08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

40<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Susan, mwenye umri wa miaka 19, ana mzunguko wa kawaida wa siku 28. Mwezi Aprili, alianza<br />

kutoka damu tarehe 1, hivyo hedhi nyingine ilikuwa tarehe 29 ya Aprili. Mwezi Mei alipata hedhi<br />

tarehe 27. Mwezi wa sita alipata hedhi tarehe 23. Mwezi wa saba aliingia mwezini tarehe 20<br />

Mwezi wa nane aliingia mwezini tarehe 16 . Umegundua kuwa hedhi inaanza siku tofauti kila<br />

mwezi japo mzunguko wake una mpangilio uliotulia.<br />

Kumbuka, utaratibu wa kuwa na kalenda ni mzuri. Hukusaidia kufanya mandalizi ya kuingia<br />

mwezini lakini sio njia nzuri ya kujua siku salama zitakuwa lini. Kama unapenda sana kufanya<br />

ngono tafuta njia bora ya kujikinga dhidi ya mimba na magonjwa ya ngono, pamoja na VVU/<br />

UKIMWI.<br />

heDhi inaVYOKOSeSha Raha<br />

Wasichana wengi matiti huvimba na kuongezeka na yanakuwa laini sana kabla ya kuingia<br />

mwezini au wakati yai limerutubishwa.Hali hii haifurahishi, ila ni ya kawaida.Hali hii<br />

inasababishwa na homoni zinazosababisha tishu za matiti kuwa na majimaji zaidi kuliko ilivyo<br />

kawaida. Ukivaa sidiria inayokutosha vizuri itakufanya ujisikie vizuri, na vyakula vyenye chumvi<br />

kidogo vitakusaidia kupunguza kiasi cha maji kinachohifadhiwa na mwili.<br />

Hedhi inaweza kumwathiri mwanamke katika hali yake kitabia. Kabla ya hedhi kuanza kila mwezi,<br />

wasichana wengine hujisikia kulia au kuwa na huzuni. Mara nyingine wasichana wanakuwa na<br />

hasira kwa sababu ya kuvimba matiti yao au mwili kuvimba kidogo au kuvimba sana. Hali hii<br />

mara nyingine inajulikana kama “mahangaiko kabla ya hedhi” na ni matatizo ya kawaida. Jaribu<br />

kuyapuuza yasikusumbue sana.<br />

Wasichana wengine hujisikia maumivu kidogo ya tumbo au mkakamao wa tumbo wakati wa siku<br />

zao za hedhi. Huu mkakamao unatokea kwa sababu misuli ya tumbo la uzazi inabana wakati<br />

ngozi laini inayozunguka tumbo la uzazi inapojiachia na ukuta. Mkakamao huo ni wa kawaida<br />

na unaweza ukavumilika. Iwapo maumivu ni makali lala chini na jaribu kuupumzisha mwili kwa<br />

kuvuta hewa nyingi na taratibu. Vilevile unaweza kuliminyaminya tumbo lako. Njia nyingine ni<br />

kuweka chupa ya maji ya moto tumboni na itakusaidia kupata nafuu. Kama njia hii haikusaidii,<br />

tafuta dawa za tumbo za kutuliza maumivu kwenye maduka ya dawa au dukani.<br />

Mazoezi pia yanaweza kusaidia japo hili halitakuwa jambo la kwanza kulifikiria. Unaweza<br />

kujisikia kama kulala chini, lakini kufanya matembezi au kukimbia huwa kunawasaidia baadhi ya<br />

wasichana kushughulikia tatizo la mkakamao wa tumbo. Ukiweza kupata kisodo aina ya tampoon<br />

unaweza hata kwenda kuogelea. Kuwa katika hedhi kisiwe kikwazo cha kufanya shughuli zako za<br />

kila siku ikiwa ni pamoja na kufanya mambo unayoyafurahia.<br />

Mkakamao wakati wa hedhi na maumivu mara nyingi ndio dalili za awali za balehe na<br />

unapofikisha umri wa miaka 18 au zaidi pengine mambo haya hayatakusumbua sana. Lakini<br />

wasichana wengine hupata maumivu yasiyo ya kawaida wakati wa siku zao. Hawa mara nyingi ni<br />

wasichana wenye hedhi nzito.<br />

Wasichana wenye hedhi nzito mara nyingi wanatumia pedi nyingi usiku na mchana na bado<br />

wanaacha alama ya damu kwenye mashuka au nguo. Mara nyingine wanakosa kwenda shule kwa<br />

