Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
2<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Mwonekano wako mpya na kujitambua kwako kunawafanya wazazi, shangazi zako na wajomba<br />
kuwa na wasiwasi kwa sababu wasingependa upate matatizo na wala wasingependa ufanye<br />
makosa makubwa kama vile kupata mimba (au kwa kumpa mimba rafiki wa kike) wakati ungali<br />
unasoma. Zaidi ya yote wanakuwa na wasiwasi kwa sababu wanafahamu kwamba umri kati ya 10-<br />
19 unaweza kuwa na athari kubwa katika ukuaji wako na aina ya maisha utakayokuwa nayo.<br />
nini Maana Ya ujana balehe?<br />
• Ujana balehe ni kipindi ambacho unabadilika na kukua kimwili na kiakili kutoka utoto na<br />
kuingia utu uzima. Wakati wa ujana balehe mambo yafuatayo hutokea:<br />
• Mwili wako utabadilika kwa jinsi unavyopenda uwe au wakati mwingine hata usivyopenda<br />
uwe.<br />
• Utaanza kupata hisia za kutaka kujamiiana, na unaweza usijue ufanye nini baada ya kupata<br />
hisia hizo.<br />
• Utaanza kufikiri bila ya kumtegemea mtu mwingine na kutaka kufanya maamuzi peke yako.<br />
• Hisia zako kuhusu familia na mahusiano yako na wazazi, yanaweza kubadilika kwa uzuri<br />
au kwa ubaya. Wazazi wanaweza kukupa majukumu zaidi ambayo ni dalili nzuri kwamba<br />
wanakuamini na kukutegemea. Lakini wanaweza vilevile wakaanza kuwa wakali hata<br />
kutokuruhusu ukutane na marafiki zako. Wakati mwingine watajaribu kufanya maamuzi<br />
kuhusu masomo na mustakabali wa maisha yako ya baadaye. Wanaweza wakaonyesha<br />
kuwa na upendo mdogo kwako kuliko walivyokuwa huko nyuma na unaweza vilevile usipate<br />
mahusiano yenye upendo kama ulivyokuwa ukiwa mtoto.<br />
• Marafiki zako, na hata yale wanayofikiria, vinaweza kuwa vya muhimu zaidi kuliko ilivyokuwa<br />
awali.<br />
• Hisia zako zinaweza kuwa na utata zaidi kuliko ulivyozoea na wakati mwingine wewe<br />
mwenyewe unaweza usifahamu hasa kile unachohisi au ni kwa nini unahisi hivyo.<br />
• Kwa hakika unaweza kuhisi kutaka kupendwa au kuwa karibu na mtu mwingine.<br />
• Unaweza kukumbana na maamuzi mazito na zinaweza kuwepo nyakati ambapo hujui umtake<br />
nani ushauri.<br />
Ujana balehe ni kipindi maalum kwa kila mtu, kote duniani – mashariki au magharibi,kaskazini<br />
au kusini.Lakini pia ni kipindi chenye changamoto. Hiki ni kipindi cha mabadiliko makubwa, na<br />
mabadiliko makubwa huchukua muda. Utakutana na mambo mengi ya kuyafanyia maamuzi<br />
unapopitia ujana balehe na maamuzi mengine utakayofanya yatadumu nawe katika maisha yako<br />
yote.<br />
Yapo mambo mengi sana ambayo unaweza kuyafanya ili kupitia salama ujana balehe. Hivyo<br />
ni vema uelewe mwili wako na mabadiliko yanayotokea .Ni vema ujielewe na pia uelewe kile<br />
unachokitaka katika maisha. Tumia muda kufikiria maisha yako ya baadaye na kupanga<br />
yatakuwaje. Utu uzima una majukumu makubwa hivyo basi ni lazima kujiandaa vema wakati wa<br />
ujana balehe.<br />
Wakati wa ujana usiwe mpweke na kufanya mambo peke yako. Umezungukwa na watu<br />
wanaoshughulikia matatizo muhimu kila siku. Unao ndugu wengi, kama akina shangazi, wajomba,<br />
binamu na wengi wengineo, amabao unaweza kuwaomba ushauri. Pia kwa vile wewe ni sehemu ya<br />
jamii, zipo mila na desturi nyingi ambazo mafunzo yake yanaweza kukusaidia.<br />
SURA YA 1 | UJANA BALEHE: BADILIKO KUBWA CHANGAMOTO KUBWA<br />
Mahali pengi ujana umekuwa mgumu kueleweka, na hasa siku hizi vijana wanapata matatizo<br />
ambayo wazazi wao, mabibi hata babu zao hawakuwahi kuyapitia; matatizo hayo ni:<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Msukumo wa kutaka kujamiiana.<br />
Madawa ya kulevya shuleni na kwenye jamii.<br />
Wazazi ambao kwa sababu ya shughuli nyingi hawana muda au wanaona aibu kuzungumza<br />
kuhusu mabadiliko yanayowatokea watoto wao.<br />
Magonjwa yaambukizwayo kwa kujamiiana ikiwa ni pamoja na VVU/UKIMWI.<br />
Kuwa yatima kwa sababu ya UKIMWI au ajali.<br />
Vita au kuyumba kisiasa kwa nchi.<br />
Ili kuyamudu yote haya na kupitia kipindi cha ujana balehe salama unahitaji kuwa jasiri , mbunifu,<br />
mtafutaji na mwenye kujipa matumaini. Jaribu kujifunza kutoka kwa watu wanaokuzunguka<br />
ambao ni jasiri na watulivu wakati unapokutana na matatizo. Kila wakati jione kuwa utashinda<br />
matatizo yako kama walivyoweza wengine.<br />
Vijana huFiKiRia KWaMba haKuna janGa linalOWeZa KuWaPata<br />
Ni tabia ya vijana duniani kote, katika nchi tajiri na maskini – kufikiria kwamba mambo mabaya<br />
hayawezi kuwatokea. Hujiambia,<br />
“ Haitatokea kwangu”. Wakati mwingine hujiamini sana<br />
na kuhisi wako salama mno.<br />
Je wewe uko hivi? Unadhani unaweza kujaribu kitu cha hatari<br />
na lisikupate jambo? Kwa mfano, wewe na rafiki yako wa kike<br />
(msichana) mnafahamu kuhusu dawa za kuzuia mimba. Lakini<br />
mnadhani kwamba ili mradi hamjamiiani mara kwa mara,<br />
msichana hawezi akapata mimba.<br />
Au unaweza ukawa na ufahamu mkubwa kuhusu<br />
VVU, virusi vinavyo sababisha UKIMWI. Unaweza<br />
ukafahamu kwamba maambukizi yanaweza<br />
kutokea kwa njia ya kujamiiana bila kinga,<br />
lakini unafikiri kwamba rafiki yako wa kiume<br />
hawezi kuwa na maambukizo. Unakataa kufikiri<br />
kuwa unaweza kupata maambukizo ya VVU na<br />
haiwezekani pia kwa wale watu unaowafahamu<br />
kupata ugonjwa huo.<br />
je haya yanakuhusu? Kama ndivyo, hapa kuna<br />
mambo ambayo unahitaji kuyazingatia:<br />
Vijana wengi hujiingiza kwenye vitendo vya<br />
hatari wakidhani kuwa hawatadhurika....<br />
3