Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Wewe Maisha Yako Ndoto Zako - Family Care International
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
18<br />
WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO<br />
kuanza kukua, unaweza kujikuta wewe ni mrefu kuliko wavulana wengine waliopata msukumo wa<br />
ukuaji mapema.<br />
Sauti YaKO<br />
Sauti yako ni dalili nyingine ya uhakika kwamba unaingia kipindi cha balehe. Sauti huanza<br />
kubadilika baada ya mfoko wa ukuaji kuanza, kwa kawaida ni katika umri wa miaka 14 au 15.<br />
Sauti ya wavulana hubadilika kuwa ya chini na nzito katika kipindi cha balehe, kwa sababu ya<br />
homoni inayoitwa “testosterone”.Aina hii ya homoni husababisha zoloto (sehemu ya mwanzo wa<br />
koromeo inayohusika na utoaji wa sauti) kuwa kubwa. Kwa jinsi nyuzi za sauti zinavyokuwa nene<br />
na ndefu ndivyo sauti inavyokuwa ya chini na nzito.<br />
Precious, mvulana kutoka Ghana (umri, miaka 15 )<br />
“Kitu cha kwanza nilichogundua ni kukatika kwa sauti, kupanuka kifua<br />
na mabega. Nilifurahi kwa sababu niliona kwamba sasa ninakuwa<br />
kijana balehe.”<br />
Panaito, kutoka Kenya.<br />
“Nilipata mabadiliko ya sauti mara baada ya kupata ndoto nyevu.”<br />
aloysious kutoka uganda (umri, miaka 19)<br />
“Sauti yangu ilipobadilika nikiwa na umri wa miaka 15. Nilitambua kuwa<br />
nilikuwa ninakua. Nilikua haraka sana na nilifurahi.”<br />
Dalili ya kwanza kuonyesha kwamba sauti yako inabadilika ni kuanza kukwaruza kwa sauti<br />
ghafla. Wavulana wengine hujisikia vibaya sauti zao zinapoanza kukwaruza, kwa vile mara nyingi<br />
haitabiliki itaanza lini.<br />
Sauti huwa ya kawaida na kubadilika katika muda mfupi. Mara inakuwa ya kawaida, dakika<br />
chache baadaye inakuwa ya juu na nyembamba.<br />
SURA YA 3 | WAvULANA<br />
Via VYaKO VYa uZaZi (SeheMu ZaKO Za SiRi)<br />
Uume umetengenezwa na misuli inayozunguka mrija mwembamba. Mrija huu hupitisha mkojo na<br />
shahawa. Uume una kichwa na mwili.Mwili au mpini ni ile sehemu ya uume kama bomba. Kichwa<br />
ni ile sehemu ya juu ya uume. Ni sehemu ambayo ina hisia kali na inahitaji uangalifu mkubwa.<br />
Unapozaliwa kichwa cha uume kinakuwa kimefunikwa<br />
na ngozi nyembamba iliyojikunja. Ngozi hii inaitwa<br />
“govi” Jamii nyingi za Afrika huondoa govi kwa njia<br />
ya upasuaji. Kitendo hiki kinaitwa “kutahiri”. (Angalia<br />
ukurasa wa 20 kwa maelezo zaidi kuhusu kutahiri.)<br />
Ukubwa wa uume unatofautiana kati ya mwanaume na<br />
mwanaume na hauna uhusiano kabisa na ukubwa wa<br />
mwili. Mara nyingi, jinsi uume unavyokuwa mkubwa<br />
ukiwa laini ndivyo unavyoongezeka kidogo unapokuwa<br />
umedinda. Vivyo hivyo, kama ni mdogo unapokuwa<br />
laini unaweza kuongezeka zaidi unapokuwa umedinda.<br />
Vijana wengi wa kiume, “hata wanaume wakubwa”<br />
wanatumia muda mwingi kufikiri na kuwa na wasiwasi<br />
kuhusu uume wao. Je ni mdogo sana? Kwa nini<br />
umepinda kuelekea huku? Je, kuna tatizo lolote?<br />
Sehemu za siri za mwanaume kwa ndani<br />
aloysius kutoka uganda (umri, miaka 19)<br />
“Wakati mwingine tulikuwa tunavuta uume na kulinganisha nani<br />
anao mkubwa zaidi?!”<br />
Iwapo umewahi kujishangaa kama uume wako una ukubwa wa kutosha, kumbuka tu kwamba<br />
tendo la ngono halitegemei ukubwa wa uume. Kwa uhakika ni kwamba ukubwa wa uume hauna<br />
athari zozote kwa mwanamke katika kufurahia tendo la kujamiiana (ngono).<br />
Ukweli ni kwamba kufurahia ngono kwa wanawake na wanaume wengi kunategemea zaidi jinsi<br />
gani kila mmoja wapo anavyompenda mwenzie. Kilicho cha muhimu ni mahusiano na wala sio<br />
ukubwa wa uume.<br />
Kinachoning’inia chini ya uume ni mapumbu. Pumbu ni kama mfuko au kifuko cha ngozi<br />
kinachoshikilia korodani au makende, ambako mbegu za kiume hutengenezwa tangu kipindi<br />
cha balehe hadi uzeeni. Ngozi ya mapumbu ina nywele kidogo na mafuta. Hudaka uchafu ambao<br />
kama haukusafishwa husababisha harufu mbaya.<br />
Katika kipindi cha utoto, mapumbu hujikunja na kuwa karibu na mwili. Lakini, kadri unapopitia<br />
balehe, mapumbu huanza kulegea na kuning’inia chini, ingawa ukijisikia baridi au kuogopa au<br />
kuwa na hamu ya kujamiiana, mapumbu yako yanaweza kujikunja na kurudi karibu na mwili.<br />
Mapumbu yananing’inia chini kwa sababu korodani zinahitaji kuwa katika hali yenye joto chini ya<br />
joto la mwili ili kutengeneza mbegu za kiume.<br />
19