08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

110<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Magonjwa mengine ya zinaa kama kaswende, klamidia na kisonono ni hatari vilevile. Magonjwa<br />

haya yanatibika na tunaweza kuyathibiti. Lakini yanaweza kuleta athari za muda mrefu:<br />

•<br />

•<br />

Kusababisha ugumba yaani kushindwa kupata watoto.<br />

Kusaidia virusi vya UKIMWI kuingia mwilini kwa urahisi.<br />

Kwa ufupi, zipo njia tatu za kuepuka magonjwa ya zinaa ikiwa ni pamoja na VVU.<br />

1. Usifanye ngono. Ahirisha kufanya mapenzi au acha kabisa kujamiiana.<br />

2. Unapojamiiana, hakikisha unatumia kondomu tangu mwanzo mpaka unapomaliza kitendo.<br />

3. Nenda na mpenzi/mwenzi wako kupima VVU. Kabla ya kuanza kujamiiana. Unaweza kupima<br />

VVU zaidi ya mara moja kutegemeana ni lini ulifanya ngono isiyo salama (bila kinga) ili<br />

kuhakikisha huna VVU. (Angalia ukurasa wa 116 kwa maelezo zaidi). Hakikisha kati yenu hakuna<br />

aliye na maambukizo ya VVU kabla ya kuanza kujamiiana. Kila mmoja wenu abakie mwaminifu<br />

kwa mwenzie.<br />

Mambo haya yanaonekana kuwa rahisi. Njia za kuwa salama ni hizo tatu. Lakini, yapo mengi ya<br />

kufikiria. Iwapo ulifanya ngono na baadaye ukaamua kuacha, bado utatakiwa kupima. Unaweza<br />

kuwa na ugonjwa uenezwao kwa ngono bila ya kujitambua.<br />

je, unajua kwa nini wasichana wako hatarini zaidi kupata maambukizo ya<br />

magonjwa ya zinaa hasa VVu/uKiMWi?<br />

Ingawa wote, wanaume na wanawake, wanaweza kupata maambukizo ya magonjwa ya zinaa,<br />

wanawake na wasichana wanapata maambukizo kwa urahisi zaidi kuliko wanaume/wavulana.<br />

Zipo sababu kadhaa kwa nini iwe hivyo:<br />

1. Uume wa mwanaume unaingia ndani ya uke na shahawa zake zinaweza kuwa na maambukizo.<br />

Zikikaa ndani ya mwili wa mwanamke zinaongeza uwezekano wa kupata maambukizo ndani ya<br />

tumbo la uzazi, mirija ya falopia na ovari.<br />

2. Kwa ujumla, wasichana wako hatarini kupata maambukizo ya magonjwa ya zinaa kwa sababu<br />

mlango wa mfuko wa uzazi wa msichana balehe ni laini zaidi kuliko wa mwanamke mtu mzima. Uke<br />

unaweza ukachanika wakati wa kujamiiana jambo ambalo linaweza kuongezea hatari ya kupata<br />

maambukizo ya magonjwa ya ngono.<br />

3. Wasichana wengi na wanawake wanafundishwa kuwa watiifu na wanyenyekevu kwa wanaume.<br />

Hawana stadi ya kujiamini ili kuwashawishi wenzi wao kutumia kondomu kwa ajili ya kinga.<br />

Wasichana balehe wengi, walioolewa au wasioolewa, wenzi wao wana umri mkubwa kuliko wao<br />

wenyewe. Mwenzi anapokuwa na umri mkubwa kuliko msichana, inaweza kumuwia vigumu hasa<br />

msichana kujikinga na maambukizi ya magonjwa ya zinaa na mimba. Katika jamii nyingi inaweza<br />

kumwia vigumu mwanamke kukataa kujamiiana na mme wake au kumsisitizia watumie kondomu<br />

hata kama anafikiri mwanaume wake anaweza akawa na mwanamke mwingine.<br />

4. Wanawake na wasichana wako kwenye hatari ya kufanya ngono bila kutaka. (kwa kulazimishwa<br />

au kubakwa), kuliko wanaume na wavulana. Katika mazingira magumu kama haya, inaweza kuwa<br />

vigumu kujikinga na maambukizi.<br />

5. Mambo ya kimila na utamaduni kama vile kufanya ngono kavu na kuweka dawa za kienyeji, nguo<br />

na vitu vingine ndani ya uke ili “kusafisha” au “kuubana” vyote hivi vinamwongezea mwanamke<br />

hatari ya kupata maambukizo ya magonjwa ya ngono. Kukausha uke kabla ya kujamiiana<br />

kunaweza kuongeza uwezekano wa kuchanika na kuchubuka wakati wa kujamiiana.<br />

Kama wewe na mwenzi wako mnatumia kondomu wakati wote mnapojamiiana ni vizuri sana.<br />