sababu wanatoka damu nyingi au wana maumivu makali. Hebu fikiria kukosa kwenda shule kila<br />

mwezi na madhara utakayoyapata katika masomo yako!<br />

Kuna ufumbuzi wa kushughulikia hedhi kali, hivyo usiumie bure. Iwapo kweli una maumivu makali<br />

wakati wa siku zako au unatoka sana damu – kama unakosa kwenda shule kwa sababu ya siku<br />

zako muone muhudumu wa afya. Wahudumu wengine wa afya wanaweza kupendekeza vidonge<br />

vya kuzuia mimba ili kupunguza hedhi nzito yenye maumivu makali. Vidonge vinafanya hedhi<br />

isibadilike badilike ovyo ovyo na vinasaidia kupunguza kiasi cha damu inayopotea kila mwezi.<br />

Iwapo unahitaji kuonana na mganga wako mwulize kuhusu vidonge vya kuzuia mimba. Unaweza<br />

kumeza vidonge hivi hata kama bado ungali hujaanza kufanya ngono. Vidonge vina dozi ndogo ya<br />

homoni ambayo kwa asili inapatikana mwilini. Ni salama kwa vijana wanao balehe.<br />

Kama Mganga hataki kukuandikia cheti cha dawa hizo jieleze,ukipenda mwuulize ufanye nini<br />

kupunguza udhia unaoupata kila mwezi. Usikose kwenda shule kwa sababu ya tatizo linaloweza<br />

kutatuliwa.<br />

Unaweza pia kumwona mhudumu wa afya unapoanza kutoka damu katikati ya mzunguko wa<br />

hedhi au kama siku zako za hedhi zinachukua zaidi ya siku 8.<br />

nGOnO na heDhi<br />

Hakuna ukweli kabisa kuhusu uvumi kwamba ngono inatibu maumivu ya hedhi. Ukweli ni kwamba<br />

kufanya ngono wakati wa hedhi kunaweza kukuongezea uwezekano wa kuambukizwa magonjwa<br />

ya ngono ukiwemo UKIMWI. Damu ya hedhi ni mazingira mazuri kwa bakteria na virusi kukua<br />

haraka.<br />

Iwapo mwanamke aliye katika hedhi amefanya ngono na mwanaume mwenye magonjwa ya<br />

ngono, kuna uwezekano mkubwa kuambukizwa kuliko wakati mwingine wowote wa mzunguko<br />

wake; vilevile kuna uwezekano wa kupata maradhi mengine hatari wakati wa hedhi. Hii ni kwa<br />

sababu mlango wa tumbo la uzazi hufunguka kuliko kawaida ili damu ya hedhi iweze kupita.<br />

Vijidudu vya magonjwa ya ngono vinaweza kusafiri hadi kwenye tumbo la uzazi na kupitia mirija<br />

ya kupitishia mayai, hivyo kusababisha maambukizi kwenye via vya uzazi vya mwanamke,na<br />

hatimaye kusababisha ugumba.<br />

Kwa mwanaume, kufanya ngono na mwanamke aliye katika hedhi ni hatari vilevile.<br />

Kama ameambukizwa VVU, damu yake itakuwa na virusi vingi vya VVU.<br />

KujiSiKia ViZuRi, aFYa na uSaFi<br />

Katika tamaduni zingine, wanawake walio katika hedhi wanachukuliwa kama wachafu. Lakini<br />

ukweli damu ya hedhi ni safi. Baada ya damu ya hedhi kutoka mwilini bakteria wanaweza<br />

wakakua ndani yake, na kusababisha inuke, ndio maana usafi ni muhimu unapokuwa katika hali<br />

hii. Wakati wa hedhi, oga angalau mara moja ili uwe msafi. Usitumie manukato kwenye via vya<br />

uzazi yanaweza kukusababishia muwasho.<br />

Vidokezi vitakavyosaidia kuzifanya siku zako ziwe nyepesi na starehe:<br />

•<br />

•<br />

SURA YA 4 | WASICHANA<br />

Wakati wote kuwa tayari, zijue siku zako za hedhi ili usije ukashitukizwa.<br />

Acha kutumia chumvi nyingi, chumvi inafanya mwili wako uwe na maji mengi, hasa wakati wa<br />

siku zako.Hii inaweza kukufanya kujisikia mwili mzito kuvimba tumbo kutokuwa na raha na<br />

kuwa na mfadhaiko.<br />

41

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!