08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

140<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Je, unajua njia zipi za kuzuia mimba ambazo ni salama kwa vijana?<br />

Njia zote hizi za kuzuia mimba ni salama kwa vijana:<br />

Kondomu: Kondomu ni mpira laini ambao huwekwa kwenye uume<br />

uliosimama kabla ya kujamiiana. Mwanaume anapotoa shahawa (“anafikia<br />

mshindo”) zinanaswa nchani mwa kondomu. Majimaji toka kwa mwanaume<br />

hayamwingii mwanamke na majimaji toka kwa mwanamke hayagusi uume<br />

wa mwanaume. Kondomu zinatoa kinga nzuri dhidi ya magonjwa ya ngono, pamoja na VVU/ UKIMWI<br />

na huzuia mimba. Bei ya kondomu ni ndogo na zinawasaidia wanaume wengine kuchelewa kutoa<br />

shahawa mapema.<br />

Vidonge: Vidonge vina kiasi kidogo sana cha homoni. Homoni hii huzuia uovishaji<br />

kutoka kwenye makokwa ya mayai. Mwanamke aliyeingia kwenye hedhi<br />

anapomeza kidonge lakini kidonge kinafanya hedhi ya mwanamke kuwa nyepesi<br />

na maumivu kuwa mepesi. Pia matokeo ya kuzuia mimba kwa kutumia vidonge<br />

ni mazuri sana, lakini lazima umeze kila siku. Ukikosa kumeza zaidi ya siku moja<br />

unaweza kupata mimba kwa sababu rutuba inarudi pindi unapoacha kumeza<br />

vidonge. Vidonge havizuii VVU au mangojwa mengine ya zinaa. Kwa hiyo, ni vizuri<br />

iwapo unatumia kondomu, uwe na mwenzi mmoja tu na wote muwe mmepima na kuthibitisha hamna<br />

magonjwa ya ngono/VVU.<br />

Sindano: Sindano ina homoni ambazo zinazuia yai kurutubishwa. Huanza<br />

kufanya kazi katika muda wa saa 24 na hutoa kinga dhidi ya mimba kwa<br />

muda wa miezi mitatu. Kudunga sindano ni rahisi kwa sababu huhitaji<br />

kukumbuka kumeza kidonge kila siku au kufanya chochote kabla ya<br />

kujamiiana. Sindano pia inatunza siri, hakuna anayeweza kujua kwamba<br />

unatumia mtindo huu kwa kuzuia mimba. Sindano zinafanya siku zako za<br />

hedhi ziwe nyepesi na zenye maumivu kidogo ambapo zinaweza kuwasaidia<br />

vijana wanaopata maumivu au hedhi nzito. Unapoacha kudunga sindano, huwi na rutuba tena mara<br />

moja, kwa sababu homoni zinakaa mwilini kwa muda . Wanawake wengi wanakuwa na rutuba tena<br />

ndani ya mwaka mmoja wanapoacha kutumia sindano, lakini wengine wanapata mimba mapema.<br />

Sindano hazizuii magonjwa ya zinaa/VVU hivyo zinafaa tu kama unatumia kondomu au kama unaye<br />

mwenzi mmoja na wote mmepima magonjwa ya ngono/VVU.<br />

Vipandikizi: Vipandikizi ni vimrija vidogo vinavyowekwa ndani ya ngozi kwenye<br />

mkono chini kidogo ya bega. Vimirija hivyo huwa vinatoa homoni inayozuia yai<br />

kurutubishwa. Kama ilivyo kwa sindano huhitaji kukumbuka kumeza vidonge<br />

au kufanya lolote kabla ya kujamiiana. Vipandikizi vinadumu miaka mitano.<br />

Lakini vinaweza kuondolewa mapema. Ni kinga nzuri sana kuzuia mimba, lakini<br />

haizuii magonjwa ya zinaa/VVU. Kwa hiyo unatakiwa kutumia kondomu au kuhakikisha kuwa wewe na<br />

mwenzi wako hamna magonjwa ya ngono/VVU.<br />

Dawa ya kuulia mbegu za kiume (vidonge mafuta au krimu na povu): Dawa<br />

hizi zinaua mbegu za mwanaume kabla hazijaingia ndani ya mfuko wa kizazi,<br />

lakini hazimuumizi mwanaume au mwanamke. Zipo aina mbalimbali za dawa<br />

na zinaingizwa ukeni kabla ya kujamiiana. Dawa hizi zitumike na kondomu kwa<br />

sababu zina kinga ndogo sana dhidi ya magonjwa ya zinaa/VVU. Zaidi ya hapo,<br />

hazina kinga madhubuti kama ya vidonge au sindano katika kuzuia mimba.<br />

Tofauti na vidonge na sindano, huhitaji kuzipata kutoka kwa mhudumu wa afya; unaweza kupata moja<br />

