15.01.2013 Views

2 - мгимо

2 - мгимо

2 - мгимо

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

zilipunguzwa. Lakini wagonjwa walizidi sana kwenda hospitali kupata<br />

matibabu. Ingawa hivyo yalikuwapo mafanikio mema fulani. Kazi<br />

iliyokuwa ya maana sana ilikuwa ni kutiliwa mkazo kwa ubora wa<br />

chakula kizuri kwa mwili na magonjwa yanayotokana na kutokula<br />

chakula cha kutosha na cha kufaa.<br />

Baada ya vita, Idara ya Utibabu ilifanya maendeleo mazuri ingawa<br />

mambo mengine mabaya, kwa mfano kuwa na hospitali mbali<br />

kwa Wazungu, yalikuwa bado yapo. Kazi za dawa hazikutosheleza<br />

mahitaji ya watu kwa vile ambavyo watu wengi walikwenda hospitali<br />

kutibiwa na kuacha miti shamba. Fedha iliyoongezwa haikutosha kununua<br />

vifaa vya hospitali na pia haikutosha kupanua shule za kufundishia<br />

waganga. Licha ya fedha, hawakuwapo (3) watu wa kutosha<br />

wenye elimu iliyotakiwa ili wachukue mafunzo mbali mbali ya uganga.<br />

Kazi za utibabu hazikuweza kuendelea pasipo Waafrika wenyewe kupewa<br />

ujuzi na madaraka katika kila daraja la wauguzi. Manesi na<br />

madaktari Waafrika wengi walitakiwa.<br />

Katika mwaka 1951 halmashauri ya mafunzo ya waganga ilianzishwa.<br />

Mafunzo ya miaka mitatu ya wasaidizi wa madaktari yaliendelea<br />

Dar es Salaam wakiwa wanachukuliwa wanafunzi waliohitimu<br />

darasa la kumi (4). Mafunzo ya miaka miwili kwa wasaidizi wa madaktari<br />

katika hospitali za shamba, yaliendelea Mwanza. Kwa shule ya<br />

Mwanza walichukuliwa wanafunzi waliohitimu darasa la nane.<br />

Lakini kwa upande wa kuzuia magonjwa maendeleo hayakuwa<br />

makubwa. Mahitaji ya kuwapo (3) kwa vituo vya kutolea dawa na<br />

kuzuia magonjwa katika sehemu za shamba na pia kwa ajili ya kutolea<br />

elimu ya mambo ya usafi na afya nzuri yalikuwa makubwa sana. Vituo<br />

hivyo vingalikuwa vinatoa dawa (5) na kuwa na vyumba vidogo vya<br />

kulaza wagonjwa, vyumba vya kuzalishia na sehemu za kuangalia afya<br />

ya watoto wachanga, na pia vyumba vya kutolea mafunzo ya elimu ya<br />

usafi na afya. Ilitazamiwa kuwa hatimaye vituo hivyo vingelikuwa<br />

badala ya hospitali ndogo.<br />

Katika mwaka 1960 hospitali kubwa ilifunguliwa mjini Dar es<br />

Salaam, yaani hospitali iitwayo Muhimbili sasa. Palikuwa pia na hospitali<br />

arobaini na nane nyingine za serikali, hospitali kwa matibabu<br />

maalumu sita na hospitali ndogo ishirini.<br />

204

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!