Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
100<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
Kama walivyo wasichana, wavulana wanaweza kupoteza ubikira wao kwa kujamiiana. Watu<br />
wengine wanafikiri sio muhimu kwa wavulana kuwa bikira kama ilivyo kwa wasichana.Zaidi, video<br />
nyingi unazozitazama na riwaya nyingi unazosoma zinafanya ionekane muhimu kwa wanaume<br />
kuwa na uzoefu zaidi wa ngono. Mara nyingine inaonekana kana kwamba ili uonekane mwanaume<br />
lijali lazima ufanye ngono. Lakini kufanya ngono hakukufanyi uwe mwanaume zaidi. Kwa mvulana<br />
au msichana kutunza ubikira wako ni vizuri. Ni njia nzuri sana kwa kinga ya kweli dhidi ya VVU, na<br />
magonjwa ya ngono na mimba zisizotakiwa.<br />
KuPOteZa ubiKiRa<br />
Uwe mvulana au msichana, unapaswa wewe mwenyewe kuamua wakati gani upoteze ubikira<br />
wako. Usije kuwaruhusu watu wengine kukuamulia au kukushinikiza uupoteze. Chagua muda<br />
wako. Na chagua mtu anayefaa. Subiri hadi unakuwa na uhakika kwamba unaweza kujizuia dhidi<br />
ya magonjwa ya ngono, pamoja na VVU/UKIMWI na mimba zisizotakiwa.<br />
adam, kutoka uganda (umri wa miaka 13)<br />
“Nafikiri muda mzuri wa kuanza kujamiiana ni wakati nikiwa na umri wa<br />
miaka 20. Nitamaliza masomo yangu na pengine kufanya kazi.Hata kama<br />
muda huo ukifika nitatumia kondomu”.<br />
Mfune, kutoka Zambia (umri wa miaka 13)<br />
“Nitasubiri hadi nioe au nipate fedha za kunisaidia kwa sababu msichana<br />
ukipata mimba nitahitaji fedha za kulelea mtoto”.<br />
Mara nyingine wenzako wanaweza kukulazimisha kufanya ngono.<br />
Douglas, kutoka Zambia (umri wa miaka 12)<br />
“Vijana wengine wakubwa kwetu au waliojaliwa kuwa<br />
na miili mikubwa wanatucheka na kutuambia sisi ni bikira”.<br />
andrew, kutoka tanzania (umri wa miaka 17)<br />
“Rafiki yangu wa kiume ananicheka na kunisihi niwe na rafiki wa kike.<br />
Wanasema utaishije bila rafiki wa kike wewe sio mwanaume”.<br />
Mildred, kutoka uganda (umri wa miaka 17)<br />
“Wakati fulani, unajisikia umeachwa na marafiki zako wakianza<br />
kuzungumzia masuala ya ngono. Unaweza tu kuingilia mazungumzo yao<br />
kutokana na ulichosoma kwenye kitabu cha hadithi au ulichoona kwenye<br />
sinema. Kama huna mwelekeo mzuri unaweza ukadanganywa. Nimechagua<br />
kubakia bikira mpaka nimpate mwanaume mzuri wa kunifaa.”<br />
lois, kutoka tanzania (umri wa miaka 13)<br />
“Nazungumza na marafiki zangu kuhusu kufanya ngono. Wapo baadhi ya<br />
wasichana na wavulana wanaosema kwamba ukikataa kufanya ngono<br />
unafanana na mtu ambaye hakusoma”.<br />
Vijana balehe wengi siku hizi wanaelewa kwamba kufanya ngono ni uamuzi wao wenyewe na<br />
kwamba asiwepo mtu wa kuwalazimisha kufanya ngono.<br />
Patrick, kutoka uganda (umri wa miaka 17)<br />
“Marafiki zangu wote wanafanya ngono<br />
na marafiki zao wa kike, na kidogo tu<br />
niwafuate kutokana na kulazimishwa na<br />
marafiki zangu. Lakini niligundua kwamba<br />
sikuwa na uhakika na nilichanganyikiwa.<br />
Isitoshe ninataka kufanya mambo yangu<br />
mwenyewe. Nitasubiri.”<br />
lois, kutoka tanzania (umri wa miaka 13 )<br />
“Hakuna atakayenilazimisha kufanya<br />
ngono. Nitaamua mwenyewe”<br />
Milensu, kutoka Zambia (umri wa miaka<br />
13)<br />
“Sitafanya ngono kwa sababu itabidi nisubiri hadi niolewe nitakapokuwa tayari kwa<br />
matokeo ya kufanya ngono. Sitarajii rafiki zangu kunishinikiza nifanye ngono. Uamuzi ni<br />
wangu.”<br />
andrew, kutoka tanzania (umri wa miaka 17)<br />
“Kama nitataka kufanya ngono utakuwa ni utayari wangu mwenyewe. Rafiki zangu<br />
hawatanishawishi kufanya hivyo.”<br />
KujaMiiana<br />
Kujamiiana ni wakati mwanaume na mwanamke wana ileta miili yao karibu na mwanaume<br />
anasimamisha uume na unaingia ukeni kwa mwanamke.<br />
Kwa nini watu wanajamiiana? Kuna sababu nyingi – nzuri na mbaya. Zifuatazo ni baadhi ya<br />
sababu:<br />
•<br />
•<br />
SURA YA 9 | UJINSIA NA NGONO<br />
Simama imara dhidi ya shinikizo la kundi<br />
rika. usifanye mapenzi eti kwa sababu rafiki<br />
zako wanafikiri unatakiwa kufanya.<br />
Upendo na mapenzi ya dhati. Kwa watu wawili walio karibu sana, kujamiiana kunaweza kuleta<br />
mapenzi ya dhati na yenye upendo. Hata hivyo watu wengine wanafanya ngono kwa sababu<br />
wanafikiri itawaletea kupendana na mapenzi ya dhati kwenye uhusiano wao. Wanafikiri<br />
kujamiiana kutathibitisha mapenzi kati yao. Hii mara nyingi haisaidii. Mapenzi ya dhati<br />
yanakuja kwa kuzungumza mambo ya uaminifu na kushirikiana katika hisia. Ngono haiwezi<br />
kuwaunganisha watu pamoja kama hawakuwa karibu kabla. Kufanya ngono hakumaanishi<br />
watu wanapendana.<br />
Kuridhisha hamu ya mapenzi na mahitaji ya kimwili. Watu wengine wanafikiri kwamba<br />
unahitaji kujamiiana ili kukidhi hisia za kufanya mapenzi – kama unavyohitaji kunywa<br />
unaposikia kiu. Lakini kujamiiana hakuko hivyo. Ukweli wakati mwingine kujamiiana<br />
hakuridhishi kuliko kushikana mikono, kukumbatiana, kubusu, kama watu wawili hawana<br />
mahusiano ya karibu, kufanya ngono kunaweza kusiwaridhishe.<br />
101