Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
110<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Magonjwa mengine ya zinaa kama kaswende, klamidia na kisonono ni hatari vilevile. Magonjwa<br />
haya yanatibika na tunaweza kuyathibiti. Lakini yanaweza kuleta athari za muda mrefu:<br />
•<br />
•<br />
Kusababisha ugumba yaani kushindwa kupata watoto.<br />
Kusaidia virusi vya UKIMWI kuingia mwilini kwa urahisi.<br />
Kwa ufupi, zipo njia tatu za kuepuka magonjwa ya zinaa ikiwa ni pamoja na VVU.<br />
1. Usifanye ngono. Ahirisha kufanya mapenzi au acha kabisa kujamiiana.<br />
2. Unapojamiiana, hakikisha unatumia kondomu tangu mwanzo mpaka unapomaliza kitendo.<br />
3. Nenda na mpenzi/mwenzi wako kupima VVU. Kabla ya kuanza kujamiiana. Unaweza kupima<br />
VVU zaidi ya mara moja kutegemeana ni lini ulifanya ngono isiyo salama (bila kinga) ili<br />
kuhakikisha huna VVU. (Angalia ukurasa wa 116 kwa maelezo zaidi). Hakikisha kati yenu hakuna<br />
aliye na maambukizo ya VVU kabla ya kuanza kujamiiana. Kila mmoja wenu abakie mwaminifu<br />
kwa mwenzie.<br />
Mambo haya yanaonekana kuwa rahisi. Njia za kuwa salama ni hizo tatu. Lakini, yapo mengi ya<br />
kufikiria. Iwapo ulifanya ngono na baadaye ukaamua kuacha, bado utatakiwa kupima. Unaweza<br />
kuwa na ugonjwa uenezwao kwa ngono bila ya kujitambua.<br />
je, unajua kwa nini wasichana wako hatarini zaidi kupata maambukizo ya<br />
magonjwa ya zinaa hasa VVu/uKiMWi?<br />
Ingawa wote, wanaume na wanawake, wanaweza kupata maambukizo ya magonjwa ya zinaa,<br />
wanawake na wasichana wanapata maambukizo kwa urahisi zaidi kuliko wanaume/wavulana.<br />
Zipo sababu kadhaa kwa nini iwe hivyo:<br />
1. Uume wa mwanaume unaingia ndani ya uke na shahawa zake zinaweza kuwa na maambukizo.<br />
Zikikaa ndani ya mwili wa mwanamke zinaongeza uwezekano wa kupata maambukizo ndani ya<br />
tumbo la uzazi, mirija ya falopia na ovari.<br />
2. Kwa ujumla, wasichana wako hatarini kupata maambukizo ya magonjwa ya zinaa kwa sababu<br />
mlango wa mfuko wa uzazi wa msichana balehe ni laini zaidi kuliko wa mwanamke mtu mzima. Uke<br />
unaweza ukachanika wakati wa kujamiiana jambo ambalo linaweza kuongezea hatari ya kupata<br />
maambukizo ya magonjwa ya ngono.<br />
3. Wasichana wengi na wanawake wanafundishwa kuwa watiifu na wanyenyekevu kwa wanaume.<br />
Hawana stadi ya kujiamini ili kuwashawishi wenzi wao kutumia kondomu kwa ajili ya kinga.<br />
Wasichana balehe wengi, walioolewa au wasioolewa, wenzi wao wana umri mkubwa kuliko wao<br />
wenyewe. Mwenzi anapokuwa na umri mkubwa kuliko msichana, inaweza kumuwia vigumu hasa<br />
msichana kujikinga na maambukizi ya magonjwa ya zinaa na mimba. Katika jamii nyingi inaweza<br />
kumwia vigumu mwanamke kukataa kujamiiana na mme wake au kumsisitizia watumie kondomu<br />
hata kama anafikiri mwanaume wake anaweza akawa na mwanamke mwingine.<br />
4. Wanawake na wasichana wako kwenye hatari ya kufanya ngono bila kutaka. (kwa kulazimishwa<br />
au kubakwa), kuliko wanaume na wavulana. Katika mazingira magumu kama haya, inaweza kuwa<br />
vigumu kujikinga na maambukizi.<br />
5. Mambo ya kimila na utamaduni kama vile kufanya ngono kavu na kuweka dawa za kienyeji, nguo<br />
na vitu vingine ndani ya uke ili “kusafisha” au “kuubana” vyote hivi vinamwongezea mwanamke<br />
hatari ya kupata maambukizo ya magonjwa ya ngono. Kukausha uke kabla ya kujamiiana<br />
kunaweza kuongeza uwezekano wa kuchanika na kuchubuka wakati wa kujamiiana.<br />
