08.06.2013 Views

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

18<br />

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />

kuanza kukua, unaweza kujikuta wewe ni mrefu kuliko wavulana wengine waliopata msukumo wa<br />

ukuaji mapema.<br />

Sauti YaKO<br />

Sauti yako ni dalili nyingine ya uhakika kwamba unaingia kipindi cha balehe. Sauti huanza<br />

kubadilika baada ya mfoko wa ukuaji kuanza, kwa kawaida ni katika umri wa miaka 14 au 15.<br />

Sauti ya wavulana hubadilika kuwa ya chini na nzito katika kipindi cha balehe, kwa sababu ya<br />

homoni inayoitwa “testosterone”.Aina hii ya homoni husababisha zoloto (sehemu ya mwanzo wa<br />

koromeo inayohusika na utoaji wa sauti) kuwa kubwa. Kwa jinsi nyuzi za sauti zinavyokuwa nene<br />

na ndefu ndivyo sauti inavyokuwa ya chini na nzito.<br />

Precious, mvulana kutoka Ghana (umri, miaka 15 )<br />

“Kitu cha kwanza nilichogundua ni kukatika kwa sauti, kupanuka kifua<br />

na mabega. Nilifurahi kwa sababu niliona kwamba sasa ninakuwa<br />

kijana balehe.”<br />

Panaito, kutoka Kenya.<br />

“Nilipata mabadiliko ya sauti mara baada ya kupata ndoto nyevu.”<br />

aloysious kutoka uganda (umri, miaka 19)<br />

“Sauti yangu ilipobadilika nikiwa na umri wa miaka 15. Nilitambua kuwa<br />

nilikuwa ninakua. Nilikua haraka sana na nilifurahi.”<br />

Dalili ya kwanza kuonyesha kwamba sauti yako inabadilika ni kuanza kukwaruza kwa sauti<br />

ghafla. Wavulana wengine hujisikia vibaya sauti zao zinapoanza kukwaruza, kwa vile mara nyingi<br />

haitabiliki itaanza lini.<br />

Sauti huwa ya kawaida na kubadilika katika muda mfupi. Mara inakuwa ya kawaida, dakika<br />

chache baadaye inakuwa ya juu na nyembamba.<br />

SURA YA 3 | WAvULANA<br />

Via VYaKO VYa uZaZi (SeheMu ZaKO Za SiRi)<br />

Uume umetengenezwa na misuli inayozunguka mrija mwembamba. Mrija huu hupitisha mkojo na<br />

shahawa. Uume una kichwa na mwili.Mwili au mpini ni ile sehemu ya uume kama bomba. Kichwa<br />

ni ile sehemu ya juu ya uume. Ni sehemu ambayo ina hisia kali na inahitaji uangalifu mkubwa.<br />

Unapozaliwa kichwa cha uume kinakuwa kimefunikwa<br />

na ngozi nyembamba iliyojikunja. Ngozi hii inaitwa<br />

“govi” Jamii nyingi za Afrika huondoa govi kwa njia<br />

ya upasuaji. Kitendo hiki kinaitwa “kutahiri”. (Angalia<br />

ukurasa wa 20 kwa maelezo zaidi kuhusu kutahiri.)<br />

Ukubwa wa uume unatofautiana kati ya mwanaume na<br />

mwanaume na hauna uhusiano kabisa na ukubwa wa<br />

mwili. Mara nyingi, jinsi uume unavyokuwa mkubwa<br />

ukiwa laini ndivyo unavyoongezeka kidogo unapokuwa<br />

umedinda. Vivyo hivyo, kama ni mdogo unapokuwa<br />

laini unaweza kuongezeka zaidi unapokuwa umedinda.<br />

Vijana wengi wa kiume, “hata wanaume wakubwa”<br />

wanatumia muda mwingi kufikiri na kuwa na wasiwasi<br />

kuhusu uume wao. Je ni mdogo sana? Kwa nini<br />

umepinda kuelekea huku? Je, kuna tatizo lolote?<br />

Sehemu za siri za mwanaume kwa ndani<br />

aloysius kutoka uganda (umri, miaka 19)<br />

“Wakati mwingine tulikuwa tunavuta uume na kulinganisha nani<br />

anao mkubwa zaidi?!”<br />

Iwapo umewahi kujishangaa kama uume wako una ukubwa wa kutosha, kumbuka tu kwamba<br />

tendo la ngono halitegemei ukubwa wa uume. Kwa uhakika ni kwamba ukubwa wa uume hauna<br />

athari zozote kwa mwanamke katika kufurahia tendo la kujamiiana (ngono).<br />

Ukweli ni kwamba kufurahia ngono kwa wanawake na wanaume wengi kunategemea zaidi jinsi<br />

gani kila mmoja wapo anavyompenda mwenzie. Kilicho cha muhimu ni mahusiano na wala sio<br />

ukubwa wa uume.<br />

Kinachoning’inia chini ya uume ni mapumbu. Pumbu ni kama mfuko au kifuko cha ngozi<br />

kinachoshikilia korodani au makende, ambako mbegu za kiume hutengenezwa tangu kipindi<br />

cha balehe hadi uzeeni. Ngozi ya mapumbu ina nywele kidogo na mafuta. Hudaka uchafu ambao<br />

kama haukusafishwa husababisha harufu mbaya.<br />

Katika kipindi cha utoto, mapumbu hujikunja na kuwa karibu na mwili. Lakini, kadri unapopitia<br />

balehe, mapumbu huanza kulegea na kuning’inia chini, ingawa ukijisikia baridi au kuogopa au<br />

kuwa na hamu ya kujamiiana, mapumbu yako yanaweza kujikunja na kurudi karibu na mwili.<br />

Mapumbu yananing’inia chini kwa sababu korodani zinahitaji kuwa katika hali yenye joto chini ya<br />

joto la mwili ili kutengeneza mbegu za kiume.<br />

19

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!