Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
56<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Kujienzi ni kitu ambacho kipo ndani yako. Lakini hiyo haimaanishi huwezi kuifanyia kazi au<br />
kuhitaji kuikuza na kuijenga. Unaweza kuzingatia yafutayo ili ujenge tabia ya kujienzi:<br />
•<br />
•<br />
JE UNAJUA Maana ya kuwa na Afya nzuri kihisia?<br />
Inaweza ikawa vigumu kuelezea afya nzuri ya kihisia. Lakini kawaida utaijua kwa kuona.<br />
Kwa mfano tumchukulie Rose, anaelekea kuwa na furaha wakati wote na anaonekana<br />
kuyamudu maisha ya raha na tabu.<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Anapopata maksi za chini anakubaliana nazo na anaongeza bidii.<br />
Akiachwa na mpenzi wake, analia lakini baadaye anaamua kwamba siyo mwisho wa<br />
dunia.<br />
Kipindi cha mitihani, huwa hafadhaiki sana. Hufanya mazoezi na kuzungumza na rafiki<br />
yake mpenzi kukabili mfadhaiko.<br />
Rose anajienzi sana. Hashindwi na hisia anapoachwa na mpenzi wake. Hujitambua kama ni<br />
mtu muhimu. Vile vile anajiamini sana. Ni kweli kwamba alifanya vibaya kwenye majaribio,<br />
lakini anajua anaweza kufanya vizuri zaidi. Hahitaji kumlaumu mwalimu. Njia anayotumia<br />
kupambana na mfadhaiko ni nzuri. Michezo na kumwambia rafiki anayemwamini matatizo<br />
yanayomsibu kunamsaidia kushughulikia wasiwasi na kisha kusonga mbele.<br />
Aidha, watu wengine wanapata shida sana kumudu raha na shida za maisha. Kwa mfano<br />
Emma, ambaye yuko katika mazingira yanayofanana na ya Rose, hufanya kila kitu tofauti.<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Hakubali kukosolewa badala yake humlaumu mwalimu kwa kupata alama mbaya.<br />
Akiachwa na mpenzi wake anafadhaika. Hutangaza mambo ya uongo kuhusu mvulana<br />
huyo na huanza kufanya mbwembwe na wavulana wengine.<br />
Anapokuwa na mfadhaiko anaanza kunywa pombe na kuvuta sigara.<br />
Inakuwaje Emma anapata shida sana kuyamudu matatizo haya? Jambo mojawapo ni<br />
kujienzi. Anaumia sana anapoachwa na mpenzi wake na anayamudu maumivu kwa<br />
kumsema rafiki yake vibaya. Anajaribu kujihakikishia kwamba bado anapendwa kwa<br />
kumpenda mvulana mwingine. Njia yake ya kupambana na mfadhaiko haifai kabisa, pombe<br />
na sigara vinaweza kukusahaulisha kwa muda lakini havitatui tatizo.<br />
Epuka kujilinganisha na wengine mara kwa mara. Weka malengo yako, na usijihukumu<br />
mwenyewe kwa kuangalia mafanikio ya mtu mwingine. <strong>Maisha</strong> ni safari ndefu. Kuna wakati<br />
utaenda mbele na wakati mwingine utarudi nyuma.<br />
Tambua vipaji vyako na kujikubali vile ulivyo.Tengeneza orodha ya mambo unayoyafanya<br />
vizuri. Je wewe ni msanii? Mwanariadha.Mwimbaji, msimuliaji wa hadithi au mnenguaji<br />
(mcheza dansi) Ni masomo gani unayofanya vizuri shuleni?<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
•<br />
Fikiria wewe ni mtu wa aina gani na kutengeneza orodha ya sifa ulizonazo. Unapenda nini<br />
