15.01.2013 Views

2 - мгимо

2 - мгимо

2 - мгимо

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Wakazi wengi zaidi wa Mwanza ni Wasukuma, ingawa bado<br />

kuna mchanganyiko mkubwa wa makabila mkoani humo, mathalani,<br />

Wajita, Wakerewe, Wasumbwa na mengineyo.<br />

ТЕКСТ №3<br />

MJI WA ARUSHA<br />

Mji wa Arusha umekuwa na maendeleo ya kusisimua katika<br />

muda wa miaka michache iliyopita. Mji huu unazidi kuwa maarufu,<br />

siyo katika Tanzania tu, bali katika Afrika ya Mashariki na Afrika<br />

kwa jumla.<br />

Kwa wanasiasa jina la Arusha lawakumbusha mahali<br />

ilipotangazwa siasa ya Ujamaa na Kujitegemea ambayo siasa hiyo<br />

ilikubaliwa na kupitishwa katika kikao cha Mkutano wa TANU<br />

uliofanyika mwaka 1967. Katika Azimio la kuitangaza siasa hiyo<br />

Watanzania wameamua kukomesha kila aina ya unyonyaji, ukabaila<br />

na ubepari, na kusisitiza usawa wa binadamu. Azimio hilo limepewa<br />

jina la Azimio la Arusha.<br />

Licha ya Azimio hilo, mji huu ni maarufu kwa mambo<br />

mengine ya kihistoria pia. Hapa ndipo palikuwa na makao makuu ya<br />

Jumuiya ya nchi za Afrika ya Mashariki ambayo iliundwa zamani<br />

kwa kuyashughulikia mambo mengi ya uchumi katika nchi za Tanzania,<br />

Kenya na Uganda.<br />

Kwa siku hizi katika mji wa Arusha unaweza kuona watalii<br />

wengi mbalimbali wanaokwenda au kurudi kutoka kwenye mbuga<br />

za wanyama huko Serengeti, Ngorongoro na Ziwa Manyara. Arusha<br />

ndio mji mkubwa katika sehemu ya mbuga za wanyama za<br />

kaskazini. Watu wengi huweza kupata mahitaji yao hapa mjini.<br />

Kuna mahoteli makubwa na ya kisasa. Hoteli hizi pamoja na<br />

mashirika ya utalii yaliyomo mjini (1) hushughulika kuwapa watalii<br />

habari za mbuga zetu za wanyama. Mipango mingi ya kutalii katika<br />

mbuga hizi za wanyama hufanyika hapa mjini Arusha. Utaweza<br />

kuona magari mengi ya kutalii yakichukua wageni hawa.<br />

Watalii wanaokuja nchini kwetu hununua vitu vingi kutoka<br />

madukani, hivyo huongeza biashara ya taifa. Pia watalii hulipa<br />

ushuru wa kuingia katika mbuga hizi za wanyama pamoja na ku-<br />

25

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!