa vile wewe ni sehemu ya<br />

jamii, zipo mila na desturi nyingi ambazo mafunzo yake yanaweza kukusaidia.<br />

SURA YA 1 | UJANA BALEHE: BADILIKO KUBWA CHANGAMOTO KUBWA<br />

Mahali pengi ujana umekuwa mgumu kueleweka, na hasa siku hizi vijana wanapata matatizo<br />

ambayo wazazi wao, mabibi hata babu zao hawakuwahi kuyapitia; matatizo hayo ni:<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

Msukumo wa kutaka kujamiiana.<br />

Madawa ya kulevya shuleni na kwenye jamii.<br />

Wazazi ambao kwa sababu ya shughuli nyingi hawana muda au wanaona aibu kuzungumza<br />

kuhusu mabadiliko yanayowatokea watoto wao.<br />

Magonjwa yaambukizwayo kwa kujamiiana ikiwa ni pamoja na VVU/UKIMWI.<br />

Kuwa yatima kwa sababu ya UKIMWI au ajali.<br />

Vita au kuyumba kisiasa kwa nchi.<br />

Ili kuyamudu yote haya na kupitia kipindi cha ujana balehe salama unahitaji kuwa jasiri , mbunifu,<br />

mtafutaji na mwenye kujipa matumaini. Jaribu kujifunza kutoka kwa watu wanaokuzunguka<br />

ambao ni jasiri na watulivu wakati unapokutana na matatizo. Kila wakati jione kuwa utashinda<br />

matatizo yako kama walivyoweza wengine.<br />

Vijana huFiKiRia KWaMba haKuna janGa linalOWeZa KuWaPata<br />

Ni tabia ya vijana duniani kote, katika nchi tajiri na maskini – kufikiria kwamba mambo mabaya<br />

hayawezi kuwatokea. Hujiambia,<br />

“ Haitatokea kwangu”. Wakati mwingine hujiamini sana<br />

na kuhisi wako salama mno.<br />

Je wewe uko hivi? Unadhani unaweza kujaribu kitu cha hatari<br />

na lisikupate jambo? Kwa mfano, wewe na rafiki yako wa kike<br />

(msichana) mnafahamu kuhusu dawa za kuzuia mimba. Lakini<br />

mnadhani kwamba ili mradi hamjamiiani mara kwa mara,<br />

msichana hawezi akapata mimba.<br />

Au unaweza ukawa na ufahamu mkubwa kuhusu<br />

VVU, virusi vinavyo sababisha UKIMWI. Unaweza<br />

ukafahamu kwamba maambukizi yanaweza<br />

kutokea kwa njia ya kujamiiana bila kinga,<br />

lakini unafikiri kwamba rafiki yako wa kiume<br />

hawezi kuwa na maambukizo. Unakataa kufikiri<br />

kuwa unaweza kupata maambukizo ya VVU na<br />

haiwezekani pia kwa wale watu unaowafahamu<br />

kupata ugonjwa huo.<br />

je haya yanakuhusu? Kama ndivyo, hapa kuna<br />

mambo ambayo unahitaji kuyazingatia:<br />

Vijana wengi hujiingiza kwenye vitendo vya<br />

hatari wakidhani kuwa hawatadhurika....<br />

3

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!