kwa moja toka kwenye maduka ya dawa. Hii inaweza kuwa bahati kama una aibu kwenda kliniki, lakini<br />

kumbuka kutumia kondomu.<br />

Unapotumia vidonge vya dharura inakubidi umeze kiasi cha mchanganyiko wa vidonge vya kuzuia<br />

mimba baada ya saa 12 katika kipindi cha saa 72 za kufanya ngono bila kinga. Kinga ya dharura ya<br />

kuzuia mimba haifanyi kazi mimba inapokuwa imetungwa. Ndio maana ni muhimu kuipata haraka<br />

baada ya ngono isiyo na kinga. Usijaribu kunywa dawa hizi bila ushauri wa mhudumu wa afya<br />

mwenye ujuzi.<br />

KinGa MaRa Mbili<br />

SURA YA 11 | MIMBA NA UZUIAJI WA MIMBA<br />

Je, unafahamu kuwa wanawake waliokeketwa wana mahitaji<br />

Kuchomoa/kurusha: Kuchomoa au kurusha ni wakati mwanaume anatoa uume nje ya uke<br />

kabla ya kukojoa shahawa. Njia hii sio salama kwa sababu wanaume wengi hawawezi kuutoa<br />

uume kwa wakati unaotakiwa. Mara nyingi wanaume hawajui kwamba wanakaribia kukojoa<br />

mpaka wanapokuwa wamekaribia sana. Pia, matone machache ya shahawa yanaweza kutoka<br />

kabla ya kukojoa na matone machache haya yanatosha kusababisha mimba. Kuchomoa<br />

hakuleti kinga dhidi ya VVU/UKIMWI na magonjwa mengine ya zinaa.<br />

“Siku salama”: Wanawake wengine wanasubiri siku ambazo wanajua kwamba hawana rutuba.<br />

Utaratibu huu unafaa kwa wanawake ambao hedhi zao ni za kawaida na wenzi wao wana<br />

ushirikiano. Wasichana wa umri mdogo wengi hawana hedhi za kawaida hivyo si rahisi kujua<br />

siku salama. Kama ilivyo kwa njia ya kuchomoa, siku salama hazileti kinga dhidi ya magonjwa<br />

ya zinaa/VVU.<br />

Kitanzi: Kitanzi kinatumbukizwa kwenye tumbo la uzazi na mhudumu wa afya. Ni rahisi<br />

kukiingiza kwa mwanamke ambaye amewahi kuzaa, kwa hiyo haipendekezwi kwa vijana.<br />

Kitanzi kinaweza kusababisha ugonjwa wa ngono ukue na kufikia hali ya kutisha. Kwa vile<br />

vijana ni rahisi sana kuambukizwa magonjwa ya zinaa, wasitumie kitanzi. Kitanzi hakitoi kinga<br />

dhidi ya magonjwa ya zinaa/VVU.<br />

Kufunga kizazi: Kukata au kufunga mirija ya kupitishia mbegu ya wanaume na wanawake ni<br />

njia ya kudumu ya kuzuia mimba. Unafanyika upasuaji ambapo mirija ya kupitishia shahawa na<br />

yai inazibwa. Njia hii inawahusu wanaume na wanawake ambao wanafikiri wamepata idadi ya<br />

watoto inayowatosha. Njia hii haifai kwa vijana kwa sababu huwezi kupata watoto baada ya<br />

upasuaji. Kufunga kizazi hakutoi kinga dhidi ya magonjwa ya zinaa/VVU.<br />

Ugonjwa wa UKIMWI umebadilisha mawazo ya watu wengi kuhusu njia za kuzuia mimba.<br />

Zamani watu walilenga katika kuangalia ni njia zipi zinaleta matokeo bora katika kuzuia mimba.<br />

Hawakujali sana kama njia ya kuzuia mimba ilitoa kinga dhidi ya magonjwa ya zinaa/VVU.<br />

Leo mambo ni tofauti. Kupata VVU ni maafa makubwa kuliko kupata mimba isiyotakiwa. Siku<br />

hizi watu wanazungumzia kuhusu kinga mara mbili. Kinga mara mbili ni wakati unatumia njia<br />

ambayo matokeo yake hupunguza hatari ya mambukizo ya magonjwa ya zinaa/VVU/UKIMWI, na<br />

wakati huohuo, unatumia njia nyingine ambayo matokeo yake ni mazuri katika kukinga mimba<br />

zisizotakiwa.<br />

Angalia njia mbalimbali hapa chini uone jinsi zinavyotoa kinga dhidi ya mimba na magonjwa<br />

mengine ya ngono pamoja na VVU.<br />

141

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!