08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

100<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

Kama walivyo wasichana, wavulana wanaweza kupoteza ubikira wao kwa kujamiiana. Watu<br />

wengine wanafikiri sio muhimu kwa wavulana kuwa bikira kama ilivyo kwa wasichana.Zaidi, video<br />

nyingi unazozitazama na riwaya nyingi unazosoma zinafanya ionekane muhimu kwa wanaume<br />

kuwa na uzoefu zaidi wa ngono. Mara nyingine inaonekana kana kwamba ili uonekane mwanaume<br />

lijali lazima ufanye ngono. Lakini kufanya ngono hakukufanyi uwe mwanaume zaidi. Kwa mvulana<br />

au msichana kutunza ubikira wako ni vizuri. Ni njia nzuri sana kwa kinga ya kweli dhidi ya VVU, na<br />

magonjwa ya ngono na mimba zisizotakiwa.<br />

KuPOteZa ubiKiRa<br />

Uwe mvulana au msichana, unapaswa wewe mwenyewe kuamua wakati gani upoteze ubikira<br />

wako. Usije kuwaruhusu watu wengine kukuamulia au kukushinikiza uupoteze. Chagua muda<br />

wako. Na chagua mtu anayefaa. Subiri hadi unakuwa na uhakika kwamba unaweza kujizuia dhidi<br />

ya magonjwa ya ngono, pamoja na VVU/UKIMWI na mimba zisizotakiwa.<br />

adam, kutoka uganda (umri wa miaka 13)<br />

“Nafikiri muda mzuri wa kuanza kujamiiana ni wakati nikiwa na umri wa<br />

miaka 20. Nitamaliza masomo yangu na pengine kufanya kazi.Hata kama<br />

muda huo ukifika nitatumia kondomu”.<br />

Mfune, kutoka Zambia (umri wa miaka 13)<br />

“Nitasubiri hadi nioe au nipate fedha za kunisaidia kwa sababu msichana<br />

ukipata mimba nitahitaji fedha za kulelea mtoto”.<br />

Mara nyingine wenzako wanaweza kukulazimisha kufanya ngono.<br />

Douglas, kutoka Zambia (umri wa miaka 12)<br />

“Vijana wengine wakubwa kwetu au waliojaliwa kuwa<br />

na miili mikubwa wanatucheka na kutuambia sisi ni bikira”.<br />

andrew, kutoka tanzania (umri wa miaka 17)<br />

“Rafiki yangu wa kiume ananicheka na kunisihi niwe na rafiki wa kike.<br />

Wanasema utaishije bila rafiki wa kike wewe sio mwanaume”.<br />

Mildred, kutoka uganda (umri wa miaka 17)<br />

“Wakati fulani, unajisikia umeachwa na marafiki zako wakianza<br />

kuzungumzia masuala ya ngono. Unaweza tu kuingilia mazungumzo yao<br />

kutokana na ulichosoma kwenye kitabu cha hadithi au ulichoona kwenye<br />

sinema. Kama huna mwelekeo mzuri unaweza ukadanganywa. Nimechagua<br />

kubakia bikira mpaka nimpate mwanaume mzuri wa kunifaa.”<br />

lois, kutoka tanzania (umri wa miaka 13)<br />

“Nazungumza na marafiki zangu kuhusu kufanya ngono. Wapo baadhi ya<br />

wasichana na wavulana wanaosema kwamba ukikataa kufanya ngono<br />

unafanana na mtu ambaye hakusoma”.<br />

Vijana balehe wengi siku hizi wanaelewa kwamba kufanya ngono ni uamuzi wao wenyewe na<br />

kwamba asiwepo mtu wa kuwalazimisha kufanya ngono.<br />

Patrick, kutoka uganda (umri wa miaka 17)<br />

“Marafiki zangu wote wanafanya ngono<br />

na marafiki zao wa kike, na kidogo tu<br />

niwafuate kutokana na kulazimishwa na<br />

marafiki zangu. Lakini niligundua kwamba<br />

sikuwa na uhakika na nilichanganyikiwa.<br />

Isitoshe ninataka kufanya mambo yangu<br />

mwenyewe. Nitasubiri.”<br />

lois, kutoka tanzania (umri wa miaka 13 )<br />

“Hakuna atakayenilazimisha kufanya<br />

ngono. Nitaamua mwenyewe”<br />

Milensu, kutoka Zambia (umri wa miaka<br />

13)<br />

“Sitafanya ngono kwa sababu itabidi nisubiri hadi niolewe nitakapokuwa tayari kwa<br />

matokeo ya kufanya ngono. Sitarajii rafiki zangu kunishinikiza nifanye ngono. Uamuzi ni<br />

wangu.”<br />

andrew, kutoka tanzania (umri wa miaka 17)<br />

“Kama nitataka kufanya ngono utakuwa ni utayari wangu mwenyewe. Rafiki zangu<br />

hawatanishawishi kufanya hivyo.”<br />

KujaMiiana<br />

Kujamiiana ni wakati mwanaume na mwanamke wana ileta miili yao karibu na mwanaume<br />

anasimamisha uume na unaingia ukeni kwa mwanamke.<br />

Kwa nini watu wanajamiiana? Kuna sababu nyingi – nzuri na mbaya. Zifuatazo ni baadhi ya<br />

sababu:<br />

•<br />

•<br />

SURA YA 9 | UJINSIA NA NGONO<br />

Simama imara dhidi ya shinikizo la kundi<br />

rika. usifanye mapenzi eti kwa sababu rafiki<br />

zako wanafikiri unatakiwa kufanya.<br />

Upendo na mapenzi ya dhati. Kwa watu wawili walio karibu sana, kujamiiana kunaweza kuleta<br />

mapenzi ya dhati na yenye upendo. Hata hivyo watu wengine wanafanya ngono kwa sababu<br />

wanafikiri itawaletea kupendana na mapenzi ya dhati kwenye uhusiano wao. Wanafikiri<br />

kujamiiana kutathibitisha mapenzi kati yao. Hii mara nyingi haisaidii. Mapenzi ya dhati<br />

yanakuja kwa kuzungumza mambo ya uaminifu na kushirikiana katika hisia. Ngono haiwezi<br />

kuwaunganisha watu pamoja kama hawakuwa karibu kabla. Kufanya ngono hakumaanishi<br />

watu wanapendana.<br />

Kuridhisha hamu ya mapenzi na mahitaji ya kimwili. Watu wengine wanafikiri kwamba<br />

unahitaji kujamiiana ili kukidhi hisia za kufanya mapenzi – kama unavyohitaji kunywa<br />

unaposikia kiu. Lakini kujamiiana hakuko hivyo. Ukweli wakati mwingine kujamiiana<br />

hakuridhishi kuliko kushikana mikono, kukumbatiana, kubusu, kama watu wawili hawana<br />

mahusiano ya karibu, kufanya ngono kunaweza kusiwaridhishe.<br />

101

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!