08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

56<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Kujienzi ni kitu ambacho kipo ndani yako. Lakini hiyo haimaanishi huwezi kuifanyia kazi au<br />

kuhitaji kuikuza na kuijenga. Unaweza kuzingatia yafutayo ili ujenge tabia ya kujienzi:<br />

•<br />

•<br />

JE UNAJUA Maana ya kuwa na Afya nzuri kihisia?<br />

Inaweza ikawa vigumu kuelezea afya nzuri ya kihisia. Lakini kawaida utaijua kwa kuona.<br />

Kwa mfano tumchukulie Rose, anaelekea kuwa na furaha wakati wote na anaonekana<br />

kuyamudu maisha ya raha na tabu.<br />

•<br />

•<br />

•<br />

Anapopata maksi za chini anakubaliana nazo na anaongeza bidii.<br />

Akiachwa na mpenzi wake, analia lakini baadaye anaamua kwamba siyo mwisho wa<br />

dunia.<br />

Kipindi cha mitihani, huwa hafadhaiki sana. Hufanya mazoezi na kuzungumza na rafiki<br />

yake mpenzi kukabili mfadhaiko.<br />

Rose anajienzi sana. Hashindwi na hisia anapoachwa na mpenzi wake. Hujitambua kama ni<br />

mtu muhimu. Vile vile anajiamini sana. Ni kweli kwamba alifanya vibaya kwenye majaribio,<br />

lakini anajua anaweza kufanya vizuri zaidi. Hahitaji kumlaumu mwalimu. Njia anayotumia<br />

kupambana na mfadhaiko ni nzuri. Michezo na kumwambia rafiki anayemwamini matatizo<br />

yanayomsibu kunamsaidia kushughulikia wasiwasi na kisha kusonga mbele.<br />

Aidha, watu wengine wanapata shida sana kumudu raha na shida za maisha. Kwa mfano<br />

Emma, ambaye yuko katika mazingira yanayofanana na ya Rose, hufanya kila kitu tofauti.<br />

•<br />

•<br />

•<br />

Hakubali kukosolewa badala yake humlaumu mwalimu kwa kupata alama mbaya.<br />

Akiachwa na mpenzi wake anafadhaika. Hutangaza mambo ya uongo kuhusu mvulana<br />

huyo na huanza kufanya mbwembwe na wavulana wengine.<br />

Anapokuwa na mfadhaiko anaanza kunywa pombe na kuvuta sigara.<br />

Inakuwaje Emma anapata shida sana kuyamudu matatizo haya? Jambo mojawapo ni<br />

kujienzi. Anaumia sana anapoachwa na mpenzi wake na anayamudu maumivu kwa<br />

kumsema rafiki yake vibaya. Anajaribu kujihakikishia kwamba bado anapendwa kwa<br />

kumpenda mvulana mwingine. Njia yake ya kupambana na mfadhaiko haifai kabisa, pombe<br />

na sigara vinaweza kukusahaulisha kwa muda lakini havitatui tatizo.<br />

Epuka kujilinganisha na wengine mara kwa mara. Weka malengo yako, na usijihukumu<br />

mwenyewe kwa kuangalia mafanikio ya mtu mwingine. <strong>Maisha</strong> ni safari ndefu. Kuna wakati<br />

utaenda mbele na wakati mwingine utarudi nyuma.<br />

Tambua vipaji vyako na kujikubali vile ulivyo.Tengeneza orodha ya mambo unayoyafanya<br />

vizuri. Je wewe ni msanii? Mwanariadha.Mwimbaji, msimuliaji wa hadithi au mnenguaji<br />

(mcheza dansi) Ni masomo gani unayofanya vizuri shuleni?<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

•<br />

Fikiria wewe ni mtu wa aina gani na kutengeneza orodha ya sifa ulizonazo. Unapenda nini<br />

kuhusu wewe mwenyewe? Wema wako? Ucheshi? Ubunifu? Umakini?<br />

Fahamu mambo yanayokuhusu ambayo ungependa kuyaboresha, lakini usijikosoe sana.<br />