Endelea!Watu wengi wanaanza kwa kutumia kondomu. Lakini baada ya muda wanaanza<br />

kufikiri. “Ninamwaminimwenzi wangu, tunaweza kuacha kutumia kondomu”. Hii siyo sawa!<br />

Kabla hamjaacha kutumiakondomu, wote wawili mnahitaji kupima kwa ajili ya magonjwa ya<br />

ngono pamoja na angalau, kipimokimoja cha VVU. Hata kama wewe na mwenzi wako mmepima<br />

na hamna maambukizo ya magonjwaya ngono, ni vizuri zaidi kuendelea kutumia kondomu. Je,<br />

ikitokea kwamba mmoja wenu amejamiianana mtu mwingine? Vilevile unahitaji kuzuia mimba.<br />

utajuaje KaMa uMePata MaaMbuKiZO Ya MaGOnjWa Ya Zinaa?<br />

Watu wengi hasa wanawake ambao wamepata maambukizo ya magonjwa ya zinaa<br />

hawaonyeshidalili zozote zile. Kwa mfano, hakuna dalili yoyote ya kuonyesha kwamba umepata<br />

maambukizo yaVVU kwa mara ya kwanza. Magonjwa mengine ya ngono vilevile hayana dalili za<br />

wazi, kwa hiyo kilamtu inabidi afikirie hatari ya kupata maambukizo ya magonjwa ya zinaa. Kama<br />

umeshafanya ngonobila kinga unaweza kuwa umejiweka katika hatari ya kupata maambukizo.<br />

Ukipata kidonda au kiupele sehemu za siri ambacho kinapotea, unahitaji kumwona mhudumu<br />

wa afya.Yapo magonjwa ya zinaa mengine ambayo yana dalili zinazokuja na kupotea. Kidonda<br />

cha kaswendewakati wote kinapona na vidonda vinavyotokana na malengelenge vinapona na<br />

kujirudia. Kama umewahikupata kidonda, kiupele au lengelenge kwenye via vya uzazi, unatakiwa<br />

kumwona mhudumu wa afya.Hata kama dalili za ugonjwa wa ngono zinapotea, maambukizo<br />

yanakuwepo na wala hayawezi kuponabila kupata tiba sahihi.<br />

Kwa vyovyote vile,kama<br />

umeshaanzakujamiiana au bado, ni<br />

vizuri kufahamuvia vyako vya uzazi<br />

vikoje. Ikiwa unajuavikoje ukiwa mzima,<br />

itakuwa rahisikugundua tatizo mapema.<br />

Tumia kiookujiangalia sehemu zako za<br />

siri kiurahisi.Kwa mfano, kidonda cha<br />

kaswendehakiumi, kwa hiyo unaweza<br />

usigundueisipokuwa kama ukiangalia.<br />

Kwa wasichana, ni vema kufahamu<br />

mwonekano na harufu ya kawaida<br />

yamajimaji yako ya ukeni. Majimaji<br />

yaukeni ya kawaida:. Ni kama majimaji<br />

meupe ya yai.<br />

• Ni maangavu au meupe.<br />

• Yanatoa harufu ya kawaida au yenye<br />

afya na isiyochukiza.<br />

• Hayawashi.<br />

SURA YA 10 | KUTUNZA AfYA YAKO YA KIUJINSIA<br />

Magonjwa ya ngono mara kwa mara<br />

husababisha majimaji ya ukeni kuwa na<br />

rangi ya njano au kijani na hutoa harufu<br />

mbaya na kali.<br />

je, unazijua alama na dalili za magonjwa ya<br />

zinaa?<br />

Magonjwa mengine ya zinaa hayana dalili za wazi,<br />

hasa kwa wanawake, lakini mengine yanazo.<br />

Dalili za magonjwa ya zinaa kwa wanaume ni<br />

pamoja na:-<br />

• Kidonda, vidonda, upele au malengelenge juu<br />

aukuzunguka uume.<br />

• Uume kutoa usaha.<br />

• Maumivu makali wakati wa kukojoa.<br />

• Maumivu wakati wa kujamiiana.<br />

• Maumivu na kuvimba mapumbu.<br />

• Uvimbe usio wa kawaida au kuota vitu kwenye<br />

via vya uzazi<br />

Dalili za magonjwa ya zinaa kwa mwanamke:<br />

• Kutoka kwa majimaji ukeni ambayo ni mazito;<br />

yanawasha au yana harufu na rangi isiyo ya<br />

kawaida.<br />

• Maumivu sehemu za chini ya kitovu. . Maumivu<br />

wakati wa kujamiiana.<br />

• Kutokwa kwa damu ukeni kusiko kwa kawaida<br />

na bila mpangilio.<br />

• Kuwasha maeneo ya via vya uzazi.<br />

• Uvimbe usio wa kawaida na kuota vitu kwenye<br />

via vya uzazi.<br />

111

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!