Kama wewe na mwenzi wako mnatumia kondomu wakati wote mnapojamiiana ni vizuri sana.<br />
Endelea!Watu wengi wanaanza kwa kutumia kondomu. Lakini baada ya muda wanaanza<br />
kufikiri. “Ninamwaminimwenzi wangu, tunaweza kuacha kutumia kondomu”. Hii siyo sawa!<br />
Kabla hamjaacha kutumiakondomu, wote wawili mnahitaji kupima kwa ajili ya magonjwa ya<br />
ngono pamoja na angalau, kipimokimoja cha VVU. Hata kama wewe na mwenzi wako mmepima<br />
na hamna maambukizo ya magonjwaya ngono, ni vizuri zaidi kuendelea kutumia kondomu. Je,<br />
ikitokea kwamba mmoja wenu amejamiianana mtu mwingine? Vilevile unahitaji kuzuia mimba.<br />
utajuaje KaMa uMePata MaaMbuKiZO Ya MaGOnjWa Ya Zinaa?<br />
Watu wengi hasa wanawake ambao wamepata maambukizo ya magonjwa ya zinaa<br />
hawaonyeshidalili zozote zile. Kwa mfano, hakuna dalili yoyote ya kuonyesha kwamba umepata<br />
maambukizo yaVVU kwa mara ya kwanza. Magonjwa mengine ya ngono vilevile hayana dalili za<br />
wazi, kwa hiyo kilamtu inabidi afikirie hatari ya kupata maambukizo ya magonjwa ya zinaa. Kama<br />
umeshafanya ngonobila kinga unaweza kuwa umejiweka katika hatari ya kupata maambukizo.<br />
Ukipata kidonda au kiupele sehemu za siri ambacho kinapotea, unahitaji kumwona mhudumu<br />
wa afya.Yapo magonjwa ya zinaa mengine ambayo yana dalili zinazokuja na kupotea. Kidonda<br />
cha kaswendewakati wote kinapona na vidonda vinavyotokana na malengelenge vinapona na<br />
kujirudia. Kama umewahikupata kidonda, kiupele au lengelenge kwenye via vya uzazi, unatakiwa<br />
kumwona mhudumu wa afya.Hata kama dalili za ugonjwa wa ngono zinapotea, maambukizo<br />
yanakuwepo na wala hayawezi kuponabila kupata tiba sahihi.<br />
Kwa vyovyote vile,kama<br />
umeshaanzakujamiiana au bado, ni<br />
vizuri kufahamuvia vyako vya uzazi<br />
vikoje. Ikiwa unajuavikoje ukiwa mzima,<br />
itakuwa rahisikugundua tatizo mapema.<br />
Tumia kiookujiangalia sehemu zako za<br />
siri kiurahisi.Kwa mfano, kidonda cha<br />
kaswendehakiumi, kwa hiyo unaweza<br />
usigundueisipokuwa kama ukiangalia.<br />
Kwa wasichana, ni vema kufahamu<br />
mwonekano na harufu ya kawaida<br />
yamajimaji yako ya ukeni. Majimaji<br />
yaukeni ya kawaida:. Ni kama majimaji<br />
meupe ya yai.<br />
• Ni maangavu au meupe.<br />
• Yanatoa harufu ya kawaida au yenye<br />
afya na isiyochukiza.<br />
• Hayawashi.<br />
SURA YA 10 | KUTUNZA AfYA YAKO YA KIUJINSIA<br />
Magonjwa ya ngono mara kwa mara<br />
husababisha majimaji ya ukeni kuwa na<br />
rangi ya njano au kijani na hutoa harufu<br />
mbaya na kali.<br />
je, unazijua alama na dalili za magonjwa ya<br />
zinaa?<br />
Magonjwa mengine ya zinaa hayana dalili za wazi,<br />
hasa kwa wanawake, lakini mengine yanazo.<br />
Dalili za magonjwa ya zinaa kwa wanaume ni<br />
pamoja na:-<br />
• Kidonda, vidonda, upele au malengelenge juu<br />
aukuzunguka uume.<br />
• Uume kutoa usaha.<br />
• Maumivu makali wakati wa kukojoa.<br />
• Maumivu wakati wa kujamiiana.<br />
• Maumivu na kuvimba mapumbu.<br />
• Uvimbe usio wa kawaida au kuota vitu kwenye<br />
via vya uzazi<br />
Dalili za magonjwa ya zinaa kwa mwanamke:<br />
• Kutoka kwa majimaji ukeni ambayo ni mazito;<br />
yanawasha au yana harufu na rangi isiyo ya<br />
kawaida.<br />
• Maumivu sehemu za chini ya kitovu. . Maumivu<br />
wakati wa kujamiiana.<br />
• Kutokwa kwa damu ukeni kusiko kwa kawaida<br />
na bila mpangilio.<br />
• Kuwasha maeneo ya via vya uzazi.<br />
• Uvimbe usio wa kawaida na kuota vitu kwenye<br />
via vya uzazi.<br />
111