Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
140<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Je, unajua njia zipi za kuzuia mimba ambazo ni salama kwa vijana?<br />
Njia zote hizi za kuzuia mimba ni salama kwa vijana:<br />
Kondomu: Kondomu ni mpira laini ambao huwekwa kwenye uume<br />
uliosimama kabla ya kujamiiana. Mwanaume anapotoa shahawa (“anafikia<br />
mshindo”) zinanaswa nchani mwa kondomu. Majimaji toka kwa mwanaume<br />
hayamwingii mwanamke na majimaji toka kwa mwanamke hayagusi uume<br />
wa mwanaume. Kondomu zinatoa kinga nzuri dhidi ya magonjwa ya ngono, pamoja na VVU/ UKIMWI<br />
na huzuia mimba. Bei ya kondomu ni ndogo na zinawasaidia wanaume wengine kuchelewa kutoa<br />
shahawa mapema.<br />
Vidonge: Vidonge vina kiasi kidogo sana cha homoni. Homoni hii huzuia uovishaji<br />
kutoka kwenye makokwa ya mayai. Mwanamke aliyeingia kwenye hedhi<br />
anapomeza kidonge lakini kidonge kinafanya hedhi ya mwanamke kuwa nyepesi<br />
na maumivu kuwa mepesi. Pia matokeo ya kuzuia mimba kwa kutumia vidonge<br />
ni mazuri sana, lakini lazima umeze kila siku. Ukikosa kumeza zaidi ya siku moja<br />
unaweza kupata mimba kwa sababu rutuba inarudi pindi unapoacha kumeza<br />
vidonge. Vidonge havizuii VVU au mangojwa mengine ya zinaa. Kwa hiyo, ni vizuri<br />
iwapo unatumia kondomu, uwe na mwenzi mmoja tu na wote muwe mmepima na kuthibitisha hamna<br />
magonjwa ya ngono/VVU.<br />
Sindano: Sindano ina homoni ambazo zinazuia yai kurutubishwa. Huanza<br />
kufanya kazi katika muda wa saa 24 na hutoa kinga dhidi ya mimba kwa<br />
muda wa miezi mitatu. Kudunga sindano ni rahisi kwa sababu huhitaji<br />
kukumbuka kumeza kidonge kila siku au kufanya chochote kabla ya<br />
kujamiiana. Sindano pia inatunza siri, hakuna anayeweza kujua kwamba<br />
unatumia mtindo huu kwa kuzuia mimba. Sindano zinafanya siku zako za<br />
hedhi ziwe nyepesi na zenye maumivu kidogo ambapo zinaweza kuwasaidia<br />
vijana wanaopata maumivu au hedhi nzito. Unapoacha kudunga sindano, huwi na rutuba tena mara<br />
moja, kwa sababu homoni zinakaa mwilini kwa muda . Wanawake wengi wanakuwa na rutuba tena<br />
ndani ya mwaka mmoja wanapoacha kutumia sindano, lakini wengine wanapata mimba mapema.<br />
Sindano hazizuii magonjwa ya zinaa/VVU hivyo zinafaa tu kama unatumia kondomu au kama unaye<br />
mwenzi mmoja na wote mmepima magonjwa ya ngono/VVU.<br />
Vipandikizi: Vipandikizi ni vimrija vidogo vinavyowekwa ndani ya ngozi kwenye<br />
mkono chini kidogo ya bega. Vimirija hivyo huwa vinatoa homoni inayozuia yai<br />
kurutubishwa. Kama ilivyo kwa sindano huhitaji kukumbuka kumeza vidonge<br />
au kufanya lolote kabla ya kujamiiana. Vipandikizi vinadumu miaka mitano.<br />
Lakini vinaweza kuondolewa mapema. Ni kinga nzuri sana kuzuia mimba, lakini<br />
haizuii magonjwa ya zinaa/VVU. Kwa hiyo unatakiwa kutumia kondomu au kuhakikisha kuwa wewe na<br />
mwenzi wako hamna magonjwa ya ngono/VVU.<br />
Dawa ya kuulia mbegu za kiume (vidonge mafuta au krimu na povu): Dawa<br />
hizi zinaua mbegu za mwanaume kabla hazijaingia ndani ya mfuko wa kizazi,<br />
lakini hazimuumizi mwanaume au mwanamke. Zipo aina mbalimbali za dawa<br />
na zinaingizwa ukeni kabla ya kujamiiana. Dawa hizi zitumike na kondomu kwa<br />
sababu zina kinga ndogo sana dhidi ya magonjwa ya zinaa/VVU. Zaidi ya hapo,<br />
hazina kinga madhubuti kama ya vidonge au sindano katika kuzuia mimba.<br />
