19.05.2013 Views

constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet

constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet

constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Namwacha na watoto hao. Mama hana shamba, na watoto hawana elimu, kwa hivyo umaskini unaongezeka. Huyo bwana<br />

aliyetunga huyo mwanamke mimba anafaa achukuliwe na ashtakiwe. Akishtakiwa, huyo mtoto naye anafaa asomeshwe na<br />

Serikali, ikiwa huyo ameshtakiwa.<br />

Kwa andikwa: – Mimi naonelea , iwe kama vile ilikuwa zamani, ili watu waandikwe, kwa sababu hawa watoto maskini<br />

wanaosoma, hawawezi kuandikwa kazi, Kwa vile ukiitwa, unaitishwa pesa. Unaambiwa, ah, lete kitu kidogo, ili mtoto<br />

andikwe. Sasa mimi nikiitishwa elfu hamsini, nitatoa wapi? Huyo mtoto hawezi kusoma. Serikali pia, haisemi uitishe mtu pesa.<br />

Mtu kama huyo akipatikana anafaa afutwe kazi, na ashtakiwe kwa kuharibu kazi yake. Hayo ndiyo maoni yangu.<br />

Com. Lenaola: Asante sana.<br />

Wilson Marete: Mimi bado sija maliza . Hawa wanawake nao, wanaotaka ukubwa kwa mabwana, ai, kweli, wanataka<br />

ukweli. Lakini zamani hata ukiangalia kwa maumbile hata kutoka kwa Mungu, kitabu cha Mungu hakikubali mwanamke awe<br />

juu ya mwanamme. Watu ni wawili hata ukiangalia, iko Mungu, iko Yesu, na iko Malaika. Yesu hawezi kupanda juu ya<br />

Mungu, na malaika hawezi kupanda juu ya Yesu. Kwa hivyo, watu wanafaa watumie mila yao. Kwa sababu, wale<br />

wanaoharibu hivi ni kitu tunawekelewa sisi. Mwanamke yule aliyeshindwa na bwana yake, ni jina anaye ile ya kuolewa, lakini<br />

alitupa bwana na akatupa watoto. Ndiyo anakwenda kujigamba kwenda Beijing, sijui wapi. Haija umiza bwana. Sasa<br />

nikikasirika, si nitamwacha na watoto. Watoto hao, hawana shamba, mama hana shamba na hiyo shamba watatuma niuuze.<br />

Wakati nitakapouza, mwanamke na mtoto wanaangamia, na umaskini unangia hapo, na wezi wanakuwa wengi. Kwa hivyo,<br />

huyo mtu, anafaa achukuliwe na afanyiwe vile inavyowezakana, ili iwe adhabu kali kwake. Kuna mtu mwingine pia, anayeweza<br />

kuenda kuuwa kijana kama huyu. Kumuua tu; akienda kotini, kesho unamuona hapa, na anakuambia, nilimuua na ulinipeleka<br />

kotini, kwa hivyo hata wewe nitakuuwa.<br />

Kitabu cha Mungu kinasema hivi, ukiuwa na panga, hata wewe utauwawa na panga ukiuwa na kamba, hata wewe unyongwe<br />

na kamba. Kwa hii naye, maskini ananyakuliwa hata mali yake na mawakili. Mimi naweza kuwa sina mali, lakini tajiri<br />

anayekujua, (akiona hii shamba yako) anasema, ah hii shamba si yako. Court injuction – naondolewe na shamba ni yangu. Sina<br />

mtu wa kunisaidia. Sina pesa ya kufuata. Hapo inakuwa ni mahangaiko. Hiyo Serikali inafaa ichukue hatua, mtu kama ni<br />

mwizi, awe kama huyo, mwingine anaiba mtu na panga. Ikiwa ni kunyongwa anyongwe kwa sababu hakuna mwizi wa panga<br />

na wa kukunyanganya hivyo – mwizi ni mwizi.<br />

Mashamba: – Kuna watu wanaambiwa kuwa Serikali inawapa mashamba; huko mashambani eka mbili, eka tatu, eka tano, au<br />

eka kumi, lakini baadaye Serikali ililipa hayo mashamba, na baadaye, wanakuja kuitishwa pesa, ukaambiwa lete pesa ya<br />

shamba ulilopewa. Sasa nilipewa nikiwa maskini, nitatoa pesa wapi bwana. Kwa hivyo, huyo mtu anafaa awachiwe shamba<br />

kwa sababu alipewa free, afanye kazi yake free, kwa sababu huyo ni maskini ndiye aliyesaidiwa. Hii mashamba makubwa ya<br />

wengine, tuseme wazungu wako na mashamba makubwa sana, jamaa anashikilia shamba kutoka hapa mpaka huko Tigania<br />

8

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!