kuhusu wewe mwenyewe? Wema wako? Ucheshi? Ubunifu? Umakini?<br />
Fahamu mambo yanayokuhusu ambayo ungependa kuyaboresha, lakini usijikosoe sana.<br />
Kuwa mhalisi na weka malengo ambayo yanatekelezeka na yatakayoonyesha mafanikio ili<br />
uridhike unapoyakamilisha.<br />
Jiamini, na jiambie “ninaweza!”.<br />
Tumia muda wako na watu wanaokujali wanaofanya ujisikie vizuri na kuongeza hadhi ya<br />
kujiheshimu. Kaa mbali na watu wanaojaribu kuharibu heshima yako, hasa kama wanafanya<br />
hivyo kwa sababu fulani.<br />
Kwa vyovyote vile kuifanyia kazi heshima yako haina maana kuwa hutaweza kupata matatizo.<br />
Kuifanyia kazi heshima yako itakusaidia matatizo kuwa mepesi. Kujiheshimu kunakulinda wewe<br />
binafsi. Wakati mtu anakutendea vibaya hisia za kujiheshimu zinapiga kelele “Hee! haya ni<br />
makosa, usiruhusu mtu huyu akakutendea hivi”.<br />
Hebu fikiria kana kwamba marafiki zako wamekuacha. Wamejiunga pamoja na kukuacha peke<br />
yako. Ghafla unajisikia kutetemeka na huna uhakika wa mambo yako. Ni kwa nini hawakutaki<br />
tena? Je kuna makosa umefanya? Heshima yako inaanza kufifia kama ua linavyonyauka.Unaanza<br />
kujisikia vibaya.<br />
Katika mazingira ya namna hii, watu wengine hupata hofu. Wanachukua njia rahisi ya kurudisha<br />
heshima inayoshuka ili apendwe tena, hata kama itamaanisha kufanya jambo ambalo wanafikiria<br />
ni kosa. Kwa mfano, vijana wengine ambao wamekataliwa na marafiki zao wa zamani huanza<br />
kujiunga na makundi ya vijana wanaokunywa pombe, wanaovuta bangi na kujiingiza kwenye<br />
matatizo makubwa. Hivyo wanaanza nao kula madawa ya kulevya, kunywa pombe ili waweze<br />
kukubalika.<br />
Ni vizuri kutafuta kukubalika na kweli inapandisha hadhi lakini haisaidii kutatua matatizo ya<br />
kujiheshimu na wala kukubalika hakudumu. Unaweza kujisikia vizuri kwa muda lakini baada<br />
ya muda mfupi sauti ndogo ndani yako huanza kukusumbua: “Watu hawa hawako makini”. Sauti<br />
hii ni kwamba haujawa mkweli kwako mwenyewe, unajizuia kufanya mambo unayoyataka na<br />
unayoyaweza. Hujisikii vizuri kutokana na yale unayoyafanya kwa mkumbo...” Hiyo sauti ndogo ni<br />
nafsi yako. Ni vema wakati wowote kuisikiliza.<br />
Kurekebisha kujienzi kwako ni kazi kubwa kuliko kujiunga na makundi mapya, au kupoteza<br />
mawazo kwa kutumia pombe, na madawa ya kulevya, (kwa taarifa zaidi kuhusu madawa ya<br />
kulevya na pombe soma sura ya 12). Itakusaidia zaidi kurekebisha kujienzi kwako. Unapopitia<br />
matatizo ya kujienzi, yafuatayo ni mambo machache unayoweza kuyafanya ili yakusaidie:-<br />
•<br />
•<br />
SURA YA 6 | UTUNZAJI AfYA YA AKILI NA MOYO<br />
Jaribu kuliweka tatizo lililopo katika mtazamo sahihi. Jaribu kukumbuka kwamba dunia<br />
imejaa mambo ya raha na shida, na kwamba huu sio mwisho wa dunia.<br />
Zungumza na mtu wa karibu yako na unayemwamini kuhusu matatizo yako na hisia<br />
zako. Mtafute kijana mtoa ushauri nasaha au mtu ambaye anakujali na ambaye anaweza<br />
kukusaidia.<br />
57