Tofauti na vidonge na sindano, huhitaji kuzipata kutoka kwa mhudumu wa afya; unaweza kupata moja<br />
kwa moja toka kwenye maduka ya dawa. Hii inaweza kuwa bahati kama una aibu kwenda kliniki, lakini<br />
kumbuka kutumia kondomu.<br />
Unapotumia vidonge vya dharura inakubidi umeze kiasi cha mchanganyiko wa vidonge vya kuzuia<br />
mimba baada ya saa 12 katika kipindi cha saa 72 za kufanya ngono bila kinga. Kinga ya dharura ya<br />
kuzuia mimba haifanyi kazi mimba inapokuwa imetungwa. Ndio maana ni muhimu kuipata haraka<br />
baada ya ngono isiyo na kinga. Usijaribu kunywa dawa hizi bila ushauri wa mhudumu wa afya<br />
mwenye ujuzi.<br />
KinGa MaRa Mbili<br />
SURA YA 11 | MIMBA NA UZUIAJI WA MIMBA<br />
Je, unafahamu kuwa wanawake waliokeketwa wana mahitaji<br />
Kuchomoa/kurusha: Kuchomoa au kurusha ni wakati mwanaume anatoa uume nje ya uke<br />
kabla ya kukojoa shahawa. Njia hii sio salama kwa sababu wanaume wengi hawawezi kuutoa<br />
uume kwa wakati unaotakiwa. Mara nyingi wanaume hawajui kwamba wanakaribia kukojoa<br />
mpaka wanapokuwa wamekaribia sana. Pia, matone machache ya shahawa yanaweza kutoka<br />
kabla ya kukojoa na matone machache haya yanatosha kusababisha mimba. Kuchomoa<br />
hakuleti kinga dhidi ya VVU/UKIMWI na magonjwa mengine ya zinaa.<br />
“Siku salama”: Wanawake wengine wanasubiri siku ambazo wanajua kwamba hawana rutuba.<br />
Utaratibu huu unafaa kwa wanawake ambao hedhi zao ni za kawaida na wenzi wao wana<br />
ushirikiano. Wasichana wa umri mdogo wengi hawana hedhi za kawaida hivyo si rahisi kujua<br />
siku salama. Kama ilivyo kwa njia ya kuchomoa, siku salama hazileti kinga dhidi ya magonjwa<br />
ya zinaa/VVU.<br />
Kitanzi: Kitanzi kinatumbukizwa kwenye tumbo la uzazi na mhudumu wa afya. Ni rahisi<br />
kukiingiza kwa mwanamke ambaye amewahi kuzaa, kwa hiyo haipendekezwi kwa vijana.<br />
Kitanzi kinaweza kusababisha ugonjwa wa ngono ukue na kufikia hali ya kutisha. Kwa vile<br />
vijana ni rahisi sana kuambukizwa magonjwa ya zinaa, wasitumie kitanzi. Kitanzi hakitoi kinga<br />
dhidi ya magonjwa ya zinaa/VVU.<br />
Kufunga kizazi: Kukata au kufunga mirija ya kupitishia mbegu ya wanaume na wanawake ni<br />
njia ya kudumu ya kuzuia mimba. Unafanyika upasuaji ambapo mirija ya kupitishia shahawa na<br />
yai inazibwa. Njia hii inawahusu wanaume na wanawake ambao wanafikiri wamepata idadi ya<br />
watoto inayowatosha. Njia hii haifai kwa vijana kwa sababu huwezi kupata watoto baada ya<br />
upasuaji. Kufunga kizazi hakutoi kinga dhidi ya magonjwa ya zinaa/VVU.<br />
Ugonjwa wa UKIMWI umebadilisha mawazo ya watu wengi kuhusu njia za kuzuia mimba.<br />
Zamani watu walilenga katika kuangalia ni njia zipi zinaleta matokeo bora katika kuzuia mimba.<br />
Hawakujali sana kama njia ya kuzuia mimba ilitoa kinga dhidi ya magonjwa ya zinaa/VVU.<br />
Leo mambo ni tofauti. Kupata VVU ni maafa makubwa kuliko kupata mimba isiyotakiwa. Siku<br />
hizi watu wanazungumzia kuhusu kinga mara mbili. Kinga mara mbili ni wakati unatumia njia<br />
ambayo matokeo yake hupunguza hatari ya mambukizo ya magonjwa ya zinaa/VVU/UKIMWI, na<br />
wakati huohuo, unatumia njia nyingine ambayo matokeo yake ni mazuri katika kukinga mimba<br />
zisizotakiwa.<br />
Angalia njia mbalimbali hapa chini uone jinsi zinavyotoa kinga dhidi ya mimba na magonjwa<br />
mengine ya ngono pamoja na VVU.<br />
141