Kuwa mhalisi na weka malengo ambayo yanatekelezeka na yatakayoonyesha mafanikio ili<br />

uridhike unapoyakamilisha.<br />

Jiamini, na jiambie “ninaweza!”.<br />

Tumia muda wako na watu wanaokujali wanaofanya ujisikie vizuri na kuongeza hadhi ya<br />

kujiheshimu. Kaa mbali na watu wanaojaribu kuharibu heshima yako, hasa kama wanafanya<br />

hivyo kwa sababu fulani.<br />

Kwa vyovyote vile kuifanyia kazi heshima yako haina maana kuwa hutaweza kupata matatizo.<br />

Kuifanyia kazi heshima yako itakusaidia matatizo kuwa mepesi. Kujiheshimu kunakulinda wewe<br />

binafsi. Wakati mtu anakutendea vibaya hisia za kujiheshimu zinapiga kelele “Hee! haya ni<br />

makosa, usiruhusu mtu huyu akakutendea hivi”.<br />

Hebu fikiria kana kwamba marafiki zako wamekuacha. Wamejiunga pamoja na kukuacha peke<br />

yako. Ghafla unajisikia kutetemeka na huna uhakika wa mambo yako. Ni kwa nini hawakutaki<br />

tena? Je kuna makosa umefanya? Heshima yako inaanza kufifia kama ua linavyonyauka.Unaanza<br />

kujisikia vibaya.<br />

Katika mazingira ya namna hii, watu wengine hupata hofu. Wanachukua njia rahisi ya kurudisha<br />

heshima inayoshuka ili apendwe tena, hata kama itamaanisha kufanya jambo ambalo wanafikiria<br />

ni kosa. Kwa mfano, vijana wengine ambao wamekataliwa na marafiki zao wa zamani huanza<br />

kujiunga na makundi ya vijana wanaokunywa pombe, wanaovuta bangi na kujiingiza kwenye<br />

matatizo makubwa. Hivyo wanaanza nao kula madawa ya kulevya, kunywa pombe ili waweze<br />

kukubalika.<br />

Ni vizuri kutafuta kukubalika na kweli inapandisha hadhi lakini haisaidii kutatua matatizo ya<br />

kujiheshimu na wala kukubalika hakudumu. Unaweza kujisikia vizuri kwa muda lakini baada<br />

ya muda mfupi sauti ndogo ndani yako huanza kukusumbua: “Watu hawa hawako makini”. Sauti<br />

hii ni kwamba haujawa mkweli kwako mwenyewe, unajizuia kufanya mambo unayoyataka na<br />

unayoyaweza. Hujisikii vizuri kutokana na yale unayoyafanya kwa mkumbo...” Hiyo sauti ndogo ni<br />

nafsi yako. Ni vema wakati wowote kuisikiliza.<br />

Kurekebisha kujienzi kwako ni kazi kubwa kuliko kujiunga na makundi mapya, au kupoteza<br />

mawazo kwa kutumia pombe, na madawa ya kulevya, (kwa taarifa zaidi kuhusu madawa ya<br />

kulevya na pombe soma sura ya 12). Itakusaidia zaidi kurekebisha kujienzi kwako. Unapopitia<br />

matatizo ya kujienzi, yafuatayo ni mambo machache unayoweza kuyafanya ili yakusaidie:-<br />

•<br />

•<br />

SURA YA 6 | UTUNZAJI AfYA YA AKILI NA MOYO<br />

Jaribu kuliweka tatizo lililopo katika mtazamo sahihi. Jaribu kukumbuka kwamba dunia<br />

imejaa mambo ya raha na shida, na kwamba huu sio mwisho wa dunia.<br />

Zungumza na mtu wa karibu yako na unayemwamini kuhusu matatizo yako na hisia<br />

zako. Mtafute kijana mtoa ushauri nasaha au mtu ambaye anakujali na ambaye anaweza<br />

kukusaidia.<br />

57

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!