19.05.2013 Views

constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet

constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet

constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Upande wa mambo haya mengine vile vile, ukiuliza swali lolote, unaambiwa yanatoka juu. Sasa, Bwana Commisioner, tunataka<br />

mambo yawe yakitoka chini, kama vile tukichagua wale watu kuenda juu. Tuwe tukielewa ni kitu gani kinaendelea, mpaka<br />

huko juu. Yaani tukiuliza swali, tujue tunauliza swali la aina gani. Hii ni kwa sababu tunaambiwa, ni kama mtoto. Sasa wakati<br />

huu, wananchi wa kawaida ni kama watoto wale wamezaliwa, wale wachanga kabisa. Ni kuambiwa tunaambiwa. Yaani, sisi<br />

hatusemi. Ni nikuambiwa tunaambiwa tu. Kwa hivyo sasa, kuanzia hii Katiba tunatengeneza sasa mwananchi wa kawaida<br />

anapaswa kuwa akijua kila kitu kilicho, au kila kitu kinachoendelea. Hawa Wajumbe tuliwachagua kuenda Parliament,<br />

wakatuongoze kwa mambo yale, kwa sababu ndio wako huko juu, watugawie kile kinatakikana. Ni ajabu sasa, kuona wale<br />

tulipeleka Parliament, ndio wenye kila kitu. Mahindi, kahawa, mandizi haya tunalima huku, ni kama ndio wenyewe. Ukiwauliza<br />

maswali wakija huku, wanasema Serikali imesema. Tukiendelea kuuliza maswali tunaambiwa Serikali ni sisi. Je Serikali ni sisi<br />

na tuna taabika?<br />

Kwa upande ule mwingine, nchi yetu ya Kenya iko na area kubwa sana, ile haifanyiwi kazi. Serikali yetu ya wakati huu inajua,<br />

na inaona. Tunashangaa ni kwa nini, kama wanatembea kama tuseme President Wetu ameshawahi kwenda mahali pengi sana.<br />

Mahali kule kulikuwa dry kama upande huu wa Isiolo huko, upande wa Garissa, ameshawahi kwenda huko. Huko sasa wakati<br />

huu, wale watu wanalima, na wanalima na maji. Bahati yetu sisi tuna milima miwili hapa karibu sana na ina maji. Tuna Mount<br />

Kenya hapa, tuna Nyambene hapa, mahali pengi sana. Pale maji yanaweza kufikiriwa, ikafikia wale watu wakaanza kulima.<br />

Sasa msaada, ni huu msaada tunaona unapita na ma-lorry kuteremka chini, na kesho yake tunaona unapanda juu na lorry zile<br />

zile? That means, wale wanapelekewa wanagonga kidole. Wanaweka kidole, kesho yake mahindi yanabebwa tena tunakuja<br />

kuuziwa huku, na ni ya msaada. Sasa ningependelea hivi, maoni yangu, huo msaada, uwe ukijulikana kutoka mahali kule<br />

unatoka huko store, ma-store yao huko Nairobi, iwe ikujulikana inakwenda Garissa, au Marsabit, na iwe announced katika<br />

radio. Watu wa Marsabit wawe wanangojea malorry matano ya mahindi. Wajue itafika kama kweli, ama <strong>constitution</strong> yangu<br />

ndiyo inasema hivyo. Kila kitu kikipatikana kwa msaada kiwe kina pelekwa mahali pale kinatakikana na wananchi wakule<br />

wakiwa wanajua, kuna kitu kinakuja, na wangojee. Hii ni kwa sababu sasa, tunasikia tu msaada. Watu wanapatiwa msaada,<br />

lakini hatuwezi kujua ni msaada wa aina gani.<br />

Ni mshangao mkuu, kwa sababu wengi wetu kama hapa, wengi wetu wameelimika, ama, watoto wetu wameelimika kiasi<br />

kikuu. Upande wa kazi, mtoto akiandika application, mara moja tu, barua ina-regret, hatuna kazi. Mimi ningependelea,<br />

mbeleni hapo, mtoto akiwa amehitimu mtihani fulani, ilikuwa tu ni application kusomwa na kuonekana huyu mtoto amepita<br />

kiwango fulani, na hii kazi kweli inapaswa ipatiwe mtoto huyu, Sio kuwachunguza kabila hii au kabla ile, hapana. Sio kusema<br />

ati, tuje na hii, inaitwa back doors, hapana direct namna hivyo. Ikifanyikana hivyo, Serikali yetu itaendelea, na tutakuwa tukijua<br />

Serikali ni gani, na tutakuwa tukisema ina tufanyia kazi. Asanteni sana.<br />

Com. Lenaola: Mr. Kimakia, njoo ujiandikishe pale. Peter Kiambi, Erastus M’torukuma, utamfuata.<br />

44

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!